TRENDING NOW






Mafunzo Elekezi kwa Watumishi Wapya wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) yameanza leo, Mei 28, 2026, ikiwa ni hatua muhimu ya kuandaa wataalamu wa mamlaka hiyo kwa kuzingatia misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali. Watumishi wapya 29 wanashiriki mafunzo haya .yanayotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. 


"Tunatarajia kuwa baada ya mafunzo haya, mtakuwa watumishi wa umma wanaofuata maadili ya utumishi wa umma, wakiwasiliana kwa ufanisi na kuheshimu usiri wa taarifa na nyaraka za serikali, huku pia wakielewa haki na wajibu wao," amesema.

Kwa upande wake, Bi. Zena Hussein ambaye ni Meneja wa kituo cha mafunzo kwa njia ya Mtandao  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, amesema kuwa mafunzo haya ni muhimu na lazima kwa watumishi wapya katika utumishi wa umma. 
"Mafunzo haya yanalenga kuimarisha uelewa wa misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi," amesisitiza.

Aidha amesema kuwa Mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza uelewa wa watumishi wapya kuhusu misingi ya utumishi wa umma na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ndani ya TISEZA. Vilevile, mchakato huo unazingatia taratibu na miongozo ya serikali, kwa lengo la kuhakikisha majukumu yanatekelezwa kwa uwajibikaji, uadilifu, na ufanisi.
Mafunzo haya ni utekelezaji waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2011, uno wataka waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wapya wanapatiwa mafunzo elekezi ndani ya miezi sita tangu kuajiriwa,

Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.

Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.

Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.

“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.

Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.

Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.

“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.


Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dkt. Christopher Timbuka.

Na Mwandishi Wetu, Siha

Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro inatarajiwa kupokea zaidi ya washiriki 800 kutoka ndani na nje ya Tanzania katika mashindano makubwa ya michezo na utalii yajulikanayo kama West Kili Forest Tour Challenge, yatakayofanyika Juni 20 hadi 21, 2026 katika ukanda wa msitu wa West Kilimanjaro.

Mashindano hayo yamezinduliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dkt. Christopher Timbuka, aliyesema tukio hilo litakuwa chachu ya kuitangaza Siha kimataifa kupitia utalii wa asili, michezo na shughuli za kijamii zitakazochochea uchumi wa wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Timbuka alisema mashindano hayo yatahusisha mbio za kilomita 5, 10 na 21, pamoja na mashindano ya baiskeli na pikipiki yatakayopita katika maeneo yenye mandhari ya kuvutia ya msitu wa West Kilimanjaro.

“Tunatarajia kupokea washiriki wengi kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na nje ya nchi. Hii ni fursa kubwa kwa Siha kuendelea kujitangaza kama kitovu cha utalii wa michezo na uhifadhi wa mazingira,” alisema Dkt. Timbuka.

Aliongeza kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika ili kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa mafanikio makubwa huku yakitoa nafasi kwa wananchi kunufaika kupitia biashara mbalimbali zikiwemo malazi, chakula, usafiri na huduma nyingine za kijamii.

Kwa mujibu wa waandalizi, kabla ya siku ya mashindano kutafanyika mkesha maalumu wa burudani utakaojumuisha shughuli za kijamii, muziki, chakula na vinywaji kwa washiriki na wadau mbalimbali.

Mashindano hayo yanaungwa mkono na kampuni ya Mati Super Brands Ltd ambayo imeahidi kushirikiana kuhakikisha tukio hilo linakuwa la kipekee na lenye mafanikio makubwa.

Akizungumza kuhusu malengo ya mashindano hayo, Mratibu wa West Kili Forest Tour Challenge, Bw. Mensier Elly, alisema tukio hilo si la michezo pekee bali ni jukwaa muhimu la kutangaza vivutio vya utalii vya West Kilimanjaro na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira kupitia michezo na utalii endelevu.

“Tunataka kutumia michezo kama njia ya kuhamasisha jamii kuthamini mazingira na wakati huo huo kuitangaza West Kilimanjaro kwa dunia,” alisema Bw. Elly.

Mashindano hayo yanatarajiwa kuwa miongoni mwa matukio makubwa ya michezo na utalii nchini mwaka huu kutokana na ushiriki mkubwa unaotarajiwa pamoja na mvuto wa kipekee wa mazingira ya West Kilimanjaro.



Mbunge wa Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro, Dkt. Godwin Mollel akitoa neno.

Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti West Kilimanjaro, PCO Robert Faida akisoma risala. 

 Mratibu wa West Kili Forest Tour Challenge, Bw. Mensier Elly 


















Mmoja ya Wazee wa Siha akitoa neno.










Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Kampuni ya teknolojia ya kifedha ya Black Swan-Tanzania imeingia kwenye orodha ya kampuni 25 bora zinazochipukia barani Afrika kwa mwaka 2026 iliyotolewa na taasisi kubwa ya habari za fedha duniani, Bloomberg.

Black Swan, kampuni iliyosajiliwa Tanzania na inayojihusisha na huduma za kifedha kupitia teknolojia ya akili mnemba (AI), imetambuliwa kutokana na mchango wake wa kurahisisha upatikanaji wa mikopo nafuu na ya haki kwa Waafrika ambao bado hawajahudumiwa kikamilifu na mifumo rasmi ya kifedha.

Orodha hiyo ya Bloomberg hutambua kampuni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika zinazotatua changamoto muhimu kwa kutumia teknolojia na ubunifu wenye matokeo chanya katika jamii na uchumi.

Kupitia teknolojia yake, Black Swan hubadilisha taarifa za miamala ya kifedha inayofanyika kwenye simu za mkononi kuwa taarifa zinazoweza kusaidia taasisi za fedha kufanya tathmini sahihi za mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara wadogo ambao mara nyingi hawapo kwenye mfumo rasmi wa benki.

Akizungumzia mafanikio hayo, Mwanzilishi Mwenza na Afisa Mkuu Mtendaji wa Black Swan, Derick Kazimoto, alisema kutambuliwa huko ni ishara kuwa dunia inaanza kuona mchango wa kampuni hiyo katika kuboresha ujumuishaji wa kifedha barani Afrika.

“Tunafurahia kuona juhudi zetu zinatambulika kimataifa. Mamilioni ya Watanzania wanafanya kazi na biashara kila siku lakini bado hawaonekani katika mifumo rasmi ya fedha. Tuliianzisha Black Swan kubadilisha hali hiyo,” alisema Kazimoto.

Alisema teknolojia ya kampuni hiyo inachakata taarifa za kifedha kwa usalama na kwa idhini ya watumiaji ili kusaidia wakopeshaji kufanya maamuzi ya haraka, sahihi na yenye uwazi zaidi.

Kwa sasa Black Swan inahudumia zaidi ya taasisi 30 za kifedha Afrika Mashariki katika tathmini za mikopo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo mikopo midogo, mikopo ya kidijitali, ufadhili wa magari na mali nyingine pamoja na huduma za kawaida za mikopo.

Miongoni mwa bidhaa zake kuu ni “Kopa Gari”, mfumo wa kidijitali unaorahisisha upatikanaji wa mikopo ya magari ambapo majibu ya awali ya ustahiki wa mkopo hutolewa ndani ya dakika tano pekee.

Kampuni hiyo pia imeanzisha mfumo wa “Manka”, unaotumia akili mnemba kusaidia wakopeshaji kupata taarifa sahihi kuhusu uwezo wa mkopaji kulipa, hali inayosaidia kuongeza kasi na usahihi wa utoaji wa mikopo.

Kutambuliwa kwa Black Swan kunakuja wakati kampuni changa za teknolojia Afrika zikiendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya bara hilo kutokana na mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa kidijitali.

Kupitia mafanikio hayo, Tanzania imeendelea kujijengea nafasi kwenye ramani ya ubunifu wa teknolojia Afrika sambamba na mataifa kama Nigeria, Kenya, Afrika Kusini na Morocco yaliyowakilishwa katika orodha hiyo ya Bloomberg.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.



Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Jaji Mwambegele pia amewasisistiza watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .

Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.



Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno akizungumza na kusema kua maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
By Zamda George, CMU

DAR ES SALAAM — An atmosphere of pride, academic excellence and national prestige filled Mlimani City Hall on May 25, 2026, as the University of Dar es Salaam (UDSM) conferred degrees to 876 graduates, including 94 new PhD holders, during Cluster I of its 56th Graduation Ceremony.

The ceremony, presided over by the University Chancellor and former President of Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, reaffirmed UDSM’s position as one of Africa’s leading centres of research, innovation and intellectual leadership.

The 94 doctoral graduates came from 15 academic disciplines, reflecting the University’s growing role in producing highly skilled researchers, innovators and professionals capable of contributing to national transformation and global development.

Unlike the lively celebrations commonly associated with undergraduate graduations, the PhD ceremony carried an atmosphere of academic maturity and scholarly prestige. Dressed in elegant academic regalia, the graduates proudly crossed the stage, symbolizing years of sacrifice, resilience, rigorous research and dedication.

Speaking during the ceremony, Chancellor Kikwete urged graduates to use their education and research to solve societal challenges and contribute to national development.

“Your education must become a tool for bringing positive change to society. The knowledge and expertise you have acquired should help drive innovation, leadership and transformation for the benefit of Tanzania and the wider global community,” said Dr. Kikwete.

He further emphasized the importance of research and knowledge creation in shaping Africa’s future, noting that universities must continue producing scholars capable of providing evidence-based solutions to emerging challenges.

UDSM Vice Chancellor, Prof. William A. L. Anangisye, described the graduation ceremony as a reflection of the University’s continued growth in teaching, research, innovation and international competitiveness.

Presenting the University’s annual progress report, Prof. Anangisye revealed that UDSM currently has 235 researchers ranked among Tanzania’s top 1,000 researchers according to the AD Scientific Index 2026. This represents 23.5 percent of all top researchers across 50 institutions nationwide.

He added that the University has continued strengthening academic quality and labour market relevance through curriculum reforms, with 285 undergraduate and postgraduate programmes reviewed based on stakeholder feedback and changing market demands.

Prof. Anangisye also highlighted major achievements in innovation and research commercialization. During the 2025/2026 academic year, UDSM researchers and innovators registered six patents through BRELA, some involving student innovators.

The registered innovations include technologies for bioethanol production, mushroom cultivation using sisal waste, organic fertilizer production, protein feed development using Black Soldier Fly larvae, and wine production from bamboo juice.

“These achievements demonstrate UDSM’s ability to add value to local resources, promote the green economy and use science to provide practical development solutions,” said Prof. Anangisye.

The Vice Chancellor further revealed that through the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project, the University is currently constructing 21 new buildings and renovating three others, a move expected to increase student capacity by 4,812 spaces.

He added that UDSM has also expanded digital learning infrastructure by increasing internet capacity, digitizing more than 1,000 courses and providing short-term professional training to nearly 3,000 staff members.

Addressing graduates directly, Prof. Anangisye reminded them that education is both a privilege and a responsibility to society.

“Education is not merely a personal achievement or decoration. It is a responsibility and a debt to the nation. Use the knowledge you have acquired to serve society, create opportunities and contribute to national development,” he said.

He encouraged graduates to embrace innovation, entrepreneurship and opportunities within the digital economy, especially in situations where formal employment opportunities may not immediately be available.

One of the most inspiring moments of the ceremony was the graduation of Dr. Paul Msoka, a visually impaired scholar who earned a PhD in Education after previously completing both his Bachelor’s and Master’s degrees within the UDSM system.

Dr. Msoka’s achievement stood out as a powerful testimony to resilience, determination and the University’s commitment to inclusive education and equal access to academic opportunities.

A researcher specializing in inclusive education and visual impairment studies, Dr. Msoka has contributed scholarly work focused on improving learning opportunities for students with visual impairment in Tanzania’s inclusive schools.

His achievement inspired many graduates, lecturers, family members and guests attending the ceremony, particularly young Tanzanians living with disabilities who aspire to pursue higher education and professional excellence.

Throughout the ceremony, emotional moments unfolded as graduates celebrated with supervisors, colleagues, friends and family members. Smiles, embraces and photographs reflected years of perseverance, sacrifice and academic dedication behind every success story.

Established in 1961, the University of Dar es Salaam remains Tanzania’s premier institution of higher learning and a symbol of academic excellence. Over the decades, the University has produced influential leaders, policymakers, scholars, diplomats, entrepreneurs and professionals who continue shaping Tanzania, Africa and the wider world.

For the Class of 2026, the graduation ceremony marked not only the completion of an academic journey, but also the beginning of a new chapter of leadership, innovation and national service.

As celebrations continued outside Mlimani City Hall, one message remained clear — the future of Tanzania’s intellectual, scientific and developmental transformation continues to be shaped at the University of Dar es Salaam.

 Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwasilisha nakala za hati za utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026.
 Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwa katika mazungumzo mafupi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, mara baada ya kuwasilisha nakala za hati za utambulisho jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026. Mazungumzo hayo yalihusu uimarishaji wa ushirikiano na uhusiano baina ya nchi hizi mbili.


 


Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Taasisi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya “Kutoa Ni Moyo” yenye lengo la kuchangisha fedha na kuongeza uelewa kwa ajili ya kusaidia watoto wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo nchini.

Kampeni hiyo iliyozinduliwa Mei 25, 2026 jijini Dar es Salaam inalenga kuwaunganisha Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za jamii ili kuwapa watoto wanaozaliwa na matatizo ya moyo nafasi ya kupata matibabu na huduma muhimu za moyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge alisema zaidi ya watoto 16,000 huzaliwa kila mwaka nchini Tanzania wakiwa na matatizo ya moyo, hali inayozifanya familia nyingi kukumbana na changamoto kubwa za kiafya na kifedha.

Alisema takribani watoto 4,000 wanahitaji upasuaji wa moyo kwa haraka, huku akibainisha kuwa kwa familia nyingi muda si suala la fedha pekee bali ni suala la kuokoa maisha.
"Kupitia kampeni ya Kutoa Ni Moyo, tunatoa wito kwa Watanzania wote, taasisi, makampuni binafsi pamoja na taasisi za serikali kuwa sehemu ya harakati hizi za kuokoa maisha ya watoto," alisema Dkt. Kisenge.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa HTAF, Dkt. Naizihijwa Majani alisema kampeni hiyo imekusudia si tu kukusanya fedha, bali pia kujenga uelewa wa muda mrefu kuhusu afya ya moyo na umuhimu wa jamii kushiriki kusaidia.
Alisema Tanzania ina utamaduni mkubwa wa mshikamano na kusaidiana, hivyo kampeni hiyo inalenga kubadili michango midogo ya wananchi kuwa nguvu kubwa ya kitaifa yenye matokeo makubwa.

"Hii si kampeni ya kuchangisha fedha pekee, ni harakati inayojengwa juu ya huruma, umoja na imani kuwa kuokoa maisha ya mtoto ni jukumu la kila mmoja wetu," alisema Dkt. Majani.
Takwimu zinaonyesha kuwa magonjwa ya moyo husababisha vifo vya watu milioni 17.9 duniani kila mwaka, huku mtoto mmoja kati ya watoto 100 akizaliwa akiwa na tatizo la moyo.

Kampeni hiyo inalenga kukusanya shilingi bilioni 25 kupitia michango ya wananchi, makampuni, wadau wa maendeleo, taasisi mbalimbali, Watanzania waishio nje ya nchi, watu maarufu, jumuiya za michezo na jamii kwa ujumla.
Fedha zitakazokusanywa zitatumika kugharamia upasuaji na matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, uchunguzi wa mapema, programu za elimu ya afya ya moyo pamoja na kusaidia familia zinazokabiliwa na changamoto hiyo.

Aidha, kampeni hiyo itatumia mifumo ya kidijitali na majukwaa ya uchangishaji mtandaoni ili kurahisisha Watanzania kuchangia kwa uwazi na urahisi kutoka ndani na nje ya nchi.

Taarifa zinaonyesha kuwa juhudi za awali za uchangishaji tayari zimefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 3.08 kupitia fedha taslimu na misaada ya vifaa mbalimbali.

Na Mwandishi Wetu. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na maendeleo ya taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma.

“Tukitazama baadhi ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni, mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika jamii ya Watanzania,” amesema.

Amesisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na yanalinda maslahi ya taifa.

“Tunachosimamia ni kuhakikisha Mwandishi wa Habari anayepata ithibati anakuwa na kiwango cha elimu kisichopungua Diploma, lakini tunataka pia Waandishi wa Habari waendelee kupata mafunzo ili waweze kuimarika zaidi kitaaluma,” amesema.

Amesema ipo haja ya sekta ya habari kutafakari aina ya maudhui yanayopewa kipaumbele, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kujenga fikra na mwelekeo wa jamii.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Rabia Hussein Mohamed kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Immaculata Kajetan Banzi kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Cyprian Phocas Mkeha kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Yohane Bokobora Masara kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Juliana Laurent Masabo kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Abdi Shaaban Kagomba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Majaji 9 wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha na Majaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.