Articles by "HABARI PICHA"
Showing posts with label HABARI PICHA. Show all posts

 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akizungumza katika mkutano wa hadhara eneo la Kimani Mtaa wa Kinyamwezi, Kata ya Pugu, Ilala Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya utatuzi wa mgogoro wa ardhi Februari 13, 2026.
Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya, akizungumza wakati wa utatuzi wa mgogoro huo.
 Viongozi wakipitia ramani eneo lenye 
Ukaguzi wa eneo lenye mgogoro ukiendelea
Ukaguzi wa eneo hilo ukiendelea
Bicon zikiangaliwa eneo la tukio.
Wananchi wakiwa kwenye eneo hilo.
Msafara ukielekea kukagua eneo lenye mgogoro
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo (kushoto), akioneshwa mipaka ya eneo hilo.
Wananchi wakiwa eneo la lenye mgogoro.
Wakina mama wakiwa eneo la mgogoro.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, ameleta nafuu kwa wakazi wa Pugu baada ya Serikali kuingilia kati mgogoro wa muda mrefu wa ardhi inayodaiwa kuvamiwa licha ya kutengwa kwa matumizi ya makaburi.

Mgogoro huo unahusu eneo la Kimani, Mtaa wa Kinyamwezi, Kata ya Pugu jijini Dar es Salaam, ambapo wakazi walimtuhumu Elizabeth Mwakapangala kwa madai ya kuuza eneo hilo na kufukua makaburi kinyume cha sheria.

 Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Februari 13, 2026, Mpogolo alisema ramani ya upimaji inaonesha wazi kuwa eneo hilo lilitengwa rasmi kwa ajili ya maziko kwa mujibu wa mipango miji ya Serikali.
Mpogolo alieleza kuwa kesi ya ardhi namba 202/2020 iliyofunguliwa na Mwakapangala, aliyekuwa msimamizi wa mirathi, ilihusisha Halmashauri ya Jiji, Tanzania Airports Authority na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akisoma hukumu ya Mahakama iliyotolewa na A. M. Msafiri, alisema mlalamikaji alistahili kulipwa fidia lakini hakuwa na haki ya kuuza ardhi ya makaburi wala kuhamisha mabaki ya miili bila kufuata sheria.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya, aliwataka wananchi kuwa watulivu huku Serikali ikiendelea kufuatilia suala hilo kwa mujibu wa sheria. 

Wananchi walidai eneo hilo lilitengwa kwa maziko ya wakazi waliohamishwa kutoka Kipawa kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Hata hivyo, Mwakapangala amekanusha tuhuma hizo akidai hajawahi kufukua makaburi na kusisitiza kuwa eneo hilo ni mali yake halali, akisema anazo nyaraka zote baada ya kushinda kesi mahakamani mwaka 2022. 

Serikali imesema itaendelea kushughulikia suala hilo kwa mujibu wa sheria ili kulinda maslahi ya umma na kuhakikisha haki inatendeka.
Dar es Salaam — Kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kinywaji chake cha kifahari cha Tanzanite Royal Gin imezindua rasmi kampeni maalum ya msimu wa Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day) ijulikanayo kama “Tanzanite Royal Gin – Royal Love Challenge 2026”, yenye lengo la kuimarisha uhusiano na wateja pamoja na kusherehekea mapenzi kwa njia ya kipekee.

Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Izack Piganio, Meneja wa Chapa Mati Super Brands, alisema, "Royal Love Challenge ni njia yetu ya kuwapa wateja uzoefu wa kipekee wa kusherehekea Valentine’s Day, huku tukijenga uhusiano wa karibu na wapenzi na wanandoa kupitia chapa ya Tanzanite Royal Gin. Tunataka mapenzi yashehereke kwa hadhi ya kifalme, na washiriki washindwe kwa ubunifu na upendo wao."
Shindano hili la mtandaoni litafanyika kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram, likiwalenga wapenzi, couples na wanandoa. Washiriki wanatakiwa kupiga picha wakionyesha upendo wao pamoja na chupa halisi ya Tanzanite Royal Gin, kisha kuipakia kwenye akaunti zao za Instagram. Ili kushiriki kikamilifu, washiriki wanapaswa kutag ukurasa rasmi wa @TanzaniteRoyalGin, kutumia hashtag #RoyalLoveChallenge, na kufanya collaboration na ukurasa wa kampeni.

Kwa upande wake, Meneja wa hoteli ya Asmorain, Amina Mrutu, alisema: "Tunakufariji kuwa sehemu ya kampeni hii ya Royal Love Challenge. Tunatarajia mshindi atapata zawadi za kipekee zenye mchanganyiko wa mapenzi na burudani, ikiwemo usiku mmoja katika hoteli yetu, chakula cha jioni cha kimapenzi na safari ya kupumzika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire."

Mshindi wa Royal Love Challenge 2026 atatangazwa Februari 12, 2026, huku zawadi zote zikitolewa rasmi Februari 14, siku ya Valentine’s Day. Kampeni hii inatarajiwa kuleta burudani, ushindani chanya, na kuendeleza utamaduni wa kusherehekea mapenzi kwa hadhi ya kifalme.
Na Mwandishi Wetu, Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amekabidhi pikipiki ya umeme ya magurudumu matatu iliyotolewa na Mati Foundation kwa binti mwenye ulemavu, Bertina Francis, aliyepoteza wazazi wake wote wawili kufuatia maporomoko ya tope yaliyotokea Wilaya ya Hanang’ mwezi Desemba 2023.

Bertina Francis, ambaye kwa sasa anaishi katika moja ya nyumba zilizojengwa na Serikali kwa ajili ya waathirika wa maporomoko hayo katika eneo la Waret wilayani Hanang’, ameelezwa kuwa anajishughulisha na biashara ndogo ya uuzaji wa vitafunwa. Kupatikana kwa pikipiki hiyo ya umeme kunatarajiwa kumrahisishia shughuli zake za kiuchumi hususan katika usambazaji wa bidhaa zake na hivyo kuongeza kipato na kujitegemea.
Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mhe. Sendiga amesema msaada huo ni matokeo ya ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali na sekta binafsi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo una mchango mkubwa katika kugusa maisha ya wananchi wenye uhitaji. Amempongeza mwekezaji David Mulokozi kupitia taasisi yake ya Mati Foundation kwa moyo wa kujitolea na kusaidia makundi maalum katika jamii.

“Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji na taasisi binafsi kushiriki katika maendeleo ya jamii. Msaada huu ni mfano mzuri wa namna sekta binafsi inavyoweza kushirikiana na Serikali kuwainua wananchi walioko katika mazingira magumu,” amesema RC Sendiga.
Kwa upande wake, Bertina Francis ameishukuru Serikali pamoja na Mati Foundation kwa msaada huo, akieleza kuwa pikipiki hiyo itamfungulia fursa zaidi za kiuchumi na kumpa matumaini mapya ya maisha. Ameiomba taasisi hiyo kuendelea kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao wajisikie kuwa sehemu ya jamii na kuchangia katika maendeleo yao binafsi na ya Taifa.

Pikipiki hiyo ya umeme ni sehemu ya mpango unaoendelea wa kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia taasisi yake ya Mati Foundation wa kugawa pikipiki za magurudumu matatu kwa watu wenye ulemavu zaidi ya 2,000 kote nchini. Mpango huo ulianza rasmi mwezi Septemba 2025 ukiwa na lengo la kuwawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni mchango muhimu katika juhudi za Serikali za kuhakikisha makundi maalum yanapata fursa sawa za maendeleo na kujitegemea kiuchumi, hususan kwa waathirika wa majanga mbalimbali nchini.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Edward Mpogolo, amewataka wakazi wa wilaya hiyo kuonyesha uzalendo wa kweli kwa kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira, hususan kupitia zoezi la upandaji wa miti katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa Januari 27, 2026, wakati wa maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, yaliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Jangwani jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wanafunzi, walimu na wananchi waliojitokeza kushiriki tukio hilo, Mheshimiwa Mpogolo amesema uzalendo wa dhati hauishii kwenye maneno bali unaonekana kupitia vitendo vinavyolinda rasilimali za taifa, huku akisisitiza kuwa mazingira ni msingi wa maisha na maendeleo endelevu.
“Rais Samia amekuwa kinara wa kampeni ya nchi ya kijani. Ni wajibu wetu sisi wananchi kuenzi maono haya kwa vitendo ili kulinda mustakabali wa kizazi cha sasa na kijacho,” amesema Mpogolo.

Katika kuimarisha utekelezaji wa wito huo, Mkuu wa Wilaya amewataka wakazi wa Ilala kuhakikisha kila kaya inapanda angalau miti mitatu, akisisitiza kuwa zoezi hilo linapaswa kuambatana na uangalizi na utunzaji wa miti hiyo ili iweze kukua na kutoa manufaa yaliyokusudiwa.

Aidha, amewaagiza wakuu wa shule na viongozi wa taasisi mbalimbali kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wa karibu wa miti inayopandwa katika maeneo yao badala ya kuishia kwenye kampeni za siku moja bila ufuatiliaji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Ndugu Elihuruma Mabelya, amesema halmashauri imejipanga kutekeleza kikamilifu kaulimbiu inayosema “Uzalendo ni Kutunza Mazingira” kwa kupanda zaidi ya miti milioni moja katika maeneo mbalimbali ya jiji.

Mabelya ameongeza kuwa pamoja na upandaji miti, halmashauri inaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama mkakati wa kupunguza uharibifu wa misitu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Maadhimisho hayo yamefanyika ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Ofisi ya Ikulu lililoelekeza jamii kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Rais Samia kwa kushiriki katika shughuli za kijamii zenye mchango wa moja kwa moja katika utunzaji wa mazingira, ikiwa ni ishara ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kukabiliana na changamoto za tabianchi.
Na Mwandishi Wetu, Morogoro.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kuongeza rasilimali watu, bajeti, miundombinu na kufanya maboresho ya kisheria, hatua iliyoongeza ufanisi wa mapambano dhidi ya rushwa nchini.

Dkt. Nchemba alisema kuwa kutokana na jitihada hizo, TAKUKURU imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi bilioni 60.2, fedha ambazo zimeelekezwa kwenye huduma muhimu za jamii zikiwemo afya, elimu, maji, umeme na miundombinu.

Akizungumza leo Jumatatu, Januari 26, 2026 jijini Morogoro, wakati akimwakilisha Rais katika Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa TAKUKURU unaofanyika katika ukumbi wa Cate Convention Centre, Waziri Mkuu alisema kuwa katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2025, Jamhuri ilishinda asilimia 68.8 ya kesi 489 zilizofikishwa mahakamani, hali inayoonyesha kuimarika kwa ubora wa uchunguzi na ushirikiano kati ya TAKUKURU na Mahakama.

“Rushwa inadhalilisha utu wa binadamu na inazorotesha utoaji wa huduma za jamii. Ni lazima tuchukue hatua za kuizuia kabla haijaleta madhara makubwa. Rushwa ni ajenda ya kitaifa,” alisisitiza Dkt. Nchemba.

Waziri Mkuu aliagiza taasisi zote za Serikali kubaini na kuziba mianya ya rushwa, hususan katika maeneo ya manunuzi ya umma, utekelezaji wa miradi na usimamizi wa mikataba, akibainisha kuwa zaidi ya asilimia 75 ya bajeti ya Serikali hupitia kwenye maeneo hayo, hivyo yanahitaji uangalizi wa karibu.

Aidha, aliwahimiza wananchi kushirikiana na TAKUKURU kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa, akiahidi kuwa Serikali itaendelea kulinda usiri na usalama wa watoa taarifa. Pia alisisitiza umuhimu wa kushirikisha sekta binafsi, wadau wa maendeleo, vijana na wanawake katika mapambano hayo.

Dkt. Nchemba aliongeza kuwa Serikali iko tayari kufanya marekebisho ya kisheria na kiutawala pale itakapobainika kuna vikwazo vinavyoathiri utendaji wa TAKUKURU, na kuwataka viongozi wa taasisi hiyo kutoa mapendekezo yao kwa uwazi. Pia alielekeza kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya TAKUKURU na Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma kwa lengo la kujenga misingi imara ya uadilifu na uwajibikaji.

Akihusisha mapambano dhidi ya rushwa na maendeleo ya Taifa, Waziri Mkuu alisema jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025–2030, ambazo zimeweka wazi kuwa utawala bora na kupambana na rushwa ni nguzo muhimu za ustawi wa wananchi.

Akihitimisha hotuba yake, Dkt. Nchemba aliwataka viongozi wa TAKUKURU kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanakuwa chachu ya kuongeza juhudi zaidi, huku akirejea kaulimbiu ya mkutano:

“Kuzuia Rushwa ni Jukumu Lako na Langu; Tutimize Wajibu Wetu.”

Baada ya hotuba hiyo, Waziri Mkuu alitangaza rasmi kufunguliwa kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka 2025 wa Viongozi wa TAKUKURU.

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.(Picha na INEC).
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza leo tarehe 26 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.

Meza Kuu ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele ikiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufungaji mafunzo yao ya siku tatu.
Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufungaji mafunzo yao ya siku tatu.
Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufungaji mafunzo yao ya siku tatu.

Sehemu ya wajumbe wa Menejiment ya INEC ikiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo.

Na. Mwandishi Wetu, Iringa.

Watendaji wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na udiwani katika Kata ya Shiwinga unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.

Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk Mkoani Iringa leo tarehe 26 Januari, 2026 wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uchaguzi yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 24 Januari, 2026.

“Ni matazamio ya Tume kwamba, baada ya kupatiwa mafunzo haya, mtatekeleza majukumu yenu kwa ufanisi na weledi mkizingatia ratiba ya utekelezaji ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na Udiwani katika Kata ya Shiwinga unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026,” amesema Jaji Mbarouk.

Amesisitiza kuwa ili ufanisi uwepo ni muhimu watendaji hao wazingatie sifa na uwezo wakati wa kuteua na kuajiri watendaji wa vituo vya kupigia kura kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni.

“Kuhusu ajira za kupata watendaji wa vituo, tunayo imani kuwa mtateua na kuajiri watendaji wenye sifa na uwezo wa kufanya kazi hii muhimu……kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni. Kazi ambayo inahitaji umahiri, umakini na weledi katika kuitekeleza,” amesema Jaji Mbarouk.

Amewataka watendaji hao kuhakikisha kuwa mafunzo ya watendaji wa vituo yanafanyika kwa ufanisi na weledi katika tarehe zilizopangwa kwenye ratiba ya utekelezaji wa shughuli za uchaguzi.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo ili waweze kufahamu majukumu yao na kuyatekeleza ipasavyo wakati wa uchaguzi.

Jaji Mbarouk amewakumbusha watendaji hao kuwa shughuli zote za uchaguzi zinaongozwa na Katiba, sheria, kanuni, maadili ya uchaguzi na maelekezo ya Tume na kuongeza kuwa kuna umuhimu wa kutenga sehemu ya muda wao kusoma Katiba, sheria na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ili yawaongoze katika kusimamia uchaguzi utakaokuwa huru na wa haki.

Mafunzo hayo yamewahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa ya Songwe na Ruvuma, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu.

Mada kadhaa ziliwasilishwa ikiwa ni pamoja na Majukumu ya Watendaji wa Uchaguzi, Mambo Muhimu ya Kuzingatia, Uteuzi wa Wagombea, Maadili na Kampeni za Uchaguzi, Wajibu na Majukumu ya Watendaji wa Vituo na Utambulisho wa Mawakala wa Vyama vya Siasa, Taratibu za Upigaji Kura, Taratibu za Kuhesabu Kura, Kujumlisha Kura na Kutangaza Matokeo, Fomu Zinatotumika kwenye Uchaguzi, Mapokezi na Utunzaji wa Vifaa vya Uchaguzi na Usimamizi wa Fedha za Uchaguzi.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akizungumza leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akizungumza leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.


Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.
Meza Kuu ikiwa katika mafunzo hayo.
Viongozi kutoka Managementi ya Tume wakiwa katika mkutano huo.


Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mwemyekiti wa Tume.

Na Mwandishi Wetu, Iringa.

Watendaji wa uchaguzi wametakiwa kuvishirikisha kwa ukaribu vyama vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote za mchakato wa uchaguzi katika maeneo yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe.

Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.

“Wakati wote wa mchakato wa uchaguzi huu, ni vema mkavishirikisha kwa karibu vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili na wadau wengine wa uchaguzi katika maeneo yenu kuhusu masuala ya kiuchaguzi ambayo wanastahili kushirikishwa kwani jambo hilo litawarahisishia utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema Jaji Mwambegele.

Ameongeza kuwa watendaji hao wa uchaguzi wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo watakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea.

“Nachukua nafasi hii kuwaasa kuwa, pamoja na uzoefu ambao baadhi yenu mnao katika uendeshaji wa uchaguzi, mhakikishe mnazingatia maelekezo mtakayopewa na Tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea. Kwani kila uchaguzi unatofautiana na uchaguzi mwingine,” amesema.

Amewataka watendaji hao kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.

Jaji Mwambegele amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha wanaajiri watendaji wa vituo wenye sifa, weledi, wanaojitambua na kuachana na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi.

“Mhakiki vifaa vya uchaguzi mnavyopokea kutoka Tume na kuhakikisha kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya uchaguzi vinavyohitajika mapema na muweke utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kufunguliwa saa 1:00 asubuhi,” amesema.

Aidha, washiriki wa mafunzo hayo kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe walikula viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo.

Mafunzo hayo ya siku tatu yamewahusisha Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa ya Songwe na Ruvuma, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya Kata, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ununuzi na Wahasibu.
Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo akiongoza viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na Kiapo cha kutunza siri kwa washiriki wa mafunzo hayo.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo.


Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo.

Washiriki wa mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe wakila viapo vya kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Rehema Mayagilo.