










Na Jawadu Kinyobwa WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa viongozi waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
Akizungumza Mei 15, 2026 katika Mahafali ya Tisa ya Taasisi hiyo yaliyofanyika katika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Mhe. Ridhiwani alisema dunia ya sasa inahitaji viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi ya wananchi.
Alisema uadilifu ni sifa muhimu ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo wahitimu wanapaswa kutumia maarifa na ujuzi walioupata kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwazi na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa viongozi wenye uzalendo. Tukumbuke msemo
wa wahenga kwamba adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti
mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za umma,”
alisema Ridhiwani.
Aidha, aliwataka wahitimu hao kulinda
rasilimali za taifa na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika maamuzi
yao ya kila siku ili kusaidia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi
nchini.
Alisema Tanzania inahitaji viongozi waaminifu na wenye
uwajibikaji ambao watatumia nafasi zao kuendeleza ustawi wa wananchi na
kuimarisha misingi ya utawala bora. 
Sambamba na hilo, Waziri
Ridhiwani alisema uongozi unaozingatia haki na uwazi utaendelea
kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya
nchi.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu
wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo alisema taasisi hiyo imetimiza
miaka 15 tangu kuanzishwa kwake rasmi Julai mwaka 2010 kwa Hati ya Rais
kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu kwa ajili ya kujenga na
kuimarisha viongozi barani Afrika.
Alisema kwa kipindi hicho,
taasisi hiyo imefanikiwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi, kuandaa
mijadala ya kisera pamoja na kufanya tafiti na machapisho yaliyosaidia
kukuza maarifa ya kiuongozi.
Kwa upande wake, akizungumza kwa
niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed alisema mafunzo hayo
yamewajengea uwezo mkubwa wa kiuongozi na kuwasaidia kufanya maamuzi
yenye tija kwa taasisi na jamii.
Alisema mahafali hayo hayakuwa
tu hitimisho la mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko makubwa ya
kiuongozi na maendeleo binafsi waliyoyapata ndani ya miezi sita ya
programu hiyo.














RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amewasili nchini Botswana leo tarehe 15 Mei 2026 kumwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika shughuli za Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Botswana, Hayati Festus Gontebanye Mogae.
Hayati Mogae alifariki dunia tarehe 08 Mei 2026 akiwa na umri wa miaka 86. Mazishi hayo yanatarajiwa kufanyika kesho, tarehe 16 Mei 2026, jijini Gaborone.
Mara baada ya kuwasili nchini humo, Mheshimiwa Dkt. Kikwete alifika katika Ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Botswana ambako alisaini katika Kitabu cha Rambirambi kuenzi mchango mkubwa wa Hayati Mogae kwa taifa la Botswana na bara la Afrika kwa ujumla.
Pichani Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Kikwete anaonekana akisaini kitabu cha rambirambi huku nyuma yake akiwa amesimama Mheshimiwa James Bwana, Balozi wa Tanzania nchini Botswana.
Katika picha ya pili, Mheshimiwa Dkt. Kikwete anaonekana akiwa pamoja na Mheshimiwa Dithapelo Keorapetse, Spika wa Bunge la Botswana, pamoja na Dkt. Gabriel Goitsemodimo Gosiame Malebang, Katibu wa Bunge la Botswana.
Wengine ni Mheshimiwa Balozi James Bwana pamoja na Balozi Mstaafu Dkt. Athalia Molokomme ambaye alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Botswana wakati wa mapokezi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu.

.jpeg)
Alisema wateja wanaweza kupakua programu hiyo, kujisajili kwa kutumia namba ya simu na kuanza kupata pointi mara moja kwa kuonyesha QR Code wanapofanya malipo katika vituo vya Puma..jpeg)
Kwa mujibu wa kampuni hiyo, mfumo wa PRIS tayari umefanikiwa katika baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Zimbabwe, Malawi na Botswana ambako umeongeza ushiriki wa wateja katika huduma za kampuni hiyo..jpeg)
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).