TRENDING NOW






Na Mwandishi Wetu, Michezo

Nyota wa soka duniani, Cristiano Ronaldo, amezungumza kwa uwazi kuhusu hali yake ya kifedha, akisema licha ya kutajwa kuwa bilionea, bado anajiona “maskini” kwa sababu ya majukumu makubwa anayobeba kwa familia na jamii inayomtegemea.

Akihojiwa na mwandishi maarufu Morgan, Ronaldo alifichua kuwa alifikia hadhi ya kuwa bilionea akiwa na umri wa miaka 39, lakini bado anaendelea kutafuta fedha kwa bidii kila siku.

“Mwezi mmoja uliopita watu walisema mimi ni bilionea, lakini ukweli ni kwamba nilikuwa bilionea nikiwa na miaka 39,” alisema Ronaldo. “Ninaheshimu mali zangu, fedha zangu na kila kitu ninachomiliki. Nina HR wangu ambaye tunawasiliana mara mbili kwa siku — asubuhi na usiku — kujua nini kimeingia, kimepungua na nini cha kufanya kuongeza zaidi.”

Hata hivyo, Ronaldo alisisitiza kuwa pamoja na utajiri huo, bado hajitoshelezi kifedha kwa sababu ana wajibu mkubwa wa kusaidia watu wengi wanaomtegemea.

“Mimi ni baba, lakini pia nina jamii kubwa nyuma yangu. Kila mwezi nachangia zaidi ya milioni 450 za Tanzania kusaidia familia na watu wanaonihitaji. Hivyo, siwezi kusema nina pesa nyingi, maana bado nina kazi ya kutafuta zaidi,” alisema nyota huyo wa Al-Nassr.

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali, Ronaldo ndiye mchezaji anayelipwa zaidi duniani, akiwa na mkataba wa mamilioni ya dola kwa mwaka, lakini kauli yake imeonyesha upande wa utu na uwajibikaji wa kijamii unaokwenda mbali zaidi ya umaarufu na fedha.

Mashabiki wengi mitandaoni wameitafsiri kauli hiyo kama somo muhimu kuhusu unyenyekevu na kujituma, huku wengine wakisema Ronaldo amethibitisha kwamba “tajiri wa kweli ni yule anayejua kutumia utajiri wake kusaidia wengine.”
Kulikuwa na kijiji kimoja kilichoishi watu wema na wabaya kwa pamoja. Kijiji kilibarikiwa na mto ulioleta uhai kwa kila kiumbe. Ng’ombe walikunywa maji yale na kutoa maziwa matamu, lakini vilevile, nyoka walikunywa maji hayo hayo na kutengeneza sumu kali.
(Maji yaleyale anayokunywa ng’ombe kutengeneza maziwa, ndiyo hayo hayo anayokunywa nyoka kutengenezea sumu yake.)

Katika kijiji hicho, aliishi mzee mmoja mwenye mbwa aliyekuwa mwaminifu. Lakini siku moja, mbwa yule akaanza kumbwekea bwana wake kila alipomkaribia. Mzee akagundua kuwa jirani yake alikuwa amemzoesha kumpa mifupa kwa siri.
(Mbwa wako akianza kukubwekea, tambua kuna mtu mwingine anamlisha.)

Siku moja, mzee huyo aliona panya akimcheka paka wake shupavu. Alishangaa, lakini hakujua kuwa panya alikuwa amejificha karibu na shimo lake la kutorokea.
(Ukiona panya anamcheka paka, ujue yupo karibu na shimo.)

Baadaye, mbweha alifika nyumbani kwake kuomba msamaha baada ya kuiba vifaranga wawili. Kwa moyo wa huruma, mzee akamsamehe. Lakini haikupita muda, mbweha huyo akarudi tena — safari hii akaiba mbuzi wake mzima.
(Ukimsamehe mbwea kwa kukuchukulia vifaranga wako, kuna siku atakuibia mbuzi wako.)

Mzee alijaribu kumshawishi nyani wake wa shambani kwamba asali ni tamu kuliko ndizi, lakini nyani akacheka tu na kusema, “Hata tamu ya dunia, siwezi kuiacha ndizi yangu.”
(Huwezi kumshawishi ngedere asali ni tamu kuliko ndizi.)

Siku moja mzee alipokuwa akipita shambani, alikuta mzoga wa mbuzi wake kati ya mimea ya viazi. Wengi walidhani labda alikufa kwa njaa, lakini macho ya mzee yaliona zaidi — alijua kuwa kilichomuua kilikuwa sumu kutoka kwa nyoka aliyekunywa maji yale yale ya mtoni.
(Ukikuta mzoga wa mbuzi kwenye shamba la viazi, unapaswa kujua kilichomuua si njaa.)

Baadaye, tumbili walianza kumpigia makofi kila alipopita, wakimsifia kwa maneno matamu. Lakini ndani ya usiku ule ule, walimuangushia ndizi zake zote ardhini.
(Tumbili akikupigia makofi, ujue anakaribia kukuangushia ndizi zako.)

Mwishowe, mzee akaenda kumshauri kijana wa kijiji aliyekuwa anajulikana kwa ukaidi. Alimwambia, “Usisubiri hadi uharibifu ukufike ndipo usikie.” Lakini kijana hakusikia. Ilibidi apitie mateso ndipo ajifunze.
(Kenge huwa hasikii mpaka atokwe na damu masikioni.)

Ndipo mzee akakaa chini ya mti wa mwembe, akatazama mto ule ule, akatabasamu kwa uchungu na kusema:

“Maisha ni kama maji yale ya mtoni — yanamlisha ng’ombe na nyoka kwa pamoja. Uamuzi ni wako kama utakua wa kutoa maziwa au sumu.”
Na Mwandishi Wetu, Siaya

Mbunge wa eneo la Wantam, Mheshimiwa Nuru Maloba Okanga, ametoa heshima zake za mwisho kwa marehemu kiongozi wa kisiasa na mwanademokrasia mashuhuri, Baba Raila Amollo Odinga, akimtaja kama shujaa wa kweli aliyepigania haki, usawa na sauti ya wananchi wa kawaida.

Akizungumza baada ya kufanya ziara katika Shamba la Opoda lililopo Kaunti ya Siaya, Mheshimiwa Okanga alimshukuru Raila Junior kwa ukarimu na mapokezi mazuri waliyopokea wakati wa ziara hiyo ya kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.
“Natoa shukrani za dhati kwa Raila Junior kwa ukarimu wake na kuhakikisha tumepokelewa vyema tulipofika Opoda Farm kutoa heshima zetu za mwisho kwa Baba Raila Amollo Odinga,” alisema Mheshimiwa Okanga.

Amesema kuwa akiwa amesimama katika eneo la mapumziko ya milele ya Raila Odinga, alihisi uchungu mkubwa na kufahamu kuwa Kenya na dunia kwa ujumla zimepoteza kiongozi wa kipekee na mwenye misimamo thabiti.

“Niliposimama katika kaburi la Baba, nilikumbuka kuwa Kenya na dunia zimepoteza mwana wa haki wa kweli — kiongozi jasiri aliyesimama kwa ajili ya demokrasia na haki za mwananchi wa kawaida,” aliongeza.
Mheshimiwa Okanga alibainisha kuwa marehemu Raila alikuwa mtu wa umoja na aliamua kuunga mkono serikali ya sasa kwa nia njema ya kudumisha amani na mshikamano wa kitaifa, lakini yeye binafsi hawezi na hatakuwa tayari kuunga mkono serikali ya Rais William Ruto.

“Baba alikuwa mtu wa watu na alisimama pamoja nao kila wakati. Ingawa aliunga mkono serikali kwa sababu ya umoja wa taifa, mimi binafsi siungi na sitawahi kuunga mkono serikali ya Ruto. Moyo wangu na sauti yangu vinabaki na wananchi wa Wantam,” alisema kwa msisitizo.

Akihitimisha hotuba yake, Mheshimiwa Okanga alitoa salamu za rambirambi kwa familia ya Odinga na Wakenya wote, akisema kuwa ndoto ya marehemu Raila ya Kenya yenye haki, usawa na umoja itaendelea kuishi milele.

“Lala salama Baba. Ndoto yako ya Kenya yenye haki, usawa na umoja itaendelea kuishi vizazi na vizazi,” alisema Mheshimiwa Nuru Maloba Okanga kwa huzuni.

Na Mwandishi Wetu, Mombasa

Mwananchi wa Kisauni, Yusuf Garare, ameweka historia mpya baada ya kuvunja rekodi ya dunia ya Guinness kwa kuchoma nyama (barbecue) kwa muda mrefu zaidi duniani, akifikisha saa 87, dakika 10 na sekunde 30 bila kukoma.

Tukio hilo la kihistoria limefanyika katika eneo la Kisauni, Mombasa, likishuhudiwa na mamia ya wananchi, wadau wa chakula na wageni kutoka sehemu mbalimbali za Pwani ya Kenya, waliokusanyika kushuhudia safari hiyo ya kipekee.

Hadi kufikia muda huo, Garare alikuwa ameweka rekodi mpya ya “Longest Barbecue Marathon (Individual)”, akiipiku rekodi ya awali iliyoshikiliwa na mpishi kutoka nchi nyingine.
Akizungumza baada ya kumaliza zoezi hilo la zaidi ya siku nne mfululizo, Garare alieleza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya maombi, nidhamu na ushirikiano mkubwa kutoka kwa jamii ya Kisauni na wafuasi wake kote nchini.

“Nilijituma kwa moyo wote nikijua kwamba hii siyo tu kuhusu mimi, bali ni kuhusu Pwani na vijana wote wa Afrika Mashariki. Nimefanya hili kuonyesha kuwa tukiamua, tunaweza kufikia viwango vya dunia,” alisema Garare kwa furaha.

Kwa sasa, matokeo hayo yanatarajiwa kuthibitishwa rasmi na Guinness World Records, baada ya kupitia ushahidi wote wa muda, video na mashahidi wa tukio hilo.

Wakazi wa Mombasa na maeneo jirani wameelezea fahari yao kwa Garare, wakisema amekuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wanaotafuta mafanikio kupitia juhudi na ubunifu.

“Huu ni ushindi wa Pwani, ushindi wa Kenya na ushindi wa Afrika Mashariki,” alisema mmoja wa mashabiki wake.

Tukio hilo limeendelea kuwa gumzo katika mitandao ya kijamii, ambapo watu wengi wanampongeza Garare kwa kuonyesha moyo wa kujituma, uvumilivu na kujenga imani mpya kwa kizazi kipya cha vijana wajasiriamali.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Katibu wa Bunge, Baraka I. Leonard, amewataka wabunge wote wateule kufika Dodoma kuanzia Novemba 8 hadi 10, 2025 kwa ajili ya usajili na maandalizi ya kikao cha kwanza cha Bunge la Kumi na Tatu, kitakachofanyika Novemba 11, 2025.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa tarehe 5 Novemba 2025, kikao hicho kitajumuisha shughuli mbalimbali ikiwemo kusomwa kwa tangazo la Rais la kuitisha Bunge, uchaguzi wa Spika na Naibu Spika, kiapo cha uaminifu kwa wabunge wote, pamoja na uteuzi wa Waziri Mkuu.

Aidha, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atazindua rasmi Bunge jipya katika hafla itakayofanyika siku hiyo hiyo ya Novemba 11.

Wabunge wote wateule wametakiwa kufika wakiwa wamevaa mavazi rasmi na kuwasilisha nyaraka muhimu kama vile hati za kuchaguliwa, vitambulisho vya taifa, namba za akaunti za benki, vyeti vya ndoa (kwa walioo ama kuolewa), vyeti vya kuzaliwa kwa watoto walio chini ya miaka 21, vyeti vya elimu pamoja na wasifu binafsi (CV).

Kwa mujibu wa tangazo hilo, uchaguzi wa Spika na Naibu Spika utafanyika kujaza nafasi zilizotangazwa katika tangazo la Serikali Na. 1482A na 1482B la tarehe 4 Novemba 2025.
Dodoma, Tanzania — Mr. Sanjeev Mansotra, Chairman, Planet One Group today announced the launch of the Sanjeev Mansotra Foundation (SMF) in Tanzania, marking a significant milestone in its mission to help transform education in Africa. The Foundation’s inaugural initiative will fund the renovation and expansion of four schools in Dodoma, under the aegis of the City Council.

Founded by Sanjeev Mansotra, SMF is guided by a bold vision to ensure that education and health are no longer privileges, but universal rights. The Foundation is committed to strengthening educational institutions, promoting skills development, and improving the well-being of underserved communities.“The establishment of this Foundation is rooted in my firm belief that education is the cornerstone of a thriving national economy,” said Sanjeev Mansotra. “By expanding access to quality education, we empower individuals and lay the foundation for sustainable economic growth and prosperity.”

The launch comes at a critical juncture for education in Africa. A recent report by UNESCO, UNICEF, and the African Union reveals that while school enrollment has increased by 75 million since 2015, the number of out-of-school children has surged by 13.2 million, now exceeding 100 million. As it stands, four out of five African children aged 10 cannot read and understand a simple text. The report cites rapid population growth, humanitarian crises, and a massive annual education funding gap of US$77 billion as key barriers to progress.

Rural and marginalised communities are disproportionately affected, with secondary school completion rates among rural youth up to 20 percentage points lower than their urban peers.
Recognising these challenges, SMF’s work in Dodoma will include the construction of new classrooms, science laboratories, and libraries, alongside the provision of school uniforms, stationery, clean drinking water, and health camps for students and surrounding communities. These efforts are designed to bridge the urban-rural divide and create pathways to opportunity for future generations.

“By investing in infrastructure and essential resources, we aim to inspire students and teachers alike, boost enrollment, and improve learning outcomes,” Mansotra commented. 

The Foundation’s launch in Tanzania follows a formal invitation from the City Council of Dodoma, which oversees school education in the region. Local stakeholders have welcomed the initiative, offering full support and collaboration.

Looking ahead, SMF plans to expand its philanthropic initiatives to other African nations, including Ghana, Guinea, Togo, and Sierra Leone, as well as India.

“Our long-term vision is to serve as a catalyst for transformative change. We are deeply committed to nurturing the next generation by equipping them with education, skills, and aptitude they need to thrive. From imagination to impact, our mission is to ensure no one is left behind,” Mansotra concluded.