Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kutwa Ingri mara baada ya kuwasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa lengo la kuzindua shule hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (kushoto) akipiga makofi mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Rorya wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara. Aliyevaa kofia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evance Mtambi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Wa pili kutoka kushoto) akisisitiza jambo wakati akielekea kuweka jiwe la msingi katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Rorya alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evance Mtambi na kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Dkt. Khalfan Haule.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kutwa Ingri mara baada ya kuzindua shule hiyo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Rorya.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Dkt. Khalfan Haule wakati akifafanua jambo kuhusu Shule ya Sekondari ya Kutwa Ingri kabla ya Waziri huyo kuzindua Shule hiyo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.
Mwonekano wa ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya uliowekwa jiwe la msingi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara.
Mwonekano wa madarasa ya Shule ya Sekondari ya Kutwa Ingri iliyozinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akivalishwa skafu na vijana wa Skauti mara baada ya kuwasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa lengo la kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Mara.

Na Veronica Mwafisi-Rorya.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amezindua Shule ya Sekondari ya Kutwa Ingri huku akiwasisitiza wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii kwa maendeleo yao ya baadae na taifa kwa ujumla.

Mhe. Simbachawene amesema hayo tarehe 2 Oktoba, 2024 wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya mkoani Mara ikiwa ni siku yake ya pili ya kukagua utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo katika mkoa huo.

Waziri Simbachawene amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetekeleza miradi mingi ikiwemo ya elimu hivyo ili kuunga mkono jitihada za Rais, wanafunzi hao hawana budi kusoma kwa bidii.

Shule nzuri namna hii kujengwa kijijini ni maendeleo makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita, hivyo ni wajibu wenu ninyi wanafunzi kusoma kwa bidii kwa maendeleo yenu na taifa kwa ujumla,Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Ujenzi wa Shule ya Sekondari Ingri umeigharimu Serikali kiasi cha shilingi milioni 584 mpaka kukamilika kwake ambapo inajumuisha madarasa, maabara, chumba cha TEHAMA na Maktaba.

Ujenzi wa shule hiyo umewaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kwa wanafunzi hao na kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule waliokuwa wakisoma awali.

Mhe. Simbachawene amewasisitiza wanafunzi na watumishi wa shule hiyo kutunza majengo na vifaa vyote vilivyomo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Simbachawene amezindua ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya utakaotumika kufanya shughuli mbalimbali kwa maendeleo ya Halmashauri hiyo.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: