TRENDING NOW








Na Mwandishi Wetu

Tasnia ya filamu nchini imepata pigo kufuatia kifo cha msanii mkongwe, Mzee Kambi, kilichotokea leo Aprili 27, 2026.

Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na Msemaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Coletha Raymond, aliyesema kuwa msanii huyo alifariki dunia ghafla alipokuwa akiendelea na shughuli zake za kazi.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Coletha alisema Mzee Kambi alikuwa ametoka mkoani Tabora kikazi na aliporejea alielekea moja kwa moja katika shughuli zake kwenye studio za Pilipili, kabla ya kuanza kujisikia vibaya.

“Ni kweli tumempoteza Mzee Kambi. Alikuwa ametoka Tabora na alipofika alienda moja kwa moja kazini katika studio za Pilipilibl. Akiwa kazini ndipo alipozidiwa ghafla na kukimbizwa hospitali, lakini kwa bahati mbaya alifariki dunia,” alisema Coletha.

Aliongeza kuwa chanzo cha kifo kinahusishwa na matatizo ya kiafya yaliyokuwa yakimsumbua, ikiwemo presha na kisukari.

Aidha, alisema Shirikisho la Filamu Tanzania linaendelea na taratibu za ndani kwa kushirikiana na familia ya marehemu ili kupanga mipango ya mazishi, ambapo taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
Kifo cha Mzee Kambi kimeacha pengo kubwa katika tasnia ya filamu nchini, ambapo amekuwa mmoja wa wasanii waliotoa mchango mkubwa katika kukuza sanaa hiyo kwa muda mrefu.
Na WMMJWM - Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amesema Ukanda wa Maziwa Makuu umepiga hatua kubwa tangu kupitishwa kwa Azimio namba 1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la mwaka 2000 ambalo ni kiashiria muhimu cha kuonesha juhudi zetu za kushughulikia masuala ya kijinsia kwa amani na usalama. 

Dkt. Jingu ameyasema hayo tarehe 27, Aprill 2026 jijini Dar es Salaam wakati anafungua mkutano wa mafunzo kwa maafisa wanaoratibu utekelezaji wa Ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu, Viongozi na Wawakilishi wa Sekretarieti ya Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).

"Migogoro kwenye baadhi ya nchi za Maziwa Makuu imeleta mateso makali hasa kwa wanawake na wasichana kupitia unyanyasaji wa kingono na kijinsia. Iwapo migogoro hiyo haitadhibitiwa ipasavyo, kuna uwezekano wa kuleta madhara makubwa zaidi ", amesema Dkt. Jingu.

ICGR inajumuisha nchi wanachama 12 ikiwamo Tanzania, ambazo zinashirikiana katika masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa kuangazia amani, usalama,utawala na maendeleo.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na na Shirika la ujerumani la Deutsche Gesellschaft für Internationale Zusammenarbeit.
Mkuu wa Chuo na Afisa Mtendaji Mkuu wa TPSC, Dr. Ernest Mabonesho  akizungumza wakati wa   mafunzo ya kujenga uwezo watumishi wa Serikali ya Somalia  leo jijini Dar es Saam.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Xavier Daudi Mrope akiwa kwenye za pamoja
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Xavier Daudi Mrope akizungmza wakati wa kufungua  mafunzo ya kujenga uwezo  kwa watumishi wa Serikali ya Somalia Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), jijini Dar es Salaam
Sehemu ya washiriki wa Mafunzo hayo.

Na Mwandishi Wetu. 

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) imepokea ujumbe wa ngazi ya juu kutoka Serikali ya Shirikisho la Somalia kwa ajili ya mafunzo ya kujenga uwezo katika utumishi wa umma, hatua inayoonesha kuimarika kwa ushirikiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.

Mafunzo hayo yanafanyika katika Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) jijini Dar es Salaam, yakihusisha watumishi kutoka Idara ya Masuala ya Baraza la Mawaziri chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia. Lengo kuu ni kuimarisha mifumo ya uratibu wa serikali, usimamizi wa kumbukumbu, ulinganifu wa sera na ufuatiliaji wa maamuzi.

Hafla ya ufunguzi ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa serikali, akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Xavier Daudi Mrope, aliyemwakilisha Serikali ya Tanzania.

Katika hotuba ya ufunguzi, Mkuu wa Chuo na Afisa Mtendaji Mkuu wa TPSC, Dr. Ernest Mabonesho alieleza kuwa mpango huo ni hatua muhimu katika kuimarisha taasisi za umma na kuongeza ufanisi wa utendaji wa serikali. Chuo hicho, kilichoanzishwa rasmi mwaka 2000 baada ya kuunganishwa kwa taasisi za mafunzo ya utumishi wa umma, kimeendelea kuwa kitovu cha ubora katika mafunzo, utafiti na ushauri wa kiutawala.

Imeelezwa kuwa mpango huo umeandaliwa kwa ombi la Serikali ya Somalia, kufuatia majadiliano kati ya TPSC na Ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Mafunzo yanajumuisha nadharia, vitendo na uzoefu wa taasisi mbalimbali, yakilenga kuwapatia washiriki mbinu zitakazoweza kutumika katika kuboresha mifumo ya utawala nchini Somalia.

Mpango huo pia umeelezwa kuwa ni matokeo ya kuimarika kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Somalia, hasa baada ya ziara ya ngazi ya juu ya Serikali ya Tanzania nchini Somalia mwezi Desemba 2025, iliyoweka msingi wa ushirikiano katika maendeleo ya sekta ya umma.

Washiriki na viongozi wamebainisha kuwa mbali na kujenga ujuzi, mafunzo hayo yanatarajiwa kuimarisha mitandao ya kitaaluma na ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.

Hatua hii inaonesha nafasi ya Tanzania katika kusaidia maendeleo ya taasisi za umma katika ukanda huu, huku nchi mbalimbali zikiongeza juhudi za kushirikiana kuboresha utawala na utoaji wa huduma kwa wananchi.

 

Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akizungumza wakati akifunga rasmi Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026 yaliofanyika Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akihutubia wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika kwenye Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa walimu waliofanya vizuri kwenye somo analofundisha katika Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026 yaliofanyika Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akihutubia wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika kwenye Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Sehemu ya wadau wa elimu wakiwa kwenye hafla ya Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika katika Halmashauri ya Momba, Mkoani Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akipokelewa alipowasili kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akitembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akitembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akitembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye (mwenye skafu) akiteta jambo na Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala (wa pili kushoto) kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro akifuatilia.
Sehemu ya wanafunzi na wadau wa elimu wakiwa kwenye maandamano ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika katika Halmashauri ya Momba, Mkoani Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye (mwenye skafu), Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bw. Simon Nanyaro (wa pili kulia) na Mratibu wa TEN/MET, Bi. Martha Makala (wa kwanza kushoto) pamoja na meza kuu wakipokea maandamano ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akwa katika picha ya pamoja na wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.

Na Mwandishi Wetu, Songwe

MTANDAO wa Elimu Tanzania (TEN/MET) umechangia kiasi cha shilingi Millioni 53,250,000 ikiwa ni mchango kutatua baadhi ya changamoto za elimu zilizobainika kwenye kilele cha maadhimisho ya Juma la Elimu Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.

Akizungumza katika hafla ya kilele cha maadhimisho ya Juma la Elimu Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Bw. Simon Nanyaro alisema fedha hiyo imetoa kusaidia kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwenye baadhi ya shule zenyechangamoto.

Akifafanua zaidi, Bw. Nanyaro alisema shilingi milioni 26,000,000/= zitatumika kukamilisha ujenzi wa boma la madarasa mawili na ofisi moja ya walimu katika Shule ya Msingi maalum ya Ndalambo pamoja na kugharamia viti mwendo vitatu kwa wanafunzi wenye ulemavu shuleni hapo vyenye thamani ya shilini million 2,250,000/=.

Alisema shilingi milioni 5,000,000/= zitatumika kugharamia utengenezaji madawati 60 kwa Shule ya Msingi Msia, huku shilingi milioni 20,000,000/= itumike kukamilisha ujenzi wa darasa moja kwenye shule ya Msingi Chiwanda.

“…TEN/MET tunapenda kupongeza jitihada za Serikali katika kutoa fursa ya elimu kwa wote, kwa mfano Mpango wa Elimu Changamani (IPOSA) ambayo kwa mkoa huu ina jumla ya washiriki 1,256. Lakini pia MEMKWA yenye jumla ya washiriki 2,922 na jambo zuri zaidi ni Elimu Masafa ambayo kwa mkoa huu tumetaarifiwa kuwa ina jumla ya washiriki 23,” alisema Mwenyekiti huyo wa Bodi ya TEN/MET.

Aidha alisema miongoni mwa changamoto walizozibaini kipindi chote cha maadhimisho ni pamoja na wanafunzi kutembea Umbali Mrefu kufika shuleni, upungufu wa miundombinu ya kujifunzia kama madarasa, matundu ya vyoo, maabara, maktaba na vifaa vya amali. Ukosefu wa Karakana kwa shule ya sekondari Msangano inayotoa masomo ya Amali, kutokuwepo kwa vifaa wezeshi vya kujifunzia kwa vitendo kwa fani ya afya ya Wanyama (animal health production) - shule ya sekondari ya amali Msangano na uhaba wa madawati kwa baadhi ya shule za msingi na sekondari.

Kwa upande wake Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akizungumza wakati akifunga rasmi Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, ameupongeza Mtandao wa Elimu Tanzania kwa kuratibu kwa mafanikio makubwa maadhimisho hayo, pamoja na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.

“GAWE 2026 imekuja katika wakati muhimu sana ambapo sekta ya elimu inahitaji mjadala wa kina kuhusu uendelevu wa ufadhili wa elimu. Katika miaka ya hivi karibuni, dunia imeshuhudia kupungua kwa misaada ya maendeleo katika sekta ya elimu, hali ambayo inaathiri uwezo wa nchi nyingi kuendelea kuboresha ubora, usawa, na ujumuishaji katika elimu,” alisisitiza Dkt. Simbeye.

Pamoja na hayo, Dkt. Simbeye ametoa wito kwa wadau wote wa elimu kuhakikisha wanaimarisha usimamizi na uwajibikaji wa wazazi na jamii kushiriki kikamilifu katika elimu ya watoto kwa kuhakikisha wanawaandikisha na kuwasimamia kukamilisha mzunguko wao wa masomo, huku akiitaka Sekta binafsi kuwekeza zaidi katika elimu, na asasi za kiraia kuendelea kuhamasisha mabadiliko ya kijamii.

Kauli mbiu ya GAWE 2026 inahimiza “Ugemaji Rasilimali za Ndani kwa Elimu Jumuishi, Bora na yenye Kuzingatia Mahitaji Maalum”. Yaani “Domestic Resource Mobilization for Equitable, Quality and Inclusive Education” ambayo imekuwa mwongozo muhimu wa mjadala na hatua katika maadhimisho haya.
Matukio anuai kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika kwenye Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Ephreim Simbeye akitembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa elimu kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.
Matukio anuai kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2026, yaliofanyika kwenye Halmashauri ya Momba, Mkoa wa Songwe.

Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akikata Keki iliyoandaliwa na Wafanyakazi wa Ubalozi huo wakati alipowasili katika Ofisi ya Ubalozi mara baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.



Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akikabidhiwa Ua kwa ajili ya upendo wakati alipowasili katika Ofisi ya Ubalozi mara baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akiwa katika picha ya pamoja baada ya baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

 
Na Mwandishi Wetu

Balozi Sita zinazowakilisha nchi zao nchini Tanzania zimeshiriki Tamasha la Piano ya muziki wa Franco Rhumba kwa ajili kupata furaha.

Akizingumza wakati kufungua Tamasha hilo lilofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo nchini Tanzania Jean Pierre Massala amesema kuwa Muziki huo unakuwatanisha kupata furaha pamoja na kujenga umoja .

Amesema kuwa kuwa waandaji wameweza kuona umuhimu kukaa pamoja na kupata furaha kupitia muziki huo ambao unapendwa na Wakongo na Jamii zingine.

Massala amesema kuwa matamasha hayo hayo ni muhimu kwani yanakutanisha watu tofauti ambao wanafanya kujenga umoja wenye furaha.

Kwa upande wa Balozi wa Morocco nchini Tanzania Zakaria El Goumiri. amesema kuwa wameshiriki Tamasha hilo kufurahi na kutaka waandaji waendelee kuandaa kwani linawaweka pamoja

Aidha amesema kuwa furaha za muziki za muziki zinaunganisha makundi mbalimbali kwa kuleta upendo

Mmoja wa waandaji Tamasha hilo Alain Izai amesema kuwa wanashukuru mwitikio walioupata katika Tamasha kwa kuungwa na Balozi Sita Kushiriki mwanzo hadi mwisho.

Izai amesema kuwa wataendelea kuandaa matamasha hayo mara kwa mara katika kutoa burdani kujenga furaha katika nyoyo zao.

Hata hivyo amesema Muziki wa Rhumba unapendwa na kila rika ambapo kazi yao ni kuendelea kutunga katika kuboresha nyimbo za muziki huo.

Mwandishi Wetu, DODOMA, Aprili 26, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametumia mamlaka yake ya kikatiba kutoa msamaha wa kupunguza adhabu kwa wafungwa 1,369 nchini, ambapo wafungwa 436 wameachiwa huru mara moja huku wengine 933 wakipunguziwa vifungo vyao.

Uamuzi huo umetangazwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobass Katambi, ambaye amesema hatua hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Katambi amesema msamaha huo umetolewa kwa mujibu wa Ibara ya 45(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayompa Rais mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa wanaostahili.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, walionufaika na msamaha huo ni pamoja na wafungwa waliotumikia sehemu ya vifungo vyao kwa mujibu wa sheria, wagonjwa mahututi waliothibitishwa kitaalamu, wazee wenye umri wa miaka 70 na zaidi, pamoja na wanawake wajawazito au wenye watoto wachanga waliopo magerezani.

Aidha, wafungwa waliokuwa wakitumikia adhabu ndefu, wakiwemo waliokaa gerezani kwa miaka 25 na zaidi pamoja na waliokuwa chini ya kizuizi kwa muda mrefu, nao wamejumuishwa baada ya kufanyiwa tathmini maalum.

Hata hivyo, Serikali imeeleza kuwa msamaha huo haukuwahusu wafungwa waliopatikana na hatia ya makosa mazito ikiwemo ugaidi, uharamia, ubakaji, biashara ya binadamu, rushwa, uhujumu uchumi, pamoja na wanaotumikia kifungo cha maisha.

Pia wafungwa waliowahi kunufaika na msamaha wa Rais hapo awali hawakujumuishwa katika orodha ya walionufaika safari hii.

Serikali imesema hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya pili kwa wafungwa waliorekebika ili warejee katika jamii na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya taifa.

“Ni matarajio ya Serikali kuwa wale walioachiwa huru watarejea katika jamii wakiwa na nidhamu, wakijihusisha na shughuli halali za kiuchumi na kuepuka kurejea kwenye vitendo vya uhalifu,” ilieleza taarifa hiyo.

Hatua hiyo imepokelewa na wananchi kama ishara ya huruma na dhamira ya Serikali ya kuendelea kuimarisha haki, utu na mageuzi ya mfumo wa marekebisho ya tabia nchini.

Wachambuzi wa masuala ya kijamii wanasema msamaha huo pia utasaidia kupunguza msongamano magerezani na kuongeza ufanisi wa huduma za marekebisho.

Maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano yanaendelea kuambatana na hatua mbalimbali za kijamii na kiuchumi zinazolenga kuimarisha mshikamano wa kitaifa na ustawi wa wananchi
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda, amezindua mradi wa basi dogo wa kikundi cha vijana cha UNAMA, kinachotoa huduma ya usafirishaji wa abiria katika kijiji cha Picha ya Ndege, kata ya Vikindu wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Aprili 24, 2026, Mwang’onda amewapongeza vijana hao kurejesha fedha za mkopo na kuaminiwa kuongezewa fedha kiasi cha milioni 85.2, kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. 


Aidha amewahimiza vijana kote nchini kutumia kikamilifu fursa ya mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri, akieleza kuwa ni nyenzo muhimu ya kujikwamua kiuchumi na kujenga ajira binafsi.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega, ameeleza utekelezaji wa mikopo hiyo unatoa fursa halisi kwa vijana kujiajiri kupitia miradi yenye tija.

“Tunampongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo ya utoaji wa mikopo kupitia halmashauri, pamoja na kusisitiza ukusanyaji wa mapato ya ndani unaowezesha kutengwa kwa asilimia 10 kwa ajili ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu,” amesema Ulega.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nasir, amesema jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi milioni 39.5 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2026, baada ya kupokelewa kutoka Wilaya ya Kisarawe.

Kati ya Miradi hiyo ni usambazaji wa nishati safi ya kupikia, kiwanda cha vinywaji baridi cha Yaket International, ujenzi wa uzio wa Shule ya Sekondari Mwinyi, ujenzi wa boksi kalavati, pamoja na mradi wa maji katika kijiji cha Sotele.

Mwenge wa Uhuru umefikisha siku ya saba mkoani Pwani tangu ulipopokelewa Aprili 18, 2026, na unatarajiwa kuendelea na mbio zake Aprili 25, 2026 katika Wilaya ya Kibiti.

Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameihimiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kuendelea kuimarisha ushirikiano wake na viwanda ili kuongeza fursa za ajira na ujuzi kwa vijana nchini.

Wito huo umetolewa Aprili 23, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya ufundi wa aluminium na ufungaji wa vioo kwa wakufunzi pamoja na mafundi wa fani ya useremala.

Tukio hilo pia limeambatana na uzinduzi wa mtaala mpya wa mafunzo hayo unaoendeshwa na kampuni ya Emirates Aluminium Profile kwa kushirikiana na VETA, ukiwa na lengo la kuzalisha wataalamu wenye ujuzi unaohitajika katika soko la ajira.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Wanu alisema hatua hiyo inaendana na maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha rasilimali watu sambamba na kasi ya mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia duniani.

“Ushirikiano kati ya vyuo vya VETA, sekta ya uzalishaji, waajiri na viwanda ni muhimu ili kuhakikisha wahitimu wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji halisi ya soko la ajira,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alisema mafunzo kwa wakufunzi ni hatua muhimu katika kuboresha ubora wa ufundishaji na kuongeza ushindani wa wahitimu katika soko la ajira.

Kasore alisema awamu ya kwanza ya mafunzo hayo imehusisha wakufunzi 18 wa fani ya useremala watakaopatiwa ujuzi wa vitendo unaohitajika viwandani.

Alifafanua kuwa washiriki hao watajengewa uwezo katika maeneo mbalimbali ikiwemo makadirio ya vifaa na gharama, uundaji wa miundo ya aluminium, ufungaji wa vioo, utengenezaji wa samani za chuma pamoja na ufungaji wa dari.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Emirates Aluminium Profile, Deogratius Marandu, alisema mafunzo hayo yataongeza thamani kwa mafundi na kuwapa utambuzi unaohitajika katika soko la ajira.

Marandu aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuwawezesha vijana kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Wadau wa elimu wameeleza kuwa ushirikiano kati ya VETA na sekta binafsi ni njia sahihi ya kuzalisha vijana wenye ujuzi wa kisasa unaoendana na mahitaji ya soko la ajira nchini

 

Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Dodoma

WAKAZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameendelea kupata huduma bora za afya katika Hospitali ya Jiji huku Bohari ya Dawa(MSD)ikiwezesha utolewaji wa huduma hizo kupitia vifaa tiba vya kisasa na dawa zote muhimu ilivyopeleka hospitalini hapo.
Kuanza kwa huduma kwa Hospitali hiyo imewezesha wakazi  wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapato 765,179 wakiwemo wanaume 373,440 na wanawake 391,739 kufurahia matunda ya hitaji ya sera ya mwaka 2009 ya kusogeza huduma karibu na wananchi ,hivyo kupitia fedha za halmashauri  na Serikali kuu ujenzi ulianza na sasa wananchi wanapata huduma za matibabu kwa raha mustarehe.

Kupitia ziara iliyoandaliwa na MSD kwa wahariri na waandishi wa habari Mganga Mfawindhi wa Hospitali ya Dodoma Dk.Joshua Mwalongo amesema hadi sasa jumla ya fedha ambazo zimepelekwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ni Sh.bilioni 2.8.

Kwa mujibu wa Dk.Mwalongo hospitali hiyo imekuwa na manufaa makubwa hasa ya kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi na tangu ilipoanza kutoa huduma Januari 20,2025 wananchi wameendelea kuongezeka siku hadi siku huku akisisitiza MSD imewezesha vifaa tiba vya kisasa kwa ajili ya matibabu mbalimbali.

Akifafanua kuhusu mradi huo amesema ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ulitokana na uhitaji wa wanachi kupata huduma za ngazi ya hospitali ya wilaya na hiyo ni kutokana na changamoto ya kukosa Hospitali ya Wilaya kwa muda mrefu.
“Pia ujenzi ulitokana na hitaji la sera ya Afya ya mwaka 2009 la kusogeza huduma karibu na wananchi hivyo kupitia fedha za Halmashauri na Serikali kuu, ujenzi wa hospitali hii ya Wilaya ulianza rasmi mnamo mwaka 2023,”amesema na kuongeza shilingi 100,000,000.00 zimetumika kununua vifaa tiba kutoka Bohari ya Dawa MSD.

Akieleza zaidi amesema hospitali hiyo hadi sasa ina majengo 10 ya kutolea huduma , na kuomgeza kwa mwezi wanahudumia wagonjwa 700

Katika kutambua mchango wa Serikali katika ujenzi wa hospitali hiyo Dk.Mwalongo amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa hospitali hiyo ambayo imepunguza msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na Hospitali ya Makole.

“Wananchi hawaendi huko wanakuja katika hospitali ya Wilaya na kwa kweli tunaishukuru MSD kwa kutuwezesha vifaa tiba vya kisasa pamoja na dawa zote muhimu ambazo tunazipata kwa wakati.Upatikanaji dawa kwetu ni zaidi ya asilimia 93.”

Awali Meneja MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema uwepo wa hospitali hiyo sambamba na na vifaa tiba vinavyosambazwa MSD itasaidia kutoka huduma za uhakika na kupunguza msomgamano katika hospitali nyingine huku akiwahakikishia watanzania MSD itaendelea kupeleka Dawa na vifaa tiba vya kisasa kwa wakati.

Pamoja na hayo jambo la kufurahisha zaidi hospitali hiyo kuanza kutoa huduma za matibabu kwa magonjwa mbalimbali pia imefungua fursa ya ajira kwa vijana wa kitanzania kwani idadi kubwa ya watoa huduma katika hospitali hiyo ni vijana zaidi ambao hivi sasa wanaenjoi kutoa huduma kwa vifaa tiba vya kisasa.Madaktari wanabofya tu.