Articles by "UTALII"
Showing posts with label UTALII. Show all posts
Dar es Salaam – On March 21, U.S. Ambassador Michael Battle, alongside Mafia District's Administrative Secretary, Hon. Olivanus Paul Thomas, commemorated the successful completion of the third phase of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation (AFCP) project to restore the historic Swahili ruins of Kua on Juani Island, within the Mafia Island archipelago.

From 2017 through 2022, the U.S. Embassy awarded a total of $434,929 (approximately Tshs 1.1 billion) to World Monuments Fund (WMF) via the AFCP program of the U.S. Department of State. This funding supported the preservation of these ancient ruins in a collaborative effort with the local community. The celebratory event at the Kua Ruins hosted local government officials, a delegate from the Ministry of Natural Resources, WMF representatives, and community members.

Nestled off Tanzania's coast on Juani Island, the ancient Swahili town of Kua traces back to the 13th century, standing as one of East Africa's largest medieval Swahili settlements. The site boasts a significant number of residential structures that have withstood the test of time, including a grand palace and five mosques. Protected under the Antiquities Act No. 10 of 1964, as amended by Act No. 22 of 1979, the Kua Ruins are a testament to Swahili architectural ingenuity and historical importance. Ambassador Battle noted, “Through the AFCP program, the U.S. has not only preserved the essence of Kua but also ensured local communities benefit from these preservation efforts.”

Since it's inception in 2001, the Ambassador’s Fund for Cultural Preservation (AFCP) has aimed to safeguard notable cultural heritage sites across the globe. The American people have generously contributed over one million dollars in grants since 2002, supporting a wide range of preservation projects in Tanzania. These projects include the restoration of the 18th-century Kizimkazi Mosque in Zanzibar, the ancient trade port ruins of Kilwa Kisiwani, the prehistoric rock art in Kondoa, the 19th-century Bwanga House in Pangani, and the historical Shumba and Micheweni mosques in Pemba, among others.

World Monuments Fund (WMF), the project's lead implementing organization, is a premier non-profit entity dedicated to preserving the world’s most iconic heritage sites. With over 50 years of experience in more than 90 countries, WMF’s skilled experts employ advanced preservation techniques to safeguard architectural and cultural landmarks worldwide.

Embracing Cultural Heritage and Partnership: U.S. Ambassador Michael Battle alongside District Administrative Secretary Olivanus Paul Thomas (4th from left), other district and community leaders and World Monument Fund (WMF) representatives at Kua Ruins, commemorating the completion of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation’s (AFCP) project phase 3 for the restoration of Swahili ruins of Kua on Juani Island, Mafia. From 2017 to 2022, the U.S. Embassy awarded the WMF a total of $434,929 to preserve these ancient Swahili ruins in collaboration with local residents.
Na Andrew Chale, Zanzibar.
MTOTO wa gwiji wa muziki wa Afrika, Hayati Oliver Mutukudzi, Selmor Mutukudzi amekonga nyoyo za mashabiki mbalimbali waliofurika viunga vya Ngome Kongwe ndani ya Mambo Club Unguja, Zanzibar, katika usiku wa tamasha la 21, lililoanza leo Februari 9-11, 2024.

Selmor Mutukudzi ambaye alipanda jukwaani na bendi yake, aliweza kuanza na vionjo vya nyimbo maarufu za Baba yake ikiwemo‘Neria’ na Todii’ ambavyo viliamasha hisia za mashabiki wengi waliolipuka kwa shangwe na kuimba nae pamoja.

Kando ya jukwaa hilo, awali, Selmor Mutukudzi amesema kuwa, ilikuwa ni ndoto yake ya muda mrefu kushiriki tamasha la Sauti za Busara ambapo amekuwa akituma maombi ya kushiriki ila akikosa nafasi.

‘’Nimekuwa, nikiomba kushiriki Sauti za Busara, muda mrefu ila nikikosa nafasi. Nashukuru kwa mwaka huu kwani imenipa hali kubwa ya kuonesha owezo wangu.

Selmor Mutukudzi kipaji chake kilioneka tokea akiwa na miaka 10, baada ya baba yake kumuingiza kwenye muziki na kuonesha nyota yake ambapo akaweza kuwa na nyimbo mbalimbali ikiwemo Albamu aliyoipa jina la ‘Shungu’ aliyoitoa mwaka 2008 huku ikiwa na nyimbo kama Chiro,Iwewe, Neni, Shungu na kibao cha Handiende.

Hadi sasa ameweza kufikisha Albamu Sita ambazo zikiwa na nyimbo mbalimbali, aidha mbali ya muziki pia ni mwanaharakati wa utetezi wa mabinti wa kike na hata kuungana kuimba wimbo wa ‘’Strong Girls’’ ikiwa ni harakati za kutetea mabinti hao Afrika.
Burudani ikiendelea...
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akizungumza na wakazi wa mji wa Moshi waliojitokeza katika uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU Forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS). Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho akisoma risala kwa Mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU Forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).
Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu akitoa shukrani wa wakazi wa Moshi na viunga vyake waliohudhuria katika uzinduzi katika kampeni ya kutangaza vivutio vilivyopo katika hifadhi ya msitu Rau.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori (wa pili toka kushoto) akiwa ameongozana na viongozi wengine wakipata maelezo toka kwa Afisa Uhifadhi wa msitu Rau wakati wakitembelea vivutio vilivyopo katika msitu huo.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG

...KAMPENI YA KUTANGAZA UTALII 'TWENDE TUKACHARU RAU' YAWA KIVUTIO KWA WAKAZI WA MOSHI, KILIMANJARO

Mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori ametoa rai wa Wananchi kuendelea kutunza hifadhi ya msitu wa Rau na kuacha tabia kutupa taka taka ndani ya hifadhi.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kutangaza Utalii 'TWENDE TUKACHARU RAU forest 2023' lililofanyika mwishoni wa wiki iliyopita katika hifadhi ya Msitu wa Rau -Moshi inayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Amesema kuwa hifadhi ya Msitu Rau ni mapafu wa mji wa Moshi kwa vile husaidia kufyonza hewa chafu hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha unaendelea kutunzwa na kuacha mara tabia ya baadhi ya watu wanaovamia na kufanya shughuli za kibinadamu.

"Hakikisheni msitu huu unatunzwa, acheni kufanya shughuli za kilimo ndani hifadhi, acheni kuingiza mifungo ndani hifadhi," amesema.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akipitishwa katika mashamba ya mpunga.
Safari ya kutembelea vivutia vya hifadhi ya msitu wa Rau.
Utalii ukiendelea ndani ya hifadhi ya msitu Rau.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori akiwa na wageni wengine wakitazama moja ya chemchem za maji zilizo katika msitu huo.
---
Pia ametoa rai kwa TFS na makapuni za watalii kuendelea kuwahamasisha watalii kutembelea vivutuo vilivyopo ndani msitu huo, kwani hifadhi hiyo ipo mita chache kutoka mji wa Moshi na inafikika kirahisi.

Amesema rais Dkt Samia Suluhu amefungua fursa za Utalii kupitia filamu yake 'Royal Tour', hivyo ni vyema kuendelea kuunga mkono juhudi zake ili kuweza kuongeza idadi ya watalii nchini na ndiyo maana Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi wakishirikiana na Ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS) Moshi wamezindua Kampeni ya Kutangaza Utalii ikolojia ndani ya Hifadhi ya Misitu wa Rau ili kuongeza idadi ya watalii.

Aliongeza kuwa mpaka sasa hivi hafurahishwi na idadi ndogo ya watalii wanaofika kutembelea msitu huo, lija ya ukaribu uliopo ambapo ni watalii 1,200 tu kwa mwaka hutembelea msitu huo.

Awali akisoma taarifa kwa niaba Mkuu wa hifadhi ya msitu Rau, Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho, amesema  ndani msitu huo kuna chemchem 20 ambazo zinapeleka kuwepo mito mikubwa 3 inayotiririsha maji kipindi chote cha mwaka.

Aidha amesema mito hiyo ni chanzo cha maji inayotumika katika kilimo cha umwagiliaji cha mpunga ambapo hekta takriban 3,000  hutegemea maji kutoka msitu huu.

"Msitu una vivutio vingi ikiwemo mimea pamoja na miti ya asili ambayo haipatikana katika maeneo mengine, ikiwemo Mti wa Mvule ambayo unazaidi ya miaka 200 ni mrefu kuliko yote barani Afrika," amesema.

Aliongeza kuwa utalii mkubwa unaofanyika katika msitu huo ni Utalii wa baiskeli, ibada,  tafiti na masomo, picha, nyuki na kuangalia madhari ya misitu ndege na wanyama wanaopatikana ndani ya hifadhi.

Mazoezi ya viungo nayo yalikuwepo katika ya kuingia msituni.
Waendesha baskeli nao walinyoosha viungo.
Mhifadhi daraja la pili msitu wa Rau Zayana Mrisho akiwakaribisha wageni.
Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu akiwasalimia wageni.
Mgeni Rasmi mkuu wa Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Kisare Makori (kushoto) akiwa pamoja na Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu (kulia) wakizindua utalii wa baskeli.
Utalii wa baskeli nao ulifanyika.
Kwa upande wake Meya wa manispaa ya Moshi Zuberi Kidumu amefurahishwa na ubunifu wa kuandaa kampeni ili kutangaza vivutio vilivyopo katika hifadhi ya msitu Rau.

"Nawaomba waandaaji kuendelea kuandaa matamasha mengi zaidi yatakayosaidia wananchi wengi ili waweze kutembelea msitu huo na kujifunza mambo mbali mbali," amesema Meya Kidumu.

Hifadhi ya Misitu Rau ulianzishwa ukiwa na ukubwa  hekari 3526, ambapo kwa sasa ni hekta 584 zimebaki kutokana uvamizi wa Wananchi na kuanzisha shughuli za kilimo.

Mkuu wa sehemu ya Utangazaji Utalii wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Anna Lawuo (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu vivutio mbalimbali vinavyopatikana kwenye hifadhi zinazosimamiwa na Wakala huo. Kulia ni Mhifadhi Mwandamizi wa TFS katika Shamba la Miti West Kilimanjaro, Robert Faida
Mratibu wa mashindano ya Marathon West Kili Tour Challenge 2023 Mensieur Elly akiwa kwenye kikao na waandishi wa habari wakati akielezea maandalizi ya mashindano hayo yanayotarajia kufanyika Juni 24 na Juni 25 mwaka huu katika Shamba la Miti West Kilimanjaro mkoani Kilimanjaro
WAKALA wa Huduma za Misitu Tazania (TFS) kupitia Shamba la Miti la West Kilimanjaro wameandaa mashindano ya michezo ya pikipiki, baiskeli pamoja na mbio za marathon zinazotarajia kufanyika Juni 24 na 25, mwaka 2023 ambazo zitafanyika katika Misitu hiyo.

Akizungumza leo Juni 14, 2023 jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari kuelekea West Kili Tour Challenge 2023 , Mratibu wa mashindano hayo Mensieut Elly amefafanua kutakuwa na michezo ya watoto na watu wazima watakaokimbia mbio za marathon za km tano, 10 na 21.

Pia amesema kutakuwa na waendesha pikipiki watakaoendesha km 35 mpaka 75 wakipita kwenye kingo za Mlima Kilimanjaro sambamba na matembezi ya kuona maporomoko ya maji, mapango, ambapo litawahusisha wanamichezo na watu wa kawaida wanaotaka kwenda kutembelea na kula nyama choma.

"Gharama za ushiriki wa challenge hizi ni Sh 10,000 kwa watu wa kawaida wanaotaka kwenda kutembea na kula, sh 15,000 watakaoenda kwenye maporomoko na sh 35,000 kwa wanaotaka kushiriki mbio za marathon ambapo watapata medali na kila kitu.Mashindano yatashirikisha wageni kutoka Canada, Marekani, Kenya, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani na Tanzania, " amesema.

Awali Mhifadhi Mwandamizi wa TFS Shamba la miti west Kilimanjaro Robert Faida amesema michezo hiyo imeandaliwa ikiwa ni sehemu mojawapo ya kutekeleza maelekezo ya Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa ya kuhimiza umuhimu wa kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kutangaza utalii.

Ameongeza kupitia kampeni ya 'West kili Tour Challenge' itahusisha michezo mbalimbali huku akitumia nafasi hiyo kuihimiza jamii kushiriki kikamilifu kwenye ualii wa ndani kwa kutembelea vivutio, kutengeneza mitandao na watu wa Kimataifa pamoja na kufanya uwekezaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Sehemu ya Utangazaji Utalii TFS Anna Lawuo ameeleza kwamba kuna misitu 23 ya kupandwa inayotumika kufanya michezo ya aina mbalimbali ikiwemo ya mbio za magari ambayo ina vigezo vya kitaifa na Kimataifa.

"Katika msitu huo kuna changamoto ya hotel hivyo, ni fursa kwa Watanzania kwenda kwenye michezo hiyo kuangalia maeneo yanayofaa kwa uwekezaji wa hoteli, " amesema.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohammed Mchengerwa (wa pili kushoto) akiwa katika pikipiki zilizokabidhiwa na Benki ya CRDB kwa Kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia jijini Arusha kwa ajili ya kusaidia katika doria na kuimarisha ulinzi na usalama kwa watalii. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia), Mkuu wa Wilaya Arusha, Felician Mtahengerwa (wa kwanza kulia), na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo.
---
Arusha Tarehe 18 Mei 2023 - Serikali imeipongeza Benki ya CRDB kwa kutoa msaada wa pikipiki 15 kwa Jeshi la Polisi mkoani Arusha ili kuimarisha doria zitakazoongeza usalama kwa watalii wanaokuja nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Utalii na Maliasili, Mohamed Mchengerwa alipopokea pikipiki hizo zenye thamani ya TZS 40 milioni kwenye hafla fupi iliyofanyika katika Kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia kilichopo jijini hapa.
Waziri amesema sekta ya utalii ina umuhimu mkubwa katika uchumi na maendeleo ya wananchi nchini kwani ndiyo inayoongoza kwa kuliingizia taifa fedha nyingi za kigeni, ikiwa ya pili kwa kuchangia kwenye Pato la Taifa (GDP), na ya tatu kwa kutoa ajira.

“Ripoti za Benki Kuu Tanzania (BOT) zinaonyesha sekta ya utalii inaendelea kuimarika baada ya kuathiriwa na janga la UVIKO-19. Mapato yatokanayo na utalii kwa Machi yalifikia Dola za Marekani bilioni 2.787 ikilinganishwa na dola milioni 885 kipindi kama hicho mwaka 2021. Katika mwezi huo, jumla ya watalii 1,574,630 waliingia nchini,” amesema Mchengerwa na kuongeza huku akipongeza jitihada kubwa zilizofanywa na Rais Samia katika kuitangaza Tanzania kupitia filamu ya Royal Tour.

“Kipeeke kabisa naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa msaada huu wa pikipiki 15 ambao Benki yetu ya CRDB imeutoa kwa kituo chetu hichi. Pikipiki hizi zitawawezesha askari kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Askari watakabiliana haraka na dharula jambo litakalosaidia kuimarisha usalama kwa watalii na kuifanya nchi yetu kuwa kivutio kikubwa hivyo wageni wengi kuja kuitembelea.”
Mwaka 2020, sekta ya utalii ilichangia asilimia 10.6 kwenye pato la taifa ila kiasi hichi kilishuka hadi asilimia 5.7 mwaka 2021 kutokana na athari za UVIKO-19 hivyo kuilazimu Serikali kuchuku ahatua za makusudi kuifufua kwa kufuata taratibu za Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufanya matangazo kimataifa kwa Rais Samia Suluhu Hassan mwenyewe kurekodi filamu ya ‘The Royal Tour.’

Ili kuhakikisha usalama wa watalii wanaokuja nchini, Serikali ilianzisha kitengo maalum cha utalii na diplomasia kwa ajili ya kuwahudumia watalii na wanadiplomasia wanaofika nchini kutalii ama kuwekeza kwa haraka.

Kwa kuwa jiji la Arusha ndio kitovu cha utalii nchini, kituo hicho kimejengwa huko na askari wake walipewa mafunzo ya ziada ndani na nje ya nchi juu ya namna bora ya kuhudumia watalii. Vituo vingine vidogo vimefunguliwa katika wilaya za Arumeru, Karatu, Monduli na Longido.
Akikabidhi pikipiki hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kila mmoja anafahamu umuhimu wa amani, utulivu na usalama katika maendeleo ya nchi kiuchumi, kijamii na kisiasa hivyo ni jukumu la jamii nzima kushiriki kuuimarisha.

“Pamoja na kuwepo hali ya amani na utulivu nchini, bado baadhi ya matukio ya uhalifu hujitokeza kama vile vile uporaji wanaofanyiwa raia hata watalii wanaokuja kutembelea vivutio vilivyopo nchini. Ili Jeshi la Polisi litekeleze majukumu yake kwa ufanisi linahitaji vitendea kazi vya kutosha,” amesema Nsekela.

Mkurugenzi huyo amesema wanayo furaha kubwa kukabidhi pikipiki hizo ili kuwasaidia askari kukimbizana na wahalifu wanaowapora watalii au kusafirisha mihadarati hivyo kuharibu sifa njema za jiji hili la kitalii.
“Tunaamini matumizi sahihi ya pikipiki hizi yatasaidia kudhibiti uhalifu jijini hapa na tunaahidi tutaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini kupunguza baadhi ya changamoto zinazokwamisha ufanisi wake ili nchi yetu iendelee kuwa salama kwa biashara na uwekezaji,” amesema Nsekela.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Edith Swebe, amesema jitihada zinazoendelea kuutanga utalii wa Tanzania umelifanya Jiji la Arusha kupokea wageni wengi wanaoongeza haja ya askari polisi kuwapo katika kila eneo.
“Tunachokifanya sasa hivi ni kusimamia mradi wa utalii salama ambao unahitaji askari kuwapo kila walipo wageni. Pikipiki hizi tunazozipokea zitasaidia kuwafikisha askari kwenye maeneo ambako magari hayawezi kufika kwa urahisi zikiwamo barabara nyembamba. Jeshi la Polisi linaaminimazingira salama ni kivutio cha utalii,” amesema Edith ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa kamanda wa Mkoa wa Simiyu.

Hata hivyo, ameiomba Serikali na wadau wengine wa utalii kuliwezesha jeshi hilo kupata pikipiki nyingine 10 zitakazofanya kata zote 25 za Jiji la Arusha kuwa na pikipiki moja ya doria itakayosaidia utekelezaji wa mradi wa utalii salama.