Articles by "MIKOANI"
Showing posts with label MIKOANI. Show all posts

Na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/Michuzi TV, Manyara.

Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga (kwanza kushoto) leo Januari 29, 2025 amemuapisha Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Bw. Michael John Semindu aliyeteuliwa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika ukumbi wa Ofisi ya  mjini Babati, Manyara.

Hafla hiyo ya uapisho ilihudhuriwa na Wakuu wote wa Wilaya (5) za Mkoa wa Manyara, wakuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama.

Akizungumza na Wakuu wa Wilaya mara baada ya uapisho Mkuu Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga alitoa pongezi kwa Mkuu wa Wilaya mpya na kumshukuru  Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa uteuzi alioufanya.
Mhe. Sendiga aliweza kuwaelekeza Wakuu wa Wilaya hao vipaumbele vyake katika utendaji wa kazi ikiwemo ukusanyaji wa mapato ili Serikali iweze kuwahudumia Wananchi wake na kuleta maendeleo katika Taifa, usikilizaji na utatuzi wa kero za Wananchi kuanzia Ngazi ya Mtaa mpaka katika Halmashauri zao, kusimamia ulinzi na usalama kwa kuweka mikakati ya kudhibiti Uhalifu, ufuatiliaji na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Sambamba na hayo amesema; “Nendeni mkatimize wajibu wenu ipasavyo na mkatekeleze matarajio ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwani amewaamini na ndio maana amewapa nafasi hizo.”
Aidha Mhe. Sendiga amewaagiza wakuu wa wilaya Mkoani humo kushirikiana na jamii katika kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa Wanawake na wanaume kwani kumekuwepo na malalamiko juu ya wanaume kupigwa na wake zao hasa wilayani Hanang'.
Mhe. Sendiga amesema wakuu wa wilaya wanawajibu wa kuelimisha jamii juu ya ukatili wa kijinsia bila kuwasahau wanaume ambao nao wamekuwa wahanga wakubwa wa vipigo kutoka Kwa wake zao.

Naye mkuu wa wilaya ya Hanang' Mhe. Almishi Azal amekiri kuwepo kwa matukio ya wanaume wengi kunyanyaswa na wake zao.

Akitoa neno la shukrani, Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael John Semindu aliahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na watendaji wenzake pamoja na kuyapokea maagizo yote yaliyoagizwa na mkuu wa Mkoa na kuyatekeleza majukumu yao yote kwa weledi.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga (wa tatu kutoka kulia) akifurahi pamoja na Wakuu wa Wilaya, kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mhe. Fakii Raphael Lulandala, Mkuu wa Wilaya ya Hanang' Mhe Almishi Issa Hazal, Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Emmanuela Kaganda. Wa kwanza kutoka kushoto ni  Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Remidius Mwema pamoja na Mkuu Mpya wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael John Semindu.
Wanahabari wakiwa katika picha na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga (wa tatu kutoka kushoto waliokaa pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa.
Na Mwandishi Wetu.

Wakati zoezi la uhakiki, usasishaji na usajili wa Anwani za Makazi likiendelea katika Halmashauri sita za Mkoa wa Arusha, Halmashauri ya Monduli imefanikiwa kufikia asilimia 22.77 ya usasishaji anwani za makazi ndani ya siku 5 kutoka Agosti 17 hadi  21 mwaka huu 2024.

Akizungumzia maendeleo ya zoezi hilo ofisini kwake tarehe 21  Agosti, 2024, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Bi Happiness Laizer, amesema Anwani zilizosasishwa hadi leo mchana ni  6621 kati ya 29,082 zilizosajiliwa mwaka 2022.

Bi. Laizer amesema anwani mpya zilizosajiliwa ni 1,358 sawa na ongezeko la asilimia 4.67 yakiwa ni mafanikio makubwa kwa eneo hilo linalokaliwa na jamii ya Kimasai.

Waratibu wa Anwani za Makazi Taifa walipotembelea Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bi. Happiness Laizer, tarehe 21 Agosti, 2024.

Pamoja na mambo mengine wamezungumzia zoezi la Uhakiki, Usasishaji wa Anwani za Makazi na Usajili wa Anwani mpya linaloendelea pamoja na matumizi ya Mfumo wa programu Tumizi ya NaPA na huduma ya Barua ya Utambulisho Kidigitali.

Waratibu wa Anwani za Makazi Taifa walipotembelea Kaburi la Hayati Edward Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu katika Serikali ya Awamu ya Nne lililopo nyumbani kwake Kijiji cha Ngarashi, Halmashauri ya Wilaya ya Monduli. 

Timu hiyo ya wataalamu ikifika katika makazi ya kiongozi huyo wakati wa zoezi la Uhakiki wa Anwani za Makazi linaloendelea katika kijiji hicho tarehe 21 Agosti, 2024.
Waratibu wa Anwani za Makazi Taifa walipotembelea makazi ya Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Moringe Sokoine yaliyopo katika Kata ya Monduli Juu, Halmashauri ya Wilaya ya Monduli. 

Wataalam hao walipata nafasi hiyo wakati wakikagua maendeleo ya zoezi la Uhakiki wa Anwani za Makazi ambapo walipata nafasi ya kutembelea Kaburi la Kiongozi huyo lililopo nyumbani kwake tarehe 21 Agosti, 2024.
Na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/MMG, Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga mapema leo Januari 23, 2024 amefanya ziara ya kukagua baadhi ya miradi inayoendelea katika mkoa wake wilayani Babati.

Ziara hiyo ilianzia katika Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharula (EMD) katika Hospitali ya Mji wa Babati, ambapo amewataka wasimamizi wa mradi huo akiwemo mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange kujitahidi ujenzi wa jengo hilo unakamilika kwa haraka.

Akitoa taarifa Mganga Mkuu wa Mji Daktari Kyabaroti Kyabaroti amesema kuwa jengo hilo lilitengewa Mil. 300 ambapo mpaka sasa lipo katika hatua za umaliziaji na ifikapo mwanzoni mwa mwezi wa Februari litaanza kutumika.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga akiteta jambo na Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange mara baada ya kutembelea ujenzi wa jengo la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara ililopo eneo la Maisaka Katani kata ya Maisaka, Babati Mjini.
Pia, Mhe. Queen Sendiga alipata wasaa wa kutembelea ujenzi wa jengo la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Manyara ililopo eneo la Maisaka Katani kata ya Maisaka, Babati Mjini ulioanza Oktoba 25, 2023.

Mhe. Sendiga amejionea ujenzi huo huku akiwataka wataalamu hao kumaliza kwa wakati bila kutoa visingizio vyovyote vitavyosababisha ukwamishaji wa ujenzi huo.

Ujenzi huo unaogharimu shilingi Mil. 600 ambapo awamu ya kwanza wamepewa zaidi ya mil. 285 kwa ajili ya ukamilishaji wa Boma, msingi mpaka gorofa ya kwanza na sasa ujenzi umefikia asilimia 21.4.

Aidha Jeshi la Zimamoto Walimemshukuru Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuendelea kuwezesha majeshi ya Tanzania katika kukabiliana na majanga mbali mbali huku wakimshukuru Mhe. Sendiga na ofisi yake kwa ujumla kuweza kuwawezesha katika miongozo mbali mbali.
Mradi wa ujenzi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara linalojengwa eneo la mkoani wilayani Babati. 
Baadae Mhe. Queen Sendiga alifika katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara linalojengwa eneo la mkoani wilayani Babati. Mradi ulibuliwa baada ya Serikali kuanzisha mkoa wa Manyara mwaka 2002 na ndipo uhitaji wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa ulipotokea.

Jengo hilo la ghorafa nne ambapo likikamilika litakuwa na jumla ya vyumba vya ofisi 33 kati ya hivyo 06 ni vyumba vya ofisi za maafisa wakuu ngazi ya mkoa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, ACP George Katabazi amesema utekelezaji unaoendelea ni awamu ya Kwanza ambayo ilianza baada ya Serikali kutoa fedha mnamo mwezi Aprili 2023 jumla ya shilingi milioni mia nane tu (TShs.800,000,000.00) ambazo zilipokelewa Polisi Mkoa Manyara.

Amesema kazi zilizofanyika ni ujenzi wa msingi, nguzo na sakafu za ghorofa zote nne huku wakifanya maandalizi ya ujenzi wa kuta za pamoja na kuezeka na ujenzi wa chumba cha mitambo ya lifti ambapo wanatarajia ujenzi huo ukamilike mwishoni mwa mwezi Februari.

Nae Mhe. Sendiga amewapongeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara kwa kutekeleza mradi kwa vitendo huku akizitaka taasisi nyingine zenye miradi mkoani humo kuiga Jeshi la Polisi.

Aidha Mhe. Sendiga amemtaka mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange kuhakikisha anasimamia kwa ufasaha ujenzi wa jengo la ofisi ya yake linakamilika kwa wakati maana ujenzi wake umekuwa ukisua sua jambo linaloleta ukakasi kila anapotembelea.

Jengo la ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Babati ambapo ujenzi wake umekuwa ukisua sua. (Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason Blog/MMG, Manyara)
Mshindi wa pesa taslimu shilingi milioni 10 kupitia kampeni ya Vodacom Tanzania PLC ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, Bw. Kennedy Ntenje (wa tatu kulia) akiwa ameshikilia mfano wa hundi pamoja na Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) na wafanyakazi wa kampuni hiyo katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia tamati wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na Mkuu wa Kanda Nyanda za Juu Kusini - Vodacom Tanzania, Abednego Mhagama (wa kwanza kushoto) wakikabidhi mfano wa kadi ya bima kwa Kaimu Mganga Mfawidhi, Dkt. Scholastica Malangalila na mmojawapo wa akina mama walionufaika, Bi. Grace John (katikati) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia tamati ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) akifurahia pamoja na mmojawapo wa akina mama na mtoto wake walionufaika na bima ya bure ya afya kutoka Vodacom Tanzania, Bi. Grace John katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) akifurahia pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC mara baada ya kukabidhi bima kubwa za bure kwa akina mama na mtoto wao kwa mwaka mzima katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni yake iliyofikia kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, kampuni hii imekabidhi kadi za bima kwa akina mama 100 na watoto 100 hospitalini hapo ikiwa ni zawadi ya upendo kutoka kwa kampuni hiyo katika msimu huu wa sikukuu uliomalizika.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa luninga kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa pikipiki kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
Masta Shangwe (mwenye kofia ngumu) pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa pamoja na mshindi wa simujanja kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
Msanii wa Bongo Flava maarufu kama ‘Dogo Janja’ akijumuika pamoja na wakazi wa Iringa kutoa burudano kupitia kampeni iliyofika kikomo ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’ ya Vodacom Tanzania PLC, katika viwanja vya Stendi ya zamani ya mkoani humo mwishoni mwa wiki. Kupitia kampeni hiyo wateja walikuwa na fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.
WAZIRI wa Kilimo Hussein Bashe kulia akimgaia mche wa Mbegu ya Mchikichi zinazozalishwa na Shamba la Wakala wa Mbegu Asa Mkinga Mkulima wakati wa halfa ya ugawaji miche hiyo shamba la Mwele lililopo wilaya ya MkingaWAZIRI wa Kilimo Husein Bashe katika akionyeshwa maeneo mbalimbali yeye miche ya Michikichi kwenye Shamba la Wakala wa Mbegu Asa lililopo wilayani Mkinga wakati wa ziara yake kulia ni Mtendaji Mkuu wa Asa Sophia Kashenge na kushoto ni mkulima aliyepewa miche shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga
Waziri wa Kilimo Husein Bashe katikati akitembelea Shamba la Wakala wa Mbegu ASA wilaya ya Mkinga wakati wa ziara yake shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga kulia ni Mtendaji Mkuu wa ASA Sophia Kashenge akisisitiza jambo
Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge kushoto akimueleza jambo Waziri wa Kilimo Husein Bashe wakati alipotembelea wakala huo kwa ajili kugawa miche kwa wakulima
Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge wa pili kutoka kulia akimuonyesha kitu Waziri wa Kilimo Husein Bashe wakati wa ziara yake kwenye Shamba hilo
Waziri wa Kilimo Husein Bashe akizungumza na wakulima wa wilaya ya Mkinga wakati wa ziara yake ya kutembelea Shamba la Mwele lililopo wilayani Mkinga
Mkurugenzi wa Bodi Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona akiwa na viongozi wengine wakifuatilia kwa umakini maelekezo ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe
Watumishi wa Wakala wa mbegu za kilimo nchini (ASA) katika shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga wakiwa na viongozi wengine wakimsikiliza kwa umakini Waziri wa Kilimo Husein Bashe

Na Oscar Assenga,MKINGA

WAKALA wa mbegu za kilimo nchini (ASA) katika shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga wamezindua zoezi la ugawaji wa mbegu za michikichi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu la kutaka zao hilo litumike ipasavyo kuongeza uzalishaji wa mafuta hapa nchini.

Hatua ya utekelezaji huo imekuwa na mafanikio makubwa naa kwa sasa wana michikichi elfu 88 na lengo ni kutoa michikichi laki mbili kwa wakulima ambao wataipanda katika maeneo mbalimbali na hivyo kuwezesha kilimo cha zao kuwa na tija

Akizungumza wakati akikabidhi Miche ya Michikichi kwa Wakulima wwa zao hilo lengo likiwa ni kukabidhi michikichi laki mbili katika wilaya ya Mkinga mkoani Tanga,Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alisema wananchi wanaopewa miche hiyo lazima wajaze fomu na kusaini ikiwemo kubaki na kumbukumbu ambazo zitapelekewa Halmashauri.

Alisema zitapelekwa huko ili maafisa kilimo wapewe taarifa kwenye vijiji vyao ambavyo wananchi wamepewa miche ili wawafuatilie kwa ukaribu wanapopata matatizo waone namna ya kuyapatia ufumbuzi huko huko vijijini.

Waziri Bashe alisema kwa sababu wamekuwa bahati mbaya wakigawa miche lakini mingi inaishia njiani haikui na wananchi wanapoteza muda na kuweka nguvu zao hivyo ni muhimu uwepo wa ufuatiliaji huo

“Leo tunagawa miche ya Michikichi wilaya ya Mkinga na wananchi ambao wamepewa watajaza fomu kusaini na kubaki na kumbukumbu ambazo baadae zitapelekwa Halmashauri pia maafisa Kilimo wapewa Taarufa kwenye Vijiji vyao kwa lengo la kuwa na ufuatiliaji wa karibu watakakukumbana na matatizo waweze kuyapatia ufumbuzi”Alisema

Hata hivyo Waziri huyo alisema wataanzisha mashamba makubwa ya pamoja ambao amesema miongoni mwa wafaidika watakuwa wananchi wa maeneo husika huku akisisitiza umuhimu wa maafisa kilimo wakae vijijini.

“Kama walimu wanakaa vijijini na maafisa kilimo nao wakate vijiji lakini pia mikutano ya Serikali za vijiji ifanye kazi ya kujadili maafisa Kilimo maeneo hayo kama hawatimizi wajibu wao kama hawafanyi hivyo serikali za vijiji ziandike taarifa kwenye mustasari zipelekewe kwenye WDC halafu ziende Halmshauri”Alisema

Waziri huyo alisema kwamba katikaa taarifa hiyo waeleze Afisa kilimo walionae hajawahi kuwatembelea wakulima hata siku moja kwani Serikali imegawa pikipiki na sasa wanawapa vishkambie na wamepekea vipima afya vya udongo ili wanapopima shamba wawaambie kama shamba linafaa kulima mashina au na huduma hiyo ni bure.

Katika hatua nyengine Waziri Bashe amemuagiza Mkurugenzi wa Asa Sophia Kashenge waanze shughuli za kuzalisha miche ya minazi kwenye kituo hichgo kama wanavyozalisha mice ya mazao mengine ili wananchi waweze kupata m iche ya minazi kutoka kwenye kituo hicho,

Awali akizungumza katika Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge alisema kwa sasa wana michikichi elfu 88 na lengo ni kutoa michikichi laki mbili kwa wakulima.

Sophia alisema kwamba wamefarijika sana kuona Waziri kufika katika shamba hilo ambalo kipindi cha nyuma lilikuwa limetekelezwa lakini nguvu ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu imeonekana na wameweza kulifufua.

Alisema kwamba huwezi kufanya uzalishaji bila kuwa na miuondombinu ya umwagiliaji na hivyo lengo lao wataendelea kuongeza uzalishaji wa mbegu jambo ambalo ni kipaumbele cha nchi.

“Suala la Uzalishaji wa Mbegu za Michikichi ni Agizo la Waziri Mkuu tokea 2018 na sisi tumeitika vizuri tuna mashamba matatu ya ASA na la Mkinga ni la pili kwa uzalishaji wa michikichi na tunaamini kazi tunayoifanya ni kumuongezea mwananchi kipato”Alisema

Naye kwa upande wake Mkulima wa zao la Michikichi Mtarajiwa wilayani Mkinga Maaono Mkangwa alisema serikasli imechukua uamuzi mzuri kuwaletea kilimo hicho ambacho wanaamani kitawainua kiuchumi.

Mpango wa serikali ni kupunguza kiwango kikubwa cha kuingiza mafuta kutoka nje ya nchi wakati mafuta hayo yanaweza kuzalishwa na wakulima hapa nchini.