.jpeg)
Jijini Dar es Salaam jana kulishuhudiwa mjadala muhimu uliowakutanisha
wadau wa tasnia ya muziki kupitia jukwaa la AfroExchange,
lililodhaminiwa na Johnnie Walker, kwa lengo la kujadili namna ya
kuufikisha muziki wa Tanzania kwenye masoko ya kimataifa.
Mkutano huo ulikuwa mwanzo wa mfululizo
wa mazungumzo chini ya AfroExchange, unaolenga kubaini njia za kuweza
kukuza na kusambaza sanaa na muziki wa Afrika nje ya mipaka yake. Katika
hatua ya kwanza, mjadala uliwaweka DJs katikati, ukitambua nafasi yao
muhimu kama wachochezi wa ladha ya muziki, waunganishaji wa masoko na
daraja la kuifikisha sauti ya Afrika watu wengi zaidi.
Washiriki walijadili kwa kina changamoto zinazokwamisha muziki wa
Tanzania kupenya katika soko la kimataifa, huku wakisisitiza fursa
zilizopo kwa DJs katika kusukuma muziki huo kuvuka mipaka.
Mbali
na mazungumzo, AfroExchange pia ilitangaza hatua ya utekelezaji. Kupitia
mpango huo, DJs wa Tanzania watadhaminiwa kushiriki kwenye tukio la DJ
Consequence nchini Nigeria, fursa itakayomuwezesha kupata uzoefu wa
kimataifa pamoja na kujenga mtandao.
Hatua hii inaashiria mwanzo wa juhudi za kuimarisha ushirikiano ndani ya tasnia ya muziki barani Afrika, huku ikifungua milango kwa vipaji vya Tanzania kufikia masoko mapya.
AfroExchange inaendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha wadau, kuchochea mazungumzo yenye tija, na kuleta fursa zitakazosaidia muziki wa Tanzania kusikika kimataifa.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments: