

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.
Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.
Jaji Mwambegele pia amewasisistiza watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .
Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.
Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.
DAR ES SALAAM — An atmosphere of pride,
academic excellence and national prestige filled Mlimani City Hall on
May 25, 2026, as the University of Dar es Salaam (UDSM) conferred
degrees to 876 graduates, including 94 new PhD holders, during Cluster I
of its 56th Graduation Ceremony.
The ceremony, presided over by
the University Chancellor and former President of Tanzania, Dr. Jakaya
Mrisho Kikwete, reaffirmed UDSM’s position as one of Africa’s leading
centres of research, innovation and intellectual leadership.
The
94 doctoral graduates came from 15 academic disciplines, reflecting the
University’s growing role in producing highly skilled researchers,
innovators and professionals capable of contributing to national
transformation and global development.
Unlike the lively
celebrations commonly associated with undergraduate graduations, the PhD
ceremony carried an atmosphere of academic maturity and scholarly
prestige. Dressed in elegant academic regalia, the graduates proudly
crossed the stage, symbolizing years of sacrifice, resilience, rigorous
research and dedication.
Speaking during the ceremony, Chancellor
Kikwete urged graduates to use their education and research to solve
societal challenges and contribute to national development.
“Your
education must become a tool for bringing positive change to society.
The knowledge and expertise you have acquired should help drive
innovation, leadership and transformation for the benefit of Tanzania
and the wider global community,” said Dr. Kikwete.
He further
emphasized the importance of research and knowledge creation in shaping
Africa’s future, noting that universities must continue producing
scholars capable of providing evidence-based solutions to emerging
challenges.
UDSM Vice Chancellor, Prof. William A. L. Anangisye,
described the graduation ceremony as a reflection of the University’s
continued growth in teaching, research, innovation and international
competitiveness.
Presenting the University’s annual progress
report, Prof. Anangisye revealed that UDSM currently has 235 researchers
ranked among Tanzania’s top 1,000 researchers according to the AD
Scientific Index 2026. This represents 23.5 percent of all top
researchers across 50 institutions nationwide.
He added that the
University has continued strengthening academic quality and labour
market relevance through curriculum reforms, with 285 undergraduate and
postgraduate programmes reviewed based on stakeholder feedback and
changing market demands.
Prof. Anangisye also highlighted major
achievements in innovation and research commercialization. During the
2025/2026 academic year, UDSM researchers and innovators registered six
patents through BRELA, some involving student innovators.
The
registered innovations include technologies for bioethanol production,
mushroom cultivation using sisal waste, organic fertilizer production,
protein feed development using Black Soldier Fly larvae, and wine
production from bamboo juice.
“These achievements demonstrate
UDSM’s ability to add value to local resources, promote the green
economy and use science to provide practical development solutions,”
said Prof. Anangisye.
The Vice Chancellor further revealed that
through the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project,
the University is currently constructing 21 new buildings and
renovating three others, a move expected to increase student capacity by
4,812 spaces.
He added that UDSM has also expanded digital
learning infrastructure by increasing internet capacity, digitizing more
than 1,000 courses and providing short-term professional training to
nearly 3,000 staff members.
Addressing graduates directly, Prof. Anangisye reminded them that education is both a privilege and a responsibility to society.
“Education
is not merely a personal achievement or decoration. It is a
responsibility and a debt to the nation. Use the knowledge you have
acquired to serve society, create opportunities and contribute to
national development,” he said.
He encouraged graduates to
embrace innovation, entrepreneurship and opportunities within the
digital economy, especially in situations where formal employment
opportunities may not immediately be available.
One of the most
inspiring moments of the ceremony was the graduation of Dr. Paul Msoka, a
visually impaired scholar who earned a PhD in Education after
previously completing both his Bachelor’s and Master’s degrees within
the UDSM system.
Dr. Msoka’s achievement stood out as a powerful
testimony to resilience, determination and the University’s commitment
to inclusive education and equal access to academic opportunities.
A
researcher specializing in inclusive education and visual impairment
studies, Dr. Msoka has contributed scholarly work focused on improving
learning opportunities for students with visual impairment in Tanzania’s
inclusive schools.
His achievement inspired many graduates,
lecturers, family members and guests attending the ceremony,
particularly young Tanzanians living with disabilities who aspire to
pursue higher education and professional excellence.
Throughout
the ceremony, emotional moments unfolded as graduates celebrated with
supervisors, colleagues, friends and family members. Smiles, embraces
and photographs reflected years of perseverance, sacrifice and academic
dedication behind every success story.
Established in 1961, the
University of Dar es Salaam remains Tanzania’s premier institution of
higher learning and a symbol of academic excellence. Over the decades,
the University has produced influential leaders, policymakers, scholars,
diplomats, entrepreneurs and professionals who continue shaping
Tanzania, Africa and the wider world.
For the Class of 2026, the
graduation ceremony marked not only the completion of an academic
journey, but also the beginning of a new chapter of leadership,
innovation and national service.
As celebrations continued
outside Mlimani City Hall, one message remained clear — the future of
Tanzania’s intellectual, scientific and developmental transformation
continues to be shaped at the University of Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido
Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao
katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja
ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na
maendeleo ya taifa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando
amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo
vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea
kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma.
“Tukitazama baadhi
ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni,
mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari
wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika
jamii ya Watanzania,” amesema.
Amesisitiza kuwa vyombo vya habari
vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa
kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na
yanalinda maslahi ya taifa.
“Tunachosimamia ni kuhakikisha
Mwandishi wa Habari anayepata ithibati anakuwa na kiwango cha elimu
kisichopungua Diploma, lakini tunataka pia Waandishi wa Habari waendelee
kupata mafunzo ili waweze kuimarika zaidi kitaaluma,” amesema.
Amesema
ipo haja ya sekta ya habari kutafakari aina ya maudhui yanayopewa
kipaumbele, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika
kujenga fikra na mwelekeo wa jamii.
Na Mwandishi Wetu, Michuzi TvMBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Mariam Ibrahim amemshuru Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa , Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kupendekeza jina lake na Kamati Kuu ya chama hicho kulipitisha na hatimaye kushinda kwa kura nyingi.
Ametoa
shukrani hizo kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Dk.Samia Suluhu Hassan
alipokuwa akisalimia viongozi mbalimbali wa Chama hicho wakati wa Semina
ya Uongozi na Maendeleo kwa madiwani wote wanawake wa Mkoa wa Pwani.BABATI — Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Babati mkoani Manyara imesitisha kusikiliza kesi ya jinai namba 291 ya mwaka 2026 iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini, Paulina Gekul, inayomkabili Brayton Lucas (17), baada ya kujiridhisha kuwa mshtakiwa huyo ni mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 18 na hivyo shauri hilo linapaswa kusikilizwa katika Mahakama ya Watoto kwa mujibu wa sheria.
Uamuzi huo ulitolewa baada ya Wakili wa upande wa utetezi, Thadei Lister, kuiomba mahakama kujiridhisha kuhusu umri wa mshtakiwa kwa kuwasilisha nyaraka mbalimbali ikiwemo cheti cha kuzaliwa kilichoonesha kuwa Brayton alizaliwa Novemba 12, 2008 na kwa sasa ana umri wa miaka 17 na miezi sita, tofauti na taarifa zilizokuwa katika hati ya mashtaka zilizomtaja kuwa na miaka 19.
Mahakama pia ilielezwa kuwa mtoto huyo alikuwa amechanganywa katika shauri moja na watuhumiwa watu wazima, jambo ambalo upande wa utetezi ulidai ni kinyume na sheria zinazolinda haki za mtoto.
Baada ya kupitia nyaraka zilizowasilishwa, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Babati, Ahmed Mgodo, alisema mahakama imejiridhisha kuwa Brayton Lucas ni mtoto na hivyo haina mamlaka ya kuendelea kusikiliza kesi hiyo. Kutokana na uamuzi huo, mahakama ilisimamisha shauri hilo dhidi ya mshtakiwa huyo na kuagiza polisi kuandaa hati mpya ya mashtaka kwa mujibu wa sheria zinazohusu watoto.
Brayton Lucas alipatiwa dhamana huku washtakiwa wawili wengine wakiendelea kushikiliwa. Wakili Thadei Lister amesema wako tayari kuendelea kumtetea mtoto huyo iwapo atafikishwa katika Mahakama ya Watoto.
Mama mzazi wa Brayton alisema mtoto wake alitakiwa kuwa shuleni baada ya kumaliza kidato cha nne na tayari alikuwa amepangiwa shule, lakini aliondoka nyumbani bila kutoa taarifa na baada ya juhudi za muda mrefu za kumtafuta walipata taarifa kuwa alikuwa Babati akifanya kazi.
Aidha, Digna amesema Brayton ni miongoni mwa watoto 16 kutoka kata hiyo waliotoroka shule, huku akisisitiza umuhimu wa jamii kushirikiana kuhakikisha watoto wanarudi katika mfumo wa elimu na kupata ulinzi unaostahili

Na Jawadu Kinyobwa WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa viongozi waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
Akizungumza Mei 15, 2026 katika Mahafali ya Tisa ya Taasisi hiyo yaliyofanyika katika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Mhe. Ridhiwani alisema dunia ya sasa inahitaji viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi ya wananchi.
Alisema uadilifu ni sifa muhimu ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo wahitimu wanapaswa kutumia maarifa na ujuzi walioupata kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwazi na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa viongozi wenye uzalendo. Tukumbuke msemo
wa wahenga kwamba adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti
mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za umma,”
alisema Ridhiwani.
Aidha, aliwataka wahitimu hao kulinda
rasilimali za taifa na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika maamuzi
yao ya kila siku ili kusaidia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi
nchini.
Alisema Tanzania inahitaji viongozi waaminifu na wenye
uwajibikaji ambao watatumia nafasi zao kuendeleza ustawi wa wananchi na
kuimarisha misingi ya utawala bora. 
Sambamba na hilo, Waziri
Ridhiwani alisema uongozi unaozingatia haki na uwazi utaendelea
kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya
nchi.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu
wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo alisema taasisi hiyo imetimiza
miaka 15 tangu kuanzishwa kwake rasmi Julai mwaka 2010 kwa Hati ya Rais
kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu kwa ajili ya kujenga na
kuimarisha viongozi barani Afrika.
Alisema kwa kipindi hicho,
taasisi hiyo imefanikiwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi, kuandaa
mijadala ya kisera pamoja na kufanya tafiti na machapisho yaliyosaidia
kukuza maarifa ya kiuongozi.
Kwa upande wake, akizungumza kwa
niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed alisema mafunzo hayo
yamewajengea uwezo mkubwa wa kiuongozi na kuwasaidia kufanya maamuzi
yenye tija kwa taasisi na jamii.
Alisema mahafali hayo hayakuwa
tu hitimisho la mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko makubwa ya
kiuongozi na maendeleo binafsi waliyoyapata ndani ya miezi sita ya
programu hiyo.































