


Na Ruth Kyelula, Manyara
Mkoa wa Manyara unatarajia kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kimkoa tarehe 8 Machi 2026 katika Wilaya ya Simanjiro, huku Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Queen Sendiga, akitoa wito kwa jamii kuhakikisha haki za wanawake na wasichana zinalindwa na kuheshimiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari Machi 3, 2026 ofisini kwake mjini Babati, Sendiga alisema maadhimisho hayo ni fursa muhimu ya kuhamasisha jamii kushiriki katika juhudi za kukuza usawa wa kijinsia, kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuimarisha ustawi wao katika jamii.
Alisema Mkoa wa Manyara umekuwa ukikabiliwa na changamoto ya matukio ya ukatili wa kijinsia, lakini juhudi mbalimbali zimeendelea kufanyika ili kukabiliana na tatizo hilo. Alisisitiza kuwa wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuhakikisha watoto, hususan wasichana, wanapata haki zao na kulindwa dhidi ya vitendo vya ukatili.
Sendiga alieleza kuwa chimbuko la Siku ya Wanawake Duniani linatokana na harakati za wanawake wafanyakazi waliopigania haki zao kazini, jambo linaloifanya siku hiyo kuwa jukwaa la kuhimiza uwajibikaji kwa wanawake pamoja na kuwakumbusha waajiri, taasisi na serikali kuhakikisha mazingira ya kazi yanazingatia usawa wa mishahara, maslahi na fursa.
Aliongeza kuwa Tanzania imekuwa ikiadhimisha siku hiyo tangu mwaka 1997 kwa lengo la kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa ni “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050.”




Kampuni ya kubeti ya SportPesa Tanzania imeendelea kuwapa Watanzania fursa ya kubadilisha maisha yao kupitia ushindi wa jackpot pamoja na michezo mbalimbali ya kasino na Aviator, huku zaidi ya shilingi bilioni moja zikitolewa kwa washindi wa jackpot pekee katika kipindi cha mwaka uliopita.
Miongoni mwa washindi waliopata bahati hiyo ni Hamza Athman ambaye alijishindia kiasi cha shilingi 237,897,560 kupitia mchezo wa Midweek Jackpot. Ushindi huo umeelezwa kuwa umeleta mabadiliko makubwa katika maisha yake.
Akizungumza baada ya kupokea zawadi yake rasmi, Hamza alisema ushindi huo umemfungulia ukurasa mpya wa maisha na kumpa matumaini makubwa ya baadaye. Alisema siku zote alikuwa na imani kuwa ili kushinda lazima uwe sehemu ya jukwaa la SportPesa.
Ushindi huo unaonyesha kuwa michezo hiyo imeendelea kutoa fursa kwa wachezaji wa viwango mbalimbali, iwe ni kupitia jackpot zenye odd ndefu, ubashiri wa michezo au michezo ya kasino yenye multiplier kubwa. Wachezaji wamekuwa wakipokea ushindi wao moja kwa moja kwenye akaunti zao bila ucheleweshaji.
Akizungumzia mafanikio hayo, Mkuu wa Masoko wa SportPesa Tanzania, Tracy Humplick, alisema kampuni hiyo inaendelea kuboresha mifumo yake ili kuhakikisha wateja wanapata uzoefu bora wa kucheza na kupata ushindi wao kwa urahisi.
Alisema kampuni inawekeza katika teknolojia, huduma kwa wateja na kuboresha masharti ya michezo ili kuhakikisha uwazi, haki na uendelevu wa huduma kwa wachezaji wote.
Aidha, SportPesa Tanzania inaendelea kufanya shughuli zake kwa kuzingatia sheria na kanuni za serikali, huku pia ikichangia katika mapato ya taifa, kukuza sekta ya michezo na kutoa ajira kwa maelfu ya Watanzania.
Kwa mujibu wa kampuni hiyo, hadithi za washindi kama Hamza zinaendelea kuwahamasisha Watanzania wengi kujiunga na jukwaa hilo, huku zikionesha kuwa fursa ya ushindi ipo kwa kila mchezaji anayejitosa kwa nidhamu na ujasiri. Kadri idadi ya washiriki inavyoongezeka, ndivyo mzunguko wa ushindi na fursa unavyozidi kupanuka kwa Watanzania wengi zaidi.



Kwa niaba ya Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO), tunaungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Tanzania Wildlife Management Authority (TAWA), pamoja na wadau wote wa uhifadhi wa mazingira, vyombo vya habari, na watabibu asili nchini kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanyamapori tarehe 03 Machi 2026. Aidha, tunaungana na mataifa mengine duniani kusherehekea siku hii muhimu inayotukumbusha wajibu wetu wa kulinda urithi wa asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Maadhimisho ya mwaka huu yanatukumbusha umuhimu wa kulinda na kutumia kwa busara rasilimali za asili, hususan mimea ya dawa na harufu, ambayo imekuwa nguzo muhimu katika afya ya jamii, ukuaji wa uchumi wa taifa, na ustawi wa binadamu kwa ujumla. Mimea hii si tu hazina ya tiba asilia bali pia ni rasilimali yenye mchango mkubwa katika tafiti za kisayansi, viwanda vya dawa, na maendeleo ya kijamii.
Tanzania imebarikiwa kuwa na bioanuwai adhimu ya wanyamapori, misitu, na vyanzo vya maji. Rasilimali hizi ni urithi wa taifa letu na msingi wa maendeleo endelevu. Hivyo basi, tunapaswa kushirikiana kwa dhati katika:
• Kulinda wanyamapori dhidi ya ujangili na uharibifu wa makazi yao.
• Kuhifadhi mimea ya tiba kwa matumizi endelevu yasiyoharibu mazingira.
• Kulinda vyanzo vya maji na mifumo ya ikolojia kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.
• Kuwezesha jamii kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi na kunufaika nazo kiuchumi.
Tukiongozwa na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025–2050 inayolenga kujenga taifa lenye uchumi imara, amani, utulivu na maendeleo endelevu ya watu wake, tunasisitiza kuwa:
“Uhifadhi wa rasilimali za asili ni msingi wa ustawi wa taifa na kizazi kijacho.”
Kwa pamoja, tushikamane kulinda urithi wetu wa asili, kuenzi thamani ya mimea ya dawa, na kuhakikisha matumizi yake yanafanyika kwa njia endelevu kwa manufaa ya binadamu na mazingira.
TUSHIRIKIANE KWA UHIFADHI, USTAWI NA MAENDELEO ENDELEVU
Imetolewa na: Boniventura Mwalongo
Katibu Mkuu Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO).





















