


Picha ya pamoja ya viongozi.
Na Mwandishi Wetu, Njombe.
CRDB Bank Plc imeshiriki katika kilele cha Maadhimisho ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) 2026 yanayofanyika Njombe Region, ikionesha dhamira yake ya kuunga mkono juhudi za Serikali pamoja na wadau mbalimbali katika kuboresha mazingira ya kazi na ustawi wa wafanyakazi.
Maadhimisho hayo yanabebwa na kaulimbiu isemayo, “Mazingira Bora ya Kazi Kisaikolojia ni Njia ya Kuimarisha Ustawi wa Wafanyakazi na Kujenga Taasisi Imara.”
Kilele cha maadhimisho hayo kimeongozwa na Deus Sangu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano.
Katika maonesho hayo, benki hiyo imekuwa ikiendelea kutoa huduma mbalimbali za kifedha kwa wananchi wa Njombe na maeneo ya jirani, zikiwemo ufunguzi wa akaunti, elimu ya fedha pamoja na huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.
Wananchi wengi wamejitokeza kutembelea banda la benki hiyo kwa lengo la kujifunza na kunufaika na huduma zinazotolewa, hatua inayotajwa kusaidia kuongeza uelewa kuhusu matumizi sahihi ya huduma za kifedha.
Mbali na huduma hizo, CRDB Bank Plc pia imeendelea kutoa huduma za afya bure kwa wananchi kama sehemu ya mchango wake kwa jamii.
Benki hiyo ni mdhamini mkuu wa maadhimisho hayo muhimu, ambapo ushiriki wake unaakisi dhamira ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi sambamba na kulinda afya na usalama wa jamii.

Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kisheria wa Tume, Ndg. Cyprian Mbugano akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Watendaji wa Uchaguzi na mambo muhimu ya kuzingatia.
Sehemu ya washiriki ambao ni watendaji wa Uchaguzi kutoka katika Jimbo la Isimani na Kata 12 za Tanzania Bara wakifuatilia hotuba ya ufunguzi.
Mkurugenziu wa Ofisi ya Zanzibar, Ndg. Adam Mkina akiwasilisha mada
Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu wakila viapo vya kujitoa uanachama chama cha siasa na kile cha kutunza siri.Tasnia ya filamu nchini imepata pigo kufuatia kifo cha msanii mkongwe, Mzee Kambi, kilichotokea leo Aprili 27, 2026.
Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na Msemaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Coletha Raymond, aliyesema kuwa msanii huyo alifariki dunia ghafla alipokuwa akiendelea na shughuli zake za kazi.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Coletha alisema Mzee Kambi alikuwa ametoka mkoani Tabora kikazi na aliporejea alielekea moja kwa moja katika shughuli zake kwenye studio za Pilipili, kabla ya kuanza kujisikia vibaya.
“Ni kweli tumempoteza Mzee Kambi. Alikuwa ametoka Tabora na alipofika alienda moja kwa moja kazini katika studio za Pilipilibl. Akiwa kazini ndipo alipozidiwa ghafla na kukimbizwa hospitali, lakini kwa bahati mbaya alifariki dunia,” alisema Coletha.
Aliongeza kuwa chanzo cha kifo kinahusishwa na matatizo ya kiafya yaliyokuwa yakimsumbua, ikiwemo presha na kisukari.
Aidha, alisema Shirikisho la Filamu Tanzania linaendelea na taratibu za ndani kwa kushirikiana na familia ya marehemu ili kupanga mipango ya mazishi, ambapo taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
Kifo cha Mzee Kambi kimeacha pengo kubwa katika tasnia ya filamu nchini, ambapo amekuwa mmoja wa wasanii waliotoa mchango mkubwa katika kukuza sanaa hiyo kwa muda mrefu.
Dkt. Jingu ameyasema hayo tarehe 27, Aprill 2026 jijini Dar es Salaam wakati anafungua mkutano wa mafunzo kwa maafisa wanaoratibu utekelezaji wa Ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu, Viongozi na Wawakilishi wa Sekretarieti ya Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).
"Migogoro kwenye baadhi ya nchi za Maziwa Makuu imeleta mateso makali hasa kwa wanawake na wasichana kupitia unyanyasaji wa kingono na kijinsia. Iwapo migogoro hiyo haitadhibitiwa ipasavyo, kuna uwezekano wa kuleta madhara makubwa zaidi ", amesema Dkt. Jingu.
ICGR inajumuisha nchi wanachama 12 ikiwamo Tanzania, ambazo zinashirikiana katika masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa kuangazia amani, usalama,utawala na maendeleo.
Mafunzo hayo yamefadhiliwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na na Shirika la ujerumani la Deutsche Gesellschaft für Internationale Zusammenarbeit.
.jpeg)
Na Mwandishi Wetu.
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) imepokea ujumbe wa ngazi ya juu kutoka Serikali ya Shirikisho la Somalia kwa ajili ya mafunzo ya kujenga uwezo katika utumishi wa umma, hatua inayoonesha kuimarika kwa ushirikiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Mafunzo hayo yanafanyika katika Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) jijini Dar es Salaam, yakihusisha watumishi kutoka Idara ya Masuala ya Baraza la Mawaziri chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia. Lengo kuu ni kuimarisha mifumo ya uratibu wa serikali, usimamizi wa kumbukumbu, ulinganifu wa sera na ufuatiliaji wa maamuzi.
Hafla ya ufunguzi ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa serikali, akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Xavier Daudi Mrope, aliyemwakilisha Serikali ya Tanzania.
Katika hotuba ya ufunguzi, Mkuu wa Chuo na Afisa Mtendaji Mkuu wa TPSC, Dr. Ernest Mabonesho alieleza kuwa mpango huo ni hatua muhimu katika kuimarisha taasisi za umma na kuongeza ufanisi wa utendaji wa serikali. Chuo hicho, kilichoanzishwa rasmi mwaka 2000 baada ya kuunganishwa kwa taasisi za mafunzo ya utumishi wa umma, kimeendelea kuwa kitovu cha ubora katika mafunzo, utafiti na ushauri wa kiutawala.
Imeelezwa kuwa mpango huo umeandaliwa kwa ombi la Serikali ya Somalia, kufuatia majadiliano kati ya TPSC na Ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Mafunzo yanajumuisha nadharia, vitendo na uzoefu wa taasisi mbalimbali, yakilenga kuwapatia washiriki mbinu zitakazoweza kutumika katika kuboresha mifumo ya utawala nchini Somalia.
Mpango huo pia umeelezwa kuwa ni matokeo ya kuimarika kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Somalia, hasa baada ya ziara ya ngazi ya juu ya Serikali ya Tanzania nchini Somalia mwezi Desemba 2025, iliyoweka msingi wa ushirikiano katika maendeleo ya sekta ya umma.
Washiriki na viongozi wamebainisha kuwa mbali na kujenga ujuzi, mafunzo hayo yanatarajiwa kuimarisha mitandao ya kitaaluma na ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.
Hatua hii inaonesha nafasi ya Tanzania katika kusaidia maendeleo ya taasisi za umma katika ukanda huu, huku nchi mbalimbali zikiongeza juhudi za kushirikiana kuboresha utawala na utoaji wa huduma kwa wananchi.














































.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)