Articles by "HABARI PICHA"
Showing posts with label HABARI PICHA. Show all posts
Stanley Kafu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, akizungumza wakati wa mahafali ya pili ya mpango endelevu wa kuwainua kiuchumi wanawake wajasiriamali ujulikanao kama WEP yaliyofanyika tarehe 23 Aprili, 2024, Mjini Arusha.
Mshindi wa kwanza Beatrice Alban Msafiri (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Mshindi wa tatu Rukia Said Mohamed (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu, Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (wa kwanza kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Mshindi wa pili Catherine Assenga (wa pili kulia), Zainab Nungu Mkuu wa Kitengo cha Mikopo, Exim Bank (wa kwanza kushoto), na Faraja Nyalandu Mkurugenzi Mtendaji wa Ndoto Hub (kulia) wakifurahi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu wakati wa mahafali ya mafunzo ya ujasiriamali, biashara na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali chini ya mradi wa benki hiyo yajulikanayo kama WEP katika tukio lililofanyika tarehe 23 Aprili 2024 mjini Arusha.
Washindi na baadhi ya washiriki wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Exim Bank wakati wa mahafali ya kumaliza mafunzo ya biashara, ujasiriamali, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali. Mafunzo hayo yalitolewa na Exim Bank chini ya mpango wake wa Kuwainua Kiuchumi Wanawake (WEP) na mahafali hayo yamefanyika tarehe 23 Aprili, 2024 mjini Arusha.
---
Exim Bank, kupitia Mpango wake wa Kuwawezesha Kiuchumi Wanawake (WEP), imetoa mafunzo kuhusu masuala ya ujasiriamali, biashara, na uwezeshaji kwa wanawake wajasiriamali kama sehemu ya kuunga mkono ujumuishwaji wa watu wote, wakiwemo wanawake, katika mipango mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania.

Kupitia mpango wake wa ‘Exim Cares’, mwaka jana (2023) Exim Bank ilizindua Mpango wa Kuwakwamua Kiuchumi Wanawake ujulikanao ‘Women Empowerment Program (WEP)‘ wenye lengo la kuongeza ushirikishwaji na kuleta usawa kwa wanawake barani Afrika, hasa katika nchi ambazo zina matawi ya benki hiyo ikiwemo Tanzania, Comoros, Djibouti na Uganda.

Akizungumza katika mahafali hayo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Exim Bank, Stanley Kafu, anasema, “Ukiwa mwaka wa pili mfululizo wa mpango wa Kuwakwamua Wanawake Kiuchumi (WEP), Exim Bank tunafuraha kubwa kuwa sehemu ya mafanikio haya na tunawapongeza washiriki wote kwa kuanza na kumaliza salama mafunzo haya kuhusu ujasiriamali, uwezeshaji, na biashara.”

Washindi watatu, wa awamu hii ya kwanza mwaka huu, walipata zawadi za pesa taslimu zilitolewa kwa washindi watatu ambapo mshindi wa kwanza, Beatrice A. Msafiri, akizawadiwa kiasi cha TZS 8,000,000, mshindi wa pili, Catherine Assenga akipata TZS 5,000,000 na mshindi wa tatu, Rukia S. Mohamed akiondoka na TZS 3,000,000. Pia, wahitimu wote walipata fursa ya kuweza kupata mikopo bila riba kutoka Exim Bank ili waweze kujiendeleza kiuchumi.

Exim Bank inaamini uwezeshaji wa wanawake na ujasiriamali unabaki kuwa sehemu muhimu ya mipango ya maendeleo nchini Tanzania na barani Afrika kijumla. Hii inadhihirishwa na ongezeko la idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi katika sekta mbalimbali kama siasa, kijamii na kiuchumi.

Akielezea kuhusu malengo ya mradi, Kafu alisema, “Mpango huu utakuwa ni endelevu kwa muda wa miaka mitano na tunatarajia kuwafikia wanawake zaidi ya 600,000 ifikapo mwaka 2028.”

Kafu anasisitiza kuwa Mpango wa WEP ni sehemu ya mkakati mkubwa na wa kina unaolenga kutengeneza jukwaa la wanawake ili waweze kufanikiwa na kustawi katika maisha yao, hasa kwenye eneo la uchumi.

Exim Bank imekuwa na itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo kwa Watanzania wote. Programu hii inawiana na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na itakuwa chachu katika kuimarisha ustawi wa kijamii na kiuchumi kwa wanawake.

Mkurugenzi wa Lamata Village entertainment, Bi. Leah Mwendamseke ‘Lamata’ akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA (Ukweli Upe Muda) itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.
Akizungumza leo Aprili 23, 2024 katika Uzinduzi wa app mpya ya VTV ambapo ndani yake unaweza kustream tamthilia mpya kabisa ya EZRA inayoandaliwa na kampuni ya Lamata Village entertainment, Lamata amesema kuwa tamthilia EZRA ndani yake kuna visa na mikasa, story ya aina yake ambayo itawaacha watazamaji na wasikilizaji mdomo wazi huku ukitaka kujua yaliyojiri.

Pia alitoa shukrani zake za kipekee kwa Uongozi wa Bodi ya Filamu kwa kushirikiana nao katika uzinduzi huo, huku akiwamwagia maua ya pekee kwa Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kuweza kuwashika mkono na kufanikisha kazi hiyo.Mshehereshaji Bw. Evance Bukuku akizungumza katika halfa ya uzinduzi wa Tamthilia ya EZRA na app ya VTV.Kwa upande wao Vodacom Tanzania wamewaalika watazamaji kuweza kupakua app ya VTV ili kuweza kuiona tamthilia hiyo kidijitali zaidi.

Usibaki nyuma! pakua app ya VTV leo google play au Appstore ufaidi mchapo mzima wa Ezra na burudani nyingine mbalimbali.

Wageni waalikwa.
Meneja wa Lamata Village entertainment, Bw. Danny Nyalusi akitoa machache.
Waigizaji waliopo katika tamthilia ya EZRA.
Viongozi mbali mbali wakiwa na waigizaji.
Wasanii mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.

Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga
Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga.
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika.
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika akizungumza na madereva wa bodaboda pikipiki maarufu kama bodaboda, bajaji na daladala.
Na Oscar Assenga, TANGA.

Shirika la Amend Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Switzerland Nchini,wameendesha zoezi la utoaji wa Elimu ya Usalama Barabarani kwa Madereva Daladala na Bodaboda Jiji la Tanga ikiwa ni sehemu ya kupunguza na kutokomeza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa madereva.

Akizungumza wakati wa utoaji wa Elimu hiyo ya Usalama Barabarani iliyofanyika Aprili 16,2024 katika Stendi ya Pongwe Jijini hapa,Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi, amewaambia waandishi wa habari kuwa lengo ni kuwafikia Madereva 500 na mpaka sasa Madereva 300 tayari wameshafikiwa katika awamu ya kwanza,

Alisema kwamba wamewafikia madereva wa pikipiki maarufu kama (Bodaboda) kuwapa mafunzo ya Usalama Barabarani na waliohitimu wamepewa vyeti huku akieleza wataendelea na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa awamu ya pili ambao utaanza mwezi mei mwaka huu na itakuwa endelevu.

Scholastica aliwataka Madereva wa vyombo vyote vya moto kuzingatia sheria za Usalama Barabarani ili kupunguza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa Madereva,

"Niwaombe Madereva wote hususani wa Bodaboda tuzingatie Usalama Barabarani tusibebe watoto chini ya miaka 9 kwa sababu hawana uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya Barabarani na maisha yako ni muhimu zaidi kuliko pesa wanayoitafuta"Alisema

"Tuzingatie Usalama kwanza ili ajali zipungue zibakie zile ambazo haziepukiki ikiwemo kupasuka kwa tairi ,kukatika kwa stelingi au tatizo lolote la kiufundi katika vyombo vyetu vya moto"Alisisitiza Scholastica

Kwa upande wake Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika aliwataka madereva wote kwenda darasani kama sheria inavyowataka kufanya hivyo,

"Tupo hapa kutekeleza wajibu tuliopewa na Serikali ambayo ni nyie wananchi lakini sote tunafahamu kuwa Serikali mwaka jana ilitoa maelekezo ya madereva wote kwenda kusoma pamoja na kuhakiki leseni zenu,wapo baadhi yenu wametekeleza maagizo ya Serikali" Alisema.

Hata hivyo alisisitiza umuhimu wao kuhakikisha wanalitekeleza suala la kusoma huku akiwataka wasifanye jambo kwa shuruti kwa sababu elimu wanayoenda kuipata kwa ajili ya manufaa yao hivyo hawana haja yakulazimishana.

Aidha aliwaonya Madereva wa Daladala kuacha tabia ya kusimamisha Daladala zao kwa muda mrefu kwenye maeneo yasiyokuwa na vituo katikati ya Jiji hili lenye mpangilio mzuri wa namba za Barabara za mitaa.

"Kwa Bahati mbaya wakati wanapangilia Jiji hili walisahau kuweka vituo vingi vya Daladala, hivyo sisi tumeona ni busara tu kwa baadhi ya maeneo kwenye Barabara za namba Daladala inaweza ikasimama kwa muda mfupi sana ili kuepusha msongamano unaoweza kujitokeza,unatakiwa utumie muda mfupi sana kupakia au kushusha abiria wako kwenye vituo tulivyoviruhusu" Alisisitiza SP.Mwamasika
NA WILLIUM PAUL.

JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ikiongizwa na Mwenyekiti wake Mohammed Ali Kawaida (MCC) wamekabidhi msaada wa Chakula kwa wananchi wa Rufiji walioathirika na mafuriko katika maeneo hayo.

Kawaida ameelekeza Viongozi wa Rufiji kuhakikisha misaada yote inayotolewa inawafikia wananchi hao waliothirika na Mafuriko

"Niwasihi sana viongozi hakikisheni misaada hii inawafikia walengwa ambao ni wananchi wenzetu walioathirika na mafuriko na tuendelee kuwa faraja kwa ndugu zetu" Alisema Kawaida
Aidha Kawaida amewahakikishia wananchi wa Rufiji kuwa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi itaendelea kuwa karibu nao katika kipindi hiki kigumu wanachopitia kwani ni Utamaduni wa UVCCM kuwakimbilia Wananchi pale wanapopatwa na Matatizo.

"Ndugu zangu sisi Jumuiya ya Vijana tuna utamaduni wetu wa kuishi kama ndugu wamoja ndio maana kauli Mbiu yetu ni "Kulinda na Kujenga Ujamaa", Hivyo niwahakikishie kuwa tutaendelea kuwa karibu na ninyi katika kipindi hiki kigumu"

Kawaida amewasihi Watanzania na Wadau mbalimbali wawakimbilie Wananchi wa Rufiji kuwasaidia wananchi wa Rufiji na sio kufanya Siasa.




Katika kufungua fursa za kuongeza umahiri katika fani zao, Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative (SUGECO) imesaini mkataba wa miaka mitatu kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

Akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa taasisi yake imekuwa ikitekeleza Program ya Imbeju inayotoa mafunzo ya ujasiriamali pamoja na mtaji wezeshi kwa vijana na wanawake.
Tangu walipofungua dirisha la maombi mwaka mmoja uliopita, vijana 709 walijitokeza na kati yao, asilimia 40 kati yao walitoka katika sekta ya kilimo ambayo inaongoza kwa kuliingizia taifa fedha za kigeni huku ikilihakikishia taifa chakula cha kutosha kwa mwaka mzima.

Kwa kushirikiana na wabia, Tully amesema kilimo kinapewa msisitizo zaidi kwa kutambua mchango wake katika kuliingizia taifa fedha za kigeni, kutoa ajira kwa Watanzania pamoja na kuihakikishia Tanzania usalama wa chakula.
“SUGECO ni mbia wetu mpya katika uwezeshaji wa vijana hasa wanaojihusisha na kilimo. Kwa kutambua umuhimu wa mafunzo kwa vitendo katikakuwajengea uwezo vijana, CRDB Bank Foundation imetenga Euro milioni 24 sawa na Shilingi bilioni 67 kwa ajili ya programu hii zitakazotolewa ndani ya miaka mitatu ya ushirikiano wetu na SUGECO ili kuwaandaa vijana mahiri watakaoajiria au kujiajiri kwenye sekta ya kilimo,” amesema Tully.

Tangu kuanzishwa kwake, SUGECO huwapeleka nje ya nchi wahitimu wa SUA hasa katika mataifa ya Ulaya, Amerika na Asia ambako hujifunza namna nzuri ya kufanya kilimo chenye tija lakini mchakato huo huhitaji fedha za awali kumwezesha mhitimu husika kujiandaa ipasavyo.

Kwa mwaka huu wa kwanza, Tully amesema wanatarajia kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 kwa kati ya dola 3,500 za Marekani (shilingi milioni 8.7) mpaka dola 4,500 (shilingi milioni 11.29) zinazotosha kwa mahitaji yao yanayojumuisha gharama za pasi ya kusafiria, visa pamoja na fedha ya kujikimu kabla ya kuanza kulipwa huko waendako.

“Mpango wa uwezeshaji baada ya mafunzo pia umeshaandaliwa kwa kushirikiana na SUGECO pamoja na USAID kwa kutenga maeneo maalum ya kuwekeza katika kilimo cha kisasa, na chenye tija zaidi. Taasisi yetu imejipanga kikamilifu pia katika hatua hiyo ya pili ya uwezeshaji kwa kutoa mitaji wezeshi, pamoja kuwapa mafunzo ya ujasirimali,” amesisitiza Tully.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO, Ndugu Revocatus Kimario amesema ushirikiano na Taasisi ya CRDB Bank Foundation utaongeza idadi ya wanufaika kwa kiasi kikubwa kwani mwaka jana waliweza kuwapeleka vijana 500 tu kupata mafunzo hayo kwa vitendo nje ya nchi ili kupata elimu na kujengewa uwezo zaidi katika kilimo, fani ambazo wamezisomea.

“Ushirikiano huu, tunaamini utakuwa na tija kubwa kwani ili ufanye biashara endelevu ni muhimu kuwekeza kwa watu unaowahudumia. Mkataba huu ni kati ya uwekezaji mkubwa kwa Benki ya CRDB kwani si wahitimu peke yao watakaonufaika bali wafanyakazi wao, familia hata ndugu, jamaa na marafiki zao,” amesema Kimario.
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi ya SUGECO naye, Dkt Anna Temu alikumbusha namna walivyouanzisha ushirika huo ambao mpaka sasa umewaneemesha maelfu ya wahitimu wa SUA kwa kuwaongezea maarifa juu elimu waliyoipata darasani.

“Kwa kuwa sisi tunawahudumia zaidi vijana na wanawake, tuliona CRDB Bank Foundation wenye Program ya Imbeju ni wabia muhimu wa kufikisha malengo yetu kwa jamii,” amesema Dkt Anna.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akiwa kwenye futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhamani akizungumza katika halfa hiyo
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akitunzwa baada ya kusoma Quarn Tukufu katika halfa hiyo.
Na Oscar Assenga, PANGANI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu mkoa huo umepokea fedha kiasi cha Sh.Trilioni 2.6 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Balozi Batilda aliyasema hayo wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyokwenda sambamba na Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji Jumaa Aweso iliyofanyika wilayani Pangani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali,Chama na Taasisi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa maji Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji,Mkurugenzi wa Ruwasa na wataalamu mwengine.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo likiwemo Daraja la Mto Pangani na Barabara ya Pangani pamoja na mengine ikiwemo ya elimu ambapo wanamshukuru Rais kwa ujenzi wa mabweni ya watoto wenye mahitaji maalumu yamejengwa, zahanati, nyumba za walimu na miradi ipo mingi kazi kubwa imefanywa.

“Katika hili tunamshukuru sana Mh Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutuletea fedha hizi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini namshukuru kwa imani kubwa kwangu ninahaidi sitamuangusha nitajitahidi kwa ushirikiano wenu na dua zengu niweze kutimiza yale ambayo anakusudia nitimize nikiwa hapa Tanga” Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwamba wataendelea kuhakkikisha fedha zinazokuja zinatekeleza kazi iliyokusudiwa na sio vyenginevyo pamoja na usimamizi mzuri katika miradi inayotekeleza ili iweze kuleta tija inayotakiwa.

“Nimshukuru Waziri Aweso amefanya jambo kubwa na ameendelea kufanya mambo mengi kwenye Sekta ya Maji nimetoka Tabora kwenye miradi 28 nasi tulikuwa tunanufaika nimekuja hapa Tanga nimeambiwa napo ipo ni kijana mdogo lakini mwenye hekima, hofu ya mungu, mchapakazi “Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwa hakika dhamana aliyopewa na Rais Dkt Samia Suluhu kuhakikisha anawatua wakina mama ndoo kichwani ameitekeleza vizuri kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara maji wanaendelea na kazi nzuri.

Akizungumzia suala la mabadiliko ya tabia ya nchi hasa kwenye wilaya ya Pangani RC Balozi Batilda alisema wilaya hiyo ni moja ya maeneo yaliyoathirika na kuna maeneo yakichimbwa visima kuna maji ya chumvi ndio maana kwenye mradi wa maji ya miji 28 na wao wamepelekewa na maeneo watachimba visima ili wananchi waweze kunufaika kwa kupata maji safi na salama.

Akizungumzia suala la uvuvi RC huyo alisema suala hilo katika mkoa huo ni moja ya maeneo ya uvuvi hivyo suala la maboti na vifaa vya uvuvi vitaendelea kupatikana kwenye mji wa Pangani na maeneo mengine.

“Tunapozungumzia masuala ya mazingira niwape kongole Pangani mazingira mmeendelea kuyatuza na msitu wenu wa asili unapendeleza”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema katika moja ya kuendeleza ukwekezaji Serikali kupitia Wizara Madini ilisaini mkataba na wawekezaji wa madini ya Ndovu au tembo ambayo yatachimbwa kwenye Mwambao wa Pangani karibu kilomita 15 ya ufukwe.

Alisema walichowaambia wahakikisha hawawanyi ruhusu ya wavuvi kutumia mwambao huo na matumbawe hayatavurugwa ikiwemo mikoko iliyopo wakati wanaendelea kunufaika na mradi huo na kuendelea na uvuvi,matango pori yote kuhakikisha wanakuwa na shughuli mbalimbali zinaendelea.

Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa wa Tanga ndio ambao kila kitu kinaweza kuota hivyo lazima wahakikishe utajiri huo unawanufaisha wananchi wao wote kwa kuhakikisha wanachangamkia fursa zilizopo.

“Katika ujenzi wa bomba la mafuta litapita kwenye wilaya kadhaa tunataka wana tanga wanufaike na miradi hiyo na kazi yake katiba tawala na wakuu wa wilaya na makatibu tawala ni kuwawezesha wananchu kuona fursa za uwepo wa mradi huo ili waweze kuchangamkia fursa hizo”Alisema RC Balozi Batilda ,

Awali akizungumza katika futari hiyo Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew alisema kwamba maadili mema ambayo tumeyaonyesha katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani tuendelee kuifanya na kufanya ibada ndio tunaweza kuwaponya wengi na kujiponya na sisi.

Mhandisi Mathew alisema pia waendelee kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu ili aendelea kuifanya kazi nzuri anaoendelea kuifanya na kuhakikisha wanashirikiana na Mbunge wao na kamwe wasimwangushe .

“Nataka kuwaambie wana Pangani “Dhahabu ya Pangani tunaijua wana Pangani na Dhahabu ya Tanzania tunaijua na tusije kudanganyika na kuachia dharabu hii na kwenda kuokota mawe”Alisema

Hata hivyo alimshukuru Waziri Aweso kwa jambo kubwa alilolifanya kwa wananchi wake kutokana na uwepo wa umoja na mshikamano kwa wananchi wake ambao wameitika kwa wingi kwenye tukio hilo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema safari ya kuifungua pangani kimaendeleo itafanywa na wana Pangani wenyewe na mimi ni miongoni mwa watu walishawishika na Waziri Aweso kipindi kile kwa maneno yake kwa dhamira iliyojificha ndani ya moyo wake akanitamkia ya kutaka kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo.

Alisema kwa sasa tunayaona maendeleo makubwa sana kwenye Jimbo la Pangani ikiwemo ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani –Saadani ambayo itaifungua wilaya hiyo pamoja na uwepo wa miradi ya maji ambayo awali wananchi walikuwa wakiifuata umbali mrefu.