TRENDING NOW






Na Mwandishi Wetu

Wadau wa sekta ya usafiri wa majini katika mikoa ya Mwanza, Kigoma na Kagera arehe 16 Aprili, 2026 wamejitokeza na kutoa maoni yao kuhusu athari za ongezeko la bei ya mafuta, wakisisitiza umuhimu wa kuchukua hatua stahiki zitakazolinda maslahi ya wananchi pamoja na uendelevu wa huduma hiyo.

Wakizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), maafisa waratibu wa vikao hivyo, wamesema kuwa vikao hivyo vimeandaliwa kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wowote kuhusu marekebisho ya nauli za usafiri wa majini.

Wameongeza kuwa vikao hivyo vimeitishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 29 cha Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415, kinachoitakaTASAC kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupata maoni katika michakato mbalimbali inayohitaji maoni ya wadau.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika mkoani Kagera, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) wa Mkoa wa Kagera, Bw. Isaya Tendega, ameipongeza TASAC kwa kuandaa vikao hivyo ambavyo vimefanyika katika wakati muafaka kufuatia mabadiliko ya bei ya mafuta yaliyoanza kutumika hivi karibuni, hali inayoweza kuongeza gharama za uendeshaji wa vyombo vya usafiri majini na kuathiri maisha ya wananchi.
Baadhi ya wadau walioshiriki mkutano huo walieleza kuwa ni muhimu kwa mamlaka husika kuzingatia uwiano kati ya gharama za uendeshaji na uwezo wa wananchi kumudu nauli ili kuepusha kuwaongezea mzigo wananchi, hususan wale wanaotegemea usafiri wa majini kwa shughuli zao za kila siku.

Aidha, wadau wengine walipendekeza kuwepo kwa mikakati mbadala ya kupunguza gharama za uendeshaji, ikiwemo matumizi ya nishati mbadala na kuboresha ufanisi wa vyombo vya usafiri, badala ya kutegemea zaidi ongezeko la nauli.

TASAC imebainisha kuwa itaendelea kupokea maoni hadi tarehe 26 Aprili, 2026 kabla ya kukamilisha mchakato wa kufanya maamuzi ambao utakuwa shirikishi na wa uwazi, ukizingatia maoni ya wadau wote pamoja na hali halisi ya soko.
Na Mwandishi Wetu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula , amesema uandishi wa habari usiozingatia maadili unaweza kuhatarisha umoja wa kitaifa, amani na utulivu wa jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari  ambao ni wanachama wa JUMIKITA, TADIO na TBN, leo Ijumaa Aprili 17, 2026 jijini Dar es Salaam, Kipangula alisema waandishi wa habari wanapaswa kutambua uzito wa nafasi yao katika jamii, hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, ambapo taarifa wanazozitoa zina athari kubwa kwa mwenendo wa jamii.

Alifafanua kuwa amani ni hali ya kutokuwepo kwa migogoro au vurugu, huku utulivu ukimaanisha usalama na uhakika wa maisha ya wananchi bila hofu, akibainisha kuwa hali hizi mbili haziwezi kudumu bila uwepo wa umoja wa kitaifa unaojengwa juu ya mshikamano wa wananchi bila kujali tofauti zao.
“Pale ambapo uandishi hauzingatii maadili, unaweza kuchochea migawanyiko, kupotosha ukweli na hatimaye kuvuruga mshikamano wa kitaifa. Hivyo, ni muhimu kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji,” alisema Kipangula.

Alibainisha kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa msingi wa kukusanya, kuchakata na kusambaza taarifa sahihi, pamoja na kusaidia kuunda mitazamo ya wananchi kwa njia inayochangia maridhiano na maendeleo ya jamii.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Taaluma ya Uandishi wa Habari, akibainisha kuwa maadili hayo yanahimiza ukweli, usawa, uwazi na heshima kwa haki za binadamu, mambo ambayo ni msingi wa kulinda amani, kuimarisha utulivu na kukuza umoja wa kitaifa.
Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) limetoa limesisitiza kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda urithi wa mila, utamaduni, tiba asili na mazingira kama nguzo muhimu ya maendeleo endelevu ya Taifa.

TRAMEPRO inasisitiza kuwa maeneo ya mila, maarifa ya tiba asili, pamoja na mifumo ya jadi ya uhifadhi wa mazingira ni sehemu muhimu ya utambulisho wa jamii zetu. Taarifa iliyotolewa leo Aprili 17, 2026 kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) Boniventura Mwalongo,

amesema kumekuwepo na changamoto za uvamizi wa maeneo ya mila, mabadiliko holela ya matumizi ya ardhi, pamoja na kuongezeka kwa upotoshaji wa dhana ya tiba asili.

“Mwito kwa Wazee na Machifu wa Mila

TRAMEPRO inatoa wito kwa viongozi wa mila kuendelea kusimamia kwa uaminifu maeneo ya jadi, kulinda urithi wa mababu, na kuendeleza maarifa ya tiba asili. Ushirikiano na Serikali na taasisi husika ni muhimu katika kuhakikisha amani na mshikamano wa kijamii unadumishwa.

Wito kwa Jamii kwa Ujumla

“Wananchi wote wanahimizwa kuthamini urithi wa kitamaduni, kuachana na imani potofu zinazokwamisha maendeleo, na kuzingatia sheria na miongozo rasmi. Umoja na uwajibikaji ni msingi wa ustawi wa Taifa.”

Aidha ametoa ombi kwa Serikali na Wadau wa Maendeleo kuviwezesha na kuviimarisha vikundi vinavyoendeleza tiba asili, utamaduni na uhifadhi wa mazingira, Kuimarisha ushirikiano wa tafiti kati ya taasisi za ndani na za kimataifa na Kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria za ardhi na utamaduni

Pia kuchukua hatua dhidi ya vitendo vinavyosababisha migogoro ya kijamii na uvunjifu wa amani.

“Nukuu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Kuhusu Mazingira na Utamaduni

“Tunapaswa kuthamini na kulinda mila zetu njema pamoja na mazingira yetu, kwa sababu hayo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu ya Taifa letu.”

“Pia Shirika linamkumbuka kiongozi mashuhuri wa dunia, Benjamin Franklin, aliyezaliwa tarehe 17 Aprili 1706. Alikuwa mfano wa maarifa, ubunifu na maadili mema, akisisitiza umuhimu wa elimu, nidhamu na hekima katika kujenga jamii imara,” amesema Mwalongo,

Aidha amesema TRAMEPRO inawahimiza wananchi wote kushirikiana katika kulinda urithi wa utamaduni, kuendeleza tiba asili kwa misingi ya sayansi na teknolojia, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid, amefanya Kikao kazi na Kansela wa Chama Cha Kikomunisti (CPC), Ubalozi wa China nchini Tanzania Ndg. Xu Sujiang leo tarehe 16.04.2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Lengo la kikao hicho ni kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha uhusiano na itikadi za vyama hivyo.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wadau wa Sekta ya Afya pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kufungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wadau wa Sekta ya Afya pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kufungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima ya Kibinadamu ya Upasuaji wa Ubongo kutoka kwa Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Tanzania (TNS) Dkt. Othman Kiloloma kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima ya Kibinadamu ya Upasuaji wa Ubongo kutoka kwa Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Tanzania (TNS) Dkt. Othman Kiloloma kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Wafanyakazi wa Sekta ya Afya wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Wadau wa Sekta ya Afya wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.


 Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akupewa maelezo juu ya mradi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ alipokuwa Mgeni rasmi katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Janjaa: Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akikagua na kupewa maelezo juu ya maabara ya TEHAMA ambayoni ‘Smart Class” na Mkuu wa Shule hiyo alipokuwa Mgeni rasmi katika n Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akimpongeza na kumshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo kwa kujitolea computer zenye thamani ya shilingi milioni 170 kama mchango wake yeye na Alumni wengine kwa kuboresha elimu ya Sayansi katika shule hiyo.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, akiwatambulisha baadhi ya Alumni walio katika kamati ya mradi wa ujenzi wa jengo la maabara ya TEHAMA ambayo ni ‘Smart Class’ katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, akifuatiwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo.
Sehemu ya wahitimu wa kidato cha sita katika Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari 
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatano, Aprili 15, 2026, amehudhuria Mahafali ya 59 ya Shule ya Sekondari Kibaha (KSS) kama mgeni rasmi, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani.

Akiwa katika mahafali hayo, Dkt. Kikwete amezindua harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo la ghorofa la maabara ya TEHAMA na masomo mengine, ambalo linatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.

Amesema ujenzi huo ni muhimu katika kuendeleza ubunifu na uwezo wa wanafunzi katika masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM).

Aidha, Dkt. Kikwete amekubali kuwa mlezi wa kamati ya kukusanya michango kwa ajili ya mradi huo mkubwa ambao kwa sasa umefikia hatua ya msingi.

Pia, Rais Mstaafu ameishukuru jumuiya ya wanafunzi wa zamani (alumni) wa shule hiyo, wakiuongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Abdul Mombokaleo, kwa kuchangia kompyuta zenye thamani ya Shilingi Milioni 170 kwa ajili ya “Darasa Janja” (Smart Class) lililoanzishwa shuleni hapo.

Darasa hilo litakuwa ni kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa shule hiyo na shule nyingine zitakazounganishwa kupitia mfumo wa mtandao, ambapo mwalimu anaweza kufundisha madarasa yaliyoko nje ya Kibaha kwa wakati mmoja kwa njia ya kidigitali.

Katika ziara yake, Dkt. Kikwete alipata fursa ya kutembelea na kukagua Darasa Janja hilo, akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Shule kuhusu namna teknolojia hiyo inavyotumika kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji shuleni hapo.

Shule ya Sekondari Kibaha, inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha na kusimamiwa na Kurugenzi ya Hud uma za Elimu, ilianzishwa mwaka 1965 kupitia ushirikiano kati ya Serikali ya Tanganyika ya wakati huo na nchi za Nordic – Denmark, Finland, Norway, na Sweden. Wakati inaanzishwa, shule ilikuwa na wanafunzi 110 wa Kidato cha Kwanza na 60 wa Kidato cha Tano.

Kwa sasa, shule hiyo ya bweni kwa wavulana ina uwezo wa kuchukua zaidi ya wanafunzi 800 na imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi kongwe na zenye heshima kubwa katika sekta ya elimu nchini.

Dkt. Kikwete ni miongoni mwa alumni mashuhuri wa Shule ya Sekondari Kibaha, alikosoma zaidi ya miaka 60 iliyopita. Wengine waliopitia shule hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Bw. Peter Ulanga, Balozi Lazaro Nyalandu, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Nchini Prof. Hamisi Malebo, Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Bw. Abdul Mombokaleo, na Mwenyekiti Mstaafu wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe, miongoni mwa wengine wengi.

Aidha, kwa kutambua mchango mkubwa wa alumni wake, Shule ya Sekondari Kibaha inaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa elimu ili kuhakikisha inaendelea kuwa kinara katika utoaji wa elimu ya ubora nchini.
Kibaha, Katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Tumbi, Kibaha Mji, mkoani Pwani. (Picha na Habari na Issa Michuzi)
mm

Na Mwandishi Wetu.

Chuo Kikuu cha Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS) kimeendelea kuthibitisha ubora wake katika utafiti baada ya watafiti wake kadhaa kuingia katika orodha ya wanasayansi 20 bora nchini kwa mujibu wa AD Scientific Index ya mwaka 2026.

Kwa mujibu wa tangazo rasmi la chuo hicho, Profesa Mecky Matee ameongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa, akifuatiwa na marehemu Profesa Ferdinand Mugusi aliyeshika nafasi ya saba. Wengine ni Profesa Sylvia Kaaya (nafasi ya 13), Profesa Karim Manji (nafasi ya 14), Profesa Bruno Sungunya (nafasi ya 15), pamoja na Profesa Eligius Lyamuya aliyeshika nafasi ya 17.

MUHAS imesema mafanikio hayo yanaakisi mchango mkubwa wa chuo hicho katika tafiti za afya, ubunifu wa kisayansi pamoja na juhudi zake za kuimarisha huduma za afya kitaifa na kimataifa.

Aidha, chuo hicho kimetoa heshima maalum kwa marehemu Profesa Ferdinand Mugusi, kikieleza kuwa mchango wake katika tafiti na malezi ya wataalamu utaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya taaluma ya afya nchini.

Katika taarifa hiyo, MUHAS pia imewapongeza watafiti wengine wa chuo hicho waliotajwa katika viwango vya kitaifa, ikisisitiza kuwa juhudi zao zinaendelea kuimarisha hadhi ya taasisi hiyo katika jumuiya ya kitaaluma.

“Hongera sana kwa mafanikio haya makubwa, endeleeni kuinua kiwango,” ilisomeka sehemu ya ujumbe wa pongezi kutoka MUHAS.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Jiji la Dar es Salaam linatarajia kuandika historia mpya katika tasnia ya burudani baada ya kutangazwa kwa uzinduzi wa tamasha la kwanza la kimataifa la vichekesho, Punchline International Comedy Festival (PICF) 2026, litakalofanyika kuanzia Mei 25 hadi Juni 1, 2026.

Tamasha hilo lililotangazwa na Punchline Africa, linatarajiwa kuwakutanisha wachekeshaji kutoka nchi mbalimbali za Afrika kwa kipindi cha wiki moja, likijumuisha maonesho ya jukwaani, shughuli za vyombo vya habari pamoja na ubadilishanaji wa utamaduni. Kilele cha tamasha hilo kitakuwa Grand Finale itakayofanyika katika ukumbi wa The Superdome.

PICF 2026 itahusisha maonesho ya vichekesho kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza, hatua inayolenga kuonesha utofauti wa vipaji vya wacheshi barani Afrika. Waandaaji wamesema mbali na burudani, tamasha hilo lina lengo la kuhamasisha umuhimu wa vichekesho katika kuboresha afya ya akili kwa kuwapa watu nafasi ya kucheka, kupunguza msongo wa mawazo na kuunganishwa kijamii.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwanzilishi Mwenza wa Punchline Africa, Evans Bukuku, alisema tamasha hilo ni jukwaa muhimu la kuleta watu pamoja na kuwapa nafuu ya kihisia kupitia sanaa ya uchekeshaji.“Comedy siyo kuchekesha tu, ni njia ya kuelewa maisha na kupunguza msongo wa mawazo. Kupitia PICF tunataka watu waondoke wakiwa na nafuu hata kama changamoto bado zipo,” alisema.

Kwa upande wake, Balozi wa Ufaransa nchini, Anne Sophie Ave, alisema wameamua kuunga mkono tamasha hilo kutokana na mchango wa sanaa katika kukuza vipaji vya vijana na kuwajengea kujiamini.

Aliongeza kuwa Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji kutokana na nafasi yake kama kitovu cha Afrika Mashariki na historia yake katika harakati za Pan-Afrika, akisisitiza kuwa sanaa ya vichekesho inaweza kuwa daraja la kuunganisha bara hilo.
Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Filamu nchini, Emmanuel Ndumukwa, alisema serikali inaunga mkono juhudi hizo na kuona kuwa tamasha hilo linaweza kuwa chachu ya kukuza tasnia ya uchekeshaji nchini.

Kwa upande wa wasanii, mchekeshaji Humphrey Richard alisema PICF 2026 ni fursa adhimu kwa wacheshi kujifunza, kubadilishana uzoefu na kufikia masoko ya kimataifa.
Tamasha hilo linaandaliwa kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali wakiwemo Alliance Française Dar es Salaam, Tanzania Film Board pamoja na SGA Security.

Aidha, PICF ni sehemu ya mradi wa Création Africa unaofadhiliwa na Ubalozi wa Ufaransa, unaolenga kuwawezesha wasanii na taasisi za ubunifu nchini.

Tamasha hilo linatarajiwa kuvutia maelfu ya washiriki na kufikia zaidi ya watu milioni moja kupitia majukwaa ya kidigitali, huku taarifa za wasanii watakaoshiriki na ratiba kamili zikitolewa katika siku zijazo.

Dar es Salaam/Zanzibar

Kituo cha wanyamapori cha Serval Wildlife kimetoa tamko rasmi kufuatia taarifa za kifo cha mwanahabari na mtengeneza maudhui mtandaoni, Ashley, kikieleza masikitiko yake na kufafanua kuhusu tukio hilo lililozua mjadala mkubwa mitandaoni.

Kupitia taarifa hiyo, Serval Wildlife ilieleza kuwa inatoa pole za dhati kwa familia, ndugu na marafiki wa marehemu, ikisisitiza kuwa wako pamoja nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Aidha, taasisi hiyo imeweka wazi kuwa tukio la kifo hicho halikutokea katika eneo lao, bali lilitokea visiwani Zanzibar, jambo lililothibitishwa pia na Zanzibar Police Force kupitia taarifa yao rasmi.

Serval Wildlife imefafanua kuwa marehemu Ashley aliwahi kutembelea kituo hicho na kupata uzoefu mzuri, huku akiondoka katika hali njema. Imeongeza kuwa video zinazosambaa mtandaoni kwa sasa zinatokana na ziara yake katika kituo hicho, hali iliyosababisha mkanganyiko kuhusu eneo halisi la tukio.

Katika hatua nyingine, taasisi hiyo imesema haitashiriki wala kuchapisha tena picha au video za marehemu kwenye kurasa zake, kwa heshima na kuepuka kuonekana kama inatumia tukio hilo kwa masoko.

Tamko hilo limehitimishwa kwa kuomba uelewa kutoka kwa umma pamoja na kuendelea kuiombea familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi.

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Aprili 14, 2026 amekutana na kuzungumza na mjumbe maalum Jumuiya ya Madola (Commonwealth) Rais wa zamani wa Malawi Mhe.Lazarus McCarthy Chakwera ambaye alitembelea ofisi za Tume Njedengwa jijini Dodoma. Ziara hiyo maalum ya mjumbe huyo wa Jumuia ya Madola ililenga kuangalia namna Uchaguzi Mkuu wa 2025 ulivyofanyika. (Picha na INEC).