Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.













Mkuu wa Mkoa wa Tanga akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa zao hilo katika Mtaa wa Sahare Kijijini Kata ya Mzingani Jijini Tanga ambao pia alizungumza na wakulima wa zao hilo kwenye wilaya za Tanga,Mkinga ,Muheza na Pangani ikiwa ni kuelekea Shamrashamra za kuelekea miaka 60 ya Muungano.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitembea kuelekea baharini kuangalia kilimo cha Mwani wakati wa ziara yake ya kuwatembelea wakulima hao.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitoka kukagua zao la Mwani wakati wa ziara yake.
Afisa Mfawidhi Idara ya Ukuzaji wa Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mkoa wa Tanga Omari Ally Mohamed akieleza jambo wakati wa ziara hiyo.

Na Oscar Assenga, TANGA.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wanunuzi wa zao la mwani mkoani humo kuheshimu mikataba wanayoingia na wakulima ili waweze kulima kwa tija na hivyo kuweza kujikwamua kimaendeleo.

Amesema kutokuheshimu mikataba hiyo hawatakubali kuona linatokea badala yake wataona namna ya kufatuta njia nyengine za kuwahudumia ikiwemo mabenki kwa ajili ya kuwawezesha kupata mikopo yenye riba ndogo na nafuu.

RC Batilda aliyasema hayo wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa zao hilo katika Mtaa wa Sahare Kijijini Kata ya Mzingani Jijini Tanga ambao wametokea kwenye wilaya za Tanga,Mkinga ,Muheza na Pangani ikiwa ni kuelekea Shamrashamra za kuelekea miaka 60 ya Muungano.

Ambapo pia alitembelea shamba la wakulima wa Mwani pamoja na kugawa kofia,mabuti ,nyundo,kamba na taitai ili kuweza kuwawezesha wakulima hao wa mwani kutekeleza vema shughuli zao za kila siku .

Alisema kwasababu haiwezekani wanunuzi wa zao hilo wanaingia mikataba na wakulima lakini wanashindwa kutoa vifaa, kutokuwahudumia wala kutoa pembejeo kitendo ambacho kinapelekea wakulima kuhangaika bila kujua kamba wanatoa wapi.

“Hii haiwezekani mkulima wa mwani anakopa hii sio sawa unamuumiza mkulima kutokana na kwamba wanafanya kazi kubwa yenye tija lakini kama mkipata mwekezaji mzuri mtaweze kujikwamua kiuchumi nimewaelekeza Jiji na nitaongea na Waziri wa Uvuvi aweze kuona namna ya kuwasaidia tupate boti”Alisema

“Lakini niwaambie wanunuzi kama hii kazi imewashinda tutavunja mikataba tuweze kujua wakulima wetu tunawahudumiaje tuwaitea mabenki waje watoe mikopo kama benki ya kilimo TIDB wanatoa mikopo yenye riba ndogo sana chini ya asilimia 4 mpaka 3waweze kuwakopesha waweze kununua kamba,taitai,troliki waweze kufanya kazi kwa tija yenye faida” Alisema.

Aidha Mkuu huyo wa mkoa alisema Wizara ya Uvuvi watashirikiana nao kwenye suala la masoko huku akimpongeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Ulega kwa kuanzisha stakabadhi ghalani kama ilivyo mazao mengine ya kilimo.

Alisema mfumo huo utawezesha za la Mwani kuwekwa kwenye stoo utapigwa mnada na watapata bei ya soko kuliko ilivyokuwa bei ya sasa ambao madalali wanapanga bei wanayotaka jambo ambalo linawaumiza wakulima wengi.

“Nimetembelea Shamba la Mwana nimeona changamoto hawana vifaa vya kubebea mwani kutoka baharini mpaka nchi kavu ,hawana chombo wanatumia kama boya mpaka kufika pwani hiyo ni kazi kubwa ina tija hivyo nimewaekeza jiji nitaongoea pia na Waziri wa Uvuvi awasaidie mpate (faiba) boti hata ndogo milioni 15”Alisema

“Ndugu zangu hapa nimesikia mnachangamoto ya Kamba kazi hii bila kuwa navyo itakuwa ni ngumu hivyo nitawasaidia milioni 3 (3000, 000) kwa ajili ya kununua kamba taitai ili msimu utaoanza mwezi wa saba usipite bila kuwa nazo”Alisema RC huyo.

“Lakini lazima tuhakikishe kwanza tunakwenda na kauli mbiu ya Rais Dkt Samia Suluhu na Rais za Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi ya uchumbi wa bluu kwa Mkoa wa Tanga tuliokuwa nao ni zao la mwani na ufungaji magongoo bahari na kwenda kwenye ufungaji wa pweza,kaa na majongoo bahari, chaza, kamba”Alisema RC

Hata hivyo katika kuhakikisha analitilia mkazo zao hilo ,RC Batilda alisema kwamba Aprili 29 mwaka huu atakuwa na viongozi wa wavuvi na viongozi makampuni yanayonunua mwani ili kuweza kuweka mikakati ya namna ya kuweza kuhakikisha wakulima wanaendelea kupata tija. Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alitumia wasaa huo kueleza kwamba vitu ambayo atasimama navyo ni kuhakikisha wanavidhibiti uvuvi haramu huku akiwaonya wanaojihusisha na uvuvi haramu kuachana nao.
Stanley Kafu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, akizungumza wakati wa mahafali ya pili ya mpango endelevu wa kuwainua kiuchumi wanawake wajasiriamali ujulikanao kama WEP yaliyofanyika tarehe 23 Aprili, 2024, Mjini Arusha.
Mshindi wa kwanza Beatrice Alban Msafiri (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Mshindi wa tatu Rukia Said Mohamed (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Mshindi wa pili Catherine Assenga (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Washindi na baadhi ya washiriki wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Exim Bank wakati wa mahafali ya kumaliza mafunzo ya biashara, ujasiriamali, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali. Mafunzo hayo yalitolewa na Exim Bank chini ya mpango wake wa Kuwainua Kiuchumi Wanawake (WEP) na mahafali hayo yamefanyika tarehe 23 Aprili, 2024 mjini Arusha.
---
Exim Bank, kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi Wanawake (WEP), imetoa mafunzo kuhusu masuala ya ujasiriamali, biashara, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali kama sehemu ya kuunga mkono ujumuishwaji wa watu wote, wakiwemo wanawake, katika mipango mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania.

Kupitia mpango wake wa ‘Exim Cares’, mwaka jana (2023) Exim Bank ilizindua Mpango wa Kuwakwamua Kiuchumi Wanawake ujulikanao ‘Women Empowerment Program (WEP)‘ wenye lengo la kuongeza ushirikishwaji na kuleta usawa kwa wanawake barani Afrika, hasa katika nchi ambazo zina matawi ya benki hiyo ikiwemo Tanzania, Comoros, Djibouti na Uganda.

Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu, anasema, “Ukiwa mwaka wa pili mfululizo wa mpango wa Kuwakwamua Wanawake Kiuchumi (WEP), Exim Bank tunafuraha kubwa kuwa sehemu ya mafanikio haya na tunawapongeza washiriki wote kwa kuanza na kumaliza salama mafunzo haya kuhusu ujasiriamali, uwezeshaji, na biashara.”

Washindi watatu, wa awamu hii ya kwanza mwaka huu, walipata zawadi za pesa taslimu zilitolewa kwa washindi watatu ambapo mshindi wa kwanza, Beatrice A. Msafiri, akizawadiwa kiasi cha TZS 8,000,000, mshindi wa pili, Catherine Assenga akipata TZS 5,000,000 na mshindi wa tatu, Rukia S. Mohamed akiondoka na TZS 3,000,000. Pia, wahitimu wote walipata fursa ya kuweza kupata mikopo bila riba kutoka Exim Bank ili waweze kujiendeleza kiuchumi.

Exim Bank inaamini uwezeshaji wa wanawake na ujasiriamali unabaki kuwa sehemu muhimu ya mipango ya maendeleo nchini Tanzania na barani Afrika kijumla. Hii inadhihirishwa na ongezeko la idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi katika sekta mbalimbali kama siasa, kijamii na kiuchumi.

Akielezea kuhusu malengo ya mradi, Kafu alisema, “Mpango huu utakuwa ni endelevu kwa muda wa miaka mitano na tunatarajia kuwafikia wanawake zaidi ya 600,000 ifikapo mwaka 2028.”

Kafu anasisitiza kuwa Mpango wa WEP ni sehemu ya mkakati mkubwa na wa kina unaolenga kutengeneza jukwaa la wanawake ili waweze kufanikiwa na kustawi katika maisha yao, hasa kwenye eneo la uchumi.

Exim Bank imekuwa na itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo kwa Watanzania wote. Programu hii inawiana na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na itakuwa chachu katika kuimarisha ustawi wa kijamii na kiuchumi kwa wanawake.

Mkurugenzi wa Lamata Village entertainment, Bi. Leah Mwendamseke ‘Lamata’ akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA (Ukweli Upe Muda) itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.
Akizungumza leo Aprili 23, 2024 katika Uzinduzi wa app mpya ya VTV ambapo ndani yake unaweza kustream tamthilia mpya kabisa ya EZRA inayoandaliwa na kampuni ya Lamata Village entertainment, Lamata amesema kuwa tamthilia EZRA ndani yake kuna visa na mikasa, story ya aina yake ambayo itawaacha watazamaji na wasikilizaji mdomo wazi huku ukitaka kujua yaliyojiri.

Pia alitoa shukrani zake za kipekee kwa Uongozi wa Bodi ya Filamu kwa kushirikiana nao katika uzinduzi huo, huku akiwamwagia maua ya pekee kwa Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kuweza kuwashika mkono na kufanikisha kazi hiyo.Mshehereshaji Bw. Evance Bukuku akizungumza katika halfa ya uzinduzi wa Tamthilia ya EZRA na app ya VTV.Kwa upande wao Vodacom Tanzania wamewaalika watazamaji kuweza kupakua app ya VTV ili kuweza kuiona tamthilia hiyo kidijitali zaidi.

Usibaki nyuma! pakua app ya VTV leo google play au Appstore ufaidi mchapo mzima wa Ezra na burudani nyingine mbalimbali.

Wageni waalikwa.
Meneja wa Lamata Village entertainment, Bw. Danny Nyalusi akitoa machache.
Waigizaji waliopo katika tamthilia ya EZRA.
Viongozi mbali mbali wakiwa na waigizaji.
Wasanii mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.