
Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma waliokua katika kituo cha mafunzo cha Maposeni Sekondari wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi.Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, leo Alhamis, Februari 12, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini, Mheshimiwa Gabriel Pandureni Sinimbo.
Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, yakilenga kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya vyama hivyo viwili pamoja na mataifa yao.
Katika kikao hicho, viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kisiasa na kidiplomasia, wakisisitiza umuhimu wa kudumisha urafiki wa kidugu uliodumu kwa miaka mingi kati ya CCM na Chama cha SWAPO cha Namibia.
Uhusiano kati ya Tanzania na Namibia umejengwa katika misingi ya mshikamano wa kihistoria tangu enzi za harakati za ukombozi wa Afrika, ambapo Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kuunga mkono mapambano ya uhuru wa Namibia.
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza rasmi uteuzi wa Mbunge na Diwani Mwanamke wa Viti Maalumu kufuatia nafasi zilizoachwa wazi baada ya vifo vya waliokuwa wakizishikilia awali.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Tume hiyo Januari 30, 2026, Jijini Dodoma, uteuzi huo umefanyika kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 78(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na kifungu cha 112 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Sura ya 343.
Katika uteuzi huo, Tume imemteua Ndugu Bengi Mazana Issa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Mbunge Mwanamke wa Viti Maalumu. Nafasi hiyo imekuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge Mwanamke wa Viti Maalumu kupitia CCM, Ndugu Halima Idd Nassor, aliyefariki dunia Januari 18, 2026.
Aidha, Tume hiyo imemteua Ndugu Irene Linus Mwangara wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kuwa Diwani Mwanamke wa Viti Maalumu katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Uteuzi huo umefanyika kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 25(1)(c) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288, pamoja na kifungu cha 113 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Sura ya 343.
Tume imeeleza kuwa uteuzi wa Diwani Mwanamke huyo umefanyika baada ya kukamilika kwa zoezi la uchaguzi wa marudio katika Kata ya Mzinga, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo uchaguzi huo uliahirishwa awali kutokana na kifo cha mgombea katika kata husika.
Taarifa hiyo imetolewa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, ikibainisha kuwa uteuzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya kikatiba na kisheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi katika kuhakikisha uwakilishi wa wananchi unazingatia sheria na taratibu zilizopo.
Hatua hiyo inaendelea kudumisha uwiano wa uwakilishi wa wanawake katika vyombo vya maamuzi, sambamba na misingi ya Katiba na sera ya Serikali ya kukuza usawa wa kijinsia katika uongozi.
Na Mwandishi Wetu, RUVUMA.CHAMA cha National League For Democracy (NLD) kimempitisha Mhagama Hamisi Yusufu kuwania Ubunge Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma ambayo ataipeperusha Bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mdogo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Jenista Mhagama.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,Katibu wa NLD Doyo Hassan Doyo ambapo aliwaambia kwamba siku hiyo ni muhimu kwa wananchi wa Jimbo la Peramiho kufanya maamuzi ya kiongozi wanayemtaka .
Alisema kwamba kiongozi ambaye anaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo ni mgombea wao kutokana na uongozi uliopita kwa miaka mingi umeshindwa kuwapa maendeleo na mabadiliko katika Jimbo hilo.
Katibu huyo aliwataka wananchi hao kutokufanya makosa katika uchaguzi huo wa marudio kutokana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kufariki dunia hivyo aliwataka kumchagua mgombea anayetokana na NLD ili aweze kuwapa maendeleo makubwa.
Katika uchaguzi huo Mhagama Hamis Yusuf wa NLD atachuana na wagombea wengine akiwemo Yusuf Rashid Rai wa Chama cha AAFP,Abdallah Boniface Ngonyani wa Chama cha Makini,Hanifa Sembe Mohamed wa Chama cha UMD,Beatrice Omari Muya wa UPDP,Mapunda wa Chama cha DP,Dastan Frolian Pili wa CCK,Morice Thomas Nkongo wa TLP na Mtemi Pachoto wa UDP.
Rais Yoweri Museveni amehitimisha leo miaka 40 madarakani. Museveni aliyechukua madaraka mwaka 1986, amesisitiza mchango wa serikali yake katika kuleta utulivu, usalama na maendeleo ya taifa. Kwenye hotuba yake, amewataja wapinzani wake kuwa magaidi, hatua iliyoibua mjadala mpana wa kisiasa ndani na nje ya nchi. andika habari ya gazeti
Kampala, Uganda — Rais Yoweri Museveni ameadhimisha rasmi kukamilisha miaka 40 madarakani leo, akisisitiza mchango wa serikali yake katika kudumisha utulivu, usalama na maendeleo ya taifa, licha ya malalamiko ya kimataifa na ndani ya nchi kuhusu hali ya kisiasa. Museveni, aliyekua madarakani tangu mwaka 1986, amebainisha mafanikio ya utawala wake na kujitetea dhidi ya lawama zinazotolewa na wapinzani wake.
Katika hotuba yake mbele ya maelfu ya wananchi na viongozi wa kisiasa katika kile kilichoitwa “Siku ya Maadhimisho ya Miaka 40 ya Mapinduzi,” Museveni alisema serikali yake imeleta usalama na mpango wa maendeleo uliothibitisha mafanikio kadhaa ya kiuchumi na kijamii kwa nchi nzima. Alisema utawala wake umekuwa muhimu kwa kuleta mabadiliko tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyompelekea kufika madarakani.
Hata hivyo, hotuba ya Museveni ilijumuisha masuala yanayozua mvutano. Alitaja baadhi ya wapinzani wake kama “magaidi” na “wauaji wa amani,” jambo lililochochea mjadala mkali ndani ya nchi na nje yake juu ya hali ya demokrasia na uhuru wa kisiasa nchini Uganda. Wapinzani na makundi ya haki za binadamu wanasema kauli hizo zinachangia hali ya kutisha na kutoruhusu upinzani wa kweli kisiasa.
Mwezi huu, Museveni alipata ushindi katika uchaguzi wa rais uliokua na utata, akipata zaidi ya asilimia 70 ya kura, matokeo ambayo chama tawala kilitangaza kama ushindi wa wazi, lakini chama cha upinzani kiliipinga matokeo hayo kwa madai ya udanganyifu na udhibiti wa taarifa.
Wafuatiliaji wa kisiasa na vyombo vya habari wametilia shaka mwenendo wa uchaguzi, mabadiliko ya katiba yaliyomuwezesha Museveni kuendelea kuwania madaraka, na hatua za serikali dhidi ya wanaharakati wa upinzani. Hii imeibua mjadala mpana kuhusu mustakabali wa demokrasia nchini Uganda licha ya ahadi ya Museveni ya kuendelea kusukuma maendeleo na utulivu.

Wagombea kutoka Tanzania Bara
Katika nafasi za Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa wanaotokana na Bunge kutoka Tanzania Bara, Kamati Kuu imepitisha:
● Wanaume (nafasi 2): Paul Christian Makonda na Livingstone Joseph Lusinde
● Wanawake (nafasi 1): Asia Abdulkarim Halamga
Wagombea kutoka Zanzibar
Kwa upande wa Zanzibar, walioteuliwa ni:
Wajumbe wa NEC kutoka Bunge:
● Wanaume: Khamis Mussa Omar
● Mwanamke: Tauhida Cassian Galos
Nafasi nyingine za kitaifa
Katika nafasi ya Katibu wa Wabunge wote wa CCM, ameteuliwa Agnes Elias Hokororo.
Kwa nafasi za Wenyeviti wa Bunge, waliopitishwa ni:
● Najma Murtaza Giga
● Deodatus Philippo Mwanyika
● Cecilia Daniel Pareso
Kwa upande wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, walioteuliwa ni pamoja na:
Wajumbe wa NEC kutoka Baraza la Wawakilishi:
● Wanaume: Said Ali Juma na Hamza Hassan Juma
● Mwanamke: Lela Muhamed Mussa
Aidha, Kamati Kuu imepitisha pia majina ya wawakilishi wa CCM watakaoingia Bungeni kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwemo:
● Wanaume: Bakar Hamad Bakar, Dkt. Shaame Ali Ali, na Simai Mohammed Said
● Mwanamke: Fatma Ramadhan Mandoba
Nafasi ya Katibu wa Wawakilishi wote wa CCM imeenda kwa Machano Othman Said, huku nafasi za Wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi zikiwapitisha Mahmoud Omar Hamad na Hudhaima Mbarak Tahir.
Mchakato wa Uchaguzi Mdogo Peramiho
Katika taarifa hiyo, Kamati Kuu imefanya pia uteuzi wa mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho (Mkoa wa Ruvuma), na kumpitisha Dkt. Lazaro Killian Komba kugombea ubunge, kufuatia mamlaka ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 (Toleo la Julai 2025).
CCM yasema ni kuimarisha demokrasia ya ndani
Taarifa hiyo imeeleza kuwa uteuzi huo una lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza ufanisi wa uongozi na kuendeleza misingi ya demokrasia ya ndani ya chama, sambamba na kuhakikisha makundi yote yanapata nafasi stahiki katika vyombo vya maamuzi.
CCM imewahimiza walioteuliwa kuzingatia maadili, umoja na mshikamano, huku ikiwataka wanachama na wananchi kuendelea kukiamini chama katika kuendeleza maendeleo ya taifa.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu, ametuma ujumbe mzito wa rambirambi kufuatia kifo cha Mwenyekiti Mwanzilishi wa chama hicho, Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, akimtaja kama mjenzi wa taifa, kiongozi wa mfano na hazina ya historia ya Tanzania.
Katika ujumbe wake alioutoa akiwa Gereza Kuu la Ukonga, Lissu amesema kifo cha Mzee Mtei ni pigo kubwa si tu kwa familia yake na wanachama wa CHADEMA, bali kwa taifa lote la Tanzania kutokana na mchango wake mkubwa katika ujenzi wa taifa, uchumi na demokrasia.
Lissu ameeleza kuwa marehemu Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa misingi ya uchumi wa Tanzania baada ya uhuru, akihudumu kama Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na baadaye Waziri wa Fedha, ambapo jina na saini yake zilionekana kwenye noti za kwanza kabisa za taifa.
Akizungumzia uadilifu wake, Lissu amesema Mzee Mtei alionesha ujasiri wa kipekee wa kisiasa pale alipothubutu kumshauri Mwalimu Julius Nyerere kubadili sera za kiuchumi za Azimio la Arusha baada ya kubaini kuwa zilikuwa zimeshindwa, na baadaye akaamua kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Fedha kwa misingi ya dhamira na uaminifu kwa nchi.
“Huu ndio uzalendo wa kweli. Mzee Mtei hakutafuta madaraka, bali alisimamia ukweli na maslahi ya taifa,” amesema Lissu katika ujumbe wake.
Kuhusu mchango wake ndani ya CHADEMA, Lissu amesema marehemu alikuwa mfano wa uongozi wa kujitolea, kwani hakuwahi kupokea mshahara, posho wala kunufaika binafsi kupitia nafasi yake ya uongozi ndani ya chama.
Ameongeza kuwa Mtei aliimarisha utamaduni wa uongozi wa kupisha damu changa, alipostaafu uenyekiti wa chama mwaka 1998 akiwa na umri wa miaka 66, jambo linaloendelea kuifanya CHADEMA kuwa chama chenye misingi ya kidemokrasia.
Lissu pia amemsifu marehemu kwa kuchapisha kitabu chake cha maisha “From Goatherd to Governor” mwaka 2009, akisema kitabu hicho kimekuwa hazina muhimu ya historia ya kisiasa na kiuchumi ya Tanzania.
Akihitimisha ujumbe wake, Lissu amesema badala ya kuomboleza kifo cha Mtei, Watanzania wanapaswa kusherehekea maisha yake yenye maana, busara na mchango mkubwa kwa taifa, huku akimuombea apumzike kwa amani.




.jpeg)



.jpg)














