Articles by "TEKNOLOJIA"
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Na Mwadishi Wetu - Kajunason

MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia( COSTECH)Dk.Amos Nungu amesema pamoja na Serikali na wadau kuendelea kutoa fedha za kufadhili utafiti na ubunifu nchini, kwa ujumla bado mahitaji ya kuratibu na kuendeleza sayansi, teknolojia na ubunifu ni mengi ukilinganisha na rasilimali fedha zinazopatikana.

Akizungumza leo Juni 14, 2023/wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Nane la Kitaifa la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ambapo amewaeleza washiriki pamoja na kufadhili watafiti kufanya tafiti mbalimbali bado mahitaji ni mengi ukilinganisha na rasilimali fedha.

Amesema kuwa changamoto hiyo ya fedha inachangia taasisi nyingi za utafiti na maendeleo, pamoja na vyuo vikuu kushindwa kufanya tafiti na bunifu nyingi zaidi zitakazoleta mapinduzi makubwa ya kijamii na kiuchumi.

Pamoja na changamoto hiyo ya rasilimali fedha, ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa katika kuratibu, kukuza na kuendeleza utafiti; Tume huratibu maandalizi ya vipaumbele vya utafiti kulingana na vipaumbele vya taifa.

"Kwa sasa, upo Mwongozo wa Vipaumbele vya Kitaifa vya Utafiti vya miaka mitano yaani, mwaka 2021/22 hadi mwaka 2025/26 ambao unatumika kufadhili tafiti na pia kuwaongoza wadau wengine wanaotaka kufadhili au kuwekeza katika utafiti.

"Kwa kipindi cha miaka mitano (2018-2023 Serikali kupitia Tume imefadhili miradi 47 ya utafiti yenye thamani ya takribani Sh. billion 5 fedha za kitanzania. Katika kipindi hicho cha 2018-2023, pia Tume imefadhili miradi 11 ya miundombinu ya Utafiti yenye thamani ya zaidi ya billion 4 ya fedha za kitanzania.

"Tume imewezesha watafiti wa ndani na nje ya nchi kufanya tafiti hapa nchini kwa kuratibu utoaji wa vibali vya utafiti. Katika baadhi ya maombi ya vibali vya tafiti, Tume hushirikisha wadau wa sekta husika ili wafahamu utafiti gani unaendelea, wajiandae kupokea matokeo ya tafiti hizo yaweze kutumika na Serikali, " amesema Dk.Nungu.

Aidha katika kuendeleza na kuhawilisha teknolojia na ubunifu amesema Tume inafanya kazi kwa karibu na wabunifu walioko katika sekta rasmi na isiyo rasmi na kwamba wamekuwa wakitumia njia tatu katika kuwaendeleza wabunifu.

Ametaja njia hizo ni kutoa ushauri wa kitaalamu moja kwa moja au kupitia wabobezi wanaopatikana hapa nchini, kuwaunganisha na taasisi bobezi ili kuwapa usaidizi stahiki kulingana na aina ya ubunifu wao.

Ameongeza baadhi ya wabunifu wameunganishwa na Watanzania wabobezi walioko nje ya nchi (Diaspora) kwa ajili ya ushauri pamoja na kuwapa usaidizi wa kifedha (mwega), ambao ni uwekezaji kama wa mbegu tu ili waendeleze bunifu zao.

"Ili kuhakikisha wabunifu wengi zaidi wanafikiwa, Tume iliandaa “Mwongozo wa Kitaifa wa kutambua na kuendeleza ugunduzi, ubunifu na maarifa asilia ambao ulipitishwa na Wizara yetu ya Elimu, Sayansi na Teknilojia mwaka 2018 uliopelekea kuanzishwa Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) mwaka 2019.

"Hadi kufikia sasa, zaidi ya wabunifu 2,647 wametambuliwa na kupata usaidizi. Wabunifu 461 kati ya wale waliotambuliwa walikidhi vigezo vya kupata usaidizi wa fedha na hivyo wamepatiwa mwega wa kuendeleza bunifu zao, " amesema.

Aidha Dk.Nungu amesema moja ya miradi ya kujivunia iliyotokana na MAKISATU ni Mradi wa Dira za Maji za malipo kabla ya matumzi (prepaid water meters) ambao ulibuniwa na kijana aliyekuwa anasoma diploma na kwa sasa Mamlaka ya Maji na Usafi Vijijini (RUWASA) wametoa nafasi mita hizi zifungwe mikoa yote ya Tanzania Bara.

Ameeleza kwamba katika kila Mkoa Wilaya mbili zitachaguliwa na kufungiwa mita 8 kila moja na tayari mita zaidi ya 30 zimefungwa huku matazamio ni kwamba hadi mwishoni mwa Julai mita 4 kila Wilaya za mikoa yote Tanzania Bara zitakuwa zimefungwa.

"Tume inafanya kazi kwa karibu na taasisi zinazojihusisha na uendelezaji na uhawilishaji wa teknolojia. Kwa namna mbalimbali, Tume inaziwezesha taasisi hizi kwa kuzipatia fedha za kufadhili miradi ya ubunifu; kujengea uwezo watumishi wao, na pia kuboresha miundimbinu ya taasisi hizo.

"Taasisi hizi zimekuwa ni nyenzo muhimu za kusanifu na kutengeneza mashine mbalimbali ambazo zinawasaidia wananchi hususani katika sekta ya kilimo, mifugo, afya na uzalishaji. Pia taasisi hizi pamoja na vyuo vikuu zimekuwa ni nyenzo muhimu za kulea na kukuza vipaji vya wabunifu hapa nchini, " amesema.

Katika hatua nyingine alisema Tume kwa kushikirikiana na taasisi mbalimbali pamoja na vyuo vikuu vya hapa nchini, imewezesha wabunifu kuanzisha kampuni yanayotokana na ubunifu (startup companies) kwa kuboresha bidhaa au huduma.


Amesema kampuni hizo zimetengeneza zaidi ya ajira 1,800 za moja kwa moja na 3,000 zisizo za moja kwa moja ambapo kampuni kama vile Intemech, Magilah Tech, Scan code (T) Limited, Sahara Ventures, Nanofilter, zimeweza kubiasharisha ubunifu waao, kuwa na masoko hadi nje ya mipaka ya nchi yetu.

Amesema kwamba tayari Tanzania kwa sasa inauza hizo teknolojia nje ya nchi kama vile Malawi, Zambia, Afrika Kusini, na kwingineko.




Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda anatarajia kufungua maonesho ya nane ya Utafiti na Ubunifu yanayotarajia kuanza Mei 23 - 25, 2023 katika Viwanja vya Maktaba Mpya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumza na Wanahabari Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam- Utafiti, Prof. Nelson Boniface amesema maonesho hayo yenye kauli mbiu "Utafiti na Ubunifu kwa Ustawi wa Uchumi - jamii nchini Tanzania"

Prof. Nelson Boniface asema kuwa maonesho hayo yatataguliwa na ufunguzi ambapo wazungumzaji watakuwa ni Profesa Lettice Rutashobya ambaye ni mbobezi katika masuala ya biashara katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na Michael Shirima mwenyekiti na Mwanzilishi wa Presicion Air Tanzania.

Amesema kuwa katika maonesho hayo ya nane wanatarajia kuonesha miradi 99 iliyotokana na maonesho yalifanyika katika ngazi ya vitengo ambapo jumla ya miradi 350 na wakachagua hiyo 99.

"Malengo ya Tafiti hizi ni kuwavutia wanataaluma kutoka chuo chetu na taasisi nyingine zinazohusiana na Taaluma Pamoja na utafiti na watu wote wa serikalini ikijumlisha wenye viwanda kuja kushuhudia tafiti na bunifu zao wanazofanya katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam," amesema Prof. Nelson Boniface.

Ameongeza kuwa tafiti zote zinazofanywa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zinalengo la kuboresha maisha ya Watanzania hivyo ni vyema watu wakajitokeza kwa wingi kuhudhuria maonesho hayo ili waweze kujifunza mambo mbali mbali. 
Mkuu wa Idara ya Udhibiti Ubora wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga (Bombo ) Joseph Nzige akitoa mafunzo ya uboreshaji wa mazingira ya mtoa huduma kwa dhana ya 5S-KAIZEN kwa Maafisa Tehama wa Hospitali hiyo,Picha na Hospitali ya Rufaa ya Bombo
Mkuu wa Idara ya Udhibiti Ubora wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga (Bombo ) Joseph Nzige akitoa mafunzo ya uboreshaji wa mazingira ya mtoa huduma kwa dhana ya 5S-KAIZEN kwa Maafisa Tehama wa Hospitali hiyo, Picha na Hospitali ya Rufaa ya Bombo
Mkuu wa Idara ya Tehama wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo William Masika wa kwanza kulia akiwa na maafisa tehama wengine wakifuatilia mafunzo hayo

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt Jabiri Bakari (kushoto) akiwa sambamba na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Mathew (wa pili katikati) wakimkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika TCRA kwa ziara ya mafunzo akiambatana na Maafisa Waandamizi wa Tume ya Mawasiliano Uganda(UCC) (hawamo pichani). Wa kwanza kulia anaeshuhudia ni Msaidizi wa Waziri wa Uganda.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (wa kwanza kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari (wa pili kulia) walipomkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (katikati) kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma-TCRA Bi. Lucy Mbogoro. Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (kulia) akiperuzi jambo kwenye kijitabu wakati alipomkaribisha Mgeni wake Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (anaesaini kitabu cha wageni kushoto) Waziri huyo wa Uganda alioongozana ujumbe wa maafisa wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) waliokuja Tanzania kwa ziara ya mafunzo ya usimamizi wa sekta ya Mawasiliano kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikiwa ni mkakati wa kuboresha Sheria ya Mawasiliano ya nchini kwao.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kundo Mathew (kushoto), akimweleza jambo Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika Tanzania kwa ziara ya mafunzo. Katika tukio hili anakaribishwa kujifunza kutoka TCRA namna Sheria za Mawasiliano zinavyowezesha usimamizi wa Sekta ya mawasiliano nchini. Picha na TCRA

Na Mwandishi Wetu
TANZANIA imeihakikishia Uganda kuwa itaendelea kuipa ushirikiano katika kujenga uwezo wa usimamizi wa sekta ya Mawasiliano na TEHAMA, sambamba na kudumisha ushirikiano wa kitaalam katika usimamizi wa sekta hizo.

Akizungumza wakati alipoukaribisha ujumbe wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) ukiongozwa na Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey uliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ziara ya Mafunzo na kubadilishana ujuzi, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrew Mathew alibainisha kuwa, Tanzania imefanikiwa kusimamia vilivyo sekta ya Mawasiliano kwa kuweka Sera Madhubuti za usimamizi wa huduma za Mawasiliano, huku akiwahakikishia wageni fursa tele ya kujifunza katika sekta ya Mawasiliano.

“Tanzania imepitisha sera zinazounga mkono ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA na mfumo wa kisheria na udhibiti unaounga mkono ukuzaji wa uchumi wa kidijiti,” alisisitiza Kundo na kuongeza kuwa “Ninakuhakikishia ujumbe wako kwamba utapata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu ambao utakuwa muhimu katika marekebisho ya Sheria yenu ya Mawasiliano ya 2013,” alibainisha.

Kwa upande wake Waziri Kabbyanga akishukuru baada ya ukaribisho alimweleza Naibu Waziri Kundo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri Bakari na Menejimenti ya TCRA lengo la ziara yao Tanzania kuwa ni kujifunza zaidi namna Tanzania inavyosimamia huduma za Mawasiliano ambao ziara yao mahususi katika ofisi za TCRA ililenga kujifunza namna Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali inavyowezesha usimamizi wa sekta ya Mawasiliano.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuwasili kwenye ofisi za TCRA jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi anaeshughulikia Ulinzi na TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey alimweleza mgeni wake Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mheshimiwa Kundo Mathew kwamba Uganda imeona vema kuja kujifunza Tanzania kwa kuzingatia ujirani na namna ambavyo Tanzania imefanikiwa katika kusimamia na kudhibiti sekta ya Mawasiliano.

“Tumeambiwa kwamba Tanzania mnazo Sheria Madhubuti za usimamizi wa sekta ya mawasiliano Tumekuja hapa kwa sababu mazingira yetu ni sawa na ya Tanzania hivyo tumeona hapa kwenu tutajifunza na kupata maarifa yenye uhalisia zaidi, tofauti na tungeamua kwenda kujifunza sehemu nyingine,” alisisitiza Kabbyanga.

Alieleza kwamba pia Uganda inanuia kuboresha huduma za Mawasiliano ya simu kwa raia wake hivyo imeamua kuja Tanzania kujifunza katika eneo linalohusu Mawasiliano ya simu.

Ziara ya Tume ya Mawasiliano Uganda kuzuru Tanzania, na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni mwendelezo wa Mamlaka mbalimbali za Usimamizi wa Mawasiliano za Afrika kufika Tanzania kujifunza na kubadilishana ujuzi wa usimamizi wa huduma za Mawasiliano. Miongoni mwa nchi nyingine zilizozuru TCRA mwaka huu ni pamoja na Malawi, Zimbabwe, Burundi, Rwanda, Uganda, na Msumbiji.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewafungulia milango muhimu vijana wabunifu katika Teknolojia, Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa kuwapa uwezeshaji uliokuwa unakwamisha ubunifu miaka yote nchini. 

TCRA kwa ushirikiano na taasisi nyingine, imeweka mazingira rafiki kwa vijana wabunifu wa TEHAMA kutengeneza fursa za kukuza ubunifu na hatimaye kuzaa ajira kwa vijana. Fursa zilizotolewa zinahitaji kijana kuwa na ubunifu kama mtaji wake na vifaa vya gharama nafuu vya TEHAMA kama vile kompyuta mpakato na simu ya kiganjani au vifaa rununu pendwa kama vile kishikwambi kukamilisha ubunifu wake. 

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabir Bakari amesema Serikali ya Tanzania imeamua kutoka rasilimali kwa vijana wabunifu katika sekta ya TEHAMA. Rasilimali za mawasiliano zinazotolewa na TCRA kwa ajili ya vijana wabunifu kufanya majaribio ni pamoja na misimbo ya USSD, yaani rasilimali-namba. Hizi ni namba maalum zinazotumika kumpa mbunifu fursa ya kusambaza teknolojia aliyoibuni ndani na nje ya nchi. 

Pia TCRA kwa sasa wanato kikoa (domain) cha dot tz (.tz) na masafa ya mawasiliano. Kuanzia mwaka 2021, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk. Jabir (Pichani juu), amesisitiza kuwa vijana wabunifu na wavumbuzi wa programu mbalimbali za kidijitali sasa wanaweza kujitokeza kupata rasilimali hizo zitakazowawezesha kupata fursa ya kutengeneza ajira; kujiletea kipato na kutatua changamoto mtambuka za jamii. 

“Tumejipanga kuhakikisha wabunifu wapya hasa wa sekta ya TEHAMA, wanaoweza kutatua changamoto za jamii yetu wanapata rasilimali hizi za mawasiliano, ili washiriki katika uchumi wa kidijiti,” amesisitiza Mkurugenzi Mkuu Dk. Jabir. 

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania imeondoa malipo ya ada ya maombi na usajili wa leseni wa rasilimali hizo kwa ajili ya wabunifu wenye nia ya kubuni suala lolote litakalorahisisha mazingira ya kawaida ya kila siku ya mwananchi. Wabunifu wanaotaka kutumia fursa hii wanaweza kuwasiliana na Dawati la Huduma la TCRA kupitia namba 0800008272 au kutembelea tovuti www.tcra.go.t.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 50 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela ikiwa ni uwezeshaji kwa biashara bora changa za TEHEMA (digital startups) kupitia programu ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake ya benki hiyo inayofahamika kama "IMBEJU" ambayo imezinduliwa katika Kongamano la Sita la TEHAMA lililofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar Ijumaa iliyopita. Wengine pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib, Iddrisa Kitwana (watatu kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonazi (wapili kushoto), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Mohammed Abdull (wakwanza kushoto),Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya TEHAMA, Prof. Leornad Mselle (wapili kulia), na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA, Dkt. Nkundwe Mwasaga. Picha zote na Othman Michuzi.


======= ======= =======


Ikiendeleza jitihada zake za kukuza ujumuishi wa kiuchumi nchini, Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Tume ya TEHAMA imezindua programu mpya ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake wajasiriamali, Sh. bilioni 5 zatengwa.

Programu hiyo iliyopewa jina la ‘IMBEJU’ imezinduliwa katika kilele cha Kongamano la Sita la TEHAMA lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Golden Tulip na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na taasisi kutoka ndani na nje ya 
Akielezea kuhusu programu hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kupitia ‘IMBEJU’, benki hiyo itakuwa ikitoa mitaji wezeshi kwa vijana na wawawake wajasiriamali wenye biashara na mawazo bunifu.

Nsekela alisema kupitia programu hiyo vijana watakuwa wakiwasilisha mpango wa biashara zao, na mawazo bunifu kwa upande wa wanafunzi, kisha wataalamu wabobezi watakuwa wakichambua na kuidhinisha mtaji na mafunzo kulingana na vigezo.

“Katika programu ya IMBEJU tutakuwa pia tukitoa mafunzo ya usimamizi wa biashara, matumizi ya mifumo ya TEHAMA, elimu ya fedha na masoko, na usaidizi wa kuboresha bidhaa na mawazo bunifu,” alisema Nsekela.
Aliongezea kuwa Benki hiyo pia imeanzisha kituo maalum cha mafunzo na ubunifu wa biashara katika Makao Makuu ya zamani ya Benki hiyo mtaa wa Azikiwe jijini Dar es Salaam. Kituo hicho kitasimamiwa kwa ushirikiano na Tume ya TEHAMA nchini.

“Katika programu za vijana wajasiriamali tumeweka mkazo mkubwa zaidi katika biashara zinazoanza katika sekta ya TEHAMA tukilenga zaidi kuchochea uchumi wa kidijitali. Biashara katika sekta nyengine pia zitakuwa zikipata uwezeshaji,” alifafanua.
Kwa upande wa uwezeshaji wa wanawake wajasiriamali, Nsekela alisema Benki hiyo itakuwa ikifanya kazi na taasisi na mashirika yaliyojikita katika kufanya uwezeshaji kwa wanawake. Uwezeshaji utafanyika kwa vikundi na wajasiriamali mmoja mmoja.

Kwa kuanzia katika uzinduzi huo wa programu ya IMBEJU Benki ya CRDB imekabidhi jumla ya shilingi milioni 50 kwa Tume ya TEHAMA ikiwa ni uwezeshaji kwa biashara change katika sekta ya TEHAMA (digital startups).
Akizindua programu hiyo, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuanzisha programu hiyo ya ‘IMBEJU’ akisema itasaidia kukuza ujumuishi wa kiuchumi kwa vijana na wanawake.

“Idadi kubwa ya watu hapa nchini ni vijana na wanawake. Licha ya hivyo ndio watu tegemezi zaidi kiuchumi. Serikali imekuwa ikiweka jitihada kubwa katika kuliwezesha kundi hili. Niipongeze Benki ya CRDB kwa kuunga mkono,” alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya TEHAMA, Dkt. Nkundwe Mwasaga alisema wamejipanga vilivyo kuhakikisha programu ya ‘IMBEJU’ inakwenda kuchochea kwa kasi ukuaji wa biashara changa nchini.

IMBEJU inaenda sambamba na kauli mbiu ya “Leave No One Behind” ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SGD) 2030 inayosisitiza uwezeshaji kwa makundi yaliyotengwa na kukabiliana na ukosefu wa usawa katika fursa za kiuchumi.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akizungumza wakati akifunga Kongamano la Sita la TEHAMA lililofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar Ijumaa iliyopita.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Iddrisa Kitwana akizungumza wakati katika Kongamano la Sita la TEHAMA lililofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar Ijumaa iliyopita.

Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia, Mheshimiwa Nape Nnauye akizungumza na wageni waalikwa kwenye ukumbi wa Mlimani city kupitia teknolojia ya hologramu, iliyomwezesha kuonekana kama yupe ukumbuni hapo kiuhalisia lakini hakuwepo hapo. Hii ni baada ya Vodacom kuzindua rasmi mtandao wa 5G. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Hilda Bujiku
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Hilda Bujiku
Baadhi ya wadau wa teknolojia wakijadili mapinduzi ya kidigitali yanayotarajiwa kuletwa Tanzania na 5G
---
Dar es Salaam. Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC imezindua huduma ya mpya teknolojia 5G ikisema italeta mapinduzi na kuongeza ushiriki wa Taifa katika kuleta mageuzi ya nne ya viwanda.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Septemba Mosi, 2022 na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Hilda Bujiku wakati wa halfa ya uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City.

"Teknolojia hii ya 5G inakuja na fursa kubwa hapa nchini kwa wabunifu kuleta bidhaa na huduma mpya kwa wananchi. Vodacom sio tu itaendelea kubuni huduma mpya bali kuwezesha jamii ili kutimiza ndoto za kujenga Taifa bora.

Katika uzinduzi huo, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye aliyeeleza kuwa, Mei mwaka huu aliahidi Bungeni kwamba Tanzania itaanzisha 5G hapa nchini jambo hilo limetia leo kwa kampuni ya Vodacom kulitekeleza.

"Tuliposema ilikuwa kama ndoto lakini leo karibu miezi mitatu, lakini Vodacom wametekeleza na kutusaidia kuingia kwenye orodha ya nchi chache Afrika zilizoanzisha huduma ya teknolojia ya 5G.Vodacom wamekuwa wa kwanza kwenye mambo mengi wameanza na M-Pesa na mambo mengine nawashukuru," amesema Nape.
Wawakilishi kutoka sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi saba wanakutana leo jijini Dar es Salaam kuhudhuria kongamano linalolenga kuangalia namna ya kunufaika na 5G na teknolojia nyingine za kisasa za mawasiliano.

Kongamano hilo la siku tatu linafadhiliwa na Serikali ya Marekani na Taasisi ya Mafunzo ya Mawasiliano ya Simu ya Marekani (United States Telecommunication Training Institute –USTTI) kwa ushirikiano na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ya Tanzania.  Naibu Waziri Kundo Mathew alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya ufunguzi wa kongamano hilo, ambayo pia ilihudhuriwa na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright na Mwenyekiti wa USTTI Jim O’Conner.

Lengo la kongamano hili ni kuchangia mawazo na mbinu mbalimbali zenye ufanisi (best practices) za kutumia kikamilifu teknolojia zinazochipukia na kizazi kijacho cha teknolojia za mawasiliano ya kimtandao yasiyotumia waya (wireless networks) na wakati huo huo kushughulikia hatari na wasiwasi kuhusiana na usalama wa mtandao na faragha za watu. Semina zitakazotolewa zitaangazia mbinu bora za udhibiti (regulatory best practices), Mawasiliano ya Intaneti kuunganishwa na vitu mbalimbali (Internet of Things –IOT) na teknolojia ya satelaiti zinazozunguka zikiwa umbali mfupi kutoka uso wa dunia (Low Earth Orbit – LEO – satellite tecknology). Washiriki wa kongamano hili wametoka katika nchi za Msumbiji, Rwanda, Uganda, Kenya, Tanzania na Marekani. Makampuni ya sekta binafsi yaliyowakilishwa ni pamoja na Walt Disney Company, Inmarsat, Qualcomm, American Tower, ICANN, Microsoft na Meta.
Katika hotuba yake, Balozi Wright alisema kuwa Marekani ingependa kuona kwamba duniani kote kuna uchumi imara wa kidijitali unaowawezesha raia wote kunufaika kutokana na faida nyingi za kizazi cha tano cha mawasiliano ya kimtandao (5G) na upatikanaji wa kuaminika wa mawasiliano ya intaneti.

 “Kuna umuhimu mkubwa sana hivi sasa wa kuhakikisha usalama wa mitandao hii ya mawasiliano kuliko ilivyokuwa wakati mwingine wowote. Teknolojia za 5G na 6G zinaleta mageuzi makubwa mno na zitagusa kila nyanja ya maisha yetu, ikiwemo miundombinu muhimu kama vile usafiri na usafirishaji, huduma za kifedha, usambazaji wa umeme, huduma za afya na afya ya umma na huduma nyingine nyingi. Nchi na raia wanahitaji kuhakikishiwa na kuweza kuwa na imani kwamba makampuni ya mawasiliano na mamlaka za udhibiti hazita anzisha vitu vitakavyoleta hatari zitakazotishia usalama wa taifa, faragha au haki za binadamu,” alisema Balozi Wright.
  
Balozi Wright alisema pia kuwa kongamano hili ni mwanzo wa ubia wenye thamani ya takribani Dola za Kimarekani Milioni Moja kati ya Marekani na Tanzania katika masuala ya mawasiliano ya kimtandao unaolenga kutoa msaada wa kitaalamu/kiufundi katika teknolojia ya 5G, kukabiliana na uhalifu wa kimtandao na kuimarisha usalama mtandaoni. 
Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) leo Machi 8, 2022 imesaini mkataba na Kampuni ya Arqes Africa Architechs & Interior Designesers kwaajili ya kusanifu majengo ya Kituo cha Kikanda cha Umahiri wa Tehama (RAFIC) kazi ambayo inatakiwa kuanza mara moja na kukamilika ndani ya miezi minne.

Kazi ambazo anatakiwa kufanya mshauri elekezi huyo ni pamoja na kutengeneza 'Master Plan' ya DIT Kampasi Kuu ya Dar es Salaam, kusanifu majengo ya RAFIC na kumsimamia mkandarasi wakati wa ujenzi. Thamani ya kazi hiyo ni Sh 756,539,200

Hata hivyo Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof Preksedis Ndomba ameomba kazi hiyo ikiwezekana ikamilike ndani ya miezi miwili ili kupatikana kwa mkandarasi na kazi ya ujenzi ianze mara moja.

Katika tukio hilo la kusaini mkataba huo, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Arch. Lazaro Peter ameahidi kufanya kazi hiyo kwa umahiri mkubwa na ikiwezekana anajitahidi kukamilisha kazi ndani ya miezi miwili.
Naibu Katibu Mkuu-Uchukuzi, Dkt. Ally Possi, akisisitiza jambo kwa viongozi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), wakati alipotembelea ofisi za Mamlaka jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi na Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Hali ya Hew ana Utafiti wa Mamlaka hiyo, Dkt. Ladislaus Chang’a.
Naibu Katibu Mkuu-Uchukuzi, Dkt. Ally Possi, akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi, kuhusu utendaji wa Mamlaka hiyo wakati Naibu Katibu Mkuu huyo alipotembelea ofisi za Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu-Uchukuzi, Dkt. Ally Possi, akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Hali ya Hewa na Utafiti wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Dkt. Ladislaus Chang’a, wakati alipotembelea ofisi ya uchakataji taarifa za hali za hali hewa, jijini Dar es Salaam.

Na Karama Kenyunko Michuzi TV

SERIKALI imeitaka Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini ( TMA) kubuni vyanzo vya Mapato vsivyomkandamiza mwananchi wala kuidumaza Taasisi ili waweze kujiendesha na kuendelea kutoa huduma bora na zenye viwango.

Hayo yamesemwa leo Februari 7, 2022 jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi), Dkt. Ally Possi, wakati wa ziara yake ya kikazi TMA kuangalia utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

"Nawapongeza sana ninyi wote lakini kwa kipekee nampongeza Mkurugenzi mkuu, mama yetu mama Kijazi kwa Mapinduzi makubwa sana ambayo umekuwa ukiyafanya kwa sababu Taasisi hii imekuwepo kwa muda mrefu lakini ni kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ikifanya Mapinduzi makubwa sana." Amesema Dkt. Possi.

Amesema kwa kutambua umuhimu wa Taasisi hiyo mpaka sasa imeishapokea sh. Bilioni saba ili ziendelee kuboresha huduma za hali ya hewa na miradi yake mbali mbali.

"Serikali inatoa jicho lake TMA kwa sababu inaona kazi zinazofanywa na Taasisi hii ambazo siyo tu kwa ajili ya nchi yetu pekee bali hata kimataifa na pia zimekuwa zikisaidia ukuaji wa sekta zingine, hususani sekta ya maji na kilimo" amesema Dkt. Kijazi Possi

Ameagiza Taasisi kuhakikisha inafuatiliwa kwa karibu miradi yake ili isichukue muda mrefu kukamilika, iishe kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa ili mwisho wa siku thamani ya pesa zinazotolewa na serikali ziweze kuonekana.

Amesema pamoja na mambo mengine uchumi wa nchi yetu unategemea sana shughuli za bandari na bandari yetu inaweza kuonekana siyo sehemu sahihi sana kwa mizigo kushindwa kufika huku kwetu kama hakutakuwa na Utabiri uliosahihi.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya hali ya hewa ili kuongeza uhakika wa taarifa kwa kuwa sekta ya hali ya hewa inazitegemeza sana sekta nyingine hususani za usafirishaji pamoja na kilimo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi, amemuhakikishia Naibu Katibu Mkuu huyo kuwa Mamlaka imejipanga kikamilifu kuboresha miundombinu pamoja na kusomesha watumishi ili kuendeleza weledi katika sekta hiyo.
Katika mkuu wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya habari Dkt Jimmy Yonazi akiongea wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau wa kidigitali cha kujadili tathimini ya mahitaji ya taaluma ya TEHAMA
Mratibu wa mradi wa Tanzania ya kidigitali Honest Njau kutoka wizara ya habari mawasiliano na teknolojia ya habari akielezea mradi huo

Katibu mkuu wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Dkt Jimmy Yonazi akiwa katika picha ya pamoja na maafisa rasilimali watu na wataalamu wa TEHAMA kutoka wizara mbalimbali
Baadhi ya maafisa rasilimali watu na wataalamu wa TEHAMA wakifuatilia jambo katika kikao cha wadau wa kidigitali cha kujadili tathimini ya mahitaji ya taaluma ya TEHAMA

Vero Ignatus, Arusha

Katibu mkuu wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari Dkt Jimmy Yonazi amewataka maafisa rasilimali watu pamoja na wataalamu wa TEHAMA kuhakikisha wanatambua vipaji na kuviendeleza kupitia uchumi wa kidigitali na mabadiliko ya teknolojia yanayoendelea Duniani.

Dkt. Yonazi aliyasema hayo wakati akifungua kikao Cha wadau wa digitali Cha kujadili tathimini ya mahitaji ya taaluma ya TEHAMA yatayotekelezwa kupitia mradi wa Tanzania ya kidigitali ambapo alisema kuwa ni wajibu wao kuhakikisha vipaji hivyo vinawapeleka pale wanapopataka kwa TEHAMA kuchangia kukuza uchumi.

“Dunia imebadikika sana na teknolojia ya sasa inabadilika kila siku na cha kwanza ni uelewa wa watu na namna wanavyotumia teknolojia, watu wanazidi kupata fursa ya kutumia TEHAMA katika mambo mbalimbali kwahiyo nyie wataalamu ni lazima muwe wabunifu na kuhakikisha kuwa eneo hili la kidigitali linafikisha nchi tunapopataka,” Alisema Dkt Yonazi.

Alieleza kuwa ni lazima kuwa wanafunzi wa kudumu kwa kuwa tayari kujifunza kila mabadiliko yanapotokea kwasababu mabadiliko yanayoendelea kutokea ni makubwa na yanatokea kila siku na TEHAMA ya nchi haitaendelea kama wao hawatafanya jambo jipya.

“Kila siku muwe wabunifu na wawajibikaji kwa kufanya tafiti na naamini mafunzo haya yatayotolewa kwa watumishi 500 kutoka tasisi mbalimbali yatakuwa ni chachu kwaajili ya kuleta ubunifu na tafiti zenye tija kwa maendeleo ya watu wa nchi yetu,” Alieleza.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya kidigitali Honest Njau alisema kuwa mradi huo wenye thamani ya Dola milioni 150 ni wa miaka mitano na upo chini ya ufadhili wa benki ya Dunia ambapo lengo ni kuendeleza na kupata mawasiliano ambayo ni rahisi na na yenye ubora.

Alifafanua kuwa mradi huo wa Tanzania ya kidigitali unalenga kuboresha na kukuza maunganisho ya kidigitali ya ndani, kikanda na Kimataifa ili kufikisha huduma za mawasiliano pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali za kidigitali kwa wananchi na kuweza kuboresha na kukuza ubunifu kwenye TEHAMA.

Alisema kuwa mradi umegawanyika kwenye maeneo matatu ambayo mojawapo ni ikolojia ya kidigitali ambapo lengo lake ni kujenga taifa la kidigitali kwa kustawisha mazingira wezeshi katika nyanja za uwekezaji kwenye TEHAMA, na nyingine ni uunganishaji wa kidigitali unalenga kuboresha miundombinu ya mawasiliano ya serikali na kuendeleza jitihada za kupunguza ukosefu wa mawasiliano hususani sehemu za pembezoni mwa nchi na sehemu zisizo na mawasiliano kama vile vijijini.

“Upande wa ikolojia ya kidigitali malengo yake yatatekelezwa kupitia mazingira wezeshi ya kidigitali pamoja na upande wa miundombinu ya kusaidia maendeleo ya TEHAMA na kuimarisha biashara ya kieletroniki lakini pia eneo la uunganishaji wa kidigitali itafanyika katika maunganisho ya serikali na kuendeleza mawasiliano vijijini na maeneo yasiyo na mvuto wa kibiashara kwa watoa huduma za mawasiliano,” Alisema.

Alifafanua kuwa eneo la tatu ni jukwaa la huduma za kidigitali ambapo eneo hilo litaongeza litaongeza uwezo wa miundombinu ya msingi inayohitajila katika utoaji wa huduma za umma za kidigitali ili kuongeza ufanisi wa shughuli za ndani za serikali na kuendeleza majukwaa ya uzalishaji wa huduma za umma za kidigitali.

“Katika eneo hili la jukwaa la huduma za kidigitali eneo hili litatekelezwa kupitia huduma za kidigitali na mifumo ya uzalishaji, miundombinu ya kuhifadhia Data pamoja na uwelewa na kujenga uwezo katika masuala ya kidigitali,” Alisema.
Ni Msimu wa Sikukuu na mapumziko kwa watoto... Mpatie mwanao furaha na tabasamu huku ukiipumsha simu yako kwa kumpatia Laptops za Watoto ili ajifunze TEHAMA.

Uwezo:

√ Zinatumia mfumo wa Android
√ Ni Touch screen
√ Zimesheni masomo Nursery mpaka Class 7
√ O-level
√ Anatumia mtoto kuanzia miaka 2-14
√ Cartoon na Games
√ YouTube Kids
√ Zoom Touch
√ Unaweza kuzitumia kwa muonekano wa Tables au Computer kawaida
√ Hard Disk 8GB
√ RAM 2GB
√ Internet kwa WiFi, Hotspot au Modem
√ USB Ports 2
√ HDMI
√ Card Reader 1
√ Earphone na Microphone
√ Unacharge na umeme na inaweza kukaa na betri zaidi ya SAA 8 na kuendelea.
Laptop hizi ni imara na zinawafaa hata wale watoto watundu.
Laptop zinamuonekano wa Tables au Computer kawaida

Tunatuma popote ulipo ndani ya Tanzania kwa gharama za mteja. 
Tunapatikana Mbezi kwa Msuguli, Dar es Salaam.
Kwa maelezo zaidi
Please call 0735997777 au
WhatsApp 0787999774
E-mail; cathbert39@gmail.com