Na Mwandishi Wetu
Zaidi ya mastaa na watengeneza maudhui 30 wamesafirishwa kwa ndege binafsi kutoka Dar es Salaam hadi Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kushiriki uzinduzi wa kinywaji kipya cha Serengeti Premium Apple, kilichoelezwa kuwa cha kwanza cha aina ya premium (RTD) kutengenezwa nchini Tanzania na kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL).
Uzinduzi huo wa siku tatu mfululizo umefanyika kwa mtindo wa kipekee uliolenga kuunganisha burudani, ubunifu, utalii pamoja na ladha mpya ya kinywaji hicho.
Safari hiyo ilianza kwa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kabla ya wageni hao kusafirishwa kwa ndege binafsi hadi Serengeti, ambako walipokelewa kwa hafla maalumu ndani ya hifadhi hiyo maarufu duniani.
Wakiwa Serengeti, mastaa hao walipata nafasi ya kutembelea vivutio vya utalii, kushiriki chakula cha mchana na jioni katika mazingira ya kuvutia, sambamba na burudani mbalimbali zilizopangwa kwa ustadi.
Katika siku iliyofuata, wageni hao walishiriki tukio maalumu la “Toast in the Sky”, lililofanyika angani kupitia puto maalumu la moto (hot air balloon), tukio lililoibua hisia na kuvutia wengi.
Kwa mujibu wa waandaaji, uzinduzi huo umeakisi misingi ya chapa mpya ya Serengeti Premium Apple ikiwemo ladha laini na ya kuburudisha ya apple, ubunifu wa Kitanzania, maisha ya kisasa pamoja na mafanikio ya Mtanzania wa leo.
Aidha, kampuni ya Serengeti Breweries Limited imesema uzinduzi huo unaonyesha uwezo wa Tanzania kuzalisha bidhaa zinazokidhi viwango vya kimataifa huku ikitumia vivutio vya ndani kuitangaza nchi na ubunifu wake.
Uzinduzi huo umevutia hisia za wengi huku ukiweka historia mpya katika sekta ya vinywaji na burudani nchini.










































.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)







