Articles by "SIASA"
Showing posts with label SIASA. Show all posts
-Asisitiza uadilifu na uwajibikaji kwa mali za umma

-Apongeza Serikali Njombe mrejesho kwa wananchi, chama kwa usimamizi

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, amesema kazi kubwa iliyofanywa na Serikali, chini ya uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ndani ya miaka mitatu, ni nyezo inayobeba ukweli wa kutosha kusambaratisha uongo unaoenezwa na baadhi ya wapinzani wa kisiasa kupitia mikusanyiko yao.

Amewataka wana-CCM wote kuendelea kujiamini na kutembea kifua mbele wanapozisema, kuzitangaza na kuikumbusha jamii kuhusu kazi za maendeleo na ustawi wa jamii, zinazofanywa na Serikali za CCM ili wananchi waendelee kuuona ukweli, wakitofautisha na uongo unaoenezwa kwa propaganda nyepesi za kisiasa.

Balozi Nchimbi amesema hayo leo, Aprili 19, 2024, alipokuwa akiwahutubia maelfu ya wanaCCM wa Mkoa wa Njombe, kupitia Mkutano Maalum wa Mkoa, uliofanyika mjini Njombe.

“Mambo yaliyofanywa na Serikali ndani ya hii miaka mitatu, unaweza kuona kama ni miujiza. Kazi kubwa sana inafanyika. Ni wajibu wetu kuitumia nyenzo yenye ukweli kupambana,” amesema.

Kupitia mkutano huo, ambao Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Antony Mtaka aliwasilisha taarifa ya mrejesho wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 - 2025, iliyohusisha miradi mbalimbali ya maendeleo na ustawi wa wananchi, Balozi Nchimbi pia amerudia kusisitiza kwa watendaji wa Chama na Serikali ulazima na umuhimu wa kuwa waadilifu wakati wote kwenye masuala yanayohusu rasilimali za umma, kwa kupiga vita rushwa na ubadhirifu.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024.

Na Munir Shemweta, MLELE

Mbunge wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Mhe, Pinda amefanya ukaguzi wa jengo hilo leo tarehe 10 April 2024 akiwa njiani kielekea jimboni kwake Kavuu halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi kusheherekea Siku Kuu ya Eid El Fitri na waumini wa dini ya kiislamu katika jimbo lake sambamba na kukagua shughuli za maendeleo.

Mhe, Pinda akiambatana na Mkuu wa wilaya ya Mlele Alhaji Majid Mjengwa ameoneshwa kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo la CCM ambalo mbali na ofisi, litakuwa na ukumbi wa mikutano.

"Niwapongeze kwa kazi nzuri, naona jengo limefikia katika hatua nzuri na muda si mrefu wilaya yetu itakuwa na jengo lake zuri, hongereni sana" alisema Mhe. Pinda.

Kwa mujibu wa Mbunge wa Jimbo la Kavuu, ujenzi wa jengo hilo la CCM wilaya ya Mlele ni juhudi binafsi za yeye pamoja na mbunge mwenzake wa jimbo la Mlele Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe.

Amesema, kukamilika kwa jengo hilo kutawawezesha watendaji wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mlele kuwa na ofisi nzuri na hivyo kufanya kazi zao kwa ifanisi.

Akiwa jimboni kwake Mhe, Pinda mbali na kujumuika na waumini wa dini ya kiislamu katika kusheherekea Siku Kuu ya Eid El Fitri na kukagua shughuli za maendeleo katika jimbo lake pia atashiriki ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Balozi Dkt Emanuel Nchimbi anayetarajiwa kufanya ziara mkoa wa Katavi mwishoni mwa wiki.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akisisitiza jambo wakati wa kukagua maendeleo ya ujenzi jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024. Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mlele Alhaji Majid Mjengwa.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ndg. Mary Chatanda kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali wametoa mafunzo maaalum kwa viongozi wanawake kutoka mikoa 9 ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Ziwa Magharibi. Dhima kuu ikiwa ni kuwajengea uwezo Wanawake namna ya kutumia matokeo ya Sensa katika kuchochea maendeleo sanjari na Kuleta ufanisi wa Utendaji wa kazi katika kujikwamua kiuchumi na kijamii.

Mafunzo hayo ya Siku moja yamehusisha viongozi wanawake pamoja na Waheshimiwa Madiwani Viti Maalum kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera, Katavi, Shinyanga, Simiyu, Geita, Kigoma, Tabora pamoja na Mkoa wa Mara leo tarehe 27/3/2024 Katika Ukumbi wa Winterfell Mkoani Mwanza.

Kadharika mafunzo hayo yamehudhuriwa na Mhe. Anne Makinda Spika Mstaafu wa Bunge La Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamisaa wa Sensa, Katibu Mkuu wa UWT Ndg. Jokate Mwegelo, Naibu katibu Mkuu UWT Bara Ndg. Riziki Kingwande pamoja na Mhe. Amina Makilagi Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji (Rufaa) Mhe. Jacobs Mwambegele akizungumza jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Machi, 2024 wakati akitoa Risala ya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika kata 22 za Tanzania Bara.
***********Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.
Wagombea Udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa Kura katika Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika kata 22 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika kesho tarehe 20 Machi, 2024.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji (Rufaa) Mhe. Jacobs Mwambegele jijini Dar es Salaam wakati akitoa Risala ya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani katika kata 22 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele amesema kati ya wagombea hao 127 wagombea wanaume ni 89 na wanawake ni 38 na kuongeza kuwa wapiga kura 128,157 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi huo mdogo na jumla ya vituo 373 vya kupigia kura vitatumika.

"Tume inatoa pongezi kwa wadau wote wakiwemo wapiga kura na wananchi katika kata (22) zenye uchaguzi kwa utulivu waliouonesha wakati wote wa kipindi cha kampeni,” amesema Jaji Mwambegele.

Jaji Mwambegele wasimamizi wa uchaguzi katika kata husika wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi.

"Mawakala wanawajibika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao na katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu za uchaguzi na Maelekezo ya Tume.", amefafanua Jaji Mwambegele.

Aliwataka wapiga kura katika uchaguzi huu mdogo, kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya kupigia kura hapo kesho, ili kuwachagua viongozi wanaowataka huku akivikumbusha vyama vya siasa, wagombea na wadau wengine wa Uchaguzi kujiepusha na vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani.

"Mafanikio ya uchaguzi huu yatatokana na kuwepo kwa hali ya utulivu na amani katika maeneo yote yenye uchaguzi. Hivyo, Tume inatarajia kuona hali ya amani na utulivu iliyopo sasa inaendelea kuwepo hadi shughuli za uchaguzi zitakapokamilika.", aliongeza Jaji Mwambegele.

Alivikumbusha vyama vya siasa, wagombea, mawakala, wapiga kura na wananchi wote kwa ujumla kuzingatia kuwa kampeni za uchaguzi mdogo wa Udiwani katika kata 22, zinahitimishwa rasmi leo tarehe 19 Machi, 2024, hivyo vyama vya siasa, wagombea na wafuasi wao hawatakiwi kufanya kampeni za aina yeyote zaidi ya saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni ya leo.

Ametaja mambo mengine ambayo hayaruhusiwi kufanyika baada ya saa 12:00 na siku ya uchaguzi kuwa ni pamoja na kutumia alama za vyama vya siasa zinazoashiria kampeni kama vile vipeperushi, bendera na mavazi na kwamba upigaji kura katika maeneo yote ya uchaguzi, utafanyika katika vituo vile vile vilivyotumika wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.

Alikumbusha kuwa vituo vya Kupigia Kura vitafunguliwa saa moja kamili (1:00) asubuhi na kufungwa saa kumi kamili (10:00) jioni. Iwapo, wakati wa kufunga kituo watakuwepo wapiga kura katika mstari ambao wamefika kabla ya saa kumi kamili jioni (10:00) na hawajapiga kura, wataruhusiwa kupiga kura na mtu yeyote hataruhusiwa kujiunga katika mstari wa wapiga kura baada ya saa kumi kamili (10:00) jioni.

"Watakaoruhusiwa kupiga kura ni wale tu ambao wamo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye kata husika na wana kadi zao za mpiga kura. Hata hivyo, Tume kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 62 (a) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, imeruhusu wapiga kura ambao wamepoteza kadi zao au kadi kuharibika kutumia vitambulisho mbadala kama vile, Pasi ya Kusafiria, Leseni ya Udereva au Kitambulisho cha Uraia kinachotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili mradi majina yaliyopo katika vitambulisho hivyo, yawe sawa na yaliyokuwepo katika kadi ya mpiga kura.", amefafanua Jaji Mwambegele na kuongeza kuwa:

"Mpiga Kura aliyepoteza kadi yake au kadi yake kuharibika ataruhusiwa kutumia kitambulisho mbadala, iwapo tu; atakuwa ameandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na jina lake lipo katika orodha ya wapiga kura katika kituo anachokwenda kupiga kura. Aidha, majina yake yaliyopo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yawe yanafanana na yale yaliyopo katika kitambulisho mbadala."

Jaji Mwambegele alieleza kuwa kutakuwa na majalada ya nukta nundu katika vituo vya kupigia kura kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye uoni hafifu na wenye ulemavu wa kuona ili yawasaidie kupiga kura bila usaidizi na kwa wapiga kura wenye ulemavu wa kuona na ambao hawawezi kutumia majalada hayo, wataruhusiwa kwenda vituoni na watu ambao wanawaamini na ambao watawachagua wenyewe kwa ajili ya kuwasaidia kupiga kura.

Kuhusu kipaumbele kwa wapiga kura, Jaji Mwambegele alisema katika vituo vya kupigia kura, kipaumbele kitatolewa kwa wagonjwa, watu wenye ulemavu, wazee, wajawazito na akina mama wanaonyonyesha watakaofika na watoto wao vituoni.

Alisisitiza kuwa kwa mujibu wa maelekezo yaliyomo kwenye Maadili ya Uchaguzi ya Mwaka 2020, wapiga kura watatakiwa kuondoka vituoni mara tu baada ya kupiga kura. Hivyo, Tume inawashauri wananchi kujiepusha na mikusanyiko katika maeneo ya vituo vya kupigia kura.

Kata zinazofanya uchaguzi ni Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Mshikamano (Halmashauri ya Manispaa ya Musoma), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga), Fukayosi (Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

Kata nyingine ni Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu), Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga)."
Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam.

Na Mroki Mroki

TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Machi 20,2024 kuwa ni siku ya kupiga kura katika Uchaguzi Mdogo wa udiwani katika Kata 23 za Tanzania Bara.

Tume ilitangaza uchaguzi huo baada ya kuketi katika kikao chake cha Februari 15 mwaka huu na siku hiyohiyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akatoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa uchaguzi huo mdogo.

Tayari mchakato wa Uchaguzi huo umeshaanza ambapo Februari 27 hadi Machi 4, 2024 wagombea walichukua fomu za uteuzi, uteuzi ulifanyika Machi 4,2024 na kampeni za uchaguzi zilianza Machi 5,2024 na zinaendelea hadi tarehe 19 Machi, 2024.

Hata hivyo, baada ya hatua ya uteuzi, Kata ya Nkokwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ilipata mgombea mmoja tu aliyeteuliwa bila kupingwa hivyo hakutakuwa na kampeni kwenye Kata hiyo. Hivyo, uchaguzi utafanyika kwenye kata 22 zilizobakia.

Kata zitakazofanya uchaguzi huo mdogo ni Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Fukayosi(Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

Nyingine ni Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Mshikamano (Halmashauri ya Manispaa ya Musoma), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu) Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga).

Katika Uchaguzi huu wa Kata 22, Vyama vya siasa 18 vimesimamisha wagombea 127 kati ya hao wanaume ni 89 na wanawake ni 38. Wagombea kutoka kwenye vyama hivyo walichukua fomu za uteuzi na kuzirejesha na hatimaye wakateuliwa kuwania nafasi hiyo.
Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam.

Wagombea wote wameaminiwa na kupewa ridhaa na vyama vyao vya siasa kuwania nafasi zilizowazi, kwa kufanya hivyo, vyama hivyo vya siasa vimewatendea haki wanachama wao na wananchi kwa ujumla kwa kuwa wamepata haki ya kikatiba ya kugombea lakini pia wanachama na wananchi, watapata haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na kuwachagua viongozi wanaowataka.

Wagombea walioteuliwa na Tume ni wale waliopendekezwa na vyama vyao vya siasa kugombea kiti cha udiwani ambapo pia walijaza na kuwasilisha fomu za uteuzi katika Ofisi za Uchguzi katika Kata husika.

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata walisimamia vyema majukumu yao ya kutoa fomu za uteuzi. Fomu za uteuzi za wagombea wote ziliwasilishwa siku ya uteuzi kabla ya saa kumi kamili (10:00) jioni.

Wagombea hawa wote siku ya uteuzi walijaza na kusaini mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Fomu Na. 10 ya maadili ya uchaguzi.

Wagombea hawa walijaza fomu hizo kukiri kuheshimu na kuyazingatia maadili ya uchaguzi yaliyosainiwa na viongozi wa vyama vyao mwaka 2020 wakati wa uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Madiwani kwa Tanzania Bara.

Uwepo wa maadili ya Uchaguzi unalenga hasa kuwa na uchaguzi huru, wa haki, uwazi na wa kuaminika. Na kwamba amani, ustawi wa nchi, usalama wa raia, uhuru wa vyama vya siasa na utii wa sheria , kanuni na taratibu za uchaguzi ndio msingi wa uchaguzi ulio huru, haki na wenye kuzingatia ushiriki wa makundi yote ya jamii katika uchaguzi.

Vyama vya Siasa, Serikali na Tume walikubaliana kuwajibika kuyatekeleza Maadili hayo yanayotokana na kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343. Viongozi hao kwa pamoja walisema “Tutafanya jitihada za wazi kuhakikisha Maadili haya yanajulikana na kuheshimiwa na wagombea pamoja na wanachama wote wa vyama vya siasa”.

Sheria, Kanuni na miongozo yote iliyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 bado inatumika na kufuatwa na vyama vya siasa, Tume ya Taifa ya Uchagzi na Serikali katika chaguzi hizi ndogo za udiwani.

Tayari Kampeni za uchaguzi zimeanza tangu siku moja baada ya uteuzi na zitaendelea hadi siku moja kabla ya siku ya kupiga kura.

Wakati wote wa kampeni wagombea wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni za uchaguzi, Maadili ya Uchaguzi na ratiba za kampeni.

Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi na ratiba za kampeni utasaidia katika kuweka uwanja sawa katika kipindi chote cha kampeni na siku ya uchguzi.

Vyama vya Siasa na wagombea pamoja na wafuasi wao wanapaswa kuepuka kufanya siasa za fujo na za vitisho dhidi ya upande mwingine.

Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 4C cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, imepewa jukumu la kutoa elimu ya mpiga kura nchi nzima, kuratibu na kusimamia taasisi au asasi za kiraia zinazotoa elimu hiyo.

Tume itatoa elimu kwa wananchi katika maeneo yote ambayo yanafanya uchaguzi mdogo. Lakini pia zipo asasi ambazo zimepewa kibali na Tume kutoa elimu hiyo kwa baadhi ya maeneo.

Elimu hiyo inayotolewa ni ile ya kumuwezesha Mpiga Kura kutambua sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kufunguliwa na kufungwa kwa vituo vya kupigia kura.

Lakini pia elimu hiyo itasaidia kutoa hamasa kwa wananchi kutumia haki yao ya kikatiba katika kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka.

Ni muhimu wananchi katika maeneo yote yanayofanya uchaguzi mdogo wakajitokeza kwa wingi kusikiliza sera za vyama na wagombea kisha kwa utashi wao wachague viongozi wanaowafaa kujaza nafasi zilizowazi katika Kata 23 za Tanzania Bara.

Mwandishi wa Makala haya ni Afisa Habari Msaidizi Mwandamizi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi amesema dhamira ya Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha nchi inaongozwa kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na utawala bora na hivyo haipaswi kutiliwa shaka hata kidogo.

Balozi Nchimbi amesema katika utekelezaji wa dhana ya utawala bora, chini ya uongozi wa Rais Samia, Tanzania imeendelea kushuhudia kuwapo kwa uhuru wa mihimili mitatu ya dola, ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama.

Amesema mihimili hiyo ya dola imeendelea kutimiza wajibu wake kwa kufanya kazi vizuri na hivyo kuaminiwa na wananchi.

Balozi Nchimbi amesisitiza kuwa CCM chini ya Rais Samia, kitahakikisha dhamira hiyo pia inaendelezwa kwa vitendo kwa kuunga mkono uwapo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar kwa maslahi ya nchi na taifa kwani umoja huo ni zaidi ya vyama vya siasa.

Katibu Mkuu huyo wa CCM amesema hayo Jumanne, Machi 5, 2024, alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini, Michael Battle, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi hao walijadiliana masuala anuai kuhusu ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.

Katika mazungumzo yao, wamekubaliana nchi zote mbili kuangalia maeneo yanayoweza kuboreshwa kwa manufaa ya pande zote mbili hasa katika nyanja za biashara, uchumi na uwekezaji.

Vilevile, viongozi hao kwa pamoja wameelezea umuhimu wa kurahisishwa kwa upatikanaji viza.

“Ni wajibu wetu kuimarisha na kuuboresha uhusiano huu wa muda mrefu kama tulivyoupokea kutoka kwa waasisi na watangulizi wetu kama ulivyosema balozi. Tuuboreshe kwa ajili ya manufaa ya wananchi wetu wa pande zote mbili,'' anasema Balozi Nchimbi.

Naye Balozi Battle aliupongeza uongozi wa Rais Samia kwa jinsi ambavyo umekuwa wa wazi, imara na jasiri katika kusimamia misingi ya demokrasia na utawala bora.

“Kama unavyojua uhusiano huu ni wa muda mrefu, ukaboreshwa zaidi na urafiki uliokuwapo kati ya (Mwalimu) Nyerere na (John) Kennedy. Lakini pia kulikuwa na ukaribu kati ya (Jakaya) Kikwete na (George) Bush…na sasa tunaona ukaribu kati ya Rais Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Rais (wa Marekani) Kamala Harris. Napenda kukuhakikishia na ujue kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani ni mkubwa na halisi,” amesema Balozi Battle.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Michael Battle, walipokutana Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, kujadiliana masuala mbalimbali yanayohusu uhusiano kati ya Tanzania na Marekani, Machi 5, 2024.

Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Kata ya Kimbiji, Bw. Ricky Pascal na Bi. Twidike Ntwima wakibandika fomu za utezi wa wagombea wa udiwani Kata ya Kimbiji leo baada ya muda wa uteuzi kumalika Saa 10:00 jioni ya Machi 4,2024. Wagombea 14 waliochukua fomu wameteuliwa kuwania nafasi hiyo. Wagombea wa Udiwani Kata ya Kimbiji wakitazama fomu za uteuzi zilizobandikwa katika ubao wa Matangazo katika Ofisi za Kata ya Kimbiji. Wagombea 14 waliochukua fomu wameteuliwa kuwania nafasi hiyo.
Wagombea wa Udiwani Kata ya Kimbiji wakitazama fomu za uteuzi zilizobandikwa katika ubao wa Matangazo katika Ofisi za Kata ya Kimbiji. Wagombea 14 waliochukua fomu wameteuliwa kuwania nafasi hiyo.


Wagombea wakikabidhiwa fomu zao za uteuzi baada ya Tume kuwateua kuwa wagombea udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mdogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.

Wagombea wakikabidhiwa fomu zao za uteuzi baada ya Tume kuwateua kuwa wagombea udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mdogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.
Wagombea wakikabidhiwa fomu zao za uteuzi baada ya Tume kuwateua kuwa wagombea udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mdogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.


Wagombea wakikabidhiwa fomu zao za uteuzi baada ya Tume kuwateua kuwa wagombea udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mdogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.



Wagombea wakikabidhiwa fomu zao za uteuzi baada ya Tume kuwateua kuwa wagombea udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mdogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.

Na Mwandishi Wetu, Kigamboni.

Wagombea 14 waliochukua fomu za utezi kuwania udiwani Kata ya Kimbiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dares Salaam wamerejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi Mfogo wa udiwani uyakaofanyika Machi 20,2024.

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Kimbiji, Bw.Ricky Pascal alisema wagombea hao walianza kuchukua fomu za uteuzi kama Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilivyopanga Februari 27,2024 hadi leo Machi 4,2024 na wote kukamilisha ujazaji fomu na kuzirejesha.

"Wagombea wote waliochukua fomu za uteuzi Kata ya Kimbiji wamerejesha fomu na kutimiza matwaka ya ujazaji fomu, hivyo wagombea wote 14 wameteuliwa na tume kuwania nafasi ya Udiwani katika uchaguzi utakaofanyika Machi 20,2024,"alisema Pascal.

Pascal aliwataja wagombea walioteuliwa kuwa ni Bi. Rachel Paulo Mwikola (UPDP), Bi. Halima Abdallah Mbago (NLD), Bw. Shabani Hassan Chumu ( Demokrasia Makini), Bw. Kondo Abdu Hatibu 'Lukali' (CUF), Bi. Diana-Rose Joseph Mhoja (ADA Tadea), Bi. Maimuna Mwinyipingu Yusufu (CCM) na Bi. Shani Ally Kitumbua (AAFP),

Wengine ni Bw. Michael Makile Mzalendo (UDP), Joyce Ephraimu Mweigule (DP),Bi. Janeth Pius Mhando (TLP),Nasra Twalib Kimo,Bw. Innocent Fratern Shirima (CCK), Neema Kassimu Yegeyege (UMD) na Juma Hassan Abdalah (NCCR-Mageuzi.
Wagombea hao walikabidhiwa fomu zao za uteuzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Kata ya Kimbiji, Bw. Ricky Pascal na Bi. Twidike Ntwima.

Tume ilitangaza uchaguzi Mdogo katika Kata 23 za Tanzania bara kufanyika Machi 20,2024 na fomu za uteuzi zilianza kutolewa Februari 27 hadi Machi 4 mwaka huu.

Mbali na Kata Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kata zingine zinazofanya uchaguzi ni Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Fukayosi (Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

Nyingine ni Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Mshikamano (Halmashauri ya Wilaya ya Musoma), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Nkokwa (Halmashauri ya Wilaya ya Kyela), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu) Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga).
Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji Rufaa (Mstaafu) Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati akifunga mafunzo kwa watendaji wa Uchaguzi ambao wanakwenda kusimamia uchaguzi mdogo katika Kata 23 za Tanzania Bara yaliyofanyika kwa siku tatu mkoani Morogoro. Uchaguzi unataraji kufanyika Machi 20,2024.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasiliamaliwatu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Silas Marwa akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uchaguzi.
Mwenyekiti wa Mafunzo hayo, ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Hamlmashauri ya Mji wa Kibaha, Eng. Mshamu Ally Munde akizungumza kwa niaba ya washiriki.
Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mhe. Jaji George Kazi na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa ZEC Thabit Idarous Faina (kushoto) wakifuatilia ufungaji wa mafunzo.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo kwa watendaji wa Uchaguzi mdogo wa udiwani kwa Kata 23 za Tanzania bara yaliyofanyika mkoani Morogoro kwa siku tatu. Uchaguzi unataraji kufanyika Machi 20,2024.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo kwa watendaji wa Uchaguzi mdogo wa udiwani kwa Kata 23 za Tanzania bara yaliyofanyika mkoani Morogoro kwa siku tatu. Uchaguzi unataraji kufanyika Machi 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo kwa watendaji wa Uchaguzi mdogo wa udiwani kwa Kata 23 za Tanzania bara yaliyofanyika mkoani Morogoro kwa siku tatu. Uchaguzi unataraji kufanyika Machi 20,2024.
********************
Na Mwandishi wetu, Morogoro.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewakumbusha watendaji wa uchaguzi kwenye uchaguzi mdogo wa kata 23 za Tanzania Bara kukamilisha maandalizi muhimu kwa wakati ili kuwezesha uchaguzi huo kufanyika kwa ufanisi.

Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji Rufaa (Mstaafu) Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk leo tarehe 22 Machi, 2024 wakati akifunga mafunzo kwa watendaji hoa yalifanyika mkoani Morogoro.

Uchaguzi huo utafanyika tarehe 20 Machi, 2024 ambapo fomu za uteuzi zitatolewa kuanzia tarehe 27 Februari, 2024 hadi tarehe 04 Machi, 2024, uteuzi wa wagombea utafanyika tarehe 04 Machi, 2024 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 05 hadi 19 Machi, 2024.

“Mnatakiwa kukamilisha mambo yote muhimu yanayotakiwa kwenye mchakato wa uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kubandika matangazo na mabango mbalimbali ya kisheria kuhusiana na uchaguzi kwa mujibu wa maelekezo,” amesema Jaji Mbarouk.

Aliwakumbusha watendaji hao kuwa wapo wadau mbalimbali wa uchaguzi kama vile vyama vya siasa, wananchi na watazamaji ambao wanafuatilia uendeshwaji wa uchaguzi na kiwango cha uzingatiwaji wa sheria zinazohusiana na uchaguzi. Hivyo, ni muhimu wakatekeleza kila hatua na kila jambo linalotakiwa kwa mujibu wa kalenda ya uchaguzi.

“Jukumu lililopo mbele yetu ni kubwa na muhimu na linahitaji umakini, na kujitoa, na hasa baada ya kupatiwa mafunzo haya, mtatekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na weledi mkizingatia ratiba ya utekelezaji ili kufanikisha uchaguzi wa tarehe 20 Machi, 2024,” Jaji Mbarouk amewaambia watendaji hao.

Amesisitiza juu ya umuhimu wa watendaji hao kutenga sehemu ya muda wao kusoma Katiba, Sheria na Maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ili yawaongoze katika kusimamia uchaguzi utakaokuwa huru na wa haki.

Kata zitakazofanya uchaguzi huo mdogo ni Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Fukayosi (Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

Nyingine ni Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Mshikamano (Halmashauri ya Wilaya ya Musoma), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Nkokwa (Halmashauri ya Wilaya ya Kyela), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu) Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga).
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza leo wakati wa kufungua mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi katika uchaguzi mdogo wa Kata 23 unaotaraji kufanyika Machi 20,2024. Mafunzo hayo ya watendaji wa uchaguzi yanayofanyika Mkoani Morogoro.

Watendaji wa uchaguzi wanaohudhuria mafunzo ya siku tatu yaliyoanza leo Februari 20,2024 hadi Februari 23,2024 wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi aliyekua akifungua mafunzo hayo Mkoani Morogoro.


Watendaji wa uchaguzi wanaohudhuria mafunzo ya siku tatu yaliyoanza leo Februari 20,2024 hadi Februari 23,2024 wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi aliyekua akifungua mafunzo hayo Mkoani Morogoro.


Watendaji wa uchaguzi wanaohudhuria mafunzo ya siku tatu yaliyoanza leo Februari 20,2024 hadi Februari 23,2024 wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi aliyekua akifungua mafunzo hayo Mkoani Morogoro.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Aisha Hassan Waziri akiwaapisha watendaji wa Uchaguzi watakaoshiriki katika Uchaguzi Mdogo wa Udiwani wa Kata 23 za Tanzania bara. Watendaji hao wamekula kiapo cha kutunza Siri na kujitoa uanchama wakati wa mafunzo yao ya siku tatu yanayofanyika Mkoani Morogoro kuanzia leo Februari 20 hadi 23,2024.

Watendaji wa Uchaguzi watakaoshiriki katika Uchaguzi Mdogo wa Udiwani wa Kata 23 za Tanzania bara wakila kiapo cha kutunza Siri na kujitoa uanchama wakati wa mafunzo yao ya siku tatu yanayofanyika Mkoani Morogoro kuanzia leo Februari 20 hadi 23,2024.
************Na Mwandishi wetu, Morogoro
Watendaji wa uchaguzi kwenye uchaguzi mdogo wa kata 23 za Tanzania Bara uliotangazwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wametakiwa kuwashirikisha kwa ukaribu wadau wa uchaguzi kwenye maeneo yao.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele leo Februari 20, 2024 wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yanayofanyika Mkoani Morogoro.

Uchaguzi huo utafanyika Machi 20, 2024 ambapo fomu za uteuzi zitatolewa kuanzia Februari 27, 2024 hadi Machi 4, 2024, uteuzi wa wagombea utafanyika Machi 4, 2024 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Machi 5 hadi 19, 2024.

“Napenda niwakumbushe na kuwasisitiza kuwa, wakati wote wa mchakato wa uchaguzi , ni vema mkavishirikisha kwa karibu vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika maeneo yenu kuhusu masuala ya kiuchaguzi ambayo wanastahili kushirikishwa kwani jambo hilo litawarahisishia utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Jaji Mwambegele.

Pia, amekumbusha juu ya umuhimu wa kuvipatia vyama vya siasa orodha ya vituo vya kupigia kura ili kuviwezesha kupanga mawakala.

Ameongeza kuwa ni muhimu kwa watendaji hao wa uchaguzi, kuhakikisha wanayatambua na kuyajua vyema maeneo ambayo uchaguzi utaendeshwa ikiwemo miundombinu ya kufika katika kata na vituo vya kupigia kura.
Jaji Mwambegele alisisitiza kuhusu umuhimu wa kufanya utambuzi na kukagua vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika kwa lengo la kuhakikisha mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Mwenyekiti huyo wa Tume amekumbusha juu ya wajibu wa kuhakikisha kwamba watendaji wa vituo watakao ajiriwa wanakuwa watu wenye weledi na wanaojitambua.

“Tuachane na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi,” amesema Jaji Mwambegele.

“Mhakikishe siku ya uchaguzi mnaweka utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kinafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufanya mawasiliano na Tume pale ambapo utahitajika ushauri kuhusiana na masuala ya uchaguzi,” Jaji Mwambegele aliwasisitiza watendaji hao.

Aliwakumbusha kuwa uchaguzi ni jambo la kisheria na kwamba sheria na taratibu zikifuatwa ndio msingi wa uchaguzi kuwa mzuri, wenye ufanisi na hivyo kupunguza kama siyo kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

“Nachukua nafasi hii kuwaasa kuwa pamoja na uzoefu ambao baadhi yenu mnao katika uendeshaji wa uchaguzi, mhakikishe mnazingatia maelekezo mtakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea. Hata kama umeshasimamia chaguzi kadhaa hapo nyuma, lakini uchaguzi huu mdogo unaojumuisha kata 23 haujawahi kuusimamia,” amesema.

Kata zitakazofanya uchaguzi huo mdogo ni Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Fukayosi (Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

Nyingine ni Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Mshikamano (Halmashauri ya Wilaya ya Musoma), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Nkokwa (Halmashauri ya Wilaya ya Kyela), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu) Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga). [21/02, 08:38] Mroki Mroki: WATENDAJI WA UCHAGUZI WAHIMIZWA KUWASHIRIKISHA WADAU