Articles by "KITAIFA"
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

Na Mwandishi Wetu.

Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Saidi Yakubu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Masuala ya Idadi ya Watu (UNFPA) kwa nchi za Comoro, Mauritius, Seychelles na Madagascar, Bi. Josiane Yaguibou, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika masuala ya sensa.

Katika mazungumzo hayo, pande hizo mbili zilijadili maandalizi ya Sensa ya Watu itakayofanyika nchini Comoro mwaka 2027, ambapo UNFPA ni miongoni mwa waratibu wakuu wa zoezi hilo. Walizungumzia namna Tanzania inaweza kushiriki kama mdau kwa kutoa uzoefu na utaalamu wake katika uendeshaji wa sensa.

Balozi Yakubu alimueleza Bi. Yaguibou kuwa Tanzania ilifanikiwa kwa kiwango kikubwa kuendesha Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 kwa kutumia vifaa vya kisasa vya kidijitali pamoja na kushirikisha waangalizi wa kimataifa, jambo lililoongeza uwazi na ufanisi wa zoezi hilo.
Kwa upande wake, Bi. Yaguibou aliahidi kuendeleza mawasiliano na Ubalozi wa Tanzania ili kupata uzoefu na mbinu bora zilizotumika katika sensa ya mwaka 2022, kwa lengo la kuhakikisha Sensa ya Comoro 2027 inakuwa ya mafanikio.

Mazungumzo hayo yanafungua ukurasa mpya wa ushirikiano kati ya Tanzania, Comoro na UNFPA katika kuimarisha mifumo ya takwimu na upangaji wa maendeleo kwa kuzingatia taarifa sahihi za idadi ya watu.

Dar es Salaam, Februari 10, 2025 — Kampuni ya Samsung Electronics East Africa imezindua rasmi maduka mawili mapya ya chapa (Brand Stores) katika maeneo ya Kunduchi na Ubungo, ikiwa ni mkakati wa kupanua uwekezaji wake nchini Tanzania na kuimarisha ushindani katika soko la teknolojia na rejareja.

Maduka hayo yamebuniwa kuunganisha bidhaa za simu za mkononi na vifaa vya kielektroniki vya nyumbani chini ya paa moja, yakilenga kuwapatia wateja uzoefu wa moja kwa moja wa mfumo wa bidhaa unaofanya kazi kwa pamoja. Kupitia mpangilio huo, wateja wanapata fursa ya kuona, kujaribu na kuelewa namna simu janja, kompyuta kibao, runinga, vifaa vya kuvaa pamoja na vifaa vya nyumbani vinavyoweza kuunganishwa ili kurahisisha shughuli za kila siku.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Kitengo cha Simu za Mkononi wa Samsung Electronics East Africa (Tanzania), Mgope Kiwanga, alisema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kampuni katika soko la Tanzania. Alisema maduka hayo yanatoa nafasi kwa wateja kujionea kwa vitendo namna teknolojia ya Samsung inavyoweza kuleta tija katika mawasiliano, burudani na matumizi ya nyumbani.

Tofauti na maduka ya kawaida ya rejareja, maduka hayo mapya ni makubwa na yameundwa mahsusi kuonesha wigo mpana wa bidhaa za kampuni hiyo. Mbali na mauzo, yanatoa maelezo ya kitaalamu, maonesho ya matumizi ya bidhaa (product demonstrations), upatikanaji wa vifaa halisi (original accessories) pamoja na huduma baada ya mauzo kupitia wafanyakazi waliofunzwa na kuthibitishwa na Samsung.

Kwa upande wake, Meneja wa Biashara wa Samsung Tanzania, Daesong Ra, alisema uwekezaji huo unaonesha imani ya kampuni katika ukuaji wa soko la Tanzania na mchango wake katika mageuzi ya kidijitali. Alibainisha kuwa upanuzi huo unachochea ajira, unakuza ujuzi wa wafanyakazi wa ndani na kuongeza upatikanaji wa teknolojia bora kwa watumiaji.

Mbali na kuboresha uzoefu wa wateja, maduka hayo yanatarajiwa kuchangia ukuaji wa uchumi wa ndani kupitia ajira na mafunzo ya kitaalamu kwa Watanzania, huku yakiiweka Samsung katika nafasi imara zaidi ya ushindani katika sekta ya teknolojia inayokua kwa kasi nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 07 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 07 Februari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2026.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo ya pamoja na Ujumbe wa Uganda uliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki mjadala katika Jukwaa la Serikali za Dunia (WGS2026), tarehe 4 Februari, 2026 Madinat Jumeirah, Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).

Na Mwandishi Wetu

UZINDUZI rasmi wa Global Africa Investment Summit (GAIS) jijini Dubai umeashiria mabadiliko makubwa ya mtazamo kuhusu uwekezaji barani Afrika, ukilenga uaminifu wa taasisi, uthabiti wa sera na miundo imara kama msingi wa uwekezaji wa muda mrefu, badala ya kutegemea fursa za muda mfupi pekee.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika pembezoni mwa Mkutano wa World Governments Summit, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amethibitisha utayari wa Tanzania kushiriki kikamilifu GAIS kama mshirika wa kimkakati anayelenga faida endelevu. Alisisitiza kuwa changamoto kuu ya Afrika si ukosefu wa rasilimali, bali ni miundo na mifumo ya kuziwezesha rasilimali hizo kuzalisha matokeo chanya.

Rais Dkt. Samia alitolea mfano uwekezaji unaotekelezwa Tanzania katika miundombinu ya kimkakati ikiwemo umeme wa maji, reli ya kisasa (SGR), bandari na barabara, pamoja na uthabiti wa sera na utekelezaji wa ahadi za Serikali kama nguzo za kuvutia wawekezaji wa kimataifa.

Kwa upande wake, Rais wa Angola na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Mheshimiwa João Lourenço, alisema GAIS ni jukwaa muhimu linalosaidia Afrika kubadilisha namna inavyoshirikiana na mitaji ya kimataifa, akisisitiza kuwa Afrika lazima ichukue umiliki mkubwa wa maliasili zake na kuzisimamia kwa uwazi, ushindani na uwajibikaji.

Naye Rais wa zamani wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Adesina, alisema GAIS inaakisi ukomavu wa kisera wa Afrika na utayari wake wa kushirikiana na wawekezaji wa kimataifa kwa kuzingatia viwango vya juu vya utawala, uwazi na usimamizi wa vihatarishi. Aliongeza kuwa tatizo si ukosefu wa rasilimali bali ni miundo dhaifu, gharama kubwa za tathmini ya uwekezaji (due diligence) na mifumo ya utawala iliyogawanyika.

Katika hotuba zao, viongozi wengine akiwemo Rais wa Ghana, Mheshimiwa John Mahama, walisisitiza umuhimu wa mageuzi ya kisera, ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), ubia wa kibiashara (joint ventures) na uanzishaji wa maeneo maalum ya kiuchumi (SEZs) ili kuharakisha viwanda, kuongeza ajira kwa vijana na kukuza mauzo ya nje.

Kwa Tanzania, GAIS inatarajiwa kufungua fursa za kimkakati za kuvutia mitaji binafsi na ya kimataifa katika maeneo ya bandari na biashara ya kikanda, nishati na viwanda, pamoja na kuiimarisha nchi kama kitovu cha uzalishaji na usafirishaji ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati.

Global Africa Investment Summit ni jukwaa la uwekezaji linaloongozwa na Afrika, lililoanzishwa kwa ushirikiano wa viongozi wa Afrika na wadau wa maendeleo ya kimataifa, likilenga kuibadilisha Afrika kutoka utegemezi wa misaada kwenda kwenye ukuaji unaoongozwa na uwekezaji, ubunifu na ushirikiano wa kimkakati wa muda mrefu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, mara baada ya mazungumzo kati yao, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026.

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) zimekubaliana kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukuza uwekezaji, biashara na ustawi wa uchumi wa pande zote mbili.

Makubaliano hayo yamefikiwa kufuatia mazungumzo ya pande mbili kati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa UAE pamoja na Mtawala wa Dubai, Mtukufu Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, yaliyofanyika pembezoni mwa Mkutano wa World Governments Summit (WGS) 2026 jijini Dubai.

Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamekubaliana kukamilisha utekelezaji wa Mikataba ya Ushirikiano wa Biashara (CEPA) na Mikataba ya Uwekezaji wa Nchi na Nchi (BIT), hatua inayolenga kuboresha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji baina ya Tanzania na UAE.

Aidha, wamejadili utekelezaji wa miradi ya pamoja ikiwemo kuanzishwa kwa safari mpya za ndege za Shirika la Ndege la Emirates, zikiwemo safari za Kilimanjaro na Zanzibar, kwa lengo la kukuza sekta ya utalii, biashara na usafirishaji wa anga.

Rais Dkt. Samia amewasilisha uzoefu wa Tanzania katika kutekeleza mageuzi ya kiuchumi na kisheria, ikiwemo maboresho ya sera, sheria na taratibu za uwekezaji, akisisitiza umuhimu wa uthabiti wa sera, uwazi wa mifumo ya utawala na ulinzi wa maslahi ya wawekezaji kama msingi wa kujenga imani ya muda mrefu kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa.

Vilevile, Rais Dkt. Samia ameainisha uwekezaji mkubwa unaotekelezwa na Serikali katika miundombinu ya kimkakati ikiwemo reli ya kisasa (SGR), bandari za Bahari ya Hindi na maziwa makuu pamoja na mtandao wa barabara, akibainisha kuwa hatua hizo zimeipanga Tanzania kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia ameshiriki katika mjadala wa kimataifa kuhusu uwekezaji uliofanyika ndani ya Mkutano wa World Governments Summit 2026, wenye mada “Serikali na Mustakabali wa Uwekezaji: Mtazamo wa Afrika”, uliolenga kujadili nafasi ya serikali katika kuvutia mitaji na kukuza uchumi barani Afrika.

Kwa upande wake, Mtukufu Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano wa karibu na Tanzania kupitia miradi ya maendeleo, akisisitiza dhamira ya UAE katika kukuza ustawi wa kiuchumi wa pande zote mbili.

Kwa mujibu wa maelezo kwa vyombo vya habari, uhusiano wa kibiashara kati ya Tanzania na UAE umeendelea kuimarika kwa kasi, ambapo thamani ya biashara imeongezeka kutoka dola za Marekani milioni 985.31 mwaka 2018 hadi dola bilioni 2.1 mwaka 2024, na kuifanya Tanzania kuwa mshirika muhimu wa kibiashara wa UAE barani Afrika.

Rais wa Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026. 
Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Rais wa Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço kwenye hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus akihutubia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus kwenye hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026. Kushoto ni Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina ambaye ni Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama wa kwanza (kulia), Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus wa pili (kulia) pamoja na Mwanzilishi Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya uzinduzi rasmi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), uliofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 03 Februari, 2026.

Na Mwandishi Wetu, Dubai

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, jana usiku alishiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS) jijini Dubai, tukio lililoashiria mwelekeo mpya wa Afrika katika kuvutia mitaji ya kimataifa kupitia uwekezaji uliopangiliwa, wenye uhalisia wa kifedha na matokeo ya muda mrefu.

Akihutubia katika uzinduzi huo, Rais Dkt. Samia alisema kuwa wawekezaji wa leo hawatafuti fursa pekee, bali wanahitaji uaminifu unaojengwa kupitia uthabiti wa sera, taasisi imara na serikali zinazotekeleza ahadi zake kwa vitendo. Alisisitiza kuwa imani hiyo ndiyo msingi wa uwekezaji wa kudumu na wenye tija kwa pande zote.

Rais Samia alieleza kuwa Tanzania imechukua hatua za kimkakati kuimarisha mazingira ya uwekezaji kwa kuwekeza kwenye sekta muhimu ikiwemo nishati, reli ya kisasa, bandari na miundombinu ya uchukuzi, sambamba na kuanzisha Maeneo Maalum ya Uwekezaji pamoja na mfumo wa Dirisha Moja la Uwekezaji ili kurahisisha na kuharakisha huduma kwa wawekezaji.

Aliongeza kuwa ushiriki wa Tanzania katika GAIS unaakisi dhamira ya nchi ya kujenga ushirikiano uliopangiliwa vizuri, unaoendana na vipaumbele vya maendeleo ya taifa na matarajio ya wawekezaji wa kimataifa, huku ukilenga kuleta ajira, uhamishaji wa teknolojia na kukuza uchumi jumuishi.
Na WMJJWM – Dodoma

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, ametambuliwa rasmi kuwa miongoni mwa Wanawake 100 Wanaoheshimiwa wa Asili ya Afrika kwa mwaka 2026, kutokana na mchango wake mkubwa katika uongozi na maendeleo ya kijamii nchini na barani Afrika kwa ujumla.

Tuzo hiyo hutolewa na Kongamano la Wanawake wa Afrika (Africa Women Summit) kama heshima maalum kwa wanawake waliodhihirisha uongozi wa kipekee, uadilifu wa hali ya juu na mchango chanya katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Orodha hiyo inalenga kuenzi wanawake wanaovunja vikwazo, kubadilisha simulizi za maendeleo na kuhamasisha kizazi kijacho cha viongozi wanawake.

Katika toleo la mwaka 2026, wanawake mashuhuri kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wametambuliwa, huku Tanzania ikiwakilishwa na Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, kutokana na juhudi zake katika kuendeleza usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa wanawake, ulinzi wa watoto na ujumuishaji wa makundi maalum katika mipango ya maendeleo ya taifa.

Akizungumza baada ya kutambuliwa, Dkt. Gwajima amesema heshima hiyo ameipokea kwa shukrani kubwa, akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa kinara wa uwezeshaji wa wanawake duniani na kwa kuendelea kuwaamini na kuwapa nafasi wanawake kushika nafasi za uongozi. Amesema utambuzi huo ni matokeo ya imani na malezi ya kiuongozi aliyopata chini ya Rais Samia.

Dkt. Gwajima ameahidi kuendelea kuchochea utekelezaji wa falsafa ya Kazi na Utu kwa kujituma na kuhakikisha huduma na programu za wizara yake zinawafikia wananchi wote, hususan wanawake, watoto na makundi yenye mahitaji maalum, ili kuenzi heshima hiyo na kutimiza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa muda wake katika uongozi, Dkt. Gwajima amekuwa mstari wa mbele katika kuongoza mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, kuimarisha ulinzi wa mtoto, kukuza usawa wa kijinsia na kuhakikisha makundi maalum yanajumuishwa kikamilifu katika mipango na fursa za maendeleo, hatua zilizomjengea heshima kubwa ndani na nje ya nchi.

Vatican City — Tanzania has reaffirmed its long-standing diplomatic and moral partnership with the Holy See, emphasizing shared commitments to peace, dialogue, human dignity, and social development.

The message was delivered by the Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation, Hon. Mahmoud Thabit Kombo (MP), during an official audience with Pope Leo XIV at the Vatican on 29 October 2025. Minister Kombo conveyed warm greetings and a special message from President Samia Suluhu Hassan, underscoring Tanzania’s appreciation for the Catholic Church’s contribution to education, healthcare, social welfare, and national cohesion.
He praised the Church’s moral leadership and its role in promoting unity and peaceful coexistence in Tanzania, noting that its institutions continue to complement government efforts, particularly among vulnerable communities.

Tanzania also welcomed the Holy See’s proposal to establish a resident diplomatic mission at the Vatican, describing the move as an important step toward strengthening structured cooperation. Currently, Tanzania is represented by a non-resident ambassador based in Berlin.

During discussions, Minister Kombo briefed the Pope on Tanzania’s commitment to national reconciliation following post-election tensions, guided by President Samia’s 4R philosophy — Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. He highlighted ongoing efforts, including inclusive dialogue and the establishment of an independent review process to promote accountability and prevent future unrest.

Pope Leo XIV welcomed Tanzania’s approach and expressed his readiness to continue praying for peace, unity, and stability in the country. He also recalled his pastoral experiences in Tanzania, saying they left a lasting impression and strengthened his personal connection to the nation.

In addition to the Papal audience, Minister Kombo held talks with senior Vatican officials, including Archbishop Paul Richard Gallagher, focusing on deepening diplomatic cooperation and collaboration in social development.

The Ministry of Foreign Affairs said the engagement reflects Tanzania’s diplomatic direction of being “non-aligned but multi-engaged,” pursuing partnerships that advance national unity, peace, and shared prosperity.
Na Mwandishi Wetu – Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Madini imezidi kuonesha dhamira yake ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uwekezaji wa kimkakati barani Afrika, baada ya kukaribisha rasmi kampuni kutoka Korea Kusini kuja kuwekeza katika sekta ya madini nchini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, amesema uwekezaji huo unahitajika zaidi katika maeneo ya utafiti wa madini, uongezaji thamani, pamoja na matumizi ya teknolojia za kisasa katika uchimbaji na uchakataji wa madini, hususan madini muhimu na ya kimkakati.
Mbibo ametoa kauli hiyo Januari 28, 2026 jijini Dodoma, wakati wa kikao kati ya Wizara ya Madini na ujumbe kutoka Korea Kusini uliowakilisha Shirika la Kukuza Biashara na Uwekezaji la Korea (KOTRA) pamoja na Kampuni ya HD Construction Equipment, inayojihusisha na utengenezaji wa mitambo na teknolojia za uchimbaji madini.

Amesema maboresho ya sera na sheria yaliyofanywa na Serikali yamelenga kuvutia wawekezaji wenye mtaji, teknolojia na nia ya kuwekeza kwa muda mrefu, hasa katika ujenzi wa viwanda vya kuchakata madini ndani ya nchi na uhamishaji wa teknolojia kwa Watanzania.

“Tanzania iko tayari kwa ubia wa kimkakati unaoongeza ajira, mapato ya ndani na ushindani wa kimataifa. Tunakaribisha wawekezaji wanaoleta suluhisho za kisasa kwenye mnyororo mzima wa thamani wa madini, kuanzia utafiti hadi uongezaji thamani ndani ya nchi,” amesema Mbibo.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi na Kamishna wa Biashara wa KOTRA Ofisi ya Dar es Salaam, Kim Sangwoo, amesema Korea Kusini ina dhamira ya kuongeza uwekezaji wake katika Ukanda wa Afrika Mashariki kupitia miradi yenye tija na uwajibikaji, huku Tanzania ikitajwa kuwa miongoni mwa nchi zenye mazingira rafiki ya uwekezaji.

Naye Meneja Mkuu wa Kampuni ya HD Construction Equipment, Soohong Min, amesema kampuni za Korea zina uzoefu mkubwa katika teknolojia za kisasa za uchimbaji, mitambo mizito, pamoja na mifumo bora ya uzalishaji, ambayo inaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ajenda ya Tanzania ya uongezaji thamani wa madini.
● Majadiliano kati ya pande hizo mbili yalihusisha maeneo muhimu kama:

● Utafiti wa kina wa madini kwa kutumia teknolojia za kisasa

● Uchakataji na uongezaji thamani wa madini

● Ujenzi wa viwanda na miundombinu ya uzalishaji

● Uhamishaji wa teknolojia kwa wataalamu wa ndani

Kwa pamoja, pande zote zimeonesha dhamira ya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kiteknolojia, huku Serikali ikisisitiza kuwa mlango uko wazi kwa wawekezaji wanaoendana na dira ya maendeleo jumuishi na endelevu ya Taifa.

KOTRA ni taasisi ya Serikali ya Korea Kusini iliyoanzishwa mwaka 1962 kwa lengo la kukuza biashara ya kimataifa na uwekezaji wa kigeni, na ina ofisi katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania kupitia ofisi yake ya Dar es Salaam.

Rais Yoweri Museveni amehitimisha leo miaka 40 madarakani. Museveni aliyechukua madaraka mwaka 1986, amesisitiza mchango wa serikali yake katika kuleta utulivu, usalama na maendeleo ya taifa. Kwenye hotuba yake, amewataja wapinzani wake kuwa magaidi, hatua iliyoibua mjadala mpana wa kisiasa ndani na nje ya nchi.   andika habari ya gazeti

Kampala, Uganda — Rais Yoweri Museveni ameadhimisha rasmi kukamilisha miaka 40 madarakani leo, akisisitiza mchango wa serikali yake katika kudumisha utulivu, usalama na maendeleo ya taifa, licha ya malalamiko ya kimataifa na ndani ya nchi kuhusu hali ya kisiasa. Museveni, aliyekua madarakani tangu mwaka 1986, amebainisha mafanikio ya utawala wake na kujitetea dhidi ya lawama zinazotolewa na wapinzani wake.

Katika hotuba yake mbele ya maelfu ya wananchi na viongozi wa kisiasa katika kile kilichoitwa “Siku ya Maadhimisho ya Miaka 40 ya Mapinduzi,” Museveni alisema serikali yake imeleta usalama na mpango wa maendeleo uliothibitisha mafanikio kadhaa ya kiuchumi na kijamii kwa nchi nzima. Alisema utawala wake umekuwa muhimu kwa kuleta mabadiliko tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyompelekea kufika madarakani.

Hata hivyo, hotuba ya Museveni ilijumuisha masuala yanayozua mvutano. Alitaja baadhi ya wapinzani wake kama “magaidi” na “wauaji wa amani,” jambo lililochochea mjadala mkali ndani ya nchi na nje yake juu ya hali ya demokrasia na uhuru wa kisiasa nchini Uganda. Wapinzani na makundi ya haki za binadamu wanasema kauli hizo zinachangia hali ya kutisha na kutoruhusu upinzani wa kweli kisiasa.

Mwezi huu, Museveni alipata ushindi katika uchaguzi wa rais uliokua na utata, akipata zaidi ya asilimia 70 ya kura, matokeo ambayo chama tawala kilitangaza kama ushindi wa wazi, lakini chama cha upinzani kiliipinga matokeo hayo kwa madai ya udanganyifu na udhibiti wa taarifa.

Wafuatiliaji wa kisiasa na vyombo vya habari wametilia shaka mwenendo wa uchaguzi, mabadiliko ya katiba yaliyomuwezesha Museveni kuendelea kuwania madaraka, na hatua za serikali dhidi ya wanaharakati wa upinzani. Hii imeibua mjadala mpana kuhusu mustakabali wa demokrasia nchini Uganda licha ya ahadi ya Museveni ya kuendelea kusukuma maendeleo na utulivu.