

The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.
"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.
“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima
Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.
“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.
DAR
ES SALAAM, Tanzania – Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania,
Manzi Rwegasira, atajumuika na viongozi wa kimataifa, mawaziri, watunga
sera, wawekezaji, taasisi za fedha za maendeleo pamoja na viongozi wa
biashara katika Mkutano wa Infra for Africa Forum 2026, unaofanyika
jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 5 hadi 6 Agosti 2026.
Mkutano huo, ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Africa50, utawakutanisha wadau muhimu kujadili mbinu bunifu za kuharakisha maendeleo na uwekezaji katika miundombinu barani Afrika, huku Mgeni Rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Tarehe 5 Agosti, Rwegasira atashiriki katika mjadala wa ngazi ya juu wenye mada “Reinvesting for Expansion: Asset Recycling as a Multiplier”, akiwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Nishati na Miundombinu Duniani wa Standard Bank Group, Dele Kuti, na viongozi wengine waandamizi. Katika mjadala huo atazungumzia ugharamiaji wa miundombinu, uhamasishaji wa mitaji na ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuharakisha uwekezaji katika miundombinu barani Afrika.
Tarehe 6 Agosti, pia atazungumza katika kikao cha jumla chenye mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led”, sambamba na viongozi waandamizi kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ecobank, ATIDI na Mfuko wa Uwekezaji wa Taifa wa Angola. Kikao hicho kitachambua namna taasisi za fedha za Afrika, wawekezaji wa kitaifa, benki na wadau wa miundombinu wanavyoweza kuhamasisha mitaji ya ndani, kuimarisha mifumo ya kupunguza hatari na kuharakisha ugharamiaji wa miundombinu kupitia suluhu zinazoongozwa na Waafrika.
Stanbic Bank Tanzania inaeleza kuwa maendeleo ya miundombinu yanaendelea kuwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi, mtangamano wa kikanda na ustawi wa muda mrefu, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo endelevu kupitia suluhu bunifu za kifedha na ushirikiano wa kimkakati unaochochea ajenda ya maendeleo ya Tanzania na ukuaji wa Afrika.
AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw. Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026
Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam. Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Benki ya Exim Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wamezindua rasmi Programu ya YST 2026, wakiahidi kuendelea kuwawezesha vijana wabunifu kupitia sayansi, teknolojia, utafiti na ubunifu.
Uzinduzi huo uliofanyika Julai 31, 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim (Exim Tower), Dar es Salaam, umeadhimisha miaka sita ya ushirikiano kati ya taasisi hizo katika kukuza vipaji vya wanafunzi wa shule za sekondari nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D'Souza, alisema benki hiyo inaamini kuwa uwekezaji kwa vijana ni msingi wa kujenga taifa lenye ushindani na maendeleo endelevu.
Alisema kupitia falsafa ya benki hiyo ya *"Ubunifu ni Maisha"*, Exim imeendelea kuwaunga mkono wanafunzi wenye vipaji vya ubunifu na kuwapa fursa ya kutumia sayansi na utafiti kutatua changamoto zinazozikabili jamii.
Kwa mujibu wa D'Souza, programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya baada ya kupokea miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya tathmini ya kitaalamu, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia yatakayofanyika Septemba 17, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Alieleza kuwa wataalamu wa benki hiyo wamekuwa wakishiriki moja kwa moja katika kutembelea shule, kutoa ushauri wa kitaalamu kwa walimu na wanafunzi pamoja na kusaidia kuboresha tafiti na miradi ya ubunifu.
Hata hivyo, Dkt. Kamugisha alisema YST bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa rasilimali fedha na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.
Alisisitiza kuwa maendeleo ya taifa hayawezi kufikiwa bila uwekezaji wa kutosha katika sayansi, teknolojia na ubunifu wa vijana, akibainisha kuwa mataifa yaliyopiga hatua yamefanikiwa kutokana na kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika tafiti na ugunduzi.
Kwa zaidi ya miaka 16, YST imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu, huku ushirikiano wake na Benki ya Exim ukiendelea kusaidia vijana kubuni suluhisho katika maeneo mbalimbali ikiwemo akili unde (AI), kilimo, afya, uhifadhi wa mazingira, usalama wa chakula na teknolojia za mawasiliano.

Ataka Uwekezaji wenye Tija
Na Mwandishi Wetu - Dar eś Salaam
Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imeelekezwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali ili kuhakikisha mfuko unaendelea kuwa imara, endelevu na wenye uwezo wa kutoa huduma bora kwa wanachama.
Amesema hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mfuko huo wa PSSSF iliyofanyika leo Agosti 1, 2026, PSSSF Commercial Complex, Jijini Dar es Salaam.
Aidha, Mhe. Sangu amesema jukumu kuu la bodi ni kusimamia shughuli za mfuko kama ilivyoainishwa katika Sheria ya PSSSF, kifungu cha 11 hususan katika maeneo makuu ya usimamizi ikiwemo huduma kwa wanachama, ukusanyaji wa michango, uwekezaji wa rasilimali za mfuko na ulipaji wa mafao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa PSSSF jijini Dar es Salaam Agosti 1, 2026
Vile vile, amesisitiza kuwa katika kutekeleza majukumu hayo, bodi inapaswa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na miongozo ya Serikali pamoja na Mpango Mkakati wa PSSSF, ambao umeanza kutekelezwa pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Wajumbe mmeingia katika kipindi muhimu ambapo mfuko umeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano. Huu ndio utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa majukumu na kufanikisha malengo ya mfuko,” amesema.
Kadhalika, amewataka wajumbe kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao, akibainisha kuwa Serikali ina matarajio makubwa kwa PSSSF katika kuhakikisha mfuko huo unakuwa imara.
Kuhusu uwekezaji, Waziri alisema fedha za wanachama zinapaswa kuwekezwa kwa umakini na weledi ili kulinda thamani yake na kuhakikisha zinazalisha faida itakayowezesha mfuko kutimiza wajibu wa kulipa mafao kwa wakati, hata baada ya miongo kadhaa.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo
“Fedha za wanachama zinawekwa leo kwa matarajio ya kulipa mafao miaka ijayo. Hivyo, ni muhimu ziwekezwe katika miradi yenye tija, salama na inayozingatia miongozo ya uwekezaji iliyowekwa na Serikali,” alisisitiza.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo



























