Articles by "HABARI"
Showing posts with label HABARI. Show all posts
Tanzania Breweries Limited (TBL), one of Tanzania’s top manufacturers and employers and a key partner in the socio-economic development of the country, has today signed a Memorandum of Understanding (MoU) with the CRDB Bank Foundation to collaboratively implement the Barley Farming Pre-financing Seed Capital Scheme.

This collaboration, rooted in TBL's Smart Agriculture Initiative, represents a key milestone in the company's efforts to promote sustainable farming practices and empower local communities across Tanzania.

The TBL’s Smart Agriculture Initiative aims to equip 100% of its direct farmers by 2025, ensuring they are skilled, connected, and financially empowered. By focusing on cultivating sorghum, barley, and grapes, which are essential resources for TBL's operations, the initiative directly supports farmers in enhancing productivity and leveraging natural resources efficiently.
With excitement for the collaboration, Michelle Kilpin, Tanzania Breweries Limited Managing Director, said: “By combining the efforts of both TBL and CRDB Bank Foundation, the partnership aims to significantly boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers in Tanzania.

I believe our partnership is a good example of how collaboration can play a positive role in bringing about positive change and creating value for various stakeholders. Having reached this milestone today, we are confident that it will be the catalyst for similar activities across the country, and we believe that this initiative will be an inspiration to others.”
Through this alliance with the CRDB Bank Foundation, TBL seeks to integrate financially empowered criteria into its smart agriculture framework, enabling farmers to adopt sustainable practices that promote environmental stewardship and reduce reliance on chemical inputs.

This partnership underscores TBL's broader commitment to achieving the United Nations Sustainable Development Goals, particularly SDG 2, which emphasizes achieving zero hunger; SDG 12, for responsible consumption and production; SDG 13, for climate action; and SDG 17, to enhance partnership for the goals.

The Foundation’s initiative, named the iMbeju program, aims to boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers across Manyara, Karatu, and Monduli Districts for the 2024 agriculture season. The TBL and CRDB Bank Foundation aspire to drive long-term sustainability and resilience in the agriculture sector.
The CRDB Bank Foundation Managing Director, Ms. Tully Esther Mwambapa, says the iMbeju program has been on the market for almost a year now and has attracted a huge number of youth and women, its primary target. To date, she says that the program, which involves financial literacy training and the provision of seed capital, has trained around 250,000 women and offered seed capital to the tune of TZS 5 billion.

“We both seek to enhance sustainable agricultural practices through empowering our farmers. Once farmers are financially stable, production will more than double in all key produce, stabilize our food safety, and increase surpluses for local trading and export. This will have a positive impact on our GDP, where agriculture contributes a lion’s share,” she narrated.
Under this affiliation, farmers will have timely access to agricultural inputs, be exposed to smart technology utilization, and receive comprehensive training, all of which are going to boost yields and improve incomes for farming families.

Furthermore, the effort fosters economic growth and rural prosperity in Tanzania by supporting community development.
Through the collaboration, TBL and the CRDB Bank Foundation will be providing capacity-building programs, seed capital, insurance coverage, the supply of essential agricultural inputs such as fertilizers and agrochemicals, and support for cost-effective harvesting logistics. The goal is not only to boost barley production but also to equip farming communities with the necessary tools and knowledge for sustainable agricultural practices and financial management.
The MoU includes a comprehensive framework for collaboration, detailing roles, responsibilities, and operational mechanisms to ensure the scheme’s success.

TBL and the CRDB Bank Foundation will work together to deliver on commitments around the following:
Community Development: By prioritizing livelihood improvement, the program contributes to broader community development, fostering economic growth, food security, and rural prosperity.

Sustainable Agricultural Practices: By promoting smart agriculture and financially empowering farmers, the program encourages sustainable practices that protect the environment and reduce chemical inputs.
Capacity Building: The partnership facilitates the transfer of financial literacy knowledge and skills to local farmers, empowering them to make informed decisions and adapt to evolving agricultural practices and market demands.

Increased Yields and Incomes: Through timely access to agricultural inputs, smart technology utilization, and training, farmers can enhance productivity, leading to higher yields and improved incomes for their families.
Katika kufungua fursa za kuongeza umahiri katika fani zao, Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative (SUGECO) imesaini mkataba wa miaka mitatu kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

Akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa taasisi yake imekuwa ikitekeleza Program ya Imbeju inayotoa mafunzo ya ujasiriamali pamoja na mtaji wezeshi kwa vijana na wanawake.
Tangu walipofungua dirisha la maombi mwaka mmoja uliopita, vijana 709 walijitokeza na kati yao, asilimia 40 kati yao walitoka katika sekta ya kilimo ambayo inaongoza kwa kuliingizia taifa fedha za kigeni huku ikilihakikishia taifa chakula cha kutosha kwa mwaka mzima.

Kwa kushirikiana na wabia, Tully amesema kilimo kinapewa msisitizo zaidi kwa kutambua mchango wake katika kuliingizia taifa fedha za kigeni, kutoa ajira kwa Watanzania pamoja na kuihakikishia Tanzania usalama wa chakula.
“SUGECO ni mbia wetu mpya katika uwezeshaji wa vijana hasa wanaojihusisha na kilimo. Kwa kutambua umuhimu wa mafunzo kwa vitendo katikakuwajengea uwezo vijana, CRDB Bank Foundation imetenga Euro milioni 24 sawa na Shilingi bilioni 67 kwa ajili ya programu hii zitakazotolewa ndani ya miaka mitatu ya ushirikiano wetu na SUGECO ili kuwaandaa vijana mahiri watakaoajiria au kujiajiri kwenye sekta ya kilimo,” amesema Tully.

Tangu kuanzishwa kwake, SUGECO huwapeleka nje ya nchi wahitimu wa SUA hasa katika mataifa ya Ulaya, Amerika na Asia ambako hujifunza namna nzuri ya kufanya kilimo chenye tija lakini mchakato huo huhitaji fedha za awali kumwezesha mhitimu husika kujiandaa ipasavyo.

Kwa mwaka huu wa kwanza, Tully amesema wanatarajia kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 kwa kati ya dola 3,500 za Marekani (shilingi milioni 8.7) mpaka dola 4,500 (shilingi milioni 11.29) zinazotosha kwa mahitaji yao yanayojumuisha gharama za pasi ya kusafiria, visa pamoja na fedha ya kujikimu kabla ya kuanza kulipwa huko waendako.

“Mpango wa uwezeshaji baada ya mafunzo pia umeshaandaliwa kwa kushirikiana na SUGECO pamoja na USAID kwa kutenga maeneo maalum ya kuwekeza katika kilimo cha kisasa, na chenye tija zaidi. Taasisi yetu imejipanga kikamilifu pia katika hatua hiyo ya pili ya uwezeshaji kwa kutoa mitaji wezeshi, pamoja kuwapa mafunzo ya ujasirimali,” amesisitiza Tully.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO, Ndugu Revocatus Kimario amesema ushirikiano na Taasisi ya CRDB Bank Foundation utaongeza idadi ya wanufaika kwa kiasi kikubwa kwani mwaka jana waliweza kuwapeleka vijana 500 tu kupata mafunzo hayo kwa vitendo nje ya nchi ili kupata elimu na kujengewa uwezo zaidi katika kilimo, fani ambazo wamezisomea.

“Ushirikiano huu, tunaamini utakuwa na tija kubwa kwani ili ufanye biashara endelevu ni muhimu kuwekeza kwa watu unaowahudumia. Mkataba huu ni kati ya uwekezaji mkubwa kwa Benki ya CRDB kwani si wahitimu peke yao watakaonufaika bali wafanyakazi wao, familia hata ndugu, jamaa na marafiki zao,” amesema Kimario.
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi ya SUGECO naye, Dkt Anna Temu alikumbusha namna walivyouanzisha ushirika huo ambao mpaka sasa umewaneemesha maelfu ya wahitimu wa SUA kwa kuwaongezea maarifa juu elimu waliyoipata darasani.

“Kwa kuwa sisi tunawahudumia zaidi vijana na wanawake, tuliona CRDB Bank Foundation wenye Program ya Imbeju ni wabia muhimu wa kufikisha malengo yetu kwa jamii,” amesema Dkt Anna.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akiwa kwenye futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhamani akizungumza katika halfa hiyo
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akitunzwa baada ya kusoma Quarn Tukufu katika halfa hiyo.
Na Oscar Assenga, PANGANI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu mkoa huo umepokea fedha kiasi cha Sh.Trilioni 2.6 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Balozi Batilda aliyasema hayo wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyokwenda sambamba na Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji Jumaa Aweso iliyofanyika wilayani Pangani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali,Chama na Taasisi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa maji Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji,Mkurugenzi wa Ruwasa na wataalamu mwengine.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo likiwemo Daraja la Mto Pangani na Barabara ya Pangani pamoja na mengine ikiwemo ya elimu ambapo wanamshukuru Rais kwa ujenzi wa mabweni ya watoto wenye mahitaji maalumu yamejengwa, zahanati, nyumba za walimu na miradi ipo mingi kazi kubwa imefanywa.

“Katika hili tunamshukuru sana Mh Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutuletea fedha hizi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini namshukuru kwa imani kubwa kwangu ninahaidi sitamuangusha nitajitahidi kwa ushirikiano wenu na dua zengu niweze kutimiza yale ambayo anakusudia nitimize nikiwa hapa Tanga” Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwamba wataendelea kuhakkikisha fedha zinazokuja zinatekeleza kazi iliyokusudiwa na sio vyenginevyo pamoja na usimamizi mzuri katika miradi inayotekeleza ili iweze kuleta tija inayotakiwa.

“Nimshukuru Waziri Aweso amefanya jambo kubwa na ameendelea kufanya mambo mengi kwenye Sekta ya Maji nimetoka Tabora kwenye miradi 28 nasi tulikuwa tunanufaika nimekuja hapa Tanga nimeambiwa napo ipo ni kijana mdogo lakini mwenye hekima, hofu ya mungu, mchapakazi “Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwa hakika dhamana aliyopewa na Rais Dkt Samia Suluhu kuhakikisha anawatua wakina mama ndoo kichwani ameitekeleza vizuri kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara maji wanaendelea na kazi nzuri.

Akizungumzia suala la mabadiliko ya tabia ya nchi hasa kwenye wilaya ya Pangani RC Balozi Batilda alisema wilaya hiyo ni moja ya maeneo yaliyoathirika na kuna maeneo yakichimbwa visima kuna maji ya chumvi ndio maana kwenye mradi wa maji ya miji 28 na wao wamepelekewa na maeneo watachimba visima ili wananchi waweze kunufaika kwa kupata maji safi na salama.

Akizungumzia suala la uvuvi RC huyo alisema suala hilo katika mkoa huo ni moja ya maeneo ya uvuvi hivyo suala la maboti na vifaa vya uvuvi vitaendelea kupatikana kwenye mji wa Pangani na maeneo mengine.

“Tunapozungumzia masuala ya mazingira niwape kongole Pangani mazingira mmeendelea kuyatuza na msitu wenu wa asili unapendeleza”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema katika moja ya kuendeleza ukwekezaji Serikali kupitia Wizara Madini ilisaini mkataba na wawekezaji wa madini ya Ndovu au tembo ambayo yatachimbwa kwenye Mwambao wa Pangani karibu kilomita 15 ya ufukwe.

Alisema walichowaambia wahakikisha hawawanyi ruhusu ya wavuvi kutumia mwambao huo na matumbawe hayatavurugwa ikiwemo mikoko iliyopo wakati wanaendelea kunufaika na mradi huo na kuendelea na uvuvi,matango pori yote kuhakikisha wanakuwa na shughuli mbalimbali zinaendelea.

Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa wa Tanga ndio ambao kila kitu kinaweza kuota hivyo lazima wahakikishe utajiri huo unawanufaisha wananchi wao wote kwa kuhakikisha wanachangamkia fursa zilizopo.

“Katika ujenzi wa bomba la mafuta litapita kwenye wilaya kadhaa tunataka wana tanga wanufaike na miradi hiyo na kazi yake katiba tawala na wakuu wa wilaya na makatibu tawala ni kuwawezesha wananchu kuona fursa za uwepo wa mradi huo ili waweze kuchangamkia fursa hizo”Alisema RC Balozi Batilda ,

Awali akizungumza katika futari hiyo Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew alisema kwamba maadili mema ambayo tumeyaonyesha katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani tuendelee kuifanya na kufanya ibada ndio tunaweza kuwaponya wengi na kujiponya na sisi.

Mhandisi Mathew alisema pia waendelee kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu ili aendelea kuifanya kazi nzuri anaoendelea kuifanya na kuhakikisha wanashirikiana na Mbunge wao na kamwe wasimwangushe .

“Nataka kuwaambie wana Pangani “Dhahabu ya Pangani tunaijua wana Pangani na Dhahabu ya Tanzania tunaijua na tusije kudanganyika na kuachia dharabu hii na kwenda kuokota mawe”Alisema

Hata hivyo alimshukuru Waziri Aweso kwa jambo kubwa alilolifanya kwa wananchi wake kutokana na uwepo wa umoja na mshikamano kwa wananchi wake ambao wameitika kwa wingi kwenye tukio hilo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema safari ya kuifungua pangani kimaendeleo itafanywa na wana Pangani wenyewe na mimi ni miongoni mwa watu walishawishika na Waziri Aweso kipindi kile kwa maneno yake kwa dhamira iliyojificha ndani ya moyo wake akanitamkia ya kutaka kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo.

Alisema kwa sasa tunayaona maendeleo makubwa sana kwenye Jimbo la Pangani ikiwemo ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani –Saadani ambayo itaifungua wilaya hiyo pamoja na uwepo wa miradi ya maji ambayo awali wananchi walikuwa wakiifuata umbali mrefu.
Meneja Mawasiliano (Corporate Communication and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa (wa pili kutoka kushoto) akimkabidhi moja ya vifaa vya kisasa vya kupima ulevi kwa madereva vilivyotolewa na Barrick kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama barabarani kanda maalum ya Dar es Salaam, Mohamed Bahashwan, katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa hivyo kwa Jeshi la Polisi iliyofanyika katika Kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam , wengine pichani ni Kamanda wa Polisi wa Kinondoni SACP Mtatiro Kitinkwi (kushoto) na Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani wa Dar es Salaam SACP William Mkonda.

Na Mwandishi Wetu.

Katika kuendeleza mkakati wa kuhamasisha jamii kuzingatia usalama wakati wote, kampuni ya Barrick kupitia kampeni yake ya ‘Journey to Zero’ imekabidhi Jeshi la Polisi msaada wa vifaa vya kupima ulevi kwa madereva wa vyombo vya moto vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100 katika hafla iliyofanyika katika kituo cha polisi cha Oysterbay kilichopo wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika hafla ya kupokea vifaa hivyo,Kamanda wa Polisi wa kanda ya Kinondoni, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mtatiro Kitinkwi,alisema msaada huyo wa vifaa vya kisasa vya kupima kilevi umetolewa kwa wakati mwafaka ambao Jeshi hilo linaendelea na mikakati ya kukomesha vitendo vya ulevi kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto ambao umekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali nyingi za barabarani zinazotokea nchini.

“Tunawashukuru Barrick kwa kuendelea kuwa wadau wakuu wa kusaidia kampeni za ualama barabarani nchini na sisi tunawahodi kuwa vifaa hivi tutavitumia vizuri ili vifanikishe lengo lililokusudiwa la udhibiti wa madereva kutumia vinywaji vyenye kilevi kupita kiasi”.alisema Kitinkwi.

Alisema Jeshi la Polisi kupitia kikosi chake cha Ualama Barabarani pia litaendelea kutoa elimu ya unywaji kistaarabu kwa madereva wa vyombo vya moto ili kuhakikisha ajali nyingi zinazotokana na ulevi zinatokomezwa nchini na alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizi kwa kuwa suala la usalala linamgusa kila mwananchi.

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa, alisema kuwa msaada huo ni mwendelezo wa kampeni ya Barrick ya Journey to zero ambayo inalenga kuhamasisha afya na usalama kwa wafanyakazi wake na wadau wengine wote kwenye jamii.

“Kampeni yetu ya 'Journey to Zero' inalenga kuhakikisha wafanykazi wote wa kampuni wanakuwa salama wakati wote wanapokuwa kazini hadi wanaporudi nyumbani hivyo tumehakikisha kampeni hii inavuka mipaka hadi nje ya kampuni kuhakikisha jamii nzima inakuwa salama na ndio maana tunaendelea kuunga mkono Serikali kupitia Jeshi la Polisi kupambana na changamoto ya ajali za barabarani.

Mutagahywa alisema Barrick, siku zote itaendelea kuwa mstari wa mbele kushirikiana na wadau mbalimbali kuunga mkono kampeni hizi za usalama barabarani na inaamini vifaa hivi vya kisasa vya kupima kilevi vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Polisi vitasaidia kuwabaini madereva wanaoendesha vyombo vya moto wakiwa wamelewa na kuchukuliwa hatua za kisheria ili kudhibiti na kupunguza matukio ya ajali za barabarani.

Naye Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan, aliishukuru Barrick, kwa kutoa msaada huo na kwa kuwa mdau mkuu wa kusaidia kampeni ya usalama , alitoa rai kwa watumiaji wa vifaa hivyo kuvitunza vizuri ili kuweza kufanikisha malengo mazuri yaliyokusudiwa sambamba na kuwarahisishia kazi, “Katika dunia ya sasa ya matumizi ya teknolojia nina imani vifaa hivi vitarahisisha kazi ya polisi wetu kuwanasa madereva walevi” alisisitiza.
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan akiongea katika hafla hiyo.
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi walipata fursa ya kuongea katika hafla hiyo.
Viongozi wa kamati za usalama barabarani, Jeshi la Polisi na Barrick walipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na wageni waliohudhuria katika hafla hiyo.
Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo akizungumza wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga.
Na Oscar Assenga, KOROGWE.

WATANZANIA wametakiwa kuienzi amani iliyopo hapa nchini ambayo ni tunu kubwa iliyoacha na waasisi wa Taifa hili na wasikubali kamwe ichezewe kutokana na kwamba kufanya hivyo itaondoa umoja wetu ambao ni chachu ya maendeleo.

Wito huo ulitolewa na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga

Alisema wao kama Kanisa wanatambua kwamba amani ni kitu muhimu sana kwa ustawi wa jambo lolote lile hivyo ni lazima itunze na iendelee kuenziwa na ndio maana wameona mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufuturisha kutokana na umoja uliopo na kwamba wao ni ndugu moja.

Futari hiyo iliandaliwa na Kanisa hilo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ambapo ililenga makundi ya Makondakta,Waendesha bajaji,Wajasiriamali ,Wamachinga ambapo pia viongozi wengine wa kiserikali nao walishiriki lengo likiwa ni kuhimiza umoja na kudhimisha amani.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa futari hiyo Mchungaji wa Kanisa hilo Mbwambo alisema kwamba wao kama viongozi wa dini ni kuonyesha umma kwamba katika suala la mungu ni lazima kuwe na umoja na mshikamano kutokana na kwamba wao ni wametoka kwa baba mmoja.

“Futari hii ni kuonyesha umoja sisi kama kanisa na tunaendelea kusisitiza mshikamano na amani kwa sababu hivyo ndio vitu muhimu kwa ustawi wa jamii yoyote ile hivyo tuendelee kuitunza na kuienzi na tusiwafumbie macho wale ambao watakaojaribu kuichezea”Alisema

Hata hivyo alitoa wito kwa taasisi na watu wenye uwezo kuona namna ya kuwasaidia wahitaji wanapokuwa kwenye mwezi mtufuku wa ramadhani kuhakikisha wanayagusa makundi yaliyokuwa kwenye hali ya chini.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda akiwasili uwanja wa Ndege Arusha.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda akisalimiana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Justine Msejo.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda akisalimiana mkuu Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Messaile Musa Kushoto kwake ni mkuu wa wilaya wa Arusha Felician Mtahengerwa. Picha zote na Vero Ignatus Arusha.
MKUU wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga leo mapema akiwa kwenye ziara yake katika Mji mdogo wa Mererani Wilayani Simanjiro, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Naepo iliyopo katika Kata ya Naisinyai kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Aprili 2024 mradi uwe umekamilika na unaanza kufanya kazi.

Zahanati ya Naepo inajengwa kwa fedha kutoka vyanzo mbalimbali ambapo shilingi Mil. 50 ni fedha za mapato ya ndani, Mil. 48 fedha za nguvu za Wananchi na Mil. 20 ni fedha ambazo zimechangiwa na mdau hivyo kufanya jumla ya Shilingi Mil. 118.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya Sokoni Mirerani - Mgodini Tanzanite kilomita 1.2 kwa kiwango cha lami inayotekelezwa na Mkandarasi M/S EMMA & SONS CONTRACTORS LTD. Mradi huu ulitengewa jumla ya shilingi milioni 898 hadi kukamilika. 

Katika hatua nyingine, Mhe. RC Sendiga amemuagiza na kumpa mwezi mmoja Meneja wa TARURA Wilaya ya Simanjiro kusimamia na kuhakisha mradi huo uwe umeshakamilika alipotembelea mradi huo unaotekelezwa kwa fedha za tozo ya mafuta.

Miradi mingine ambayo imetembelewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa ni pamoja na ujenzi wa Soko la madini, mradi unaotekelezwa kwa fedha shilingi Bilioni 5.43 na hadi sasa mradi upo katika asilimia 80 (80%) ya utekelezaji. Mradi mwingine ni ujenzi wa kituo cha Afya cha Tanzanite kilichopo kata ya Mirerani. Mradi huu umetengewa fedha kutoka Serikali kuu shilingi milioni 500 kujenga jengo la wagonywa wa nje (OPD), Maabara na jengo la mama na mtoto. Mradi huu upo katika hatua ya msingi.

Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiongea na Wanafunzi wa Vyuo vikuu wakati wa kongamano la kuwajengea uwezo wa kuhimili ushindani wa ajira na kujiajiri lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC) lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kwa udhamini wa kampuni ya Barrick.

Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya Barrick nchini, imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuibua na kukuza vipaji vya vijana wasomi wa vyuo vya elimu ya juu na kati nchini ili waweze kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea kutokea duniani na kuhimili ushindani katika soko la ajira sambamba na kuweza kujiamini kutumia ujuzi na taaluma zao kujiajiri kwa ajili ya kujenga mustakabali endelevu.

Hayo yameeleza na Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiongea na Wanafunzi wa Vyuo vikuu wakati wa kongamano la kuwajengea uwezo wa kuhimili ushindani wa ajira na kujiajiri lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC) lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) kampasi ya Mlimani kwa udhamini wa Barrick ambayo inaendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Shimbi, pia aliwaeleza wasomi hao shughuli za kampuni ya Barrick nchini na mkakati wake wa kuinua vipaji vya vijana sambamba na kuwezesha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ili wapate fursa ya kupata ajira katika sekta ya madini ambayo kwa sasa asilimia kubwa inatawaliwa na wanaume.

Kongamano hilo kubwa limehusisha makampuni mengine makubwa ya ndani na nje kwa ajili ya kuwanoa wanafunzi kuhusiana na mabadiliko ya teknolojia,ajira na kujiajiri wenyewe pindi wamalizapo masomo yao.
Wanafunzi wakifuatilia mada kutoka kwa Watendaji wa makampuni mbalimbali walioshiriki katika kongamano hilo.
Afisa Raslimali wa Barrick Tanzania, Isentruda Mkumba (kushoto) akiongea na wanafunzi waliotembelea banda la maonesho la Barrick kwenye kongamano hilo.
Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiwa na viongozi wa AIESEC.
Washiriki wakifanya mazoezi ya kujiweka sawa.