TRENDING NOW






KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda, amezindua mradi wa basi dogo wa kikundi cha vijana cha UNAMA, kinachotoa huduma ya usafirishaji wa abiria katika kijiji cha Picha ya Ndege, kata ya Vikindu wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Aprili 24, 2026, Mwang’onda amewapongeza vijana hao kurejesha fedha za mkopo na kuaminiwa kuongezewa fedha kiasi cha milioni 85.2, kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. 


Aidha amewahimiza vijana kote nchini kutumia kikamilifu fursa ya mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri, akieleza kuwa ni nyenzo muhimu ya kujikwamua kiuchumi na kujenga ajira binafsi.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega, ameeleza utekelezaji wa mikopo hiyo unatoa fursa halisi kwa vijana kujiajiri kupitia miradi yenye tija.

“Tunampongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo ya utoaji wa mikopo kupitia halmashauri, pamoja na kusisitiza ukusanyaji wa mapato ya ndani unaowezesha kutengwa kwa asilimia 10 kwa ajili ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu,” amesema Ulega.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Khadija Nasir, amesema jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi milioni 39.5 imepitiwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2026, baada ya kupokelewa kutoka Wilaya ya Kisarawe.

Kati ya Miradi hiyo ni usambazaji wa nishati safi ya kupikia, kiwanda cha vinywaji baridi cha Yaket International, ujenzi wa uzio wa Shule ya Sekondari Mwinyi, ujenzi wa boksi kalavati, pamoja na mradi wa maji katika kijiji cha Sotele.

Mwenge wa Uhuru umefikisha siku ya saba mkoani Pwani tangu ulipopokelewa Aprili 18, 2026, na unatarajiwa kuendelea na mbio zake Aprili 25, 2026 katika Wilaya ya Kibiti.

Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameihimiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kuendelea kuimarisha ushirikiano wake na viwanda ili kuongeza fursa za ajira na ujuzi kwa vijana nchini.

Wito huo umetolewa Aprili 23, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya ufundi wa aluminium na ufungaji wa vioo kwa wakufunzi pamoja na mafundi wa fani ya useremala.

Tukio hilo pia limeambatana na uzinduzi wa mtaala mpya wa mafunzo hayo unaoendeshwa na kampuni ya Emirates Aluminium Profile kwa kushirikiana na VETA, ukiwa na lengo la kuzalisha wataalamu wenye ujuzi unaohitajika katika soko la ajira.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Wanu alisema hatua hiyo inaendana na maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha rasilimali watu sambamba na kasi ya mabadiliko ya kiuchumi na teknolojia duniani.

“Ushirikiano kati ya vyuo vya VETA, sekta ya uzalishaji, waajiri na viwanda ni muhimu ili kuhakikisha wahitimu wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji halisi ya soko la ajira,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alisema mafunzo kwa wakufunzi ni hatua muhimu katika kuboresha ubora wa ufundishaji na kuongeza ushindani wa wahitimu katika soko la ajira.

Kasore alisema awamu ya kwanza ya mafunzo hayo imehusisha wakufunzi 18 wa fani ya useremala watakaopatiwa ujuzi wa vitendo unaohitajika viwandani.

Alifafanua kuwa washiriki hao watajengewa uwezo katika maeneo mbalimbali ikiwemo makadirio ya vifaa na gharama, uundaji wa miundo ya aluminium, ufungaji wa vioo, utengenezaji wa samani za chuma pamoja na ufungaji wa dari.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Emirates Aluminium Profile, Deogratius Marandu, alisema mafunzo hayo yataongeza thamani kwa mafundi na kuwapa utambuzi unaohitajika katika soko la ajira.

Marandu aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuwawezesha vijana kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Wadau wa elimu wameeleza kuwa ushirikiano kati ya VETA na sekta binafsi ni njia sahihi ya kuzalisha vijana wenye ujuzi wa kisasa unaoendana na mahitaji ya soko la ajira nchini

 

Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Dodoma

WAKAZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameendelea kupata huduma bora za afya katika Hospitali ya Jiji huku Bohari ya Dawa(MSD)ikiwezesha utolewaji wa huduma hizo kupitia vifaa tiba vya kisasa na dawa zote muhimu ilivyopeleka hospitalini hapo.
Kuanza kwa huduma kwa Hospitali hiyo imewezesha wakazi  wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapato 765,179 wakiwemo wanaume 373,440 na wanawake 391,739 kufurahia matunda ya hitaji ya sera ya mwaka 2009 ya kusogeza huduma karibu na wananchi ,hivyo kupitia fedha za halmashauri  na Serikali kuu ujenzi ulianza na sasa wananchi wanapata huduma za matibabu kwa raha mustarehe.

Kupitia ziara iliyoandaliwa na MSD kwa wahariri na waandishi wa habari Mganga Mfawindhi wa Hospitali ya Dodoma Dk.Joshua Mwalongo amesema hadi sasa jumla ya fedha ambazo zimepelekwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ni Sh.bilioni 2.8.

Kwa mujibu wa Dk.Mwalongo hospitali hiyo imekuwa na manufaa makubwa hasa ya kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi na tangu ilipoanza kutoa huduma Januari 20,2025 wananchi wameendelea kuongezeka siku hadi siku huku akisisitiza MSD imewezesha vifaa tiba vya kisasa kwa ajili ya matibabu mbalimbali.

Akifafanua kuhusu mradi huo amesema ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ulitokana na uhitaji wa wanachi kupata huduma za ngazi ya hospitali ya wilaya na hiyo ni kutokana na changamoto ya kukosa Hospitali ya Wilaya kwa muda mrefu.
“Pia ujenzi ulitokana na hitaji la sera ya Afya ya mwaka 2009 la kusogeza huduma karibu na wananchi hivyo kupitia fedha za Halmashauri na Serikali kuu, ujenzi wa hospitali hii ya Wilaya ulianza rasmi mnamo mwaka 2023,”amesema na kuongeza shilingi 100,000,000.00 zimetumika kununua vifaa tiba kutoka Bohari ya Dawa MSD.

Akieleza zaidi amesema hospitali hiyo hadi sasa ina majengo 10 ya kutolea huduma , na kuomgeza kwa mwezi wanahudumia wagonjwa 700

Katika kutambua mchango wa Serikali katika ujenzi wa hospitali hiyo Dk.Mwalongo amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa hospitali hiyo ambayo imepunguza msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na Hospitali ya Makole.

“Wananchi hawaendi huko wanakuja katika hospitali ya Wilaya na kwa kweli tunaishukuru MSD kwa kutuwezesha vifaa tiba vya kisasa pamoja na dawa zote muhimu ambazo tunazipata kwa wakati.Upatikanaji dawa kwetu ni zaidi ya asilimia 93.”

Awali Meneja MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema uwepo wa hospitali hiyo sambamba na na vifaa tiba vinavyosambazwa MSD itasaidia kutoka huduma za uhakika na kupunguza msomgamano katika hospitali nyingine huku akiwahakikishia watanzania MSD itaendelea kupeleka Dawa na vifaa tiba vya kisasa kwa wakati.

Pamoja na hayo jambo la kufurahisha zaidi hospitali hiyo kuanza kutoa huduma za matibabu kwa magonjwa mbalimbali pia imefungua fursa ya ajira kwa vijana wa kitanzania kwani idadi kubwa ya watoa huduma katika hospitali hiyo ni vijana zaidi ambao hivi sasa wanaenjoi kutoa huduma kwa vifaa tiba vya kisasa.Madaktari wanabofya tu.






Wadau mbalimbali wa elimu wakiwa katika mikutano na Wanafunzi wa baadhi ya Shule za wilayani Momba, ambapo maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yanafanyika.

MAADHIMISHO ya Juma la Elimu Kitaifa yanaendelea Mkoani Songwe ambapo TEN/MET na wadau wa Elimu nchini wametembelea shule ya wasichana ya Songwe, Wilayani Momba. Shule hiyo iliyoanza na wanafunzi 25 chini ya usimamizi wa mkoa, sasa imekua hadi kufikia idadi ya wanafunzi 161 na walimu 15 wenye dhamira thabiti ya kuinua elimu ya mtoto wa kike.

Akizungumza na wadau wa elimu, Mkuu wa Shule Bi. Janeth Mwamwile amesema kuwa kwa miaka minne mfululizo shule imepata ufaulu wa asilimia 100, na hivyo kung’ara katika ngazi ya wilaya, mkoa na hata taifa. Lakini pamoja na mafanikio hayo, amebainisha shule bado inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo za miundombinu kama nyumba za walimu, maabara, bwalo la chakula, mabweni, jengo la utawala, jiko hivyo kutoa wito kwa wadau wa sekta ya elimu kuwashika mkono ili kuchochea mafanikio hayo.

Kwa upande wa Mtandao wa Elimu Tanzania @tenmet Bi. Martha Makala, Mratibu wa Mtandao), amesisitiza umuhimu wa kusaidia wasichana ili waweze kutimiza ndoto zao akitolea mfano wa Elimu yake aliyoipata kutoka shule ya wasichana kama chachu ya kufanikiwa maishani. Aidha, Bi. Makala ameahidi kuwa changamoto zilizobainishwa zimepokelewa na zitachakatwa ili kuona namna wadau wa TEN/MET wanavyoweza kushirikiana katika utatuzi wake.
Usione aibu kupambana kutafuta maisha halali. Watu watasema, watacheka na kukubeza, lakini hakuna hata mmoja wao atakayelipa bili zako. Endelea kujituma, kuwa na nidhamu, na amini safari yako. Mafanikio huja kwa wanaothubutu kusonga mbele licha ya kelele za watu.

WAKAZI zaidi ya 600 wa Dar es Salaam wamepewa siku 14 kulipa madeni ya pango la ardhi ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria.Kamishna Msaidizi wa Wizara ya Ardhi Mkoa huo, Shukrani Kyando, amesema hayo leo Aprili 24,2026  ambapo amesema kuwa wadaiwa hao tayari waliwahi kupewa notisi ya zaidi ya miezi mitatu pamoja na kukumbushwa mara kadhaa bila mafanikio.

“Kabla ya kufikia hatua ya kuwafikisha mahakamani, wizara imefuata taratibu zote za kibusara kwa kuwapa wadaiwa muda wa siku 14, siku 90, na sasa imeongeza tena siku 14 kuanzia Aprili 24, 2026.”

Kwa mujibu wa Kyando, yeyote atakayeshindwa kulipa ndani ya muda huo atafikishwa mahakamani kujibu mashitaka kwa mujibu wa sheria.
Amesisitiza kila mmiliki wa ardhi ana wajibu wa kulipa pango la ardhi kwa wakati, na kushindwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha kupoteza haki ya umiliki pamoja na kukosa sifa za kupata mikopo.

“Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na lengo la kukusanya shilingi bilioni 83, lakini hadi sasa zimekusanywa takribani shilingi bilioni 63, hali inayochelewesha kufikiwa kwa malengo ya asilimia 100.”
Kwa upande wake, Mratibu wa Kodi Mkoa huo, Alfred Thomas, amewataka wananchi kulipa kodi kwa wakati ili kulinda haki zao za msingi katika umiliki wa ardhi.
Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi na Naibu Waziri wa nishati Mhe. Salome Makamba wakiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania. Bi. Fatma Abdallah pamoja na Mkuu wa Idara ya Sheria na Mahusiano wa Puma Energy, Bw. Emmanuel G. Bakilana

Mr. Saviour Chibiya (third from right), Absa Bank East Africa Regional Executive, engaged in a strategic discussion with Mr. Rumisho Shikonyi (third from right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during his courtesy visit to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. He was accompanied by Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second from right), along with members of the executive committee. The engagement centered on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Obedi Laiser (third from left), Managing Director of Absa Bank Tanzania, engages in conversation with Mr. Rumisho Shikonyi (right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during a courtesy visit by Mr. Saviour Chibiya (second from left), Absa’s East Africa Regional Executive, to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. The meeting focused on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Mr. Saviour Chibiya (left), Absa Bank East Africa Regional Executive, listens attentively to Mr. Rumisho Shikonyi (right), Country Manager of Watu Credit Tanzania, during his courtesy visit to the asset finance company in Dar es Salaam yesterday. He was accompanied by Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second from left), along with members of the executive committee. The engagement centered on strengthening collaboration, unlocking new opportunities, and driving sustainable growth across the region. Mr. Chibiya is currently in Tanzania on his official working visit.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na The Runners Club, imezindua rasmi mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zinazotarajiwa kufanyika Mei 17 mwaka huu jijini Dar es Salaam, huku zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakitarajiwa kushiriki.

Tukio hilo linalozidi kujizolea umaarufu kila mwaka, linalenga kuhamasisha mazoezi ya mwili, kukuza mshikamano wa kijamii pamoja na kuendeleza mtindo wa maisha yenye afya miongoni mwa Watanzania.

Kwa mujibu wa waandaaji, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na makundi matatu ya mbio ambayo ni kilomita 21.1 (Nusu Marathon), kilomita 10 na kilomita 5, yakitoa fursa kwa washiriki wa rika na viwango tofauti kushiriki.

Usajili wa kushiriki mbio hizo tayari umefunguliwa kupitia majukwaa rasmi, ambapo wakimbiaji wa kada zote, kuanzia wanariadha wakongwe hadi wapenda mazoezi na washiriki wa burudani, wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisema mbio hizo ni zaidi ya mashindano ya riadha, bali ni jukwaa muhimu la kuimarisha afya na ustawi wa jamii.

“Katika Absa, tunaamini katika kuleta athari chanya katika jamii tunazozihudumia. Absa Dar City Marathon siyo tu mbio, bali ni jukwaa linalokuza afya, umoja na ustawi wa jamii,” alisema Luhanga.

Aliongeza kuwa benki hiyo inajivunia kushirikiana na The Runners Club katika kuandaa tukio hilo na kuhimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki katika mazoezi ya mwili.

Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo na Makamu wa Rais wa The Runners Club, Godphrey Mindu, alisema marathon hiyo inaonesha ukuaji wa kasi wa utamaduni wa kukimbia nchini.

“Tumeshuhudia jamii zikikusanyika kupitia mazoezi ya viungo, na tukio hili ni sherehe ya mshikamano huo. Tunatarajia kuwapokea wakimbiaji wa viwango vyote na kuwapatia uzoefu bora siku ya mashindano,” alisema Mindu.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Felix Donald, alisema mbio hizo zina mchango mkubwa katika kukuza vipaji vya wanariadha chipukizi pamoja na kuimarisha nidhamu na afya kwa jamii.

“Matukio kama haya ni msingi wa kukuza riadha nchini. Tunayaunga mkono kwa sababu yanasaidia kujenga kizazi kipya cha wanamichezo,” alisema Donald.

Wawakilishi kutoka vilabu mbalimbali vya kukimbia walisisitiza kuwa tukio hilo limekuwa kiunganishi muhimu cha jamii. Johnson Mbunda “Balozi” kutoka Goba Roads Runners alisema marathon hiyo inawaunganisha wakimbiaji kutoka maeneo mbalimbali na kuwajengea urafiki wa kudumu.

Kwa upande wake, mwanachama wa Kigamboni Runners alisema tukio hilo limekuwa sehemu ya mkusanyiko wa kila mwaka unaowapa fursa washiriki kuungana na marafiki, familia pamoja na kukutana na watu wapya huku wakifurahia mandhari ya jiji la Dar es Salaam.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wanachama wa vilabu mbalimbali vya kukimbia ikiwemo Tabata Runners, TOT Runners, Absa Running Club, Salasala Runners na Kigamboni Runners, pamoja na wadhamini wa tukio hilo.

Ushiriki wao umeendelea kuonesha kukua kwa kasi kwa utamaduni wa kukimbia nchini na mshikamano mkubwa wa jamii katika kuunga mkono jitihada za kukuza afya kupitia michezo.

Watu kadhaa wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana uso kwa uso na lori katika eneo la Mlima “S”, kijiji cha Lumango, wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Ajali hiyo ilihusisha basi la kampuni ya ZL Super Safari lililokuwa likitoka Ifakara kuelekea Morogoro, pamoja na lori lililokuwa limebeba kokoto.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa lori aliyekuwa akijaribu bajaji iliyokuwa mbele yake, hali iliyosababisha kugongana na basi hilo.

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ili kuzungumzia tukio hilo zinaendelea.