TRENDING NOW






Tanzania Bloggers Network (TBN) Chairman Beda Msimbe (left) meets with the Journalism Accreditation Board’s Acting Director General, Advocate Patrick Kipangula, during their meeting at the Board’s offices in Dar es Salaam on 16 July 2026. The meeting followed TBN’s formal request for professional training for more than 200 bloggers on media law, journalistic ethics and the importance of accreditation.

By TBN Staff Writer

The Journalists’ Accreditation Board (JAB) has received a formal request from the Tanzania Bloggers Network (TBN) seeking training for its more than 200 members on the Media Services Act, journalism ethics, and the importance of obtaining professional accreditation.

The request was submitted on 16 July 2026, when TBN Chairman Beda Msimbe met with JAB’s Acting Director General, Advocate Patrick Kipangula, during discussions held at the Board’s offices in Dar es Salaam.

Speaking after the meeting, Advocate Kipangula said the Board had received the request and was ready to work with the network to help bloggers gain a deeper understanding of the Media Services Act, professional ethics, and the value of accreditation.

He said the training would begin with bloggers who are already accredited, aimed at strengthening their professionalism and understanding of their professional responsibilities, before extending to those who have not yet obtained accreditation.

“Those without accreditation will get the opportunity to be guided on the legal requirements for obtaining it, including the necessary qualifications required under the Media Services Act. Those who do not yet meet the required qualifications will be advised to pursue further education so they can meet the criteria for accreditation,” Advocate Kipangula said.

For his part, TBN Chairman Beda Msimbe said the training would help the network’s members carry out their duties in line with the law, ethics, and professionalism, while also contributing effectively to informing the public and promoting Tanzania through coverage of development initiatives being implemented across various sectors.

He added that the collaboration between the network and JAB would help build the capacity of bloggers and strengthen their contribution to the country’s media sector.

Background

The request marks a notable step in efforts to bring Tanzania’s growing community of digital content creators and bloggers into closer alignment with the formal regulatory framework governing media practice in the country.

The Media Services Act has, since its introduction, set out qualification requirements and ethical standards that traditional journalists are expected to meet, and the extension of similar guidance to bloggers reflects the increasing recognition of digital platforms as a significant source of public information.

TBN’s more than 200 members represent a wide cross-section of Tanzania’s online content creators, many of whom operate blogs, social media pages, and other digital platforms that reach large audiences, particularly among younger Tanzanians who increasingly turn to online sources for news and updates.

By prioritising already-accredited bloggers in the first phase of training, JAB appears to be taking a phased approach that rewards those who have already engaged with the formal accreditation process, while creating a clear pathway for others to follow.

The emphasis on further education for those who do not yet meet the qualification criteria suggests the Board intends the programme to be developmental rather than punitive, encouraging capacity-building rather than simply excluding non-accredited bloggers from practice.

Observers of Tanzania’s media landscape note that partnerships of this kind between regulatory bodies and digital media associations could help address longstanding tensions between traditional journalism institutions and the newer wave of online content creators, many of whom have historically operated outside formal press structures.

No specific date has yet been announced for when the training sessions will begin, though both JAB and TBN indicated their intention to move forward with the collaboration.

Further details on the training schedule, curriculum, and criteria for accreditation are expected to be announced in due course as the two organizations finalize the arrangements for the programme.

Na Mwandishi Wetu, JAB

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imepokea ombi kutoka Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) la kutoa mafunzo kwa wanachama wake zaidi ya 200 kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, Maadili ya Uandishi wa Habari na umuhimu wa kupata ithibati.

Ombi hilo limetolewa leo, tarehe 16 Julai, 2026, na Mwenyekiti wa Mtandao wa Mabloga Tanzania, Bw. Beda Msimbe, alipokutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, katika mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Bodi jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya mazungumzo hayo, Wakili Kipangula amesema Bodi imepokea ombi hilo na iko tayari kushirikiana na Mtandao huo katika kuwawezesha bloga kupata uelewa wa kina kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma pamoja na umuhimu wa kupata ithibati.

Amesema mafunzo hayo yataanza kutolewa kwa bloggers wenye ithibati ili kuimarisha weledi na uelewa wao wa majukumu ya kitaaluma, kabla ya kuendelea kuwafikia wale ambao bado hawajapata ithibati.

"Wale ambao hawana ithibati watapata fursa ya kuelekezwa kuhusu masharti ya kisheria ya kupata ithibati, ikiwemo umuhimu wa kuwa na sifa zinazotakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari. Wasio na sifa stahiki watashauriwa kujiendeleza kielimu ili waweze kukidhi vigezo vya kupata ithibati," amesema Wakili Kipangula.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtandao wa Mabloga Tanzania, Bw. Beda Msimbe, amesema mafunzo hayo yatawasaidia wanachama wa chama hicho kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, maadili na weledi, sambamba na kuchangia kwa ufanisi katika kuhabarisha umma na kuitangaza Tanzania kupitia taarifa za maendeleo zinazotekelezwa katika sekta mbalimbali.

Amesema ushirikiano kati ya Mtandao huo na JAB utasaidia kujenga uwezo wa bloggers na kuimarisha mchango wao katika sekta ya habari nchini.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza udhamini wa Mashindano ya Golf ya Vodacom Corporate Masters 2026, yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na Lugalo Golf Club kwa lengo la kuunganisha jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania, kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kukuza ushirikiano na kuleta fursa zenye tija kwa wateja, washirika wa kibiashara na wadau muhimu nchini. Mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 1 Agosti 2026 yanaendelea kuimarisha nafasi ya Vodacom kama mshirika wa kuaminika katika teknolojia na huduma za mawasiliano kwa taasisi na mashirika yanayoendelea kukua katika mazingira ya uchumi wa kidijitali. Uzinduzi huo umefanyika tarehe 16 Julai 2026 jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Katibu wa Corporate Masters, Maryanne Mugo (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Mbaya (kulia).

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yatakayofanyika katika Uwanja wa Gofu wa Lugalo kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kufungua fursa mpya kwa wateja, washirika na wadau wa sekta mbalimbali.

Mashindano hayo, yanayoandaliwa kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited kupitia kitengo cha Vodacom Business, yatawakutanisha viongozi wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu wa sekta mbalimbali na wapenzi wa mchezo wa gofu kwa lengo la kujenga mitandao ya biashara na kubadilishana uzoefu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania PLC, Joseph Sayi, alisema kampuni hiyo imeendelea kudhamini mashindano hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo kwa kuwa yanaendana na dhamira ya kuimarisha mahusiano ya muda mrefu na jumuiya ya wafanyabiashara.

Alisema mashindano hayo si ya michezo pekee, bali ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujadili fursa mpya za uwekezaji na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.

Sayi alisema katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho mbalimbali za kidijitali ikiwemo huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi, kukuza biashara na kuimarisha ushindani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Corporate Masters, Ken Kariuki, alisema mashindano hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la makampuni kujitangaza, kujenga mitandao ya kibiashara na kuzalisha fursa mpya za biashara huku yakiimarisha ushiriki wa wateja.

Mashindano hayo yatashirikisha timu 10 za makampuni zitakazowania taji la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na maonesho ya biashara, burudani, maonesho ya vitu vya kale na eneo maalumu la watoto, hatua inayolenga kuwafanya washiriki na familia zao kufurahia tukio hilo katika mazingira rafiki.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji, Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (kulia) na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (kushoto), wakiwa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.
Meneja Masoko wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Caleb Majo (kushoto), akitoa elimu kuhusu huduma zinazotolewa na Vodacom Tanzania wakati wa mahojiano maalumu na Azam Media katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini. Wengine ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Alex Bitekeye (wa pili kushoto), Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (wa pili kulia), na Mtangazaji wa Azam Media, Jafar Mponda (kulia).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi (aliyekaa katikati), Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga (aliyekaa kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE, Latifa Khamis (aliyekaa kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa kampuni mbalimbali, akiwemo Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (aliyevaa tisheti nyekundu), muda mfupi baada ya kufungwa kwa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (SABASABA). Vodacom Tanzania Plc ilitambuliwa kama mshirika muhimu wa maonesho hayo baada ya kupewa tuzo mbili; Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kufanikisha maonesho hayo.
Mkuu wa idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (wa sita kulia), na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (wa sita kushoto) wakiwa katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wengine wa Vodacom wakiwa wa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA) muda mfupi baada ya kufungwa rasmi kwa maonesho hayo. Kwa siku zote 13 za maonesho hayo Vodacom Tanzania ilishiriki fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.

Na Mwandishi Wetu.

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amesema Serikali yake inaendelea kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya taifa kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta mbalimbali zinazolenga kuongeza ajira, kukuza vipaji na kuimarisha uchumi.

Ruto amesema Serikali imewekeza katika michezo, uchumi wa ubunifu na kidijitali, ajira za nje ya nchi, uwezeshaji wa biashara, makazi nafuu pamoja na maendeleo ya miundombinu, hatua ambazo zimeanza kuzaa matunda kwa kuunda mamilioni ya nafasi za ajira na fursa nyingine kwa vijana.
Amesema katika sekta ya michezo pekee, Serikali inaendelea kujenga na kuboresha viwanja 34 vya michezo nchini ili kusaidia kukuza vipaji vya vijana na kuongeza fursa za maendeleo kupitia michezo.

Kwa mujibu wa Rais huyo, uwekezaji huo umeanza kuleta mafanikio, huku wanamichezo wa Kenya wakiendelea kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa. Pia aliipongeza timu ya taifa ya wasichana wenye umri chini ya miaka 17, Junior Harambee Starlets, kwa kuweka historia ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la FIFA kwa wanawake chini ya miaka 17.
Ruto aliyasema hayo baada ya kuikaribisha Ikulu ya Nairobi timu ya Migori Youth FC, mabingwa wa National Super League msimu wa 2025/26, ambapo aliikabidhi basi maalumu litakalowasaidia kusafiri kwa urahisi katika mechi za ligi nchini kote.

Aidha, alisema Serikali inaendelea kujenga uwanja wa kisasa katika Kaunti ya Migori utakaotumiwa na Migori Youth FC pamoja na jamii kwa ujumla, kwa lengo la kuimarisha mazingira ya kukuza vipaji vya michezo na maendeleo ya vijana nchini Kenya.

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Kampuni ya Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya jamii na uchumi wa ndani kupitia kampeni yake ya Cheers to Bars, inayotambua mchango mkubwa wa baa katika kuwaleta watu pamoja, kukuza biashara ndogo ndogo na kuimarisha shughuli za kiuchumi nchini.

TBL imesema kuwa baa zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya Watanzania, zikitoa nafasi kwa marafiki na majirani kukutana, mashabiki wa soka kushuhudia mechi pamoja na wafanyabiashara wadogo kuendesha shughuli zao. Kampeni hiyo inalenga kuzisherehekea baa kwa mchango wake katika kujenga mshikamano wa kijamii na kuchochea maendeleo ya uchumi.

Mbali na kuwa sehemu za burudani, TBL imeeleza kuwa baa zimeendelea kutoa ajira kwa maelfu ya Watanzania, wakiwemo wamiliki wa baa, wahudumu, wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, walinzi, wasafishaji pamoja na watoa huduma za usafiri, hali inayochangia kuongeza kipato kwa watu wengi na kuimarisha mzunguko wa fedha katika jamii.

Kampeni ya Cheers to Bars pia imeangazia nafasi ya baa wakati wa matukio makubwa ya michezo, hususan soka, ambapo mashabiki wengi hupendelea kutazama mechi kwa pamoja katika mazingira yanayowapa fursa ya kushirikiana, kushangilia na kujenga kumbukumbu za pamoja.

Hali hiyo ilijidhihirisha katika Baa ya Kitambaa Cheupe jijini Dar es Salaam, ambapo mashabiki walikusanyika kushuhudia mechi ya robo fainali kati ya Hispania na Ubelgiji. Mechi hiyo iligeuka kuwa zaidi ya mchezo wa soka, huku ikiunganisha watu wa kada mbalimbali walioshiriki kushangilia na kufurahia burudani kwa pamoja.
Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Ushirika wa TBL, Neema Temba, alisema Cheers to Bars si kampeni inayolenga soka pekee, bali ni jukwaa la kutambua mchango wa baa na watu wanaoziendesha katika maendeleo ya jamii na uchumi wa Tanzania.

"Baa ni sehemu muhimu ya maisha ya kijamii na kiuchumi ya Watanzania. Zinasaidia kujenga maisha ya watu, zinatoa fursa kwa biashara ndogo ndogo na zinatoa nafasi kwa jamii kukutana na kuimarisha mahusiano. Kupitia Cheers to Bars, tunazisherehekea baa hizi pamoja na watu wanaoziendesha, huku tukiwahamasisha watumiaji kufurahia vinywaji kwa kuwajibika," alisema Neema.
Aliongeza kuwa wakati wa mechi kubwa za soka, shughuli za biashara huongezeka kwa kiasi kikubwa katika baa na maeneo yanayozizunguka. Wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, madereva wa usafiri na watoa huduma wengine wote hunufaika kutokana na ongezeko la wateja, jambo linaloifanya sekta ya ukarimu kuwa kichocheo muhimu cha uchumi wa ndani.

Kwa mujibu wa TBL, mafanikio ya kampeni hiyo yanaonesha kuwa baa za kienyeji zimeendelea kuwa sehemu muhimu zinazochangia maendeleo ya jamii kwa kuunganisha watu kupitia michezo na burudani, huku zikitoa fursa za ajira na biashara kwa makundi mbalimbali.

Kampuni hiyo imewataka Watanzania kuendelea kuunga mkono baa za kienyeji na kushiriki burudani katika mazingira salama kwa kutumia vinywaji kwa uwajibikaji. TBL imeeleza kuwa itaendelea kutekeleza kampeni ya Cheers to Bars kama sehemu ya juhudi zake za kuthamini mchango wa baa katika ukuaji wa uchumi, maendeleo ya jamii na ustawi wa sekta ya ukarimu nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi, Mawakili, wageni mbalimbali, kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Viongozi, wageni mbalimbali wakiwa kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya nakala ya Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia (Mama Samia Doctrine of Law); kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Hamza Johari kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026. Kitabu hicho kinaelezea historia, falsafa na mafanikio ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia.
Picha namba 04. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Serikali Bw. Bavoo Anatoly Junus kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Serikali Bw. Bavoo Anatoly Junus kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Mabanda ya maonesho ya masuala mbalimbali ya Sheria kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha, tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) kwa ajili ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) Jijini Arusha, tarehe 13 Julai, 2026.