TRENDING NOW








NA K-VIS BLOG, GEITA.

WANACHAMA wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) wametakiwa kutumia fursa ya Maonesho ya 6 ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Bombambili vilivyopo eneo la EPZA, mkoani humo Geita, kufika kwenye banda la Mfuko huo ili kuhudumiwa na kupata elimu inayohusiana na uanachama wao, Meneja wa PSSSF Kanda ya Ziwa Magharibi, Bw. Geofrey Kolongo, amesema.

Ameyasema hayo leo Septemba 22, 2023 kwenye banda la PSSSF, kwenye maonesho hayo ambayo PSSSF ni miongoni mwa taasisi za umma zinazoshiriki ili kuwahudumia wananchi na watumishi wanaoshiriki katika maonesho hayo.

“Tunatoa huduma zote ambazo zinapatikana kwenye ofisi zetu zilizoenea kote nchini, ambambo mwanachama ataweza kupata taarifa za Michango yake, taarifaz a Mafao yatolewayo na PSSSF, Wastaafu wataweza kujihakiki kwa njia ya biometric, lakini pia elimu kuhusu Hifadhi ya Jamii, jinsi ya kutumia huudma za PSSSF kiganjani, na taarifa za uwekezaji.” Alisema Bw. Kolongo.

Maonyesho hayo ambayo hufanyika kila mwaka, yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 23, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dotto Biteko na yatafikia kilele Septemba 30, 2023.

Maonesho hayo yenye kauli mbiu; Matumizi ya teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi mazingira yamewaleta pamoja washiriki zaidi ya 400.




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Benki ya CRDB na Hospitali ya Kanda ya KCMC iliyopo mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro, zimeingia makubaliano ya kuendelea kuifanya Benki ya CRDB kuwa mtoaji wa huduma za fedha hasa ukusanyaji mapato hospitalini hapo.

Azma ya Benki ya CRDB siku zote ni kuhakikisha inatoa huduma bora na shindani zinazokidhi mahitaji ya wateja wake ikiamini kuwa huduma bora, za kisasa, jumuishi na rahisi za fedha ni muhimu kwa maendeleo ya taifa. Hivyo, Benki ya CRDB imewekeza rasilimali zake katika ubunifu wa huduma na bidhaa zake, ikiwamo kuanzisha na kuboresha kiendelevu mfumo wa upokeaji na ufanyaji malipo kwa njia za kieletroniki unaotumika kwenye taasisi tofauti ikiwemo hii ya Hospitali ya KCMC.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema Hospitali ya KCMC ni moja ya taasisi za mwanzo kuingia ubia na Benki ya CRDB kutumia mfumo huu wa malipo, mwaka 2014. Ubia huu ulienda sambamba na uzinduzi wa kadi maalum ya malipo ya Hospitali ya KCMC iliyopewa jina “TemboCard KCMC.”

Katika mwaka wa kwanza tangu kuanza kutumika kwa mfumo huo hospitalini hapo, zaidi ya shilingi bilioni 4.1 zilikusanywa na mpaka mwaka 2022, makusanyo hayo yameongezeka mara mbili na kufika shilingi bilioni 8.7 kwa mwaka.

“Tangu tulipoingia mkataba na Hospitali ya KCMC kuanza kuutumia mfumo wetu mpaka mwaka jana, tumeiwezesha Hospitali ya KCMC kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 52.8. Hiki ni kiasi kikubwa kukusanywa ndani ya miaka minane na makusanyo yamekuwa yakiongezeka kila mwaka,” amesema Raballa.
Raballa amesema katika kuimarisha ushirikiano na hospitali na pia ili kusogeza karibu zaidi huduma kwa wateja wake mwaka 2020 Benki ya CRDB ilifungua tawi hospitaini hapo. Tawi hilo linawafaa pia wafanyakazi wa hospitali, wanafunzi wanaojifunza hospitalini hapa, wagonjwa, wafanyabiashra na wananchi kwa ujumla wanaoishi au kupita maeneo ya hospitali.

Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya KCMC, Profesa Gileard Masenga amesema kabla hawajaanza kutumia mfumo wa Benki ya CRDB, walikuwa wanakusanya mapato kidogo na kuna nyakati walilipwa hata kwa fedha bandia .

“Kama mnavyofahamu uendeshaji wa hospitali ni wa gharama kubwa, hivyo usimamizi wa mapato ni kati ya vipaumbele muhimu vya hospitali yoyote. Ndio maana leo tupo tena hapa kuuhuisha mkataba wetu ili kuendelea kuwa na ufanisi mkubwa katika ukusanyaji wa mapato yetu,” amesema Profesa Masenga.
Awali, mkurugenzi huyo amesema wahasibu walilazimika kukaa na fedha nyingi kwenye ofisi zao jambo lililokuwa linawaweka kwenye hatari ya kuvamiwa hivyo kupoteza mapato ya hospitali ndio maana mwaka 2004 ilikuwa rahisi kwa menejimenti ya hospitali kushawishika kuingia makubaliano na Benki ya CRDB kutumia teknolojia ya kisasa kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mapato na kwamba mfumo huu umeondoa makosa ya kibinadamu kwa kiasi kikubwa hivyo kuongeza makusanyo.

Profesa Masenga pia amesema uhusiano wa Benki ya CRDB na Hospitali ya KCMC hauishii kwenye huduma za benki pekee kwani wao ni miongoni mwa wanufaika wa uwekezaji unaofanywa kwa jamii na Benki ya CRDB.
Profesa Masenga amesema Benki ya CRDB imewajengea eneo la mapumziko kwa wagonjwa na wasaidizi wao, na mara kadhaa imewasaidia vifaatiba na kompyuta ili kuboresha utoaji wa huduma hospitalini.

Kutokana na makubaliana haya, sio hospitali pekee itakayonufaika na mfumo huu bali pia wale wote wanaohudumiwa hospitalini hapa. Malipo sasa yatakuwa yanafanyika kutumia ‘control number’ . Hivyo yeyote anayehudumiwa Hospitali ya KCMC hata hitaji kufanya malipo kwa fedha taslimu, hivyo kuweza kufanya malipo kielektroniki.

Mhudumiwa ataweza kulipa kwa kutumia kadi za benki ikiwemo za Visa na MasterCard, pia ataweza kutumia SimBanking, internet banking na pia CRDB wakala. Malipo haya ya kisasa yanamwezesha mfanya malipo yoyote kulipia huduma ya kwake au ya mtu mwingine moja kwa moja hospitalini, akiwa popote alipo, ndani au nje ya nchi ilimradi awe na control number, ulipo tupo!



Mwanaume mmoja katika Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu ameridhia kufunga mirija ya uzazi kama njia ya kudumu ya uzazi wa mpango, kwa lengo la kuwa na watoto wachache anaomudu kuwahudumia.

Mwanaume huyo, John Sayi (47) mkazi wa Kijiji cha Sulu Kata ya Mbalagani amesema tayari ana watoto sita hivyo ameridhia kwa hiari uamuzi huo baada ya kupata elimu ya umuhimu uzazi wa mpango kupitia vyombo vya habari.

“Nilipata msukumo kutoka kwa baba mzazi ambaye alikuwa na wanawake wanne lakini hakutana kuwa na watoto wengi kwani alizaa watoto sita tu. Wake zake watatu kila mmoja alizaa mtoto mmoja akiwemo mama yangu na mwingine alizaa watoto watatu” amesema Sayi.

Amesema alipata nafasi ya kuongea na baba yake ambaye ametangulia mbele za haki aliyemweleza kwamba alikuwa akitumia njia ya asili ya uzazi wa mpango hivyo na yeye ikamuingia akilini kuwa na watoto wachache.

Mwaka 1998 Sayi alioa mke wa kwanza na kuzaa naye watoto wawili kabla ya kutengana mwaka 2002 ambapo kwa sasa anaishi na mke wa pili aliyemuoa mwaka 2,000 na kujaaliwa kupata watoto wanne hadi alipofunga mirija mwaka huu 2023.

“Wasukuma tuna tabia ya kuzaa watoto wengi, mwanaume ukimwambia mwanamke aache kuzaa anafikiri akifanya hivyo utaendelea kuzaa na wanawake wengine hivyo nilipomwambia mke wangu nataka kufunga uzazi aliamini nimedhamiria kutoendelea kuzaa” amesema Sayi na kuongeza na kukubaliana nami;

“Kwenye tendo la ndoa najisikia vizuri maana kwa sasa nachelewa kumaliza tofauti na hapo awali, wengi hatupendi kumaliza mapema hivyo wanaume wenzangu wasiwe na hofu kwamba ukifunga mirija ya uzazi utapata madhara” ameeleza Sayi.

Inaelezwa watu wengi wamekuwa wakitumia njia za uzazi wa mpango za muda mfupi na muda mrefu ambazo ni pamoja na vidonge, vipandikizi, vitanzi na kondomu tofauti na ilivyo kwa njia ya kudumu ambayo ni kufunga mirija ya uzazi kama alivyofanya Sayi.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi wa USAID Afya Yangu- RMNCAH, Mratibu wa afya ya uzazi na mpango mkoa wa Simiyu, Mary Makunja amesema wanawake wanaoongoza kwa kutumia uzazi wa mpango ikilinganishwa na wanaume.

“Kabla ya mradi huduma za uzazi wa mpango zilikuwa asilimia 36 mwaka 2022 lakini kwa sasa (2023) ni asilimia 45 huku idadi ya wanawake wanaojifungulia katika vituo vya afya/ hospitali ikifikia asilimia zaidi ya 90” amesema Makunja.

Amebainisha kuwa mwitikio wa kutumia njia za uzazi wa mpango za muda mfupi na mrefu ni mkubwa ikilinganishwa na njia ya kudumu; akisema “kwa mwaka idadi ya wanawake wanaoridhia kufunga mirija ya uzazi inafikia 100 huku wanaume wakiwa kati ya mmoja hadi watatu”.

Makunja ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa jamii ya wakazi wa Simiyu kutumia uzazi wa mpango hatua itakayowasaidia kuwalea vyema watoto wao tofauti na ilivyo sasa ambapo mwanamke anaweza kuwa na nzao kati ya saba hadi kumi jambo ambalo ni hatari kiafya.

“Jamii ya watu wa huku asilimia kubwa ni wakulima hivyo wanaona ni fahari kuoa mwanamke zaidi ya mmoja na kuzaa watoto wengi wakiamini watawasaidia kwenye shughuli za uzalishaji mali hivyo tunaendelea kuwaelimisha” amesema Makunja.

Kutokana na umuhimu wa uzazi wa mpango katika kukabiliana na vifo vya uzazi kwa wanawake na watoto, Serikali imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali likiwemo shirika la JHPIEGO linalotekeleza mradi wa USAID Afya Yangu- RMNCAH kuelimisha jamii, kuwajengea uwezo wataoa huduma za afya pamoja na kuboresha huduma katika vituo vya afya na hospitali ili kuimarisha upatikanaji wa huduma hiyo.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Mmoja wa wanaume mkoani Simiyu, John Sayi (47) aliyeridhia kutumia njia ya uzazi wa mpango ya kudumu akizungumza na wanahabari waliomtembelea wilayani Maswa kwa ajili ya kufanya naye mahojiano.
Mratibu wa afya ya uzazi na mpango mkoa wa Simiyu, Mary Makunja akizungumzia hali ya utoaji huduma za uzazi wa mpango.
Mwenyekiti wa Global Islamic Finance Awards (GIFA), Profesa Humayon Dar (kushoto) akikabidhi tuzo ya huduma bora za zinazofuata misingi ya dini ya kiislamu ‘the Best Upcoming Islamic Banking Window 2023’ kwa Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wa Kati Benki ya CRDB, Bonaventure Paul (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Benki za Kiislamu Benki ya CRDB, Rashid Rashid (katikati) iliyotolewa katika hafla ya 13 ya Global Islamic Finance Awards iliyofanyika katika Hoteli ya King Fahd Palace jijini Dakar, Senegal hivi karibuni.

Dar es Salaam. Tarehe 20 Septemba 2023: Ikiwa ni siku chache baada ya kuzindua kadi za Akaunti ya Al Barakah, Benki ya CRDB imekuwa benki ya kwanza katika ukanda wa Afrika ya Mashariki kutunukiwa tuzo ya ubora katika huduma za benki zinazofuata misingi ya sharia mwaka 2023 katika hafla ya 13 ya tuzo za Global Islamic Finance Awards (GIFA) iliyofanyika katika Hoteli ya King Fahd Palace jijini Dakar, Senegal.

Benki ya CRDB imepata tuzo hiyo ikiwa ni miaka miwili tangu Benki ya CRDB izindue dirisha la huduma za kibenki zinazofuata masharti ya Kiislamu “CRDB Al Barakah”. Akikabidhi tuzo hiyo, Mwenyekiti wa GIFA, Profesa Humayon Dar, amesema CRDB inafungua milango kwa taasisi za fedha Afrika Mashariki kuwahudumia Waislamu ambao wangefurahi kuhudumiwa kwa misingi ya imani yao.

“Benki ya CRDB ni taasisi ya kwanza ya fedha kushinda tuzo zetu. Tunaamini mtakuwa mabalozi wazuri wa kulinadi dirisha hili muhimu katika huduma za kibenki katika kuwahudumia Waislamu katika ukanda huo. Tunaamini tutaendelea kushirikiana kufungua fursa zaidi za mitaji na uwekezaji kwa wananchi mnaowahudumia,” amesema Profesa Dar.
Benki ya CRDB ilizindua huduma za Al Barakah mwishoni mwa mwaka 2021 na Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ali Mwinyi akawa mteja wa kwanza kufungua akaunti na wiki hivi karibuni benki ilimpa heshima ya kuwa mteja wa kwanza kukabidhiwa kadi ya akaunti hiyo hivyo kufungua milango kwa zaidi ya wateja 70,000 ilionao mpaka sasa.

Mpaka sasa, tayari benki imekopesha zaidi ya shilingi bilioni 90 kupitia dirisha hilo huku ikipokea amana zenye thamani ya shilingi 85 bilioni nchini kote.

Akipokea tuzo hiyo, Paul amesema inawatia moyo kuona kwamba ubunifu wanaoufanya unatambulika kimataifa hivyo akaahidi kwamba watauendeleza ili kukidhimahitajina matarajio ya wateja na wawekezaji wanaowahudumia nchini na nje ya nchi ambako Benki ya CRDB inatoa huduma zake.

“Sisi ndio benki ya kwanza kutoa Islamic banking (huduma za kibenki kwa misingi ya Kiislamu) kupitia mtandao mpana zaidi. Huduma zetu zinapatikana kwenye matawi yetu yote 260. Washindani wetu wanahudumia katika maeneo machache lakini sisi tunafika kwenye mikoa yote,” amesema Paul.
Ukiacha Zanzibar na mikoa yenye idadi kubwa ya Waislamu ukiwamo Tanga, Kigoma, Mtwara Lindi na Tabora pekee, ambako Benki ya CRDB imejielekeza, Paul amesema huduma za Al Barakah zinapatikana hata kwenye mikoa yenye idadi ndogo ya waumini wa dini hii.

Kwa upande wake, Rashid amesema imezoeleka kusikia na kuona benki na taasisi nyingine za fedha zikipata tuzo kutokana na huduma za kawaida zinazotolewa kwa wateja ila sasa ni wakati wa tuzo za huduma za benki zinazozingatia 
“Tulete tuzo za huduma zinazofuata misingi ya sharia ili kuudhihirishia ulimwengu kwamba sekta hii ni kubwa na muhimu kwa uchumina maendeleo ya Tanzania. Kwa tuzo tuliyoipata, ninaamini nchi yetu ipo kwenye nafasi nzuri ya kunufaika na fursa za uwekezaji na uwezeshaji wananchi kwa huduma za fedha zinazofuata sharia,” amesema Rashid.

Tuzo hizi za 13 za GIFA zilizoanzishwa mwaka 2011, zilitolewa mbele ya Rais wa Senegal, Macky Sall na kuhudhuriwa na mamia ya washiriki wakiwamo watafiti, wakurugenzi wa kampunina mashirika ya kimataifa kutoka kila pembe ya dunia kutambua mchango wa washindi wake ambao katika kipindi chote, wanafika zaidi ya 700. -- Ot Mi
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akishuhudia makabidhiano ya ofisi kati ya aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Everisto Longopa (kulia) ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ya vitendea kazi Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali mpya, Balozi Prof. Kennedy Gaston. Hafla hiyo fupi iliyofanyika katika Makao Makuu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Septemba 20, 2023.Hafla hiyo pia ilihusisha kumuaga Dkt Longopa.
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa na Jaji Dkt. Longopa nyaraka mbalimbali za kufanyia kazi.



Jaji Dkt. Longopa (kushoto) akimkabidhi rasmi ofisi Balozi Prof. Gaston.

Balozi Prof. Gaston akisaini kwenye kitabu baada ya kukabidhiwa ofisi.

Jaji Dkt. Longopa akizungumza wakati wa hafla hiyo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Balozi Prof. Gaston.

Balozi Prof. Gaston akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa ofisi na Jaji Dkt. Longopa na kuomba ushirikiano na watumishi wa ofisi hiyo.
Katibu Sheria Mkuu wa ofisi hiyo, Esther Cheyo akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston.
Mwandishi Mkuu wa Sheria wa ofisi hiyo, Onorius Njole akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston kwa niaba ya watumishi wa ofisi hiyo na kuahidi kwamba watumishi wako tayari kutoa ushirikiano kwake.
Baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo wakiwa nje tayari kumlaki Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa shada la maua alipowasili katika ofisi hiyo.

Mkurugenzi wa Divisheni ya Uratibu na Huduma za Ushauri wa ofisi hiyo, Dkt. Gift Kweka akitoa neno la kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Feleshi kuzungumza wakati wa makabidhiano hayo.

Baadhi ya viongozi wa ofisi hiyo.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akizungumza wakati wa makabidhiano hayo na kuwataka watumishi kutoa ushirikiano wa dhati kwa Balozi Prof. Gaston.




Mwanasheria Mkuu wa Seikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (katikati) akiwa na Balozi Prof. Gaston (kulia) pamoja na Jaji Dkt. Longopa.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

0754264203

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbarali, Bw. Missana Kwangura akitangaza matokeo ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Mbarali.
Mshindi wa Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Mbarali, Bi. Bahati Ndingo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) akitoa shukurani kwa baadhi ya wapiga kura wake walioshuhudia akitangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho.
************
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbarali, Bw. Missana Kwangura amemtangaza Bi. Bahati Ndingo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge wa Jimbo hilo baada ya kupata kura 44,334 kati ya kura 56,095 halali zilizopigwa kwenye vituo 490 vya kupigia kura.
 
Bi. Ndingo amewashinda wagombea wengine 12 ambao walikuwa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubunge kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika jana tarehe 19 Septemba, 2023.
 
Kwenye uchaguzi huo ushindani mkubwa ulioneka ukiwa baina ya Bi. Ndingo na Bw. Modestus Kilufi aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, aliyepata kura 10,014.
 
Akitangaza matokeo hayo Wilayani Mbarali leo tarehe 20 Septemba, 2023 Bw. Kwangura amesema wapiga kura yalioandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Jimbo la Mbarali ni 185,836 ambapo kati yao 56,662 ndio waliopiga kura. Ameongeza kuwa kura halali ni 56,095 na kura zilizokataliwa ni 567.
 
Wengine waliokuwa wanagombea Ubunge kwenye Jimbo hilo na idadi ya kura walizopata ni Halima Abdalah Magambo (AAFP) aliyepata kura 336, Osward Joseph Mndeva (DP) aliyepata kura 130, Zavely Raurent Seleleka (UDP) aliyepata kura 158, Exavery Town Mwataga (CCK) aliyepata kura 118 na Morris Thomas Nkongolo (TLP) aliyepata kura 139.
 
Wengine ni Mary Moses Daudi (UPDP) aliyepata kura 113, Fatuma Rashidi Ligania (NLD) aliyepata kura 105, Bariki Oswald Mwanyalu (Demokrasia Makini) aliyepata kura 207, Hashim Abasi Mdemu (ADC) aliyepata kura 173, Mwajuma Noty Mirambo (UMD) aliyepata kura 113 na Husseni Hasani Lusewa kutoka Chama cha ADA- TADEA aliyepeata kura 155.
 
Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Mbarali umefanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Francis Mtega kilichotokea tarehe 01 Julai, 2023 kwa ajali ya kugongwa na trekta dogo (power tiller).
 
Sanjari na uchaguzi huo wa Ubunge, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imefanya uchaguzi mdogo kwenye kata sita za Tanzania Bara ambapo matokeo yaliyotangazwa na Wasimamizi wa Uchaguzi wa kata zilizofanya uchaguzi yanaonesha kuwa Bw. Helman Masila wa CCM ameshinda kwenye Kata ya Nala iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Bw.  Kayombo Christopher Fabian ameshinda kwenye Kata ya Mfaranyaki iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea.
 
Matokeo mengine yanaonesha kuwa Bw. Ng’wanza Venance Mathias ameshinda kwenye Kata ya Mwaniko iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bw. Peter Dastan Massawe wa CCM ameshinda katika Kata ya Old Moshi Magharibi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Bw. Simon Rogath Massawe wa CCM ameshinda katika Kata ya Marangu Kitowo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Bw. Diwani Twaibu Ngonyani wa CCM ameshinda katika Kata ya Mtyangimbole iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.