Articles by "SIASA"
Showing posts with label SIASA. Show all posts

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Uboreshaji wa Daftari utafanyika Mkoa wa Tanga kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza sambamba na Mkoa wa Pwani kuanzia Februari 13 hadi 19,2025 ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.


Akizungumza na Maafisa hao Mhe. Jaji Mwambegele aliwasisitiza kutambua umuhimu wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kitaifa na kuwahimiza pia kushirikiana na wadau wa Uchaguzi wakiwepo Vyama vya Siasa alivyovitaka vihakikishe vinateua mawakala katika kila kituo ili waweze kusaidia kuwatambua wananchi kutoka maeneo husika.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo tarehe 07 Februari, 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira, amewataka watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ngazi Kata, kuwa waadilifu wakati wote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Mhe.Rwebangira ametoa maelekezo hayo leo Februari 07, 2025, alipotembelea mafunzo kwa watendaji hao katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, unaotarajiwa kuanza Februari 13, 2025 hadi Februari 19, 2025, katika mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.


Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.




Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Jiji la Tanga , Mwanaidi Nondo, akiwa katika mafunzo hayo.




Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.










Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.





Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo Februari 07 , 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.




Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar akitembelea mafunzo ya kwa vitendo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.
 
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV.

TUNDU Lissu ameibuka mshindi katika nafasi ya Mwenyekiti Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) dhidi ya mpinzani wake ambaye mtangulizi wake, Freeman Mbowe aliyekuwa anatetea nafasi yake.

Katika ukurasa wake wa Mtandao kijamii wa X, Mbowe ameandika ujumbe wa kukubali kushindwa kwa kusema "Nimepokea kwa mikono miwili maamuzi ya Uchaguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama chetu CHADEMA uliohitimishwa leo asubuhi 22 Januari 2025. Nampongeza Mhe. Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la Uongozi wa Chama",

Mbowe ameikiongoza Chama tangu alipochaguliwa nafasi hiyo mwaka 2004 akirithi mikoba ya Bob Makani aliyeongoza chama hicho kuanzia mwaka 1999. Tundu Lissu nae amekuwa kwenye Chama hicho kwa zaidi ya miaka 20 huku akishika nafsi mbalimbali za uongozi ndani ya Chama ambapo kabla ya uchaguzi huu alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu) Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu) Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar.
Mwenyekiti wa Mafunzo, Bw. Khalid Khalif akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Na Mwandishi wetu, Songea
Watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura mkoani Ruvuma wametakiwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao baadae mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Zakia Mohamed Abubakar kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu) Dkt. Rose Likangaga wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji hao mkoani Ruvuma.

“Mnahimizwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.

Dkt Likangaga akisoma hotuba hiyo alisema ni matarajio ya Tume kuwa, mara baada ya zoezi hili lililopo mbele yao kukamilika watu watakaokuwa wamepatiwa kadi watakuwa ni Wapiga Kura Halali.

Aidha alisema, jukumu la uhamasishaji linawahusu moja kwa moja wao watendaji kwa kushirikiana na wadau wengine katika maeneo yao kupitia nyenzo walizonazo.

“Ninasisitiza kwamba, mabango na vipeperushi mtakavyopewa na Tume mvisambaze mapema katika kata zote zilizopo katika halmashauri zenu. Kazi yenu kubwa ni kusimamia na kuendesha shughuli zote za uboreshaji katika halmashauri zenu,”ilisisitiza hotuba hiyo.

Watendaji hao wameatakiwa kuisoma kwa umakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Sheria za Uchaguzi, Kanuni za Uboreshaji, Maelekezo na Miongozo yote inayotolewa na Tume ili kazi yao ifanyike kwa uadilifu na haki.

Pia wametakiwa kuwasiliana na Tume kwa ajili ya ufafanuzi wa masuala yote yanayohusiana na utekelezaji wa majukumu yao pindi wanapokutana na changamoto zozote.

“Tume imetekeleza jukumu lake katika hatua ya mafunzo na hivyo nanyi mna wajibu wa kuhakikisha kuwa mnatekeleza kikamilifu majukumu yote mliyokasimiwa,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.

Pia Tume imewataka watendaji hao kuwa makini katika kila eneo la usambazaji na utunzaji wa vifaa na muda sahihi wa ufunguaji na ufungaji wa vituo vya kuandikishia wapiga kura.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unataraji kuanza Januari 12 hadi 18, 2025 katika mikoa ya Songwe, Njombe, Rukwa na Ruvuma kwenye Halmashauri za Wilaya ya Nyasa, Mbinga, Mbinga Mji, Wilaya ya Songea na Manispaa ya Songea ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

Mafunzo hayo yaliwahusisha Maafisa Waandikishaji,Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi, Maafisa TEHAMA wa Halmashauri.


Washiriki wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea

mmoja wa wakufunzi akitoa maelekezo wakati wa mafunzo kwa vitendo.

Washiriki wakifanya mafunzo kwa vitendo.
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Kilimanjaro.


Washiriki wa mafunzo kutoka Mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Arusha.
******************Na Waandishi wetu, Arusha, Kilimanjaro na Dodoma
Watendaji wa uchaguzi kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Dodoma leo tarehe 30 Novemba, 2024 wamepatiwa mafunzo ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ikiwa ni maandalizi ya kuanza kwa zoezi la uboreshaji wa daftari hilo katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, na Halmashauri za Wilaya ya Kondoa, Kondoa Mji na Chemba. Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 11 hadi 17 Desemba, 2024.

Akifungua mafunzo hayo jijini Arusha, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele, amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa watendaji hao kwa sababu ujuzi na elimu watakayopata itawawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kufanikisha uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

“Mafunzo haya yanalenga kuwajengea umahiri watendaji wetu ili waweze kuwafundisha Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata, ambao nao watatoa mafunzo kwa Waendeshaji wa Vifaa vya Bayometriki na Waandishi Wasaidizi, ambao ndio watakaohusika moja kwa moja na uandikishaji wa wapiga kura katika vituo,” amesema Jaji Mwambegele.

Pia, Jaji Mwambegele amesisitiza umuhimu wa kutumia uzoefu wa watendaji waliowahi kushiriki katika mchakato wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ili kusaidia wenzao ambao hawajawahi kushiriki katika zoezi kama hili, na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Katika mkoa wa Kilimanjaro, mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi ngazi ya mkoa yalifunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Mbarouk Salim Mbarouk (Mstaafu). Akizungumza katika ufunguzi, Jaji Mbarouk amesisitiza kuwa mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya kuandikishaji wapiga kura, lakini ameonya kuwa hawataruhusiwa kuingilia mchakato wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu.

“Kwa madhumuni ya kuleta uwazi, mawakala wa vyama vya siasa watasaidia kutambua waombaji wapiga kura katika maeneo yao, jambo litakalosaidia kupunguza vurugu zisizohitajika,” amesema Jaji Mbarouk. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa watendaji wa uchaguzi kutoa ushirikiano kwa mawakala hao na kuhakikisha maelekezo ya Tume yanafuatwa ipasavyo.

Vilevile, mafunzo hayo yalifanyika mkoani Dodoma, ambapo Mjumbe wa Tume na Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Asina Omari, alifungua mafunzo hayo katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Jaji Asina amesisitiza umuhimu wa utunzaji wa vifaa vya uandikishaji, akisema kuwa kutokuwa makini katika utunzaji wa vifaa hivi kutapelekea athari kubwa katika ukamilishaji wa zoezi hili muhimu.

“Vifaa vya uandikishaji vimenunuliwa kwa gharama kubwa, hivyo ni lazima tuvisimamie kwa umakini na kuhakikisha vinatumika ipasavyo katika maeneo yote ya uandikishaji,” amesema Jaji Asina.

Mafunzo hayo yamehudhuriwa na maafisa waandikishaji, maafisa TEHAMA, pamoja na maafisa ugavi kutoka halmashauri mbalimbali za mikoa hiyo. Washiriki walipata ujuzi wa jinsi ya kutumia mfumo wa Voters Registration System (VRS) pamoja na vifaa vya kisasa vitakavyotumika katika vituo vya kuandikishia wapiga kura. Vilevile, walifundishwa namna ya kukabiliana na changamoto za kiufundi zinazoweza kutokea wakati wa zoezi la uandikishaji.

Washiriki wa mkoa wa Arusha wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mafunzo.
Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji, Adrian Ntambala akiwasilisha mada kuhusu uraia kwa washiriki wa mafunzo mkoa wa Arusha.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Asina Omari akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Dodoma.



Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa Halmashauri wakila kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo yao leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Dodoma.


Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa Halmashauri wakila kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo yao leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Kilimanjaro.
Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa Halmashauri wakila kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo yao leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Kilimanjaro.
Meza kuu wakati wa mafunzo

Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa Halmashauri wakila kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo yao leo Novemba 30 hadi Disemba 1, 2024 Mkoani Arusha.