
Na Mwandishi Wetu, Manyara.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Nchemba, ametoa maagizo kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Manyara kufuatilia matumizi ya fedha zilizotumika katika ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto pamoja na ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo.
Ametoa maagizo hayo wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo, akieleza kuwa amepokea taarifa za kuwepo kwa ubadhirifu wa fedha katika utekelezaji wa mradi huo. Waziri Mkuu alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, kwa kufuatilia suala hilo na kufanikisha kurejeshwa kwa fedha zilizobainika kupotea, huku akisisitiza kuwa wahusika wote wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Faraja Ngerageza, alisema mradi huo ulianza mwaka 2023 na unatarajiwa kuanza kutumika mwezi Machi mwaka huu.
Baadhi ya wananchi wa Kiteto walimshukuru Waziri Mkuu kwa kutembelea eneo hilo, kusikiliza kero zao na kuahidi kuzitatua, wakieleza kuwa ziara hiyo imeongeza matumaini ya kuboreshwa kwa huduma za maendeleo katika wilaya hiyo.
Ziara ya Waziri Mkuu inaendelea katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Manyara, ambapo kwa sasa yupo wilayani Simanjiro akizindua miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa siku 100 kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Wafanyakazi wa Umma (PSSSF) Ndg. Abdul-Razaq Badru kuhakikisha Awamu ya Pili ujenzi wa kiwanda cha kuchakata Bidhaa za Ngozi Kilimanjaro unakamilika na kuanza kufanya kazi ifikapo Julai 2024.
Agizo hilo amelitoa leo Februari 22, 2024 alipo fanya ziara ya kukagua ujenzi katika kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) ikiwa ni sehemu ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.
Mhandisi Luhemeja amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani ya zao la ngozi ghafi, kufungua fursa za soko la uhakika la Ngozi kutoka kwa wafugaji, kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya fedha za ndani na za kigeni.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemaja (kushoto) akikagua bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) leo Februari 22, 2024 ikiwa ni mwendelezo wa kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa wakati alipokagua ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) ya Dodoma katika eneo la Mkonze jijini Dodoma






Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akifuatilia Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8) unaoendelea katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Palais des Congres mjini Tunis,Tunisia, Agosti 27, 2022. Waziri Mkuu anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo.




















.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

















