Articles by "HABARI ZA KIJAMII"
Showing posts with label HABARI ZA KIJAMII. Show all posts
Tanzania Breweries Limited (TBL), one of Tanzania’s top manufacturers and employers and a key partner in the socio-economic development of the country, has today signed a Memorandum of Understanding (MoU) with the CRDB Bank Foundation to collaboratively implement the Barley Farming Pre-financing Seed Capital Scheme.

This collaboration, rooted in TBL's Smart Agriculture Initiative, represents a key milestone in the company's efforts to promote sustainable farming practices and empower local communities across Tanzania.

The TBL’s Smart Agriculture Initiative aims to equip 100% of its direct farmers by 2025, ensuring they are skilled, connected, and financially empowered. By focusing on cultivating sorghum, barley, and grapes, which are essential resources for TBL's operations, the initiative directly supports farmers in enhancing productivity and leveraging natural resources efficiently.
With excitement for the collaboration, Michelle Kilpin, Tanzania Breweries Limited Managing Director, said: “By combining the efforts of both TBL and CRDB Bank Foundation, the partnership aims to significantly boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers in Tanzania.

I believe our partnership is a good example of how collaboration can play a positive role in bringing about positive change and creating value for various stakeholders. Having reached this milestone today, we are confident that it will be the catalyst for similar activities across the country, and we believe that this initiative will be an inspiration to others.”
Through this alliance with the CRDB Bank Foundation, TBL seeks to integrate financially empowered criteria into its smart agriculture framework, enabling farmers to adopt sustainable practices that promote environmental stewardship and reduce reliance on chemical inputs.

This partnership underscores TBL's broader commitment to achieving the United Nations Sustainable Development Goals, particularly SDG 2, which emphasizes achieving zero hunger; SDG 12, for responsible consumption and production; SDG 13, for climate action; and SDG 17, to enhance partnership for the goals.

The Foundation’s initiative, named the iMbeju program, aims to boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers across Manyara, Karatu, and Monduli Districts for the 2024 agriculture season. The TBL and CRDB Bank Foundation aspire to drive long-term sustainability and resilience in the agriculture sector.
The CRDB Bank Foundation Managing Director, Ms. Tully Esther Mwambapa, says the iMbeju program has been on the market for almost a year now and has attracted a huge number of youth and women, its primary target. To date, she says that the program, which involves financial literacy training and the provision of seed capital, has trained around 250,000 women and offered seed capital to the tune of TZS 5 billion.

“We both seek to enhance sustainable agricultural practices through empowering our farmers. Once farmers are financially stable, production will more than double in all key produce, stabilize our food safety, and increase surpluses for local trading and export. This will have a positive impact on our GDP, where agriculture contributes a lion’s share,” she narrated.
Under this affiliation, farmers will have timely access to agricultural inputs, be exposed to smart technology utilization, and receive comprehensive training, all of which are going to boost yields and improve incomes for farming families.

Furthermore, the effort fosters economic growth and rural prosperity in Tanzania by supporting community development.
Through the collaboration, TBL and the CRDB Bank Foundation will be providing capacity-building programs, seed capital, insurance coverage, the supply of essential agricultural inputs such as fertilizers and agrochemicals, and support for cost-effective harvesting logistics. The goal is not only to boost barley production but also to equip farming communities with the necessary tools and knowledge for sustainable agricultural practices and financial management.
The MoU includes a comprehensive framework for collaboration, detailing roles, responsibilities, and operational mechanisms to ensure the scheme’s success.

TBL and the CRDB Bank Foundation will work together to deliver on commitments around the following:
Community Development: By prioritizing livelihood improvement, the program contributes to broader community development, fostering economic growth, food security, and rural prosperity.

Sustainable Agricultural Practices: By promoting smart agriculture and financially empowering farmers, the program encourages sustainable practices that protect the environment and reduce chemical inputs.
Capacity Building: The partnership facilitates the transfer of financial literacy knowledge and skills to local farmers, empowering them to make informed decisions and adapt to evolving agricultural practices and market demands.

Increased Yields and Incomes: Through timely access to agricultural inputs, smart technology utilization, and training, farmers can enhance productivity, leading to higher yields and improved incomes for their families.
NA WILLIUM PAUL.

JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ikiongizwa na Mwenyekiti wake Mohammed Ali Kawaida (MCC) wamekabidhi msaada wa Chakula kwa wananchi wa Rufiji walioathirika na mafuriko katika maeneo hayo.

Kawaida ameelekeza Viongozi wa Rufiji kuhakikisha misaada yote inayotolewa inawafikia wananchi hao waliothirika na Mafuriko

"Niwasihi sana viongozi hakikisheni misaada hii inawafikia walengwa ambao ni wananchi wenzetu walioathirika na mafuriko na tuendelee kuwa faraja kwa ndugu zetu" Alisema Kawaida
Aidha Kawaida amewahakikishia wananchi wa Rufiji kuwa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi itaendelea kuwa karibu nao katika kipindi hiki kigumu wanachopitia kwani ni Utamaduni wa UVCCM kuwakimbilia Wananchi pale wanapopatwa na Matatizo.

"Ndugu zangu sisi Jumuiya ya Vijana tuna utamaduni wetu wa kuishi kama ndugu wamoja ndio maana kauli Mbiu yetu ni "Kulinda na Kujenga Ujamaa", Hivyo niwahakikishie kuwa tutaendelea kuwa karibu na ninyi katika kipindi hiki kigumu"

Kawaida amewasihi Watanzania na Wadau mbalimbali wawakimbilie Wananchi wa Rufiji kuwasaidia wananchi wa Rufiji na sio kufanya Siasa.




Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024.

Na Munir Shemweta, MLELE

Mbunge wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Mhe, Pinda amefanya ukaguzi wa jengo hilo leo tarehe 10 April 2024 akiwa njiani kielekea jimboni kwake Kavuu halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi kusheherekea Siku Kuu ya Eid El Fitri na waumini wa dini ya kiislamu katika jimbo lake sambamba na kukagua shughuli za maendeleo.

Mhe, Pinda akiambatana na Mkuu wa wilaya ya Mlele Alhaji Majid Mjengwa ameoneshwa kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo la CCM ambalo mbali na ofisi, litakuwa na ukumbi wa mikutano.

"Niwapongeze kwa kazi nzuri, naona jengo limefikia katika hatua nzuri na muda si mrefu wilaya yetu itakuwa na jengo lake zuri, hongereni sana" alisema Mhe. Pinda.

Kwa mujibu wa Mbunge wa Jimbo la Kavuu, ujenzi wa jengo hilo la CCM wilaya ya Mlele ni juhudi binafsi za yeye pamoja na mbunge mwenzake wa jimbo la Mlele Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe.

Amesema, kukamilika kwa jengo hilo kutawawezesha watendaji wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mlele kuwa na ofisi nzuri na hivyo kufanya kazi zao kwa ifanisi.

Akiwa jimboni kwake Mhe, Pinda mbali na kujumuika na waumini wa dini ya kiislamu katika kusheherekea Siku Kuu ya Eid El Fitri na kukagua shughuli za maendeleo katika jimbo lake pia atashiriki ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Balozi Dkt Emanuel Nchimbi anayetarajiwa kufanya ziara mkoa wa Katavi mwishoni mwa wiki.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024.
Mbunge wa jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akisisitiza jambo wakati wa kukagua maendeleo ya ujenzi jengo la Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati akielekea jimboni kwake Kavuu tarehe 10 April 2024. Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mlele Alhaji Majid Mjengwa.
Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo akizungumza wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga.
Na Oscar Assenga, KOROGWE.

WATANZANIA wametakiwa kuienzi amani iliyopo hapa nchini ambayo ni tunu kubwa iliyoacha na waasisi wa Taifa hili na wasikubali kamwe ichezewe kutokana na kwamba kufanya hivyo itaondoa umoja wetu ambao ni chachu ya maendeleo.

Wito huo ulitolewa na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga

Alisema wao kama Kanisa wanatambua kwamba amani ni kitu muhimu sana kwa ustawi wa jambo lolote lile hivyo ni lazima itunze na iendelee kuenziwa na ndio maana wameona mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufuturisha kutokana na umoja uliopo na kwamba wao ni ndugu moja.

Futari hiyo iliandaliwa na Kanisa hilo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ambapo ililenga makundi ya Makondakta,Waendesha bajaji,Wajasiriamali ,Wamachinga ambapo pia viongozi wengine wa kiserikali nao walishiriki lengo likiwa ni kuhimiza umoja na kudhimisha amani.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa futari hiyo Mchungaji wa Kanisa hilo Mbwambo alisema kwamba wao kama viongozi wa dini ni kuonyesha umma kwamba katika suala la mungu ni lazima kuwe na umoja na mshikamano kutokana na kwamba wao ni wametoka kwa baba mmoja.

“Futari hii ni kuonyesha umoja sisi kama kanisa na tunaendelea kusisitiza mshikamano na amani kwa sababu hivyo ndio vitu muhimu kwa ustawi wa jamii yoyote ile hivyo tuendelee kuitunza na kuienzi na tusiwafumbie macho wale ambao watakaojaribu kuichezea”Alisema

Hata hivyo alitoa wito kwa taasisi na watu wenye uwezo kuona namna ya kuwasaidia wahitaji wanapokuwa kwenye mwezi mtufuku wa ramadhani kuhakikisha wanayagusa makundi yaliyokuwa kwenye hali ya chini.
MKUU wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga leo mapema akiwa kwenye ziara yake katika Mji mdogo wa Mererani Wilayani Simanjiro, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Naepo iliyopo katika Kata ya Naisinyai kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Aprili 2024 mradi uwe umekamilika na unaanza kufanya kazi.

Zahanati ya Naepo inajengwa kwa fedha kutoka vyanzo mbalimbali ambapo shilingi Mil. 50 ni fedha za mapato ya ndani, Mil. 48 fedha za nguvu za Wananchi na Mil. 20 ni fedha ambazo zimechangiwa na mdau hivyo kufanya jumla ya Shilingi Mil. 118.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya Sokoni Mirerani - Mgodini Tanzanite kilomita 1.2 kwa kiwango cha lami inayotekelezwa na Mkandarasi M/S EMMA & SONS CONTRACTORS LTD. Mradi huu ulitengewa jumla ya shilingi milioni 898 hadi kukamilika. 

Katika hatua nyingine, Mhe. RC Sendiga amemuagiza na kumpa mwezi mmoja Meneja wa TARURA Wilaya ya Simanjiro kusimamia na kuhakisha mradi huo uwe umeshakamilika alipotembelea mradi huo unaotekelezwa kwa fedha za tozo ya mafuta.

Miradi mingine ambayo imetembelewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa ni pamoja na ujenzi wa Soko la madini, mradi unaotekelezwa kwa fedha shilingi Bilioni 5.43 na hadi sasa mradi upo katika asilimia 80 (80%) ya utekelezaji. Mradi mwingine ni ujenzi wa kituo cha Afya cha Tanzanite kilichopo kata ya Mirerani. Mradi huu umetengewa fedha kutoka Serikali kuu shilingi milioni 500 kujenga jengo la wagonywa wa nje (OPD), Maabara na jengo la mama na mtoto. Mradi huu upo katika hatua ya msingi.

Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiongea na Wanafunzi wa Vyuo vikuu wakati wa kongamano la kuwajengea uwezo wa kuhimili ushindani wa ajira na kujiajiri lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC) lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kwa udhamini wa kampuni ya Barrick.

Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya Barrick nchini, imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuibua na kukuza vipaji vya vijana wasomi wa vyuo vya elimu ya juu na kati nchini ili waweze kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea kutokea duniani na kuhimili ushindani katika soko la ajira sambamba na kuweza kujiamini kutumia ujuzi na taaluma zao kujiajiri kwa ajili ya kujenga mustakabali endelevu.

Hayo yameeleza na Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiongea na Wanafunzi wa Vyuo vikuu wakati wa kongamano la kuwajengea uwezo wa kuhimili ushindani wa ajira na kujiajiri lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AIESEC) lililofanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) kampasi ya Mlimani kwa udhamini wa Barrick ambayo inaendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Shimbi, pia aliwaeleza wasomi hao shughuli za kampuni ya Barrick nchini na mkakati wake wa kuinua vipaji vya vijana sambamba na kuwezesha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ili wapate fursa ya kupata ajira katika sekta ya madini ambayo kwa sasa asilimia kubwa inatawaliwa na wanaume.

Kongamano hilo kubwa limehusisha makampuni mengine makubwa ya ndani na nje kwa ajili ya kuwanoa wanafunzi kuhusiana na mabadiliko ya teknolojia,ajira na kujiajiri wenyewe pindi wamalizapo masomo yao.
Wanafunzi wakifuatilia mada kutoka kwa Watendaji wa makampuni mbalimbali walioshiriki katika kongamano hilo.
Afisa Raslimali wa Barrick Tanzania, Isentruda Mkumba (kushoto) akiongea na wanafunzi waliotembelea banda la maonesho la Barrick kwenye kongamano hilo.
Mratibu wa mafunzo (Supervisor Learning And Development) wa Barrick Tanzania, Elly Shimbi akiwa na viongozi wa AIESEC.
Washiriki wakifanya mazoezi ya kujiweka sawa.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb.) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba.

Na Mwandishi Wetu.

Kampuni za Denmark zimealikwa kuja kuwekeza nchini katika sekta za uchukuzi, nishati, madini, mazingira na uchumi wa buluu ambazo ni moja ya sekta za kipaumbele za Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mwaliko huo umetolewa wakati wa mikutano baina ya Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo na Masuala ya Hali ya Hewa wa Denmark, Mhe. Dan Jorgensen na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo iliyofanyika jijini Dodoma leo Aprili 5, 2024.

Waziri Nchemba alisema Serikali inajenga miundombinu ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) ambapo Serikali ya Denmark imesaidia kipande cha kutoka Morogoro hadi Makutupora ambapo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 90. Alisema Serikali inakaribisha wawekezaji kuendesha reli hiyo ambapo itakapokamilika itaunganisha Tanzania na nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Rwanda.

Dkt. Nchemba pia alizitaka kampuni za Denmark kuchangamkia fursa za ujenzi wa barabara ya mwendo kasi (express way) ya kutoka Dar Es Salaam hadi Dodoma ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kupunguza msongamano wa magari katika barabara hiyo kuu nchini.

Kwa upande wake, Dkt. Jafo alisisitiza umuhimu wa Denmark kushirikiana na Tanzania katika programu za utunzaji wa mazingira ikiwemo uwekezaji katika sekta ya nishati jadidifu. Aliiomba Denmark kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Misaada inayohitajika, alisema kuwa ni pamoja na kujenga uwezo wa watumishi, misaada ya kiufundi na rasilimali mbalimbali zikiwemo fedha.

Prof. Mkumbo, kwa upande wake alisisitiza umuhimu wa kampuni za Denmark kuja kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani (processing industries) hususan katika madini hadimu nchini. Alisema fursa katika sekta hiyo ni kubwa kwa kuwa Tanzania ina takribani aina 10 za madini hayo.

Aliiomba Denmark kuunga mkono jitihada za Serikali za kuchochea sekta binafsi nchini ambayo mchango wake bado uko chini, licha ya umuhimu wake katika kuongeza ajira na kuondoa umasikini nchini. “Tunaomba kuungwa mkono katika misaada ya kiufundi, elimu ya ufundi, urasimishaji wa sekta binafsi, kuchochea uhai wa sekta binafsi ili tuweze kujenga uwezo wa watu wetu hasa vijana kuwa na mbinu za kujiajiri wenyewe”, Prof. Mkumbo alisema.

Waheshimiwa Mawaziri walihitimisha mazungumzo yao kwa kuishukuru Denmark kwa misaada inayoipatia Tanzania katika sekta mbalimbali. Ulitolewa mfano wa msaada wa Krone bilioni 1.95 uliotolewa na Denmark kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2014 hadi 2021.

Kwa upande wake, Mhe. Jorgensen alieleza kuwa Tanzania ni moja ya nchi za mwanzo kabisa barani Afrika kuanza ushirikiano wa kidiplomasia na Denmark katika miaka ya 1960. Hivyo, ameahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa kuzingatia vipaumbele vitakavyobainishwa na pande zote mbili.
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.
Dkt. Mwigulu akimuaga Mhe. Dan Jørgensen.
Picha ya pamoja.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Tausi Kida.
Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen akizungumza na Mhe. Prof. Mkumbo jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024.
Picha ya pamoja.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira ), Mhe. Dkt. Selemani Jafo (wa pili kushoto) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Wa pili kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Denmark mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Olotu.
Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (wa tatu kulia) akizungumza na Mhe. Dkt. Jafo (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024.
Picha ya pamoja.


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia Programu ya Ruzuku ndogo inayotekelezwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) limesaini makubaliano ya kutoa sh 4.04 bilioni kwa mashirika yasiyo ya kiserikali 44 nchini ili kutekeleza miradi ya Uhifadhi wa Mazingira, Misitu, kuendeleza ufugaji nyuki, kutunza vyanzo vya Maji na uwezeshaji Jamii kiuchumi.

Utiaji saini wa Makubaliano hayo umefanyika leo April 4, 2024 katika Makao Makuu ya Jengo la Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na kuongozwa na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP, Bw. Shigeki Komatsubara.

Miongoni mwa mashirika yaliyosaini mkataba wa kupatiwa fedha hizo ni Shirika la Connecting Youth Connecting Tanzania (CYCT) ambalo limekuwa likihamasisha uhifadhi wa mazingira, Misitu na Mabadiliko ya tabia nchi kuhusisha vijana, Wanawake na Wanafunzi na Kundi la watu Maalum

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Komatsubara amesema kuwa mashirika zaidi ya 400 yalituma maombi kuomba fedha za kutekeleza miradi midogo midogo nchini Tanzania bara na Zanzibar lakini ni mashirika 44 tu ndio yamefanikiwa.

“Hongereni sana leo kuwa miongoni mwa mashirika na asasi ambazo zimepata fursa kutekeleza miradi midogo Tanzania.

Bw. Komatsubara amesema anaimani kubwa mashirika ambayo yanapewa fedha hizo yatakwenda kutekeleza vyema miradi ambayo itagusa jamii hasa wanawake, vijana, Walemavu na Jamii za pembezoni.

“Tunatarajia miradi yetu itakwenda kuchochea maendeleo katika jamii ikiwepo pia kukabiliana na vichocheo vya uharibifu wa mazingira” amesema.

Naye Mwakilishi kwa niaba ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Bi. Lilian Lukambuzi akizungumza katika hafla hiyo alitaka mashirika yaliyopewa fedha hizo kuzitumia kama ilivyokusudia.

Amesema serikali itafuatilia miradi ambayo inakwenda kutekelezwa ili kuhakikisha inakuwa na tija.

Awali, mratibu wa programu ya ruzuku ndogo za GEF nchini, Bw. Faustine Ninga amesema haikuwa kazi rahisi kupitisha mashirika hayo machache kupata ruzuku kutokana na uhitaji mkubwa kutoka katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kamati ya Uendeshaji ya programu hiyo ya Ruzuku Ndogo za GEF ambayo inaundwa na wataalam kutoka sekta mbalimbali na taasis zisizo za Kiserikali kwa kushirikia na UNDP ilifanya kazi kubwa ya kuchambua maandiko ya miradi zaidi ya 400.

Hata hivyo, amesema kutokana na uhitaji kuwa mkubwa ni mashirika 44 tu ndio yalipitishwa, ijapokuwa mashirika mengine yalikuwa na madokezo mazuri ya miradi.

Hata hivyo ameyataka mashirika haya kufuata kanuni na taratibu za nchi na miongozi ya uendeshaji wa taasisi zisizo za kiserikali katika utekelezaji wa miradi yao ili miradi iwe na matokeo mazuri.

Amesema kamati ya ufuatiliaji miradi hiyo itakagua na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi yote ili kuhakikisha kuwa jamii zinanufaika.

Wakizungumza baada ya kusaini mikataba baadhi ya watendaji wa mashirika hayo walipongeza UNDP kwa kuendelea kutoa fedha za kutekeleza miradi midogo katika jamii.
Mratibu wa Shirika la CYCT, Bw. Mensieur Elly amesema hii ni mara ya kwanza shirika hilo kupata fedha kutoka kwa wahisani hao.

“Tunatarajia kushirikiana na wadau mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kutunza Ikolojia ya mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya “Go green, serve Nature “ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Siha, Mkurugenzi Siha, TFS West na North Kilimanjaro, Afisa mipango na maendeleo jamii, Afisa elimu, mwenyekiti wa Halmashauri, afisa Tarafa, afisa Mtendaji, madiwani na vikundi vya vijana na wanawake West Kilimanjaro katika kutekeleza na kupata matokeo chanya na yanayoshikika.

Nae mratibu miradi wa Shirika la WODSTA, Bi. Clara Chuwa amesema wanakwenda kutekeleza mradi kwa ajili kuwezesha kutunza mazingira na matumizi endelevu ya msitu na chanzo cha maji kijiji Cha lemanda, Kata ya Oldonyosambu, Wilaya ya Arumeru.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la SECCA, Bw. Esaya Yusufu amesema wanakwenda kutekeleza mradi wa upandaji miti na kuchimba kisima katika eneo la ikolojia ya Serengeti.

Mfuko wa mazingira Duniani (GEF) ulianzishwa mwaka 1992 na umekuwa na miradi katika nchi 136 Duniani.