Na Mwandishi Wetu.
DAR ES SALAAM: Wataalamu wa masuala ya jamii na saikolojia wameeleza kuwa changamoto nyingi zinazohusishwa na mitandao ya kijamii hazisababishwi na teknolojia yenyewe bali ni ukosefu wa nidhamu, kujitawala na uelewa wa watumiaji.
Kauli hiyo imesisitizwa na mtaalamu wa masuala ya kijamii, Dkt. Chris Nwachukwu, akieleza kuwa mitandao ya kijamii ni kioo kinachoakisi tabia za binadamu.
Akizungumza kupitia makala yake ya kielimu, Dkt. Nwachukwu amesema mitandao ya kijamii kama Instagram, Facebook, TikTok na X (zamani Twitter) imeleta mapinduzi makubwa katika mawasiliano, elimu na biashara, lakini matumizi yasiyo na nidhamu yameibua changamoto kama uraibu, maisha ya kuigiza, utegemezi wa misaada ya mtandaoni na njaa ya kuthaminiwa kwa “likes”.
Kwa mujibu wa mtaalamu huyo, uraibu wa mitandao ya kijamii unatokana zaidi na kushindwa kujidhibiti kuliko teknolojia yenyewe. Amesema watu wengi hutumia muda mwingi mtandaoni wakikwepa majukumu ya msingi kama kazi, masomo na familia, hali inayochochewa na upweke, msongo wa mawazo na kutokuwepo kwa malengo binafsi.
Ameongeza kuwa mitandao hiyo imekuza utamaduni wa maisha ya kuigiza, ambapo baadhi ya watumiaji huonyesha maisha ya kifahari yasiyo halisi, hali inayosababisha wivu, msongo wa mawazo na hata maamuzi mabaya ya kifedha. “Tatizo si picha au video, tatizo ni kushindwa kuchambua ukweli na kudhibiti hisia,” amesema.
Dkt. Nwachukwu pia amegusia ongezeko la tabia ya kuomba misaada mtandaoni bila mipaka, akisema hali hiyo inachochea utegemezi na kuporomosha uwajibikaji binafsi. Amesisitiza kuwa kusaidia ni jambo jema, lakini bila nidhamu kunazalisha utamaduni wa kuomba badala ya kufanya kazi.
Kuhusu afya ya akili, amesema njaa ya kuthaminiwa kupitia ‘likes’ na ‘followers’ imewafanya baadhi ya watu kupima thamani yao kwa idadi ya maoni mtandaoni, jambo linalodhuru ustawi wa kisaikolojia. “Nidhamu ya ndani ndiyo ngao dhidi ya shinikizo la uthibitisho wa mtandaoni,” ameeleza.
Kwa kuhitimisha, Dkt. Nwachukwu amesema mitandao ya kijamii ikitumika kwa nidhamu inaweza kuwa chombo chenye nguvu cha elimu, ujasiriamali na mabadiliko ya kijamii. Ameitaka jamii, hususan vijana, kujenga maadili, kujitawala na fikra makini ili kuitumia teknolojia kwa maendeleo badala ya kujiharibia maisha.
Amesisitiza kuwa suluhisho si kuilaumu mitandao ya kijamii, bali ni kujenga nidhamu ya matumizi, akisema: “Mitandao ya Jamii si adui; nidhamu ndiyo ufunguo wa mafanikio.”

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Karia Magaro, amesisitiza umuhimu wa uongozi unaozingatia sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa Halmashauri ili kuhakikisha maamuzi yanayofikiwa yanazingatia hekima, busara na maslahi mapana ya wananchi. Kauli hiyo aliitoa wakati wa kuhitimisha hotuba yake katika Mkutano wa Kawaida wa Robo ya Pili wa Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Katika mkutano huo, Magaro alieleza kuwa utekelezaji wa bajeti iliyopitishwa unahitaji ufuatiliaji wa karibu na mshikamano baina ya viongozi wa kuchaguliwa na watumishi wa Halmashauri, akibainisha kuwa ushirikiano huo ni nguzo muhimu ya kulinda utulivu na kuongeza ufanisi wa utendaji wa taasisi hiyo.
Akitoa taarifa ya mapato na matumizi, Magaro alisema Halmashauri imefanikiwa kukusanya Shilingi bilioni 6.3 za mapato ya ndani, sawa na asilimia 45.42 ya lengo la mwaka. Aidha, Halmashauri imepanga kusimamia na kutekeleza miradi ya maendeleo yenye thamani ya Shilingi bilioni 20.9, fedha zitakazotokana na mapato ya ndani, wahisani pamoja na Serikali Kuu.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Silvester Kahesi, alipongeza ushirikiano uliopo kati ya madiwani na wataalamu kuanzia ngazi ya kamati hadi Baraza, akieleza kuwa mshikamano huo umechangia kufanikisha vikao vyenye tija na maamuzi yanayoakisi matarajio ya wananchi wa Geita.
Katika hatua nyingine, Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Geita lilielekezwa kuongeza juhudi katika kusimamia na kuboresha hali ya usafi katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Geita, Katibu Tawala wa Wilaya, Lucy Beda, alisema kuwa Katoro ni lango muhimu la mkoa na ni lazima hadhi yake iendane na usafi wa mazingira, hususan ikizingatiwa kuwa ni eneo linalopokea viongozi na wageni mbalimbali wanaoingia mkoani Geita.
Akifungua kikao kazi hicho, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara hiyo, Bw. Benard Lubogo, alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wataalamu ili waweze kufanya ukokotoaji sahihi wa mchango wa sekta ya sanaa na burudani katika uchumi wa Taifa.

ZANZIBAR – Vodacom Tanzania Foundation imeanza rasmi utekelezaji wa kambi za afya bure Zanzibar kwa lengo la kusaidia jamii kupata uchunguzi wa mapema, elimu na huduma za kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza (NCDs), yakiwemo shinikizo la damu na kisukari, ambayo yameendelea kuwa changamoto kubwa kwa afya ya wananchi.
Takwimu zinaonesha kuwa takribani asilimia 34 ya magonjwa sugu nchini Tanzania yanahusishwa na magonjwa yasiyoambukiza, hali inayosababisha madhara makubwa kiafya endapo hayatagunduliki mapema. Zanzibar imekuwa miongoni mwa maeneo yenye ongezeko la wagonjwa wa shinikizo la damu na kisukari, hali iliyochochea haja ya kuimarisha jitihada za kinga na uchunguzi wa afya katika jamii.
Kambi ya afya inayofanyika kuanzia Februari 3 hadi 6, 2026 inalenga kutoa huduma za upimaji wa afya, ushauri wa kitaalamu na elimu kwa jamii kuhusu namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza. Uzinduzi rasmi wa kambi hiyo ulifanyika Februari 4, 2026, na kuhudhuriwa na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Msafiri Marijani.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Marijani alisema magonjwa ya shinikizo la damu na kisukari mara nyingi hayana dalili za awali, hivyo uchunguzi wa mapema ni muhimu katika kuzuia madhara makubwa ya kiafya. Alipongeza mchango wa Vodacom Tanzania Foundation katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha afya ya jamii kupitia mipango ya kinga na elimu.
Kwa upande wake, Meneja wa Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Sandra Oswald, alisema kambi hizo zimebuniwa mahsusi ili kupeleka huduma za afya moja kwa moja kwa wananchi, hususan wale wenye ufinyu wa upatikanaji wa huduma za uchunguzi wa mara kwa mara. Alisema kuanza kwa mpango huo Zanzibar ni hatua muhimu katika kupanua wigo wa huduma na kuongeza athari chanya kwa jamii.
Aliongeza kuwa Vodacom Tanzania Foundation itaendelea kushirikiana na wataalamu wa afya pamoja na wadau mbalimbali ili kuendeleza na kupanua mpango huo katika maeneo mengine ya nchi, ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika kufanikisha Lengo la Maendeleo Endelevu namba 3 (SDG 3) la Afya Njema na Ustawi.
Foundation hiyo imewahimiza wakazi wa Zanzibar kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kambi hizo za afya, ikisisitiza kuwa uchunguzi wa mapema, elimu na hatua za kinga ni msingi muhimu katika kujenga jamii yenye afya njema na ustawi endelevu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, mara baada ya mazungumzo kati yao, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026. 

















.jpeg)




.jpeg)











.jpeg)