TRENDING NOW







Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakjati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yamefungwa leo tarehe 30 Aprili, 2026 na yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakjati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yamefungwa leo tarehe 30 Aprili, 2026 na yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa rufani Jacobs Mwambegele akiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo.



Na. Mwandishi Wetu, Morogoro
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetoa wito kwa watendaji wa uchaguzi kuhakikisha wanatumia muda wao kusoma Katiba, sheria za uchaguzi, kanuni na maelekezo ya Tume ili waweze kusimamia uchaguzi kwa weledi.

Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk Mkoani Morogoro leo tarehe 30 Aprili, 2026 wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mchakato wa maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye Jimbo la Ismani Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 01 Juni, 2026.

“Natumia nafasi hii kuendelea kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kutenga sehemu ya muda wenu kusoma Katiba, sheria na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ili yawaongoze katika kusimamia uchaguzi utakaokuwa huru na wa haki,” amesema Jaji Mbarouk.

Amewataka watendaji hao wa uchaguzi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi ili kufanikisha uchaguzi huo mdogo ambao unafanyika kujaza nafasi wazi ya mbunge na madiwani.

“Jukumu lililopo mbele yetu ni kubwa na muhimu, linahitaji umakini na kujituma. Ni matazamio ya Tume kwamba, baada ya kupatiwa mafunzo haya, mtatekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na weledi mkizingatia ratiba ya utekelezaji ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Ismani na Kata 12 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 01 Juni, 2026,” amesema Jaji Mbarouk.

Amesisitiza kuwa ili ufanisi uwepo ni muhimu watendaji hao wazingatie sifa na uwezo wakati wa kuteua na kuajiri watendaji wa vituo vya kupigia kura kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni.

“Kuhusu ajira za watendaji wa vituo, tunayo imani kuwa mtateua na kuajiri watendaji wenye sifa na uwezo wa kufanya kazi hii muhimu kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni. Kazi ambayo inahitaji umahiri, umakini na weledi katika kuitekeleza.,” amesema Jaji Mbarouk.

Amewataka watendaji hao kuhakikisha kuwa mafunzo ya watendaji wa vituo yanafanyika kwa ufanisi na weledi katika tarehe zilizopangwa kwenye ratiba ya utekelezaji wa shughuli za uchaguzi.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo ili waweze kufahamu majukumu yao na kuyatekeleza ipasavyo wakati wa uchaguzi.

Mafunzo hayo yamewahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu.

Kata 12 za Tanzania Bara zitakazofanya uchaguzi wa Udiwani ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.


Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026.



Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026.



Sehemu ya watendaji wa uchaguzi katika jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania bara wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika mkoani Morogoro kuanzia tarehe 28 hadi 30 Aprili, 2026.


















Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameielekeza Ofisi ya Waziri Mkuu kufanyia kazi kwa kina hoja zote zilizowasilishwa na wafanyakazi nchini, zilizotolewa katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika leo.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo akiwa Mgeni Rasmi wa maadhimisho hayo yaliyofanyika leo mkoani Njombe, ambapo amesisitiza umuhimu wa serikali kuzipokea na kuzifanyia kazi hoja hizo kwa umakini ili kuendelea kulinda na kuimarisha hadhi, haki na maslahi ya wafanyakazi nchini.

Amesema kuwa wafanyakazi ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa, hivyo serikali haina budi kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa njia ya majadiliano na utekelezaji wenye tija.

Katika hotuba yake, Rais Samia pia amewataka wafanyakazi kujiandaa kukabiliana na mabadiliko ya dunia ya sasa, ikiwemo mageuzi ya kiuchumi na kiteknolojia ambayo yanaathiri soko la ajira na namna ya utoaji wa huduma kazini.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani, ushirikiano na kuaminiana miongoni mwa wananchi na wafanyakazi, akibainisha kuwa misingi hiyo ndiyo mhimili mkuu wa maendeleo na ustawi wa taifa.

Hata hivyo Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyama vya wafanyakazi pamoja na wadau wa ajira nchini ili kuhakikisha changamoto zinazojitokeza kazini zinapatiwa ufumbuzi wa haraka na wa kudumu. Amesema lengo la serikali ni kujenga mazingira bora ya kazi yanayochochea tija, nidhamu na uzalishaji, huku haki za wafanyakazi zikiendelea kulindwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo nchini.

Amesema endapo mshikamano na utulivu vitaendelea kudumishwa, Tanzania itaendelea kuwa nchi salama, yenye maendeleo endelevu na mazingira bora ya kazi kwa wananchi wake wote.



Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakiwa katika ushiriki wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.
Bw. Mussa Lugembe, Mkurugenzi wa Kampasi ya Dar es Salaam, akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kwa niaba ya Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu.

Na Mwandishi Wetu.

Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakiwemo wa makao makuu na Kampasi ya Dar es Salaam, wameungana na wafanyakazi wengine kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.

Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, sekta binafsi pamoja na mashirika ya umma, yakilenga kutambua mchango wa wafanyakazi katika maendeleo ya taifa na kujadili masuala ya ustawi wao mahali pa kazi.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye alitoa wito kwa wafanyakazi wote nchini kuzingatia uadilifu, uwajibikaji na nidhamu kazini ili kulinda taswira ya serikali.

Akizungumza mbele ya mamia ya wafanyakazi waliojitokeza kusherehekea siku hiyo, Chalamila alisema kuwa wafanyakazi ndio sura halisi ya serikali kwa wananchi, hivyo wanapaswa kutambua uzito wa nafasi walizonazo katika kuhudumia jamii.

“Tunaposherehekea siku hii muhimu, ni vyema tukatambua kuwa mfanyakazi mmoja anaweza kufanya serikali ipendwe au ichukiwe. Hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kufanya kazi kwa uaminifu, bidii na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma,” alisema Chalamila.

Aliongeza kuwa serikali inaendelea kuthamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuboresha mazingira ya kazi pamoja na maslahi yao ili kuongeza tija na ufanisi katika utoaji huduma kwa wananchi.

Kwa upande wao, watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania walieleza kuwa ushiriki wao katika maadhimisho hayo ni sehemu ya kuonesha mshikamano na wafanyakazi wengine nchini pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha utumishi wa umma.

Maadhimisho ya Mei Mosi hufanyika kila mwaka duniani kote, yakilenga kuenzi mchango wa wafanyakazi na kuhamasisha haki, usawa na ustawi wao katika maeneo ya kazi. 

Jijini Dar es Salaam jana kulishuhudiwa mjadala muhimu uliowakutanisha wadau wa tasnia ya muziki kupitia jukwaa la AfroExchange, lililodhaminiwa na Johnnie Walker, kwa lengo la kujadili namna ya kuufikisha muziki wa Tanzania kwenye masoko ya kimataifa.

Mkutano huo ulikuwa mwanzo wa mfululizo wa mazungumzo chini ya AfroExchange, unaolenga kubaini njia za kuweza kukuza na kusambaza sanaa na muziki wa Afrika nje ya mipaka yake. Katika hatua ya kwanza, mjadala uliwaweka DJs katikati, ukitambua nafasi yao muhimu kama wachochezi wa ladha ya muziki, waunganishaji wa masoko na daraja la kuifikisha sauti ya Afrika watu wengi zaidi.
Washiriki walijadili kwa kina changamoto zinazokwamisha muziki wa Tanzania kupenya katika soko la kimataifa, huku wakisisitiza fursa zilizopo kwa DJs katika kusukuma muziki huo kuvuka mipaka.

Mbali na mazungumzo, AfroExchange pia ilitangaza hatua ya utekelezaji. Kupitia mpango huo, DJs wa Tanzania watadhaminiwa kushiriki kwenye tukio la DJ Consequence nchini Nigeria, fursa itakayomuwezesha kupata uzoefu wa kimataifa pamoja na kujenga mtandao.
Hatua hii inaashiria mwanzo wa juhudi za kuimarisha ushirikiano ndani ya tasnia ya muziki barani Afrika, huku ikifungua milango kwa vipaji vya Tanzania kufikia masoko mapya.

AfroExchange inaendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha wadau, kuchochea mazungumzo yenye tija, na kuleta fursa zitakazosaidia muziki wa Tanzania kusikika kimataifa.

By Staff Writer

Dar es Salaam. Puma Energy Tanzania has strengthened its standing in the country’s energy and distribution sector after receiving two major industry awards within the same week, highlighting its operational excellence and contribution to Tanzania’s business ecosystem.

The awards were presented during events organised by CSW Tanzania Events, which brought together stakeholders from the transport, energy and business sectors to celebrate outstanding performance, innovation and service delivery.

At the Africa Transportation Excellence Awards Night 2026 held at Serena Hotel, Puma Energy Tanzania was named Best Fuel and Energy Distribution Company of the Year.
The award recognised the company’s strong performance in fuel distribution, innovation in energy solutions, and its contribution to improving efficiency and reliability across Tanzania’s transportation value chain.

In a separate recognition during the General Trading Business Networking Gala in Dar es Salaam, the company was also awarded a Trophy of Recognition for Best Trading, Distribution & Business Solutions Company.

This second accolade acknowledged Puma Energy Tanzania’s achievements in trading, supply chain management and its support for oil and gas distribution networks across the country.
Speaking on the recognitions, company representatives said the awards reflect Puma Energy Tanzania’s continued focus on delivering reliable services, driving innovation and supporting sustainable business growth.

The dual recognition further cements Puma Energy Tanzania’s reputation as one of the leading companies in Tanzania’s energy and distribution landscape, underscoring its role in strengthening the country’s fuel supply chain and broader business environment.

Rais Mstaafu, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (kushoto), pamoja na Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, wakiwa washiriki wa Programu ya Uongozi wa Mawaziri ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard Ministerial Leadership Program). Wapo pia na mwanafunzi wa Kitanzania wa Shahada ya Uzamivu (PhD), Bi. Ngasuma Eva Kanyeka, mshindi wa tuzo inayotolewa na programu hiyo na kudhaminiwa na taasisi ya Tessa Jowell Foundation. 

Rais Mstaafu, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa na mwanafunzi wa Kitanzania wa Shahada ya Uzamivu (PhD), Bi. Ngasuma Eva Kanyeka, mshindi wa tuzo ya Programu ya Uongozi wa Mawaziri ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard Ministerial Leadership Program), inayodhaminiwa na taasisi ya Tessa Jowell Foundation, pamoja na maafisa wa taasisi hiyo katika Chuo Kikuu cha Harvard, kilichopo Cambridge, jimbo la Massachusetts, nchini Marekani.

Bi. Ngasuma Eva Kanyeka, mwanafunzi wa Kitanzania wa Shahada ya Uzamivu (PhD), aliyeshinda tuzo inayotolewa na Programu ya Uongozi wa Mawaziri ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard Ministerial Leadership Program), inayodhaminiwa na taasisi ya Tessa Jowell Foundation. 

Na Mwandishi Maalumu, Havard

Akiwa katika Chuo Kikuu cha Harvard, jijini Cambridge, jimbo la Massachusetts, nchini Marekani, Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amempongeza mwanafunzi wa Kitanzania wa Shahada ya Uzamivu (PhD), Bi. Ngasuma Eva Kanyeka, kwa kushinda tuzo inayotolewa na Programu ya Uongozi wa Mawaziri ya Chuo Kikuu cha Harvard (Harvard Ministerial Leadership Program – HMLP), inayodhaminiwa na taasisi ya Tessa Jowell Foundation.

Dkt. Kikwete ni mmoja wa watoa mada katika programu hiyo ya HMLP, iliyoanzishwa mwaka 2012 kama ushirikiano wa Harvard T.H. Chan School of Public Health, Harvard Kennedy School of Government na Harvard Graduate School of Education kwa kushirikiana na Big Win Philanthropy. 

Programu hiyo hufanya kazi na viongozi wa serikali, hususan barani Afrika pamoja na Asia ya Kusini-Mashariki na Amerika ya Kusini, kwa kuwajengea uwezo mawaziri kuwa na dira iliyo wazi na uongozi thabiti wa kuendesha mageuzi makubwa yenye matokeo ya kudumu. HMLP huendesha makundi mawili kila mwaka, yakijumuisha mawaziri wa sekta mbalimbali pamoja na viongozi wa ngazi ya juu wenye majukumu ya kitaifa. 

Tuzo hiyo yenye ushindani mkubwa hutolewa kila mwaka kwa mwanafunzi mmoja wa PhD wa Harvard anayefanya utafiti unaochangia maendeleo ya nchi zinazoendelea. Tuzo hiyo inatolewa kwa udhamini wa Tessa Jowell Foundation, taasisi iliyoanzishwa kuenzi mchango wa marehemu Baroness Tessa Jowell, aliyekuwa kinara wa kuhimiza mifumo ya afya yenye huruma na maendeleo jumuishi ya utotoni. 

Kwa sasa, taasisi hiyo inaongoza juhudi za kimkakati katika kuboresha matibabu na huduma za saratani ya ubongo, pamoja na kuimarisha maendeleo ya awali ya mtoto. Kupitia uchangishaji fedha, ushawishi wa sera na ushirikiano mpana, inaunganisha wadau kutoka NHS, serikali, vyuo vikuu na asasi za kiraia ili kuleta mageuzi endelevu katika sekta ya afya na ustawi wa watoto.

Utafiti wa Bi. Kanyeka unatumia teknolojia ya akili mnemba (Artificial Intelligence) kuboresha mifumo ya dhamana ya mikopo (AI credit models), kwa lengo la kuwawezesha wanawake na vijana kupata mikopo nafuu, kuongeza kipato na kuboresha afya ya kaya.

Bi. Kanyeka ni miongoni mwa wanafunzi wachache wa Kitanzania waliopata nafasi ya kusomea Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Harvard tangu kuanzishwa kwake mwaka 1636, na ndiye wa kwanza kushinda tuzo hiyo ya kifahari.

Rais Mstaafu Dkt. Kikwete alimpongeza kwa kuiwakilisha vyema Tanzania katika jukwaa la kimataifa na kuitangaza nchi kwa heshima kubwa ndani ya Chuo Kikuu cha Harvard.  

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa I. Mzenzi akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA zilizopo jijini Dar es Salaam.
CPA. Bertha Kipangula, Mkuu wa Sehemu ya Usajili wa Wanachama, Uzingatiaji wa Sheria na Maendeleo ya Kitaaluma akitoa elimu kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Kurugenzi yake na faida ya CPA na kuwa mwanachama wa Bodi.
Magreth Kageya, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano ya Umma wa NBAA akitoa mada kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na NBAA "NBAA Overview" kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA.
CPA George Lazaro, Mkaguzi wa ndani wa NBAA akitoa elimu kuhusu Ukaguzi na majukumu mbalimbali ya Mkaguzi kwa wanafunzi wa Kidato cha tano kutoka Shule ya Sekondari ya Baobab waliotembelea na kupata mafunzo katika ofisi za Bodi ya NBAA.
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Baobab Stephen Mahundi akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania (NBAA) walipotembelea ofisi za Bodi ya NBAA.
Baadhi ya wafanyakazi wa NBAA na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara katika Shule ya Sekondari ya Baobab wakifuatilia mada kwa wataalam kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) walipotembelea ofisi za Bodi hiyo zilizopo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa I. Mzenzi (waliokaa, katikati) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyakazi wa Bodi hiyo, walimu na wanafunzi wa Kidato cha Tano wanaosoma masomo ya Biashara kutoka Shule ya Sekondari ya Baobab walipotembelea ofisi za NBAA kwa ajili ya kupata elimu.

Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendelea kuimarisha juhudi zake za kutoa elimu kwa wanafunzi mbalimbali wa Sekondari na Elimu ya Juu nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukuza Taaluma ya Uhasibu na kuongeza uelewa kuhusu majukumu ya Bodi hiyo.

Katika mwendelezo wa juhudi hizo, wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Baobab wametembelea NBAA na kupatiwa mafunzo maalum yaliyolenga kuwajengea uelewa mpana kuhusu shughuli za Bodi pamoja na fursa zilizopo katika Taaluma ya Uhasibu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa I. Mzenzi , aliipongeza shule hiyo kwa jitihada za kuwawezesha wanafunzi wake kupata elimu ya vitendo nje ya darasa, hususan wale wanaosoma masomo ya biashara na Uhasibu.

Aidha, alieleza kuwa NBAA iko wazi kwa wanafunzi wanaosomea masomo ya uhasibu, na aliwasisitiza wasibadilishe taaluma kwa kuwa tayari wana msingi mzuri wa uhasibu. Pia alielezea kuwa hata wanafunzi wa michepuo wa masomo mengine ambao hawajasomea Uhasibu wanaweza kujiunga na mitihani ya Bodi hiyo kuanzia ngazi ya awali na hatimaye kufikia sifa za kuwa wahasibu kitaaluma.

CPA Prof. Siasa I. Mzenzi aliwasisitiza wanafunzi hao kufanya vizuri katika masomo yao ili kufikia malengo waliyojiwekea, alieleza kwamba Taaluma ya Uhasibu ina nafasi kubwa katika Taasisi mbalimbali kutokana na uhaba wa Wahasibu nchini.

Pia aliongeza kwa kuanzia ngazi za awali za masomo kunawasaidia wanafunzi kujengwa kitaaluma na kuwa wahasibu bora wa baadaye, huku akisisitiza umuhimu wa uadilifu, uaminifu na kufanya kazi kwa bidii bila kusimamiwa ili kuendeleza na kulinda hadhi ya Taaluma hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya, alisema ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wanafunzi hao, kwani imewapa fursa ya kupata taarifa sahihi na muhimu kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na mwelekeo wa Taaluma ya Uhasibu.

Naye mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Baobab, Stephen Mahundi, aliishukuru NBAA kwa kuwapatia wanafunzi elimu ya Uhasibu, akisema itawasaidia katika masomo yao ya sasa na kuwaandaa kufikia malengo yao.

Ziara hiyo ni miongoni mwa juhudi za NBAA za kuendelea kujenga kizazi cha wataalamu wa Uhasibu wenye uelewa mpana na uwezo wa kukidhi mahitaji ya soko la ajira la ndani na kimataifa na kukuza uchumi wa nchi.