TRENDING NOW






Dar es Salaam, Agosti 5, 2026 – Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limetoa wito kwa Serikali, wataalamu wa afya, wataalamu wa tiba asili, wakunga, wadau wa mazingira na jamii kwa ujumla kushirikiana katika kulinda afya na uhai wa mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani yanayoendelea kuanzia Agosti 1 hadi 7, 2026.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, TRAMEPRO limesema linaungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Shirika la Afya Duniani (WHO), UNICEF, Wizara ya Afya na wadau wengine wa afya duniani katika kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kama njia muhimu ya kuboresha afya ya watoto na akina mama.

Shirika hilo limeeleza kuwa Wiki ya Unyonyeshaji Duniani ilianzishwa mwaka 1992 na World Alliance for Breastfeeding Action (WABA) kwa ushirikiano na WHO na UNICEF, kufuatia Azimio la Innocenti la mwaka 1990, lenye lengo la kulinda, kuhamasisha na kuunga mkono unyonyeshaji wa maziwa ya mama duniani.

Kwa mujibu wa TRAMEPRO, unyonyeshaji wa maziwa ya mama ni moja ya njia bora za kupunguza vifo vya watoto wachanga na kuboresha afya ya mama. Shirika hilo limeunga mkono mapendekezo ya WHO yanayosisitiza mtoto kuanza kunyonya ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa, kupewa maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya kwanza, na kuendelea kunyonyeshwa pamoja na vyakula vya nyongeza hadi miaka miwili au zaidi.

TRAMEPRO pia limebainisha kuwa Tanzania hupata wastani wa watoto kati ya milioni 2.2 na 2.4 wanaozaliwa hai kila mwaka, huku Afrika ikichangia takribani asilimia 70 ya vifo vya akina mama duniani. Aidha, zaidi ya watoto wachanga milioni moja hufariki kila mwaka barani humo kutokana na sababu zinazoweza kuzuilika, ikiwemo kuzaliwa kabla ya wakati, maambukizi, kukosa hewa wakati wa kuzaliwa na utapiamlo.

Shirika hilo limeeleza kuwa afya ya mama na mtoto haiwezi kutenganishwa na mazingira bora, likisisitiza umuhimu wa upatikanaji wa maji safi, lishe bora, usafi wa mazingira, hewa safi na uhifadhi wa bioanuwai. Pia limefafanua kuwa mimea tiba, ambayo ni sehemu ya tiba asili, hutegemea mazingira salama na uhifadhi wa misitu pamoja na vyanzo vya maji.

Katika taarifa hiyo, TRAMEPRO limetoa wito maalumu kwa wataalamu wa tiba asili, wakunga wa jadi na wakunga wataalamu kuzingatia sheria, maadili ya taaluma na ushahidi wa kisayansi katika utoaji wa huduma. Pia limewahimiza kuwashauri wajawazito kuhudhuria kliniki mapema, kujifungulia katika vituo vya afya, kutambua dalili za hatari mapema na kushirikiana kwa karibu na wataalamu wa afya ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Aidha, shirika hilo limetoa wito kwa Serikali kuendelea kuwekeza katika huduma za afya ya uzazi, kuongeza idadi ya wakunga na wahudumu wa afya, kuimarisha lishe, chanjo, maji safi na usafi wa mazingira, pamoja na kuwekeza katika tafiti za tiba asili salama.

TRAMEPRO pia limealika Wizara, taasisi za Serikali, mashirika ya kimataifa, asasi za kiraia, vyuo vikuu, taasisi za utafiti, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kushirikiana katika kuendeleza tafiti, elimu ya afya, uhifadhi wa mimea tiba na ulinzi wa mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Shirika hilo limemalizia kwa kusisitiza kuwa kulinda afya ya mama na mtoto ni jukumu la kila mwananchi na kwamba ushirikiano kati ya sekta ya afya, tiba asili na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa kujenga Taifa lenye watoto wenye afya, akina mama salama na maendeleo endelevu.

 The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.

Dar es Salaam, Tanzania – 5 August, 2026 – Plaza Premium Group (PPG), the global leader in integrated, 360-degree airport hospitality experiences and passenger service solutions, has officially announced its strategic expansion into Tanzania ahead of its upcoming launch of the country’s first Plaza Premium Lounge at Julius Nyerere International Airport (JNIA), Terminal 3 in Dar es Salaam.

To mark this milestone, PPG hosted an executive stakeholder engagement in Dar es Salaam, bringing together key stakeholders across Tanzania's aviation, tourism, financial, corporate and government sectors. The session focused on establishing collaborative partnerships to support Tanzania's premium travel infrastructure and passenger experience.
Scheduled to officially open later this month, Plaza Premium Lounge at JNIA Terminal 3 will welcome all travellers with an elevated pre-flight experience that reflects Plaza Premium Group's award-winning global expertise and thoughtfully integrated local hospitality. Guided by the philosophy of Your Destination Before Departure, the lounge will offer elevated dining and beverage experiences, premium lounge facilities, shower suites, a dedicated prayer room, business amenities and personalised service, creating a seamless and memorable start to every traveller’s journey.

"Tanzania represents one of the most promising aviation and tourism markets in East Africa,” said Okan Kufeci, Senior Vice President, Europe, Middle East and Africa (EMEA), adding that “Continued investment in infrastructure, growing international connectivity, and a vibrant tourism sector are creating the right conditions for premium airport hospitality. Today's engagement marks the beginning of a long-term commitment to collaborate with government institutions, airlines, and industry partners to elevate the passenger experience while supporting Tanzania’s broader growth ambitions.

"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.

Mkurugenzi wa Biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania Plc Brigita Shirima (katikati), Mkurugenzi wa Vodacom Business wa kampuni hiyo Nguvu Kamando (kulia), pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Tulisindo Mlupilo (kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya "Zaidi ya Mtandao" yenye lengo la kuimarisha dhamira ya kuleta fursa na huduma kwa wateja wake ikiwa ni zaidi ya huduma za mawasiliano ila ni suluhisho halisi la maisha ya kila siku kwa jamii. Tukio hilo limefanyika leo tarehe 4 August 2026, Makao makuu ya Vodacom Tanzania Plc, jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.

“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima

Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.

“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.

 Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Vodacom Tanzania Plc, Tulisindo Mlupilo, alisema M-Pesa inaendelea kuwa nguzo muhimu ya ujumuishaji wa kifedha kwa kuwawezesha mamilioni ya Watanzania kupata huduma za kifedha kwa urahisi na usalama.

"Mfumo wa M-Pesa unahudumia zaidi ya watumiaji hai milioni 14.1 kila mwezi kupitia huduma zinazowawezesha kuweka akiba kupitia M-KOBA, kupata mikopo kupitia SONGESHA, kuwekeza kupitia M-WEKEZA, kufanya malipo ya biashara kupitia LIPA na kutuma na kupokea fedha kwa urahisi. Maboresho ya mfumo wa M-Pesa yataongeza uwezo wetu wa kutoa huduma za kifedha kwa ufanisi zaidi na kuendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania za kujenga uchumi wa kidijitali. Dhamira ya Vodacom ni kuendelea kutumia teknolojia kama chachu ya ujumuishaji wa kifedha na kuongeza thamani kwa wateja wetu, tukiendelea kutekeleza falsafa ya ‘Zaidi ya Mtandao’." alisema Mlupilo.

Vodacom inaamini kuwa thamani ya mtandao haipimwi kwa wigo wa huduma, kasi au teknolojia pekee, bali kwa fursa na matokeo chanya unayowezesha katika maisha ya watu kila siku.

Kadri Vodacom inavyoendelea kuwekeza katika mtandao wake, kuboresha uzoefu wa wateja na kuendeleza suluhisho bunifu za kidijitali, "Zaidi ya Mtandao" itaendelea kuwa msingi wa dhamira ya kampuni ya kuunda fursa, kuwezesha maendeleo na kuboresha maisha ya Watanzania.

Kufuatia mwaliko wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Jamhuri ya Uganda atafanya ziara rasmi nchini kuanzia tarehe 5 hadi 6 Agosti 2026.

Wakati wa ziara hiyo, Mheshimiwa Rais Museveni atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, yatakayojikita katika kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika maeneo mbalimbali, ikiwemo biashara na uwekezaji, miundombinu na usafirishaji, nishati, utalii, masuala ya ulinzi na usalama, na mtangamano wa kikanda.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha zaidi mahusiano ya kihistoria, ya kindugu na ya kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda. Aidha, viongozi hao watapitia maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya pamoja na kujadili hatua za kuondoa vikwazo vinavyoathiri biashara, uwekezaji na ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.

Baada ya mazungumzo rasmi, viongozi hao wawili wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU) katika masuala ya nishati. Aidha, watazungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa pamoja ambapo wataeleza masuala yaliyojadiliwa, makubaliano na maamuzi yaliyofikiwa, pamoja na mwelekeo wa kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Ziara hiyo ni ya pili kwa Mheshimiwa Rais Museveni nchini Tanzania katika mwaka 2026, na itatoa fursa kwa viongozi hao kutathmini utekelezaji wa maamuzi yaliyokwishafikiwa kati ya Tanzania na Uganda, ikiwemo maazimio ya Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) uliofanyika mwezi Machi 2026. Vilevile, viongozi hao wanatarajiwa kutoa mwelekeo wa hatua za kuimarisha zaidi ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili.

 DAR ES SALAAM, Tanzania – Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, atajumuika na viongozi wa kimataifa, mawaziri, watunga sera, wawekezaji, taasisi za fedha za maendeleo pamoja na viongozi wa biashara katika Mkutano wa Infra for Africa Forum 2026, unaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 5 hadi 6 Agosti 2026.

Mkutano huo, ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Africa50, utawakutanisha wadau muhimu kujadili mbinu bunifu za kuharakisha maendeleo na uwekezaji katika miundombinu barani Afrika, huku Mgeni Rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tarehe 5 Agosti, Rwegasira atashiriki katika mjadala wa ngazi ya juu wenye mada “Reinvesting for Expansion: Asset Recycling as a Multiplier”, akiwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Nishati na Miundombinu Duniani wa Standard Bank Group, Dele Kuti, na viongozi wengine waandamizi. Katika mjadala huo atazungumzia ugharamiaji wa miundombinu, uhamasishaji wa mitaji na ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuharakisha uwekezaji katika miundombinu barani Afrika.

Tarehe 6 Agosti, pia atazungumza katika kikao cha jumla chenye mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led”, sambamba na viongozi waandamizi kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ecobank, ATIDI na Mfuko wa Uwekezaji wa Taifa wa Angola. Kikao hicho kitachambua namna taasisi za fedha za Afrika, wawekezaji wa kitaifa, benki na wadau wa miundombinu wanavyoweza kuhamasisha mitaji ya ndani, kuimarisha mifumo ya kupunguza hatari na kuharakisha ugharamiaji wa miundombinu kupitia suluhu zinazoongozwa na Waafrika.

Stanbic Bank Tanzania inaeleza kuwa maendeleo ya miundombinu yanaendelea kuwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi, mtangamano wa kikanda na ustawi wa muda mrefu, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo endelevu kupitia suluhu bunifu za kifedha na ushirikiano wa kimkakati unaochochea ajenda ya maendeleo ya Tanzania na ukuaji wa Afrika.

Na Oscar Assenga, TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Rashid Mchatta amefungua kikao kazi cha Wakurugenzi na Mameneja wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini huku akisisitiza matumizi teknolojia ya kisasa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao.

Wito huo umetolewa jijini Tanga na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Sekta ya Maji nchini.
Kikao hicho kinafanyika chini ya kaulimbiu “Huduma Janja: Matumizi ya Teknolojia kwa Huduma Bora kwa Wateja”, kikilenga kuwawezesha wakurugenzi na mameneja hao kubadilishana uzoefu na kujadili mbinu mbalimbali za kuboresha huduma kwa wananchi.

Mchatta aliipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini na kuiwezesha Wizara ya Maji kutekeleza miradi na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na huduma za usafi wa mazingira nchini.
Pia aliipongeza uongozi wa Wizara ya Maji unaoongozwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Naibu Waziri, Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Rose Ambrose, kwa juhudi wanazofanya katika kusimamia utekelezaji wa majukumu ya wizara hiyo.

Alisema mafanikio yanayoonekana katika sekta ya maji, kuanzia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati hadi uboreshaji wa huduma kwa wananchi, yanaonesha kuwa uongozi wa wizara hiyo umejikita katika kuhakikisha huduma zinaboreshwa kila siku.
“Viongozi hawa wameonesha weledi, uzoefu na uthubutu katika kusimamia sekta ya maji. Ushirikiano wao umeendelea kuleta mafanikio yanayoonekana na wananchi wanaendelea kushuhudia mabadiliko katika huduma za maji na usafi wa mazingira,” alisema Mchatta.

Alisema kikao hicho ni fursa muhimu kwa wakurugenzi na mameneja wa huduma kwa wateja kujifunza, kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma.
Kwa mujibu wa Mchatta, mafunzo hayo pia yanahusu ufanisi wa biashara katika mamlaka za maji pamoja na mbinu za uwekezaji binafsi, ambapo wataalamu kutoka UTT-AMIS wanashiriki kutoa elimu kwa washiriki.
Aliwataka washiriki kutumia kikamilifu fursa hiyo kujifunza mbinu mpya, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma kwa wateja.

“Ninaamini mafunzo haya yatakuwa chachu ya kuboresha ufanisi mtakaporudi katika vituo vyenu vya kazi na hivyo kuongeza ubora wa huduma mnazozitoa kwa wananchi,” alisema.

JUKWAA LA WAKURUGENZI LAZIDI KUKUA

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini, Alawi Ahmad, alisema jukwaa hilo ni sehemu muhimu ya uongozi katika sekta ya maji, kwa kuwa linawapa nafasi wakurugenzi na mameneja kukutana, kujadiliana na kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma.
Alisema jukwaa hilo limekuwa likifanya vikao kila mwaka na kwa sasa lina takribani miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.

“Jukwaa hili limekuwa likitusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utoaji wa huduma kwa wateja na pia limetumika kama sauti ya pamoja ya wakurugenzi wa huduma kwa wateja katika sekta ya maji,” alisema Ahmad.
Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi  Abbas Muslim Pyarali  alisema kikao hicho kinawakutanisha wakurugenzi wa mamlaka za maji wanaojikita katika utoaji wa huduma kwa wateja.

Abbas ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Maji alisema kikao hicho kitakachodumu kwa siku tatu kitawapa washiriki nafasi ya kupata mafunzo maalumu na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora ya utoaji wa huduma kwa wananchi.
Alisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Wizara ya Maji za kuhakikisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira zinaendelea kuboreshwa nchini.
AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw. Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026

Dodoma, Agosti 2, 2026

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika Maonesho ya Nanenane 2026 kwa kutoa huduma mbalimbali na elimu kuhusu Hifadhi ya Jamii kwa wanachama wake na wananchi kupitia mabanda yake yaliyopo katika kanda tano nchini, ikiwemo Zanzibar.
Msanii maarufu nchini ,Mrisho Mpoto (wa pili kushoto) akiwa ameshika mkanda ,moja ya bidhaa zinazozalishwa katika kiwanda cha KLICL,Kinachomilikiwa na PSSSF kwa ushirikiano na Jeshi la Magereza ,alipotembelea Banda la Mfuko wa PSSSF kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026,kushoto ni Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Mfuko wa PSSSF Bw.Abdul Njaidi na kulia ni Afisa Mauzo kiwanda cha KLICL, Bi. Mary Muna

Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa PSSSF, Bw. Abdul Njaidi, PSSSF imeshiriki maonesho hayo katika Kanda ya Kati viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma, ambako Maonesho ya Nanenane 2026 yanafanyika kitaifa na tayari yamezinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Agosti 1, 2026. Kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘Tambua Soko; Ongeza Tija na Thamani ya Kuelekea Dira 2025’.
Wanachama wa Mfuko wa PSSSF wakihudumiwa kwenye Banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti2, 2026.

Katika maonesho ya mwaka huu, PSSSF inashiriki; Zanzibar katika viwanja vya Dole, Kanda ya Magharibi mkoani Tabora katika viwanja vya Ipuli Mnadani, Kanda ya Ziwa jijini Mwanza katika viwanja vya Nyamhungolo, Kanda ya Kusini mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini jijini Mbeya, viwanja vya Nanenane.
Afisa Matekelezo wa Mfuko wa PSSSF Bi.Esther Mpemba (kulia ) akimuunganisha Mwanachama wa PSSSF ,Bi.Maliasa Sajoho na Mfumo wa PSSSF Member Portal ambao unamuwezesha kupata huduma za mfuko Kidijitali,kwenye maonesho ya Nanenane Viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026

"Tunawakaribisha wanachama wetu na wananchi wote kutembelea mabanda ya PSSSF katika kanda hizo ili kupata huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu kuhusu mafao, kuhakiki taarifa zao na michango, pamoja na kuwaunganisha katika huduma zetu za kidijitali, huku tukiwahakikisha kesho ya uhakika wanachama wetu’" alisema Bw. Njaidi.
Afisa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa PSSSF ,Bi .Saluna Ally (kushoto) akimuhudumia Mstaafu anayepokea Pensheni PSSSF ,Bw.Mwakibete G.Kasilati,kwenye banda la mfuko huu katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwenye viwanja vya Nanenane Jijini Mbeya,Agosti 2,2026

Aidha, watakaotembelea kwenye mabanda ya PSSSF watapata nafasi ya kuona fursa za uwekezaji wa Mfuko ambazo ni pamoja na bidhaa za ngozi zinazotengenezwa na Kiwanda cha KLICL na nyama kutoka machinjio ya Kimataifa ya Nguru.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 1, 2026.
Meneja wa PSSSF Kanda ya Magharibi Bw.Eliadi Mndeme akitoa elimu kwa mwanachama wa PSSSF wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi ambayo yanafanyika viwanja vya Ipuli mkoani Tabora Agosti 2, 2026.
Mtoa huduma wa Vodacom Tanzania Catherine Masanja (kushoto) akimsajilia line ya Lipa mkazi wa Igoma Irene Ernest, kwenye maonesho ya Wakulima katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza, Kampuni hiyo iko katika maonesho ya Nanenane ikiwaelezea wananchi bidhaa na huduma mablimbali inazotoa ikiwamo M-Kulima huduma inayowapa wakulima njia rahisi na salama ya kulipwa mapato yao pindi wanapouza mazao mbalimbali.
Mtoa huduma wa Vodacom Tanzania, akiwaeleza wateja kuhusu Router kwenye maonesho ya Wakulima katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza.
Kampuni ya Vodacom Tanzania inaendelea kuimarisha huduma za kifedha na mawasiliano kwa wananchi kupitia ushiriki wake katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza.

Katika maonesho hayo, watoa huduma wa kampuni hiyo wamekuwa wakitoa elimu na kusajili wananchi kwenye huduma mbalimbali, ikiwemo huduma ya Lipa.

Kupitia huduma ya M-Kulima, Vodacom inalenga kuwapatia wakulima suluhisho rahisi, salama na la uhakika la kupokea malipo yao wanapouza mazao. 

Huduma hii inalenga kuongeza uwazi na ufanisi katika miamala ya kifedha kwa wakulima, huku ikichangia kukuza uchumi wa sekta ya kilimo nchini. Vodacom inaendelea kujitolea kutoa huduma bunifu zitakazowawezesha wananchi, hasa wakulima, kunufaika zaidi na teknolojia ya kidijitali.

Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam. Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Benki ya Exim Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wamezindua rasmi Programu ya YST 2026, wakiahidi kuendelea kuwawezesha vijana wabunifu kupitia sayansi, teknolojia, utafiti na ubunifu.

Uzinduzi huo uliofanyika Julai 31, 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim (Exim Tower), Dar es Salaam, umeadhimisha miaka sita ya ushirikiano kati ya taasisi hizo katika kukuza vipaji vya wanafunzi wa shule za sekondari nchini.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D'Souza, alisema benki hiyo inaamini kuwa uwekezaji kwa vijana ni msingi wa kujenga taifa lenye ushindani na maendeleo endelevu.

Alisema kupitia falsafa ya benki hiyo ya *"Ubunifu ni Maisha"*, Exim imeendelea kuwaunga mkono wanafunzi wenye vipaji vya ubunifu na kuwapa fursa ya kutumia sayansi na utafiti kutatua changamoto zinazozikabili jamii.

Kwa mujibu wa D'Souza, programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya baada ya kupokea miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya tathmini ya kitaalamu, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia yatakayofanyika Septemba 17, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Mwanzilishi Mwenza wa YST, Dkt. Gozbert Kamugisha, aliishukuru Benki ya Exim Tanzania kwa kuendelea kuisaidia taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka sita, akisema ushirikiano huo umeongeza zaidi ya udhamini wa kifedha.

Alieleza kuwa wataalamu wa benki hiyo wamekuwa wakishiriki moja kwa moja katika kutembelea shule, kutoa ushauri wa kitaalamu kwa walimu na wanafunzi pamoja na kusaidia kuboresha tafiti na miradi ya ubunifu.

Hata hivyo, Dkt. Kamugisha alisema YST bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa rasilimali fedha na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.

Alisisitiza kuwa maendeleo ya taifa hayawezi kufikiwa bila uwekezaji wa kutosha katika sayansi, teknolojia na ubunifu wa vijana, akibainisha kuwa mataifa yaliyopiga hatua yamefanikiwa kutokana na kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika tafiti na ugunduzi.

Kwa zaidi ya miaka 16, YST imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu, huku ushirikiano wake na Benki ya Exim ukiendelea kusaidia vijana kubuni suluhisho katika maeneo mbalimbali ikiwemo akili unde (AI), kilimo, afya, uhifadhi wa mazingira, usalama wa chakula na teknolojia za mawasiliano.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa HIfadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) jijini Dar es Salaam, Agosti 1, 2026.

Ataka Uwekezaji wenye Tija

Na Mwandishi Wetu - Dar eś Salaam 

Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imeelekezwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali ili kuhakikisha mfuko unaendelea kuwa imara, endelevu na wenye uwezo wa kutoa huduma bora kwa wanachama.

Amesema hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mfuko huo wa PSSSF iliyofanyika leo Agosti 1, 2026, PSSSF Commercial Complex, Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mhe. Sangu amesema jukumu kuu la bodi ni kusimamia shughuli za mfuko kama ilivyoainishwa katika Sheria ya PSSSF, kifungu cha 11 hususan katika maeneo makuu ya usimamizi ikiwemo huduma kwa wanachama, ukusanyaji wa michango, uwekezaji wa rasilimali za mfuko na ulipaji wa mafao.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa PSSSF jijini Dar es Salaam Agosti 1, 2026

Vile vile, amesisitiza kuwa katika kutekeleza majukumu hayo, bodi inapaswa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na miongozo ya Serikali pamoja na Mpango Mkakati wa PSSSF, ambao umeanza kutekelezwa pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Wajumbe mmeingia katika kipindi muhimu ambapo mfuko umeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano. Huu ndio utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa majukumu na kufanikisha malengo ya mfuko,” amesema.

Kadhalika, amewataka wajumbe kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao, akibainisha kuwa Serikali ina matarajio makubwa kwa PSSSF katika kuhakikisha mfuko huo unakuwa imara.

Kuhusu uwekezaji, Waziri alisema fedha za wanachama zinapaswa kuwekezwa kwa umakini na weledi ili kulinda thamani yake na kuhakikisha zinazalisha faida itakayowezesha mfuko kutimiza wajibu wa kulipa mafao kwa wakati, hata baada ya miongo kadhaa.

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo

“Fedha za wanachama zinawekwa leo kwa matarajio ya kulipa mafao miaka ijayo. Hivyo, ni muhimu ziwekezwe katika miradi yenye tija, salama na inayozingatia miongozo ya uwekezaji iliyowekwa na Serikali,” alisisitiza.

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo