Articles by "HABARI ZA KIJAMII"
Showing posts with label HABARI ZA KIJAMII. Show all posts

Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema uhuru wa uhariri ni nguzo muhimu katika taaluma ya habari na unapaswa kulindwa ili vyombo vya habari viweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwajibikaji na kwa maslahi ya umma.

Akizungumza Mei 26, 2026 katika mahojiano maalum yaliyofanyika katika Ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, Wakili Kipangula alisema hakuna mtu anayepaswa kuingilia maamuzi ya uhariri wa chombo cha habari, awe ni chanzo cha taarifa, mmiliki wa chombo, mwanasiasa au mtu mwingine yeyote mwenye maslahi binafsi.

Alisema uhuru huo unapaswa kuendana sambamba na uwajibikaji wa kitaaluma, huku akisisitiza kuwa maadili ya taaluma ya habari yanamtaka mwandishi kufanya kazi kwa uadilifu, bila upendeleo na kuhakikisha taarifa zote zinathibitishwa kabla ya kuchapishwa au kurushwa.

“Ukweli ndio mlinzi wa taaluma ya habari. Mwandishi anatakiwa kutoa taarifa ambazo amezithibitisha na ana uhakika nazo kwa sababu jamii inategemea kupata taarifa sahihi na kwa wakati ili iweze kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo,” amesema Wakili Kipangula.

Aidha, alisema waandishi wa habari wana nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye uelewa, mshikamano na maendeleo, hivyo ni muhimu kutumia uhuru wa habari kwa kuzingatia sheria, maadili ya taaluma pamoja na kuheshimu haki na uhuru wa wengine kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.

Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri, Bw. Deodatus Balile, alisema uhuru wa vyombo vya habari utakuwa na maana halisi pale vyombo hivyo vitakapokuwa na uwezo wa kiuchumi wa kujiendesha bila kutegemea ushawishi wa nje.

“Uhuru wa vyombo vya habari utakuwa uhuru wa kweli pale vyombo vya habari vitakapokuwa na nguvu ya kiuchumi,” amesema Balile.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.



Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele akizungumza wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani waogozaji Wapiga Kura katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe.Jacobs Mwambegele amewataka watendaji wa uchaguzi ambao ni Makarani waongozaji Wapiga kura kufanya kazi yao kwa kufuata Sheria, Kanuni na utaratibu wakati wa uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.

Jaji Mwambegele ameyasema hayo wakati akitembelea mafunzo ya siku moja kwa Makarani hao waogozaji katika Jimbo la Isimani yaliyofanyika katika Shule Sekondari Ufundi Ifunda mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi huo utakaofanyika Jumatatu ya Juni 1, 2026.

Jaji Mwambegele pia amewasisistiza watendaji hao kuishi kwenye viapo vyao wakati wa utekelezaji majukumu yao ya Uchaguzi ili kujiepusha na upendeleo wa aina yoyote.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mafunzo hayo ya Makarani Waongozaji Wapiga Kura Vituoni Bw. Baraka Matonya amemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwamba watafuata sheria, kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume wakati wote wa Utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi .

Naye Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno amesema maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.

Uchaguzi huo utafanyika sambamba na uchaguzi mdogo katika kata 12 za Tanzania Bara ambazo ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.



Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Isimani,Bi. Caroline Otieno akizungumza na kusema kua maandalizi ya uchaguzi huo Mdogo wa Jimbo hilo, yamekamilika kwa asilimia 100 ambapo vifaa vyote vimepokelewa.
By Zamda George, CMU

DAR ES SALAAM — An atmosphere of pride, academic excellence and national prestige filled Mlimani City Hall on May 25, 2026, as the University of Dar es Salaam (UDSM) conferred degrees to 876 graduates, including 94 new PhD holders, during Cluster I of its 56th Graduation Ceremony.

The ceremony, presided over by the University Chancellor and former President of Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, reaffirmed UDSM’s position as one of Africa’s leading centres of research, innovation and intellectual leadership.

The 94 doctoral graduates came from 15 academic disciplines, reflecting the University’s growing role in producing highly skilled researchers, innovators and professionals capable of contributing to national transformation and global development.

Unlike the lively celebrations commonly associated with undergraduate graduations, the PhD ceremony carried an atmosphere of academic maturity and scholarly prestige. Dressed in elegant academic regalia, the graduates proudly crossed the stage, symbolizing years of sacrifice, resilience, rigorous research and dedication.

Speaking during the ceremony, Chancellor Kikwete urged graduates to use their education and research to solve societal challenges and contribute to national development.

“Your education must become a tool for bringing positive change to society. The knowledge and expertise you have acquired should help drive innovation, leadership and transformation for the benefit of Tanzania and the wider global community,” said Dr. Kikwete.

He further emphasized the importance of research and knowledge creation in shaping Africa’s future, noting that universities must continue producing scholars capable of providing evidence-based solutions to emerging challenges.

UDSM Vice Chancellor, Prof. William A. L. Anangisye, described the graduation ceremony as a reflection of the University’s continued growth in teaching, research, innovation and international competitiveness.

Presenting the University’s annual progress report, Prof. Anangisye revealed that UDSM currently has 235 researchers ranked among Tanzania’s top 1,000 researchers according to the AD Scientific Index 2026. This represents 23.5 percent of all top researchers across 50 institutions nationwide.

He added that the University has continued strengthening academic quality and labour market relevance through curriculum reforms, with 285 undergraduate and postgraduate programmes reviewed based on stakeholder feedback and changing market demands.

Prof. Anangisye also highlighted major achievements in innovation and research commercialization. During the 2025/2026 academic year, UDSM researchers and innovators registered six patents through BRELA, some involving student innovators.

The registered innovations include technologies for bioethanol production, mushroom cultivation using sisal waste, organic fertilizer production, protein feed development using Black Soldier Fly larvae, and wine production from bamboo juice.

“These achievements demonstrate UDSM’s ability to add value to local resources, promote the green economy and use science to provide practical development solutions,” said Prof. Anangisye.

The Vice Chancellor further revealed that through the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project, the University is currently constructing 21 new buildings and renovating three others, a move expected to increase student capacity by 4,812 spaces.

He added that UDSM has also expanded digital learning infrastructure by increasing internet capacity, digitizing more than 1,000 courses and providing short-term professional training to nearly 3,000 staff members.

Addressing graduates directly, Prof. Anangisye reminded them that education is both a privilege and a responsibility to society.

“Education is not merely a personal achievement or decoration. It is a responsibility and a debt to the nation. Use the knowledge you have acquired to serve society, create opportunities and contribute to national development,” he said.

He encouraged graduates to embrace innovation, entrepreneurship and opportunities within the digital economy, especially in situations where formal employment opportunities may not immediately be available.

One of the most inspiring moments of the ceremony was the graduation of Dr. Paul Msoka, a visually impaired scholar who earned a PhD in Education after previously completing both his Bachelor’s and Master’s degrees within the UDSM system.

Dr. Msoka’s achievement stood out as a powerful testimony to resilience, determination and the University’s commitment to inclusive education and equal access to academic opportunities.

A researcher specializing in inclusive education and visual impairment studies, Dr. Msoka has contributed scholarly work focused on improving learning opportunities for students with visual impairment in Tanzania’s inclusive schools.

His achievement inspired many graduates, lecturers, family members and guests attending the ceremony, particularly young Tanzanians living with disabilities who aspire to pursue higher education and professional excellence.

Throughout the ceremony, emotional moments unfolded as graduates celebrated with supervisors, colleagues, friends and family members. Smiles, embraces and photographs reflected years of perseverance, sacrifice and academic dedication behind every success story.

Established in 1961, the University of Dar es Salaam remains Tanzania’s premier institution of higher learning and a symbol of academic excellence. Over the decades, the University has produced influential leaders, policymakers, scholars, diplomats, entrepreneurs and professionals who continue shaping Tanzania, Africa and the wider world.

For the Class of 2026, the graduation ceremony marked not only the completion of an academic journey, but also the beginning of a new chapter of leadership, innovation and national service.

As celebrations continued outside Mlimani City Hall, one message remained clear — the future of Tanzania’s intellectual, scientific and developmental transformation continues to be shaped at the University of Dar es Salaam.

 


Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM — Taasisi ya Heart Team Africa Foundation (HTAF) kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya “Kutoa Ni Moyo” yenye lengo la kuchangisha fedha na kuongeza uelewa kwa ajili ya kusaidia watoto wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo nchini.

Kampeni hiyo iliyozinduliwa Mei 25, 2026 jijini Dar es Salaam inalenga kuwaunganisha Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za jamii ili kuwapa watoto wanaozaliwa na matatizo ya moyo nafasi ya kupata matibabu na huduma muhimu za moyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge alisema zaidi ya watoto 16,000 huzaliwa kila mwaka nchini Tanzania wakiwa na matatizo ya moyo, hali inayozifanya familia nyingi kukumbana na changamoto kubwa za kiafya na kifedha.

Alisema takribani watoto 4,000 wanahitaji upasuaji wa moyo kwa haraka, huku akibainisha kuwa kwa familia nyingi muda si suala la fedha pekee bali ni suala la kuokoa maisha.
"Kupitia kampeni ya Kutoa Ni Moyo, tunatoa wito kwa Watanzania wote, taasisi, makampuni binafsi pamoja na taasisi za serikali kuwa sehemu ya harakati hizi za kuokoa maisha ya watoto," alisema Dkt. Kisenge.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa HTAF, Dkt. Naizihijwa Majani alisema kampeni hiyo imekusudia si tu kukusanya fedha, bali pia kujenga uelewa wa muda mrefu kuhusu afya ya moyo na umuhimu wa jamii kushiriki kusaidia.
Alisema Tanzania ina utamaduni mkubwa wa mshikamano na kusaidiana, hivyo kampeni hiyo inalenga kubadili michango midogo ya wananchi kuwa nguvu kubwa ya kitaifa yenye matokeo makubwa.

"Hii si kampeni ya kuchangisha fedha pekee, ni harakati inayojengwa juu ya huruma, umoja na imani kuwa kuokoa maisha ya mtoto ni jukumu la kila mmoja wetu," alisema Dkt. Majani.
Takwimu zinaonyesha kuwa magonjwa ya moyo husababisha vifo vya watu milioni 17.9 duniani kila mwaka, huku mtoto mmoja kati ya watoto 100 akizaliwa akiwa na tatizo la moyo.

Kampeni hiyo inalenga kukusanya shilingi bilioni 25 kupitia michango ya wananchi, makampuni, wadau wa maendeleo, taasisi mbalimbali, Watanzania waishio nje ya nchi, watu maarufu, jumuiya za michezo na jamii kwa ujumla.
Fedha zitakazokusanywa zitatumika kugharamia upasuaji na matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, uchunguzi wa mapema, programu za elimu ya afya ya moyo pamoja na kusaidia familia zinazokabiliwa na changamoto hiyo.

Aidha, kampeni hiyo itatumia mifumo ya kidijitali na majukwaa ya uchangishaji mtandaoni ili kurahisisha Watanzania kuchangia kwa uwazi na urahisi kutoka ndani na nje ya nchi.

Taarifa zinaonyesha kuwa juhudi za awali za uchangishaji tayari zimefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 3.08 kupitia fedha taslimu na misaada ya vifaa mbalimbali.

Na Mwandishi Wetu. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na maendeleo ya taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma.

“Tukitazama baadhi ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni, mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika jamii ya Watanzania,” amesema.

Amesisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na yanalinda maslahi ya taifa.

“Tunachosimamia ni kuhakikisha Mwandishi wa Habari anayepata ithibati anakuwa na kiwango cha elimu kisichopungua Diploma, lakini tunataka pia Waandishi wa Habari waendelee kupata mafunzo ili waweze kuimarika zaidi kitaaluma,” amesema.

Amesema ipo haja ya sekta ya habari kutafakari aina ya maudhui yanayopewa kipaumbele, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kujenga fikra na mwelekeo wa jamii.

Na Mwandishi Wetu, Michuzi Tv

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Mariam Ibrahim amemshuru Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa , Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kupendekeza jina lake na Kamati Kuu ya chama hicho kulipitisha na hatimaye kushinda kwa kura nyingi.

Ametoa shukrani hizo kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Dk.Samia Suluhu Hassan alipokuwa akisalimia viongozi mbalimbali wa Chama hicho wakati wa Semina ya Uongozi na Maendeleo kwa madiwani wote wanawake  wa Mkoa wa Pwani.

“Nitumie nafasi hii kwa dhati ya moyo wangu kumshukuru Mwenyekiti wetu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kunipendekeza mimi na Kamati Kuu kurudisha jina langu na kuja katika Mkoa wa Pwani na kupigiwa kura nyingi.

“Waheshimiwa madiwani hatujaonana toka Uchaguzi mkuu ulivyopita hivyo naomba kuchukua fursa hii kuwashukuru nyote kwa kura zenu za kishindo.Nasema ahsanteni sana,amesema mbele ya madiwani hao pamoja na viongozi wa Mkoa huo.
 
Amesisitiza ameamua kutoa shukrani hizo kwasababu ndio mara yake ya kwanza wanakutana ambapo ametumia nafasi hiyo pia kuwaaahidi kuendelea kushirikiana nao na yupo tayari kwa wakati wowote ambao atahitahika.“Tutakuwa pamoja katika kila hali.”






Na Mwandishi Wetu

BABATI — Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Babati mkoani Manyara imesitisha kusikiliza kesi ya jinai namba 291 ya mwaka 2026 iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini, Paulina Gekul, inayomkabili Brayton Lucas (17), baada ya kujiridhisha kuwa mshtakiwa huyo ni mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 18 na hivyo shauri hilo linapaswa kusikilizwa katika Mahakama ya Watoto kwa mujibu wa sheria.

Uamuzi huo ulitolewa baada ya Wakili wa upande wa utetezi, Thadei Lister, kuiomba mahakama kujiridhisha kuhusu umri wa mshtakiwa kwa kuwasilisha nyaraka mbalimbali ikiwemo cheti cha kuzaliwa kilichoonesha kuwa Brayton alizaliwa Novemba 12, 2008 na kwa sasa ana umri wa miaka 17 na miezi sita, tofauti na taarifa zilizokuwa katika hati ya mashtaka zilizomtaja kuwa na miaka 19.

Katika shauri hilo, Paulina Gekul alidai kuwa Brayton Lucas, ambaye alikuwa akichunga mifugo yake, alihusika katika wizi wa mbuzi 15 wenye thamani ya shilingi milioni tatu, kosa linalodaiwa kufanyika chini ya kifungu cha 268 cha sheria ya wizi wa mifugo. Kesi hiyo ilikuwa na jumla ya watuhumiwa watatu.

Mahakama pia ilielezwa kuwa mtoto huyo alikuwa amechanganywa katika shauri moja na watuhumiwa watu wazima, jambo ambalo upande wa utetezi ulidai ni kinyume na sheria zinazolinda haki za mtoto.

 Baada ya kupitia nyaraka zilizowasilishwa, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Babati, Ahmed Mgodo, alisema mahakama imejiridhisha kuwa Brayton Lucas ni mtoto na hivyo haina mamlaka ya kuendelea kusikiliza kesi hiyo. Kutokana na uamuzi huo, mahakama ilisimamisha shauri hilo dhidi ya mshtakiwa huyo na kuagiza polisi kuandaa hati mpya ya mashtaka kwa mujibu wa sheria zinazohusu watoto.

Brayton Lucas alipatiwa dhamana huku washtakiwa wawili wengine wakiendelea kushikiliwa. Wakili Thadei Lister amesema wako tayari kuendelea kumtetea mtoto huyo iwapo atafikishwa katika Mahakama ya Watoto.

Akizungumza nje ya mahakama, Wakili Thadei alisema Brayton ni mwanafunzi wa kidato cha nne ambaye alitoweka akiwa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha na wazazi wake walikuwa wakimtafuta kwa kipindi cha miezi mitatu kabla ya kupata taarifa kuwa amekamatwa Babati kwa tuhuma za wizi.

Mama mzazi wa Brayton alisema mtoto wake alitakiwa kuwa shuleni baada ya kumaliza kidato cha nne na tayari alikuwa amepangiwa shule, lakini aliondoka nyumbani bila kutoa taarifa na baada ya juhudi za muda mrefu za kumtafuta walipata taarifa kuwa alikuwa Babati akifanya kazi.
Wakati huo huo, Diwani wa Kata ya Maruvango Wilaya ya Arumeru Mashariki, Digna Nassari, amesema taarifa za kupotea kwa mtoto huyo zilikuwa zimetolewa polisi miezi mitatu kabla ya kufunguliwa kesi dhidi yake na Paulina Gekul.

Aidha, Digna amesema Brayton ni miongoni mwa watoto 16 kutoka kata hiyo waliotoroka shule, huku akisisitiza umuhimu wa jamii kushirikiana kuhakikisha watoto wanarudi katika mfumo wa elimu na kupata ulinzi unaostahili
Na Mwandishi Wetu-Kigali, Rwanda

TUME ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia Barani Afrika (NEISA 2026) uliofanyika Mei 19, 2026 mjini Kigali, Rwanda, ukiwakutanisha viongozi wa kitaifa, wataalamu wa nishati, wawekezaji pamoja na mashirika ya kimataifa kujadili mustakabali wa nishati ya nyuklia barani Afrika.

Mkutano huo ulilenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nyuklia pamoja na kuvutia uwekezaji katika miradi ya nishati kwa ajili ya kuimarisha uchumi endelevu.

Katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alisema Tanzania inaendelea kutathmini matumizi ya nishati ya nyuklia kama sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuongeza vyanzo vya nishati nchini.

Rais Samia alieleza kuwa teknolojia mpya za Small Modular Reactors (SMRs) na Micro Modular Reactors (MMRs) zinaweza kuwa suluhisho sahihi kwa nchi zinazoendelea kutokana na uwezo wake wa kuzalisha nishati kwa ufanisi na usalama zaidi.

Aidha, alitaja maeneo muhimu yanayopaswa kupewa kipaumbele katika maendeleo ya sayansi na teknolojia ya nyuklia kuwa ni pamoja na mifumo imara ya udhibiti, wataalamu wenye ujuzi pamoja na usimamizi madhubuti wa usalama kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Alisisitiza kuwa matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika uzalishaji wa nishati yanahitaji maandalizi ya mifumo ya udhibiti, uwezo wa taasisi, upatikanaji wa fedha, uelewa wa wananchi na ushirikiano wa kikanda.

Katika ushiriki wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania, Profesa Najat Kassim Mohammed alihudhuria mkutano huo akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Nyuklia na Huduma za Ufundi, Dkt. Remigius Kawala.

Profesa Najat alipata fursa ya kushiriki kikao cha ndani kilichoongozwa na Rais Samia ambapo alitoa ufafanuzi kuhusu maendeleo ya nyuklia nchini pamoja na miradi inayotekelezwa na TAEC kwa kushirikiana na International Atomic Energy Agency.

Miongoni mwa mipango hiyo ni Rays of Hope unaolenga kuimarisha huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani nchini, Atoms4Food unaohamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika sekta ya kilimo pamoja na ushiriki wa TAEC katika mpango wa matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa uzalishaji wa umeme.

Profesa Najat alisisitiza umuhimu wa Tanzania kuendelea kuwekeza katika utafiti, usalama na mafunzo ya wataalamu ili kuhakikisha matumizi salama na endelevu ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, viwanda, utafiti wa madini na uzalishaji wa nishati.

Kupitia mkutano huo, TAEC ilipata nafasi ya kubadilishana uzoefu na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali kuhusu usalama wa nyuklia, mifumo ya udhibiti wa teknolojia za nyuklia pamoja na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa ya nishati.

Aidha, ushiriki wa Tanzania katika NEISA 2026 uliendana na maono ya serikali ya kukuza sekta ya nishati na kuimarisha ushirikiano wa kikanda ndani ya Afrika Mashariki.

Katika mkutano huo, viongozi mbalimbali wa Afrika walisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kuendeleza miradi ya nyuklia, kuongeza uwekezaji na kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani.

Kwa ujumla, ushiriki wa TAEC katika NEISA 2026 umeiwezesha Tanzania kuendelea kujijengea nafasi katika mjadala wa kimataifa kuhusu mustakabali wa nishati ya nyuklia barani Afrika pamoja na kufungua fursa mpya za ushirikiano wa kitaalamu, kiteknolojia na kiuchumi kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Mkutano wa NEISA 2026 uliandaliwa kwa ushirikiano wa International Atomic Energy Agency, United Nations Economic Commission for Africa, World Nuclear Association pamoja na Rwanda.

MONACO - Benki ya CRDB imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya Taifa kupitia sekta mbalimbali kwa kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 81 wa Michezo ya Majeshi Duniani (81st CISM General Assembly) uliofanyika nchini Monaco kuanzia tarehe 1 hadi 9 Mei 2026.

Mkutano huo wa kimataifa uliwakutanisha viongozi wa kijeshi na wadau wa michezo kutoka zaidi ya nchi 130 duniani kwa lengo la kuimarisha mshikamano, diplomasia ya michezo na amani kupitia kaulimbiu ya “Friendship Through Sport.”
Benki ya CRDB, ikiwa miongoni mwa wadau wakubwa wa maendeleo nchini, imeendelea kuunga mkono jitihada za vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na michezo ya majeshi, hatua inayoimarisha ushirikiano wake na taasisi za Serikali katika kukuza ustawi wa askari na familia zao.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo uliongozwa na Brigedia Jenerali Saidi Hamisi Saidi, akisaidiana na Luteni Kanali Penina Anthony Igwe. Kutoka CRDB, ujumbe unajumuisha Meneja wa Kitengo cha Wateja Maalum, Crispin Sichalwe pamoja na Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Emmanuel Tupeligwe.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Sichalwe alisema CRDB imeendelea kutoa huduma maalum za kifedha kwa wanajeshi ndani na nje ya nchi, ikiwemo mikopo nafuu, bima na huduma za kifedha zinazowafikia popote walipo.

“Tunatambua mchango mkubwa wa majeshi katika usalama wa Taifa, hivyo tunahakikisha wanapata huduma bora na za haraka kupitia kitengo chetu maalum,” alisema.
Kwa upande wake, Tupeligwe alisisitiza kuwa CRDB itaendelea kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kupitia elimu ya fedha na huduma zinazowafikia wanajeshi hata wakiwa katika maeneo ya mbali au majukumu ya kimataifa.

Aidha, benki hiyo imeendelea kuimarisha ushirikiano wake wa kimkakati na JWTZ ili kuhakikisha wanajeshi wanapata huduma bora za kifedha kwa urahisi, ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika maendeleo na usalama wa Taifa.

Na Jawadu Kinyobwa 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa viongozi waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuchangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Akizungumza Mei 15, 2026 katika Mahafali ya Tisa ya Taasisi hiyo yaliyofanyika katika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Mhe. Ridhiwani alisema dunia ya sasa inahitaji viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi ya wananchi.

Alisema uadilifu ni sifa muhimu ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo wahitimu wanapaswa kutumia maarifa na ujuzi walioupata kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwazi na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa viongozi wenye uzalendo. Tukumbuke msemo wa wahenga kwamba adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za umma,” alisema Ridhiwani.

Aidha, aliwataka wahitimu hao kulinda rasilimali za taifa na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika maamuzi yao ya kila siku ili kusaidia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Alisema Tanzania inahitaji viongozi waaminifu na wenye uwajibikaji ambao watatumia nafasi zao kuendeleza ustawi wa wananchi na kuimarisha misingi ya utawala bora.
Sambamba na hilo, Waziri Ridhiwani alisema uongozi unaozingatia haki na uwazi utaendelea kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya nchi.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo alisema taasisi hiyo imetimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake rasmi Julai mwaka 2010 kwa Hati ya Rais kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu kwa ajili ya kujenga na kuimarisha viongozi barani Afrika.

Alisema kwa kipindi hicho, taasisi hiyo imefanikiwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi, kuandaa mijadala ya kisera pamoja na kufanya tafiti na machapisho yaliyosaidia kukuza maarifa ya kiuongozi.

Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed alisema mafunzo hayo yamewajengea uwezo mkubwa wa kiuongozi na kuwasaidia kufanya maamuzi yenye tija kwa taasisi na jamii.

Alisema mahafali hayo hayakuwa tu hitimisho la mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko makubwa ya kiuongozi na maendeleo binafsi waliyoyapata ndani ya miezi sita ya programu hiyo.