TRENDING NOW






Jijini Dar es Salaam jana kulishuhudiwa mjadala muhimu uliowakutanisha wadau wa tasnia ya muziki kupitia jukwaa la AfroExchange, lililodhaminiwa na Johnnie Walker, kwa lengo la kujadili namna ya kuufikisha muziki wa Tanzania kwenye masoko ya kimataifa.

Mkutano huo ulikuwa mwanzo wa mfululizo wa mazungumzo chini ya AfroExchange, unaolenga kubaini njia za kuweza kukuza na kusambaza sanaa na muziki wa Afrika nje ya mipaka yake. Katika hatua ya kwanza, mjadala uliwaweka DJs katikati, ukitambua nafasi yao muhimu kama wachochezi wa ladha ya muziki, waunganishaji wa masoko na daraja la kuifikisha sauti ya Afrika watu wengi zaidi.
Washiriki walijadili kwa kina changamoto zinazokwamisha muziki wa Tanzania kupenya katika soko la kimataifa, huku wakisisitiza fursa zilizopo kwa DJs katika kusukuma muziki huo kuvuka mipaka.

Mbali na mazungumzo, AfroExchange pia ilitangaza hatua ya utekelezaji. Kupitia mpango huo, DJs wa Tanzania watadhaminiwa kushiriki kwenye tukio la DJ Consequence nchini Nigeria, fursa itakayomuwezesha kupata uzoefu wa kimataifa pamoja na kujenga mtandao.
Hatua hii inaashiria mwanzo wa juhudi za kuimarisha ushirikiano ndani ya tasnia ya muziki barani Afrika, huku ikifungua milango kwa vipaji vya Tanzania kufikia masoko mapya.

AfroExchange inaendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha wadau, kuchochea mazungumzo yenye tija, na kuleta fursa zitakazosaidia muziki wa Tanzania kusikika kimataifa.

By Staff Writer

Dar es Salaam. Puma Energy Tanzania has strengthened its standing in the country’s energy and distribution sector after receiving two major industry awards within the same week, highlighting its operational excellence and contribution to Tanzania’s business ecosystem.

The awards were presented during events organised by CSW Tanzania Events, which brought together stakeholders from the transport, energy and business sectors to celebrate outstanding performance, innovation and service delivery.

At the Africa Transportation Excellence Awards Night 2026 held at Serena Hotel, Puma Energy Tanzania was named Best Fuel and Energy Distribution Company of the Year.
The award recognised the company’s strong performance in fuel distribution, innovation in energy solutions, and its contribution to improving efficiency and reliability across Tanzania’s transportation value chain.

In a separate recognition during the General Trading Business Networking Gala in Dar es Salaam, the company was also awarded a Trophy of Recognition for Best Trading, Distribution & Business Solutions Company.

This second accolade acknowledged Puma Energy Tanzania’s achievements in trading, supply chain management and its support for oil and gas distribution networks across the country.
Speaking on the recognitions, company representatives said the awards reflect Puma Energy Tanzania’s continued focus on delivering reliable services, driving innovation and supporting sustainable business growth.

The dual recognition further cements Puma Energy Tanzania’s reputation as one of the leading companies in Tanzania’s energy and distribution landscape, underscoring its role in strengthening the country’s fuel supply chain and broader business environment.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa I. Mzenzi akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA zilizopo jijini Dar es Salaam.
CPA. Bertha Kipangula, Mkuu wa Sehemu ya Usajili wa Wanachama, Uzingatiaji wa Sheria na Maendeleo ya Kitaaluma akitoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Kurugenzi yake na faida ya CPA na kuwa mwanachama wa Bodi.
Magreth Kageya, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano ya Umma wa NBAA akitoa mada kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na NBAA "NBAA Overview" kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA.
CPA George Lazaro, Mkaguzi wa ndani wa NBAA akitoa elimu kuhusu Ukaguzi na majukumu mbalimbali ya Mkaguzi kwa wanafunzi wa Kidato cha tano kutoka Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA.
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Baobab Stephen Mahundi akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania (NBAA) walipotembelea ofisi za Bodi ya NBAA.
Baadhi ya wafanyakazi wa NBAA na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab wakifuatilia mada kwa wataalam kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) walipotembelea ofisi za Bodi hiyo zilizopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa I. Mzenzi (waliokaa, katikati) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyakazi wa Bodi hiyo, walimu na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara kutoka Shule ya Sekondari ya Baobab walipotembelea ofisi za NBAA kwa ajili ya kupata elimu.

Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendelea kuimarisha juhudi zake za kutoa elimu kwa wanafunzi mbalimbali wa Sekondari na Elimu ya Juu nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukuza Taaluma ya Uhasibu na kuongeza uelewa kuhusu majukumu ya Bodi hiyo.

Katika mwendelezo wa juhudi hizo, wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Baobab wametembelea NBAA na kupatiwa mafunzo maalum yaliyolenga kuwajengea uelewa mpana kuhusu shughuli za Bodi pamoja na fursa zilizopo katika Taaluma ya Uhasibu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa I. Mzenzi , aliipongeza shule hiyo kwa jitihada za kuwawezesha wanafunzi wake kupata elimu ya vitendo nje ya darasa, hususan wale wanaosoma masomo ya biashara na Uhasibu.

Aidha, alieleza kuwa NBAA iko wazi kwa wanafunzi wanaosomea masomo ya uhasibu, na aliwasisitiza wasibadilishe taaluma kwa kuwa tayari wana msingi mzuri wa uhasibu. Pia alielezea kuwa hata wanafunzi wa michepuo wa masomo mengine ambao hawajasomea Uhasibu wanaweza kujiunga na mitihani ya Bodi hiyo kuanzia ngazi ya awali na hatimaye kufikia sifa za kuwa wahasibu kitaaluma.

CPA Prof. Siasa I. Mzenzi aliwasisitiza wanafunzi hao kufanya vizuri katika masomo yao ili kufikia malengo waliyojiwekea, alieleza kwamba Taaluma ya Uhasibu ina nafasi kubwa katika Taasisi mbalimbali kutokana na uhaba wa Wahasibu nchini.

Pia aliongeza kwa kuanzia ngazi za awali za masomo kunawasaidia wanafunzi kujengwa kitaaluma na kuwa wahasibu bora wa baadaye, huku akisisitiza umuhimu wa uadilifu, uaminifu na kufanya kazi kwa bidii bila kusimamiwa ili kuendeleza na kulinda hadhi ya Taaluma hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya, alisema ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wanafunzi hao, kwani imewapa fursa ya kupata taarifa sahihi na muhimu kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na mwelekeo wa Taaluma ya Uhasibu.

Naye mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Baobab, Stephen Mahundi, aliishukuru NBAA kwa kuwapatia wanafunzi elimu ya Uhasibu, akisema itawasaidia katika masomo yao ya sasa na kuwaandaa kufikia malengo yao.

Ziara hiyo ni miongoni mwa juhudi za NBAA za kuendelea kujenga kizazi cha wataalamu wa Uhasibu wenye uelewa mpana na uwezo wa kukidhi mahitaji ya soko la ajira la ndani na kimataifa na kukuza uchumi wa nchi.
Muongo mmoja wa ushirikiano na Serikali na kufanya uwekezaji wa TZS bilioni 2.5 katika miradi ya maji vijijini na SBL inaendelea kufanya uwekezaji huo.

KARATU, 30 APRILI 2026: Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo imeandika historia muhimu kwa kukamilisha mradi wake wa 30 wa maji safi na salama nchini Tanzania, uliozinduliwa rasmi katika Kata ya Baray, Wilaya ya Karatu, Mkoa wa Arusha. Hafla hiyo imeongozwa na Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Eng. Kundo A. Mathew. (Mb)

Mradi wa maji wa Baray ni miongoni mwa uwekezaji mkubwa zaidi wa SBL katika sekta ya maji, ukinufaisha zaidi ya wakazi 15,000 wa eneo hilo kwa maji safi na salama. Mradi huu una uwezo wa kuzalisha hadi mita za ujazo 110,632 kwa mwaka. Mradi huu umegharimu kiasi cha TZS milioni 344, zilizofadhiliwa kikamilifu na SBL, kwa kushirikiana na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) pamoja na Africa Community Advancement Initiative (Africai).

Baray ni miongoni mwa miradi mitatu iliyokamilishwa na SBL mwaka huu, mingine ikiwa ni katika Kata ya Kambi ya Simba (Karatu) na Kata ya Ihushi (Mwanza). Kwa pamoja, miradi hii inawakilisha uwekezaji wa TZS milioni 655 kwa mwaka wa fedha 2026, ukiwanufaisha watu 23,189 na kuongeza uwezo wa uzalishaji wa maji safi wa mita za ujazo 169,279 kwa mwaka.

Hadi sasa, SBL imewekeza takribani TZS bilioni 2.5 katika miundombinu ya maji vijijini nchini Tanzania, ikiwa imewafikia zaidi ya watu milioni 2.3.

Mpango wa “Water for Life” wa SBL umejengwa kwa kuendana moja kwa moja na Sera ya Taifa ya Maji (NAWAPO), ambayo inalenga kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika kupanga, kujenga, kuendesha, kutunza na kusimamia miradi ya maji ya jamii. Kila mradi wa SBL huanza kwa kujenga umiliki wa jamii, kwa kushirikiana kwa karibu na RUWASA, mamlaka za wilaya na vyombo vya usimamizi wa maji vya kijamii ili kuhakikisha miradi inabaki endelevu hata baada ya uzinduzi.
Mradi wa Baray unajumuisha pampu za kisasa za kuzamishwa majini (submersible pumps), nyumba za pampu, matenki ya kuhifadhia maji, mtandao wa mabomba ya usambazaji, vituo 20 vipya vya kuchotea maji, pamoja na ukarabati wa vituo 15 vilivyokuwepo awali, miundombinu ambayo sasa ni mali ya jamii inayohudumiwa.

Pamoja na miundombinu hiyo, SBL na Africai wametekeleza programu ya mafunzo ya “Women in Water, Sanitation and Hygiene (WASH)”, iliyowawezesha wanawake 30 kutoka Baray na Kambi ya Simba kupata ujuzi wa kiufundi wa matengenezo ya miundombinu ya maji na ulinzi wa vyanzo vya maji, ujasiriamali katika utengenezaji wa sabuni, elimu ya fedha na masoko, pamoja na mafunzo ya uongozi na uelewa wa ukatili wa kijinsia.

Mpango huu unaakisi imani ya msingi ya SBL kwamba maji safi ni msingi wa maendeleo ya jamii, lakini ushirikishwaji wa kiuchumi ndio unaoifanya iwe endelevu.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Eng. Kundo Mathew, aliipongeza SBL kwa mchango wake na kuhimiza ushirikiano zaidi wa sekta binafsi.

“Serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama, lakini juhudi hizi zinahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali. Tunathamini sana mchango wa sekta binafsi kama Kampuni ya Bia ya Serengeti katika kusaidia kufikia malengo haya ya kitaifa,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Dkt. Obinna Anyalebechi, alisema hatua hiyo ni kielelezo cha dhamira ya muda mrefu ya kampuni kwa nchi.

“Miradi 30 ya maji si namba tu bali ni jamii 30 ambazo maelfu ya wasichana hawalazimiki tena kutembea umbali mrefu kutafuta maji, hivyo wanaweza kwenda shule; ni akina mama wanaopata muda wa kujenga biashara zao; na ni vituo vya afya vinavyoweza kutoa huduma kwa usalama. Mradi wa Baray ni miongoni mwa miradi mikubwa zaidi tuliyowahi kutekeleza, na unatukumbusha kwa nini tulianza na kwa nini hatuachi. Sisi ni biashara ya Kitanzania, na mafanikio yetu hupimwa kwa nchi tunayojenga,” alisema.

Mkurugenzi wa Africai, Dkt. Bonus Caesar, aliongeza: “Ushirikiano huu umetuwezesha kutoa huduma muhimu kwa jamii kwa njia endelevu. Tumejipanga kuhakikisha miradi hii si tu inatekelezwa, bali pia inasimamiwa ili ilete manufaa ya muda mrefu kwa jamii. Tunashukuru SBL kwa ushirikiano wake.”

SBL ni miongoni mwa walipa kodi wakubwa nchini Tanzania na mchango wake katika uchumi wa taifa ni mkubwa. Hata hivyo, mchango wake hauishii kwenye kodi pekee, bali unaonekana katika visima vilivyochimbwa, wakulima wanaonufaika na soko, ajira zinazozalishwa na uwekezaji unaofanywa katika jamii.
Mradi wa Baray pia unasaidia moja kwa moja dira ya maendeleo ya Taifa ya Tanzania Vision 2050, inayolenga kuhakikisha angalau asilimia 85 ya wananchi wa vijijini wanapata maji safi na salama. Aidha, unatarajiwa kusaidia wakulima wa mahindi wa eneo la Karatu, wakiwemo wanaosambaza bidhaa kwa SBL.

“Wajibu wetu kwa Tanzania umejengwa kwenye nguzo tatu,” aliongeza Dkt. Anyalebechi. “Kodi tunazolipa, ajira tunazotengeneza, na uwekezaji katika jamii. Biashara endelevu na inayokua ndiyo inayowezesha nguzo hizi zote. Nguzo moja ikidhoofika, zote zinaathirika, na hivyo pia maendeleo tunayojenga pamoja na Serikali.”

Kadri Tanzania inavyojiandaa kwa malengo mapya ya mipango ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/27, SBL imeeleza dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na Serikali katika sera zinazosaidia ustahimilivu wa sekta na mapato ya taifa. Mazingira ya kodi yaliyo thabiti na yenye uwiano yanaruhusu uwekezaji wa muda mrefu unaoleta matokeo kwa jamii na miundombinu ya maji, mapato ya kodi, ajira rasmi na ukuaji wa uchumi unaohitajika nchini Tanzania.

Aidha, viongozi wa eneo la Baray pamoja na wananchi wameeleza shukrani zao kwa mradi huo na kuahidi kuuhifadhi na kuutunza kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Na Jawadu Kinyobwa

Tanzania imezidi kujiimarisha kama kitovu cha mafunzo utawala bora barani Afrika baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, kupokea ujumbe wa watu 25 kutoka nchini Somalia kwa ajili ya programu maalumu ya mafunzo ya kuendesha shughuli za utumishi wa umma kwa ufanisi.

Akizungumza mara baada ya kuwakaribisha wajumbe hao Aprili 28 , Mhe. Kikwete ameeleza kuwa ujio huo ni kielelezo cha imani ambayo mataifa mengine wanayo kwa Tanzania kama nchi ya mfano katika kuimarisha amani, utulivu na maendeleo ya kiutawala. 

Amesema lengo kuu la ugeni huo ni kujifunza namna mifumo ya utumishi wa umma nchini inavyofanya kazi, ikiwemo usimamizi wa rasilimali watu na namna utumishi huo unavyoweza kujibu kero za wananchi kwa haraka na usahihi.

Waziri Kikwete amesisitiza kuwa Watanzania wapaswa kujua kwamba "wamekalia dhahabu" kutokana na mabadiliko makubwa ya kimfumo yaliyofanyika, hususan katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita inayowezesha wananchi kuwasiliana moja kwa moja na serikali yao. 

Amebainisha kuwa matumizi ya teknolojia (Digitalization) yamerahisisha huduma ambapo kwa sasa mtumishi wa umma hahitaji kusafiri kutoka mkoani kwenda Dodoma kufuata huduma, bali anaweza kupata mahitaji yake, ikiwemo maombi ya mikopo na mawasiliano na viongozi, kupitia mifumo ya kidijitali iliyowekwa.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mkuu ambaye pia Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi, amefafanua kuwa wajumbe hao watapitishwa kwenye maeneo muhimu ya kiutendaji ikiwemo muundo wa serikali, mifumo ya Serikali Mtandao (e-Government), na mbinu za kisasa za utunzaji wa nyaraka. 

Amesema upekee wa mifumo ya Tanzania na miundombinu yake ya kisasa ya kiutendaji ndivyo vinavyovutia nchi nyingi za Afrika Mashariki na kwingineko kuja kujifunza.

Awali akizungumza Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Ernest Mabonesho, ambaye ndiye mratibu wa programu hiyo, amebainisha kuwa mafunzo hayo ni matokeo ya makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2025 kupitia Wizara ya Mambo ya Nje. 

Amesema zoezi hilo ni muendelezo wa ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Somalia, wenye lengo la kujenga kuwezesha serikali kufanya kazi kwa tija na kwa manufaa ya mataifa yote mawili.

Naye, mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo kutoka Somalia, Ayan Andullahi ameeleza kuwa kupitia mafunzo hayo amejifunza kwa kina kuhusu namna Tanzania ilivyofanikiwa kujenga mifumo madhubuti ya utumishi wa umma inayozingatia uwajibikaji, uwazi na utoaji wa huduma ufanisi na kwa wakati.

Amesisitiza kuwa, uzoefu alioupata, hususan katika matumizi ya mifumo ya kidijitali na uratibu wa rasilimali watu utakuwa chachu ya mageuzi katika taasisi yao pindi watakaporejea nchini Somalia







KATIBU Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania(TRAMEPRO) Boniventura Mwalongo amekutana na kufanya mazungumzo na Chifu Msangia Ongati Ngoje wa Rorya ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Machifu na Mzee wa Mila na Desturi Mkoa wa Mara.

Kikao hicho kilijikita katika kujadili mustakabali wa taifa letu, hususan katika maeneo ya utatuzi wa migogoro ya ardhi, maadili ya jamii, uadilifu katika utumishi wa umma, pamoja na dira ya maendeleo ya muda mrefu ya Tanzania.

Taarifa ya Makamu Mwenyekiti wa Machifu na Mzee wa Mila na Desturi Mkoa wa Mara Chifu Msangia Ongati Ngoje amesema katika kikao hicho, wamekubaliana kuimarisha nafasi ya mila na desturi katika utatuzi wa migogoro ya ardhi, kurejesha na kuendeleza maadili na uadilifu katika jamii na taasisi za umma.

Pia kujenga taifa lenye umoja, uwajibikaji na matumizi bora ya rasilimali. Aidha, walisisitiza umuhimu wa kuendeleza sekta ya tiba asili kama nyenzo ya afya na uchumi, na kulinda pamoja na kuendeleza utamaduni wa Waluo kama urithi muhimu wa taifa.

Amesena kama alivyosema mwanafalsafa mashuhuri William Shakespeare, “Ujinga ni laana; maarifa ni mabawa yanayotuinua juu.” ambapo nukuu hiyo inatukumbusha umuhimu wa sayansi, maarifa na elimu katika kuleta maendeleo endelevu ya jamii. 

Pia amesema, “Mguso mmoja wa asili huwafanya watu wote kuwa ndugu,” akisisitiza nafasi ya mazingira katika kuunganisha binadamu wote. 

Aidha, katika kuelezea maisha ya jamii na utamaduni wake, alisema, “Maisha yetu yamefumwa kwa nyuzi mchanganyiko—mema na mabaya pamoja,” jambo linalotukumbusha wajibu wa kuhifadhi mema ya utamaduni wetu na kurekebisha kasoro zilizopo.

Kwa upande wa uongozi wa kitaifa, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewahi kusisitiza kuwa, “Mila na desturi zetu ni utambulisho wetu kama taifa, ni wajibu wetu kuzilinda, kuziheshimu na kuzitumia kama chachu ya maendeleo endelevu.” 

Kauli hiyo inaonesha dhamira ya serikali katika kuendeleza urithi wa kitamaduni sambamba na maendeleo ya kisasa.

Kwa upande wa maendeleo ya eneo, Shirati ni Halmashauri ya Mji Mdogo iliyopo katika Wilaya ya Rorya, Mkoa wa Mara, Kaskazini mwa Tanzania, karibu na mpaka wa Kenya na kandokando ya Ziwa Victoria. 

“Mji huu unakadiriwa kuwa na wakazi kati ya 50,000 hadi 100,000, huku Wilaya ya Rorya ikiwa na takribani wakazi 354,490 kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2022. Idadi kubwa ya wakazi ni vijana wanaoishi vijijini.

“Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni pamoja na kilimo kinachotegemewa na zaidi ya asilimia 80 ya wananchi, kikijumuisha mazao ya mahindi, mihogo, mtama, alizeti na pamba. 

“Uvuvi pia ni shughuli muhimu inayofanyika katika Ziwa Victoria ukihusisha samaki kama sangara, sato na dagaa. Aidha, wananchi hujihusisha na ufugaji wa ng’ombe, mbuzi na kondoo pamoja na biashara ndogo ndogo, ikiwemo biashara za mipakani kati ya Tanzania na Kenya.”

Amesema Kijiografia, eneo la Shirati liko katika Mkoa wa Mara, kaskazini mwa Tanzania, karibu na mpaka wa Kenya na kuzungukwa na Ziwa Victoria, likiwa na hali ya hewa ya kitropiki yenye mvua za msimu. Hali hii huchangia kwa kiasi kikubwa shughuli za kiuchumi na maisha ya wananchi wa eneo hilo.

Amesema utamaduni wa Waluo unaendelea kuwa nguzo muhimu ya mshikamano wa jamii, ukijengwa juu ya heshima kwa wazee na viongozi wa mila, matumizi ya baraza la wazee katika utatuzi wa migogoro, mshikamano wa kifamilia na kijamii, pamoja na kuzingatia maadili ya uadilifu, uwajibikaji na upendo. 

Pamoja na hayo amesema ni wazi  ushirikiano kati ya viongozi wa mila na desturi, serikali, wataalamu na wananchi ni muhimu katika kujenga jamii yenye maadili imara, uchumi thabiti na maendeleo endelevu. 

“Tunatoa mwito kwa wadau wote kushiriki kikamilifu katika kulinda mazingira, kuendeleza tiba asili, kuhifadhi utamaduni wa Waluo na kutumia vyema fursa zilizopo kwa maendeleo ya Mkoa wa Mara na taifa kwa ujumla,”amesema Chifu Msangia Ongati Ngoje wa Rorya.