TRENDING NOW






Na Mwandishi Wetu

Zaidi ya mastaa na watengeneza maudhui 30 wamesafirishwa kwa ndege binafsi kutoka Dar es Salaam hadi Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kushiriki uzinduzi wa kinywaji kipya cha Serengeti Premium Apple, kilichoelezwa kuwa cha kwanza cha aina ya premium (RTD) kutengenezwa nchini Tanzania na kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL).

Uzinduzi huo wa siku tatu mfululizo umefanyika kwa mtindo wa kipekee uliolenga kuunganisha burudani, ubunifu, utalii pamoja na ladha mpya ya kinywaji hicho.
Safari hiyo ilianza kwa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kabla ya wageni hao kusafirishwa kwa ndege binafsi hadi Serengeti, ambako walipokelewa kwa hafla maalumu ndani ya hifadhi hiyo maarufu duniani.

Wakiwa Serengeti, mastaa hao walipata nafasi ya kutembelea vivutio vya utalii, kushiriki chakula cha mchana na jioni katika mazingira ya kuvutia, sambamba na burudani mbalimbali zilizopangwa kwa ustadi.

Katika siku iliyofuata, wageni hao walishiriki tukio maalumu la “Toast in the Sky”, lililofanyika angani kupitia puto maalumu la moto (hot air balloon), tukio lililoibua hisia na kuvutia wengi.

Kwa mujibu wa waandaaji, uzinduzi huo umeakisi misingi ya chapa mpya ya Serengeti Premium Apple ikiwemo ladha laini na ya kuburudisha ya apple, ubunifu wa Kitanzania, maisha ya kisasa pamoja na mafanikio ya Mtanzania wa leo.

Aidha, kampuni ya Serengeti Breweries Limited imesema uzinduzi huo unaonyesha uwezo wa Tanzania kuzalisha bidhaa zinazokidhi viwango vya kimataifa huku ikitumia vivutio vya ndani kuitangaza nchi na ubunifu wake.

Uzinduzi huo umevutia hisia za wengi huku ukiweka historia mpya katika sekta ya vinywaji na burudani nchini.

Na Mwandishi Wetu

Wadau wa sekta ya usafiri wa majini katika mikoa ya Mwanza, Kigoma na Kagera arehe 16 Aprili, 2026 wamejitokeza na kutoa maoni yao kuhusu athari za ongezeko la bei ya mafuta, wakisisitiza umuhimu wa kuchukua hatua stahiki zitakazolinda maslahi ya wananchi pamoja na uendelevu wa huduma hiyo.

Wakizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), maafisa waratibu wa vikao hivyo, wamesema kuwa vikao hivyo vimeandaliwa kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wowote kuhusu marekebisho ya nauli za usafiri wa majini.

Wameongeza kuwa vikao hivyo vimeitishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 29 cha Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415, kinachoitakaTASAC kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupata maoni katika michakato mbalimbali inayohitaji maoni ya wadau.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika mkoani Kagera, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) wa Mkoa wa Kagera, Bw. Isaya Tendega, ameipongeza TASAC kwa kuandaa vikao hivyo ambavyo vimefanyika katika wakati muafaka kufuatia mabadiliko ya bei ya mafuta yaliyoanza kutumika hivi karibuni, hali inayoweza kuongeza gharama za uendeshaji wa vyombo vya usafiri majini na kuathiri maisha ya wananchi.
Baadhi ya wadau walioshiriki mkutano huo walieleza kuwa ni muhimu kwa mamlaka husika kuzingatia uwiano kati ya gharama za uendeshaji na uwezo wa wananchi kumudu nauli ili kuepusha kuwaongezea mzigo wananchi, hususan wale wanaotegemea usafiri wa majini kwa shughuli zao za kila siku.

Aidha, wadau wengine walipendekeza kuwepo kwa mikakati mbadala ya kupunguza gharama za uendeshaji, ikiwemo matumizi ya nishati mbadala na kuboresha ufanisi wa vyombo vya usafiri, badala ya kutegemea zaidi ongezeko la nauli.

TASAC imebainisha kuwa itaendelea kupokea maoni hadi tarehe 26 Aprili, 2026 kabla ya kukamilisha mchakato wa kufanya maamuzi ambao utakuwa shirikishi na wa uwazi, ukizingatia maoni ya wadau wote pamoja na hali halisi ya soko.
Na Mwandishi Wetu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula , amesema uandishi wa habari usiozingatia maadili unaweza kuhatarisha umoja wa kitaifa, amani na utulivu wa jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari  ambao ni wanachama wa JUMIKITA, TADIO na TBN, leo Ijumaa Aprili 17, 2026 jijini Dar es Salaam, Kipangula alisema waandishi wa habari wanapaswa kutambua uzito wa nafasi yao katika jamii, hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, ambapo taarifa wanazozitoa zina athari kubwa kwa mwenendo wa jamii.

Alifafanua kuwa amani ni hali ya kutokuwepo kwa migogoro au vurugu, huku utulivu ukimaanisha usalama na uhakika wa maisha ya wananchi bila hofu, akibainisha kuwa hali hizi mbili haziwezi kudumu bila uwepo wa umoja wa kitaifa unaojengwa juu ya mshikamano wa wananchi bila kujali tofauti zao.
“Pale ambapo uandishi hauzingatii maadili, unaweza kuchochea migawanyiko, kupotosha ukweli na hatimaye kuvuruga mshikamano wa kitaifa. Hivyo, ni muhimu kwa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji,” alisema Kipangula.

Alibainisha kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa msingi wa kukusanya, kuchakata na kusambaza taarifa sahihi, pamoja na kusaidia kuunda mitazamo ya wananchi kwa njia inayochangia maridhiano na maendeleo ya jamii.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Taaluma ya Uandishi wa Habari, akibainisha kuwa maadili hayo yanahimiza ukweli, usawa, uwazi na heshima kwa haki za binadamu, mambo ambayo ni msingi wa kulinda amani, kuimarisha utulivu na kukuza umoja wa kitaifa.
Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) limetoa limesisitiza kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda urithi wa mila, utamaduni, tiba asili na mazingira kama nguzo muhimu ya maendeleo endelevu ya Taifa.

TRAMEPRO inasisitiza kuwa maeneo ya mila, maarifa ya tiba asili, pamoja na mifumo ya jadi ya uhifadhi wa mazingira ni sehemu muhimu ya utambulisho wa jamii zetu. Taarifa iliyotolewa leo Aprili 17, 2026 kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) Boniventura Mwalongo,

amesema kumekuwepo na changamoto za uvamizi wa maeneo ya mila, mabadiliko holela ya matumizi ya ardhi, pamoja na kuongezeka kwa upotoshaji wa dhana ya tiba asili.

“Mwito kwa Wazee na Machifu wa Mila

TRAMEPRO inatoa wito kwa viongozi wa mila kuendelea kusimamia kwa uaminifu maeneo ya jadi, kulinda urithi wa mababu, na kuendeleza maarifa ya tiba asili. Ushirikiano na Serikali na taasisi husika ni muhimu katika kuhakikisha amani na mshikamano wa kijamii unadumishwa.

Wito kwa Jamii kwa Ujumla

“Wananchi wote wanahimizwa kuthamini urithi wa kitamaduni, kuachana na imani potofu zinazokwamisha maendeleo, na kuzingatia sheria na miongozo rasmi. Umoja na uwajibikaji ni msingi wa ustawi wa Taifa.”

Aidha ametoa ombi kwa Serikali na Wadau wa Maendeleo kuviwezesha na kuviimarisha vikundi vinavyoendeleza tiba asili, utamaduni na uhifadhi wa mazingira, Kuimarisha ushirikiano wa tafiti kati ya taasisi za ndani na za kimataifa na Kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria za ardhi na utamaduni

Pia kuchukua hatua dhidi ya vitendo vinavyosababisha migogoro ya kijamii na uvunjifu wa amani.

“Nukuu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Kuhusu Mazingira na Utamaduni

“Tunapaswa kuthamini na kulinda mila zetu njema pamoja na mazingira yetu, kwa sababu hayo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu ya Taifa letu.”

“Pia Shirika linamkumbuka kiongozi mashuhuri wa dunia, Benjamin Franklin, aliyezaliwa tarehe 17 Aprili 1706. Alikuwa mfano wa maarifa, ubunifu na maadili mema, akisisitiza umuhimu wa elimu, nidhamu na hekima katika kujenga jamii imara,” amesema Mwalongo,

Aidha amesema TRAMEPRO inawahimiza wananchi wote kushirikiana katika kulinda urithi wa utamaduni, kuendeleza tiba asili kwa misingi ya sayansi na teknolojia, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa - Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid, amefanya Kikao kazi na Kansela wa Chama Cha Kikomunisti (CPC), Ubalozi wa China nchini Tanzania Ndg. Xu Sujiang leo tarehe 16.04.2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Lengo la kikao hicho ni kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha uhusiano na itikadi za vyama hivyo.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wadau wa Sekta ya Afya pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kufungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wadau wa Sekta ya Afya pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kufungua Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima ya Kibinadamu ya Upasuaji wa Ubongo kutoka kwa Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Tanzania (TNS) Dkt. Othman Kiloloma kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima ya Kibinadamu ya Upasuaji wa Ubongo kutoka kwa Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu Tanzania (TNS) Dkt. Othman Kiloloma kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Wafanyakazi wa Sekta ya Afya wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.
Wadau wa Sekta ya Afya wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Shirikisho la Dunia la Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu (WFNS) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 16 Aprili, 2026.