TRENDING NOW






Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Kampuni ya teknolojia ya kifedha ya Black Swan-Tanzania imeingia kwenye orodha ya kampuni 25 bora zinazochipukia barani Afrika kwa mwaka 2026 iliyotolewa na taasisi kubwa ya habari za fedha duniani, Bloomberg.

Black Swan, kampuni iliyosajiliwa Tanzania na inayojihusisha na huduma za kifedha kupitia teknolojia ya akili mnemba (AI), imetambuliwa kutokana na mchango wake wa kurahisisha upatikanaji wa mikopo nafuu na ya haki kwa Waafrika ambao bado hawajahudumiwa kikamilifu na mifumo rasmi ya kifedha.

Orodha hiyo ya Bloomberg hutambua kampuni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika zinazotatua changamoto muhimu kwa kutumia teknolojia na ubunifu wenye matokeo chanya katika jamii na uchumi.

Kupitia teknolojia yake, Black Swan hubadilisha taarifa za miamala ya kifedha inayofanyika kwenye simu za mkononi kuwa taarifa zinazoweza kusaidia taasisi za fedha kufanya tathmini sahihi za mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara wadogo ambao mara nyingi hawapo kwenye mfumo rasmi wa benki.

Akizungumzia mafanikio hayo, Mwanzilishi Mwenza na Afisa Mkuu Mtendaji wa Black Swan, Derick Kazimoto, alisema kutambuliwa huko ni ishara kuwa dunia inaanza kuona mchango wa kampuni hiyo katika kuboresha ujumuishaji wa kifedha barani Afrika.

“Tunafurahia kuona juhudi zetu zinatambulika kimataifa. Mamilioni ya Watanzania wanafanya kazi na biashara kila siku lakini bado hawaonekani katika mifumo rasmi ya fedha. Tuliianzisha Black Swan kubadilisha hali hiyo,” alisema Kazimoto.

Alisema teknolojia ya kampuni hiyo inachakata taarifa za kifedha kwa usalama na kwa idhini ya watumiaji ili kusaidia wakopeshaji kufanya maamuzi ya haraka, sahihi na yenye uwazi zaidi.

Kwa sasa Black Swan inahudumia zaidi ya taasisi 30 za kifedha Afrika Mashariki katika tathmini za mikopo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo mikopo midogo, mikopo ya kidijitali, ufadhili wa magari na mali nyingine pamoja na huduma za kawaida za mikopo.

Miongoni mwa bidhaa zake kuu ni “Kopa Gari”, mfumo wa kidijitali unaorahisisha upatikanaji wa mikopo ya magari ambapo majibu ya awali ya ustahiki wa mkopo hutolewa ndani ya dakika tano pekee.

Kampuni hiyo pia imeanzisha mfumo wa “Manka”, unaotumia akili mnemba kusaidia wakopeshaji kupata taarifa sahihi kuhusu uwezo wa mkopaji kulipa, hali inayosaidia kuongeza kasi na usahihi wa utoaji wa mikopo.

Kutambuliwa kwa Black Swan kunakuja wakati kampuni changa za teknolojia Afrika zikiendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya bara hilo kutokana na mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa kidijitali.

Kupitia mafanikio hayo, Tanzania imeendelea kujijengea nafasi kwenye ramani ya ubunifu wa teknolojia Afrika sambamba na mataifa kama Nigeria, Kenya, Afrika Kusini na Morocco yaliyowakilishwa katika orodha hiyo ya Bloomberg.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.



Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Jaji Mwambegele pia amewasisistiza watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .

Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.



Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno akizungumza na kusema kua maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
 Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwasilisha nakala za hati za utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026.
 Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwa katika mazungumzo mafupi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, mara baada ya kuwasilisha nakala za hati za utambulisho jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026. Mazungumzo hayo yalihusu uimarishaji wa ushirikiano na uhusiano baina ya nchi hizi mbili.


 


Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Taasisi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya “Kutoa Ni Moyo” yenye lengo la kuchangisha fedha na kuongeza uelewa kwa ajili ya kusaidia watoto wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo nchini.

Kampeni hiyo iliyozinduliwa Mei 25, 2026 jijini Dar es Salaam inalenga kuwaunganisha Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za jamii ili kuwapa watoto wanaozaliwa na matatizo ya moyo nafasi ya kupata matibabu na huduma muhimu za moyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge alisema zaidi ya watoto 16,000 huzaliwa kila mwaka nchini Tanzania wakiwa na matatizo ya moyo, hali inayozifanya familia nyingi kukumbana na changamoto kubwa za kiafya na kifedha.

Alisema takribani watoto 4,000 wanahitaji upasuaji wa moyo kwa haraka, huku akibainisha kuwa kwa familia nyingi muda si suala la fedha pekee bali ni suala la kuokoa maisha.
"Kupitia kampeni ya Kutoa Ni Moyo, tunatoa wito kwa Watanzania wote, taasisi, makampuni binafsi pamoja na taasisi za serikali kuwa sehemu ya harakati hizi za kuokoa maisha ya watoto," alisema Dkt. Kisenge.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa HTAF, Dkt. Naizihijwa Majani alisema kampeni hiyo imekusudia si tu kukusanya fedha, bali pia kujenga uelewa wa muda mrefu kuhusu afya ya moyo na umuhimu wa jamii kushiriki kusaidia.
Alisema Tanzania ina utamaduni mkubwa wa mshikamano na kusaidiana, hivyo kampeni hiyo inalenga kubadili michango midogo ya wananchi kuwa nguvu kubwa ya kitaifa yenye matokeo makubwa.

"Hii si kampeni ya kuchangisha fedha pekee, ni harakati inayojengwa juu ya huruma, umoja na imani kuwa kuokoa maisha ya mtoto ni jukumu la kila mmoja wetu," alisema Dkt. Majani.
Takwimu zinaonyesha kuwa magonjwa ya moyo husababisha vifo vya watu milioni 17.9 duniani kila mwaka, huku mtoto mmoja kati ya watoto 100 akizaliwa akiwa na tatizo la moyo.

Kampeni hiyo inalenga kukusanya shilingi bilioni 25 kupitia michango ya wananchi, makampuni, wadau wa maendeleo, taasisi mbalimbali, Watanzania waishio nje ya nchi, watu maarufu, jumuiya za michezo na jamii kwa ujumla.
Fedha zitakazokusanywa zitatumika kugharamia upasuaji na matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, uchunguzi wa mapema, programu za elimu ya afya ya moyo pamoja na kusaidia familia zinazokabiliwa na changamoto hiyo.

Aidha, kampeni hiyo itatumia mifumo ya kidijitali na majukwaa ya uchangishaji mtandaoni ili kurahisisha Watanzania kuchangia kwa uwazi na urahisi kutoka ndani na nje ya nchi.

Taarifa zinaonyesha kuwa juhudi za awali za uchangishaji tayari zimefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 3.08 kupitia fedha taslimu na misaada ya vifaa mbalimbali.

Na Mwandishi Wetu. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na maendeleo ya taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma.

“Tukitazama baadhi ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni, mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika jamii ya Watanzania,” amesema.

Amesisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na yanalinda maslahi ya taifa.

“Tunachosimamia ni kuhakikisha Mwandishi wa Habari anayepata ithibati anakuwa na kiwango cha elimu kisichopungua Diploma, lakini tunataka pia Waandishi wa Habari waendelee kupata mafunzo ili waweze kuimarika zaidi kitaaluma,” amesema.

Amesema ipo haja ya sekta ya habari kutafakari aina ya maudhui yanayopewa kipaumbele, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kujenga fikra na mwelekeo wa jamii.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Rabia Hussein Mohamed kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Immaculata Kajetan Banzi kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Cyprian Phocas Mkeha kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Yohane Bokobora Masara kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Juliana Laurent Masabo kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Abdi Shaaban Kagomba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Majaji 9 wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha na Majaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.
Na Mwandishi Wetu, Michuzi Tv

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Mariam Ibrahim amemshuru Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa , Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kupendekeza jina lake na Kamati Kuu ya chama hicho kulipitisha na hatimaye kushinda kwa kura nyingi.

Ametoa shukrani hizo kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Dk.Samia Suluhu Hassan alipokuwa akisalimia viongozi mbalimbali wa Chama hicho wakati wa Semina ya Uongozi na Maendeleo kwa madiwani wote wanawake  wa Mkoa wa Pwani.

“Nitumie nafasi hii kwa dhati ya moyo wangu kumshukuru Mwenyekiti wetu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kunipendekeza mimi na Kamati Kuu kurudisha jina langu na kuja katika Mkoa wa Pwani na kupigiwa kura nyingi.

“Waheshimiwa madiwani hatujaonana toka Uchaguzi mkuu ulivyopita hivyo naomba kuchukua fursa hii kuwashukuru nyote kwa kura zenu za kishindo.Nasema ahsanteni sana,amesema mbele ya madiwani hao pamoja na viongozi wa Mkoa huo.
 
Amesisitiza ameamua kutoa shukrani hizo kwasababu ndio mara yake ya kwanza wanakutana ambapo ametumia nafasi hiyo pia kuwaaahidi kuendelea kushirikiana nao na yupo tayari kwa wakati wowote ambao atahitahika.“Tutakuwa pamoja katika kila hali.”