TRAMEPRO imetoa mwito huo leo Julai 18,2026 katika kukimbizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela aliyekuwa Rais wa nchi ya Afrika Kusini.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu TRAMEPRO Tanzania Boniventura Mwalongo amesema wanaungana na mataifa ya Afrika na dunia kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela mmoja wa viongozi mashuhuri waliobadilisha historia ya dunia kwa kupigania uhuru, usawa, haki za binadamu na maridhiano.
Pia amesema mambo ya kujifunza kupitia kutoka kwa Nelson Mandela ni kwamba elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ya kubadilisha dunia, msamaha ni nguvu, si udhaifu; hujenga taifa lenye umoja.
Mengine ni uvumilivu na subira vinaweza kushinda hata changamoto kubwa, Uongozi ni huduma, si nafasi ya kutawala wengine, haki na usawa ni msingi wa maendeleo endelevu.
"Mandela anatufundisha pia umoja wa Waafrika na kuheshimiana ni nguzo ya maendeleo ya bara letu. Afya, mazingira na maendeleo vinapaswa kwenda pamoja kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, " amesema Mwalongo.
Akieleza zaidi amesema kwa waratibu asili Asili,TRAMEPRO Tanzania inaona mafunzo makubwa kutoka kwa Mandela katika kujenga umoja wa sekta, kuzingatia maadili ya taaluma, kuendeleza utafiti, kuhifadhi mimea tiba, kulinda mazingira na kushirikiana na taasisi za kisayansi ili tiba asili ichangie kikamilifu afya na maendeleo ya jamii.
Kuhusu historia ya Nelson Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji cha Mvezo, Mkoa wa Eastern Cape, Afrika Kusini. Jina lake la asili, Rolihlahla, katika lugha ya Kixhosa humaanisha mtu anayetikisa tawi la mti, na kwa maana ya kawaida huashiria mtu mwenye kuhoji au kupinga hali iliyopo.
Alipoanza shule ya msingi, mwalimu wake alimpa jina la Nelson, kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo katika shule nyingi za kikoloni.
Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme ya kabila la Thembu. Baba yake aliitwa Gadla Henry Mphakanyiswa Mandela, aliyekuwa mshauri wa mfalme wa Thembu, na mama yake aliitwa Nosekeni Fanny Mandela.
Kutoka kwa wazazi wake alijifunza heshima, uwajibikaji, uongozi na umuhimu wa kuitumikia jamii.
Katika elimu, Mandela alianza masomo katika shule za wamisionari, akaendelea katika Chuo cha Healdtown, kisha akasoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare.
Baadaye alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, ambako alijiandaa kuwa mwanasheria na mtetezi wa haki za wanyonge. Elimu yake ilimpa msingi wa kuelewa sheria na kuitumia kutetea usawa na utu wa binadamu.
Mandela aliongoza mapambano dhidi ya mfumo wa ubaguzi wa rangi (Apartheid). Kutokana na msimamo wake, alifungwa gerezani kwa miaka 27, lakini hakukata tamaa wala kuacha kuamini kuwa amani na maridhiano vinaweza kushinda chuki. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990, aliongoza mazungumzo yaliyoweka msingi wa Afrika Kusini mpya yenye demokrasia.
Mwaka 1994, Nelson Mandela aliingia katika historia kwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini aliyechaguliwa kidemokrasia. Uongozi wake ulijengwa juu ya maridhiano, msamaha na umoja wa kitaifa. Mwaka 1993, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mchango wake katika kumaliza Apartheid kwa njia ya amani.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yatakayofanyika katika Uwanja wa Gofu wa Lugalo kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kufungua fursa mpya kwa wateja, washirika na wadau wa sekta mbalimbali.
Mashindano hayo, yanayoandaliwa kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited kupitia kitengo cha Vodacom Business, yatawakutanisha viongozi wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu wa sekta mbalimbali na wapenzi wa mchezo wa gofu kwa lengo la kujenga mitandao ya biashara na kubadilishana uzoefu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania PLC, Joseph Sayi, alisema kampuni hiyo imeendelea kudhamini mashindano hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo kwa kuwa yanaendana na dhamira ya kuimarisha mahusiano ya muda mrefu na jumuiya ya wafanyabiashara.
Alisema mashindano hayo si ya michezo pekee, bali ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujadili fursa mpya za uwekezaji na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.
Sayi alisema katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho mbalimbali za kidijitali ikiwemo huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi, kukuza biashara na kuimarisha ushindani.

Mashindano hayo yatashirikisha timu 10 za makampuni zitakazowania taji la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na maonesho ya biashara, burudani, maonesho ya vitu vya kale na eneo maalumu la watoto, hatua inayolenga kuwafanya washiriki na familia zao kufurahia tukio hilo katika mazingira rafiki.







.jpeg)

.jpeg)

















































