


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Uganda kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni tarehe 12 Mei, 2026.


Makubaliano hayo yanatarajiwa kusaidia uratibu wa maandalizi ya miundombinu, usafiri, usalama na masuala mengine muhimu kuelekea AFCON 2027, huku yakionesha dhamira ya Tanzania, Kenya na Uganda kushirikiana kwa karibu kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa kwa viwango vya kimataifa.
Alibainisha kuwa mkutano wa Africa Forward utatoa jukwaa muhimu kwa viongozi wa Afrika kubadilishana mawazo kuhusu changamoto na fursa zinazolikabili bara hilo katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa duniani.
Katika mazungumzo hayo, Rais Ruto pia alimweleza Rais Bio kuhusu azma ya Kenya kugombea nafasi ya jaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), ambapo alimwomba kuunga mkono mgombea wa Kenya, Jaji wa Mahakama ya Juu, Njoki Ndung'u.
Ziara hiyo ya Rais Bio nchini Kenya inaonekana kuimarisha zaidi ushirikiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili, huku viongozi hao wakisisitiza umuhimu wa mshikamano wa Afrika katika kutatua changamoto za bara hilo.
Msimamizi Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay Kiptiness akiwakaribisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini wanaoshiriki zoezi hilo Jijini Nairobi leo Mei 11, 2026. Zoezi hilo linalenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.Zoezi hilo limewakutanisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kuna umuhimu mkubwa katika kuimarisha mfumo wa usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, akibainisha kuwa mabadiliko ya hali ya usalama duniani yanahitaji nchi wanachama kushirikiana kwa karibu zaidi katika kulinda amani, utulivu na ustawi wa wananchi wake.
Aidha, amesema migogoro na hali ya kutokuwa na utulivu katika maeneo mbalimbali duniani, hususani Mashariki ya Kati pamoja na maeneo mengine yenye migogoro, inaendelea kuathiri kwa namna mbalimbali uchumi, usalama na maisha ya wananchi wa nchi za EAC. Amesema hali hiyo inaonesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mshikamano wa kikanda, kubadilishana taarifa za kiusalama na kuwa na mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto hizo.
Na Mwandishi Wetu.
Benki ya Exim Tanzania imezindua rasmi tawi lake jipya mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupanua huduma za kifedha katika maeneo yenye shughuli kubwa za kiuchumi nchini. Tawi hilo linatarajiwa kuwahudumia wachimbaji wa madini, wakulima, wafanyabiashara wadogo na wa kati pamoja na wananchi wa kawaida.
Uzinduzi huo uliofanyika Mei 9, 2026, ulihudhuriwa na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, viongozi wa Serikali, wadau wa sekta ya madini pamoja na wafanyabiashara mbalimbali wa mkoa huo. Waziri Mavunde alisema uwepo wa taasisi za kifedha kama Exim Bank utaongeza upatikanaji wa mitaji kwa wachimbaji na wafanyabiashara, hatua itakayosaidia kukuza uchumi wa wananchi wa Geita.

Alisema sekta ya madini inaendelea kuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania, hivyo uwekezaji wa huduma za kifedha katika maeneo ya uzalishaji utaongeza ufanisi na manufaa kwa Watanzania wengi zaidi. Aidha, alibainisha kuwa hatua hiyo inaendana na juhudi za Serikali za kuongeza ushiriki wa wananchi katika sekta ya madini.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania, Bw. Jaffari Matundu, alisema Geita ni moja ya maeneo muhimu yenye ukuaji mkubwa wa shughuli za kiuchumi zinazotegemea sekta ya madini pamoja na biashara zinazoiunga mkono. Alisema kupitia tawi hilo, benki inalenga kutoa huduma salama, za kisasa na zinazokidhi mahitaji ya wateja mbalimbali.







































.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)





