Na Mwandishi Wetu
DODOMA, Aprili 4, 2026 — Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kuongeza muda wa kukamilisha kazi kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyochapishwa katika Gazeti la Serikali, Tume hiyo ilianza kazi zake tarehe 20 Novemba, 2025 na ilitarajiwa kukamilisha majukumu yake ndani ya kipindi cha siku 90. Hata hivyo, kutokana na sababu mbalimbali, Tume imeshindwa kukamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa.
Imeelezwa kuwa sababu za kuongezwa kwa muda huo ni pamoja na haja ya kuhakikisha uchambuzi wa kina wa ushahidi, taarifa na maoni yaliyokusanywa kutoka kwa wadau mbalimbali. Aidha, Tume imepewa fursa ya kuwashirikisha wataalamu wa uchunguzi wa kisaikolojia ili kufanikisha kazi zake kwa ufanisi zaidi.
Sababu nyingine ni kuendelea na maandalizi ya ripoti itakayowasilishwa kwa Mheshimiwa Rais pamoja na kutoa nafasi ya kufanya tathmini ya kina ya taarifa zote zilizokusanywa.
Kutokana na hali hiyo, mamlaka husika imeidhinisha kuongezwa kwa muda wa siku ishirini na moja (21) ili kuruhusu Tume kukamilisha kazi zake ipasavyo kabla ya kuwasilisha ripoti ya mwisho.
Serikali imeendelea kuwahimiza wananchi kushirikiana na Tume kwa kutoa taarifa sahihi na kuendelea kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
Taarifa hiyo imetolewa rasmi na Mwenyekiti wa Tume tarehe 3 Aprili, 2026 jijini Dodoma.
Mwalongo amesema TRAMEPRO inatoa mwito kwa wananchi wote kutafuta huduma za afya katika vituo rasmi pindi wanapopata dalili zisizo za kawaida,kupuuza na kupinga imani potofu zisizo na msingi wa kisayansi.

Rais Ruto alimshukuru Selassie kwa uongozi wake thabiti ndani ya IMF na mchango wake mkubwa kwa nchi za Afrika, akimtakia mafanikio mema katika majukumu yake yajayo baada ya kuondoka katika taasisi hiyo.

Aidha, Mbunge Reuben Nhamanilo Kwagilwa amehamishwa na kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), huku Festo John Dugange akiteuliwa kuwa Naibu Waziri TAMISEMI anayeshughulikia masuala ya elimu.
Katika hatua nyingine, Balozi Ali Jabir Mwadini ameteuliwa kuwa Katibu wa Rais, wakati Dkt. Eveline Wilbard Munisi na Bi. Angela Kizigha wameteuliwa kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Vilevile, Balozi Said Othman Yakub amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, huku uteuzi wa Dkt. James Andilile Mwainyekule kama Mkurugenzi Mkuu wa EWURA ukitenguliwa ili kupangiwa majukumu mengine.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa uapisho wa viongozi walioteuliwa utafanyika katika tarehe itakayopangwa baadaye.
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, Aprili 1, 2026 — Exim Bank Tanzania imeingia ubia wa kimkakati na The Voice TZ kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya malipo ya kidijitali na kupunguza utegemezi wa fedha taslimu, hasa katika sekta ya burudani na huduma za chakula.
Kupitia ushirikiano huo, wateja wa The Voice TZ sasa wataweza kulipia huduma kwa kutumia kadi za Exim au huduma ya Lipa ChapChap, hatua inayolenga kurahisisha miamala kwa haraka, usalama na uwazi zaidi.
“Wateja wetu sasa wataweza kufurahia huduma bila usumbufu wa kubeba fedha taslimu, huku wakinufaika na malipo ya haraka na salama,” alisema Lyimo.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, wateja watakaotumia kadi za Exim watanufaika na punguzo la asilimia 10 kwenye bili zao, huku malipo yakithibitishwa papo hapo. Endapo kutatokea hitilafu, marejesho yatafanyika mara moja, na risiti zitatolewa kupitia ujumbe mfupi wa simu au nakala ya karatasi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Stanley Kafu, alisema benki inaendelea kumweka mteja katikati ya huduma zake kwa kuleta suluhisho rahisi na za kisasa.
Hatua hiyo inatajwa kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Exim Bank Tanzania wa kuendeleza matumizi ya teknolojia katika huduma za kifedha na kukuza uchumi usiotegemea fedha taslimu nchini.
Timu ya Vodacom Tanzania ikiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukamilisha mabadiliko ya huduma ya M-Pesa kwenda mfumo mpya wa kisasa wa fintech 2.0. Tukio hili limefanyika tarehe 2 Aprili 2026, katika makao makuu ya Vodacom Tanzania, jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam — Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania imetangaza kukamilika kwa maboresho makubwa ya huduma yake ya kifedha ya M-Pesa kufuatia uwekezaji wa dola za Marekani milioni 28, hatua inayolenga kuongeza ubora, usalama na ufanisi wa huduma hiyo nchini.
Akizungumza wakati wa kutangaza mafanikio hayo Aprili 1, 2026, Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Philip Besiimire, alisema uwekezaji huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuimarisha huduma za kifedha kidijitali na kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya wateja.
“Tunaijengea M-Pesa misingi imara kwa ajili ya siku zijazo. Lengo letu ni kuhakikisha huduma inabaki kuwa salama, ya kuaminika na yenye uwezo mkubwa zaidi wa kuwahudumia wateja wetu kwa ufanisi wa hali ya juu,” alisema Besiimire.
Maboresho hayo yamehusisha uhamishaji wa mfumo kutoka teknolojia ya awali ya G2 kwenda mfumo wa kisasa wa fintech, unaotarajiwa kuongeza uwezo wa kushughulikia miamala mingi kwa wakati mmoja pamoja na kupunguza changamoto za kukatika kwa huduma.
Kwa mujibu wa Vodacom, muundo huo mpya unarahisisha matengenezo ya mfumo kwa muda mfupi zaidi, kutoka saa nyingi hadi dakika chache, hali itakayosaidia kuhakikisha huduma inaendelea bila usumbufu mkubwa kwa watumiaji.
Aidha, kampuni hiyo imeimarisha viwango vya usalama wa taarifa na miamala ya kifedha, hatua inayotarajiwa kuongeza imani ya watumiaji katika huduma za fedha kwa njia ya simu.
Kwa upande wa mawakala na wafanyabiashara, maboresho hayo yanaleta fursa ya kupata taarifa za kina za miamala, kurahisisha usimamizi wa biashara pamoja na kuboresha huduma kwa wateja.
Vodacom pia imeeleza kuwa mfumo huo mpya utawezesha kuanzishwa kwa huduma mpya kwa haraka zaidi, hususan katika maeneo ya akiba, mikopo na malipo ya kibiashara, huku ukiendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.
Katika kuhakikisha ufanisi wa huduma mpya, kampuni hiyo imeanzisha kipindi maalum cha siku 30 kinachojulikana kama HyperCare, ambapo timu za kiufundi zitakuwa zikifuatilia kwa karibu utendaji wa mfumo na kushughulikia changamoto zozote zitakazojitokeza.
Hatua hiyo inaonesha dhamira ya Vodacom Tanzania ya kuendelea kuwekeza katika mageuzi ya kidijitali, huku ikiimarisha nafasi yake kama mdau muhimu katika kukuza ujumuishwaji wa kifedha na maendeleo ya uchumi jumuishi nchini Tanzania.








































