Articles by "ELIMU"
Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga, Jennifer Dickson akifurahia tuzo ya Malkia wa Nguvu ajaye katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
------
Nyota ya Mwanafunzi wa Kike wa kitanzania Jennifer Dickson na mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga anayesoma elimu ya Chuo Kikuu mwaka wa pili nchini Rwanda katika Chuo cha Global Health Equity, akisomea fani ya Udaktari, inazidi kung’aa ambapo ametunukiwa tuzo ya Malkia wa Nguvu Ajaye 2024 katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.Tuzo hizo hutolewa na Clouds Media Group.

Maktaba aliyoianzisha Jennifer, inayojulikana kama maktaba ya kijamii ya Martha Onesmo, ilizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwaka huu ipo katika kata ya Msangeni kwa ajili ya kuwahudumia watu wote. Mgeni rasmi katika uzinduzi wake alikuwa ni Waziri wa Elimu, Profesa Adolf Mkenda.

Akiongea muda mfupi baada ya kupokea tuzo hiyo, alisema kuwa amefarijika kwa kiasi kikubwa kuona mchango wake katika jamii umetambuliwa na tuzo hiyo imezidi kumtia moyo wa kuendelea kufanya kazi za kijamii zenye mwelekeo wa kunufaisha watu wengi.

Alitoa shukrani kwa wazazi wake,marafiki zake na wa familia,na wafadhili mbalimbali ambao wamemsaidia kufanikisha ndoto yake ya kufungua maktaba ya kijamii ambayo imepelekea apate tuzo ya Malkia wa Nguvu ajae inayotolewa na kampuni ya habari ya Clouds.

Pia alitoa shukrani wa waandaaji wa tuzo hizo kwa kuona mchango wake katika jamii pia alitoa ushauri kwa vijana wenzake hususani watoto wa kike kujiamini na kupambana ili kufanikisha ndoto zao katika maisha na kuhakikisha hawabaki nyuma.

Kwa upande wa wazazi wake, walisema wamefurahi kuona kijana wao anapata mafaniko “Tuzo hii ni kielelezo kikubwa kwamba mtoto wa kike anaweza kama akiwezeshwa. Jennifer ni matokeo ya juhudi zake na ushirikiano wa jamii nzima inayomzunguka ukiaanza na sisi wazazi wake, ndugu zake wengine wa karibu hasa bibi yake mama Cecilia Ezekiel na jamii nzima ambayo ilishirikiana naye kwa hali na mali kuhakikisha anatimiza ndoto yake. Ni watu wengi wanamchango wao wa hali na mali katika kufikia hapa tulipo leo” Alisema Dk. Linda Ezekiel.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba hiyo, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amempongeza Jennifer kwa kufikia mafanikio hayo,”Ni jambo la kufurahisha kuona kijana wa umri wake anakuwa na ubunifu wa mradi ambao unaleta athari chanya kwa jamii hususani katika maeneo ya vijijini ,natoa wito kwake aendelee kupambana ili aweze kufanya mambo makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla”. Alisisitiza.

Wakati wa uzinduzi wa maktaba hiyo ya kijamii ya Martha Onesmo, mwanzilishi wake Jennifer alisema ndoto ya kuanzisha maktaba hiyo alikuwa nayo yangu anasoma kidato cha sita kwa ajili ya kuwezesha wakazi wa vijijini kupata maarifa.
Picha ya pamoja ya wanafamilia ya Jennifer na marafiki wa familia.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Dk. Kitila Mkumbo (kulia) akimpongeza mshindi wa tuzo la Malkia wa Nguvu ajaye,Jennifer Dickson katika hafla ya kutunuku tuzo hizo iliyofanyika jijini Dar es Salaam,katikati ni mwenyekiti wa bodi ya maktaba ya kijamii ya Mwanga iliyoanzishwa Jennifer, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Wanafamilia ya Jennifer na mwenyekiti wa maktaba ya Martha Onesmo wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Jennifer akiwa na wazazi wake.
Jennifer akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya maktaba ya Martha Onesmo,Profesa Bonaventure Rutinwa.

Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa, akiwa na wanafunzi wa kike waliofanya vizuri katika somo la hisabati muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi za laptop kutoka Barrick.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dk. Franklin Rwezimula (kushoto) akikabidhi cheti cha shukrani kwa Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa kwa niaba ya kampuni.
Mmoja wa wasichana waliofanya vizuri katika somo la hisabati, kutoka sekondari akipongezwa baada ya kupokea zawadi la Laptop kutoka Barrick
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari mkoani Morogoro walishiriki katika maadhimisho hayo
Wanafunzi wakishiriki kujibu maswali ya chemshabongo katika hafla hiyo.
---
Kampuni ya dhahabu ya Barrick nchini, imedhamini madhimisho ya Siku ya Hisabati Duniani ambapo kwa hapa nchini yalifanyika mkoani Morogoro kwa kuandaliwa na Chama cha Hisabati Tanzania ambacho kinashirikiana na Serikali kuongeza ufaulu wa masomo ya hisabati katika shule za msingi na Sekondari nchini.

Kwenye kilele cha maadhimisho hayo , Barrick ilieleza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha elimu nchini ikiwemo kufanikisha ufaulu wa masomo ya sayansi na TEHEMA mashuleni ili taifa lisibaki nyuma katika ulimwengu wa sayansi ya teknolojia

Pia imedhamiria kutoa hamasa na motisha kwa watoto wa kike watakaofanya vizuri katika masomo ya sayansi na kutoa wito kwa wasichana kujiamini na kuondoa dhana ya kwamba masomo ya sayansi ni kwa ajili ya wavulana.

Katika hafla hiyo wanafunzi wa kike watatu waliofanya vizuri katika somo la hisabati lililoandaliwa na Chama cha Hisabati nchini mwaka jana walizawadiwa na laptop za kisasa kila mmoja na kampuni ya Barrick .Wanafunzi hao wanatokea katika sekondari za Lumumba-Zanzibar,Canosa na Marian.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dk.Franklin Rwezimula, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo, alisema Serikali inaendeea kufanya mikakati mbalimbali kuhakikisha ufaulu wa somo la hesabu na masomo mengine ya sayansi unaongezeka na aliwapongeza wadau mbalimbali wanaounga mkono jitihada za Serikali katika kufanikisha suala hili.
In a groundbreaking display of innovation, Team Imperial Tech from Rise and Shine Secondary School in Ntinda, Uganda, has emerged as this year’s regional champions of the Sahara STEAMers Grand Demo Competition 2.0.

The competition, now in its second year, is organized by the Sahara Group Foundation and Asharami Uganda in collaboration with STEMCafe.

This year’s program, aimed at fostering innovation, creativity, and excellence in STEAM education among secondary school students in Africa, directly impacted over 200 students across the continent. The program, designed to provide participants access to deep-dive classroom learning, equipped the participating students with the practical knowledge and skills required to generate innovative solutions for real-world problems. Therefore, helping to create a pipeline of young, confident social innovators across Africa.

The top three teams to emerge from the respective National Demo Competitions in 2023 went on to represent their respective countries in the Grand Demo Day Competition. All twelve teams presented ingenious prototype designs of their solutions spanning various sectors, including home automation, agriculture, security, energy, health, and transportation before a panel of judges.

The Grand Demo Competition showdown was indeed a keenly contested competition among teams hailing from Uganda, Nigeria, Kenya, and Tanzania. Emerging as this year’s regional champions was Team Imperial Tech, comprising the following students from Rise and Shine secondary school: Anyango Winnie, Bakunga Arafat, Male Raymond, Nalweyiso Kelva, and Nambi Tracy. They developed a Soil Moisture Detector, a farm-friendly solution aimed at preventing over-cultivation and promoting soil quality and increased productivity.

Securing the second and third positions were Team Smart Blind Walking Stick from St Georges Girls Secondary School, Nairobi, Kenya, and Team Young Genius from Oshodi High School, Lagos, Nigeria, respectively. Team Smart Blind Walking Stick developed an advanced solution to aid visually impaired individuals, utilizing Arduino, distance sensors, and a buzzer. While Team Young Genius engineered an innovative Domestic Drainage System to address the issue of drainage blockage in our society by automating the drainage cleaning process, thus keeping our environment pristine.

Participating groups from Tanzania include Team KATONE from Tambaza Secondary School with their Water Salinity and PH Monitoring solution; an advanced sensor that delivers precise real-time water level data. Team Young Girls from Kisutu Secondary School with their groundbreaking Water Salinity and pH Monitoring device. This innovative tool detects contaminants promptly, allowing for a timely response to safeguard water quality for both consumption and environmental preservation. And Team STF from Tambaza Secondary School with their Car Alcohol Detection System that effectively prevents drunk driving.

Speaking at the Grand Demo Competition, Ejiro Gray, Director of the Sahara Group Foundation, expressed immense delight at the students' commitment and determination throughout the stages of the program. Reflecting on the nine-month program, she highlighted its success in inspiring creativity and critical thinking skills among students, fostering a new wave of problem solvers for Africa.

Ejiro Gray commended the winning teams and urged all participants to apply the skills acquired from the program to the benefit of their communities and society at large. She extended her gratitude to the participating students, teachers, school administrators, as well as the implementing partner STEMCafe and other stakeholders for their invaluable contributions to the program's success.

Also speaking at the event, Moses Abimpeire, Business Development Manager at Asharami Uganda Limited, stated that “Programs like the Sahara STEAMers initiative that help to foster innovation, critical thinking, and problem-solving skills among the youth are instrumental in shaping a brighter future for the country.” He affirmed Asharami's unwavering dedication to supporting such initiatives, recognizing them as catalysts for positive change and sustainable progress that align with the company's vision for a thriving and innovative Uganda.

As the curtains draw on the Sahara STEAMers Grand Demo Competition 2.0, the impact of this transformative initiative echoes beyond the competition arena. The inspiring innovation witnessed at this event underscores the program's pivotal role in nurturing a generation ready to tackle Africa's challenges with ingenuity and resilience. This accomplishment resonates not only as a testament to the potential within our youth but as a beacon illuminating the path towards a future where innovation thrives for the betterment of our communities and the continent at large.

The Sahara Group Foundation and Asharami Uganda remain steadfast in their commitment to advancing programs that propel Africa into a future characterized by innovation, sustainability, and inclusivity. Through collaborative efforts and strategic initiatives like Sahara STEAMers, we will continue to help pave the way for a brighter tomorrow, where the brilliance of African youth shines as a driving force for positive change and progress.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amefungua Warsha na Mkutano mkuu wa mwaka 2024 wa Chama cha Wakutubi Tanzania chenye lengo la kujadili Mabadiliko kwa ajili ya Mazingira Endelevu ya Kidijitali katika Ukutubi na Sayansi kilichofanyika Mjini Babati Februari 26, 2024.

Mhe. Mkuu wa Mkoa akijibu hoja iliyotolewa kwenye risala ya chama hicho kuhusu mkoa wa Manyara kukosa maktaba, ameahidi kuwa Ofisi ya mkuu wa Wilaya wameahidi kutoa eneo kwaajili ya kuanza ujenzi mara moja wa maktaba ya mkoa. Aidha sendiga amewashauri wakutubi nchini kuwa sehemu ya kusoma vitabu badala ya kuwa watunzaji pekee katika maeneo wanakofanya kazi hiyo ya ukutubi.













Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amefungua Warsha na Mkutano mkuu wa mwaka 2024 wa Chama cha Wakutubi Tanzania chenye lengo la kujadili Mabadiliko kwa ajili ya Mazingira Endelevu ya Kidijitali katika Ukutubi na Sayansi kilichofanyika Mjini Babati Februari 26, 2024.

Mhe. Mkuu wa Mkoa akijibu hoja iliyotolewa kwenye risala ya chama hicho kuhusu mkoa wa Manyara kukosa maktaba, ameahidi kuwa Ofisi ya mkuu wa Wilaya wameahidi kutoa eneo kwaajili ya kuanza ujenzi mara moja wa maktaba ya mkoa. Aidha sendiga amewashauri wakutubi nchini kuwa sehemu ya kusoma vitabu badala ya kuwa watunzaji pekee katika maeneo wanakofanya kazi hiyo ya ukutubi.

Vilevile Mkuu wa Mkoa amekipongeza Chama cha Wakutubi Tanzania kwa uamuzi wao wa kuchagua Mkoa wa Manyara, na hususan Mji wa Babati kuja kufanyia Warsha na Mkutano Mkuu wa mwaka kwa mara ya kwanza tangu Chama kilipoasisiwa mwaka 1973. “Naamini uchaguzi ulitokana na sio tu urahisi wa kufika hapa Babati kutokea kona zote za Jamhuri yetu, bali pia uwingi na ubora wa vivutio vya utalii vya kiwango cha kimataifa, Hongereni sana”. Alisema Mkuu wa Mkoa.

RC Sendiga amewashauri Chama cha Wakutubi nchini kuongeza ubunifu katika kuendana na kasi ya utandawazi ili kuweza kuhamasisha jamii kujitokeza kusoma vitabu. Mkuu wa Mkoa ameongeza na amesema ni lazima Chama hicho sasa kifikirie mbali zaidi katika kukuza na kubadilisha sekta hiyo ya usomaji wa vitabu ili kuendana na ulimwengu wa kidijitali.

Akisoma risala yao kwa mgeni rasmi Ndg LEONTIN NKEBUKWA Mwenyekiti wa TLA ameiomba serikali kuingilia kati tabia ya waajiri wa baadhi ya taasisi kutowapa haki wakutibu wao kujiunga na Chama hicho hali inayopelekea kukosa fursa ya kueleza kero mbalimbali zinazowakabili kupitia Chama hicho.

Pamoja na hilo ndg Nkebukwa ameomba uwekezaji ufanyike kwenye sekta hiyo katika uwekezaji wa miundombinu ya kidijitali kuendana na kasi ya mabadiliko ya dunia ya sasa ambapo ametaja baadhi ya mahitaji muhimu kuwa ni pamoja na kompyuta na kamera.
Kama ambavyo tumekuwa tukishirikiana mara zote katika miradi ya Serikali sisi kama Wanamanyara, Serikali imeshatufanyia kazi kubwa sana, sisi Wanamanyara wenyewe tunafanya nini?

“Mpe Maua, Atabasamu Asome Kifalme”, Ni kampeni ambayo mkoa tumeiandaa kwa lengo na makusudio ya Kuboresha Sekta ya Elimu, kampeni hii itasaidia upatikanaji wa viti na meza na Madawati.

Shahuku yetu kubwa ni kuona watoto wetu wanasoma wakiwa wamekaa kwenye madawati, viti na meza ambavyo vitakuwa vimechangiwa na wewe kwa upendo.

Mhe. Queen Cuthbert Sendiga 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara. 

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele (kulia) akishiriki Matembezi ya ufunguzi wa wiki ya sheria Kitaifa Mkoani Dodoma Januari 27,2024. Matembezi hayo yaliongozwa na Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Akson na viongozi wengine mbalimbali wa Makama. Maadhimisho ya Wiki ya sharia yalianza Januari 24,2024 na yanataraji kufikia tamati Februari 1, mwaka huu. (Picha na NEC).
Na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/MMG

Hanang', Katesh 27 Januari 2024: Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga mapema leo ameongoza zoezi la upandaji wa miti lililoendana na ukataji wa keki kwa ajili kusherekea miaka 64 ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Akiongoza zoezi hilo la upandaji na kukata keki lililofanyika katika Shule ya Sekondari ya Katesh - Hanang, Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema Miti zaidi ya 3,000 imepandwa katika maeneo yaliyoathiriwa na maporomoko ya tope, mawe na magogo ikiwa ni njia mojawapo ya kurejesha uoto wa asili uliopotea kufuatia uharibifu mkubwa wa mazingira uliosababishwa na mafuriko hayo yaliyotokea mwishoni mwa mwaka 2023. Kwa mwaka 2024, Mkoa wa Manyara umejipanga kupanda miti milioni 10.

Zoezi hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mhe. Fredrick Sumaye Waziri Mkuu Mstaafu, Wakuu wa Wilaya wote wa Mkoa wa Manyara, Wakuu wa Taasisi Mbalimbali, Wakuu wa Idara pamoja, wananchi pamoja na watoto walioathirika katika maporomoko hayo.

Pamoja na hayo, Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Wizara ya Afya umetekeleza zoezi la uhamasishaji wa mwezi wa saratani ya mlango wa kizazi, ambapo zaidi ya watu 328 katika Wilaya ya Hanang' wamejitokeza kufanya uchunguzi wa awali.

Aidha, elimu na hamasa inaendelea kutolewa kwa wananchi ili waweze kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu kwa wale watakaobainika kuwa na viashiria vya saratani.
In an inspiring event that seamlessly blended creativity, innovation, and a steadfast commitment to shaping Africa’s future, Sahara Tanzania Limited, a Sahara Group downstream company, and Sahara Group Foundation, the social sustainability vehicle for Sahara Group, hosted the first edition of the Sahara STEAMers Programme National Demo Day competition.

The Sahara STEAMers programme, an afterschool initiative in partnership with STEMCafe, was established in 2022 with the primary aim of fostering innovation, creativity, and excellence in Science, Technology, Engineering, Arts, and Mathematics (STEAM) education among secondary school students in Africa.

Equipping participants with the knowledge and skills required to create innovative solutions addressing real-world problems across various sectors, including energy, agriculture, security, healthcare, and transportation, the programme is instrumental in creating a pipeline of Africa’s next generation leaders and social innovators.

The Tanzanian Demo Day Event this year featured students from Tambaza Secondary School and Kisutu Secondary School. Collaborating in teams, these students passionately presented their innovative solutions to a panel of judges. The Demo Day showcased a diverse group of young Tanzanian problem solvers with brilliant prototype designs aimed at tackling prevalent social issues in their communities.

Deeply impressed by the students' unwavering dedication to making a tangible impact in their communities at such a young age, Ejiro Gray, Director of Sahara Group Foundation, lauded the students' passion, intelligence, creativity, and problem-solving skills. She stated that, for some of the students, their participation in the Sahara STEAMers programme marked their first real interaction with technology and its practical applications in addressing real-world challenges.

Gray extended her heartfelt congratulations to all participants, urging them to persist in cultivating their newfound skills and embracing future opportunities to refine them for driving positive societal change. In conclusion, Gray affirmed that the inspiring display witnessed at the event was not merely a fleeting moment but a clear manifestation of the steadfast commitment of both Sahara Group Foundation and Sahara Tanzania Limited to empower young minds across Africa. This commitment is geared towards nurturing a future generation equipped to lead with innovation, compassion, and a lasting impact, thereby shaping a world where positive change becomes an inherent part of their journey.

Applauding the outstanding accomplishments of the participating students, Kunle Onadeko, Terminal Operations Manager at Sahara Tanzania Limited, underscored the pivotal role of the Sahara STEAMers programme in nurturing young talents and fostering their innovative skills. He expressed, "The Sahara STEAMers programme transcends being a mere initiative; it acts as a catalyst for transformative change.

Onadeko further emphasized that the quality of innovations on display is proof of the significant impact that comes from investing in young people and igniting their minds to see no limits. He encouraged the students to continue on this innovative thinking pathway, stating that the future of Tanzania, and Africa at large, is truly sustainably bright.

After an engaging and lively competition, the judges praised the students for their ability to conceive and develop viable solutions before announcing the winners.

Team Katone from Tambaza Secondary School clinched the top position with their innovative Smart Water Leveling System, an advanced sensor that delivers precise real-time water level data. The Smart Leveling System facilitates efficient water distribution and will further encourage sustainable water management practices.

In a close pursuit, Team Young Girls from Kisutu Secondary School achieved the first runner-up position with their groundbreaking Water Salinity and pH Monitoring device. This innovative tool detects contaminants promptly, allowing for a timely response to safeguard water quality for both consumption and environmental preservation.

Securing the second runner-up position was STF from Tambaza Secondary School. The team devised a Car Alcohol Detection System that effectively prevents drunk driving. This solution seamlessly integrates alcohol detection technology into vehicles' ignition systems, ensuring only sober drivers can start the vehicle.

As we celebrate the remarkable innovations showcased on this momentous day and witness the rise of Africa's next generation social innovators, it is evident that the nexus between education and innovation plays a pivotal role in Africa's advancement. Through empowering initiatives like the Sahara STEAMers programme, Sahara Tanzania Limited and Sahara Group Foundation are actively shaping a trajectory for a more resilient, prosperous, and sustainable Africa.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC inashiriki katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Utaratibu huu wa kushiriki katika maonesho mbalimbali nchini ni sehemu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kutoa elimu ya Mpiga Kura endelevu ambapo wadau mbalimbali wa Tume hufika katika Banda hilo na kupata elimu hiyo.

Maonesho haya ambayo huandaliwa na Mahakama ya Tanzania ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya sheria na kuanza kwa mwaka mpya wa Mahakama.

Mwaka huu maonesho haya yamebeba kauli mbiu isemayo "Umuhimu wa Dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa:Nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha mfumo Jumuishi wa Haki Jinai" yameanza tarehe 24 Januari,2024 na yanatarajia kumalizika tarehe 30 Januari, 2024.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Cuthbert Mapunda (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Cuthbert Mapunda (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.
Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bi.Neseria Leng’ida (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma
Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakiwa katika banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayoendelea jijini Dodoma katika viwanja vya Nyerere Square.

Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakizungumza na mdau aliyetembelea banda la Tume katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma

Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakizungumza na mdau aliyetembelea banda la Tume katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Loshilu Saning’o (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.
Kaimu Meneja wa Mradi wa Afya wa GIZ Tanzania Erick Msoffe kulia akikabidhi vifaa vya Tehama wa kwanza kushoto ni Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi Mark Tanda akifuatiwa na Mratibu wa GIZ Apolinary Primus
Sehemu ya Vifaa hivyo

Na Oscar Assenga, KOROGWE.

Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) limetoa msaada wa vifaa vya tehama katika Hospitali ya Mji wa Korogwe ya Manundu na kuweka miundombinu ya Intaneti,Ufugaji wa Mfumo wa kieletroniki ambao ni mfumo wa taarifa za usimamizi wa Hospitali za Serikali ya Tanzania (GoTHOMIS) pamoja na kufanya mafunzo endelevu kwa watumishi.

Ambapo hadi sasa zaidi ya wafanyakazi 150 katika hospitali ya Korogwe tayari wamefundishwa jinsi ya kutumia mfumo wa GoTHOMIS ambapo uwekezaji wake wa awali umegharimu Milioni 200,000,000 uliofanywa na GIZ hadi sasa na msaada zaidi ya kuifundi umepangwa ili kuhakikisha lengo linafikiwa ifikapo mwaka 2025.

Akizungumza wvakati wa makabidhiano rasmi ya vifaa vya Tehama, Kaimu Meneja wa Mradi wa Afya wa GIZ Tanzania Erick Msoffe amesema kuwa mpango huo unalenga kubadilisha taratibu za kiutawala na kiafya katika hospitali hii kwa kuondoa matumizi ya kumbukumbu za karatasi, kuboresha uhifadhi na upatikanaji wa takwimu za wagonjwa, kuongeza hospitali ufanisi na kupunguza makosa katika takwimu.

Alisema kwa niaba ya Serikali ya Ujerumani ambao ni wafadhili wao lakini pia wameshirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya pamoja na Ofisi ya Rais Tamisemi wamekuwa wadau kwa mkoa wa Tanga kwa miaka tisa kwa awamu ya miaka mitatu mitatu.

Msoffe alisema kuwa mara nying wamekuwa kwenye awamu uliyoanza mwaka 2023 na itakwenda mpaka 2026 kwa mkoa wa Tanga na wana jumla ya Hospoitali 18 wanazozisaidia lakini katika eneo la Tehama pamoja na kwamba huyko nyumba wamefanya kazi na Hospitali nne kwenye eneo hilo lakioni watawasapoto kuweka miunbdombi na kuwafanya mafunzo watumishi waweze kuutumia.

“Kwanini tupo Korogwe kuhakikisha sisi kama wadau na Serikali ikiwemo Hospitali wanaweza kufanya juhudi za kipekee kuona ni gharama gani zinahitajika ili kuitoa Hospitali ya wilaya kutoka kwenye matumiz ya mifumo ya katarasi na kwenda katika asilimia 100 ya matumizi ya Kiletroniki”Alisema

Alisema katika mafanikio yatakayopatikana katika hospitali ya Korogwe, yatatumiwa na serikali ya Tanzania kuongeza mageuzi haya ya kidijitali kwa hospitali nyingine chini Tanzania.

“GIZ inaipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuweka mazingira bora ya kisera na kutoa msaada wa kitaalamu katika kuboresha huduma za afya chini Tanzania”Alisema.

Alisema maboresho hayo yanayoendelea katika mifumo ya kidigitali na hasa mfumo wa GOTHOMIS ambao ni moja ya mifano tosha ya dhamira ya Serikali ya Tanzania katika kusaidia vituo vya afya kuboresha huduma za afya kupitia teknolojia ya kidijitali.

Hatua hiyo ni moja ya mambo ya msingi ya kuongeza ufanisi Hospitali ya Mji wa Korogwe inatangaza kwa fahari uamuzi wake wa kuachana na mifumo inayotumia makaratasi kabisa. Hospitali hiyo inakumbatia manufaa ya teknolojia katika kuimarisha huduma za afya na kurahisisha shughuli mbali mbali.

Uamuzi huo umekuja baada ya ongozi na wafanyakazi kutambua changamoto zinazoendelea kukabili mfumo wetu wa huduma za afya zikiwemo uhaba wa watumishi, kazi kubwa inayowakabili watumishi kwa kujaza karatasi nyingi, takwim duni lakini pia muda mrefu ambao wagonjwa hukaa hospitalini kupata huduma.

Kwa hiyo hospitali ya Korogwe imejitolea kutumia maendeleo ya kidijitali ili kutoa huduma ya hali ya juu kwa wateja wake. Kuachana na matumizi ya makaratasi na kuharnia mifumo ya kidigitali ni tatua muhim katika kufikia lengo hili.

Deutsche Gesellschaft fur Internationale Zusammenarbeit (GIZ) GmbH kupitia mpango wake wa afya wa Kuboresha Huduma ya Afya Tanzania (ICP) ni mshirika wa muda mrefu na wamekuwa wakisaidia mkoa wa Tanga na haswa hospitali ya Korogwe kutekeleza afua za afya za kidijitali ambazo zinalenga kuongeza fanisi na ubora wa huduma za afya.

Awali akizungumza Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Mji wa Korogwe Dkt Heri Kilwale alisema kuwa kubadilika kutoka matumizi ya karatasi na kutumia mifumo ya kidijitali itawasaidia watoa huduma za afya kuweza kupata taarifa za mgonjwa kwa wakati na salama.

Alisema pia kutapunguza muda ambao wafanyakazi hutumia kufanya kazi za kujaza makaratasi mengi na hivyo wataalamu wa afya wataelekeza zaidi muda katika kutoa huduma kwa wagonjwa na hivyo kupelekea kuongezeka kwa ubora wa huduma zinazotolewa.

Korogwe ni miongoni mwa hospitali chache ambazo zimeanza kutumia toleo jipya la GoTHOMIS na kva msaada wa mara kwa mara kutoka kwa serikali, ongozi wa hospitali na washirika wa maendeleo, inatarajiwa kuwa hospitali ya Korogwe itafanikiwa katika dhamira yake ya mabadiliko kutoka matumizi ya karatasi Kwenda katika mifumo ya huduma za kidijitali na kwamba. Serikali itapanua msaada huo kwa hospitali zingine baada ya hapo.