Articles by "HABARI PICHA"
Showing posts with label HABARI PICHA. Show all posts
Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO),imetoa mwito kwa wananchi wote kuendelea kuwa mabalozi wa haki, upendo na mshikamano kwa watu wenye ualbino na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu.

Aidha limewataka ndugu wote wenye ualbino nchini Tanzania na duniani kote, wasikate tamaa na kuwakumbusha waendelee kuamini katika uwezo wao,kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutimiza ndoto zao na kwamba Dunia inahitaji mchango, vipaji na uwezo wenu.

Hayo yamesemwa na Boniventura Mwalongo ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)

na Mjumbe wa Kamati Maalumu ya Pamoja ya Kushughulikia Changamoto za Watu Wenye Ualbino nchini alipokuwa akitoa salamu katika Maadhimisho ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika Juni 13,2026.

“TRAMEPRO inapenda kuwahakikishia watu wote wenye ualbino kwamba itaendelea kuwa sauti yao na mshirika wao katika kutetea haki, usawa, heshima na maendeleo yao. Ahadi yetu ni kwamba kamwe hatutawasaliti katika kusimamia haki zenu na haki za binadamu kwa ujumla. 

“Tutaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha kuwa watu wenye ualbino wanapata ulinzi, heshima, fursa na haki zote wanazostahili kama raia wengine,”amesema na kuongeza "Utu, usawa, upendo na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye amani kwa wote."

Akieleza zaidi kuhusu maadhimisho hayo amesema TRAMEPRO inaamini siku hiyo ni fursa muhimu ya kuendelea kuelimisha jamii kuhusu haki, usawa, usalama, afya na ustawi wa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga ubaguzi, unyanyapaa na vitendo vyote vya ukatili vinavyokiuka haki zao za msingi. 

Pia maadhimisho hayo yanakumbusha wajibu wa pamoja wa kujenga jamii inayoheshimu utu, usawa na haki za kila mwanadamu bila kujali tofauti zake za kimaumbile.

“TRAMEPRO inatoa pongezi kwa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Albinism Sports Club, Serikali, Bunge, wataalamu wa tiba asili, wadau wa afya, elimu, michezo na mazingira pamoja na wanachama wote wa TRAMEPRO kwa mchango wao katika kuimarisha ustawi, usalama na maendeleo ya watu wenye ualbino nchini.”

Wakati huo huo Mwalongo ametumia maadhimisho hayo kueleza wanatambua na kupongeza mechi ya kirafiki iliyochezwa Juni 6,2026 kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club, ambayo imeendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya michezo katika kuhamasisha ushirikishwaji, mshikamano, uelewa na mapambano dhidi ya ubaguzi kwa watu wenye ualbino. 

Tukio hilo limeonesha michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Bunge Sports Club, Waheshimiwa Wabunge na wadau wote walioshiriki kufanikisha tukio hilo muhimu. 

Aidha, wanaguswa na moyo wa upendo, utu na kujali uliooneshwa na Salma Kikwete, ambaye baada ya kuguswa na hali halisi ya baadhi ya wachezaji wa Albinism Sports Club alionesha moyo wa kuwafariji na kuwasaidia. Kitendo hicho ni mfano wa kuigwa katika kujenga jamii yenye huruma, mshikamano na usawa.

“Pia tunatoa shukrani kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)kwa kuwezesha upatikanaji wa miche iliyotumika katika zoezi hilo. Mchango huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia na wananchi katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”

 

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Shahada ya Uzamivu ya Heshima (Honoris Causa) aliyotunukiwa na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) nchini Urusi, maarufu kama Patrice Lumumba University ni heshima kubwa kwake binafsi na kwa taifa la Tanzania kwa ujumla.

Akihutubia baada ya kutunukiwa shahada hiyo Rais Samia amesema katika dunia ya sasa inayobadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, ni muhimu kwa nchi kuwekeza katika wataalamu waliobobea ambao wanaelewa kuwa ujuzi wao ni chachu ya maendeleo endelevu ya taifa.

Ameongeza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya elimu, utafiti na teknolojia ili kuhakikisha vijana wanapata maarifa yatakayowezesha kushindana katika soko la ajira la kimataifa na kuchangia maendeleo ya kiuchumi.

Rais Samia ametunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima na Chuo Kikuu cha RUDN, kwa kutambua mchango wake katika uongozi bora, diplomasia na maendeleo ya jamii.

Shahada hiyo imetolewa wakati wa ziara ya kitaifa ya Rais Samia nchini Urusi, ambapo amekuwa akifanya mazungumzo ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Urusi.

Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari watakaoshiriki Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo (Samia Kalamu Awards - SKA) 2026 wamelazimika kukidhi sharti la kuwa na ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), hatua inayolenga kuimarisha weledi, uwajibikaji na ushindani wa haki katika taaluma hiyo.

Akizindua rasmi mchakato wa kupokea kazi za kushindanishwa, Jumapili Tarehe 31 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SKA, Mha. Peter Mwasalyanda, amesema maandalizi ya mwaka huu yanazingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kutambua mchango wa Waandishi wa Habari za maendeleo nchini.
Mwasalyanda amesema ili kuhakikisha uadilifu, uwazi na ushindani wa haki, maandalizi ya tuzo hizo yanahusisha pia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kama mdau muhimu katika kusimamia weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

“Tuzo hizi zinalenga kutambua, kuthamini na kuhamasisha uzalishaji wa maudhui ya ndani yenye ubora, yanayochangia kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, na kuimarisha taswira chanya ya Taifa kupitia habari za maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema tofauti na msimu wa kwanza wa tuzo hizo, mwaka huu washiriki wanapaswa kuhakikisha wamekidhi sharti la ithibati.

“Mtakumbuka Msimu wa kwanza wa Samia Kalamu mambo ya JAB hayakuwepo, kwa hiyo waandishi walishiriki wote bila kujali vigezo vya Ithibati lakini mwaka huu kuna hiki kigezo cha kuwa na ithibati kwa hiyo niwashauri basi wote wanaoshiriki kwenye hizi tuzo wahakikishe wanakuwa na ithibati, wamethibitishwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.” Amesema Wakili Kipangula na kuongeza;
“Ni muhimu sana kwa sababu ni takwa la kisheria na kitu ambacho hatuwezi kukikwepa. Nawahamasisha tushiriki wote kwa sababu isionekane ni tuzo za watu fulani tu, kila mmoja awasilishe kazi zake,” amesema Kipangula.

Kwa mujibu wa vigezo vya ushiriki vilivyotangazwa, Waandishi wa Habari wa Tanzania Bara wanatakiwa kuwa wamethibitishwa na JAB, huku kwa Zanzibar washiriki wakitakiwa kuwa na kitambulisho cha Mwandishi wa Habari (Press Card).

Tuzo hizo zimeanza kupokea kazi kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2026 na zinatarajiwa kutolewa kati ya Oktoba na Desemba mwaka huu.


Tanzania inaanza rasmi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 tarehe 1 Julai 2026 ikiwa na msingi imara wa kisera, kitaasisi na kiutekelezaji unaolenga kuharakisha mageuzi ya kiuchumi, kijamii na kiutawala kwa miongo ijayo.

Katika kikao chake kilichofanyika Dar es Salaam tarehe 26 Mei 2026 chini ya Mwenyekiti wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tume ya Taifa ya Mipango iliidhinisha miongozo na mifumo muhimu ya kusimamia utekelezaji wa Dira 2050 pamoja na kuelekeza kuharakishwa kwa miradi mikubwa ya kimkakati itakayokuwa nguzo kuu ya ukuaji wa uchumi wa Taifa.


Pamoja na kuidhinisha Mwongozo wa Kitaifa wa Mipango, Mwongozo wa Kitaifa wa Uidhinishaji wa Miradi ya Maendeleo, Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi ya Maendeleo na Mkakati wa Mawasiliano wa Dira 2050, Tume imeweka msisitizo maalum katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya uwekezaji inayotarajiwa kuchochea mabadiliko ya kimuundo katika uchumi wa Tanzania.

Miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Kuchakata Gesi Asilia kuwa Kimiminika (LNG), Mradi Unganishi wa Chuma cha Liganga na Makaa ya Mawe ya Mchuchuma, Mradi wa Kabanga Nickel pamoja na Kiwanda cha Usafishaji Kahama, na Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka.

Kwa pamoja, miradi hii inawakilisha uwekezaji wenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 120, sawa na takribani dola za Marekani bilioni 47.

Miradi hii imeainishwa kama sehemu muhimu ya utekelezaji wa Dira 2050 kwa sababu ina uwezo wa kuvutia uwekezaji mkubwa wa ndani na nje, kuongeza ajira, kuimarisha mapato ya Serikali, kukuza mauzo ya nje, kuongeza matumizi ya teknolojia za kisasa na kuimarisha ushindani wa Tanzania katika uchumi wa kikanda na kimataifa.

Mradi wa LNG unatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa sekta ya nishati na mapato ya fedha za kigeni.

Liganga na Mchuchuma vinatarajiwa kuweka msingi wa maendeleo ya viwanda kwa kuongeza uzalishaji wa chuma na nishati nchini. Kabanga Nickel inaipa Tanzania nafasi ya kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kijani unaochochewa na ongezeko la mahitaji ya madini muhimu kwa utengenezaji wa betri na teknolojia za nishati safi duniani.

Nayo Engaruka inafungua fursa mpya katika sekta ya kemikali na viwanda vinavyotegemea malighafi za ndani.

Kwa kuzingatia malengo ya Dira 2050 ya kufikia uchumi wa takribani dola trilioni moja, miradi hii siyo uwekezaji wa kawaida bali ni injini za mageuzi ya kiuchumi.

Uamuzi wa Tume ya Taifa ya Mipango wa kuipa kipaumbele utekelezaji wake unaashiria dhamira ya Serikali ya kuhakikisha Dira 2050 inatafsiriwa katika matokeo halisi yatakayoongeza tija, ajira, ustawi wa wananchi na ushindani wa Taifa katika miaka ijayo.













Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Rabia Hussein Mohamed kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Immaculata Kajetan Banzi kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Cyprian Phocas Mkeha kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Yohane Bokobora Masara kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Juliana Laurent Masabo kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Abdi Shaaban Kagomba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Majaji 9 wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha na Majaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri (kulia), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.