Articles by "KITAIFA"
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb.) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba.

Na Mwandishi Wetu.

Kampuni za Denmark zimealikwa kuja kuwekeza nchini katika sekta za uchukuzi, nishati, madini, mazingira na uchumi wa buluu ambazo ni moja ya sekta za kipaumbele za Serikali ya Awamu ya Sita inayongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mwaliko huo umetolewa wakati wa mikutano baina ya Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo na Masuala ya Hali ya Hewa wa Denmark, Mhe. Dan Jorgensen na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo iliyofanyika jijini Dodoma leo Aprili 5, 2024.

Waziri Nchemba alisema Serikali inajenga miundombinu ya reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) ambapo Serikali ya Denmark imesaidia kipande cha kutoka Morogoro hadi Makutupora ambapo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 90. Alisema Serikali inakaribisha wawekezaji kuendesha reli hiyo ambapo itakapokamilika itaunganisha Tanzania na nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Rwanda.

Dkt. Nchemba pia alizitaka kampuni za Denmark kuchangamkia fursa za ujenzi wa barabara ya mwendo kasi (express way) ya kutoka Dar Es Salaam hadi Dodoma ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kupunguza msongamano wa magari katika barabara hiyo kuu nchini.

Kwa upande wake, Dkt. Jafo alisisitiza umuhimu wa Denmark kushirikiana na Tanzania katika programu za utunzaji wa mazingira ikiwemo uwekezaji katika sekta ya nishati jadidifu. Aliiomba Denmark kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Misaada inayohitajika, alisema kuwa ni pamoja na kujenga uwezo wa watumishi, misaada ya kiufundi na rasilimali mbalimbali zikiwemo fedha.

Prof. Mkumbo, kwa upande wake alisisitiza umuhimu wa kampuni za Denmark kuja kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani (processing industries) hususan katika madini hadimu nchini. Alisema fursa katika sekta hiyo ni kubwa kwa kuwa Tanzania ina takribani aina 10 za madini hayo.

Aliiomba Denmark kuunga mkono jitihada za Serikali za kuchochea sekta binafsi nchini ambayo mchango wake bado uko chini, licha ya umuhimu wake katika kuongeza ajira na kuondoa umasikini nchini. “Tunaomba kuungwa mkono katika misaada ya kiufundi, elimu ya ufundi, urasimishaji wa sekta binafsi, kuchochea uhai wa sekta binafsi ili tuweze kujenga uwezo wa watu wetu hasa vijana kuwa na mbinu za kujiajiri wenyewe”, Prof. Mkumbo alisema.

Waheshimiwa Mawaziri walihitimisha mazungumzo yao kwa kuishukuru Denmark kwa misaada inayoipatia Tanzania katika sekta mbalimbali. Ulitolewa mfano wa msaada wa Krone bilioni 1.95 uliotolewa na Denmark kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2014 hadi 2021.

Kwa upande wake, Mhe. Jorgensen alieleza kuwa Tanzania ni moja ya nchi za mwanzo kabisa barani Afrika kuanza ushirikiano wa kidiplomasia na Denmark katika miaka ya 1960. Hivyo, ameahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa kuzingatia vipaumbele vitakavyobainishwa na pande zote mbili.
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.
Dkt. Mwigulu akimuaga Mhe. Dan Jørgensen.
Picha ya pamoja.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Tausi Kida.
Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen akizungumza na Mhe. Prof. Mkumbo jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024.
Picha ya pamoja.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira ), Mhe. Dkt. Selemani Jafo (wa pili kushoto) akizungumza na Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024. Wa pili kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Denmark mwenye makazi yake nchini Sweden, Mhe. Grace Olotu.
Waziri wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen (wa tatu kulia) akizungumza na Mhe. Dkt. Jafo (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 5 Aprili, 2024.
Picha ya pamoja.


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia Programu ya Ruzuku ndogo inayotekelezwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) limesaini makubaliano ya kutoa sh 4.04 bilioni kwa mashirika yasiyo ya kiserikali 44 nchini ili kutekeleza miradi ya Uhifadhi wa Mazingira, Misitu, kuendeleza ufugaji nyuki, kutunza vyanzo vya Maji na uwezeshaji Jamii kiuchumi.

Utiaji saini wa Makubaliano hayo umefanyika leo April 4, 2024 katika Makao Makuu ya Jengo la Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na kuongozwa na Mwakilishi Mkaazi wa UNDP, Bw. Shigeki Komatsubara.

Miongoni mwa mashirika yaliyosaini mkataba wa kupatiwa fedha hizo ni Shirika la Connecting Youth Connecting Tanzania (CYCT) ambalo limekuwa likihamasisha uhifadhi wa mazingira, Misitu na Mabadiliko ya tabia nchi kuhusisha vijana, Wanawake na Wanafunzi na Kundi la watu Maalum

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Komatsubara amesema kuwa mashirika zaidi ya 400 yalituma maombi kuomba fedha za kutekeleza miradi midogo midogo nchini Tanzania bara na Zanzibar lakini ni mashirika 44 tu ndio yamefanikiwa.

“Hongereni sana leo kuwa miongoni mwa mashirika na asasi ambazo zimepata fursa kutekeleza miradi midogo Tanzania.

Bw. Komatsubara amesema anaimani kubwa mashirika ambayo yanapewa fedha hizo yatakwenda kutekeleza vyema miradi ambayo itagusa jamii hasa wanawake, vijana, Walemavu na Jamii za pembezoni.

“Tunatarajia miradi yetu itakwenda kuchochea maendeleo katika jamii ikiwepo pia kukabiliana na vichocheo vya uharibifu wa mazingira” amesema.

Naye Mwakilishi kwa niaba ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Bi. Lilian Lukambuzi akizungumza katika hafla hiyo alitaka mashirika yaliyopewa fedha hizo kuzitumia kama ilivyokusudia.

Amesema serikali itafuatilia miradi ambayo inakwenda kutekelezwa ili kuhakikisha inakuwa na tija.

Awali, mratibu wa programu ya ruzuku ndogo za GEF nchini, Bw. Faustine Ninga amesema haikuwa kazi rahisi kupitisha mashirika hayo machache kupata ruzuku kutokana na uhitaji mkubwa kutoka katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kamati ya Uendeshaji ya programu hiyo ya Ruzuku Ndogo za GEF ambayo inaundwa na wataalam kutoka sekta mbalimbali na taasis zisizo za Kiserikali kwa kushirikia na UNDP ilifanya kazi kubwa ya kuchambua maandiko ya miradi zaidi ya 400.

Hata hivyo, amesema kutokana na uhitaji kuwa mkubwa ni mashirika 44 tu ndio yalipitishwa, ijapokuwa mashirika mengine yalikuwa na madokezo mazuri ya miradi.

Hata hivyo ameyataka mashirika haya kufuata kanuni na taratibu za nchi na miongozi ya uendeshaji wa taasisi zisizo za kiserikali katika utekelezaji wa miradi yao ili miradi iwe na matokeo mazuri.

Amesema kamati ya ufuatiliaji miradi hiyo itakagua na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi yote ili kuhakikisha kuwa jamii zinanufaika.

Wakizungumza baada ya kusaini mikataba baadhi ya watendaji wa mashirika hayo walipongeza UNDP kwa kuendelea kutoa fedha za kutekeleza miradi midogo katika jamii.
Mratibu wa Shirika la CYCT, Bw. Mensieur Elly amesema hii ni mara ya kwanza shirika hilo kupata fedha kutoka kwa wahisani hao.

“Tunatarajia kushirikiana na wadau mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kutunza Ikolojia ya mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya “Go green, serve Nature “ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Siha, Mkurugenzi Siha, TFS West na North Kilimanjaro, Afisa mipango na maendeleo jamii, Afisa elimu, mwenyekiti wa Halmashauri, afisa Tarafa, afisa Mtendaji, madiwani na vikundi vya vijana na wanawake West Kilimanjaro katika kutekeleza na kupata matokeo chanya na yanayoshikika.

Nae mratibu miradi wa Shirika la WODSTA, Bi. Clara Chuwa amesema wanakwenda kutekeleza mradi kwa ajili kuwezesha kutunza mazingira na matumizi endelevu ya msitu na chanzo cha maji kijiji Cha lemanda, Kata ya Oldonyosambu, Wilaya ya Arumeru.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la SECCA, Bw. Esaya Yusufu amesema wanakwenda kutekeleza mradi wa upandaji miti na kuchimba kisima katika eneo la ikolojia ya Serengeti.

Mfuko wa mazingira Duniani (GEF) ulianzishwa mwaka 1992 na umekuwa na miradi katika nchi 136 Duniani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (Kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau, aliyefika Ofisini kwa Waziri wa Fedha kwa ajili ya kujitambulisha, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo wamejadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza wakati wa kikao chake na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau, aliyefika Ofisini kwa Waziri wa Fedha kwa ajili ya kujitambulisha, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo wamejadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (watano kushoto) na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka Wizara ya Fedha na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini baada ya kikao chao, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo Balozi huyo alifika kujitambulisha na pia kujadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)

Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameushukuru Umoja wa Ulaya kwa kutenga zaidi ya EURO milioni 703 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika kipindi cha miaka 7 kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka 2027.

Dkt. Nchemba ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chistine Grau aliyefika kujitambulisha rasmi.

Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa fedha hizo zimegawanywa katika awamu mbili ikiwemo awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka 4 ilitengewa zaidi ya euro milioni 426 ambapo mpaka sasa Umoja huo umetoa zaidi ya euro milioni 373 ambazo zimeelekezwa katika miradi kadhaa ikiwemo uchumi wa buluu, ujenzi wa miji ya kisasa, upatikanaji wa mitaji, utawala wa fedha, upatikanaji wa mitaji kwa sekta binafsi, usawa wa kijinsia na mradi wa kuendeleza masuala ya kidigiti.

Aliiomba EU kuangalia uwezekano wa kutumia sehemu ya fedha, zaidi ya euro milioni 200 zitakazotumika katika awamu ya pili ya program hiyo itakayoanza mwakani kitumike kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya barabara ya kutoka Mikumi hadi Kidatu yenye urefu wa kilometa 35 ili kuchochea uchumi na maendeleo ya wakazi watakaonufaika na barabara hiyo.

Kwa upande wake, Balozi mpya wa Umoja wa Ulaya, Mhe. Christine Grau, alisifu mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea nchini kupitia kwa ungozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya MUungano wa Tanzania, yaliyoifanya Tanzania kuendelea kuwa imara na kuvutia uwekezaji na mitaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Aidha, Mhe. Balozi Grau aliarifu kuwa majadiliano ya awali ya ushirikiano mwingine wa miaka 7 unaotarajiwa kuanza mwaka 2028 hadi 2034 yataanza rasmi mwakani 2025.

Mhe. Balozi Grau aliipongeza Tanzania kwa kuridhia na kusaini mkataba mpya wa ushiriakiano kati yake na Umoja huo ujulikanao kama SAMOA ambao pamoja na mambo mengine utaiwezesha Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya kuendelea kufanyakazi zake nchini.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akifafanua kuhusu utaratibu wa kurejesha fedha kwa wamiliki wa maduka ya kubadilisha fedha waliobatilishiwa leseni zao baada ya wenye maduka hayo kukidhi vigezo vya kisheria, bungeni jijini Dodoma.
Peter Haule na Josephine Majura, WF, Dodoma

Serikali imesema kuwa ilibatilisha leseni za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni yaliyokutwa na makosa mbalimbali yakiwemo ya kujihusisha na uhamishaji wa fedha nje ya nchi bila kuwa na leseni wala kibali cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, aliyetaka kufahamu sababu za maduka ya kubadilisha Fedha kuondolewa katika biashara na Wananchi wengi kupoteza ajira zao.

Mhe. Chande alisema kuwa mwaka 2016, Benki Kuu ya Tanzania ilifanya ukaguzi wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni na kugundua miamala mbalimbali kwa baadhi ya maduka inafanyika kinyume na matakwa ya sheria na kanuni za usimamizi wa maduka ya fedha za kigeni na udhibiti wa utakasishaji wa fedha haramu.

“Mwaka 2018 na 2019, Benki Kuu kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za Serikali ilifanya operesheni ya ukaguzi maalum kwenye maduka yote ya kubadilisha fedha za kigeni nchini na kubaini makosa mbalimbali yaliyosababisha Serikali kusitisha leseni kwa waliokiuka Sheria kwa mujibu wa Kanuni ya 36 (1)(b) na 2 (d) ya Kanuni za Biashara ya Kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015 iliyorejewa mwaka 2019 ”, alisema Mhe. Chande.

Mhe. Chande alisema kuwa makosa mengine yaliyobainika ni pamoja na kutofanya utambuzi wa wateja kabla ya kutoa huduma kinyume na kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Udhibiti wa Utakasishaji Fedha Haramu, Sura 423 na kanuni ya 17 ya Kanuni za Udhibiti wa Utakasishaji Fedha Haramu.

Aidha alisema kuwa kosa lingine lilikuwa kugawa miamala ya wateja kwa lengo la kukwepa kutunza kumbukumbu muhimu zinazoonyesha uhalali wa miamala kinyume na Kanuni ya 23 ya Kanuni za Biashara ya kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015 na kutokutoa stakabadhi za miamala kinyume na Kanuni ya 23(1) ya Kanuni za Biashara ya Kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015

Mhe. Chande alibainisha makosa mengine kuwa ni pamoja na kutokuwasilisha taarifa sahihi za miamala Benki Kuu na hivyo kuathiri upatikanaji wa takwimu muhimu kwa ajili ya sughuli za kiuchumi na baadhi ya maduka yalikuwa yanajihusisha na uhamishaji wa fedha nje ya nchi bila kuwa na leseni wala kibali cha Benki Kuu.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, aliyetaka kufahamu sababu za maduka ya kubadilisha Fedha kuondolewa katika biashara na wananchi wengi kupoteza ajira zao. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Fedha)
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Asasi za Kifedha Tanzania (TAMFI) limesema lina programu maalumu ya kuchangia uhifadhi wa mazingira na kupambana na ukataji miti kwa kuwezesha nishati safi ya kupikia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry katika kongamano la Wanawake katika fedha:Kukumbatia mabadiliko ya tabia nchi lililofanyika mwishoni mwa wiki.
Alisema katika kongamano hilo lenye nia ya kuchanganya jinsia na uendelevu wa mazingira ndani ya sekta ya fedha, kuwa kuna haja kwa wadau kama wao kuchukua hatua na kuunga mkono juhudi za serikali kukabili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwezesha wanawake nishati safi ya

"Ahadi yetu ya 'Kukumbatia Mabadiliko ya Tabianchi' inazidi mjadala tu; ni wito wa kuchukua hatua. Kwa kulingana na maono ya serikali ya ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, tunalenga kushughulikia vipengele muhimu vya maji, nishati mbadala, na mabadiliko ya tabianchi na kujitolea kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu namba kumi na nne (14)" alisema Winnie.

Mkutano huo uliopata ufadhili kutoka Foundation ya Charles Stewart Mott uliweka wazi ushawishi muhimu wa taasisi za kifedha kuwezesha wanawake ndani ya sekta ya fedha kuongoza mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.
Mwenyekiti wa Bodi ya TAMFI, Devotha Ntuke Minzi alisema ni jukumu la wanawake kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.

Akisisitiza athari zisizo sawa za mabadiliko ya tabianchi kwa wanawake, hasa nchini Tanzania na kote duniani, Minzi alitaka ushirikishi katika kufanya maamuzi na kutekeleza mipango kwa vitendo. Alihimiza haja ya kuongeza sauti za wanawake katika fedha kama waendeshaji muhimu wa suluhisho endelevu kwa changamoto hizi za kimataifa.

Naye Ofisa Programu wa TAMFI, Deodati Bernard alielezea mchango mkubwa wa wanawake kwa maendeleo ya Tanzania.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa wanawake na Wakurugenzi Mtendaji kutoka Taasisi za Fedha za Daraja la Kwanza na la Pili, pamoja na wajumbe kutoka Chama cha Benki Tanzania (TBA), Chama cha Nishati Mbadala Tanzania (TAREA), Mtandao wa Maji na Usafi Tanzania (TaWaSanet), New Faces New Voices (NFNV), Amshaamsha Foundation, IMED Foundation, Elico Foundation, Water.org, Kampuni ya Huduma za Nishati Endelevu (SESCOM) na wanawake katika nyanja mbalimbali za mfumo wa mabadiliko ya tabianchi nchini.
Dar es Salaam – On March 21, U.S. Ambassador Michael Battle, alongside Mafia District's Administrative Secretary, Hon. Olivanus Paul Thomas, commemorated the successful completion of the third phase of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation (AFCP) project to restore the historic Swahili ruins of Kua on Juani Island, within the Mafia Island archipelago.

From 2017 through 2022, the U.S. Embassy awarded a total of $434,929 (approximately Tshs 1.1 billion) to World Monuments Fund (WMF) via the AFCP program of the U.S. Department of State. This funding supported the preservation of these ancient ruins in a collaborative effort with the local community. The celebratory event at the Kua Ruins hosted local government officials, a delegate from the Ministry of Natural Resources, WMF representatives, and community members.

Nestled off Tanzania's coast on Juani Island, the ancient Swahili town of Kua traces back to the 13th century, standing as one of East Africa's largest medieval Swahili settlements. The site boasts a significant number of residential structures that have withstood the test of time, including a grand palace and five mosques. Protected under the Antiquities Act No. 10 of 1964, as amended by Act No. 22 of 1979, the Kua Ruins are a testament to Swahili architectural ingenuity and historical importance. Ambassador Battle noted, “Through the AFCP program, the U.S. has not only preserved the essence of Kua but also ensured local communities benefit from these preservation efforts.”

Since it's inception in 2001, the Ambassador’s Fund for Cultural Preservation (AFCP) has aimed to safeguard notable cultural heritage sites across the globe. The American people have generously contributed over one million dollars in grants since 2002, supporting a wide range of preservation projects in Tanzania. These projects include the restoration of the 18th-century Kizimkazi Mosque in Zanzibar, the ancient trade port ruins of Kilwa Kisiwani, the prehistoric rock art in Kondoa, the 19th-century Bwanga House in Pangani, and the historical Shumba and Micheweni mosques in Pemba, among others.

World Monuments Fund (WMF), the project's lead implementing organization, is a premier non-profit entity dedicated to preserving the world’s most iconic heritage sites. With over 50 years of experience in more than 90 countries, WMF’s skilled experts employ advanced preservation techniques to safeguard architectural and cultural landmarks worldwide.

Embracing Cultural Heritage and Partnership: U.S. Ambassador Michael Battle alongside District Administrative Secretary Olivanus Paul Thomas (4th from left), other district and community leaders and World Monument Fund (WMF) representatives at Kua Ruins, commemorating the completion of the Ambassador's Fund for Cultural Preservation’s (AFCP) project phase 3 for the restoration of Swahili ruins of Kua on Juani Island, Mafia. From 2017 to 2022, the U.S. Embassy awarded the WMF a total of $434,929 to preserve these ancient Swahili ruins in collaboration with local residents.

Chuo cha Usafiri wa Anga(CATC) kimefanya hafla ya kufunga Kozi mbili za ‘Area Control Procedure’ namba 35 na Kozi ya Ndege nyuki (Drone) namba 16 kwa wakufunzi hao kuhimizwa juu ya kufanya kazi kwa weledi.

Nasaha hizo zimetolewa Machi 08, 2024 na Mkuu wa Chuo cha CATC, Aristid Kanje wakati wa kufunga kozi hizo mbili ambazo zimeambatana na mafunzo ya weledi yaliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Chama cha Wamiliki wa Mashirika ya Ndege nchini (TAOA) Bi Lathifa Sykes.

CATC moja ya vyuo vinavyotoa kozi ya Usalama wa Usafiri wa Anga (ASTC) na ni moja kati ya vyuo tisa vyenye sifa hizo Afrika na 35 duniani.












Na Mwandishi Wetu.

Ubalozi wa Qatar Tanzania kwa kushirikiana na Tasisi ya Qatar Charity, kwa niaba ya Serikali ya Qatar, imewasilisha misaada muhimu ya kibinadamu kwa waathirika wa Maporomoko ya Udongo yaliyotokea Hanang mkoani Manyara. 

Shehena ya misaada hiyo iliyotolewa leo tarehe 18 Februari 2024 kwa kutumia ndege mbili za mizigo kutoka Qatar inalenga kugusa maisha ya wananchi wa Hanang walioathirika na maafa hayo ambayo madhara yake yalikuwa makubwa. 

Serikali ya Qatar imetoa kwa ukarimu misaada hiyo ya kibinadamu inayojumuisha chakula kikavu katika vifungashio 1,440 (Dry food basket), chakula kilicho tayari kuliwa katika vifungashio 3,024 (Ready to Eat canned food) na vifaa vya usafi wa wanawake jumla 4,200 (women’s dignity kit) na hivyo kufanya jumla ya tani 90 za shehena. 

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali imepokea kwa moyo wa upendo misaada hiyo itakayoleta faraja kwa Waathirika na kuahidi kufikishwa kwa Walengwa kama ilivyokusudiwa. 

Vilevile Mhe. Nderiananga ameeleza kuwa Serikali inatambua mchango wa wadau wote ikiwemo wananchi, sekta binafsi, asasi za kiraia na kidini, mashirika ya kimataifa na umoja wa mataifa kwa ushiriki wao katika kusaidia wananchi walioathirika na maporomoko ya tope katika wilaya ya Hanang'.

Akipokea Misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe Queen Cuthbert Sendiga ameishukuru Serikali ya Qatar kupitia Qatar Charity kwa misaada hiyo ya kibinadamu ambayo itakwenda kuwasaidia wananchi wa Hanang kurejea kwenye hali yao ya kawaida.

Aidha, Mhe Mkuu wa Mkoa amesema kuwa kupatikana kwa Misaada hiyo ni matokeo ya mahusiano mazuri ya nchi ya Tanzania na nchi za jirani ambayo yameimarishwa na serikali ya awamu ya sita Chini Rais  Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ndege ya mizigo iliyosheheni misaada hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga akishuka kwenye ndege hiyo mara baada ya kufanya makabidhiano ya msaada.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo fupi iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa KIA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wafanyabiashara pamoja na Wawekezaji wa Tanzania na Indonesia katika Mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji. Mkutano huo ulifanyika Jijini Jakarta katika muendelezo wa ziara yake ya Kitaifa nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji uliofanyika Jijini Jakarta katika muendelezo wa ziara yake ya Kitaifa nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2025.
Wawekezaji pamoja na Wafanyabiashara wakiwa kwenye mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji uliofanyika Jijini Jakarta nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2025.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji uliofanyika Jijini Jakarta nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2025.Wawekezaji pamoja na Wafanyabiashara wakiwa kwenye mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji uliofanyika Jijini Jakarta nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2025.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo Januari 25, 2024 amemsindikiza na kumuaga Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar Es Salaam mara baada ya kumaliza Ziara yake nchini Tanzania.

Rais Salvador alikuwa nchini kwa Ziara ya Siku Tatu, pamoja na maeneo mengine alitembekea katika kiwanda cha ‘Tanzania Biotech Products ltd’ (TBPL) na kuzungumza na wafanyakazi ambapo alisisitiza jukumu muhimu la TBPL katika jitihada za kutokomeza Malaria nchini.

Ziara za Viongozi wa Kimataifa kuja Tanzania ni fursa ambazo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuzifungua kwa lengo la kuendeleza ushirikiano baina ya Tanzania na Mataifa mengine Duniani ili kuleta maendeleo nchini.