Articles by "HABARI NA MATUKIO"
Showing posts with label HABARI NA MATUKIO. Show all posts
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma Alhaji Mustafa Rajab Shaban kwenye picha na Watoto Yatima Shuraiya Ramadhan, Dhul-kaya Ramadhan pamoja na Ikramu Selemani wa Kituo cha Watoto Yatima cha Rahman kilichopo Chang’ombe Jijjini Dodoma mara baada ya kufuturu Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpakulia Iftar mtoto Yatima Shuraiya Ramadhan (6) wa Kituo cha Watoto Yatima cha Rahman kilichopo Chang’ombe Jijjini Dodoma. Rais Samia aliwaandalia Iftar Viongozi pamoja na Wageni mbalimbali Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa Futari mtoto Yatima Shuraiya Ramadhan (6) wa Kituo cha Watoto Yatima cha Rahman kilichopo Chang’ombe Jijjini Dodoma. Rais Samia aliwaandalia Iftari Viongozi pamoja na Wageni mbalimbali Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Iftar aliyowaandalia Viongozi pamoja na Makundi mbalimbali Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amebeba Kombe la Ubingwa wakati wa picha ya pamoja na Vijana wa Ramadhan Brothers ambao waliibuka washindi wa shindano la America’s Got Talent (AGT) mara baada ya Iftar Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiitikia Dua mara baada ya kupata Iftar aliyowaandalia Viongozi pamoja na Makundi mbalimbali Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Baadhi ya viongozi wa Dini wakiwa kwenye viwanja vya Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma kwa ajili ya Futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe 27 Machi, 2024
Wageni mbalimbali wakiwa kwenye Futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Mapacha wa Mtume Qaswida Hassan na Hussein wakitumbuiza wakati wa Iftar Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024. Mapacha wa Mtume Qaswida Hassan na Hussein wakitumbuiza wakati wa Iftar Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 27 Machi, 2024.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (Kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Abdulmajid Nsekela, wakipiga makofi mara baada ya kuzindua ushirikiano kati ya taasisi hizo unaoenda kuwezesha upatikanaji wa simujanja kwa mkopo ili kuchochea matumizi ya intaneti na ukuaji wa uchumi wa kidijiti nchini. Kulia kwa Besiimire ni Mkurugenzi wa Biashara wa Vodacom Bi. Linda Riwa na kushoto kwa Nsekela ni Afisa Biashara Mkuu wa benki hiyo Bw. Boma Raballa.
Dar es Salaam - Machi 27, 2024. Katika jitihada za kuongeza upatikanaji na matumizi ya simu janja ili kuziba pengo la kidijitali nchini, makampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Benki ya CRDB wamezindua mpango wa kuwezesha Wateja wao kumiliki simujanja zenye ubora kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo wa kukopesha simu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alieleza kuwa kampuni hiyo ya simu inatekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza gharama za vifaa vya mawasiliano ili kuwawezesha wateja wake kuhama kutoka kwenye matumizi ya mtandao wa 2G na kumiliki simu zenye uwezo wa 4G na kutumia fursa hiyo ili kunufaika na faida kemkem zinazopatikana kupitia mtandao huo.

"Tukiwa ni mdau na mshirika mkubwa wa sekta ya mawasiliano na teknolojia, Vodacom tunajivunia kuzindua mpango huu na Benki ya CRDB ambayo ni taasisi kubwa ya fedha nchini. Ushirikiano wetu unalenga kuwawezesha wateja kutoka pande zote mbili kupata aina mbalimbali za simujanja kwa bei nafuu na mpango wa malipo kwa awamu kwa kipindi fulani. Ili kujua kama amekidhi vigezo, mteja atatakiwa kupiga *150*00*44# nbaada ya hapo atafanya malipo ya awali na kupewa simujanja. Mkopo huu unaweza kulipwa kwa siku, kwa wiki au kwa mwezi kwa kipindi cha hadi miezi 12 kupitia M-Pesa," alifafanua bwana Besiimire.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema, “ushirikiano huu baina yetu na Vodacom ni fursa nzuri kwa Watanzania kupata huduma za kifedha na mawasiliano kwa gharama nafuu. Kwa hiyo kama wadau muhimu tunapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuhakikisha wananchi wake wanafaidika na ukuaji na maendeleo katika sekta hizi.”

Bwana Nsekela aliongeza kuwa, “Kwa mtandao wetu ulioenea nchi nzima, CRDB tumekuwa na mchango muhimu katika maendeleo ya Watanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha. Hivyo basi, kwa kushirikiana na Vodacom, tutaweza kutoa mchango wetu ili kuongeza matumizi ya simujanja nchini.”

Licha ya juhudi za mamlaka nchini kusogeza huduma za mawasiliano, wananchi wengi bado wanatumia huduma za mtandao wa 2G. Hii inapunguza upatikanaji wa fursa zilizopo mtandaoni pamoja na kufurahia na kunufaika na intaneti yenye kasi zaidi kutoka Vodacom pamoja na bidhaa nyingine za kidijitali.

Matumizi ya simujanja na intaneti yana faida kwa jamii kama vile kukuza ukuaji wa kiuchumi kwa kuwezesha ujasiriamali wa kidijitali na kuchochea uvumbuzi, utafutaji masoko mitandaoni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi wanaoamua kujiajili kupitia dijitali.
Vodacom Tanzania imekuwa ikishirikiana na watengenezaji mbalimbali wa simu za mkononi na taasisi za kifedha ili kuwezesha Watanzania kumiliki simu kupitia mikopo nafuu na mipango rafiki ya malipo kwa mteja.

Mwezi August 2020, Vodacom ilizindua programu ambayo inawaruhusu wateja wake kumiliki simujanja kupitia mkopo unaolipwa kwa awamu, huku kianzio kikiwa ni Shilingi 20,000 za Kitanzania kwa muda wa miezi 12.

Bwana Nsekela alimalizia kwamba anaamini kuwa taasisi hizo mbili zina huduma mbalimbali za kibunifu ambazo zitawanufaisha na kuboresha maisha ya wateja wao. Pia alitoa wito kwa Watanzania wanaotumia simu za kawaida na wanataka zenye ubora zaidi kufika katika maduka ya Vodacom na kupata simujanja kwa bei nafuu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali duniani.
MKURUGENZI Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph (wa pili kushoto) akimpa maelezo Diwani wa Kata ya Majengo, Shufaa Ibrahim namna taka ngumu zinazosababisha uzibaji wa chemba za majitaka wakati wa ziara yake leo Machi 26, 2024 ya kutembelea kata hiyo na kujionea hali ya mazingira ilivyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira DUWASA, Mhandisi Bernard Rugayi. (Picha na Mpigapicha Wetu)
MKURUGENZI Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph (kulia) akiwa na Diwani wa Kata ya Majengo, Shufaa Ibrahim wakikagua miundombinu ya majitaka katika eneo hilo wakati wa ziara yake leo Machi 26, 2024 ya kutembelea kata hiyo na kujionea hali ya mazingira ilivyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira DUWASA, Mhandisi Bernard Rugayi. (Picha na Mpigapicha Wetu)

MKURUGENZI Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph (kushoto) akimpa maelezo Diwani wa Kata ya Majengo, Shufaa Ibrahim (wa pili kulia) namna taka ngumu zinazosababisha uzibaji wa chemba za majitaka wakati wa ziara yake leo Machi 26, 2024 ya kutembelea kata hiyo na kujionea hali ya mazingira ilivyo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma DUWASA, Rahel Muhando (Picha na Mpigapicha Wetu)
MTUMISHI wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) Henry Motto, akinyonya majitaka yaliyotuama katika mtaa wa Kitenge kata ya Majengo jijini Dodoma leo Machi 26, 2024. (Picha na Mpigapicha Wetu)
---
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) Mhandisi Aron Joseph amewataka wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya utumiaji wa mfumo wa mtandao wa majitaka ili kuondokana na adha ya kuziba mara kwa mara kwa mitandao hiyo.

Ameyasema hayo leo Machi 26, 2024 wakati alipotembelea Kata ya Majengo, Mtaa wa Kitenge eneo lililoathiriwa na kujaa kwa majitaka kwa lengo la kukagua na kujionea hali ya mazingira katika eneo hilo.

“Maendeleo yanaenda na mambo mengi na yanagharama kidogo, na gharama yenyewe ndio kama hii, lakini isingekuwa hivi, kama wananchi wanazingatia matumizi sahihi ya mtandao wa majitaka”. Amesema Mhandisi Aron

Amesema uzibaji wa mara kwa mara katika mifumo ya majitaka sio kwa sababu ya majitaka kuwa mengi, bali ni kuingizwa kwa vitu na taka ngumu ambavyo vinasababisha mfumo huo kuziba.

“Tunaendelea kutoa elimu kwa wananchi watumie kwa sahihi mfumo wa majitaka, mfumo wa majitaka ni kwa ajili ya kutumia majitaka tu hata maji ya mvua hayatakiwi kuingia kwenye mfumo huo”. Amesema Mhandisi Aron

Nae Diwani wa Kata ya Majengo, Mhe. Shufaa Ibrahim ameishukuru DUWASA kwa kupokea malalamiko na kufika eneo lenye changamoto ili kujionea hali halisi na kuweza kutatua changamoto hiyo na kuahidi kuitisha mkutano wa wakazi wa eneo hilo na kuwaita wataalamu kutoka DUWASA ili waweze kutoa Elimu ya kutosha kwa wananachi.

Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi Wa Mazingira DUWASA, Mhandisi Bernard Rugayi amesema kwa sasa wanaendelea na zoezi la unyonyaji wa majitaka katika eneo hilo na ameahidi kumaliza changamoto hiyo kwa muda wa siku tano.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Tawi la Bahi Road, Kapteni Sungura Muhando amesema wananchi wanapaswa kupewa elimu kwa sababu mara nyingi wamekuwa wakiweka vitu vya ajabu katika mifumo ya majitaka.
Menejaa wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroad) Mkoa wa Tanga Mhandisi Dastan Singano akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani

Na Oscar Assenga, TANGA.

SERIKALI kupitia Wakala wa barabara nchini (Tanroad) Mkoani Tanga imetengewa Bilioni 294 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya barabara inayoendelea kwa sasa ikiwemo barabara ya Tanga-Pangani.

Hayo yalisemwa na Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoani Tanga (Tanroad) Mhandisi Dastan Singano wakati akielezea miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu ambapo alisema wanajivunia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Ambapo alisema Serikali ya awamu ya sita imejikita kuleta Maendeleo ya Miundombinu ya barabara kwa Mkoa wa Tanga na katika barabara hizo kuna miradi inayoendelea.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ule wa Barabara ya Tanga-Pangani ikiwemo Daraja la Mto Pangani mpaka Tungamaa kuelekea Mkwaja hadi Makange pamoja na Barabara ya Handeni-Mafleta.

Aidha alisema kwamba miradi hiyo inaendelea na utekelezaji wake na kwa sasa imefikia asilimia 73 vilevile Daraja la Pangani na barabara zake mradi inaendelea kutekelezwa kwa tija kubwa

“kwa kweli kwa kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu sisi kama mkoa wa Tanga tunajivunia uwepo wa miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo mradi wa Tanga-Pangani-Daraja la Mto Pangani -Tungamaa kwenda Mkwaja mpaka Makange barabara inaedelea kutekelezwa”Alisema Meneja Singano.

Meneja huyo alisema pia kwa sasa wanaendelea na utekelezaji wa barabara ya Handeni –Mafleta iliyopo chini ya Mkandarasi huyo amepata kipande kingine cha Mafleta kwenda Kweleguru hata hivyo mradi kutoka kwaleguru utakwenda hadi Kibirashi mpaka kule mpakani mwa Manyara hiyo barabara mpaka Singida inatekelezwa kwa utaratibu huo na utaona miradi mikubwa inaendelewa.

Akizungumzia kuhsu namna walivyojipanga kukabiliana na uharibifu wa muondombinu hususani katika kipindi cha mvua alisema wamejipanga kukabiliana na changamoto za barabara na Bajeti ya matengenezo ni zaidi ya milioni 12.6 imetengwa .

“Lakini pale panapotokea dharura kuna fedha za dharura ambazo wanazitumia kwa ajili ya sehemu ambazo zimepata itilafu ya kukatika kwa barabara kwa lengo la kuondosha changamoto hizo”Alisema Mhandisi Singano.

Meneja huyo alisema kwa sasa matarajio yao ni kuanza mradi wa barabara ya Soni hadi Bumbuli mpaka funta wilayani Lushoto wenye kilomita 20 na wanandelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwemo barabara ya Old Korogwe-Kwamkoro-Maramba mpaka Mabokweni.

Alisema barabara hiyo pia wanakamilisha usanifu ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami na wana mpango wa kujenga barabara kutoka njia ya panda kiomoni kwenda mpaka Bamba wilayani Mkinga kutokea Mlingano wilayani Muheza .

“Kwa hiyo utaona namna gani serikali ya awamu ya sita imejikita kuleta Maendeleo ya Miundombinu ya barabara kwa Mkoa wa Tanga zitakazokuwa na tija ya kuchochea kufungua maendeleo na kukuza uchumi”Alisema
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ndg. Mary Chatanda kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali wametoa mafunzo maaalum kwa viongozi wanawake kutoka mikoa 9 ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Ziwa Magharibi. Dhima kuu ikiwa ni kuwajengea uwezo Wanawake namna ya kutumia matokeo ya Sensa katika kuchochea maendeleo sanjari na Kuleta ufanisi wa Utendaji wa kazi katika kujikwamua kiuchumi na kijamii.

Mafunzo hayo ya Siku moja yamehusisha viongozi wanawake pamoja na Waheshimiwa Madiwani Viti Maalum kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera, Katavi, Shinyanga, Simiyu, Geita, Kigoma, Tabora pamoja na Mkoa wa Mara leo tarehe 27/3/2024 Katika Ukumbi wa Winterfell Mkoani Mwanza.

Kadharika mafunzo hayo yamehudhuriwa na Mhe. Anne Makinda Spika Mstaafu wa Bunge La Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamisaa wa Sensa, Katibu Mkuu wa UWT Ndg. Jokate Mwegelo, Naibu katibu Mkuu UWT Bara Ndg. Riziki Kingwande pamoja na Mhe. Amina Makilagi Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Kumekuwa na taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusiana na Timu ya Tabora United zikimuhusisha Kocha Mkuu Denis Laurence pamoja na msaidizi wake Masoud Juma kuwa wanataka kuondoka kwa kile kinachoelezwa hawajaridhishwa na mazingira lakini pia hawajasainishwa mikataba yao ya kazi.

Kwanza kabisa Klabu inapinga vikali upotoshwaji wa taarifa hizi kwa baadhi ya watu ambao hawanania njema na Timu ya Tabora United. Ikumbukwe kuwa Tabora United inaongozwa na viongozi ambao wanatambua na kufahamu umuhimu wa mfanyakazi kwa kila idara.

Tukianza na suala la Kocha Mkuu Denis Laurence ni kwamba kabla ya kuwasili kwa Kocha Laurence akiwa Ufaransa amekuwa akiifuatilia Timu ya Tabora United kupitia video za mechi mbalimbali lakini pia anaifahamu Timu kutokana na mazungumzo ambayo yalikuwa fakifanyika baina yake na viongozi wa klabu.

Lakini pia Kocha Laurence amewahi kufanya kazi na Msaidizi wake ambaye wanafanya kazi pamoja ndani ya Tabora United Masoud Juma na ndiye aliyempendeza hivyo hata suala la mazingira tafsiri yake ni kwamba analifahamu kwa kuwa anaifahamu vyema Timu ya Tabora United.

Kuhusu mikataba kwa hali ya kawaida hakuna mtumishi yoyote ambaye anaweza kuanza kufanya kazi pasipo kusainishwa mkataba wake hicho kitu hakiwezekani na hakijawahi kutokea tangu Dunia imeumbwa.

Kocha Laurence pamoja na Msaidizi wake Masoud walipewa mkataba na kusaini kulingana na taratibu za kazi zinavyotaka na ndio mana waliweza kuanza kazi mara moja na hadi sasa wanaendelea na majukumu yao kama kawaida ikiwa ni siku ya sita tangu walipotambulishwa.

Na hili jambo linafahamika kabisa kuwa mtu anapoanza kufanya kazi maana yake ni kwamba tayari walishakubalina na mwajiri hivyo kusema Kocha Mkuu na msaidizi wake wanaweza kuacha kazi hizo ni taarifa za uzushi na uongo na tunaomba mzipuuze.

Kuhusu mishahara ya wachezaji, viongozi pamoja na Benchi la ufundi, hakuna ambaye anadai hadi sasa na kwamba mara nyingi uongozi umekuwa ukijali masilahi ya watumishi wa idara zote kwa kuhaikisha kuwa stahiki zao wanalipwa kwa wakati.

Uongozi wa Tabora United umekuwa ukifanya mrejesho wa matumizi ya fedha zinazotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania TPLB kupitia kwa mzamini Mkuu wa haki za matangazo Azam Media kila mwezi na kwamba tumekuwa tukipokea fedha hizo. Hivyo kusema kwamba Tabora United haipatiwi fedha za haki ya matangazo huo ni upotoshwaji na kutaka kutugombanisha na mamlaka husika.

Kuhusu wachezaji wa Timu ya vijana Under 20, wote waliwasili tangu juzi Tabora wakitokea Geita ambapo walikuwa na mchezo wa Ligi ya vijana hatua ya makundi hivyo wachezaji hawajakwama sehemu yoyote.

Hivyo kauli ya Klabu ni kwamba mashabiki na wadau wote wampira ambao wanaiunga mkono Timu ya Tabora United wapuuze taarifa hizo kwani zinalenga kuchafua Brandi ya Klabu kwa makusudi hivyo kama uongozi unatambua thamani na umuhimu wa kila mmoja ndani na nje ya Klabu.

Timu inaendelea kujifua kwa ajili ya michezo ya Michuano ya kombe la Azam Sports Federation ASFC dhidi ya Singida Fountaingat pamoja na Ligi ya NBC soka Tanzania Bara itakayoendelea baada ya kumalizika kwa kalenda ya FIFA.

Imetolewa leo Machi 27
Na Christina Mwagala
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Tabora United.
Dar es Salaam – On March 21, U.S. Ambassador Michael Battle, alongside Mafia District's Administrative Secretary, Hon. Olivanus Paul Thomas, commemorated the successful completion of the third phase of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation (AFCP) project to restore the historic Swahili ruins of Kua on Juani Island, within the Mafia Island archipelago.

From 2017 through 2022, the U.S. Embassy awarded a total of $434,929 (approximately Tshs 1.1 billion) to World Monuments Fund (WMF) via the AFCP program of the U.S. Department of State. This funding supported the preservation of these ancient ruins in a collaborative effort with the local community. The celebratory event at the Kua Ruins hosted local government officials, a delegate from the Ministry of Natural Resources, WMF representatives, and community members.

Nestled off Tanzania's coast on Juani Island, the ancient Swahili town of Kua traces back to the 13th century, standing as one of East Africa's largest medieval Swahili settlements. The site boasts a significant number of residential structures that have withstood the test of time, including a grand palace and five mosques. Protected under the Antiquities Act No. 10 of 1964, as amended by Act No. 22 of 1979, the Kua Ruins are a testament to Swahili architectural ingenuity and historical importance. Ambassador Battle noted, “Through the AFCP program, the U.S. has not only preserved the essence of Kua but also ensured local communities benefit from these preservation efforts.”

Since it's inception in 2001, the Ambassador’s Fund for Cultural Preservation (AFCP) has aimed to safeguard notable cultural heritage sites across the globe. The American people have generously contributed over one million dollars in grants since 2002, supporting a wide range of preservation projects in Tanzania. These projects include the restoration of the 18th-century Kizimkazi Mosque in Zanzibar, the ancient trade port ruins of Kilwa Kisiwani, the prehistoric rock art in Kondoa, the 19th-century Bwanga House in Pangani, and the historical Shumba and Micheweni mosques in Pemba, among others.

World Monuments Fund (WMF), the project's lead implementing organization, is a premier non-profit entity dedicated to preserving the world’s most iconic heritage sites. With over 50 years of experience in more than 90 countries, WMF’s skilled experts employ advanced preservation techniques to safeguard architectural and cultural landmarks worldwide.

Embracing Cultural Heritage and Partnership: U.S. Ambassador Michael Battle alongside District Administrative Secretary Olivanus Paul Thomas (4th from left), other district and community leaders and World Monument Fund (WMF) representatives at Kua Ruins, commemorating the completion of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation’s (AFCP) project phase 3 for the restoration of Swahili ruins of Kua on Juani Island, Mafia. From 2017 to 2022, the U.S. Embassy awarded the WMF a total of $434,929 to preserve these ancient Swahili ruins in collaboration with local residents.
Mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga, Jennifer Dickson akifurahia tuzo ya Malkia wa Nguvu ajaye katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
------
Nyota ya Mwanafunzi wa Kike wa kitanzania Jennifer Dickson na mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga anayesoma elimu ya Chuo Kikuu mwaka wa pili nchini Rwanda katika Chuo cha Global Health Equity, akisomea fani ya Udaktari, inazidi kung’aa ambapo ametunukiwa tuzo ya Malkia wa Nguvu Ajaye 2024 katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.Tuzo hizo hutolewa na Clouds Media Group.

Maktaba aliyoianzisha Jennifer, inayojulikana kama maktaba ya kijamii ya Martha Onesmo, ilizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwaka huu ipo katika kata ya Msangeni kwa ajili ya kuwahudumia watu wote. Mgeni rasmi katika uzinduzi wake alikuwa ni Waziri wa Elimu, Profesa Adolf Mkenda.

Akiongea muda mfupi baada ya kupokea tuzo hiyo, alisema kuwa amefarijika kwa kiasi kikubwa kuona mchango wake katika jamii umetambuliwa na tuzo hiyo imezidi kumtia moyo wa kuendelea kufanya kazi za kijamii zenye mwelekeo wa kunufaisha watu wengi.

Alitoa shukrani kwa wazazi wake,marafiki zake na wa familia,na wafadhili mbalimbali ambao wamemsaidia kufanikisha ndoto yake ya kufungua maktaba ya kijamii ambayo imepelekea apate tuzo ya Malkia wa Nguvu ajae inayotolewa na kampuni ya habari ya Clouds.

Pia alitoa shukrani wa waandaaji wa tuzo hizo kwa kuona mchango wake katika jamii pia alitoa ushauri kwa vijana wenzake hususani watoto wa kike kujiamini na kupambana ili kufanikisha ndoto zao katika maisha na kuhakikisha hawabaki nyuma.

Kwa upande wa wazazi wake, walisema wamefurahi kuona kijana wao anapata mafaniko “Tuzo hii ni kielelezo kikubwa kwamba mtoto wa kike anaweza kama akiwezeshwa. Jennifer ni matokeo ya juhudi zake na ushirikiano wa jamii nzima inayomzunguka ukiaanza na sisi wazazi wake, ndugu zake wengine wa karibu hasa bibi yake mama Cecilia Ezekiel na jamii nzima ambayo ilishirikiana naye kwa hali na mali kuhakikisha anatimiza ndoto yake. Ni watu wengi wanamchango wao wa hali na mali katika kufikia hapa tulipo leo” Alisema Dk. Linda Ezekiel.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba hiyo, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amempongeza Jennifer kwa kufikia mafanikio hayo,”Ni jambo la kufurahisha kuona kijana wa umri wake anakuwa na ubunifu wa mradi ambao unaleta athari chanya kwa jamii hususani katika maeneo ya vijijini ,natoa wito kwake aendelee kupambana ili aweze kufanya mambo makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla”. Alisisitiza.

Wakati wa uzinduzi wa maktaba hiyo ya kijamii ya Martha Onesmo, mwanzilishi wake Jennifer alisema ndoto ya kuanzisha maktaba hiyo alikuwa nayo yangu anasoma kidato cha sita kwa ajili ya kuwezesha wakazi wa vijijini kupata maarifa.
Picha ya pamoja ya wanafamilia ya Jennifer na marafiki wa familia.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Dk. Kitila Mkumbo (kulia) akimpongeza mshindi wa tuzo la Malkia wa Nguvu ajaye,Jennifer Dickson katika hafla ya kutunuku tuzo hizo iliyofanyika jijini Dar es Salaam,katikati ni mwenyekiti wa bodi ya maktaba ya kijamii ya Mwanga iliyoanzishwa Jennifer, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Wanafamilia ya Jennifer na mwenyekiti wa maktaba ya Martha Onesmo wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Jennifer akiwa na wazazi wake.
Jennifer akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba ya Martha Onesmo,Profesa Bonaventure Rutinwa.

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni, akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD), Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024.

Na Mwandishi Wetu, Mtwara.

WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mtwara wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika maeneo yao.

Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa vikao vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia utatuzi.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay ameeleza kuwa kwa sasa kanda ya MSD Mtwara inahudumia vituo vya kutolea huduma za afya 631, na inasambaza bidhaa za afya kila baada miezi miwili.

Naye Meneja Huduma kwa Wateja na Miradi Dkt. Pamella Sawa ameeleza kuwa vikao vya MSD na wadau wake kuanzia sasa vitakuwa endelevu kila mwaka.

MSD Kanda ya Mtwara inahudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Wilaya ya Tunduru.Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay, akizungumza kwenye kikao hicho
Wadau wa MSD wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Wadau wa MSD Kanda ya Mtwara wakifuatilia mada kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao

Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba (kushoto) akimkabidhi leseni ya kuongezewa muda wa uchimbaji wa mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido katika hafla hiyo , wanaoshuhudia nyuma (kushoto) ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha. Leseni hii mpya iliyotolewa ni ya kipindi cha miaka 27.
---
Serikali kupitia Wizara ya Madini imeongeza muda wa leseni ya uchimbaji wa dhahabu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, uliopo katika wilaya za Kahama na Nyang’hwale mkoani Shinyanga kwa kipindi cha miaka 27 kuanzia mwaka huu.

Hafla ya kukabidhi leseni hiyo ilifanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Maofisa waandamizi kutoka Wizara ya madini, Wakuu wa mikoa ya Tanga na Shinyanga na wadau mbalimbali kutoka sekta ya madini ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde.

Aliyekabidhi leseni hiyo ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, na Mwakilishi wa Barrick, aliyepokea leseni hiyo kwa niaba ya kampuni ni Meneja wa Barrick Tanzania, Melkiory Ngido.

Mgodi wa Bulyanhulu tangu uanze kuendeshwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals, umefanikisha kuleta mafanikio chanya katika kukuza uchumi wa nchi ,kuongeza fursa za ajira sambamba na kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii kupitia fedha za uwajibikaji wa jamii (CSR) ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi katika maeneo yanayozunguka mgodi huo hususani katika sekta ya afya na elimu.
Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kushoto) katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa makampuni ya uchimbaji wa madini waliokabidhiwa leseni katika hafla hiyo.

Maofisa Waandamizi wa Barrick waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu.

Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita wakati wa hafla hiyo.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Antony Mavunde katika hafla hiyo.