Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akiwasili katika katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Alioongozana nao ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
“Kwa kusogeza huduma za kifedha karibu na waendeshaji wa utalii na jamii zinazowazunguka, tunaboresha ujumuishaji wa kifedha na kusaidia ukuaji endelevu wa uchumi wa Zanzibar unaotegemea utalii,” alisema Kinswaga.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wawekezaji wa Utalii Zanzibar (ZATI), Suleiman Mohammed, aliipongeza Benki ya Exim kwa mchango wake, akieleza kuwa upatikanaji wa huduma za kifedha ni nguzo muhimu kwa uendelevu wa sekta hiyo.
Kwa kudhamini Z-Summit 2026 na kupanua wigo wa huduma zake, Benki ya Exim inaendelea kujidhihirisha kama mshirika wa kimkakati katika maendeleo ya sekta ya utalii na ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.
Dar es Salaam, Februari 10, 2025 — Kampuni ya Samsung Electronics East Africa imezindua rasmi maduka mawili mapya ya chapa (Brand Stores) katika maeneo ya Kunduchi na Ubungo, ikiwa ni mkakati wa kupanua uwekezaji wake nchini Tanzania na kuimarisha ushindani katika soko la teknolojia na rejareja.
Maduka hayo yamebuniwa kuunganisha bidhaa za simu za mkononi na vifaa vya kielektroniki vya nyumbani chini ya paa moja, yakilenga kuwapatia wateja uzoefu wa moja kwa moja wa mfumo wa bidhaa unaofanya kazi kwa pamoja. Kupitia mpangilio huo, wateja wanapata fursa ya kuona, kujaribu na kuelewa namna simu janja, kompyuta kibao, runinga, vifaa vya kuvaa pamoja na vifaa vya nyumbani vinavyoweza kuunganishwa ili kurahisisha shughuli za kila siku.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Kitengo cha Simu za Mkononi wa Samsung Electronics East Africa (Tanzania), Mgope Kiwanga, alisema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kampuni katika soko la Tanzania. Alisema maduka hayo yanatoa nafasi kwa wateja kujionea kwa vitendo namna teknolojia ya Samsung inavyoweza kuleta tija katika mawasiliano, burudani na matumizi ya nyumbani.

Kwa upande wake, Meneja wa Biashara wa Samsung Tanzania, Daesong Ra, alisema uwekezaji huo unaonesha imani ya kampuni katika ukuaji wa soko la Tanzania na mchango wake katika mageuzi ya kidijitali. Alibainisha kuwa upanuzi huo unachochea ajira, unakuza ujuzi wa wafanyakazi wa ndani na kuongeza upatikanaji wa teknolojia bora kwa watumiaji.
Mbali na kuboresha uzoefu wa wateja, maduka hayo yanatarajiwa kuchangia ukuaji wa uchumi wa ndani kupitia ajira na mafunzo ya kitaalamu kwa Watanzania, huku yakiiweka Samsung katika nafasi imara zaidi ya ushindani katika sekta ya teknolojia inayokua kwa kasi nchini.

Dar es Salaam, Februari 10, 2026: Katika hatua inayoonesha mwelekeo mpya wa michezo ya kubahatisha nchini, PigaBet imezindua kampeni ya “SHINDA BODA” inayolenga si burudani pekee, bali pia kuwawezesha wachezaji—hasa vijana—kujipatia mtaji wa kujiajiri na kujiongezea kipato kupitia ushindi wa pikipiki mpya kila wiki.
Kampeni hiyo inawapa wachezaji wawili kila wiki fursa ya kushinda boda boda, zawadi ambayo kwa wengi imekuwa nyenzo muhimu ya kujiajiri au kuongeza kipato cha kila siku. Kupitia mfumo wa PigaPoints, kila mchezaji anayeshiriki michezo ya PigaBet ikiwemo Sports Betting, Casino na Aviator hujikusanyia pointi kwa kila bet au raundi, hali inayoongeza nafasi yake ya kuingia kwenye droo ya ushindi.
Akizungumza kuhusu dira ya kampeni hiyo, Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora, alisema kampeni ya Shinda Boda inalenga kuwafanya wachezaji waone thamani ya muda na ushiriki wao.
“Tumelenga kumwezesha mchezaji kubadili ushindi kuwa fursa ya maisha. Boda si zawadi tu, ni chombo cha ajira, ni mtaji na ni mwanzo wa safari ya kujitegemea kiuchumi,” alisema Kazola.
Tofauti na kampeni nyingi za awali, Shinda Boda imebuniwa kuunganisha burudani, ushindi na uwezeshaji wa kiuchumi. Wachezaji hawazuiliwi na mchezo mmoja pekee, bali wanaruhusiwa kucheza michezo mbalimbali ndani ya jukwaa la PigaBet, jambo linalowawezesha kukusanya pointi zaidi na kuongeza nafasi ya ushindi.
PigaBet pia imeendelea kuvutia wachezaji kwa promosheni zinazolinda na kuongeza thamani ya mchezaji, ikiwemo 10% Cashback kila Jumatatu kwa bet zilizopotea, Win Boost hadi 1000%, pamoja na huduma ya 2UP na Cashout, vinavyompa mchezaji udhibiti zaidi wa michezo yake.
Kwa kutambua nguvu ya mitandao ya kijamii, kampeni hiyo pia imefungua milango kwa content creators kupitia PigaBet Content Creator Challenge, itakayoratibiwa na mshirika wao WAKA.WIN. Kupitia mpango huo, wabunifu wa maudhui watapata nafasi ya kunufaika kifedha kwa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha kampeni.
Wadau wa michezo ya kubahatisha na vijana kwa ujumla wamehimizwa kujisajili kupitia www.pigabet.co.tz na kushiriki kampeni hiyo, huku PigaBet ikisisitiza umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
Kwa mtazamo mpya unaoangazia ajira na uwezeshaji, Shinda Boda imejipambanua kama kampeni inayotazama mbali zaidi ya ushindi wa muda mfupi, na kuweka msingi wa matumaini mapya kwa vijana wanaotafuta fursa za kujikwamua kiuchumi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, mara baada ya mazungumzo kati yao, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026. 


































.jpeg)







.jpeg)

.jpeg)











.jpeg)