Articles by "AFYA"
Showing posts with label AFYA. Show all posts

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge (wa pili kulia) akipokea msaada wa kibinadamu kwa ajili ya wahanga wa mafuriko ya Rufiji na Kibiti wenye thamani ya takribani shilingi 250m uliotolewa na Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation. Msaada huo ulikabidhiwa na Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Vyombo vya Habari wa kampuni ya Vodacom Tanzania Annette Kanora (katikati). Wengine pichani kutoka kushoto ni Meneja wa Vodacom Tanzania Foundation Sandra Oswald na Meneja Mauzo wa eneo hilo Suleiman Amri na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele (kulia). Msaada huo ulikabidhiwa mwishoni mwa wiki mjini Kibiti.
NA WILLIUM PAUL.

JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ikiongizwa na Mwenyekiti wake Mohammed Ali Kawaida (MCC) wamekabidhi msaada wa Chakula kwa wananchi wa Rufiji walioathirika na mafuriko katika maeneo hayo.

Kawaida ameelekeza Viongozi wa Rufiji kuhakikisha misaada yote inayotolewa inawafikia wananchi hao waliothirika na Mafuriko

"Niwasihi sana viongozi hakikisheni misaada hii inawafikia walengwa ambao ni wananchi wenzetu walioathirika na mafuriko na tuendelee kuwa faraja kwa ndugu zetu" Alisema Kawaida
Aidha Kawaida amewahakikishia wananchi wa Rufiji kuwa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi itaendelea kuwa karibu nao katika kipindi hiki kigumu wanachopitia kwani ni Utamaduni wa UVCCM kuwakimbilia Wananchi pale wanapopatwa na Matatizo.

"Ndugu zangu sisi Jumuiya ya Vijana tuna utamaduni wetu wa kuishi kama ndugu wamoja ndio maana kauli Mbiu yetu ni "Kulinda na Kujenga Ujamaa", Hivyo niwahakikishie kuwa tutaendelea kuwa karibu na ninyi katika kipindi hiki kigumu"

Kawaida amewasihi Watanzania na Wadau mbalimbali wawakimbilie Wananchi wa Rufiji kuwasaidia wananchi wa Rufiji na sio kufanya Siasa.





Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida, Hussein Simba, akizungumza wakati akiongoza kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Aprili 3, 2024. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ayubu Kambi na na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Jonathan Hemed.

Na Mwandishi Wetu, Itigi

WANANCHI wa Kata ya Rungwa iliyopo wilayani Itigi mkoani Singida wamemshuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea Kituo cha Afya ambapo sasa wajawazito wameanza kupata huduma ya upasuaji na kuondokana na changamoto waliokuwa nayo ya kufuata huduma hiyo Hospitali ya St. Gasper iliyopo Itigi.

Diwani wa Kata hiyo Said Sudi akitoa shukurani hizo kwa niaba ya wananchi wake wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichoketi Aprili 3, 2024 alisema hawana cha kumlipa Rais Samia zaidi ya kumpa kura zote katika uchanguzi mkuuu utakaofanyika mwakani.

"Kata yetu tutampa kura asilimia 100 mama yetu kwa kazi kubwa aliyotufanyia si kwa kituo cha afya pekee bali na miradi mingine mingi iliyotekelezwa. wajawazito walikuwa wakilazimika kusafiri umbali wa kilometa 194 pale walipohitaji kupata huduma ya upasuaji lakini sasa wanaipata hapahapa nyumbani ni jambo la kumshuruku sana Mungu kupitia Rais wetu," alisema Sudi.

Sudi alisema Rais Samia aliwapa Sh. Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya ambacho kimeanza kutoa huduma hiyo Februari 27, 2024 ambapo wajawazito watano wamenufaika na huduma.

Alisema wajawazito walionufaika na huduma hiyo ni kutoka vitongoji vya Mkora A na B na kata za jirani za Kiloli na Kambikatoto.

Sudi alitumia nafasi hiyo kuomba wasaidiwe kupata gari la kubebea wagonjwa, mashine ya kufulia na kunyoshea nguo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Hussein Simba alisema ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo upo vizuri hadi kufikia mwezi februari walikuwa wamefikia asilimia 95 ya mapato ya Serikali mapato huru na mapato lindwa ilikuwa ni asilimia 35 na kuwa wanaamini kwa kasi hiyo hadi mwezi machi ambao bado hawajaujadili watafikia asilimia 100.

Simba alisema kupitia fedha za Serikali kuu na wahisani wamefikia asilimia 77 ya lengo ambapo zaidi ya Sh.Bilioni 4.9 halmashauri hiyo imekwishapewa ili kukamilisha miradi mbalimbali na kuwa asilimia iliyobaki ni ndogo ambapo amewahimiza madiwani kuisimamia miradi hiyo kwa kufanya kazi kwa vitendo zaidi badala ya maneno ili kufikia malengo ya wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Kemirembe Lwota, aliomba miradi yote inayotekelezwa ikikamilike ifikapo Aprili 30, 2024 ambapo pia aliwaomba madiwani kuhimiza kampeni ya kupata madawati kufuatia kuwepo kwa changamoto ya kukosekana kwa madawati katika shule zote wilayani humo.

Aidha, Lwota alihimiza mazao yote kuuzwa kwa njia ya stakabadhi gharani badala ya kuuzwa kiholela jambo linalosababisha Serikali kukosa mapato ambapo utaratibu wa kuyauza mazo hayo unafanyika.

Katika hatua nyingine Lwota amewataka madiwani hao na watumishi wengine katika wilaya hiyo kuanza maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru ambao unatarajiwa kuanza kukimbizwa wilayani humo mwanzoni mwa mwezi wa Julai, 2024.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Manyoni, Jumanne Ismail alishukuru mshikamano uliopo baina ya chama na Serikali ambao unaendelea kuifanya halmashauri hiyo kusonga mbele.

Ismail alisema Aprili 15, 2024 wanatarajia kuanza kufanya mikutano ya hadhara katika kata zote wakianzia wilayani Manyoni na kisha Itigi na lengo la mikutano hiyo ni kuzungumza na wananchi kuhusu miradi yote iliyotekelezwa katika maeneo yao na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM.



Katika kikao hicho cha baraza la madiwani ambacho kilikuwa na ajenda nane Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Hussein Simba aliweza kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa halmashauri hiyo, Ayubu Kambi na kutoa taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa lengo la kumpa picha halisi ya miradi hiyo ili aielewe na atakapoanza kazi ajue pa kuanzia.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ayubu Kambi akizungumza.
Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemirembe Lwota akizungumza.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Manyoni, Jumanne Ismail, akizungumza.

Katibu wa CCM Wilaya ya Manyoni Maimuna Likunguni, akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Mchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Emmanuel Dyilu, akizungumza kwenye kikao hicho.
Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAFU) wa wilaya hiyo, Valence Kilasara akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya wafufaika wa mfuko huo.
Diwani wa Viti Maalumu, Elizabeth Kidolezi akiomba ukamilishwaji wa mabweni kwa wanafunzi wa Sekondari wa Kata ya Rungwa.
Diwani wa Kata ya Mgandu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Martin Kapona,akisoma taarifa katika baraza hilo.

Diwani wa Kata ya Sanjaranda, Nikodemas Nkuwi, akizungumzia wanaufaika wa TASAFU na changamoto ya Tembo wanaokula mazao ya watu ambapo ameomba msaada wa kumaliza changamoto hiyo.
Diwani wa Kata ya Rungwa, Said Sudi akitoa shukurani zake baada ya kata yake kujengewa kituo cha afya ambacho Februari mwaka huu kimeanza kutoa huduma za upasuaji kwa wajawazito.
Mwenyekiti wa Wanawake wa Samia Mkoa wa Singida, Asha Mohamed Mwandala akiutambulisha umoja huo katika kikao hicho.
Waratibu wa vikao wa Halmashauri hiyo wakiwa kazini. Kushoto ni Makandaiga Magabe na Constantine Mihambo.
Naibu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Jonathan Hemed, akitoa taarifa za kamati katika kikao hicho.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Manyoni wakiwa kwenye kikao hicho.
Diwani wa Viti Maalumu, Utukufu Gwimile (kushoto) akiwa na madiwani wenzake katika kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Baadhi ya wakuu wa Taasisi za Umma wa Wilaya ya Manyoni na Itigi na wakuu wa idara wa Wilaya ya Itigi wakiwa kwenye kikao hicho.
Wakuu wa idara wakiwa kwenye kikao hicho.
Wanachama wa Wanawake na Samia Mkoa wa Singida wakiwa kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
Viongozi wa Halmashauri hiyo wakiwa meza kuu wakati wa kikao hicho.
Kikao kikiendelea. Kutoka kushoto ni Diwani wa Viti Maalumu, Amina Msita, Diwani wa Kata ya Mgandu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Martin Kapona, Diwani wa Viti Maalumu, Utukufu Gwimile na Diwani wa Viti Maalumu, Elizabeth Kidolezi.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Asasi za Kifedha Tanzania (TAMFI) limesema lina programu maalumu ya kuchangia uhifadhi wa mazingira na kupambana na ukataji miti kwa kuwezesha nishati safi ya kupikia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry katika kongamano la Wanawake katika fedha:Kukumbatia mabadiliko ya tabia nchi lililofanyika mwishoni mwa wiki.
Alisema katika kongamano hilo lenye nia ya kuchanganya jinsia na uendelevu wa mazingira ndani ya sekta ya fedha, kuwa kuna haja kwa wadau kama wao kuchukua hatua na kuunga mkono juhudi za serikali kukabili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwezesha wanawake nishati safi ya

"Ahadi yetu ya 'Kukumbatia Mabadiliko ya Tabianchi' inazidi mjadala tu; ni wito wa kuchukua hatua. Kwa kulingana na maono ya serikali ya ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, tunalenga kushughulikia vipengele muhimu vya maji, nishati mbadala, na mabadiliko ya tabianchi na kujitolea kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu namba kumi na nne (14)" alisema Winnie.

Mkutano huo uliopata ufadhili kutoka Foundation ya Charles Stewart Mott uliweka wazi ushawishi muhimu wa taasisi za kifedha kuwezesha wanawake ndani ya sekta ya fedha kuongoza mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.
Mwenyekiti wa Bodi ya TAMFI, Devotha Ntuke Minzi alisema ni jukumu la wanawake kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.

Akisisitiza athari zisizo sawa za mabadiliko ya tabianchi kwa wanawake, hasa nchini Tanzania na kote duniani, Minzi alitaka ushirikishi katika kufanya maamuzi na kutekeleza mipango kwa vitendo. Alihimiza haja ya kuongeza sauti za wanawake katika fedha kama waendeshaji muhimu wa suluhisho endelevu kwa changamoto hizi za kimataifa.

Naye Ofisa Programu wa TAMFI, Deodati Bernard alielezea mchango mkubwa wa wanawake kwa maendeleo ya Tanzania.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa wanawake na Wakurugenzi Mtendaji kutoka Taasisi za Fedha za Daraja la Kwanza na la Pili, pamoja na wajumbe kutoka Chama cha Benki Tanzania (TBA), Chama cha Nishati Mbadala Tanzania (TAREA), Mtandao wa Maji na Usafi Tanzania (TaWaSanet), New Faces New Voices (NFNV), Amshaamsha Foundation, IMED Foundation, Elico Foundation, Water.org, Kampuni ya Huduma za Nishati Endelevu (SESCOM) na wanawake katika nyanja mbalimbali za mfumo wa mabadiliko ya tabianchi nchini.

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni, akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD), Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024.

Na Mwandishi Wetu, Mtwara.

WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mtwara wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika maeneo yao.

Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa vikao vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia utatuzi.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay ameeleza kuwa kwa sasa kanda ya MSD Mtwara inahudumia vituo vya kutolea huduma za afya 631, na inasambaza bidhaa za afya kila baada miezi miwili.

Naye Meneja Huduma kwa Wateja na Miradi Dkt. Pamella Sawa ameeleza kuwa vikao vya MSD na wadau wake kuanzia sasa vitakuwa endelevu kila mwaka.

MSD Kanda ya Mtwara inahudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Wilaya ya Tunduru.Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay, akizungumza kwenye kikao hicho
Wadau wa MSD wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Wadau wa MSD Kanda ya Mtwara wakifuatilia mada kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao

Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro kushoto akimkabidhi Kombe la Mashindano ya Odo Ummy Cup Nahodha wa timu ya Kiomoni FC mara baada ya kuibuka Mabingwa kwa kuifunga Nguvumali FC penati 3-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga juzi ambapo mshindi huyo alipatiwa pia kitita cha Sh Milioni 3,pikipiki ya magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mpira kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya ambaye ndie muandaaji wa Mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman
Na Oscar Assenga, TANGA

TIMU ya Kiomoni FC wametawazwa kuwa Mabingwa wapya wa Michuano ya Kombe la Odo Ummy Cup baada ya kuibamiza timu ya Nguvumali FC penati 3-1 katika mchezo wa Fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Lamore Jijini Tanga.

Kutokana na ushindi huo waliweza kujinyakulia kitita cha Sh.Milioni 3,Pikipiki yenye Magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mipira huku Mshindi pili timu ya Nguvumali FC waliweza kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 2.5 na Mpira na Jezi Seti 1.

Michuano hiyo ya Odo Ummy Cup huchezwa kila mwaka kwa kushirikisha kata zote za Jimbo la Tanga yakiwa na lengo la kuibua vipaji na kukuza kiwango cha soka kwa vijana ambao kupitia mpira wanaweza kujikwamua kiuchumi.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikitaka kuibuka na ushindi ili kuweza kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko zilitoka sare tasa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia ikiwa na hari kubwa kutokana na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ili kuweza kujiimarisha kwa lengo la kufanya vizuri katika michuano hiyo.

Wakionekana kucheza kwa umahiri mkubwa Kimoni FC walianza kwa kulishambulia lango la wapinzani wao bila kuwepo kwa mafanikio yoyote ambapo kila wachezaji walipokuwa wakipiga mashuti langoni mwao liligonga mwamba na kutoka nje.

Kutokana na ushindani wa mchezo huo ulizilazimu timu zote kutoka uwanjani dakika 90 bila kuona milango ya kila mmoja na hivyo mwamuzi wa mchezo huo kulazimika kupelekea mchezo huo kwenye mikwaju ya penati ambao ndipo kiomoni waliposhinda mabao hayo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mcheo huo wa Fainali Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni aliwapongeza waandaaji wa mashindano hayo huku akieleza kwamba mashindano ikiwemo Mbunge Ummy Mwalimu.

“Ukiona vyaelea ujue vimeundwa hili ya leo tuna kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza Mbunge wetu Ummy Mwalimu niseme kama Waziri mwenye thamana ya michezo nimeshahudhuia mashindano yanayoandaliwa na wabunge mwengi sana sijaona mashindano mazuri kama haya”Alisema

Alisema mashindano haya ni mazuri na makubwa ambayo sijapata kuyaona katika maeneo mengine na Mbunge Ummy ana sifa ya kipekee kwa kuwajali wananchi wa Jimbo lake kutokana na kuhakikisha anawapigania ili kuweza kuondoa kero zenu.

Aidha alisema wanaposema michezo ni ajira wanaamini pia ni uchumi na wao kama Wizara wamemua hivi sasa michezo ni ajira na uchumi hivyo mashindano kama hayo watashirikiana na waandaaji kuhakikisha wanaibua vipaji na kuviendeleza.

Hata hivyo alisema kwamba mkoa wa Tanga ndio chimbuka la vipaji na wao serikali wataendelea kuiangalia Tanga huku akieleza kwamba Mbunge Ummy amepeleka ombi kwao kwamba uwanja huo wa Lamore ambao umechezewa fainali hiyo upandwe nyasi uwe mzuri ili fainali za mwakani ziwe nzuri .

“Na mimi nimemuhaidi Mbunge Ummy kwamba nitawaleta wataalamu kufanya tathimini ili uwanja uweze kuwa katikaa hali nzuri kutokana na kwamba umuhimu wa mashindano hayo ya Odo Ummy Cup”Alisema

Awali akizungumza katika fainali hiyo ,Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya alisema kwamba suala la Odo Ummy Cup ni mchango wake katika kutekeleza ilani ya CCM ibara ya 243 ambayo inawataka kuwekeza kwenye mpira wa migu hasa kwa vijana.

Alisema wanamshukuru pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman kutokana na kwamba amekuwa akiwasaidia na kuwaleta na kuwaongoza kwenye kutekeleza ilani.

Aidha alisema mashindano hayo lengo ni kuwaleta pamoja vijana wa Tanga mjini na yameleta moja,mshikamano na hamasa ya kumweka karibu na vijana huku akishukuru timu zote kutoka Kata 27 ambazo zilishiriki kwenye michuano hiyo.

“Lakini pia nishukuru kamati za Siasa za CCM kwa kujitoa kusimamia mashindano hayo pamoja na timu ya Hamasa ya UVCCM pia niwashukuru wadhamini wetu kwa kuuunga mkono wakiwemo wadau wetu Assemble Insurance kwa kutuunga mkono”Alisema

Hata hivyo kwa upande wake,Mwenyeiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman atumia fursa hiyo kuwataka wabunge na madiwani wa mkoa huo wahakikisha wanaendelea michezo katika maeneo yao.

“Kwani kufanya hivyo ni kutekeleza kwa vitendo ilani ya CCM ambayo tumehaidi kuendeleza michezo hivyo lililofanyika linatafsiri ilani kwa vitendo hivyo wabunge na madiwani hakikisheni hili linatekelezwa”Alisema.
Afisa Mawasiliano wa Barrick, Neema Ndossi (kulia) akikabidhi msaada wa mashine ya Patient Monitor, kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala,Dkt. Zavery Benella.Wengine pichani ni Wafanyakazi wa Barrick aliongozana nao.
---
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Wafanyakazi Wanawake wa kampuni ya Barrick kutoka ofisi ya Dar es Salaam wametembelea hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, na kukabidhi msaada wa mashine ya kudhibiti maendeleo ya kiafya ya watoto waliozaliwa na matatizo (Neonatal Patient Monitor).

Akiongea wakati wa kukabidhi kifaa hicho kwa uongozi wa hospitali hiyo, Afisa Mawasiliano wa Barrick, Neema Ndossi, aliyeambatana na baadhi ya Wafanyakazi Wanawake wakiungwa mkono na wafanyakazi wenzao Wanaume alisema “Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake, mwaka huu tumeona tutoe fadhila ya msaada wa Patient Monitor kwa ajili ya kusaidia watoto wachanga wanaozaliwa na matatizo katika hospitali hii.”

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Zavery Benella, ameishukuru Barrick na wafanyakazi wake kujitolea muda wao kutembelea hospitali na kutembelea wagonjwa katika wodi ya watoto.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala,Dkt. Zavery Benella, akiongea na baadhi ya wafanyakazi wa Barrick waliotembelea hospitali hiyo.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala Dkt. Zavery Benella (kushoto) akitoa maelezo ya huduma za hospitali hiyo kwa wafanyakazi wa Barrick walipotembelea wodi ya watoto.
Mwonekano wa mashine ya Patient Monitor iliyokabidhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.
Wafanyakazi wa Barrick katika picha ya pamoja na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, Dkt. Zavery Benella.