Articles by "HABARI PICHA"
Showing posts with label HABARI PICHA. Show all posts
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar, Mh. Mudrick Soraga (kulia), akimsikiliza Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania, Shani Kinswaga, wakati wa kongamano la Z-Summit 2025 lililofanyika katika Chuo Kikuu cha SUZA, Zanzibar. Kongamano hilo la kila mwaka, lililofanyika kuanzia Februari 19-20, liliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ili kujadili changamoto na suluhisho za kuendeleza Zanzibar kama moja ya maeneo bora ya utalii duniani.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.

Zanzibar, Tanzania – Benki ya Exim Tanzania imeimarisha dhamira yake ya kukuza na kuendeleza sekta ya utalii Zanzibar kwa kushirikiana na wadau muhimu wa sekta hiyo, wakiwemo Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), ili kuwezesha waendeshaji wa shughuli za utalii kufanya malipo kama ada za kuingia kwenye hifadhi kwa haraka, kwa usalama na kwa urahisi.

Mkutano wa Z-Summit 2025, uliofanyika katika Chuo Kikuu cha SUZA, Tunguu, uliwakutanisha wadau wa serikali, wafanyabiashara, na wadau wa sekta ya utalii na ukarimu ili kujadili suluhisho bunifu za kuboresha nafasi ya Zanzibar kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani.  
Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim, Shani Kinswaga, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, alisisitiza safari ya benki hiyo na Z-Summit tangu kuanzishwa kwake, akieleza kuwa huu ni mwaka wa tatu mfululizo wa udhamini wao katika mkutano huo.  

“Mkutano huu ni jukwaa muhimu la kushirikiana, kubadilishana maarifa na kujadili mikakati ya kuimarisha zaidi nafasi ya Zanzibar kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani. Uungwaji mkono wa Benki ya Exim unaonesha imani yetu thabiti katika sekta ya utalii kama kiini cha ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii,” alisema Kinswaga.  

Kinswaga alielezea juhudi za benki hiyo katika kutumia teknolojia kutoa suluhisho rahisi za kifedha zinazokidhi mahitaji ya biashara za utalii. Kwa kuongezeka kwa mahitaji ya miamala ya kidigitali, Benki ya Exim imeanzisha huduma bunifu za kibenki, zikiwemo kutumia simu, kadi, na mifumo ya malipo mtandaoni, ili kuhakikisha ufanisi, usalama, na urahisi kwa wafanyabiashara na watalii.  
Akizungumzia ushirikiano wao na TANAPA, Andrew Lyimo, Mkuu wa Kitengo cha Benki ya Rejareja wa Benki ya Exim, alisema, “Katika Benki ya Exim, tunatambua kuwa ufanisi, usalama, na urahisi ni muhimu katika sekta ya utalii. Ndiyo maana tumeshirikiana na wadau kama TANAPA na NCAA kuwezesha malipo yasiyo ya fedha taslimu kwa huduma mbalimbali, ikiwemo ada za kuingia kwenye hifadhi. Akaunti ya Waendeshaji wa shughuli za Utalii inajumuisha Kadi ya Exim TANAPA, iliyoundwa mahsusi kurahisisha miamala katika maeneo yote ya hifadhi nchini Tanzania.”  

Katika kuthibitisha dhamira yake ya kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha, Benki ya Exim ilitangaza mpango wake wa kuendelea kupanua huduma zake Zanzibar. Ikiwa tayari na matawi mawili yanayofanya kazi, benki hiyo ina mpango wa kufungua matawi katika maeneo mengine ya kimkakati. Hii inaonesha azma ya Benki ya Exim ya kusogeza huduma za kibenki karibu na biashara, ikiwawezesha kupata suluhisho za kifedha zinazosaidia maendeleo ya miundombinu, ukuaji wa biashara, na ufanisi wa uendeshaji.  

Kadri mazingira ya utalii yanavyoendelea kubadilika, Benki ya Exim inasalia kuwa mshirika wa kuaminika wa kifedha kwa biashara zinazotaka kupanuka, kuboresha huduma zao, au kuwekeza katika fursa mpya. Suluhisho zake maalum za kifedha zimeundwa kusaidia kupata rasilimali zinazohitajika ili kustawi katika soko lenye ushindani.  

Kupitia ushirikiano imara, matumizi ya teknolojia za kidigitali, na upanuzi wa huduma zake, Benki ya Exim haitoi tu msaada kwa sekta ya utalii bali pia inachangia katika maendeleo ya uchumi wa Zanzibar kwa ujumla. Ushiriki wa Benki ya Exim katika mkutano wa Z-Summit 2025 ni uthibitisho wa dhamira yake isiyotetereka ya kusaidia ukuaji endelevu wa sekta ya utalii Zanzibar. 

Kwa kushirikiana na wawekezaji, wafanyabiashara, na mamlaka za serikali, benki hiyo inaunda mustakabali ambapo utalii utaendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya uchumi, kuongeza ajira, na kuifanya Zanzibar kuendelea kuwa kivutio kikubwa kwa watalii kutoka kote ulimwenguni.  

Na Oscar Assenga, TANGA

MABALOZI 23 wa Mkoa wa Tanga unaoundwa na Wasanii wa Filamu,Waandishi pamoja na watangazaji wametua Jijini Tanga kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Kupiga kura .

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari leo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga Ramadhani Omary alisema wameamua kujikusanya kwa pampoja kuja mkoani kwao kuleta hamasa kwenye dafrati la kudumu la wapiga kura.

Alisema kwamba watu wanapozungumzia mkoa wa Tanga hawawezi kuacha kuitaja Bandari,Zao la Mkonge ,Reli na Viwada na ukiangalia Bandari,Reli ndio ina hudumia viwanda na Rais Dkt Samia Suluhu ameweka fedha nyingi kwa ajili ya upanuzi kwenye Bandari ya Tanga .

Aidha alisema pia mkakati wa kuiboresha reli kuelekea mkoa wa Arusha na ambao itaifungua mkoa wa Tanga na serikali ina mkakati baada ya ubinafsishaji wale watu ambao hawakuviendelea viwanda vitarudi chini ya Serikali.

“Waliposikia Rais Dkt Samia Suluhu anatarajiwa kuja Tanga nao wakaamua kuja nyumbani kumpokea tutashiriki kwenye maandalizi na tutakuwepo Tanga muda wote mpaka Rais atakapowasili na leo tumeona tuhabarisha umma kupitia nyie wanahabari”Alisema

Awali akizungum za Chuchu Hans alisema kwamba wameungana na mabalozi wa Tanga na wao ni watu wa kujituma wana vipaji vingi ikiwemo ukarimu na wao wanawakilisha wenzao.

“Tumeona ni muda sahihi na umefika wakati wa kujiandikisha na tukaona tutumia nafasi hii kuhamasisha wananachi na sisi kuja kujiandikisha kwenye Daftari lakini pia Rais anakuja”Alisema.
Hata hivyo aliwaomba wananchi amba bado hawajajiandikisha kwenye daftari la kudumu la kupigia kura wakajiandikishe vituo vyote vipo wazi hivyo watumie haki yao ya msingi kwa ajili ya baadae kuwachagua viongozi wao.
Awali akizungumza katika mkutano huo na wanahabari Salim Awadhi “Gabo”- alisema wao wamekuja kuwakilisha wenzao kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kutumia haki yao ya msingi ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.



Alisema kwasababu mkoa wa Tanga ni watu wa ukarimu wao wameliona wabebe jukumu hilo kumsaidia Mkuu wa Mkoa huo Balozi Batilda Burian ambaye amekuwa kinara wa maendeleo kwenye mkoa huo.


Hata hivyo kwa upande wake Maliki Bandawe ambaye ni Msanii wa Bongo Fleva kutoka kundi la TNG alisema wameamua kurudia Tanga ili kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura lakini pia kutoa hamasa na kuwakumbusha vijana kujiandikisha kwenye daftari hilo.
“Wana Tanga tujitokezeni kwenye mapokezi ya Rais Dkt Samia Suluhu anakuja kwa mara ya kwanza baada ya kupitishwa na CCM kuwa Mgombea Urais kwenye uchaguzi Mwaka huu 2025”Alisema

Akielezea malengo ya ziara hiyo, Kiongozi wa Msafara Khalidi Swalehe alisema msafara huo mabalozi 23 kutoka mikoa tofauti wote ni wazawa wa mkoa wa Tanga ambao wanaitumia kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na mapokea ya kumlaki Rais Dkt Samia Suluhu.

“Naombeni wakazi wa Tanga waunge mkono na tulichokuja kukifanya ni kuhamasisha watu kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la kupiga kura na kuhakikisha tunaunga mkono jitihada za maendeleo kwa mkoa wa Tanga zinaofanywa na Mkuu wa Mkoa huo Balozi Dkt Batilda akimuwakilisha Rais Dkt Samia”Alisema
Hata hivyo alisema kwamba mkoa huo umeendelea kuamka kwa maana Tangu Tanzania ipate uhuru ilikuwa inasifika na kuna miradi mingi ya maendeleo imefanywa na Rais Dkt Samia Suluhu na wao wanahamasisha yale yanayopaswa kwenda masikioni mwa watu.
Meneja wa Barrick nchini, Dk.Melkiory Ngido akitoa taarifa ya utendaji wa Barrick na Twiga kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Dkt. Mathayo David akifuatilia taarifa katika mkutano huo Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu ya Barrick imechangia kiasi cha shilingi trilioni 3.6 katika Mapato ya Serikali nchini Tanzania kupitia kodi, mrabaha, na tozo mbalimbali kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2024.
Wajumbe wa Kamati wakifuatilia taarifa wakati wa mkutano huo.
Afisa Mawasiliano wa Barrick nchini Neema Ndossi katika kikao hicho.

Na Mwandishi Wetu.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Meneja wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakati akiwasilisha Maendeleo ya Kampuni Tanzu baina ya Barrick Gold na Serikali ya Tanzania ya Twiga Minerals.

Dkt. Ngido ameelezea kuwa, kwa mujibu wa takwimu za miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2024, Kampuni Barrick imewekeza zaidi ya dola bilioni 4.24 (Tsh trilioni 11) katika shughuli zake ndani ya nchi, huku dola bilioni 1.5 (Tsh trilioni 3.6) zikilipwa serikalini kupitia kodi, mrabaha, na tozo mbalimbali.

Amesema kuwa, Kampuni ya Barrick ilipochukua usimamizi wa shughuli zake nchini Tanzania mnano mwaka 2019, kampuni hiyo imeendelea kuwa mdau mkubwa wa uchumi kupitia uwekezaji, ajira, na miradi ya kijamii.

Kwa upande wa mchango wa kiuchumi Dkt. Ngido ameelezea kuwa kiasi cha Dola za Marekani milioni 158 (shilingi bilioni 412.4) sawa na asilimia 4 zimelipwa kama gawio la Serikali kutoka na ubia huo.

Sambamba na hilo, amesema kiasi cha Dola bilioni 2.3 (shilingi trilioni 6.04) sawa na asilimia 55 ya matumizi yote yameelekezwa kwa wasambazaji wa ndani, huku asilimia 32 ya uwekezaji huo kiasi cha dola bilioni 1.37 (shilingi 3.57) kimelipwa kama kodi, mrabaha, na tozo mbalimbali kwa serikali.

Ameongeza kuwa, kiasi cha dola 397 milioni (shilingi trilioni 1,03) sawa na asilimia 9 zimetumika kulipa mishahara ya wafanyakazi huku dola milioni 30 (shilingi bilioni 78.3) zikitumika kwenye utafiti wa madini katika maeneo hayo na kiasi cha dola milioni 15.6 sawa na shilingi bilioni 40.7 zimeelekezwa kwenye miradi ya kijamii.

Kuhusu ajira alisema Dkt. Ngido amesisitiza kuwa, Barrick imejizatiti katika kutoa ajira kwa Watanzania, ambapo asilimia 96 ya wafanyakazi wake ni raia wa Tanzania, ambapo hivi sasa, Kampuni ina wafanyakazi 6,185, kati yao 5,933 ni Watanzania, huku wageni wakibaki asilimia 4 pekee na kwamba asilimia 53 ya wafanyakazi hao wametoka kwenye jamii zinazozunguka migodi.

Ameongeza kuwa, asilimia 100 ya nafasi za juu za usimamizi zinashikiliwa na Watanzania huku uwakilishi wa wanawake wanawakilisha ukiwa ni asilimia 13 ya wafanyakazi wote na kwamba Barrick inazidi kuimarisha mchango wake kwa Tanzania, kwa kuwekeza zaidi katika sekta ya madini, kuinua wajasiriamali wa ndani, na kuboresha maisha ya jamii zinazozunguka migodi yake.

Ikumbukwe kuwa, Ripoti ya 14 ya Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) iliyochapishwa mwezi Juni 2024 ilithibitisha kuwa Kampuni ya Barrick Tanzania ilichangia asilimia 51 ya Mapato ya Serikali yote yaliyotokana na tasnia ya uziduaji, ikiwa ni mchangiaji mkubwa kama taasisi moja katika uchumi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Dkt. Mathayo David, ameipongeza Kampuni hiyo kwa juhudi hizo huku akitoa wito kwa watendaji na wafanyakazi wa Kitanzania walioajiriwa katika Kampuni hiyo kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa ili kulinda imani ya Kampuni pamoja na sifa ya taifa.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Madini, Kamishna Msaidizi Uendelezaji wa Madini na Migodi kutoka Wizara ya Madini Mhandisi Ally Samaje, amesema kuwa Serikali inajivunia kwa mafanikio makubwa ya Kampuni Tanzu baina ya Barrick na Serikali ya Twiga Minerals na kwamba mazungumzo ya kuanzisha Kampuni zingine za ubia kati ya Serikali na wawekezaji wengine yako katika hatua nzuri.
Na Oscar Assenga,Tanga

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi, Dkt Batilda Burian amewaomba viongozi wa dini katika mahubiri yao wawahimize waumini kuhakikisha wanajitokeza kujiandikisha Kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ikiwemo kuboresha taarifa zao.
Dkt Batilda aliyasema hayo Leo wakati akizungumza na viongozi wa dini na ya wa vyama vwanasiasa katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambapo pamoja na mambo mengine alisema zoezi la uboreshaji wa Daftari la kura litaanza February 13 mwaka huu mpaka 19.

Alisema ni upo umuhimu Makubwa viongozi hao kutumia majukwaa yao kuhakikisha wanawaelimisha waumini juu ya umuhimu wa kujiandikisha katika zoezi hilo muhimu ili kupata haki ya kuwachagua viongozi katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
"Ndugu zangu viongozi wa dini naombeni mtumie mahubiri yenu kuhakikisha mnawahamasisha wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga kura siku zimefika kesho tutakuwa na siku ya uandikishaji daftari "Alisema
"Hivyo kupitia Tume Huru ya uchaguzi walikuja na kufanya semina na viongozi wa vyama na mafunzo kwa wataalamu na Jumuiya ngazi za Kaya na Mawakala na kesho tunakwenda kwenye zoezi la uandikishaji wale vijana waliofika miaka 17 ambapo ikifika mwezi Octoba watafikisha miaka 18 wanapaswa kujitokeza kujiandikisha"Alisema

Mkuu huyo wa Mkoa alisema zoezi hilo litakwenda sambamba na la pili la kuboresha taarifa na kusahihisha taarifa ambalo pia lina umuhimu hivyo wananchi wahakikishe wanachangamkia fursa za uwepo wa zoezi hilo.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Uboreshaji wa Daftari utafanyika Mkoa wa Tanga kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza sambamba na Mkoa wa Pwani kuanzia Februari 13 hadi 19,2025 ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.


Akizungumza na Maafisa hao Mhe. Jaji Mwambegele aliwasisitiza kutambua umuhimu wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kitaifa na kuwahimiza pia kushirikiana na wadau wa Uchaguzi wakiwepo Vyama vya Siasa alivyovitaka vihakikishe vinateua mawakala katika kila kituo ili waweze kusaidia kuwatambua wananchi kutoka maeneo husika.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo tarehe 07 Februari, 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira, amewataka watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ngazi Kata, kuwa waadilifu wakati wote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Mhe.Rwebangira ametoa maelekezo hayo leo Februari 07, 2025, alipotembelea mafunzo kwa watendaji hao katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, unaotarajiwa kuanza Februari 13, 2025 hadi Februari 19, 2025, katika mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.


Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.




Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Jiji la Tanga , Mwanaidi Nondo, akiwa katika mafunzo hayo.




Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.










Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.





Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo Februari 07 , 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.




Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar akitembelea mafunzo ya kwa vitendo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.
Mjumbe wa Tuhe Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Asina Omari akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili ya watendaji wa Uboreshaji Mkoa wa Pwani. Mafunzo hayo yamefungwa leo Februari 03,2025 ambapo amewataka watendaji hao kutekeleza jukumu la kuhamasisha wananchi wa maeneo yao kushiriki kwenye uboreshaji kwa kushirikiana na wadau wengine wa uchaguzi.
Mjumbe wa Tuhe Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magadalena Rwebangira akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili ya watendaji wa Uboreshaji Mkoa wa Tanga. Mafunzo hayo yamefungwa leo Februari 03,2025 ambapo amewataka watendaji hao kutekeleza jukumu la kuhamasisha wananchi wa maeneo yao kushiriki kwenye uboreshaji kwa kushirikiana na wadau wengine wa uchaguzi.
Na Mwandishi wetu, Tanga na Pwani
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Mikoa ya Tanga na Pwani kuzingatia Katiba ya nchi, sheria za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na kanuni zake katika utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Asina Omari wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi na Maafisa TEHAMA Mkoani Pwani leo Februari 03,2025.

“Mnapaswa kutekeleza majukumu mliyopewa kwa kuzingatia Katiba ya nchi, sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na kanuni zilizotungwa chini ya vipengele vya sheria hiyo vinavyohusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,”alisema Mhe. Jaji Asina.

Aidha, alitoa wito kwa watendaji hao kuhakikisha kuwa wanaendelea kutumia muda wao wa ziada kusoma na kupitia maelekezo yote waliyopewa ili kuongeza uelewa zaidi kuhusu wajibu na majukumu yao katika zoezi hili la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

“Ni matarajio ya Tume kuwa, mara baada ya zoezi hili kukamilika watu watakaokuwa wamepatiwa kadi watakuwa ni wapiga kura halali wa kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani” amesema Mhe. Jaji Asina.

Akifunga mafunzo kama hayo Mkoani Tanga nakuhusisha washiriki kutoka katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe, Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza, Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Magdalena Rwebangira amewataka watendaji hao kutekeleza jukumu la kuhamasisha wananchi wa maeneo yao kushiriki kwenye uboreshaji kwa kushirikiana na wadau wengine wa uchaguzi.

“Mnahimizwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao,” alisema Mhe. Rwebangira.

Alisisitiza kuwa jukumu la uhamasishaji linawahusu moja kwa moja wao watendaji, kwa kushirikiana na wadau wengine katika maeneo yao kupitia nyenzo mlizo nazo.

“Mabango na vipeperushi mtakavyopewa na Tume mvisambaze mapema katika shehia zote zilizopo katika mikoa yote mitatu ya Unguja. Kazi yenu kubwa ni kusimamia na kuendesha shughuli zote za uboreshaji katika shehia zote” amesema Mhe. Magdalena.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mikoa ya Tanga na Pwani umepangwa kufanyika kuanzia tarehe 13 hadi 19 Februari, 2025 ambapo vituo vitafunguliwa Saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:00 jioni.
Meza Kuu ya Mafunzo kwa Mkoa wa Pwani ikiongoza na Makamu Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk (katikati) akifuatilia mafunzo hayo mkoani Pwani.


Washiriki wa Mafunzo kutika Mkoa wa Pwani wakiwa katika ufungaji wa mafunzo.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akiwa katika ufungaji wa mafunzo hayo mkoani Tanga.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ndg. Kailima R.K akizungumza jambo na washiriki mkoani Tanga.


Washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mkoa wa Tanga wakifuatilia hotuba ya ufungaji.
Washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mkoa wa Tanga wakifuatilia hotuba ya ufungaji.
Mwenyekiti wa Mafunzo kutoka Mkoa wa Tanga, Ndg. Mwanaidi Nondo akizungumza jambo kuhusiana na mafunzo hayo waliyopewa.

Washiriki wakifanya mazoezi kwa vitendo kwa kuandikisha wapiga Kura wapya, kuboresha taarifa na kufuta waliopoteza sifa.