

Fatma alisema katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kampuni imechangia zaidi ya shilingi trilioni 1.4 kupitia kodi na tozo mbalimbali kwa Serikali, hatua iliyoifanya kutambuliwa mara kadhaa na TRA kwa utii wa sheria za kodi na mchango wake mkubwa katika kuongeza mapato ya ndani. Aliongeza kuwa kampuni itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya nishati na kupanua huduma zake ili kuchochea maendeleo ya sekta mbalimbali za uzalishaji.Mbali na ulipaji wa kodi, Puma Energy Tanzania imeendelea kuimarisha uwekezaji wake kwa kuendesha zaidi ya vituo 100 vya huduma za mafuta, maghala ya kuhifadhi mafuta na usambazaji wa mafuta ya ndege katika viwanja vinane vya ndege, ikiwemo viwanja vyote vya kimataifa nchini. Kampuni pia inaongoza matumizi ya nishati safi kupitia Kituo Kikuu cha Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG Mother Station) pamoja na mtandao unaokua wa vituo vya CNG jijini Dar es Salaam na Morogoro.
Aidha, kampuni inaendelea kupanua huduma za gesi ya kupikia kupitia Puma Gas, biashara ya vilainishi na maduka ya Shop Express, huku ikiendelea kuchangia ukuaji wa uchumi kupitia uwekezaji, ajira na huduma za nishati zenye ubora. Tuzo hiyo imeongeza hadhi ya Puma Energy Tanzania kama mmoja wa walipa kodi wakubwa na washirika muhimu wa Serikali katika kufanikisha ajenda ya maendeleo ya Taifa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.


Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.



Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.
"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.
Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.



Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.
Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.
Vodacom Tanzania Yaimarisha Mchango Katika Ukuaji wa Uchumi Kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050












































































