

Na Mwandishi Wetu
Msanii wa muziki na mjasiriamali maarufu, Gigy Money, amesema tayari ameolewa kwa muda sasa lakini ameamua kuweka ndoa yake faraghani ili kulinda mahusiano yake dhidi ya changamoto za hadharani.
Akizungumza na waandishi wa habari, Gigy alisema kuwa watu wamezoea kumuona kwenye mahusiano mbalimbali, lakini safari hii amechagua utulivu na maisha ya kifamilia bila kelele za mitandaoni. Alisisitiza kuwa mambo mazuri yanahitaji kulindwa, akifananisha ndoa na kitu cha thamani ambacho kikifichwa hudumu zaidi kuliko kinapowekwa wazi kwa kila mtu.
Msanii huyo pia alieleza kuwa baada ya kuolewa amebadili mwenendo wa maisha, akisema sasa ameanza ukurasa mpya wa utulivu na kujitambua zaidi. Aidha, alibainisha kuwa amepewa jina jipya la Rahuya na mume wake, jambo alilolipokea kwa furaha kama ishara ya mwanzo wa maisha mapya.
Gigy alimalizia kwa kusema anachotamani zaidi kwa sasa ni amani ya moyo na ndoa yenye utulivu, akieleza kuwa amechoka kupitia misukosuko ya mahusiano ya zamani na sasa anatafuta maisha ya kudumu na yenye heshima.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KLABU ya Simba SC imemtakia kila la heri mshambuliaji wake, Kibu Denis Prosper, baada ya kukamilisha uhamisho wake kwenda klabu ya Al Nasr SC ya Libya kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu wenye thamani ya dola za Kimarekani 250,000.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Simba usiku huu, Kibu anaondoka Msimbazi baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa misimu minne na nusu tangu alipojiunga mwaka 2021 akitokea Geita Gold.
“Baada ya kuwa sehemu ya kikosi chetu kwa misimu minne na nusu, Kibu Denis ‘Mkandaji’ ameuzwa na sasa anakwenda kuanza maisha mapya nje ya Simba SC,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.
Katika kipindi chake akiwa Simba, Kibu amekuwa mshambuliaji tegemeo akichangia mabao na pasi za mabao katika mashindano ya ndani na kimataifa, huku akisaidia timu kutwaa mataji mbalimbali ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho.
Uhamisho wake kwenda Al Nasr unamkutanisha tena na mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Steven Dese Mukwala, ambaye tayari alishasajiliwa na klabu hiyo ya Libya mapema.
Hatua hiyo inaonekana kuwa sehemu ya mabadiliko ya kikosi cha Simba kuelekea nusu ya pili ya msimu, huku mashabiki wakimtakia mafanikio mema Kibu katika changamoto yake mpya nje ya Tanzania.
Kikao hicho kimeibua matumaini mapya kwa watengeneza maudhui, wengi wao wakieleza kuwa hatua ya Serikali kusogea karibu na kusikiliza changamoto zao ni mwanzo wa mabadiliko chanya katika kukuza tasnia ya filamu na maudhui ya kidijitali nchini.
Salamu kwa mashabikiAkizungumzia siku yake ya kuzaliwa, baadhi ya wanamuziki wenzake wamempongeza kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa dansi kimataifa. “Kamanda Ras Makunja ni alama ya ubunifu na uthubutu. Bila yeye, muziki wa dansi ungekuwa tofauti kabisa kwenye ramani ya kimataifa,” alisema mmoja wa wanabendi.
Mwisho wa habari
Kwa sasa, shangwe na burudani zinaendelea kambini kwao FFU-Ughaibuni, huku mashabiki wakiungana kumtakia maisha marefu, afya njema na mafanikio zaidi katika safari yake ya muziki.
Happy Birthday Kamanda Ras Makunja! 🎉🎶
Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Mbwana Yusuph maarufu kama Mbosso, amewashukuru uongozi na mashabiki wa Simba Sports Club kwa kumpa nafasi ya kipekee kuwa headliner wa Tamasha la kihistoria la SIMBA DAY lililofanyika hivi karibuni.
Kupitia barua yake ya wazi aliyoiandika kwenye mtandao wa Instagram, Mbosso alisema uongozi wa Simba SC uliweza kumpa nafasi hiyo adhimu ambayo ingeweza kupewa msanii mwingine yeyote, lakini badala yake walimchagua yeye kuongoza burudani ya tamasha hilo kubwa.
“Kwangu mimi hili ni tamasha langu kubwa la kwanza kufanyia kwenye uwanja linalohusiana na mpira wa miguu katika maisha yangu ya muziki. Ndiyo maana nilijitahidi kwa uwezo wangu wote kuhakikisha nawapa furaha mashabiki na wadau wa Simba SC,” aliandika Mbosso.
Ameeleza kuwa SIMBA DAY kwake haikuwa tu tamasha, bali pia jukwaa la kuonyesha vipaji vyake vingine ambavyo huenda havijawahi kuonekana, ikiwemo kuigiza kwa uhalisia, kuimba na kuwasilisha ubunifu kwa kiwango cha juu.
Aidha, Mbosso alibainisha kuwa licha ya kutumia gharama kubwa kuhakikisha onyesho lake linafanikiwa, hakufanya hivyo kwa faida binafsi bali kwa mapenzi yake makubwa kwa Simba Sports Club na mashabiki wake.
“Nina imani mlifurahi, na kama kulikuwa na sehemu nilikosea au kulikuwa na mapungufu, naomba mnisamehe kwa kuwa mimi ni mwanadamu na siwezi kufanya vyote kwa ukamilifu,” alisema Mbosso huku akimalizia barua yake kwa kutia sahihi ya jina lake la kisanii Mad Max Mbosso Khan.
Tamasha la SIMBA DAY ni tukio la kila mwaka la Simba SC linalokutanisha mashabiki kutoka maeneo mbalimbali nchini, likiwa na lengo la kutambulisha kikosi kipya cha wachezaji na kutoa burudani ya muziki.






“Sherehe hizi ni sehemu ya kusherehekea safari yetu ya miaka 25 ya kuunganisha Watanzania. Tunataka tuendelee kushirikiana na wateja wetu si tu kupitia huduma za kidijitali, bali pia kwa kutengeneza kumbukumbu za pamoja za furaha na mshikamano,” alisema Venanty.
Vodacom imesisitiza kuwa itaendelea na mfululizo wa matukio ya kusherekea miaka 25 yake katika mikoa mbalimbali nchini, ikilenga kuimarisha uhusiano wa karibu na wateja wake.

Na Mwandishi Wetu, Arusha.
.jpeg)



























.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)












