Rais wa Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Rais wa Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço kwenye hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus kwenye hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026. Kushoto ni Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina ambaye ni Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama wa kwanza (kulia), Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus wa pili (kulia) pamoja na Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), uliofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Na Mwandishi Wetu, Dubai
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, jana usiku alishiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS) jijini Dubai, tukio lililoashiria mwelekeo mpya wa Afrika katika kuvutia mitaji ya kimataifa kupitia uwekezaji uliopangiliwa, wenye uhalisia wa kifedha na matokeo ya muda mrefu.
Akihutubia katika uzinduzi huo, Rais Dkt. Samia alisema kuwa wawekezaji wa leo hawatafuti fursa pekee, bali wanahitaji uaminifu unaojengwa kupitia uthabiti wa sera, taasisi imara na serikali zinazotekeleza ahadi zake kwa vitendo. Alisisitiza kuwa imani hiyo ndiyo msingi wa uwekezaji wa kudumu na wenye tija kwa pande zote.
Rais Samia alieleza kuwa Tanzania imechukua hatua za kimkakati kuimarisha mazingira ya uwekezaji kwa kuwekeza kwenye sekta muhimu ikiwemo nishati, reli ya kisasa, bandari na miundombinu ya uchukuzi, sambamba na kuanzisha Maeneo Maalum ya Uwekezaji pamoja na mfumo wa Dirisha Moja la Uwekezaji ili kurahisisha na kuharakisha huduma kwa wawekezaji.
Aliongeza kuwa ushiriki wa Tanzania katika GAIS unaakisi dhamira ya nchi ya kujenga ushirikiano uliopangiliwa vizuri, unaoendana na vipaumbele vya maendeleo ya taifa na matarajio ya wawekezaji wa kimataifa, huku ukilenga kuleta ajira, uhamishaji wa teknolojia na kukuza uchumi jumuishi.