Articles by "HABARI ZA BIASHARA"
Showing posts with label HABARI ZA BIASHARA. Show all posts
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (Kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Abdulmajid Nsekela, wakipiga makofi mara baada ya kuzindua ushirikiano kati ya taasisi hizo unaoenda kuwezesha upatikanaji wa simujanja kwa mkopo ili kuchochea matumizi ya intaneti na ukuaji wa uchumi wa kidijiti nchini. Kulia kwa Besiimire ni Mkurugenzi wa Biashara wa Vodacom Bi. Linda Riwa na kushoto kwa Nsekela ni Afisa Biashara Mkuu wa benki hiyo Bw. Boma Raballa.
Dar es Salaam - Machi 27, 2024. Katika jitihada za kuongeza upatikanaji na matumizi ya simu janja ili kuziba pengo la kidijitali nchini, makampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Benki ya CRDB wamezindua mpango wa kuwezesha Wateja wao kumiliki simujanja zenye ubora kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo wa kukopesha simu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alieleza kuwa kampuni hiyo ya simu inatekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza gharama za vifaa vya mawasiliano ili kuwawezesha wateja wake kuhama kutoka kwenye matumizi ya mtandao wa 2G na kumiliki simu zenye uwezo wa 4G na kutumia fursa hiyo ili kunufaika na faida kemkem zinazopatikana kupitia mtandao huo.

"Tukiwa ni mdau na mshirika mkubwa wa sekta ya mawasiliano na teknolojia, Vodacom tunajivunia kuzindua mpango huu na Benki ya CRDB ambayo ni taasisi kubwa ya fedha nchini. Ushirikiano wetu unalenga kuwawezesha wateja kutoka pande zote mbili kupata aina mbalimbali za simujanja kwa bei nafuu na mpango wa malipo kwa awamu kwa kipindi fulani. Ili kujua kama amekidhi vigezo, mteja atatakiwa kupiga *150*00*44# nbaada ya hapo atafanya malipo ya awali na kupewa simujanja. Mkopo huu unaweza kulipwa kwa siku, kwa wiki au kwa mwezi kwa kipindi cha hadi miezi 12 kupitia M-Pesa," alifafanua bwana Besiimire.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema, “ushirikiano huu baina yetu na Vodacom ni fursa nzuri kwa Watanzania kupata huduma za kifedha na mawasiliano kwa gharama nafuu. Kwa hiyo kama wadau muhimu tunapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuhakikisha wananchi wake wanafaidika na ukuaji na maendeleo katika sekta hizi.”

Bwana Nsekela aliongeza kuwa, “Kwa mtandao wetu ulioenea nchi nzima, CRDB tumekuwa na mchango muhimu katika maendeleo ya Watanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha. Hivyo basi, kwa kushirikiana na Vodacom, tutaweza kutoa mchango wetu ili kuongeza matumizi ya simujanja nchini.”

Licha ya juhudi za mamlaka nchini kusogeza huduma za mawasiliano, wananchi wengi bado wanatumia huduma za mtandao wa 2G. Hii inapunguza upatikanaji wa fursa zilizopo mtandaoni pamoja na kufurahia na kunufaika na intaneti yenye kasi zaidi kutoka Vodacom pamoja na bidhaa nyingine za kidijitali.

Matumizi ya simujanja na intaneti yana faida kwa jamii kama vile kukuza ukuaji wa kiuchumi kwa kuwezesha ujasiriamali wa kidijitali na kuchochea uvumbuzi, utafutaji masoko mitandaoni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi wanaoamua kujiajili kupitia dijitali.
Vodacom Tanzania imekuwa ikishirikiana na watengenezaji mbalimbali wa simu za mkononi na taasisi za kifedha ili kuwezesha Watanzania kumiliki simu kupitia mikopo nafuu na mipango rafiki ya malipo kwa mteja.

Mwezi August 2020, Vodacom ilizindua programu ambayo inawaruhusu wateja wake kumiliki simujanja kupitia mkopo unaolipwa kwa awamu, huku kianzio kikiwa ni Shilingi 20,000 za Kitanzania kwa muda wa miezi 12.

Bwana Nsekela alimalizia kwamba anaamini kuwa taasisi hizo mbili zina huduma mbalimbali za kibunifu ambazo zitawanufaisha na kuboresha maisha ya wateja wao. Pia alitoa wito kwa Watanzania wanaotumia simu za kawaida na wanataka zenye ubora zaidi kufika katika maduka ya Vodacom na kupata simujanja kwa bei nafuu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali duniani.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba (kushoto) akimkabidhi leseni ya kuongezewa muda wa uchimbaji wa mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido katika hafla hiyo , wanaoshuhudia nyuma (kushoto) ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha. Leseni hii mpya iliyotolewa ni ya kipindi cha miaka 27.
---
Serikali kupitia Wizara ya Madini imeongeza muda wa leseni ya uchimbaji wa dhahabu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, uliopo katika wilaya za Kahama na Nyang’hwale mkoani Shinyanga kwa kipindi cha miaka 27 kuanzia mwaka huu.

Hafla ya kukabidhi leseni hiyo ilifanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Maofisa waandamizi kutoka Wizara ya madini, Wakuu wa mikoa ya Tanga na Shinyanga na wadau mbalimbali kutoka sekta ya madini ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde.

Aliyekabidhi leseni hiyo ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, na Mwakilishi wa Barrick, aliyepokea leseni hiyo kwa niaba ya kampuni ni Meneja wa Barrick Tanzania, Melkiory Ngido.

Mgodi wa Bulyanhulu tangu uanze kuendeshwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals, umefanikisha kuleta mafanikio chanya katika kukuza uchumi wa nchi ,kuongeza fursa za ajira sambamba na kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii kupitia fedha za uwajibikaji wa jamii (CSR) ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi katika maeneo yanayozunguka mgodi huo hususani katika sekta ya afya na elimu.
Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kushoto) katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa makampuni ya uchimbaji wa madini waliokabidhiwa leseni katika hafla hiyo.

Maofisa Waandamizi wa Barrick waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu.

Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita wakati wa hafla hiyo.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Antony Mavunde katika hafla hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Jaffari Matundu, akizungumza na wadau (hawapo pichani) katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya benki na wadau wake wakiwemo wateja na jamii katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akitoa pongezi kwa Benki ya Exim kwa kuandaa Iftar akielezea namna ambavyo imewaleta pamoja waumini wa dini ya kiislam kama ishara ya upendo, umoja na heshima kwa wadau wote katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu (wa tatu kutoka kushoto) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar (watatu kutoka kulia) wakiwa na baadhi ya viongozi wa Exim Bank wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Wadau mbalimbali na wawakilishi wa Benki ya Exim wakifurahia Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwaleta pamoja katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani kuashiria furaha, umoja, na upendo katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omar (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Exim Bank, Jaffari Matundu (watatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa benki hiyo wakati wa hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwakutanisha wateja wake pamoja katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani iliyofanyika tarehe 15 meezi Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
---
(Dar es Salaam, Machi 15 2024). Benki ya Exim imeandaa futari ya pamoja kwa wateja wake katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 15 mwezi Machi 2024.

Mgeni Rasmi katika tukio hili alikuwa Sheikh Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akiwakilisha waumini wa dini ya Kiislam ambao wapo kwenye mfungo katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza katika hafla hiyo, Sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, aliipongeza Benki ya Exim kwa juhudi zake katika kukuza maendeleo ya kijamii na kueleza shukrani zake kwa mchango wa benki hiyo kwa jamii. Alisema, “Benki ya Exim inaonyesha dhamira ya kweli katika kutumikia wateja wake na jamii kwa ujumla, lengo kuu la Ramadhani ni kuleta watu pamoja, na usiku huu, benki ya Exim imehakikisha kuendeleza lengo hilo kwa vitendo”.

Bwana Jaffari Matundu, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim, aliwakaribisha wadau wote katika Iftar hiyo huku akitambua mahusiano mazuri ya tija yaliopo baina ya Benki ya Exim na wateja wake na umuhimu wa kuyaendeleza kwa ajli ya ustawi na maendeleo ya jamii.

“Wateja wetu ni zaidi ya wateja tu, ni sehemu muhimu ya familia yetu. Tunaona kila mmoja wenu kama mshirika na mwenzetu katika safari yetu ya mafanikio”, alisisitiza Jaffari Matundu.

Pia, Mkurugenzi huyo alizungumzia hatua na maboresho mbalimbali ambayo yamefanywa na benki ya Exim ili kuendana na mabadiliko katika sekta mbalimbali ikiwemo maendeleo ya teknolojia ya kidijitali na kusogeza huduma kwa wateja.

Jaffari alifafanua kuwa, “tumefanya maboresho makubwa katika mfumo wetu wa Benki ili kuendelea kuhudumia wateja wetu vizuri zaidi kwa kutoa huduma zinazoendana na mabadiliko ya kidigitali”.

“Vile vile tumeendelea kuongeza idadi ya Mawakala wetu (maarufu kama Exim Wakala) ili kuleta huduma zetu karibu na wateja wetu popote walipo”, alimalizia Afisa Mtendaji Mkuu huyo.

Exim Bank pia imeboresha huduma za kidijitali kwa wateja wake ambapo wanaweza kupata huduma za kibenki popote pale walipo ndani na nje ya Tanzania. Hii ni kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki kwa wateja wao na maendeleo ya teknolojia yanayoendelea kutokea duniani.
Katika jitihada zake za kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali nchini, Benki ya CRDB ilizindua msimu wa tatu wa kampeni ya ‘Benki ni SimBanking’ na kutenga jumla ya zawadi zenye thamani ya Shilingi milioni 470 kwa wateja wake mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, wakati wa kutangaza washindi wa droo ya mwezi wa pili wa kampeni hiyo, Meneja Mwandamizi wa Huduma za Kidigitali wa Benki ya CRDB, Mangire Kibanda amesema lengo la kampeni hiyo ni kujenga utamaduni wa matumizi ya kidijitali katika huduma za kifedha ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuondokana na matumizi ya fedha taslimu na kuwasihi wateja kuendelea kufanya miamala kupitia 'SimBanking' sababu inalipa.

Washindi wa awamu ya kwanza wa kampeni ya Benki ni SimBanking Miamala Inalipa ni Rahma Kyalumbika wa Dar es salaam, na Kibwana Killongo (kutoka Kibaha, Pwani) ambao kila mmoja ameshinda pikipiki huku Adamu Rashid (kutikea Chanika, Dar es salaam) akiibuka mshindi wa Bajaji kwa mwezi wa pili. Vyombo vyote hivi vitawekewa mafuta 'full tank' na kukatiwa bima kubwa.

Pamoja na zawadi hizi Benki hiyo pia imetenga kiasi cha Shilingi milioni 200 zitakazotolewa kupitia Tembo Points ambazo mteja atakuwa akikusanya kila anapofanya muamala. Wateja wataweza kubadili Tembo Points zao kuwa fedha na kuzitumia kulipia huduma au bidhaa. Pia zawadi za kompyuta mpakato kufikia 10 kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu, zawadi za simu janja, pamoja na fedha taslimu.
Meneja Mwandamizi Huduma za Kidigitali wa Benki ya CRDB, Mangile Kibanda (kulia) akizungumza wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya msimu wa tatu wa kampeni ya ‘Benki ni SimBanking’ iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Daress salaam. Katika droo hiyo, Washindi watatu walipatikana ambapo Wawili wamejishndia Pikipiki moja kila mmoja na Mwingine ameshinda Bajaj. Wengine pichani ni Afisa Masoko wa Benki ya CRDB, Salim Salim (kushoto) pamoja na Afisa wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja, Clara Chacha.
Afisa Masoko wa Benki ya CRDB, Salim Salim akifafanua jambo wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya msimu wa tatu wa kampeni ya ‘Benki ni SimBanking’ iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Daress salaam. Wengine pichani ni Meneja Mwandamizi Huduma za Kidigitali wa Benki ya CRDB, Mangile Kibanda (kulia) na Katikati ni Afisa wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja, Clara Chacha.

Na. Mwandishi wetu - Kilimanjaro


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa siku 100 kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Wafanyakazi wa Umma (PSSSF) Ndg. Abdul-Razaq Badru kuhakikisha Awamu ya Pili ujenzi wa kiwanda cha kuchakata Bidhaa za Ngozi Kilimanjaro unakamilika na kuanza kufanya kazi ifikapo Julai 2024.
Agizo hilo amelitoa leo Februari 22, 2024 alipo fanya ziara ya kukagua ujenzi katika kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) ikiwa ni sehemu ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.
Mhandisi Luhemeja amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani ya zao la ngozi ghafi, kufungua fursa za soko la uhakika la Ngozi kutoka kwa wafugaji, kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya fedha za ndani na za kigeni.


Aidha, amefurahishwa na ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo na kutoa wito kwa watanzania kuwa na tamaduni za kuthamini bidhaa zinazo zalishwa nchini.


Awali akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Ndg. Abdul-Razaq Badru amesema amepokea maagizo hayo ya Katibu Mkuu Mhandisi Luhemeja na kuahidi kuwa PSSSF kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza watahakikisha wanafanya kazi kwa weledi kama ilivyo elekezwa ili watanzania waanze kunufaika na mradi huo.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho Mhandisi Saiba Edward amesema mradi huo pamoja na mambo mengine, utaongeza kipato kwa wakazi wa Kilimanjaro na Mikoa jirani kupitia fursa za uzabuni, uwakala na usambazaji wa bidhaa.


Kwa upande wake Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza Frank Mwakijungu amebainisha kuwa Magereza ni mbia wa utekelezaji wa Mradi huo hivyo watasimamia ujenzi wa kiwanda hicho ili kikamilike kwa wakati kwa manufaa ya watanzania.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemaja (kushoto) akikagua bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) leo Februari 22, 2024 ikiwa ni mwendelezo wa kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.




















Dar es Salaam 19 February 2024 – Katika jitihada za kuendeleza sekta ya habari nchini, Benki ya CRDB imeendesha semina maalum kwa wadau wa sekta ya habari nchini na uchumi “CRDB Bank Media Day” iliyofanyika katika Makao Makuu ya benki hiyo yaliyopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema “CRDB Bank Media Day” ya mwaka huu imejikita katika kuangazia ripoti ya Finscope 2023 na namna gani vyombo vya habari vinaweza kuchochea ujumuishi nchini.
“Ripoti ya Finscope ya 2023 inaonyesha ujumuishi wa kibenki upande wa huduma za benki ni 22% tu pamoja na jitihada na ubunifu mkubwa katika bidhaa. Hii inaonyesha kuna ombwe kubwa la elimu ya fedha, hivyo leo tumepata kujadili ninamna gani wenzetu wa sekta ya Habari wataweza kusaidia kutoa taarifa na huduma za fedha,” alisema Nsekela.

Katika semina hiyo waandishi wa habari walipata fursa ya kupata mafunzo ya namna ya bora ya kaandaa na kutoa mafunzo ya taarifa za biashara, fedha na uchumi. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kusaidia kujenga waandishi mahiri nchini.
Akizungumza katika semina hiyo, Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuandaa semina hiyo iliyowaleta wadau wa sekta ya habari kujadili namna ya kuongeza mchango wake katika maendeleo hususani katika kuongeza ujumuishi wa kifedha nchini. Matinyi amewahakikishia wadau wa sekta hiyo kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri yatakayosaidia kuboresha sekta ya habari.

Mada mbalimbali zimewasilishwa katika semina hiyo ikiwamo ‘Jukumu la Vyombo vya Habari katika kuchochea Ujumuishi wa Kifedha’ iliyowasilishwa na Mhariri Mstaafu wa Nationa Media Group Kenya, Charles Onyango Obbo, ‘Elimu ya Fedha kupitia Mitandao ya Jamii’ iliyowasilishwa na Fayness Sichwale amshauri wa masuala binafsi ya fedha na Mwanzilishi wa Personal Finance Hub, na Usomaji na Uwasilishaji wa Taarifa za Fedha’ iliyowasilishwa na Dkt. Ndalahwa Masanja, Mhadhiri Mwandamizi Chuo Kikuu cha ESAMI.
Katika Semina hiyo iliyohudhuriwa na waandishi na wahariri kutoka vyombo mbali nchini, Benki ya CRDB pia imezindua shindano maalum la kutafuta waandishi wahabari wachanga wa habari za biashara, fedha, na uchumi. Shindano hilo ambalo litaendeshwa kwa muda wa miezi miwili hadi Aprili 12 2024, litatoa washindi watatu ambao watajishindia zawadi ya Sh. Milioni 1 na nafasi ya kufanya kazi na Benki ya CRDB.
Aidha, katika hafla hiyo Benki ya CRDB imetoa tuzo za kutambua mchango wa waandishi wa habari wawili nguli katika sekta ya habari nchini. Waliokabidhiwa tuzo hizo ni Edda Sanga mwandishi mstaafu wa Shirika la Habari la Tanzania (TBC) na Mwenyekiti wa Umoja wa Waandishi wa Habri Wanawake (TAMWA), na Ndimara Tegambwage mwandishi wa zamani wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, na moja ya waanzilishi wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA).
Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mobhare Matinyi, akimkaidhi Tuzo ya Heshima kutoka Benki ya CRDB kwa Mwanahabari wa Habari Mkongwe nchini, Mzee Ndimara Tegambwage , ikiwa sehemu ya kutambua mchango wake katika tasnia ya Habari hapa nchini, wakati wa semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaii wa Benki va CRDB, Abdulmajid Nsekela, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki va CRDB Bruce Mwile pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa.
Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mobhare Matinyi, akimkaidhi Tuzo ya Heshima kutoka Benki ya CRDB kwa Mwanahabari wa Habari Mkongwe nchini Mama Eda Sanga, ikiwa sehemu ya kutambua mchango wake katika tasnia ya Habari hapa nchini, wakati wa semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaii wa Benki va CRDB, Abdulmajid Nsekela, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki va CRDB Bruce Mwile pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa.

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa akizunguma katika semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam.