Articles by "TEKNOLOJIA"
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) wakati wa Kikao cha Baraza hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Nishati, Judith akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni (kushoto). Kulia ni Katibu wa Baraza Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Ebeneza Mollel,wakati wa Kikao cha Baraza hilo cha kujadili Mpango na Bajeti hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) wakati wa Kikao cha Baraza hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro. Kushoto Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni.
---------
*Ataka Duru ya Tano ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia kuwa na matokeo chanya

*Aipongeza PURA kuwashirikisha Watumishi kujadili mipango ya Bajeti ya Taasisi

MOROGORO

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga ameielekeza Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) kuendelea kuvutia uwekezaji katika vitalu vilivyo wazi vya mafuta na gesi asilia ili kuongeza kiasi cha nishati hiyo nchini.

Mhe. Kapenga amesema hayo leo wilayani Morogoro, Mkoa wa Morogoro wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa PURA kinacholenga kujadili masuala mbalimbali ikiwemoMpango na Bajeti ya Taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26.

” Mkifanikiwa kuvutia uwekezaji katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi, nchi itaongeza ugunduzi wa rasilimali hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na kuogeza futi za ujazo wa gesi inayopatikana nchini, Pia mkiendelea kuvutia uwekezaji kupitia Duru ya Tano ya kunadi vitalu itakayozinduliwa mwezi machi mwaka huu, pamoja na faida zilizopo, mtakuwa mmeendeleza jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuendelea kuifungua Tanzania kiuchumi na kuvutia uwekezaji zaidi.”Amesema Kapinga.

Amesema Wizara ya Nishati inatambua umuhimu wa tukio la Duru ya Tano ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini pamoja na kutambua kazi kubwa ambayo imeshafanyika kuelekea uzinduzi wa tukio hilo ambalo amesema kuwa ni muhimu katika

kuvutia uwekezaji zaidi katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini.

“ Kwa muda mrefu sasa tumekuwa tukizungumzia ugunduzi wa futi za ujazo trilioni 57.54 pekee ni wakati sasa wa kufanya zaidi na zaidi ili tuweze kuongeza ugunduzi wa rasilimali hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa.” Amesisitiza Mhe.Kapinga

Katika kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi, ameupongeza uongozi wa PURA kwa kuendelea kuwashirikisha watumishi wake katika kujadili, kupanga na kupitisha mipango na Bajeti ya Taasisi kwenye Baraza la Wafanyakazi ikiwa ni utekelezaji pia wa Sheria ya Majadiliano ya Pamoja katika Utumishi wa Umma.

Amesema kufanyika kwa vikao hivyo ni ishara tosha ya utawala bora mahala pa kazi kwa kuwa watumishi wanapata fursa ya kuchangia mawazo yao kuhusu hali ya uendeshaji wa Taasisi hivyo kuendelea kuwa ni sehemu muhimu ya Taasisi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) Mhandisi. Charles Sangweni, amesema duru ya tano (5) ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na

gesi asilia nchini inatarajiwa kuzinduliwa mwezi Machi, 2025 Jijini Dares salaam wakati wa Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki (EAPCE’25).

Amesema PURA inaendelea kusimamia na kudhibiti shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa gesi asilia katika vitalu mbalimbali nchini na Kuhakikisha watanzania wazawa wanashirikishwa katika miradi mbalimbali ya mkondo wa juu wa petroli nchini.
Mtaalamu wa mifumo ya kompyuta wa kampuni ya Vodacom Tanzania PLC, Naamini Yonazi akiongea na wasichana wanaofanya mafunzo ya Code like a Girl yanayofadhiliwa na kampuni hiyo kupitia asasi ya dLab jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki ikiwa ni muendelezo wa programu hiyo yenye lengo la kuleta fursa kwa wasichana kujifunza na kukuza ustadi wa kidijitali, ikiwa ni hatua muhimu ya kuhakikisha wasichana wanajikita zaidi katika masomo ya Tehama.
Mkuu wa idara ya Rasilimali watu Sorayya Shareef akitoa vyeti kwa wanafunzi walioshiriki katika programu hiyo.
Wanafunzi wakiwasilisha kazi zao.
Wanafunzi wakifurahia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Phillip Besiimire (kushoto), Mkurugenzi wa Kituo cha Uendelezaji na Uhawilishaji wa Teknolojia, Dkt. Athman Mgumia (kati) akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania Shigeki Komatsubara wakiwa pamoja wakati wa kutangaza ushirikiano wao ili kuandaa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz2025) na Future Ready Summit 2025 yanayolenga kuangazia bunifu na maandalizi ya maisha katika wakati ujao, hafla hii imefanyika mnamo tarehe 5 Februari 2025 jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.

KATIKA kuendelea kuimarisha ubunifu na kuendesha mabadiliko ya kidijitali,Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania kupitia programu yake ya FUNGUO, Vodacom Tanzania, na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) wametangaza ushirikiano wa pamoja wa kuandaaWiki ya Ubunifu Tanzania 2025 (IWTz2025). 

Tukio hili kubwa, litakalojumuisha Mkutano wa Future Ready wa Vodacom, litafanyika kuanzia Mei 12 hadi 16 Mei 2025 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam, pamoja na shughuli zitakazofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.

Mada ya mwaka huu, “Ubunifu kwa Maendeleo Jumuishi naYenye Ustahimilivu”, ikilenga kuonyesha dhamira ya pamoja yakujenga jamii endelevu, jumuishi na ya kisasa katika kutatuachangamoto ya ajira kwa vijana kwenye zama hizi za kidijitalina kuchochea ukuaji wa kibiashara kupitia tafiti na ubunifu.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza ushirikiano huo kwa waandishi wa habari  Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Phillip Besiimire amesema ushirikiano huo utaleta mabadiliko katika sekta ya ubunifu nchini Tanzania, kwa kuunganisha wabunifu na wajasiriamali wa kimataifa kutoka sehemu mbalimbali za dunia. 

“Tunalenga kuleta mitazamo na taaluma za kimataifa kwenye mijadalahii na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha mabadiliko yakidijitali, sambamba na kuanzisha mifumo ya ikolojia yaubunifu inayoongozwa na vijana. 

“Jitihada za Vodacom za kutumia teknolojia kwa lengo la kuboresha maisha ndiozinazounda msingi wa ushirikiano huu unaoendeshwa na maonoyanayofanana ya kuwawezesha watanzania kuendelea kupitiaUchumi wa kidijitali ulioendelevu na jumuishi.”

Aidha amesema kuwa mkutano wa Vodacom wa Future Ready Summit (FRS2025) ni tukio linaloweka msingi wa maadhimisho hayo pamoja nakuibeba kauli mbiu ya “Kubadilisha hatma ya miji: Usasa, Uendelevu na Jumuishi”, ambayo inazungumzia umuhimu wa kuibadili miji ya Tanzania kwa ajili ya kutatua changamoto zinazotokana ukuaji wa kasi, mabadiliko ya tabia nchi namabadiliko ya teknolojia.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, Shigeki Komatsubara, amesisitiza dhamira ya UNDP ya kujenga mfumo wa ubunifuulio jumuishi na wenye ustahimilivu. 

“Tunatambua kuwa ubunifu ni nyenzo muhimu katika kushughulikia changamoto za maendeleo endelevu na kuunda fursa shirikishi.Kupitiaushirikiano huu, tunalenga kuwainua Watanzania, hasa vijana nawanawake, kuwa chachu ya mabadiliko chanya. 

“Wiki yaUbunifu Tanzania 2025 (IWTz2025) itaonyesha ari ya ubunifuTanzania kwenye jukwaa la kimataifa, kuvutia uhamasishaji naushirikiano kupitia na mifumo iliyofanikiwa duniani.”

Kuhusu ajenda zitakazohusika katika maadhimisho ya Wiki ya Ubunifu ni hayo itahusisha mijadala mtambuka, warsha na maonyesho, huku lengo likiwa ni Mustakabali wa miji mahiri, endelevu na jumuishi, Uwezeshaji wa vijana kwenye zama za kidijitali, Uboreshaji wa tafiti na ubunifu kwa ajili ya biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali, Mkurugenzi wa Kituo cha Maendeleo na Uhamisho wa Teknolojia kutoka Tume ya Sayansina Teknolojia (COSTECH), Dk Athumani Ngumia alisema mchango muhimu wa ushirikiano huo ni kukuza ubunifu.

“COSTECH imejidhatiti kuwaunganisha wadau kwa lengo la kuchochea utafiti, teknolojia na ubunifu ambao unaendana navipaumbele vya nchi katika maendeleo na maono ya mwaka2050.Maadhimisho ya Wiki ya Ubunifu kwa mwaka 2025 nijukwaa pekee kwa ajili ya sekta binafsi na umma kupeleleza nakutekeleza masuluhisho kwa ajili ya ukuaji endelevu.”

Wiki ya ubunifu 2025 (IWTZ2025) na mkutano wa Future Ready Summit (FRS2025) inatarajia kuwaleta pamoja washiriki, wazungumzaji na wabunifu kutoka Tanzania, Afrika na sehemu mbalimbali duniani na kuwa jukwaa muhimu la kubadilishana maarifa, kuendeleza ushirikiano wenye tija na kuhamasishamawazo yenye kuleta mabadiliko.

Washiriki wa matukio haya wanahamasishwa kutekeleza shughuli mbalimbali sambamba na matukio hayo muhimu kwa lengo la kuhakikisha watu wengi zaidi nchini wanawezakunufaika na mikutano hiyo itakayo kuwa inafanyika kwenyeKituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere.
 

Wakati huo huo Meneja Program kutoka FUNGUO Joseph Manirakiza ametumia nafasi hiyo kuelezea kwa kina umuhimu wa ushirikiano huo sambamba na kutambua mchango wa bunifu katika kukuza maendeleo endelevu

Kuhusu Programu ya FUNGUO ni kwamba inajitolea kuendeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) nchini Tanzania kwa kutumia mbinu shirikishi inayolenga kusaidia maendeleo ya biashara bunifu na zinazozingatia athari chanya kwa jamii, hususan kwakuimarisha mazingira ya ubunifu kwa wajasiriamali na biasharandogo na za kati (MSMEs). 

Aidha FUNGUO inatambua kuwa kusaidiana kukuza biashara hizo siyo tu kutachangia kuongeza ajira, hususan kwa wanawake na vijana, bali pia kutaboresha kipato, kuboresha hali ya maisha, na kuchochea maendeleo jumuishi naendelevu.

Pia Mpango huo unafadhiliwa kwa pamoja na Umoja wa Ulaya(kupitia Mpango wa BEGIN), Serikali ya Uingereza (kupitiaMpango wa Ushirikiano wa Teknolojia na Ubunifu barani Afrika - ATIP), na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP). 

FUNGUO unatekelezwa na UNDP Tanzania kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja waMataifa (UNCDF). Ushirikiano huu wa wadau mbalimbali unahakikisha ufanisi na athari chanya katika mazingira yaubunifu nchini Tanzania. 

Kwa kushirikiana kwa karibu na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH) pamoja nataasisi nyingine za serikali, FUNGUO inalenga kuchangia maendeleo endelevu nchini kwa kuweka mazingira wezeshi kwabiashara bunifu na MSMEs.

Kuhusu Vodacom Tanzania ni mtoa huduma wa mawasiliano anaeongoza nchini Tanzania, ikiwa na mtandao wa data wa kasi zaidi. Tunahudumia zaidi ya wateja milioni 26.3. Vodacom Tanzania na kampuni zake tanzu ni sehemu ya Vodacom Group yenye usajili nchini Afrika Kusini, ambayo nayo inamilikiwa naVodacom Group Plc yenye makao makuu Uingereza. 

Wakati COSTECH ni Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania iliyoanzishwa kupitia Sheria ya Bunge Na. 7 ya mwaka 1986.Pia ni shirika la umma linalohusika na kuratibu na kukuza shughuli za utafiti na maendeleo yateknolojia nchini. 

Pia, inatoa ushauri kwa serikali kuhusumasuala yote yanayohusiana na sayansi, teknolojia, na ubunifu(STI) kwa lengo la kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamiinchini Tanzania.COSTECH inafanya kazi chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi naTeknolojia.
Mkuu wa Idara ya Mkakati wa TEHAMA na Uhandisi wa Programu wa Vodacom Tanzania PLC Cleopatra Mukangara (kushoto), akipokea tuzo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Ukaguzi na Udhibiti wa Mifumo ya Taarifa (ISACA) Abdulrahman Hussein (kulia) kwa Kujitolea na Kuchangia Ukuaji wa ISACA Tanzania Chapter (Usalama wa Mtandao, Ukaguzi na Hatari) mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Tuzo hii inatambua juhudi za kampuni ya Vodacom katika kukuza uvumbuzi na ubora kaVodacom yapewa tuzo kwa Kujitolea katika Sekta ya TEHAMA.
tika sekta ya teknolojia. Wafanyakazi wengine watatu wa kampuni hiyo pia walipewa tuzo kwa kuthamini mchango wao katika Sekta ya TEHAMA.
Dar es Salaam, Tanzania, 25 Novemba 2024 – MultiChoice Tanzania imetangaza ushirikiano na Vodacom Tanzania PLC, kampuni inayoongoza katika mawasiliano ya simu nchini, kwa ajili ya kuzindua Showmax – jukwaa maarufu la burudani kupitia video barani Afrika. Ushirikiano huu muhimu unaashiria zama mpya za burudani bora na rahisi kufikiwa Tanzania, huku ukiunga mkono matumizi ya kidijitali nchini na kuinua vipaji vya ndani.  

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi, Jacqueline Woiso, Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania, alisema, “hili ni tukio kubwa nchini kwetu ambapo makampuni makubwa mawili katika sekta za mawasiliano na burudani wameungana kwa maslahi ya wateja wetu. Ushirikiano huu unasisitiza dhamira yetu ya kutoa maudhui ya kimataifa ya kiwango cha juu huku tukitumia teknolojia ya kisasa ya Vodacom Tanzania.”

Woiso aliongeza, “Ushirikiano huu utawezesha wateja wa Vodacom kote Tanzania kupata maudhui bora ya vipindi vya TV, filamu, michezo, na makala kupitia Showmax, hivyo kufanya burudani ya kiwango cha juu iwe rahisi kufikiwa katika vifaa mbalimbali vya kidijitali. Showmax ina maktaba kubwa ya maudhui inayojumuisha uzalishaji wa ndani na nje ya Tanzania, pamoja na michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza, ikienda sambamba na ladha mbalimbali za burudani. Ushirikiano huu ni mfano dhahiri wa jinsi ushirikiano unavyoweza kuleta thamani kubwa kwa wateja, kuweka maslahi yao mbele ya ushindani.”  

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Phillip Besiimire, alisema “Ushirikiano huu unaendana kikamilifu na dhamira yetu ya kusaidia Tanzania kuelekea zama za kidijitali huku tukiboresha maisha kupitia teknolojia. Kadri upatikanaji wa simu janja unavyoongezeka nchini, tumejikita katika kuboresha huduma zetu za kidijitali kwenye burudani, elimu, kilimo, afya, na usafiri. Leo, tunajivunia kuongeza Showmax katika orodha yetu ya burudani, tukiwawezesha wateja wetu kufurahia maudhui ya kiwango cha juu yanayowagusa moja kwa moja.”  
Uzinduzi wa Showmax pia unaangazia umuhimu wa kuunga mkono vipaji na uzalishaji wa maudhui ya ndani. Kupitia maudhui ya ndani yanayoonyeshwa kwenye jukwaa hili, lengo ni kuinua sauti za wasanii wa Kitanzania na kuhakikisha kazi zao zinafikia hadhira kubwa zaidi. Hatua hii si tu inaimarisha sekta ya burudani bali pia inachangia ukuaji wa uchumi wa ubunifu wa ndani. 
 
Ili kunufaika na ushirikiano huu, Vodacom na MultiChoice wanatoa vifurushi vya kipekee vya data vinavyowezesha wateja wa Vodacom kufurahia maudhui ya burudani kwa gharama nafuu. Watumiaji wanaweza kupakua programu ya Showmax, kununua kifurushi, na kufurahia ulimwengu wa burudani ya kuvutia.

Mkuu wa Idara ya Usalama wa Mtandaoni kutoka Vodacom Tanzania Plc Bw. Joel Kazoba akizungumza katika uzinduzi wa klabu ya usalama wa mitandao uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam cha Tehama kilichopo Kijitonyama. Klabu hiyo imezinduliwa kwa ushirikiano baina ya Vodacom na chuo hicho cha Tehama yenye madhumuni ya kuhamasisha wanafunzi kujiunga katika masomo ya usalama mtandaoni na kuwapa uzoefu wa vitendo katika kukabiliana na vitisho vya usalama wa kidijitali. Pembeni ni Mkuu wa Kitengo cha mafunzo ya kielectroniki Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Baraka Maiseli.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bi. Warda Obathany (Kushoto) akimkabidhi cheti mshindi wa kwanza mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam cha Tehama Alexus Samson (Kulia) wa michezo ya vitendo maarufu kama “capture the flag”. wa mashindano ya kudukua mifumo (capture the flag) Mashindano hayo yalifanyika katika uzinduzi wa klabu ya usalama Chuoni hapo wiki hii. Uzinduzi huo ulifanywa na Vodacom Tanzania plc kwa kushirikiana na chuo cha Tehama UDSM klabu hii inaenda kuhamasisha wanafunzi kujiunga katika masomo ya usalama mtandaoni na kuwapa uzoefu wa vitendo katika kukabiliana na vitisho vya usalama wa kidijitali.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bi. Warda Obathany (Kushoto) akimkabidhi zawadi mshindi wa tatu mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar Es Salaam cha Tehama UDSM Rafia Maganga (Kulia) wa mashindano ya kudukua mifumo (capture the flag) Mashindano hayo yaliofanyika katika uzinduzi wa klabu chuoni hapo wiki hii. Uzinduzi huo ulifanywa na Vodacom Tanzania plc kwa kushirikiana na chuo cha Tehama UDSM klabu hii inaenda kuhamasisha wanafunzi kujiunga katika masomo ya usalama mtandaoni na kuwapa uzoefu wa vitendo katika kukabiliana na vitisho vya usalama wa kidijitali.

Na Mwandishi Wetu.

Vodacom Tanzania Plc, kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wameanzisha Klabu ya Usalama wa Mitandao katika Chuo Kikuu ch dar es Salaam na kuzindua siku ya michezo kwa vitendo maarufu kama “Capture the Flag (CTF)”. Uzinduzi huu wa pamoja, ulimefanyika katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam cha Tehama (CoICT) kilichopo Kijitonyama.

Klabu hii imeanzishwa mahsusi ili kuhamasisha wanafunzi wa Kitanzania kujiunga na masomo ya usalama wa mitandao, kutoa uzoefu kwa vitendo katika kukabiliana na vitisho vya usalama wa kidijitali na kukuza ushirikiano kati ya wataalamu wa sekta, wanafunzi na viongozi wa serikali.

Kuundwa kwa Klabu ya Usalama wa Mitandao ya UDSM ni hatua muhimu katika kukabiliana na mahitaji yanayokua ya wataalamu wenye ujuzi katika usalama wa mitandao nchini Tanzania. Klabu hii itawapa wanafunzi fursa za mafunzo ya vitendo na kuwapa uzoefu kuhusu changamoto zinazoikabili sekta ya usalama wa kidijitali leo na hatimaye kusaidia kulinda mustakabali wa dijitali hapa nchini.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Usalama Mtandaoni Joel Kazoba kutoka Vodacom aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Tehama wa Kampuni hiyo, Athuman Mlinga alisema, “Tunafuraha kushirikiana na CoICT kuzindua Klabu ya Usalama wa Mitandao na kuandaa michezo hii ya CTF, tunawapa wanafunzi zaidi ya maarifa ya nadharia pekee. Capture the Flag (CTF) ni aina ya mashindano ambapo watu wanatatua mafumbo na matatizo yanayohusiana na usalama wa mtandao ili kupata vidokezo vilivyofichwa katika mifumo.”

Kazoba aliongeza kwamba mchezo huu unasaidia kuboresha ujuzi katika udukuzi wa mifumo na kulinda kompyuta. Kila changamoto, au kidokezo inawakilisha udhaifu wa usalama katika mifumo ambao timu inapaswa kugundua na kushughulikia, hii inahimiza fikra za kina na ukuzaji wa ujuzi. Kwa kushiriki katika michezo hii ya CTFs, wanafunzi wanajifunza kufikiri kama wataalamu wa usalama wa mtandao wakichambua udhaifu, kutathmini hatari na kuunda suluhu za kujihami dhidi ya mashambulizi halisi katika mifumo ya kompyuta.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tawala wa wilaya ya Kinondoni Warda Obathany aliyemwakilisha mgeni rasmi Mh Naibu Waziri wa Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Patrobas Katambi alisisitiza umuhimu wa mpango huu, akisema, “Klabu za usalama wa mtandao ni zaidi ya shughuli za ziada; ni njia ya mafunzo kwa walinzi wa kidijitali wa kesho.”

Mh aliongeza kwamba, “hivi sasa kuna ongezeko la matumizi ya dijitali nchini, Hivyo kuna haja kubwa ya wataalamu wa usalama wa mitandao wa ndani ya nchi wanaoelewa changamoto za mifumo zinazoikabili Tanzania. Na mpango huu ni maendeleo makubwa katika kukabiliana na mahitaji yanayokua ya Tanzania ya wataalamu wenye ujuzi katika usalama wa mtandao,” aliongezea.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo ya Elekroniki na Mawasiliano Profesa Baraka Maiseli aliyemwakilisha Mkuu wa chuo cha Tehama cha UDSM, Profesa Joel Mtebe, alifafanua kwamba “Mbali na ujuzi wa vitendo, ushirikiano huu unawapa wanafunzi wetu njia ya kuelekea kwenye sekta ya usalama wa mitandao, ukitoa maarifa watakayopata, ushauri, na uhusiano ambao utasaidia katika nyanja zao za kazi. Tunawashukuru Vodacom kwa uwekezaji katika mpango huu, unaoakisi maono ya muda mrefu kwa Tanzania yenye usalama wa kidijitali, na viongozi vijana walio tayari kukabiliana na changamoto za usalama wa mtandao zinazo endelea kuibuka,” aliongeza.

Kadri vitisho vya mtandao vinavyoendelea kuibuka, umuhimu wa mafunzo ya awali na ukuzaji wa ujuzi utaendelea kukua. Kwa mpango huu, Vodacom Tanzania na UDSM sio tu kwamba wanakuza wataalamu wenye ujuzi wa usalama wa mtandao bali pia wanachangia katika mustakabali salama na thabiti wa dijitali kwa Watanzania wote. Shughuli za klabu na michezo ijayo ya CTF zitaendelea kuwahamasisha, kuwafundisha na kuwapa nguvu wanafunzi kuwa viongozi katika usalama wa mtandao na pia kuhakikisha Tanzania inabaki salama katika enzi hizi za kidijitali.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewahimiza vijana nchini kuchangamkia fursa za kidijitali ikiwemo akili bandia (Artificial Intelligence), kwa kubuni mifumo itakayotatua changamoto za kijamii na hivyo kujipatia kipato.

Meneja TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali ametoa rai hiyo Ijumaa Oktoba 11, 2024 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana 2024 yanayofanyika katika uwanja wa Furahisha jijini Mwanza kuanzia Oktoba 08-14, 2024 yakiwa na kaulimbiu ya "vijana na matumizi ya fursa za kidijitali kwa maendeleo endelevu".

Amesema mamlaka hiyo inawawezesha vijana kunufaika na matumizi ya kidijitali kwa kutoa rasilimali za mawasiliano ili kufanikisha mawazo yao ya kibunifu ikiwemo kupata masafa na namba za kuwafikia wateja bure.

"Vijana wenggi wamekuwa na kasumba ya kupuuzia fursa mbalimbali za kimaendeleo zinazotangazwa mpaka waone watu wengine wamefanikiwa, tunapaswa kuchangamkia soko la kidijiti ili kujikwamua kiuchumia" amesema John Waronga ambaye ni mmoja wa vijana waliotembelea banda la TCRA.

Maonesho ya wiki ya vijana yamefunguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye amewataka vijana kutumia mitandao kujiajiri na kukuza uchumi ili kuwa na taifa lenye uchumi imara huku akiwataka kutotumia maendeleo hayo ya kidijitali kwa matumizi mabaya ikiwemo kuchochea chuki, kueneza taarifa za uongo na picha ama video zisizo na maadili katika jamii.


Majaliwa amesema ili kufikia dira ya maendeleo ya taifa 2050, teknolojia ya kidijitali ina fursa muhimu na maadhimisho hayo ni jukwaa muhimu kwa vijana kuwa chachu ya maendeleo na kwamba Serikali itaendelea kuwajengea vijana uwezo ili kufanikisha bunifu zao.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akitoa ufafanuzi wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete (kushoto) alipotembelea banda la TCRA.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete (kushoto) alipotembelea banda la TCRA.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akitoa elimu kwa mwananchi aliyetembelea maonesho ya wiki ya vijana kuhusu kampeni ya 'Ni Rahisi Sana' inayoendeshwa na TCRA kwa lengo la kuhamasisha jamii kutambua fursa za kidijiti nk.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akioa elimu kwa mwananchi aliyeembelea banda la TCRA.
Tazama Video hapa chini