Articles by "TANZIA"
Showing posts with label TANZIA. Show all posts
Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Dotto Biteko pamoja na Viongozi mbalimbali wakiwasili kuhudhuria shughuli ya mazishi ya aliyekuwa waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa leo Februari 17, 2024 katika kijiji cha Ngarash wilayani ya Monduli mkoa wa Arusha asubuhi hii.
Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Edward Lowassa (70) amefariki dunia leo Jumamosi Februari 10,2024 wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam.

Tangazo la kifo cha Lowassa kimetangazwa Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt Philip Mpango.

Katika tangazo fupi alilolitoa kupitia televisheni ya taifa, Mpango amesema kuwa Lowassa ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania mwaka 2005-2008 amefikwa na umauti katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akisani kitabu cha maombolezi kufuatilia kifo cha Rais Mstafu wa Jamhuri ya Watu wa China, Jiang Zemin, kwenye ubalozi Mdogo wa China uliopo Mazizini Jijini Zanzibar leo Desemba 2, 2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akisani kitabu cha maombolezi kufuatilia kifo cha Rais Mstafu wa Jamhuri ya Watu wa China, Jiang Zemin, kwenye ubalozi Mdogo wa China uliopo Mazizini Jijini Zanzibar leo Desemba 2, 2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuagana na Balozi Mdogo wa Jamhuri ya Watu wa China anayefanyika Kazi zake Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng,baada ya kumaliza kutia saini kitabu cha maombelezi kufuatilia kifo cha Rais Mstafu wa Jamhuri ya Watu wa China Jiang Zemin, leo 2-12-2022 katika ubalozi mdogo wa China Mazizini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi anasikitika kutangaza kifo cha Ndg. Gerald Mwanilwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, kilichotokea tarehe 02 Novemba, 2022 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mipango ya Mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Goba Dar es Salaam, Ilazo Dodoma na Makorongoni Iringa.

Kwa masikitiko makubwa tunatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh. Hemed Suleiman Abdulla pamoja na wananchi tayari wamefika katika Uwanja wa Magufuli uliopo Chato mkoani Geita tayari kwa ajili ya kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.



























Huzuni na simanzi zilipotawala wakati mwili wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ukiingia katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza leo tarehe 24 Machi, 2021.