TRENDING NOW








Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu wa Tatu wa Uganda Mhe. Rukia Isaya Nakadama mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe nchini humo tarehe 12 Mei, 2026. Rais Dkt. Samia amewasili nchini Uganda kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule nchi hiyo, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, zitakazofanyika katika Viwanja vya Kololo Jijini Kampala nchini humo.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Uganda kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni tarehe 12 Mei, 2026.








Dar es Salaam, Tanzania — Women leaders, professionals and changemakers have been urged to embrace continuous learning and digital skills development in order to remain competitive in today’s rapidly evolving workplace shaped by artificial intelligence (AI) and digital transformation.

The call was made during this year’s Mother’s Day Dinner organized by Hold a Sister’s Hand, which brought together influential women from different sectors for high-level discussions under the theme “Reskilling While Caregiving.” The event focused on empowering mothers and caregivers to balance family responsibilities while adapting to the changing demands of the modern workforce.
Speakers at the event emphasized that the rise of AI and digital technologies is transforming industries globally, creating both opportunities and challenges for women. They noted that many working mothers risk being left behind if they fail to upgrade their skills and embrace innovation-driven careers.

The discussions explored critical issues affecting women in the digital era, including bridging the digital gender gap in AI adoption, ethical leadership, responsible use of technology, and addressing bias in AI-driven recruitment and promotions. Participants also highlighted the importance of adaptability, lifelong learning, and mentorship in helping women remain relevant in highly competitive environments.
Organizers of the event said the initiative aimed to create a safe and inspiring platform where women could openly discuss challenges facing mothers and caregivers in workplaces increasingly influenced by automation and digital systems. They stressed that caregiving responsibilities should not prevent women from pursuing professional growth and leadership opportunities.

Interactive live discussions allowed attendees to share personal experiences on balancing career growth with parenting and caregiving duties. Many participants called for stronger workplace policies that support women through flexible work arrangements, digital training opportunities, and inclusive leadership programs.

The event concluded with a renewed call for governments, private sector institutions, and development partners to invest more in women’s digital empowerment and skills development to ensure they fully participate in shaping the future economy. Participants agreed that empowering women with technology and leadership skills is essential for sustainable social and economic development in Africa’s digital age.


























Nchi waandaji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027) ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda zimesaini hati ya makubaliano ya pamoja inayojulikana kama CAF Joint Resolution – TotalEnergies AFCON PAMOJA 2027, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika maandalizi ya mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Utiaji saini wa makubaliano hayo umefanyika Mei 11, 2026 na kushuhudiwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Patrice Motsepe, ambaye amepongeza hatua hiyo kuwa muhimu katika kuhakikisha maandalizi yanaenda kwa ufanisi na mshikamano miongoni mwa nchi hizo tatu.

 Tanzania iliwakilishwa katika hafla hiyo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda pamoja na viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakiongozwa na Rais wa TFF, Wallace Karia.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kusaidia uratibu wa maandalizi ya miundombinu, usafiri, usalama na masuala mengine muhimu kuelekea AFCON 2027, huku yakionesha dhamira ya Tanzania, Kenya na Uganda kushirikiana kwa karibu kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa kwa viwango vya kimataifa.

Rais wa Kenya, William Ruto, amempokea Rais wa Sierra Leone, Julius Maada Bio, katika Ikulu ya Nairobi kwa ziara rasmi inayohusiana na Mkutano wa Africa Forward unaotarajiwa kuanza leo Jumatatu Mei 11, 2026 nchini humo.

Akizungumza baada ya mazungumzo yao, Rais Ruto alisema Kenya na Sierra Leone zinaendelea kudumisha uhusiano wa karibu unaojengwa katika misingi ya kuheshimiana, umoja wa Afrika na kudumisha utulivu wa kikanda. Alieleza kuwa mataifa hayo mawili yataendelea kushirikiana katika kusukuma mbele ajenda za maendeleo ya bara la Afrika.

Ruto alisema nchi hizo pia zinashirikiana katika kuhimiza mageuzi ya mfumo wa fedha wa kimataifa, maboresho ya utawala wa dunia hususan katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, pamoja na masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Alibainisha kuwa mkutano wa Africa Forward utatoa jukwaa muhimu kwa viongozi wa Afrika kubadilishana mawazo kuhusu changamoto na fursa zinazolikabili bara hilo katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa duniani.

Katika mazungumzo hayo, Rais Ruto pia alimweleza Rais Bio kuhusu azma ya Kenya kugombea nafasi ya jaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), ambapo alimwomba kuunga mkono mgombea wa Kenya, Jaji wa Mahakama ya Juu, Njoki Ndung'u.

Ziara hiyo ya Rais Bio nchini Kenya inaonekana kuimarisha zaidi ushirikiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili, huku viongozi hao wakisisitiza umuhimu wa mshikamano wa Afrika katika kutatua changamoto za bara hilo.

 Msimamizi Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay Kiptiness akiwakaribisha  viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini wanaoshiriki zoezi hilo Jijini Nairobi leo Mei 11, 2026. Zoezi hilo linalenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.
Na Aron Msigwa – Nairobi, Kenya

Msimamizi Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay Kiptiness amesisitiza umuhimu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuendelea kuimarisha umoja, ushirikiano na utayari wa pamoja katika kukabiliana na majanga, vitisho na changamoto mbalimbali za kiusalama zinazoweza kuhatarisha amani na utulivu wa kikanda.

Balozi Kiptiness amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati wa mapokezi ya washiriki wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” lililoanza rasmi Jijini Nairobi, Kenya. 

Zoezi hilo limewakutanisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kuna umuhimu mkubwa katika kuimarisha mfumo wa usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, akibainisha kuwa mabadiliko ya hali ya usalama duniani yanahitaji nchi wanachama kushirikiana kwa karibu zaidi katika kulinda amani, utulivu na ustawi wa wananchi wake.

Aidha, amesema migogoro na hali ya kutokuwa na utulivu katika maeneo mbalimbali duniani, hususani Mashariki ya Kati pamoja na maeneo mengine yenye migogoro, inaendelea kuathiri kwa namna mbalimbali uchumi, usalama na maisha ya wananchi wa nchi za EAC. Amesema hali hiyo inaonesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mshikamano wa kikanda, kubadilishana taarifa za kiusalama na kuwa na mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto hizo.

Balozi Kiptiness ameongeza kuwa Zoezi la “Ushirikiano Imara 2026” ni jukwaa muhimu linalowezesha taasisi za ulinzi na usalama za nchi wanachama kuongeza uwezo wa uratibu wa operesheni, kuimarisha mipango ya kimkakati na kujenga uaminifu miongoni mwa mataifa shiriki. Amesema hatua hiyo inaakisi dhamira ya pamoja ya nchi za EAC katika kuhakikisha ukanda huo unaendelea kuwa wa amani, usalama na utulivu.

Aidha, amesisitiza kuwa amani na usalama ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu, ushirikiano wa kikanda, biashara na ustawi wa kiuchumi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki akitoa wito kwa nchi wanachama kuendelea kuwekeza katika mipango ya pamoja ya kuzuia migogoro, kuimarisha utayari wa kukabiliana na majanga pamoja na kuboresha mifumo ya utoaji wa misaada ya kibinadamu katika ukanda huo.

Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” linatarajiwa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama wa EAC na kuendeleza dira ya pamoja ya kuwa na Afrika Mashariki yenye amani, usalama na ustahimilivu mkubwa dhidi ya changamoto mbalimbali

Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde (wa pili kutoka kushoto), ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, akikata utepe wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi wa tawi la Exim Bank Tanzania katika Mkoa wa Geita Region, akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba (wa tatu kutoka kushoto). Pia pichani ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Exim Bank Tanzania, Bw. Jaffari Matundu (wa kwanza kutoka kushoto), pamoja na viongozi wengine wa Serikali na Benki ya Exim katika tukio hilo lilofanyika mnamo tarehe 09 May 2026, Geita.

Na Mwandishi Wetu.

Benki ya Exim Tanzania imezindua rasmi tawi lake jipya mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupanua huduma za kifedha katika maeneo yenye shughuli kubwa za kiuchumi nchini. Tawi hilo linatarajiwa kuwahudumia wachimbaji wa madini, wakulima, wafanyabiashara wadogo na wa kati pamoja na wananchi wa kawaida.

Uzinduzi huo uliofanyika Mei 9, 2026, ulihudhuriwa na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, viongozi wa Serikali, wadau wa sekta ya madini pamoja na wafanyabiashara mbalimbali wa mkoa huo. Waziri Mavunde alisema uwepo wa taasisi za kifedha kama Exim Bank utaongeza upatikanaji wa mitaji kwa wachimbaji na wafanyabiashara, hatua itakayosaidia kukuza uchumi wa wananchi wa Geita.

Alisema sekta ya madini inaendelea kuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania, hivyo uwekezaji wa huduma za kifedha katika maeneo ya uzalishaji utaongeza ufanisi na manufaa kwa Watanzania wengi zaidi. Aidha, alibainisha kuwa hatua hiyo inaendana na juhudi za Serikali za kuongeza ushiriki wa wananchi katika sekta ya madini.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania, Bw. Jaffari Matundu, alisema Geita ni moja ya maeneo muhimu yenye ukuaji mkubwa wa shughuli za kiuchumi zinazotegemea sekta ya madini pamoja na biashara zinazoiunga mkono. Alisema kupitia tawi hilo, benki inalenga kutoa huduma salama, za kisasa na zinazokidhi mahitaji ya wateja mbalimbali.

Aliongeza kuwa benki hiyo itaendelea kutoa suluhisho za kifedha zitakazochochea ukuaji wa biashara na kuongeza ushirikishwaji wa kifedha nchini. Matundu alisema jukumu la Exim Bank linaenda zaidi ya kutoa huduma za benki, bali kuwa mshirika wa maendeleo ya biashara na jamii.

Katika kuendeleza uwajibikaji kwa jamii kupitia programu ya Exim Cares, benki hiyo pia ilitoa msaada kwa Hospitali ya Manispaa ya Geita kusaidia kuboresha huduma za afya ya uzazi, watoto wachanga na huduma za dharura. Msaada huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa hospitali kutoa huduma kwa wakati na kuboresha afya ya jamii.

Benki hiyo imeendelea kuimarisha mtandao wake wa huduma katika maeneo mbalimbali nchini sambamba na kuanzisha ushirikiano wa kimkakati na taasisi tofauti ili kurahisisha huduma za kifedha kwa wananchi na biashara. Hatua hiyo inaonyesha dhamira ya Exim Bank katika kuimarisha uchumi wa Tanzania kupitia ubunifu, uwekezaji na huduma bora za kifedha