TRENDING NOW






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiondoka nchini kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Julai, 2026 kuelekea Accra, Ghana ambapo atashiriki katika Mkutano Mkuu Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu afya, utakaofanyika tarehe 22 Julai, 2026 jijini Accra.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Accra, Ghana kushiriki katika Mkutano Mkuu Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu afya, utakaofanyika tarehe 22 Julai, 2026 jijini Accra.

Na Mwandishi Wetu, Accra, Ghana

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amezitaka nchi za Afrika kuacha kutegemea matamko na ahadi zisizoambatana na utekelezaji, badala yake ziongeze uwekezaji wa ndani, uwajibikaji na matumizi ya ubunifu ili kuimarisha mifumo ya afya barani humo.

Dk. Kikwete alitoa kauli hiyo Julai 20, 2026, wakati akizungumza katika Mjadala wa Ngazi ya Juu wa Sera uliofanyika katika Hoteli ya Kempinski jijini Accra, Ghana, pembezoni mwa Mkutano Maalumu wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya.

Mjadala huo uliwakutanisha mawaziri, watunga sera, taasisi za kikanda, washirika wa maendeleo, viongozi wa sekta binafsi na wataalamu wa afya kutoka mataifa mbalimbali, ukiandaliwa kwa ushirikiano kati ya African Renaissance Trust, Wakfu wa Jakaya Mrisho Kikwete, Tume ya Umoja wa Afrika na wadau wengine.

Akizungumza katika mkutano huo, Dk. Kikwete alisema utegemezi wa muda mrefu wa misaada ya nje katika kugharamia sekta ya afya hauwezi kuendelea kuwa msingi wa mifumo ya afya ya Afrika, hasa wakati misaada ya maendeleo inapopungua na mahitaji ya huduma bora za afya yakiongezeka.

Alisema bara hilo linapaswa kuongeza uwezo wa kugharamia huduma zake za afya kupitia mapato ya ndani, matumizi yenye ufanisi wa rasilimali na uwajibikaji katika matumizi ya fedha za umma.

“Ujumbe kutoka Eswatini hadi Accra ni mmoja; Afrika lazima igharamie, izalishe na ilinde mustakabali wake wa afya,” alisema.

Dk. Kikwete alikumbusha kuwa ni miaka 25 sasa tangu kupitishwa kwa Azimio la Abuja la mwaka 2001 lililozitaka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kutenga angalau asilimia 15 ya bajeti zao kwa sekta ya afya, lakini nchi nyingi bado hazijafikia lengo hilo.

Alisema hali hiyo imeendelea kuchangia mzigo mkubwa wa magonjwa kama UKIMWI, kifua kikuu, malaria, pamoja na vifo vinavyoweza kuzuilika vya wajawazito na watoto wachanga.

Katika hotuba yake, Dk. Kikwete alieleza kuwa usalama wa afya ya mama na mtoto unapaswa kuwa kipaumbele kikuu, akibainisha kuwa takribani wanawake 260,000 hufariki kila mwaka duniani kutokana na matatizo yanayohusiana na ujauzito na kujifungua, huku karibu asilimia 70 ya vifo hivyo vikirekodiwa barani Afrika.

Alisisitiza kuwa changamoto si ukosefu wa maarifa, dawa au teknolojia, bali ni kushindwa kuzifikisha huduma hizo kwa wananchi wanaozihitaji.
“Mama anaporudi nyumbani salama, ni kwa sababu fedha, ushahidi wa kisayansi na utoaji wa huduma vimefanikiwa kukutana,” alisema.

Akitoa mfano wa Tanzania, Dk. Kikwete alisema ushirikiano kati ya Wakfu wa Jakaya Mrisho Kikwete, Wizara ya Afya na taasisi za utafiti umechangia kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto kupitia tafiti na mikutano ya kisayansi inayofanyika kila baada ya miaka miwili.

Alisema juhudi hizo zimechangia kupungua kwa vifo vya wajawazito kutoka zaidi ya vifo 550 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa hai hadi vifo 104, hatua inayoiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kufikia lengo la Maendeleo Endelevu la kupunguza vifo hivyo hadi 70 ifikapo mwaka 2030.

Aidha, alisema mafanikio ya sekta ya afya hayapaswi kupimwa kwa kiwango cha fedha kinachotengwa pekee, bali kwa matokeo yanayowafikia wananchi.

“Swali si tunatumia kiasi gani katika afya. Swali ni kama uwekezaji wetu unawafikia wananchi wanaouhitaji zaidi,” alisema.

Katika mkutano huo pia ulizinduliwa mfumo wa African Renaissance Health Financing Insights Dashboard, utakaosaidia serikali kufuatilia ahadi za kifedha, matumizi ya bajeti, mapungufu ya fedha pamoja na matokeo ya uwekezaji katika sekta ya afya.

Dk. Kikwete alisema mfumo huo utasaidia kuimarisha uwajibikaji na ushirikiano kati ya wizara za afya na wizara za fedha ili kuhakikisha fedha zinazotengwa zinaleta matokeo yanayotarajiwa.

Pia alihimiza Afrika kupunguza utegemezi wa dawa na chanjo kutoka nje kwa kuwekeza katika uzalishaji wa ndani, kuimarisha Wakala wa Dawa wa Afrika na kutumia fursa za biashara ya kikanda kuimarisha usalama wa afya.

Katika mapendekezo yake, Dk. Kikwete aliwasilisha vipaumbele vitano ambavyo ni kuifanya afya kuwa uwekezaji wa kimkakati, kuongeza mapato ya ndani kupitia bima na kodi bunifu, kulinda huduma muhimu wakati misaada inapopungua, kuimarisha uwajibikaji na kuongeza ushirikiano wa kikanda.

Kwa upande wake, Kamishna wa Umoja wa Afrika anayeshughulikia Afya, Masuala ya Kibinadamu na Maendeleo ya Jamii, Balozi Amma Twum-Amoah, alisema mafanikio ya sera za afya yanapaswa kupimwa kwa maboresho yanayoonekana katika maisha ya wananchi.

Akihitimisha hotuba yake, Dk. Kikwete alisema Afrika haina upungufu wa mikakati wala ubunifu, bali changamoto iliyopo ni utekelezaji wa maamuzi yaliyokwishafikiwa.

“Tuondoke Accra tukiwa na dhamira ya kubadili ahadi kuwa bajeti, bajeti kuwa programu, programu kuwa matokeo yanayopimika, na matokeo kuwa maisha marefu, yenye afya na uzalishaji zaidi kwa wananchi tunaowahudumia,” alisema.
Na Mashaka Mhando, Tanga

VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ngazi ya majimbo mkoani Tanga, wamemtaka Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Bara), John Heche, kujiuzulu au kukaa pembeni kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha zinazomkabili.

Sambamba na shinikizo hilo la ndani ya chama, viongozi hao wameiomba Serikali kupitia Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kufuta kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wao wa Taifa, Tundu Lissu, na kumuachia huru.

Msimamo huo umetolewa Julai 20 na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Handeni Mjini, Kombo Mohamed Maturu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akiwa ameambatana na viongozi wa majimbo mbalimbali na wanachama.
Taharuki na Tuhuma Dhidi ya Heche

Katibu huyo alieleza kuwa wamelazimika kuita waandishi kutokana na taharuki kubwa inayoendelea ndani ya chama chao inayotokana na misigano kati ya viongozi na wanachama, jambo linalokosesha chama afya. Alifichua kuwa awali walipanga kufanya maandamano makubwa kufikisha kilio chao.

"Kwanini Heche asizijibu hizi tuhuma au asitupishe akae pembeni ili tuchunguze tuhuma zake? Badala yake anakuja kujibu kwa kuwasema vibaya watu ambao tunawategemea kama wawakilishi... chama kipo chini kwa wanachama," alisema Matumla.

Maturu alimshutumu Heche kwa kutumia lugha isiyo ya kiungwana dhidi ya wawakilishi wao kwa kuwaita ‘mbwa’ badala ya kujibu hoja zinazoelekezwa kwake, huku akimtaka aache kugombana na Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema.

"Haya ni masikitiko yetu makubwa. Makamu Mwenyekiti wetu anatuhumiwa kufanya ubadhirifu halafu anajifanya mbabe. Tunataka ajibu tuhuma hizi au ajiuzulu mara moja. Hiki si chama cha mtu binafsi, ni taasisi ya watu. Tunampenda sana Heche, lakini atupishe hata wiki moja tufanye uchunguzi," alisisitiza.
Madai ya Meli ya Mafuta na Wito kwa Msajili

Katika madai mazito zaidi, Maturu alidai kuwa chama hicho kimekosa ujasiri wa kulalamikia upandaji wa bei za mafuta nchini kutokana na madai kuwa kiongozi wao wa juu anashirikiana na wafanyabiashara wa mafuta. Alihusisha hilo na tukio la hivi karibuni la kukamatwa kwa meli ya mafuta huko Yemen iliyokuwa inapeperusha bendera ya Tanzania.

Kutokana na mzozo huo, viongozi hao wamemwomba Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, kuunda tume ya kuchunguza madai hayo na asifanye mzaha na kauli za viongozi kuitana 'mbwa'. Pia, wamemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuingilia kati mgogoro huo ili kunusuru chama.
Kilio kwa Tundu Lissu

Kuhusu hali ya kisiasa, Maturu alisema licha ya kutokubaliana na ushindi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilio chao kikubwa kwa sasa ni kutaka Lissu aachiwe huru.

"Tunaomba Serikali iwe na huruma. Hii kesi ya Lissu ni ya kisiasa, haiwezekani mwaka wa pili sasa aendelee kushikiliwa kizuizini. Nchi inaingia kwenye migogoro na mataifa ya Ulaya na tunazuiwa misaada. Tunamuomba DPP aifute hii kesi, hakuna faida kuendelea kumshikilia," aliomba Maturu.
Msimamo wa BAVICHA na BAWACHA

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) Jimbo la Lushoto, Mambo Nassor Mkuya, aliunga mkono uamuzi wa viongozi hao wa Tanga wa kumtaka Heche apishe uchunguzi kwa kuwa chama ni cha wanachama na tuhuma hizo haziwezi kuachwa zipite. Mkuya alisisitiza kuwa kama Lissu angekuwepo, ubadhirifu huo usingetokea.

Naye Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Lushoto ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA wilayani humo, Jerida Ramadhani Mosha, alisema kuendelea kubaki ofisini kwa Heche kunaleta mgogoro. Aidha, alimuomba DPP "kuvaa viatu vya Lissu" na kujiona kama sehemu ya familia inayopata uchungu wa kiongozi huyo kukaa ndani kwa miaka miwili.


The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi, has thanked the Government of India for its continued efforts to strengthen cooperation with Tanzania in the sectors of education, health, trade, investment, water, science and technology.

President Dr. Mwinyi made the remarks today, July 19, 2026, when he met with India's Minister of External Affairs, Hon. Dr. S. Jaishankar, at a conference hall at the Taj Palace Hotel in New Delhi, India.

During the discussions, President Dr. Mwinyi asked India to increase the number of scholarship and training opportunities for students and professionals from Zanzibar, as well as to strengthen the IIT Madras Zanzibar campus by introducing more academic programmes and supporting the construction of its permanent campus.

President Dr. Mwinyi also handed over to Minister Jaishankar the Master Plan for the construction of the permanent IIT Madras Zanzibar campus, aimed at making Zanzibar a hub for higher education, research, innovation and technology for the African region.

For his part, Minister Dr. Jaishankar commended the progress made by IIT Madras Zanzibar and reaffirmed the Indian Government's commitment to continuing to strengthen cooperation with Tanzania across various development sectors.

President Dr. Mwinyi continues his visit to India, where he is meeting with various leaders with the aim of strengthening development cooperation between Zanzibar, Tanzania and India.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania(TRAMEPRO Tanzania ) limetoa mwitokwa Watanzania, Waafrika na jumuiya ya kimataifa kuendelea kujenga jamii inayoheshimu utu wa kila mtu, kuwekeza katika elimu, afya, sayansi, mazingira na amani.

TRAMEPRO imetoa mwito huo leo Julai 18,2026 katika kukimbizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela aliyekuwa Rais wa nchi ya Afrika Kusini. 

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu TRAMEPRO Tanzania  Boniventura Mwalongo amesema wanaungana na mataifa ya Afrika na dunia kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela mmoja wa viongozi mashuhuri waliobadilisha historia ya dunia kwa kupigania uhuru, usawa, haki za binadamu na maridhiano.

Pia amesema mambo ya kujifunza kupitia kutoka kwa Nelson Mandela ni kwamba elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ya kubadilisha dunia, msamaha ni nguvu, si udhaifu; hujenga taifa lenye umoja.

Mengine ni uvumilivu na subira vinaweza kushinda hata changamoto kubwa,  Uongozi ni huduma, si nafasi ya kutawala wengine, haki  na usawa ni msingi wa maendeleo endelevu.

"Mandela anatufundisha pia umoja wa Waafrika na kuheshimiana ni nguzo ya maendeleo ya bara letu. Afya, mazingira na maendeleo vinapaswa kwenda pamoja kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, " amesema Mwalongo. 

Akieleza zaidi amesema kwa waratibu asili Asili,TRAMEPRO Tanzania inaona mafunzo makubwa kutoka kwa Mandela katika kujenga umoja wa sekta, kuzingatia maadili ya taaluma, kuendeleza utafiti, kuhifadhi mimea tiba, kulinda mazingira na kushirikiana na taasisi za kisayansi ili tiba asili ichangie kikamilifu afya na maendeleo ya jamii.

Kuhusu historia ya Nelson Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji cha Mvezo, Mkoa wa Eastern Cape, Afrika Kusini. Jina lake la asili, Rolihlahla, katika lugha ya Kixhosa humaanisha mtu anayetikisa tawi la mti, na kwa maana ya kawaida huashiria mtu mwenye kuhoji au kupinga hali iliyopo.

Alipoanza shule ya msingi, mwalimu wake alimpa jina la Nelson, kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo katika shule nyingi za kikoloni.

Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme ya kabila la Thembu. Baba yake aliitwa Gadla Henry Mphakanyiswa Mandela, aliyekuwa mshauri wa mfalme wa Thembu, na mama yake aliitwa Nosekeni Fanny Mandela.

 Kutoka kwa wazazi wake alijifunza heshima, uwajibikaji, uongozi na umuhimu wa kuitumikia jamii.

Katika elimu, Mandela alianza masomo katika shule za wamisionari, akaendelea katika Chuo cha Healdtown, kisha akasoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare. 

Baadaye alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, ambako alijiandaa kuwa mwanasheria na mtetezi wa haki za wanyonge. Elimu yake ilimpa msingi wa kuelewa sheria na kuitumia kutetea usawa na utu wa binadamu.

Mandela aliongoza mapambano dhidi ya mfumo wa ubaguzi wa rangi (Apartheid). Kutokana na msimamo wake, alifungwa gerezani kwa miaka 27, lakini hakukata tamaa wala kuacha kuamini kuwa amani na maridhiano vinaweza kushinda chuki. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990, aliongoza mazungumzo yaliyoweka msingi wa Afrika Kusini mpya yenye demokrasia.

Mwaka 1994, Nelson Mandela aliingia katika historia kwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini aliyechaguliwa kidemokrasia. Uongozi wake ulijengwa juu ya maridhiano, msamaha na umoja wa kitaifa. Mwaka 1993, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mchango wake katika kumaliza Apartheid kwa njia ya amani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, ameongoza mamia ya wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira katika matembezi ya Save Soil Walkathon, huku akitoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda udongo na mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu ya taifa.

Mhe. Masauni, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa tukio hilo, alishiriki matembezi hayo yaliyoandaliwa na Lions Club of Dar es Salaam Mazingira chini ya kaulimbiu ya “Save Soil, Save Our Future” (Linda Udongo, Linda Mustakabali Wetu). 

Tukio hilo liliwakutanisha wadau wa mazingira, taasisi mbalimbali, sekta binafsi na wananchi katika kampeni ya kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kuhifadhi afya ya udongo na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

Akizungumza baada ya matembezi hayo, Mhe. Masauni alisema afya ya udongo ni msingi wa usalama wa chakula, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa uchumi wa taifa, hivyo kuna umuhimu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kuutunza.
"Udongo ni rasilimali muhimu inayobeba maisha yetu ya kila siku. Bila udongo wenye afya hatuwezi kuwa na usalama wa chakula, mazingira bora wala maendeleo endelevu. Ni wajibu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia ardhi kwa njia zinazohifadhi uhai wake kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho," alisema Mhe. Masauni.

Katika kuonesha kwa vitendo dhamira ya kulinda mazingira, Mhe. Masauni pia alipanda mti ikiwa ni ishara ya kujitolea katika uhifadhi wa udongo na mazingira pamoja na kuhamasisha wananchi kushiriki katika upandaji miti kama sehemu ya juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa ardhi.

Kwa upande wake, Rais wa Lions Club of Dar es Salaam Mazingira, Lion Ramadevi, alisema Save Soil Walkathon ni sehemu ya kampeni pana inayolenga kuhamasisha jamii kutambua mchango mkubwa wa udongo katika maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.

"Save Soil Walkathon si matembezi pekee, bali ni harakati ya kuhamasisha mabadiliko ya tabia na kuwajengea wananchi uelewa wa umuhimu wa kulinda udongo. Tunataka kuona jamii, taasisi na sekta binafsi zikichukua hatua za pamoja katika kuhifadhi mazingira kwa mustakabali wa taifa letu," alisema Lion Ramadevi.

Naye Esther Msuya, Meneja wa Afya, Usalama, Ulinzi na Mazingira (HSSE) wa GSG Energies, alisema kampuni hiyo itaendelea kuunga mkono mipango na kampeni zinazolenga uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu nchini.

"Kulinda mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. GSG Energies tunaamini kuwa maendeleo ya kweli lazima yaende sambamba na uhifadhi wa mazingira.

Ushiriki wetu katika Save Soil Walkathon unaonesha dhamira yetu ya kusaidia juhudi za kuongeza uelewa wa jamii na kulinda rasilimali za asili kwa manufaa ya vizazi vijavyo."

"Tutaendelea kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kutekeleza miradi na kampeni zinazochochea utunzaji wa mazingira, matumizi bora ya rasilimali za asili na maendeleo endelevu nchini," alisema Esther Msuya.

Save Soil Walkathon imeonesha nguvu ya ushirikiano kati ya Serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi na wananchi katika kuendeleza agenda ya utunzaji wa mazingira. Washiriki walihamasishwa kuchukua hatua za vitendo ikiwemo upandaji miti, matumizi bora ya ardhi, uhifadhi wa vyanzo vya maji na ulinzi wa rasilimali za asili kwa ajili ya mustakabali wa taifa.

Wadhamini wa Save Soil Walkathon
GSG Energies
META JCB
SRL
UHAI Pure Drinking Water
ISUZU Tanzania
Tanzania Bloggers Network (TBN) Chairman Beda Msimbe (left) meets with the Journalism Accreditation Board’s Acting Director General, Advocate Patrick Kipangula, during their meeting at the Board’s offices in Dar es Salaam on 16 July 2026. The meeting followed TBN’s formal request for professional training for more than 200 bloggers on media law, journalistic ethics and the importance of accreditation.

By TBN Staff Writer

The Journalists’ Accreditation Board (JAB) has received a formal request from the Tanzania Bloggers Network (TBN) seeking training for its more than 200 members on the Media Services Act, journalism ethics, and the importance of obtaining professional accreditation.

The request was submitted on 16 July 2026, when TBN Chairman Beda Msimbe met with JAB’s Acting Director General, Advocate Patrick Kipangula, during discussions held at the Board’s offices in Dar es Salaam.

Speaking after the meeting, Advocate Kipangula said the Board had received the request and was ready to work with the network to help bloggers gain a deeper understanding of the Media Services Act, professional ethics, and the value of accreditation.

He said the training would begin with bloggers who are already accredited, aimed at strengthening their professionalism and understanding of their professional responsibilities, before extending to those who have not yet obtained accreditation.

“Those without accreditation will get the opportunity to be guided on the legal requirements for obtaining it, including the necessary qualifications required under the Media Services Act. Those who do not yet meet the required qualifications will be advised to pursue further education so they can meet the criteria for accreditation,” Advocate Kipangula said.

For his part, TBN Chairman Beda Msimbe said the training would help the network’s members carry out their duties in line with the law, ethics, and professionalism, while also contributing effectively to informing the public and promoting Tanzania through coverage of development initiatives being implemented across various sectors.

He added that the collaboration between the network and JAB would help build the capacity of bloggers and strengthen their contribution to the country’s media sector.

Background

The request marks a notable step in efforts to bring Tanzania’s growing community of digital content creators and bloggers into closer alignment with the formal regulatory framework governing media practice in the country.

The Media Services Act has, since its introduction, set out qualification requirements and ethical standards that traditional journalists are expected to meet, and the extension of similar guidance to bloggers reflects the increasing recognition of digital platforms as a significant source of public information.

TBN’s more than 200 members represent a wide cross-section of Tanzania’s online content creators, many of whom operate blogs, social media pages, and other digital platforms that reach large audiences, particularly among younger Tanzanians who increasingly turn to online sources for news and updates.

By prioritising already-accredited bloggers in the first phase of training, JAB appears to be taking a phased approach that rewards those who have already engaged with the formal accreditation process, while creating a clear pathway for others to follow.

The emphasis on further education for those who do not yet meet the qualification criteria suggests the Board intends the programme to be developmental rather than punitive, encouraging capacity-building rather than simply excluding non-accredited bloggers from practice.

Observers of Tanzania’s media landscape note that partnerships of this kind between regulatory bodies and digital media associations could help address longstanding tensions between traditional journalism institutions and the newer wave of online content creators, many of whom have historically operated outside formal press structures.

No specific date has yet been announced for when the training sessions will begin, though both JAB and TBN indicated their intention to move forward with the collaboration.

Further details on the training schedule, curriculum, and criteria for accreditation are expected to be announced in due course as the two organizations finalize the arrangements for the programme.

Na Mwandishi Wetu, JAB

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imepokea ombi kutoka Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) la kutoa mafunzo kwa wanachama wake zaidi ya 200 kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, Maadili ya Uandishi wa Habari na umuhimu wa kupata ithibati.

Ombi hilo limetolewa leo, tarehe 16 Julai, 2026, na Mwenyekiti wa Mtandao wa Mabloga Tanzania, Bw. Beda Msimbe, alipokutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, katika mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Bodi jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya mazungumzo hayo, Wakili Kipangula amesema Bodi imepokea ombi hilo na iko tayari kushirikiana na Mtandao huo katika kuwawezesha bloga kupata uelewa wa kina kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma pamoja na umuhimu wa kupata ithibati.

Amesema mafunzo hayo yataanza kutolewa kwa bloggers wenye ithibati ili kuimarisha weledi na uelewa wao wa majukumu ya kitaaluma, kabla ya kuendelea kuwafikia wale ambao bado hawajapata ithibati.

"Wale ambao hawana ithibati watapata fursa ya kuelekezwa kuhusu masharti ya kisheria ya kupata ithibati, ikiwemo umuhimu wa kuwa na sifa zinazotakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari. Wasio na sifa stahiki watashauriwa kujiendeleza kielimu ili waweze kukidhi vigezo vya kupata ithibati," amesema Wakili Kipangula.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtandao wa Mabloga Tanzania, Bw. Beda Msimbe, amesema mafunzo hayo yatawasaidia wanachama wa chama hicho kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, maadili na weledi, sambamba na kuchangia kwa ufanisi katika kuhabarisha umma na kuitangaza Tanzania kupitia taarifa za maendeleo zinazotekelezwa katika sekta mbalimbali.

Amesema ushirikiano kati ya Mtandao huo na JAB utasaidia kujenga uwezo wa bloggers na kuimarisha mchango wao katika sekta ya habari nchini.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza udhamini wa Mashindano ya Golf ya Vodacom Corporate Masters 2026, yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na Lugalo Golf Club kwa lengo la kuunganisha jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania, kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kukuza ushirikiano na kuleta fursa zenye tija kwa wateja, washirika wa kibiashara na wadau muhimu nchini. Mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 1 Agosti 2026 yanaendelea kuimarisha nafasi ya Vodacom kama mshirika wa kuaminika katika teknolojia na huduma za mawasiliano kwa taasisi na mashirika yanayoendelea kukua katika mazingira ya uchumi wa kidijitali. Uzinduzi huo umefanyika tarehe 16 Julai 2026 jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Katibu wa Corporate Masters, Maryanne Mugo (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Mbaya (kulia).

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yatakayofanyika katika Uwanja wa Gofu wa Lugalo kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kufungua fursa mpya kwa wateja, washirika na wadau wa sekta mbalimbali.

Mashindano hayo, yanayoandaliwa kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited kupitia kitengo cha Vodacom Business, yatawakutanisha viongozi wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu wa sekta mbalimbali na wapenzi wa mchezo wa gofu kwa lengo la kujenga mitandao ya biashara na kubadilishana uzoefu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania PLC, Joseph Sayi, alisema kampuni hiyo imeendelea kudhamini mashindano hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo kwa kuwa yanaendana na dhamira ya kuimarisha mahusiano ya muda mrefu na jumuiya ya wafanyabiashara.

Alisema mashindano hayo si ya michezo pekee, bali ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujadili fursa mpya za uwekezaji na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.

Sayi alisema katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho mbalimbali za kidijitali ikiwemo huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi, kukuza biashara na kuimarisha ushindani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Corporate Masters, Ken Kariuki, alisema mashindano hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la makampuni kujitangaza, kujenga mitandao ya kibiashara na kuzalisha fursa mpya za biashara huku yakiimarisha ushiriki wa wateja.

Mashindano hayo yatashirikisha timu 10 za makampuni zitakazowania taji la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na maonesho ya biashara, burudani, maonesho ya vitu vya kale na eneo maalumu la watoto, hatua inayolenga kuwafanya washiriki na familia zao kufurahia tukio hilo katika mazingira rafiki.