Dar es Salaam, Tanzania – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameipatia Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) Tuzo ya Rais ya Walipakodi Bora katika Sekta ya Uzalishaji (Manufacturing), ikiwa ni kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia ulipaji sahihi wa kodi, uzalishaji wa ndani, uwekezaji na uundaji wa ajira.
Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Mlimani City, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 1 Julai 2026.
Uamuzi wa Mheshimiwa Rais kuongoza binafsi utoaji wa tuzo hizo kwa mwaka wa pili mfululizo unaonesha umuhimu ambao Serikali inaweka katika kuhimiza ulipaji wa kodi na kutambua mchango wa sekta binafsi katika kufanikisha maendeleo ya nchi.
Kwa TBL, tuzo hii ni uthibitisho wa mchango mpana wa kampuni katika maendeleo ya Tanzania. Mbali na kulipa kodi kwa wakati na kwa usahihi, kampuni inaendelea kuchangia maendeleo kupitia ajira inazozalisha, ushirikiano wake na wakulima, wasambazaji, wafanyabiashara pamoja na jamii mbalimbali zinazozunguka shughuli zake.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Breweries Public Limited Company, Michelle Kilpin, alisema kuwa tuzo hiyo ni ishara ya dhamira ya kampuni ya kuendesha biashara kwa uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya Taifa.
"Tunajivunia kupokea heshima hii kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kulipa kodi kikamilifu na kwa wakati ni wajibu wetu kama kampuni ya Kitanzania na sehemu ya mchango wetu katika maendeleo ya nchi. Tuzo hii ni ya wafanyakazi wetu, wakulima, wasambazaji, wauzaji, washirika wetu wa biashara na wadau wote katika mnyororo wetu wa thamani. Tutaendelea kuwekeza nchini na kuwa mshirika wa kuaminika katika safari ya maendeleo ya Tanzania," alisema Kilpin.
Kupitia shughuli zake za uzalishaji wa ndani, TBL inaendelea kuzalisha manufaa yanayovuka mipaka ya viwanda vyake kwa kusaidia wakulima, wasafirishaji, wasambazaji, wafanyabiashara wadogo na wa kati pamoja na wadau wengine wa biashara nchini. Aidha, kupitia ununuzi wa mazao ya ndani kama shayiri (barley) na mtama (sorghum), kampuni inachochea maendeleo ya sekta ya kilimo, kuongeza kipato cha wakulima na kuhakikisha thamani kubwa zaidi ya uchumi inabaki nchini.
Mbali na mchango wake wa kiuchumi, TBL inaendelea kuwekeza katika miradi ya uendelevu ikiwemo usimamizi wa rasilimali za maji, kuwawezesha wakulima, ununuzi wenye uwajibikaji, matumizi ya mifumo ya ufungashaji unaorejelezwa pamoja na programu za urejelezaji wa taka, hatua zinazolenga kuhifadhi mazingira na kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali zinazoiwezesha kampuni kuendesha shughuli zake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Kampuni wa TBL, Neema Temba, alisema kuwa biashara yenye uwajibikaji hupimwa kwa kuzingatia utekelezaji wa sheria pamoja na athari chanya inayozalisha kwa jamii.
"Heshima hii inaakisi msingi wa maadili unaotuongoza kila siku. Tunaamini katika kufanya biashara kwa uwazi, kutimiza wajibu wetu wa kisheria na kushirikiana na Taifa ambalo limekuwa makazi ya biashara yetu kwa miongo mingi. Kampuni zinapolipa kodi stahiki, kuwekeza katika maeneo zinayofanyia kazi na kulinda rasilimali zinazowezesha shughuli zao, nchi nzima hunufaika na kusonga mbele," alisema Temba.
Tuzo hii inaongeza orodha ya mafanikio ambayo TBL imeendelea kuyapata katika maeneo ya ulipaji wa kodi, uendelevu wa biashara na uwajibikaji wa kampuni kwa jamii.
Kadiri Tanzania inavyoendelea kutekeleza agenda ya ukuaji wa viwanda na mageuzi ya uchumi, TBL imesisitiza kuwa itaendelea kuwekeza nchini, kushirikiana na jamii pamoja na kuunda thamani ya kudumu kupitia biashara inayozingatia uwajibikaji.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), wakifurahia ushindi baada ya kampuni yao kutunukiwa tuzo mbili: Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi Julai 3, 2026, na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye kabla ya hafla ya ufunguzi aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutembelea banda la Vodacom na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.


Fatma alisema katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kampuni imechangia zaidi ya shilingi trilioni 1.4 kupitia kodi na tozo mbalimbali kwa Serikali, hatua iliyoifanya kutambuliwa mara kadhaa na TRA kwa utii wa sheria za kodi na mchango wake mkubwa katika kuongeza mapato ya ndani. Aliongeza kuwa kampuni itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya nishati na kupanua huduma zake ili kuchochea maendeleo ya sekta mbalimbali za uzalishaji.Mbali na ulipaji wa kodi, Puma Energy Tanzania imeendelea kuimarisha uwekezaji wake kwa kuendesha zaidi ya vituo 100 vya huduma za mafuta, maghala ya kuhifadhi mafuta na usambazaji wa mafuta ya ndege katika viwanja vinane vya ndege, ikiwemo viwanja vyote vya kimataifa nchini. Kampuni pia inaongoza matumizi ya nishati safi kupitia Kituo Kikuu cha Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG Mother Station) pamoja na mtandao unaokua wa vituo vya CNG jijini Dar es Salaam na Morogoro.
Aidha, kampuni inaendelea kupanua huduma za gesi ya kupikia kupitia Puma Gas, biashara ya vilainishi na maduka ya Shop Express, huku ikiendelea kuchangia ukuaji wa uchumi kupitia uwekezaji, ajira na huduma za nishati zenye ubora. Tuzo hiyo imeongeza hadhi ya Puma Energy Tanzania kama mmoja wa walipa kodi wakubwa na washirika muhimu wa Serikali katika kufanikisha ajenda ya maendeleo ya Taifa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.


Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.



Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.
"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.
Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.



Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.
Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.








































.jpg)



