TRENDING NOW







Mr. Saviour Chibiya (third from right), Absa Bank East Africa Regional Executive, engaged in a strategic discussion with Mr. Rumisho Shikonyi (third from right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during his courtesy visit to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. He was accompanied by Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second from right), along with members of the executive committee. The engagement centered on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Obedi Laiser (third from left), Managing Director of Absa Bank Tanzania, engages in conversation with Mr. Rumisho Shikonyi (right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during a courtesy visit by Mr. Saviour Chibiya (second from left), Absa’s East Africa Regional Executive, to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. The meeting focused on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Mr. Saviour Chibiya (left), Absa Bank East Africa Regional Executive, listens attentively to Mr. Rumisho Shikonyi (right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during his courtesy visit to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. He was accompanied by Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second from left), along with members of the executive committee. The engagement centered on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na The Runners Club, imezindua rasmi mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zinazotarajiwa kufanyika Mei 17 mwaka huu jijini Dar es Salaam, huku zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakitarajiwa kushiriki.

Tukio hilo linalozidi kujizolea umaarufu kila mwaka, linalenga kuhamasisha mazoezi ya mwili, kukuza mshikamano wa kijamii pamoja na kuendeleza mtindo wa maisha yenye afya miongoni mwa Watanzania.

Kwa mujibu wa waandaaji, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na makundi matatu ya mbio ambayo ni kilomita 21.1 (Nusu Marathon), kilomita 10 na kilomita 5, yakitoa fursa kwa washiriki wa rika na viwango tofauti kushiriki.

Usajili wa kushiriki mbio hizo tayari umefunguliwa kupitia majukwaa rasmi, ambapo wakimbiaji wa kada zote, kuanzia wanariadha wakongwe hadi wapenda mazoezi na washiriki wa burudani, wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisema mbio hizo ni zaidi ya mashindano ya riadha, bali ni jukwaa muhimu la kuimarisha afya na ustawi wa jamii.

“Katika Absa, tunaamini katika kuleta athari chanya katika jamii tunazozihudumia. Absa Dar City Marathon siyo tu mbio, bali ni jukwaa linalokuza afya, umoja na ustawi wa jamii,” alisema Luhanga.

Aliongeza kuwa benki hiyo inajivunia kushirikiana na The Runners Club katika kuandaa tukio hilo na kuhimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki katika mazoezi ya mwili.

Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo na Makamu wa Rais wa The Runners Club, Godphrey Mindu, alisema marathon hiyo inaonesha ukuaji wa kasi wa utamaduni wa kukimbia nchini.

“Tumeshuhudia jamii zikikusanyika kupitia mazoezi ya viungo, na tukio hili ni sherehe ya mshikamano huo. Tunatarajia kuwapokea wakimbiaji wa viwango vyote na kuwapatia uzoefu bora siku ya mashindano,” alisema Mindu.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Felix Donald, alisema mbio hizo zina mchango mkubwa katika kukuza vipaji vya wanariadha chipukizi pamoja na kuimarisha nidhamu na afya kwa jamii.

“Matukio kama haya ni msingi wa kukuza riadha nchini. Tunayaunga mkono kwa sababu yanasaidia kujenga kizazi kipya cha wanamichezo,” alisema Donald.

Wawakilishi kutoka vilabu mbalimbali vya kukimbia walisisitiza kuwa tukio hilo limekuwa kiunganishi muhimu cha jamii. Johnson Mbunda “Balozi” kutoka Goba Roads Runners alisema marathon hiyo inawaunganisha wakimbiaji kutoka maeneo mbalimbali na kuwajengea urafiki wa kudumu.

Kwa upande wake, mwanachama wa Kigamboni Runners alisema tukio hilo limekuwa sehemu ya mkusanyiko wa kila mwaka unaowapa fursa washiriki kuungana na marafiki, familia pamoja na kukutana na watu wapya huku wakifurahia mandhari ya jiji la Dar es Salaam.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wanachama wa vilabu mbalimbali vya kukimbia ikiwemo Tabata Runners, TOT Runners, Absa Running Club, Salasala Runners na Kigamboni Runners, pamoja na wadhamini wa tukio hilo.

Ushiriki wao umeendelea kuonesha kukua kwa kasi kwa utamaduni wa kukimbia nchini na mshikamano mkubwa wa jamii katika kuunga mkono jitihada za kukuza afya kupitia michezo.

Watu kadhaa wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana uso kwa uso na lori katika eneo la Mlima “S”, kijiji cha Lumango, wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Ajali hiyo ilihusisha basi la kampuni ya ZL Super Safari lililokuwa likitoka Ifakara kuelekea Morogoro, pamoja na lori lililokuwa limebeba kokoto.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa lori aliyekuwa akijaribu bajaji iliyokuwa mbele yake, hali iliyosababisha kugongana na basi hilo.

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ili kuzungumzia tukio hilo zinaendelea.

Huu ni ujumbe wa onyo la wazi na la dhati—afya si jambo la kubahatisha wala la kusukuma mbele kwa sababu yoyote ile. Kwa muda mrefu tumekuwa na mazoea ya kupuuza dalili ndogo ndogo, tukijipa faraja kwamba ni uchovu wa kazi, msongo wa mawazo, au athari za starehe za muda mfupi. Ukweli mchungu ni kwamba magonjwa mengi hayaanzi kwa kelele; huanza taratibu, kimya kimya, hadi pale yanapofikia hatua mbaya ambapo gharama yake huwa kubwa—kimwili, kifedha, na hata kisaikolojia.

Ni muhimu kuelewa kwamba mwili wako huwa unatoa ishara mapema kabisa. Maumivu ya mara kwa mara, uchovu usioelezeka, kizunguzungu, au hata mabadiliko madogo ya kawaida ya mwili—hivi vyote vinaweza kuwa ni tahadhari. Lakini wengi wetu huchagua kuvipuuzia, aidha kwa sababu ya shughuli nyingi, hofu ya kugundua tatizo, au imani kwamba “bado niko sawa.” Hapo ndipo tunapokosea.

Ukweli ni huu: kuchelewa kuchukua hatua kunaweza kugharimu maisha. Ugonjwa unapokuwa umechelewa kugundulika, matibabu yake huwa magumu zaidi, gharama zake huongezeka, na wakati mwingine hata uwezekano wa kupona hupungua. Wakati mwingine tunajikuta tukitumia nguvu nyingi kupambana na kitu ambacho kingeweza kuzuilika au kudhibitiwa mapema kabisa.

Kwa vijana hasa, kuna changamoto ya maisha ya kasi—kazi, starehe, mitandao, na pilika pilika zisizoisha. Katika harakati hizi, afya huwekwa pembeni. Wengine huona kwenda hospitali kama kupoteza muda, au huogopa majibu watakayopata. Lakini ukweli ni kwamba, kujua hali yako ya afya mapema ni nguvu, si udhaifu. Ni hatua ya ujasiri na kujipenda.

Ni wakati sasa wa kubadili mtazamo:
Afya iwe kipaumbele, si chaguo la ziada.
Kufanya uchunguzi wa afya iwe sehemu ya ratiba yako ya kawaida, si jambo la dharura tu.
Kusikiliza mwili wako iwe kawaida, si mpaka uumie sana ndipo uchukue hatua.

Jamii yenye watu wenye afya bora ni jamii yenye nguvu, maendeleo, na ustawi. Lakini jamii inayopuuzia afya yake hujikuta ikikumbwa na mzigo mkubwa wa magonjwa, vifo vya mapema, na hasara zisizo za lazima.

Hivyo basi, huu ni wito wa tahadhari kwa kila mmoja:
Usisubiri hadi hali iwe mbaya.
Usidharau dalili yoyote.
Usikimbie ukweli wa afya yako.

Chukua hatua sasa. Jilinde. Jipende. Afya yako ni jukumu lako.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 21 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (African Women Leaders Network - AWLN), ulioongozwa na Marais wastaafu wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Sahle-Work Zewde, jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yalijikita katika hali ya kisiasa nchini pamoja na matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, yakihusisha pia umuhimu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
Ujumbe huo upo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kufanya mashauriano na viongozi mbalimbali wa kitaifa kuhusu maendeleo ya kisiasa na juhudi zinazoendelea za kuimarisha demokrasia na utawala bora, ikiwa ni sehemu ya mchango wa wanawake viongozi wa Afrika katika kulinda amani na utulivu barani.



Na Janeth Raphael MichuziTv .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu mkubwa wa kundi la Mama na Baba Lishe nchini, akieleza kuwa ni mhimili muhimu katika kuendeleza ustawi wa jamii na uchumi wa taifa.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika Kongamano la Kitaifa la Mama na Baba Lishe Tanzania, Rais Samia amesema kundi hilo lina mchango mkubwa katika kuhakikisha wananchi, wakiwemo wafanyakazi, wanafunzi na wasafiri, wanapata huduma ya chakula kwa wakati, jambo linalosaidia kuimarisha shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii.

Ameeleza kuwa chakula ni afya, na hivyo Mama na Baba Lishe wanachangia moja kwa moja katika afya na ustawi wa wananchi, hivyo wanastahili kutambuliwa, kuheshimiwa na kulindwa katika shughuli zao za kila siku.

“Shughuli za Mama na Baba Lishe zinapaswa kutambuliwa na kuheshimiwa kwa hadhi inayolingana na mchango wao katika maisha ya kila siku. Hawapaswi kusumbuliwa wala kunyanyaswa,” amesema Rais Samia.



Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha inatoa mazingira bora ya kisera na kisheria yatakayowezesha kutambuliwa rasmi kwa kundi hilo, pamoja na kuimarisha mchango wao katika uchumi wa taifa. Amesema hatua hiyo pia inahusisha kuimarisha sekta ya biashara ndogo ndogo kupitia mipango ya urasimishaji na uwezeshaji.

Rais Samia pia amebainisha kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuweka mikakati mahususi ya kuwawezesha Mama na Baba Lishe, ili waweze kuwa sehemu muhimu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Katika hotuba yake, alitaja pia uamuzi wa kuunda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum kama moja ya juhudi za Serikali katika kuhakikisha makundi mbalimbali yakiwemo Mama na Baba Lishe yanapata usimamizi na heshima stahiki.

“Serikali itahakikisha inasimamia heshima yenu na kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa kazi zenu muhimu kwa taifa,” alisisitiza Rais Samia.

Kongamano hilo limewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya chakula na biashara ndogondogo, likiwa na lengo la kujadili changamoto, fursa na njia bora za kuimarisha sekta ya Mama na Baba Lishe nchini.

Na Mwandishi Wetu

Jumba la sanaa la Rangi Gallery la jijini Dar es Salaam limeandika historia baada ya kuwa taasisi ya kwanza kutoka Tanzania kushiriki katika maonesho ya kimataifa ya sanaa ya Art OnO 2026 yaliyofanyika jijini Seoul, Korea Kusini.

Maonesho hayo yaliyofanyika kuanzia Aprili 2 hadi 5 mwaka huu katika kituo cha maonesho cha SETEC, yameelezwa kuwa miongoni mwa majukwaa makubwa na yenye hadhi ya juu barani Asia yanayowakutanisha wadau wa sanaa kutoka mataifa mbalimbali duniani.

Kupitia ushiriki huo, Rangi Gallery ilisimama sambamba na majumba makubwa ya sanaa kutoka nchi 12 zikiwemo Japan, Ujerumani, Uswisi na mataifa mengine, hatua iliyotajwa kuiweka Tanzania katika ramani ya sanaa ya kisasa duniani.

Katika maonesho hayo, Rangi Gallery iliwasilisha kazi za wasanii wanne wanawake kutoka Tanzania ambao ni Theresia Venance, Tulsi Patel, Valerie Asiimwe Amani na Turakella Editha Gyindo.

Kazi za wasanii hao zilionesha upekee wa sanaa ya kisasa ya Kitanzania, zikigusa masuala ya utambulisho, mila, mabadiliko ya kijamii, uzoefu wa mwanamke pamoja na uhusiano wa binadamu na mazingira.

Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Rangi Gallery, Lorna Mashiba Albou, alisema ushiriki huo ni ushahidi kuwa sanaa ya Tanzania ina uwezo mkubwa wa kushindana kimataifa.

“Wasanii wetu wameiwakilisha vyema Tanzania katika jukwaa hili la kimataifa. Hii inaonesha vipaji vya Kitanzania vinaweza kufika mbali vikipewa nafasi sahihi,” alisema Lorna.

Aliongeza kuwa licha ya wasanii wote waliowasilishwa kuwa wanawake, jambo hilo halikupangwa mahsusi bali lilitokana na ubora wa kazi zao.

Ushiriki wa Rangi Gallery pia umepewa uzito wa kidiplomasia baada ya Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Togolani Edriss Mavura, kuhudhuria maonesho hayo na kushuhudia kazi zilizooneshwa.

Wadau wa sanaa wameeleza kuwa hatua hiyo ni mwanzo wa safari kubwa kwa Tanzania katika soko la kimataifa la sanaa, huku baadhi ya wasanii walioshiriki wakitarajiwa kuiwakilisha nchi katika maonesho makubwa ya Venice Biennale 2026 nchini Italia.

Rangi Gallery ilianzishwa jijini Dar es Salaam na Lorna Mashiba Albou, ambaye awali alikuwa mwanasheria kabla ya kuhamia katika sekta ya uchumi wa ubunifu.

Mbali na kuonesha kazi za wasanii wa ndani, jumba hilo linaendesha programu ya Rangi Nyumbani Residency, inayolenga kuwaunganisha wasanii wa Tanzania na mitandao ya kimataifa.

Wachambuzi wanasema Tanzania imekuwa na vipaji vingi vya sanaa kwa miaka mingi, lakini changamoto kubwa imekuwa ukosefu wa majukwaa ya kuvitangaza. Kupitia juhudi za taasisi kama Rangi Gallery, sasa mlango wa dunia umeanza kufunguka kwa wasanii wa Kitanzania.

Na Mwandishi Wetu

Mwanariadha nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu, ameendelea kuandika historia baada ya kutwaa ushindi mkubwa katika mbio maarufu za Boston Marathon 2026 zilizofanyika nchini Marekani, akionyesha ubora mkubwa mbele ya wakimbiaji bora duniani.

Simbu alimaliza mbio hizo za kilomita 42.195 kwa muda wa saa 2:03, akionesha kasi ya juu na uthabiti mkubwa tangu mwanzo hadi mwisho wa mashindano hayo yaliyovuta hisia za mashabiki wa riadha duniani kote.

Ushindi huo umeifanya Tanzania kuendelea kung’ara katika ramani ya michezo ya kimataifa, huku Simbu akionekana kuwa mmoja wa wakimbiaji hatari zaidi duniani kwa sasa.

Kilichowavutia wengi ni namna mwanariadha huyo alivyoimarisha rekodi yake ukilinganisha na mwaka uliopita, ambapo alitumia saa 2:05:04, jambo linaloonyesha maandalizi makubwa na nidhamu ya hali ya juu aliyonayo.

Katika mbio hizo zilizoshirikisha maelfu ya washiriki kutoka mataifa mbalimbali, Simbu alionekana mwenye kujiamini tangu mwanzo, akibaki kwenye kundi la mbele kabla ya kuongeza kasi katika hatua za mwisho na kuondoka na ushindi ulioshangiliwa na mashabiki wengi.

Baadhi ya wachambuzi wa michezo wameeleza kuwa mafanikio hayo ni ishara kuwa Tanzania bado ina hazina kubwa ya vipaji vya riadha vinavyoweza kutikisa dunia.

Mashabiki nchini Tanzania wamefurika mitandaoni kumpongeza Simbu, wakimtaja kuwa balozi mkubwa wa taifa anayelitangaza jina la nchi kupitia michezo.

Boston Marathon ni moja ya mashindano makubwa na yenye heshima duniani, hivyo ushindi wa Simbu unaongeza hadhi yake binafsi pamoja na heshima ya Tanzania kimataifa.

Kwa ushindi huo, Simbu ameendelea kuthibitisha kuwa kazi, nidhamu na kujituma vinaweza kuipeleka Tanzania kileleni mwa dunia ya michezo.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Halmashauri ya Jiji la Arusha imezindua rasmi zoezi la uhamasishaji wa wananchi kuhusu fursa mbalimbali zilizopo ndani ya jiji hilo, likihusisha taasisi za serikali pamoja na taasisi za kifedha, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Uzinduzi huo umefanyika katika Kata ya Terrat na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi waliopata fursa ya kujifunza na kuelimishwa kuhusu upatikanaji wa mikopo, uwekezaji pamoja na usimamizi bora wa fedha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Maendeleo wa Jiji la Arusha, Shabani Manyama, aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Jiji, amesema halmashauri imetenga zaidi ya Sh bilioni 5.3 kwa ajili ya mikopo kwa wananchi katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Manyama alisema fedha hizo zipo tayari kutolewa, hivyo wananchi wanapaswa kutumia nafasi hiyo kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao kupitia shughuli mbalimbali za uzalishaji.

Aidha, aliwataka wananchi kuwa makini wanapochukua mikopo kwa kuhakikisha wanakuwa na malengo mahsusi, kufanya tathmini ya biashara zao na kutumia fedha hizo kwa kazi iliyokusudiwa.

“Mkopo si fedha ya matumizi holela, bali ni nyenzo ya kukuza uchumi wa mtu binafsi na jamii kwa ujumla,” alisema Manyama.

Miongoni mwa wananchi walioshiriki uzinduzi huo, Elizabeth Shirima alisema fursa hizo zimekuja kwa wakati muafaka na zina matumaini ya kuwasaidia wananchi wengi kujikwamua kimaisha.
Alisema utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu utawapa nafasi wananchi wengi zaidi kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilaitairo, Kata ya Terrat, Aron Lukumai, alisema wananchi wamepokea kwa furaha ujio wa fursa hizo, akieleza kuwa changamoto kubwa iliyokuwepo awali ilikuwa ni ukosefu wa taarifa na uelewa.

Aliongeza kuwa kusogezwa kwa huduma karibu na wananchi kutarahisisha upatikanaji wa mikopo na kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli za kiuchumi.

Kwa ujumla, zoezi hilo limepokelewa kwa mwitikio chanya na linatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa Jiji la Arusha kupitia matumizi sahihi ya fursa zinazotolewa.
Na Mwandishi Wetu

Baadhi ya wachimbaji na wakazi wa eneo la Mirerani wilayani Simanjiro, mkoani Manyara, wameeleza kutoridhishwa na uamuzi wa wafanyabiashara wa eneo la Opec Machimboni kupandisha bei za bidhaa mbalimbali kwa madai ya kupanda kwa gharama za maisha.

Malalamiko hayo yameibuka baada ya kusambaa kwa tangazo linaloonyesha wafanyabiashara hao wamekutana na kukubaliana kuweka bei mpya za bidhaa mbalimbali zinazotumika na wachimbaji pamoja na wananchi wa eneo hilo.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, baadhi ya bidhaa zilizopandishwa bei ni pamoja na maji ya kunywa, vinywaji baridi, maziwa, vocha, soda na bidhaa nyingine za matumizi ya kila siku.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wachimbaji walisema hatua hiyo siyo sahihi kwa kuwa imefanyika kwa makubaliano ya wafanyabiashara pekee bila kuzingatia hali halisi ya uchumi wala uwezo wa watumiaji wa mwisho.

Walisema kupanda kwa bei hizo kunaongeza ugumu wa maisha kwa wachimbaji wadogo na wafanyakazi wa migodini ambao hutegemea kipato cha kila siku.

Mbali na hilo, wananchi hao pia walilalamikia nauli ya bodaboda inayotozwa ndani ya eneo tengefu la madini kutoka getini hadi Opec kufikia Sh2,000, wakidai kuwa haiendani na bei elekezi iliyotangazwa hivi karibuni na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (SUMATRA).

“Wanaoumia ni watumiaji wa mwisho. Ifike mahali wananchi wapaze sauti juu ya hali hii,” alisema mmoja wa wachimbaji aliyeomba kutotajwa jina.

Baadhi ya wananchi wamezitaka mamlaka husika kuingilia kati suala hilo kwa kufanya uchunguzi wa bei zinazotozwa na kuhakikisha kunakuwa na usimamizi wa haki kwa walaji na wafanyabiashara.

Hadi tunakwenda mitamboni, viongozi wa eneo hilo hawakuwa wametoa tamko rasmi kuhusu malalamiko hayo