TRENDING NOW







Na Mwandishi Wetu, Singida

Kampasi ya Singida ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) imekabidhi msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum wanaolelewa katika Kituo cha Malaika wa Matumaini kilichopo Ititi, mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho.

Zoezi hilo limeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Godwin Gondwe, akishirikiana na Mkurugenzi wa Kampasi ya Singida, Dkt. Emmanuel Tandika, pamoja na watumishi wa chuo hicho. Msaada huo umewajumuisha vyakula mbalimbali kama mchele, sukari, unga wa sembe na vifaa vya usafi, na umetolewa sambamba na zoezi la kufanya usafi katika mazingira ya kituo hicho.

Mhe. Gondwe, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida, ametoa pongezi kwa Kampasi ya Singida kwa kuonyesha moyo wa kujitolea na kuguswa na jamii, akisema kitendo hicho kimekuwa mfano wa kuigwa na taasisi nyingine katika mkoa huo.

“Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, tunapongeza kazi iliyofanywa na Chuo cha Utumishi wa Umma. Utoaji huu wa msaada umeonyesha upendo wa kweli kwa watoto hawa na umeunga mkono juhudi za serikali katika kuwajali makundi maalum,” amesema Mhe. Gondwe.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampasi ya Singida, Dkt. Emmanuel Tandika, amesema msaada huo umetolewa kama sehemu ya mchango wa chuo kwa jamii inayolizunguka.

“Tunaposherehekea miaka 25 ya kutoa huduma kwa umma, tumeona ni vyema kuonyesha upendo na mshikamano kwa watoto hawa wenye mahitaji maalum wajue kuwa hawako peke yao, jamii ipo pamoja nao na inawapenda.” Amesema Dkt. Tandika

Aidha, ameeleza kuwa msaada huo umetolewa pia ili kuwapa motisha masista na walezi wanaohudumia watoto hao licha ya changamoto wanazopitia kila siku.

Mlezi wa kituo hicho, Sista Rosalia Nicodemus, kwa niaba ya Mkuu wa Shirika, ameshukuru uongozi wa chuo na serikali ya mkoa kwa msaada huo, akisema umeleta faraja na matumaini kwa watoto wanaolelewa kituoni hapo.

“Kupokelewa kwa wageni kama hawa kumewatia moyo sana watoto wetu,” amesema. “Kwa kweli wamejisikia kupendwa na kuthaminiwa, jambo ambalo limewasaidia kupata nguvu mpya ya kuendelea.”

Sista Rosalia pia ametoa shukrani kwa wadau mbalimbali waliotoa misaada mingine, akiwahamasisha taasisi na watu binafsi kuendelea kushirikiana na kituo hicho kwa kutoa misaada na upendo.

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kimeendelea kufanya shughuli mbalimbali za kijamii katika kampasi zake za Dar es Salaam, Tabora, Tanga, Singida, Mtwara na Mbeya, kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 25 kitakaofanyika mwezi Juni 2026.











Na Mwandishi Wetu, Nzega.

Halmashauri ya Wilaya ya Nzega mkoani Tabora imeipongeza Kampuni ya Tumbaku ya Alliance One kwa kuwa kinara wa juhudi za upandaji miti ili kurejesha misitu iliyoharibiwa kutokana na shughuli za kibianadamu wilayani humo.

Akiongea katika hafla ya upandaji miti iliyoadaliwa na Kampuni hiyo katika shule ya msingi Ngukumo na Ikiniziwa, Mwakilishi wa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nzega Farida Hamis amesema mchango wa Alliance One ni muhimu katika kufanikisha maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan yanayoitaka kila Halmashauri kupanda miti milioni 1.5 kila mwaka.

Bi. Hamis amesema kuwa Wilaya ya Nzega imekuwa miongoni mwa maeneo yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa misitu kutokana na shughuli za kibinadamu, hususan ukataji miti kwa ajili ya kuni, uchomaji mkaa pamoja na shughuli za ukaushaji wa tumbaku.

Amesema juhudi za Kampuni ya Alliance One zimekuja wakati muafaka katika kurejesha uoto wa asili na kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Ameeleza kuwa ushirikiano kati ya Halmashauri na Kampuni hiyo umeongeza kasi ya upandaji miti pamoja na utoaji wa miche katika maeneo mbalimbali, hususan mashuleni, hatua inayosaidia kujenga msingi wa mabadiliko ya tabia kwa jamii kuanzia kwa wanafunzi.

“Kupitia wanafunzi hawa, tunajenga kizazi chenye uelewa wa thamani ya mazingira, ambacho kitaendelea kutunza miti hii hadi ikue na kutoa manufaa,” amesema.

Kwa upande wake, Mratibu wa masuala ya miti kutoka Kampuni ya Alliance One, Rashid Salum, amesema kampeni ya upandaji miti ilianza mwaka 2023 ikiwa na lengo la kurejesha misitu iliyoharibiwa na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa kuni hususan katika sekta ya tumbaku.

Amesema kuwa hadi sasa, kampuni hiyo imefanikiwa kupanda miti katika eneo la hekta 818 wilayani Nzega, huku pia wakipanua juhudi hizo katika Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma ambapo zaidi ya hekta 800 zimepandwa miti.

Ameongeza kuwa wanashirikiana kwa karibu na Halmashauri pamoja na wananchi wa maeneo husika, ambapo baadhi yao hupata ajira za muda kupitia shughuli za upandaji na utunzaji wa miti.

Salum amesisitiza kuwa moja ya mikakati yao mikubwa ni kuhakikisha miti inayopandwa inalindwa na kukua, ndiyo maana wameanza kuhusisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili kujenga tabia ya kuitunza.

“Kwa leo hii tumepanda miche 300 katika Shule ya Msingi Ngukumo na miche 200 katika Shule ya Sekondari Ikiniziwa. Wanafunzi wenyewe kwa kushirikiana na walimu wao wameipanda, jambo linalowajengea uwajibikaji wa kuitunza hadi ikue,” amesema.

Ameongeza kuwa kampeni hiyo ni endelevu katika maeneo yote yanayozalisha tumbaku, ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo na rasilimali ya kuni ya uhakika bila kuendelea kuharibu misitu ya asili. Pia ametoa wito kwa wananchi kuendelea kupanda miti katika maeneo yao binafsi ili kuongeza juhudi za uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wao, wanafunzi wa Shule ya Msingi Ngukumo, Sada Maganga na Baraka Amoni, wameishukuru Kampuni ya Alliance One kwa kuwapatia miche ya miti na kuwashirikisha moja kwa moja katika zoezi la upandaji.

Wamesema kuwa wamejifunza umuhimu wa miti katika kuhifadhi mazingira na wameahidi kuitunza miti waliyoipanda ili iweze kukua na kuleta faida kwa shule yao na jamii kwa ujumla. “Tutailinda miti hii kwa sababu tumejua umuhimu wake. Itatupatia kivuli, hewa safi na hata kuni hapo baadaye,” wamesema kwa pamoja.

Hatua hiyo inaonekana kuwa mwanzo wa mabadiliko chanya ya kimazingira wilayani Nzega, huku ushirikiano kati ya sekta binafsi, Serikali na jamii ukiendelea kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha uhifadhi endelevu wa misitu.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nzega Bi Farida Hamis akipanda moja ya miti katika shule ya msingi Ngukumo wilayani Nzega, miti ambayo imetolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngukumo wilayani Nzega,Bw Edmund Sinkonda, akipanda moja ya miti iliyotolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.
Batuli Hemedi Mtendaji wa Kijiji cha Ngukumo wilayani Nzega akipanda moja ya miti iliyotolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.
Mwanafunzi wa Darasa la Sita katika shule ya Msingi Ngukumo wilayani Nzega, Lucia Fidelis, akipanda mmoja ya miti shuleni hapo miti iliyotolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi la upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.
Baraka Amon, Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Ngukumo wilayani Nzega, akipanda moja ya miti iliyotolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.

Na Mwandishi Wetu -Narok, Kenya.

Rais wa Kenya, William Ruto, amempongeza mwanasiasa David Keter maarufu kama Dollarline kwa kushinda katika kura za mchujo za chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika Jimbo la Emurua Dikirr Constituency.

Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto alimpa pongezi Keter kufuatia ushindi huo muhimu uliompa tiketi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo ujao wa jimbo hilo.

Aidha, Rais Ruto alimpongeza pia mpinzani wake Bernard Ng'eno maarufu kama Buluu kwa kuendesha kampeni imara, akieleza kuwa ushindani huo umeimarisha misingi ya demokrasia ndani ya chama hicho kuanzia ngazi za chini.

“Tunapongeza ushindani wa haki na wa kidemokrasia uliofanyika, ambao unaimarisha chama chetu na kuonesha mshikamano wa wanachama,” ilieleza sehemu ya ujumbe wa Rais Ruto.

Rais huyo alisisitiza kuwa baada ya mchakato wa mchujo kukamilika, ni muhimu kwa wanachama wote wa UDA kuungana na kumuunga mkono mgombea aliyepitishwa ili kuhakikisha ushindi katika uchaguzi mdogo.

“Tunakwenda mbele kama timu moja imara, tukiwa tumeungana nyuma ya mgombea wetu na ajenda ya chama,” aliongeza.

Ushindi wa Keter unatarajiwa kuongeza ushindani mkali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, huku chama cha UDA kikilenga kuimarisha nafasi yake kisiasa katika Kaunti ya Narok na maeneo ya jirani.

Moshi ilichangamka kwa mara nyingine tena huku maelfu ya wakimbiaji, mashabiki, na watazamaji wakikusanyika kwa toleo la mwaka 2026 la Kilimanjaro Marathon. Kilichoanza zaidi ya miongo miwili iliyopita kama mbio, kimekua na kuwa moja ya majukwaa yenye nguvu zaidi kitaifa nchini Tanzania, yakileta pamoja michezo, utalii, utamaduni, na jamii kwa namna ya kipekee.

Mbio za mwaka huu zilivutia ushiriki mkubwa kutoka kote Tanzania na duniani kwa ujumla, na kuimarisha nafasi yake kama tukio muhimu la utalii wa michezo. Kuanzia wanariadha wa kiwango cha juu hadi wakimbiaji wa mara ya kwanza, tukio hili liliunda uzoefu wa pamoja uliovuka mstari wa mwisho wa mashindano. Haikuwa tu kuhusu ushindani, bali pia ushiriki, muunganiko, na fahari ya taifa.

Kiini cha mafanikio haya ya muda mrefu ni Tanzania Breweries Public Limited Company kupitia chapa yake kuu ya Kilimanjaro Lager, ambayo imekuwa ikiunga mkono mbio hizi kwa miaka mingi. Ushirikiano huu umechukua nafasi kubwa katika kuunda tukio hili kuwa jukwaa linalotoa thamani ya kijamii na kiuchumi.

Mbio hizi zinaendelea kuleta faida halisi kwa uchumi wa eneo husika. Hoteli zilijaa wageni, huduma za usafiri ziliongezeka, na wafanyabiashara wadogo walipata ongezeko la biashara kutokana na wageni waliokuja Moshi. Kwa biashara nyingi ndogo, wiki ya marathon ni mojawapo ya vipindi muhimu zaidi kwa mwaka. Faida hii inaonesha mchango wa tukio hili katika kusaidia maisha ya watu na kuimarisha uchumi wa ndani.
Zaidi ya shughuli za kiuchumi, marathon hii inaongeza mwonekano wa Tanzania kimataifa. Washiriki wa kimataifa na vyombo vya habari vinaendelea kuiweka Tanzania kama kivutio kinachotoa si tu uzuri wa asili bali pia uzoefu wa kiwango cha kimataifa uliopangwa vizuri. Mkoa wa Kilimanjaro hasa unafaidika na mwonekano huu, ukithibitisha nafasi yake kama kitovu cha utalii na burudani za kipekee.

Kampeni ya mwaka huu, “The Best of Us - Vyakwetu Vizuri,” iliongeza maana ya kina kwa tukio hili. Ikitokana na misemo, methali, na lugha ya kila siku ya Watanzania, kampeni hii ilisherehekea utambulisho, uthabiti, na maadili kwa pamoja. Iliunganisha chachu ya mbio na maisha halisi ya Watanzania, na kufanya marathon hii kuwa ya kibinafsi na ya kitaifa kwa wakati mmoja.

Afya na ustawi pia vinaendelea kuwa sehemu muhimu ya faida ya marathon hii. Kwa miaka mingi, tukio hili limechangia kujenga utamaduni wa kukimbia na kuishi maisha yenye afya nchini. Watu wengi zaidi wanashiriki katika shughuli za mazoezi, na taasisi mbalimbali zinaanzisha majukwaa yanayohamasisha harakati na ustawi wa mwili. Marathon imekuwa mfano wa kile ambacho juhudi endelevu za afya ya jamii zinaweza kufanikisha nchini Tanzania.

Burudani haikuishia kwenye mbio pekee. Kili Dome kwa mara nyingine ilileta pamoja michezo, muziki, sherehe, na kuunda mazingira yenye hamasa ambapo washiriki na watazamaji waliweza kuungana na kujiburudisha. Mchanganyiko huu wa michezo na maisha ya kijamii unaakisi nafasi pana ya marathon katika kuunda uzoefu wa pamoja.

Akizungumza baada ya tukio, Mkurugenzi Mtendaji Michelle Kilpin alieleza ukuaji na umuhimu unaoendelea wa marathon hii kama jukwaa la kitaifa.

“Marathon ya Kilimanjaro inaendelea kuwaleta watu pamoja kutoka asili mbalimbali kwa namna inayoakisi maana halisi ya Tanzania. Inaunga mkono utalii, inakuza afya, na inajenga mahusiano yenye maana katika jamii. Tunajivunia kuona jinsi tukio hili linavyoendelea kukua na kutoa thamani zaidi ya mbio zenyewe.”

Kadri toleo la mwaka 2026 linavyohitimishwa, Kilimanjaro Marathon inabaki kuwa zaidi ya tukio la kila mwaka la michezo. Ni jukwaa linalochochea shughuli za kiuchumi, linaimarisha mshikamano wa jamii, linahamasisha maisha yenye afya, na linaonesha Tanzania kwa dunia.

Kupitia uungwaji mkono wake unaoendelea, Tanzania Breweries Plc kupitia Kilimanjaro Lager inaendeleza dhamira yake ya kusaidia mipango inayowaunganisha watu na kuchangia maendeleo ya muda mrefu ya taifa. Mbio zinaweza kuishia kwenye mstari wa mwisho, lakini faida yake inaendelea kwa muda mrefu zaidi.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.


Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mama Anna Mkapa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa George Masaju akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tano, Hayati John Pombe Magufuli... Mama Janeth Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi Mheshimiwa Balozi Moses Kusiluka akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali wa kitaifa na serikali wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya Karimjee Hall kushiriki ibada ya kumuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Lukuvi, huku wakisaini kitabu cha maombolezo kuonesha heshima zao za mwisho.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, aliyesaini kitabu hicho akiambatana na mkewe Salma Kikwete, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mchinga.

Pia, Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, alijitokeza na kusaini kitabu hicho, akifuatiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Warioba.

Wengine waliotoa heshima zao ni pamoja na Mama Anna Mkapa, Jaji Mkuu wa Tanzania George Masaju, pamoja na Mama Janeth Magufuli.

Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi Moses Kusiluka, Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jacob Mkunda, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari, nao walifika na kusaini kitabu cha maombolezo.

Ibada hiyo imefanyika leo Machi 28, 2026, ikiwa ni sehemu ya shughuli za kitaifa za kuaga mwili wa kiongozi huyo aliyefariki dunia Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa alipokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu zao, viongozi hao walimwelezea marehemu Lukuvi kama kiongozi aliyekuwa na mchango mkubwa katika utumishi wa umma, hususan katika kusimamia sera na uratibu wa shughuli za serikali pamoja na kutetea maslahi ya watu wenye ulemavu.

Umati mkubwa wa wananchi nao umejitokeza kushiriki katika maombolezo hayo, wakionesha upendo na heshima kwa kiongozi huyo aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini.

Ratiba ya mazishi inaendelea kuratibiwa na serikali, huku Watanzania wakiendelea kuomboleza kifo cha mmoja wa viongozi waliotumikia taifa kwa muda mrefu.