TRENDING NOW







Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Katika kikao hicho kilichifanyika leo Juni 2, 2026 ambapo wajumbe wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa viwango vya kazi, ikiwemo mjadala wa jumla kuhusu ripoti kuu ya Kamati ya Mkutano na maadhimisho ya miaka 100 ya ajenda ya Kazi zenye Staha, Tathmini ya Jumla, pamoja na wajibu wa nchi wanachama katika kuwasilisha taarifa na kutekeleza majukumu mengine yanayohusiana na viwango vya kazi.


Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho ulijumuisha Jaji wa Mahakama ya Rufani Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Kazini, Suzan Mkangwa, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Khadija Mwenda, pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Usekelege Mpulla

Tanzania, ambayo ni mwanachama wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) na mjumbe wa Bodi ya Magavana inayowakilisha nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, inaendelea kushiriki Mkutano Mkuu wa 114 wa shirika hilo unaowakutanisha wawakilishi wa Serikali, Waajiri na Wafanyakazi kutoka nchi wanachama 187.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.
 
Na Albano Midelo

Wakati wengi walidhani ajali ilizika ndoto zake milele, Deogratius Chami ameandika historia mpya Tanzania kwa kuwa mtu wa kwanza mwenye ulemavu wa kutumia kiti mwendo kufika kilele cha Mlima Kilimanjaro (Uhuru Peak, mita 5,895).

Chami, mzaliwa wa Moshi ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi wa Kilimanjaro Disability Royour Tour and Safaris, alifikia mafanikio ya kupanda mlima Kilimanjaro baada ya safari ya siku saba mwaka 2014, na kurudia tena mwaka 2023 kwa siku sita pekee.

Mrajisi wa Ushirika Mkoa wa Ruvuma Venance Msafiri akizungumza siku ya maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani ambayo yalifanyika wilayani Nyasa mkoani Ruvuma,amesema ushirika umechangia mafanikio ya mwenye ulemavu huyo baada ya kumpatia mkopo wa maendeleo wa shilingi milioni nane mwaka 2023, hivyo kufanikiwa kuanzisha kampuni hiyo ya utalii..

Amesema Kupitia kampuni hiyo Chami sio tu anautangaza utalii,bali pia anautangaza ushirika na kwamba wanatarajia kumualika mkoani Ruvuma ili aweze kuja kutembelea vivutio vya Mkoa wa Ruvuma hususani wilaya ya Nyasa ambayo ni kitovu cha utalii katika Mkoa.

Akiwa na miaka 13 darasa la sita shule ya msingi Kilimanjaro,Chami alipata ajali mbaya ilimlaza kwa karibu miaka miwili katika Hospitali ya KCMC Moshi. Ndoto zake za kuwa mwanajeshi na mchezaji wa mpira zilionekana kufutika.

Hata hivyo, ushauri wa mwalimu wake wa shule ya msingi ulimgeuza kutoka nafasi ya 129 darasani hadi kuwa miongoni mwa wanafunzi bora, hatua iliyomfikisha hadi Shahada ya Maendeleo ya Jamii na Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mwaka 2013.

Kwa mujibu wa WHO (2023), watu bilioni 1.3 duniani wanaishi na ulemavu, sawa na asilimia 16 ya idadi ya watu wote. Chami amethibitisha kuwa ulemavu si mwisho wa mafanikio bali mwanzo wa njia mpya ya ushindi.


Picha mbalimbali za Deogratias Chami mtanzania wa kwanza mwenye ulemavu kupanda mlima kilimanjaro hadi kileleni  kwa kutumia kiti mwendo ,Chami amepanda mlima kilimanjaro mara mbili mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2014 ambapo alitumia siku saba kufikia kileleni na mara ya pili mwaka 2023  akiwa na kampuni yake ya utalii alifanikiwa kupanda mlima kilimanjaro kwa kutumia siku sita hadi kileleni.
Wananchi wa Kijiji cha Mkungugu jimbo la Ismani katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mkoani Iringa wakiwa katika foleni ya kupiga kura ya kumchagua Mbunge wao katuika uchaguzi mdogo uliyofanyika leo Juni 01, 2026.
Mwananchi Mkazi wa wa Kijiji cha Kihongorota katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mkoani Iringa, Angelista Mwenda akipiga kura katika uchaguzi mdogo wa Ubunge jimbo la Ismani uliofanyika leo Juni 01, 2026.
Mwananchi Mkazi wa wa Kijiji cha Kihongorota katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mkoani Iringa, Angelista Mwenda akipiga kura katika uchaguzi mdogo wa Ubunge jimbo la Ismani uliofanyika leo Juni 01, 2026.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akipita kuingia katika kituo cha Kura cha Ofisi ya Kijiji Mtera katika jimbo la Ismani Wilaya ya Iringa mkoani Iringa kukagua mwenendo wa zoezi la kupiga kura kwa wananchi wa Ismani lililofanyika leo Juni 01, 2026.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na Mawakala katika moja ya vituo alivyotembelea.
MWENYEKITI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amesema zoezi la upigaji Kura wa Ubunge katika jimbo la Isman katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara limekwenda vizuri.

Mwenyekiti huyo wa Tume Jaji Mwambegele amesema hayo leo Juni 01,2026 akiwa katika ofisi za Kijiji Igingilanyi Wilayani Iringa mara baada ya kutembelea na kukagua zoezi la upigaji Kura linavyoendelea katika vituo vya kupigia Kura vya jimbo la Isimani ambako kunafanyika uchaguzi mdogo wa ubunge.

Amesema mwitikio wa wananchi wa Ismani katika kujitokeza kupiga kura umekua mkubwa na hata katika Kata nyingine 12 ambazo nazo zinachagua Madiwani hii leo wamejitokeza kwa Wingi.

Mwenyekiti huyo wa Tume Jaji Mwambegele ameshudia upigaji kura kwa baadhi yavituo vilivyopo katika vijiji vya Igingilanyi, Mkungugu, Kihongorota na Migori.

Kata 12 zilofanya uchaguzi leo ni Mzimuni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji Kasulu.

Nyingine ni Kata ya Kala iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mwenendo wa zoezi la kupiga kura kwa wananchi wa Jimbo la Ismani lililopo Halmashauri ya Iringa mkoani Iringa hii leo Juni 01,2026.


Wananchi wakiwa katika mistari tayari kuingia vituoni kupiga Kura.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mwenendo wa zoezi la kupiga kura kwa wananchi wa Jimbo la Ismani lililopo Halmashauri ya Iringa mkoani Iringa hii leo Juni 01,2026.

Wananchi wakiwa katika mistari tayari kuingia vituoni kupiga Kura.
Na Mwandishi wetu, Iringa.

Wapiga Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani lililopo Halamashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Mei 31, 2026 Mkoani Iringa wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Juni 01, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 628 vya Kupigia Kura vitatumika.

“wapiga kura 89,753 wapo kwenye Jimbo la Ismani na wapiga kura 132,465 wapo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo na vituo 277 vipo kwenye Jimbo la Ismani na vituo 351 vipo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo.,”amesema Jaji Mwambegele.

Aidha, amesema Katika Uchaguzi huu, jumla ya wagombea 108 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi ya ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja.

“Jimbo la Ismani lina wagombea 17 wa nafasi ya Ubunge ambapo kati ya wagombea hao wagombea nane (08) sawa na asilimia 47.06 ni wanaume na wagombea tisa (09) sawa na asilimia 52.94 ni wanawake. Kata 12 zinazofanya uchaguzi mdogo wa udiwani zina jumla ya wagombea 91 ambapo kati ya hao wagombea 61 sawa na asilimia 67.03 ni wanaume na wagombea 30 sawa na asilimia 32.97 ni wanawake.” alisema Jaji Mwambegele.

“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Juni 01, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.

Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.

Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.

“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.

Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

Kata 12 zitakazo fanya uchaguzi ni Mzimuni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji Kasulu. 

Nyingine ni Kata ya Kala iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.


Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari watakaoshiriki Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo (Samia Kalamu Awards - SKA) 2026 wamelazimika kukidhi sharti la kuwa na ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), hatua inayolenga kuimarisha weledi, uwajibikaji na ushindani wa haki katika taaluma hiyo.

Akizindua rasmi mchakato wa kupokea kazi za kushindanishwa, Jumapili Tarehe 31 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SKA, Mha. Peter Mwasalyanda, amesema maandalizi ya mwaka huu yanazingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kutambua mchango wa Waandishi wa Habari za maendeleo nchini.
Mwasalyanda amesema ili kuhakikisha uadilifu, uwazi na ushindani wa haki, maandalizi ya tuzo hizo yanahusisha pia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kama mdau muhimu katika kusimamia weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

“Tuzo hizi zinalenga kutambua, kuthamini na kuhamasisha uzalishaji wa maudhui ya ndani yenye ubora, yanayochangia kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, na kuimarisha taswira chanya ya Taifa kupitia habari za maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema tofauti na msimu wa kwanza wa tuzo hizo, mwaka huu washiriki wanapaswa kuhakikisha wamekidhi sharti la ithibati.

“Mtakumbuka Msimu wa kwanza wa Samia Kalamu mambo ya JAB hayakuwepo, kwa hiyo waandishi walishiriki wote bila kujali vigezo vya Ithibati lakini mwaka huu kuna hiki kigezo cha kuwa na ithibati kwa hiyo niwashauri basi wote wanaoshiriki kwenye hizi tuzo wahakikishe wanakuwa na ithibati, wamethibitishwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.” Amesema Wakili Kipangula na kuongeza;
“Ni muhimu sana kwa sababu ni takwa la kisheria na kitu ambacho hatuwezi kukikwepa. Nawahamasisha tushiriki wote kwa sababu isionekane ni tuzo za watu fulani tu, kila mmoja awasilishe kazi zake,” amesema Kipangula.

Kwa mujibu wa vigezo vya ushiriki vilivyotangazwa, Waandishi wa Habari wa Tanzania Bara wanatakiwa kuwa wamethibitishwa na JAB, huku kwa Zanzibar washiriki wakitakiwa kuwa na kitambulisho cha Mwandishi wa Habari (Press Card).

Tuzo hizo zimeanza kupokea kazi kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2026 na zinatarajiwa kutolewa kati ya Oktoba na Desemba mwaka huu.


Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakifanya usafi katika eneo la soko hilo wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho Siku ya Mazingira Duniani, 2026.

Watumishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sheila Kikula (wa pili kutoka kushoto) na Bw. Lucas Sebida (wa pili kutoka kulia) wakiungana na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 kufanya usafi katika eneo hilo wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana (kulia) akiwa na vitendea kazi mbalimbali kwa ajili ya kuanza zoezi la usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji hilo wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amewataka Maafisa Mazingira kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wanaokiuka Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa kutupa taka ovyo ndani ya mifereji ya maji taka katika Soko Kuu la Jiji hilo.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo Mei 30, 2026 wakati alipoongoza viongozi, watendaji na wananchi Mkoa huo katika zoezi la usafi wa mazingira katika eneo la Soko Kuu la Jiji hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho kuelekea Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.

Amesema baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wamejenga mazoea ya kutupa taka ovyo katika mifereji ya maji taka katika Soko hilo hali inayochangia kukithiri kwa uchafu na hivyo kuchochea kasi ya uharibifu wa mazingira.

“Natoa maelekezo kwa maafisa mazingira wa jiji na meneja wa soko kuhakikisha kunakuwa na utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usafi wa mazingira katika Soko hili na kila anayekiuka sheria hakikisheni anatozwa faini” amesema Mtanda.

Aidha Mhe. Mtanda amesema faini hizo zitakazolipwa na wafanyabiashara hao zitatumika katika kulipa gharama za huduma ya usafi inayotolewa na Halmashauri ya Jiji na hivyo kuhimiza watumiaji wa soko kuzingatia taratibu za usafi ili kulinda mazingira.

Mhe. Mtanda pia amewalekeza maafisa mazingira kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa wafanyabiashara waliopo ndani ya soko ili kuhakikisha wanatekeleza maelekezo, miongozo na ya sheria zilizopo ili huduma za soko hilo ziendelee kuwa endelevu kwa wananchi.

Amesema suala la usafi ni ustaarabu, hivyo ni wajibu wa jamii inayozunguka katika eneo hilo kuhakikisha wanajenga utamaduni wa kupenda na kuthamini usafi wa mazingira yanayowazunguka ili kulinda afya za watumiaji wa bidhaa na huduma zinazopatikana ndani soko hilo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amewataka wananchi wa Mkoa huo kujenga utamaduni wa kupanda miti katika maeneo yao kwani kwa kufanya ni kutekeleza amri na maelekezo ya mwenyezi mungu aliyoyatoa katika vitabu takatifu.

Awali akitoa taarifa ya tathimini ya hali ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Afisa Mazingira wa Jiji hilo, Bw. Daudi Joseph amesema katika mwaka 2025/2026 Jiji hilo limefanikiwa kupanda miti 768,476 ambapo miti 176,750 imepandwa na wananchi na wadau wa mazingira.

Ameongeza pia katika kuchagiza suala la utunzaji na uhifadhi wa mazingira, Jiji hilo limeanzisha na kutekeleza kampeni mbalimbali ikiwemo Tunza Mazingira Ng’arisha Nyamagana na kusimamia shughuli za usafi wa mazingira kwa kushirikiana na viongozi wa Jiji hilo.

“Wilaya ya Nyamagana inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kushirikiana na wadau ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira katika Kata zote 18” amesema Joseph.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Afisa Misitu Mwandamizi Bw. Lucas Sabida ameupongeza Mkoa wa Mwanza kwa juhudi mbalimbali inazoendelea kuzifanya katika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kutunza mazingira.

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa timu ya wataalamu wa Mazingira ya Mkoa huo na kuufanya kuwa ni miongoni mwa Mkoa ya mfano katika uhamasishaji wa jamii kuhusu umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira.

Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, 2026 yatafanyika Kitaifa Mkoani Dodoma yakiwa na kauli mbiu isemayo Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana (kushoto) akiwa na Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Sheila Kikula (katikati) wakifanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani Mei 30, 2026 ikiwa ni maandalizi kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (Katikati-traki suti nyekundu) akiongoza viongozi na watendaji Mkoani humo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza viongozi na watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 katika zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiwa pamoja na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo wakikagua maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Jiji la Mwanza wakati wa zoezi la usafi wa eneo hilo Mei 30, 2026 kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026. Katikati ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amiri Mkalipa.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo wakikagua maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa eneo hilo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026. Kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana, Bw. Thomas Salala.




Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga, Mhe. Emmanuel Cherehani akinywa maziwa kwenye Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mei 31, 2026 katika Viwanja vya Mwembe Togwa, mjini Iringa.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga, Mhe. Emmanuel Cherehani akinywa maziwa kwenye Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mei 31, 2026 katika Viwanja vya Mwembe Togwa, mjini Iringa.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga, Mhe. Emmanuel Cherehani akinywa maziwa kwenye Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mei 31, 2026 katika Viwanja vya Mwembe Togwa, mjini Iringa.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga, Mhe. Emmanuel Cherehani, ameshiriki ufunguzi wa Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa yaliyofanyika leo Mei 31, 2026 katika Viwanja vya Mwembe Togwa, mjini Iringa.

Mgeni rasmi katika ufunguzi huo alikuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb), ambaye amefungua rasmi maadhimisho hayo yanayolenga kuhamasisha maendeleo ya sekta ya maziwa nchini kupitia uzalishaji, uchakataji na biashara ya maziwa yenye tija kwa wafugaji na taifa kwa ujumla.

Mhe. Cherehani ameshiriki hafla hiyo akiwa pamoja na wajumbe wengine wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ambao wamepata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho na kujionea shughuli zinazofanywa na wadau wa sekta ya maziwa kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa mwaka 2026 yanafanyika mkoani Iringa pamoja na maeneo mengine ya nchi yakiongozwa na kaulimbiu isemayo, "Rasimisha Biashara ya Maziwa, Okoa Maisha ya Walaji, Ongeza Kipato, Changia Uchumi."

Kaulimbiu hiyo inalenga kuhamasisha urasimishaji wa biashara ya maziwa ili kuhakikisha usalama wa walaji, kuongeza kipato kwa wafugaji na wafanyabiashara wa maziwa, pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia sekta ya mifugo.

Maadhimisho hayo yamewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya maziwa wakiwemo wafugaji, wasindikaji wa maziwa, wafanyabiashara, taasisi za serikali na binafsi pamoja na washirika wa maendeleo kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kuonesha teknolojia za kisasa na kujadili fursa zilizopo katika kuendeleza sekta ya maziwa nchini.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akizungumza wakati wa Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa yanayofanyika mkoani Iringa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akizungumza wakati wa Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa yanayofanyika mkoani Iringa.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga, Mhe. Emmanuel Cherehani akiwasalimia washiriki wa Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mei 31, 2026 katika Viwanja vya Mwembe Togwa, mjini Iringa.