TRENDING NOW






Meneja Mwandamizi wa  Mawasiliano wa Benki ya Stanbic,  Dickson Senzi (kushoto), na Meneja wa Kidijitali na Biashara Mtandaoni wa benki hiyo, Godlisten Shirima (kulia), wakimuonyesha Malipula Suti (katikati)  jinsi ya kupokea malipo kupitia LIPA SIMPO na kusisitiza kasi, usalama na gharama nafuu ya suluhisho za malipo ya kidijitali za Stanbic kwa biashara za ndani. Ziara ya kutembelea maduka yanayotumia huduma hiyo lilifanyika  jijini Dar es salaam jana.

Mkuu wa Idara ya Kidijitali na Biashara Mtandaoni Benki ya Stanbic Tanzania, Edward Balandya (watatu kushoto) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano, Dickson Senzi (wapili kushoto) wakiongea mfanyabiashara eneo la Mwenge wakati wa ziara ya kutembelea wafanyabishara na kuangalia jinsi ya kupokea malipo kupitia LIPA SIMPO ya benki hiyo na kusisitiza kasi, usalama na gharama nafuu ya suluhisho za malipo ya kidijitali za Stanbic kwa biashara za ndani.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Februari 24, 2026 — Benki ya Stanbic Bank Tanzania imezindua rasmi huduma ya Lipa Simpo kwa wateja wake, hatua inayolenga kurahisisha malipo ya bidhaa na huduma kupitia simu bila kutumia fedha taslimu.

Huduma hiyo inaruhusu wateja kufanya malipo moja kwa moja kupitia Stanbic App au kwa kutumia USSD 15029#, huku wafanyabiashara wakiendelea kupokea malipo kupitia mfumo wa QR kutoka benki na mitandao yote nchini.

Akizungumza katika ziara ya kutoa elimu kwa wateja eneo la Mwenge, Mkuu wa Huduma za Kidijitali wa benki hiyo, Edward Balandya, alisema huduma hiyo inalenga kufanya malipo kuwa ya haraka, salama na rahisi zaidi.
Aliongeza kuwa hadi Aprili 2026, miamala ya zaidi ya shilingi 40,000 itatozwa ada ya shilingi 1,000 tu, hatua inayokusudia kuwahamasisha wateja kutumia zaidi malipo ya kidijitali.

Kwa upande wake, Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano wa benki hiyo, Dickson Senzi, alisema matumizi ya malipo yasiyo ya fedha taslimu yanaongeza uwazi wa biashara, hupunguza hatari za upotevu wa fedha na kuboresha utunzaji wa kumbukumbu kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati.

Alisema kampeni za uhamasishaji zinazoendelea katika maeneo ya biashara nchini zinalenga kuonyesha matumizi halisi ya malipo kwa QR Code pamoja na kukusanya mrejesho kutoka kwa watumiaji wa huduma hiyo.

Kwa kuimarisha huduma za mawakala, malipo ya QR Code na gharama nafuu za miamala, Stanbic Bank Tanzania inaendelea kujiweka katika nafasi ya kuongoza mageuzi ya huduma za kifedha kidijitali nchini.

Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dkt. Juma Malik Akili (Wa pili kulia) pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Jafari Matundu (Wa pili kushoto)wakikata utepe kama ishara ya kufungua kwa tawi jipya la Benki hiyo Paje, linalolenga Kusogeza huduma kwa wananchi na wafanya Biashara wa eneo hilo na kusaidia katika kukuzaUtalii na uchumi wa buluu wa Zanzibar. Tukio hilo limeshudiwa na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Bunafsi wa Benki ya Exim TanzaniaAndrew Lyimo (Kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja, Mhe. Othman Ali Maulid (kulia).Hafla hiyo imefanyika tarehe 21 Februari 2026 Visiwani Paje Zanzibar.
Na Mwandishi Wetu.

Zanzibar, Februari 21, 2026 — Benki ya Exim Bank Tanzania imezindua rasmi tawi jipya katika eneo la Paje ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi na kuchochea maendeleo ya uchumi wa visiwa hivyo, hususan sekta ya utalii.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akili, pamoja na viongozi wa Serikali, taasisi za fedha, sekta binafsi na wadau wa maendeleo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Jaffari Matundu, alisema kufunguliwa kwa tawi hilo ni hatua muhimu katika kuimarisha ujumuishi wa kifedha na kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.
Alisema uwepo wa tawi hilo utaongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wawekezaji wa utalii, wajasiriamali, wavuvi na wafanyabiashara wadogo na wa kati, huku pia likitoa suluhisho za kidijitali na huduma za ufadhili wa biashara.

Kwa upande wake, Dkt. Akili alisema hatua hiyo ni muhimu katika kukuza uchumi wa Zanzibar kwa kuwa huduma za kifedha zilizo karibu na wafanyabiashara na wawekezaji huchochea biashara, ajira na mapato ya wananchi.
Mbali na huduma za kifedha, benki hiyo imeendelea kutekeleza miradi ya uwajibikaji kwa jamii kupitia mpango wake wa Exim Cares, ikichangia katika sekta za afya, elimu na mazingira. Miongoni mwa miradi hiyo ni msaada kwa taasisi za afya ikiwemo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na miradi ya elimu na usalama wa jamii Zanzibar.

Uzinduzi wa tawi hilo unaimarisha nafasi ya benki hiyo kama mshirika wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku ukilenga kuchochea ukuaji wa biashara, uwekezaji na ustawi wa wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Dar es Salaam, 23 Februari 2026 — Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amepongeza kwa ushirikiano wa kimkakati kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini, akieleza kuwa mpango maalum wa kifedha uliozinduliwa leo kwa ajili ya wachimbaji wadogo ni hatua ya kihistoria itakayobadili kabisa mfumo wa upatikanaji wa mitaji katika sekta ya madini nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma hizo na utiaji saini wa Mkataba wa Makubaliano (MOU) uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana, Waziri Mavunde alisema sekta ya madini imeendelea kukua kwa kasi, ikichangia asilimia 10 ya Pato la Taifa na zaidi ya asilimia 56 ya mapato ya fedha za kigeni kupitia mauzo ya nje yanayozidi dola za Marekani bilioni 5 kwa mwaka.
“Sekta ya madini sasa ni injini ya uchumi wetu. Tunachokishuhudia leo ni daraja linalounganisha maono ya Serikali na nguvu ya mtaji kutoka sekta ya fedha. Ushirikiano huu unaenda moja kwa moja kumgusa mchimbaji mdogo na kumwinua katika uchumi rasmi. Benki ya CRDB hakika mmeonyesha kuwa ni Benki kiongozi katika kuleta suluhisho stahiki kwa sekta mbalimbali. Tunawashukuru sana,” alisema Waziri Mavunde.

Alisisitiza kuwa chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imekuwa ikitekeleza mageuzi ya kisera, kiusimamizi na kisheria ili kuhakikisha sekta ya madini inawanufaisha Watanzania wengi zaidi, hususan wachimbaji wadogo. Alieleza kuwa azma ya Serikali ni kuona uchimbaji hauishii kwenye kuuza mawe ghafi, bali unapanuka hadi kwenye uchakataji na uongezaji thamani ndani ya nchi.
Mpango uliozinduliwa na Benki ya CRDB unaleta mageuzi makubwa katika mfumo wa dhamana kwa kutambua dhamana mbadala zinazotokana moja kwa moja na shughuli za uchimbaji. Kwa mara ya kwanza katika sekta ya benki nchini, leseni halali za uchimbaji, mikataba ya mauzo ya dhahabu, na akiba ya dhahabu iliyohifadhiwa katika viwanda vya kusafisha pamoja inatambuliwa kama dhamana zinazokubalika kwa ajili ya mikopo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema mpango huo ni mfumo kamili wa kifedha unaogusa mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya madini kuanzia uchimbaji, uchakataji, uhifadhi, usafirishaji hadi biashara na masoko ya ndani na nje ya nchi.
“Huu ni muundo mpya wa kifedha unaotambua uhalisia wa sekta ya madini. Tumekubali dhamana zinazotokana na shughuli halisi za wachimbaji badala ya mali zisizohusiana na sekta.

 Hii itafungua milango kwa maelfu ya wachimbaji wadogo waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa kifedha,” alisema Nsekela.
Alieleza kuwa mpango huo unajumuisha mikopo ya mtaji kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za uchimbaji, mikopo ya ununuzi wa mitambo na vifaa vya kisasa, mikopo inayodhaminiwa na dhahabu, huduma za bima za migodi na wafanyakazi kupitia CRDB Insurance, pamoja na akaunti maalum za miamala ya madini na dhahabu zitakazorahisisha ufuatiliaji na uwazi wa biashara.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Donald Mmari, alimweleza Waziri wa Madini kuwa Bodi imeweka miongozo ya kimkakati inayolenga kuhakikisha sekta ya madini inakua kwa kuzingatia misingi ya uendelevu, uwajibikaji na uchumi shirikishi.
“Tunataka kuona wachimbaji wadogo wanapanda ngazi kutoka uchimbaji wa jadi hadi kutumia teknolojia bora, kupata masoko rasmi na kushiriki katika uongezaji thamani. Ukuaji wa sekta ya madini lazima uwe endelevu na wenye manufaa kwa jamii,” alisema Dkt. Mmari.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi chache za kifedha zilizowekeza kwa kiwango kikubwa zaidi katika sekta ya madini nchini. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana, Benki hiyo imetoa mikopo yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 186 katika sekta ya madini, ambapo shilingi bilioni 136 zimetolewa kwa wachimbaji wakubwa na shilingi bilioni 50 kwa wachimbaji wadogo.  

Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji, Rais wa Chama cha Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA), John Bina alisema mpango huo umeleta matumaini mapya kwa wachimbaji wadogo waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya kukosa dhamana zinazokubalika na taasisi za fedha.
“Leo tunashuhudia mwanzo wa zama mpya. Wachimbaji wadogo tumepewa heshima ya kutambuliwa kama washirika halali wa maendeleo. Tunaishukuru sana Benki ya CRDB kwa kutuletea suluhisho hii, na tunawaahidi tutaendelea kushirikiana nao pamoja na Serikali kuhakikisha tunatumia fursa hii kwa uwajibikaji,” alisema.

Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya Benki CRDB na Tume ya Madini unatarajiwa kuimarisha urasimishaji wa wachimbaji, kuongeza upatikanaji wa mitaji nafuu, kukuza ajira kwa vijana na wanawake katika maeneo ya migodi, pamoja na kuongeza mapato ya Serikali kupitia uwazi wa miamala na ufuatiliaji wa kidijitali.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalifanyika katika Kumbi tatu tofauti za Seminari Kuu Peramiho, Maposeni Sekondari na Ukumbi wa Josephat Mkuwa ni maandalizi ya Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Peramiho ambao unatarajiwa kufanyika Februari 26, 2026 na utashirikisha vyama vya siasa 15.

Wajumbe wengine wa Tume walitembelea vituo hivyo vya mafunzo na kuzungumza na washiriki hao.

Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi walipotembelewa katika kituo cha mafunzo kilichopo Ukumbi wa Seminari Kuu Peramiho.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka INEC ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kisheria Ndg. Cyprian Mbugano akizungumza jambo.
Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi walipotembelewa katika kituo cha mafunzo kilichopo Ukumbi wa Seminari Kuu Peramiho.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Peramiho, wilayani Songea mkoani Ruvuma Ndg. Exavery Luyagaza akizungumza jambo wakati wa mafunzo hayo kituo cha Seminari Kuu Peramiho.


Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi walipotembelewa katika kituo cha mafunzo kilichopo Ukumbi wa Seminari Kuu Peramiho.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Mhe. Balozi Omar Ramadhan Mapuri, leo Februari 23, 2026 ametembelea na kukagua Mafunzo kwa Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Kupiga Kura katika jimbo la Peramiho, Songea mkoani Ruvuma.


Mjumbe huyo wa Tume amewapongeza washiriki wa mafunzo na kuwataka kuzingatia weledi na kuwakumbusha kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha matatizo kama yaliyojitokeza katika uchaguzi mkuu uliopita uliofanyika Oktoba 29, 2025.


Balozi Mapuri amewasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kuwa mafanikio ya uchaguzi yatatokana na wao kuzingatia mafunzo waliyoyapata ili kufanikisha uchaguzi huu mdogo unaotarajiwa kufanyika Februari 26, 2026 kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Peramiho Jenista Mhagama.

Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma waliokua katika kituo cha mafunzo cha Maposeni Sekondari wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magdalena Rwebangira leo tarehe 23 Februari, 2026 ametembelea na kukagua mafunzo kwa makarani wasimamizi na wasimamizi wasaudizi wa vituo vya kupugia kura yaliyofanyika katika ukumbi wa Josephat Mkuwa uliyopo halmashauri ya wilaya Songea Mkoani Ruvuma ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho utakaofanyika siku ya Alhamisi tarehe 26 Februari, 2026.

Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma waliokua katika kituo cha mafunzo cha Josephat Mokuwa wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi.