Articles by "ELIMU."
Showing posts with label ELIMU.. Show all posts
Mafunzo Elekezi kwa Watumishi Wapya wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) yameanza leo, Mei 28, 2026, ikiwa ni hatua muhimu ya kuandaa wataalamu wa mamlaka hiyo kwa kuzingatia misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali. Watumishi wapya 29 wanashiriki mafunzo haya .yanayotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. 


"Tunatarajia kuwa baada ya mafunzo haya, mtakuwa watumishi wa umma wanaofuata maadili ya utumishi wa umma, wakiwasiliana kwa ufanisi na kuheshimu usiri wa taarifa na nyaraka za serikali, huku pia wakielewa haki na wajibu wao," amesema.

Kwa upande wake, Bi. Zena Hussein ambaye ni Meneja wa kituo cha mafunzo kwa njia ya Mtandao  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, amesema kuwa mafunzo haya ni muhimu na lazima kwa watumishi wapya katika utumishi wa umma. 
"Mafunzo haya yanalenga kuimarisha uelewa wa misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi," amesisitiza.

Aidha amesema kuwa Mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza uelewa wa watumishi wapya kuhusu misingi ya utumishi wa umma na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ndani ya TISEZA. Vilevile, mchakato huo unazingatia taratibu na miongozo ya serikali, kwa lengo la kuhakikisha majukumu yanatekelezwa kwa uwajibikaji, uadilifu, na ufanisi.
Mafunzo haya ni utekelezaji waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2011, uno wataka waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wapya wanapatiwa mafunzo elekezi ndani ya miezi sita tangu kuajiriwa,
By Zamda George, CMU

DAR ES SALAAM — An atmosphere of pride, academic excellence and national prestige filled Mlimani City Hall on May 25, 2026, as the University of Dar es Salaam (UDSM) conferred degrees to 876 graduates, including 94 new PhD holders, during Cluster I of its 56th Graduation Ceremony.

The ceremony, presided over by the University Chancellor and former President of Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, reaffirmed UDSM’s position as one of Africa’s leading centres of research, innovation and intellectual leadership.

The 94 doctoral graduates came from 15 academic disciplines, reflecting the University’s growing role in producing highly skilled researchers, innovators and professionals capable of contributing to national transformation and global development.

Unlike the lively celebrations commonly associated with undergraduate graduations, the PhD ceremony carried an atmosphere of academic maturity and scholarly prestige. Dressed in elegant academic regalia, the graduates proudly crossed the stage, symbolizing years of sacrifice, resilience, rigorous research and dedication.

Speaking during the ceremony, Chancellor Kikwete urged graduates to use their education and research to solve societal challenges and contribute to national development.

“Your education must become a tool for bringing positive change to society. The knowledge and expertise you have acquired should help drive innovation, leadership and transformation for the benefit of Tanzania and the wider global community,” said Dr. Kikwete.

He further emphasized the importance of research and knowledge creation in shaping Africa’s future, noting that universities must continue producing scholars capable of providing evidence-based solutions to emerging challenges.

UDSM Vice Chancellor, Prof. William A. L. Anangisye, described the graduation ceremony as a reflection of the University’s continued growth in teaching, research, innovation and international competitiveness.

Presenting the University’s annual progress report, Prof. Anangisye revealed that UDSM currently has 235 researchers ranked among Tanzania’s top 1,000 researchers according to the AD Scientific Index 2026. This represents 23.5 percent of all top researchers across 50 institutions nationwide.

He added that the University has continued strengthening academic quality and labour market relevance through curriculum reforms, with 285 undergraduate and postgraduate programmes reviewed based on stakeholder feedback and changing market demands.

Prof. Anangisye also highlighted major achievements in innovation and research commercialization. During the 2025/2026 academic year, UDSM researchers and innovators registered six patents through BRELA, some involving student innovators.

The registered innovations include technologies for bioethanol production, mushroom cultivation using sisal waste, organic fertilizer production, protein feed development using Black Soldier Fly larvae, and wine production from bamboo juice.

“These achievements demonstrate UDSM’s ability to add value to local resources, promote the green economy and use science to provide practical development solutions,” said Prof. Anangisye.

The Vice Chancellor further revealed that through the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project, the University is currently constructing 21 new buildings and renovating three others, a move expected to increase student capacity by 4,812 spaces.

He added that UDSM has also expanded digital learning infrastructure by increasing internet capacity, digitizing more than 1,000 courses and providing short-term professional training to nearly 3,000 staff members.

Addressing graduates directly, Prof. Anangisye reminded them that education is both a privilege and a responsibility to society.

“Education is not merely a personal achievement or decoration. It is a responsibility and a debt to the nation. Use the knowledge you have acquired to serve society, create opportunities and contribute to national development,” he said.

He encouraged graduates to embrace innovation, entrepreneurship and opportunities within the digital economy, especially in situations where formal employment opportunities may not immediately be available.

One of the most inspiring moments of the ceremony was the graduation of Dr. Paul Msoka, a visually impaired scholar who earned a PhD in Education after previously completing both his Bachelor’s and Master’s degrees within the UDSM system.

Dr. Msoka’s achievement stood out as a powerful testimony to resilience, determination and the University’s commitment to inclusive education and equal access to academic opportunities.

A researcher specializing in inclusive education and visual impairment studies, Dr. Msoka has contributed scholarly work focused on improving learning opportunities for students with visual impairment in Tanzania’s inclusive schools.

His achievement inspired many graduates, lecturers, family members and guests attending the ceremony, particularly young Tanzanians living with disabilities who aspire to pursue higher education and professional excellence.

Throughout the ceremony, emotional moments unfolded as graduates celebrated with supervisors, colleagues, friends and family members. Smiles, embraces and photographs reflected years of perseverance, sacrifice and academic dedication behind every success story.

Established in 1961, the University of Dar es Salaam remains Tanzania’s premier institution of higher learning and a symbol of academic excellence. Over the decades, the University has produced influential leaders, policymakers, scholars, diplomats, entrepreneurs and professionals who continue shaping Tanzania, Africa and the wider world.

For the Class of 2026, the graduation ceremony marked not only the completion of an academic journey, but also the beginning of a new chapter of leadership, innovation and national service.

As celebrations continued outside Mlimani City Hall, one message remained clear — the future of Tanzania’s intellectual, scientific and developmental transformation continues to be shaped at the University of Dar es Salaam.




Na Mwandishi Wetu

Serikali ya Kenya imetoa hati rasmi za vyuo vikuu kwa Kenya Advanced Institute of Science and Technology na Kenya Medical Research Institute katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Nairobi, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya juu, utafiti wa kisayansi na ubunifu nchini humo.

Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya mkakati wa makusudi wa kupanua fursa za elimu ya juu pamoja na kuimarisha mazingira ya utafiti na uvumbuzi yatakayosaidia maendeleo ya taifa.

Kupitia hatua hiyo, Kenya inalenga kujenga mustakabali unaotegemea elimu bora, ubunifu wa ndani na maendeleo endelevu ya tafiti mbalimbali za kisayansi.

Viongozi waliozungumza wakati wa hafla hiyo walisisitiza kuwa vyuo vikuu vina nafasi muhimu katika kuandaa wataalamu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasayansi, wahandisi, madaktari na wabunifu ambao watasaidia kuleta mabadiliko ya maendeleo nchini.

Aidha, ilielezwa kuwa pamoja na kuchangia maendeleo ya kitaifa, wataalamu hao pia wanatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika nyanja mbalimbali duniani kupitia maarifa, teknolojia na suluhisho za changamoto zinazokabili jamii.

Hatua hiyo pia inatazamwa kama juhudi za Kenya za kuimarisha sekta ya elimu na kuifanya nchi hiyo kuwa kitovu cha utafiti, teknolojia na ubunifu katika ukanda wa Afrika.









Dar es Salaam- Mei 5, 2026: Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Serikali Kenya (KSG), Prof. Nura Mohamed na ujumbe wake   wametembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania leo, Mei 5, 2026, jijini Dar es Salaam.
Ziara hiyo ni sehemu ya kuanza kwa utekelezaji wa mkataba wa ushirikiano uliosainiwa Ikulu, Mei 4, 2026, mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto.

Katika kikao cha pamoja na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, chini ya Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho, wamejadiliana kwa kina kuhusu mikakati ya kuanza utekelezaji wa makubaliano hayo, huku lengo likiwa ni kuboresha utendaji wa utumishi wa umma kwa kuwajengea uwezo watumishi na Tafiti Tumizi.
Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amesema  kuwa, ushirikiano kati KSG na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania  (TPSC) unalenga kuleta maendeleo makubwa na ufanisi zaidi katika sekta ya utumishi wa umma, kwa kujenga uwezo wa watumishi kupitia mafunzo na tafiti.

 Aidha, alisisitiza kuwa, kutokana na uzoefu wa zaidi ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa KSG, ni fursa adhimu kwa TPSC kujifunza na kupata uzoefu wa kuboresha utumishi wa umma nchini Tanzania, ili kujenga utumishi wa umma imara.

Dkt. Mabonesho ameongeza kuwa, mashirikiano pia yanalenga kujenga utumishi wa umma wenye tija, wenye kuzingatia matokeo, na kuleta maendeleo chanya kwa wananchi wa Tanzania, Kenya, na jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla.
Kwa upande wake, Prof. Nura Mohamed alieleza kuwa, utekelezaji wa mkataba huo utaleta maendeleo makubwa kwa pande zote mbili, kwa kuimarisha mafunzo yanayozingatia ubora na haki za wananchi.

 Prof. Mohamed amesisitiza  kuwa, ushirikiano huo utahusisha pia kufanya tafiti za pamoja kuhusu kuboresha sera na huduma zinazohudumia jamii, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, ambazo ni haki yao ya msingi.

Ziara hiyo pia iliwapa nafasi ujumbe kutoka KSG kutembelea Makao Makuu ya Chuo yaliyopo Barabara ya Bibi Titi, Kampasi ya Dar es Salaam iliyopo Magogoni, na Kituo cha Mafunzo kwa njia ya Mtandao, ambapo walijionea mazingira ya mafunzo na shughuli zinazofanywa na chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania.





Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, John Ryoba, ametoa wito kwa madiwani kutumia fursa ya Chuo cha Furahika kupeleka vijana kupata mafunzo ya ufundi bure ili kuwajengea uwezo wa kujiajiri na kujikwamua kiuchumi.

Akizungumza katika mahafali ya wahitimu wa chuo hicho yaliyofanyika mwishoni mwa wiki, Ryoba alisema taasisi hiyo imekuwa mkombozi kwa vijana wengi waliokatisha masomo au kuishia kidato cha nne kutokana na changamoto mbalimbali.
Alisema mafunzo yanayotolewa chuoni hapo yanawawezesha vijana kupata ujuzi wa fani mbalimbali unaohitajika katika soko la ajira, huku akihimiza viongozi kuwabaini vijana wenye uhitaji na kuwapeleka chuoni hapo.

“Hiki ni chuo cha kipekee kinachotoa mafunzo bure, hivyo nawatoa wito madiwani wa Dar es Salaam na nchi nzima kuhakikisha wanawafikia vijana wenye mazingira magumu wapate elimu ya ufundi. Mimi katika Kata ya Kinyerezi nitaanza na wanafunzi 30,” alisema Ryoba.

Aidha, alisema juhudi hizo zinaunga mkono azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuwezesha vijana kupata elimu na ujuzi wa vitendo unaowawezesha kujitegemea.

Katika hatua nyingine, Ryoba alitangaza kutoa ajira kwa mwanafunzi mmoja aliyefanya vizuri pamoja na kumlipia ada mwanafunzi mwingine ili kuendeleza masomo yake. Pia aliwahimiza wahitimu kuendelea kujifunza ili kufikia malengo makubwa maishani.
Naye mwakilishi wa Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mirambo Shabani, alisema chuo hicho kinatoa mchango mkubwa katika kuwajengea vijana uwezo wa kujitegemea, huku Kaimu Mkuu wa chuo, Dkt. David Msuya, akiwataka wahitimu kuepuka tabia zisizofaa na kujikita katika kazi ili kufanikisha ndoto zao.

 

Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda akizingumza katika hafla ya kuwaaga wakufunzi 25 wa VETA kwenda Nchini Finland kujifunza ujuzi wa Teknolojia zinazohitajika katika uchimbaji na ukuzaji mnyororo wa thamani wa Madini iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Serikali imeendelea kuimarisha juhudi za kukuza ujuzi wa kisasa katika sekta ya madini baada ya wakufunzi 25 kutoka VETA kuagwa rasmi kuelekea nchini Finland kwa ajili ya mafunzo maalumu ya ufundi stadi katika sekta hiyo.

Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wakufunzi hao, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Adolf Mkenda, alisema mpango huo unalenga kuongeza idadi ya wataalamu wenye ujuzi wa kisasa watakaosaidia kuinua sekta ya madini na kutoa fursa zaidi za ajira kwa vijana nchini.
Alisisitiza kuwa wakufunzi hao wanapaswa kutumia ipasavyo fursa hiyo ili kurejea na maarifa mapya yatakayosaidia kuboresha shughuli za uchimbaji, kuongeza thamani ya madini na kuimarisha ushindani wa bidhaa za madini za Tanzania katika soko la kimataifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Anthony Kasore, alisema mafunzo hayo ni sehemu ya mradi wa kimkakati unaotarajiwa kuwafikia zaidi ya Watanzania 400, hususan wanaojihusisha na uchimbaji madini, huku ukitoa kipaumbele kwa wanawake na makundi maalum.

Naye Katibu Mtendaji wa NACTVET, Mwajuma Lingwanda, alisema mradi huo utaongeza ubora wa mafunzo ya ufundi stadi na kusaidia kuzalisha wataalamu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Baadhi ya matukio katika hafla ya kuwaaga wakufunzi 25 wa VETA kwenda Nchini Finland kujifunza ujuzi wa Teknolojia zinazohitajika katika uchimbaji na ukuzaji mnyororo wa thamani wa Madini iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
---
Aidha, mwakilishi wa Wizara ya Madini, Zephaniah Henry, alibainisha kuwa bado kuna upungufu wa wataalamu katika sekta ya uchimbaji madini, hivyo mafunzo hayo yatasaidia kuziba pengo hilo kwa kuongeza wataalamu wenye ujuzi wa kisasa.

Wakufunzi hao wanatarajiwa kupata mafunzo katika maeneo mbalimbali ikiwemo uchimbaji wa kisasa wa madini (digital mining), usalama na afya migodini, utunzaji wa mazingira pamoja na matumizi ya mitambo ya kisasa.
Akizungumza kwa niaba ya wakufunzi, Neema Lyimo kutoka VETA Dodoma alisema wamejipanga kuhakikisha ujuzi watakaoupata unasaidia kuimarisha sekta ya madini na kuwainua vijana kiuchumi kupitia ajira na ujasiriamali.
Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda akiwa katika ya pamoja na wakufunzi 25 wa VETA wanaoenda Nchini Finland kujifunza ujuzi wa Teknolojia zinazohitajika katika uchimbaji na ukuzaji mnyororo wa thamani wa Madini iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Dar es Salaam - Mei 4, 2026

Hati ya makubaliano ya mashirikiano ya kuwajengea uwezo watumishi wa umma wa  Tanzania na Kenya  imesainiwa kati ya Dkt. Ernest Francis Mabonesho, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, na Prof. Nura Mohamed, Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Serikali Kenya (Kenya School of Government), mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto.

Hafla hiyo imefanyika  Ikulu, Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 4 Mei 2026.
Makubaliano haya yanatarajiwa kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya utumishi wa umma kwa kuimarisha mafunzo na ufanisi wa watumishi wa umma pamoja na kupanua ushirikiano wa kiutendaji kati ya nchi mbili.

Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakiwa katika ushiriki wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.
Bw. Mussa Lugembe, Mkurugenzi wa Kampasi ya Dar es Salaam, akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kwa niaba ya Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu.

Na Mwandishi Wetu.

Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakiwemo wa makao makuu na Kampasi ya Dar es Salaam, wameungana na wafanyakazi wengine kushiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ 2026 yaliyofanyika kimkoa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Grounds, jijini Dar es Salaam.

Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, sekta binafsi pamoja na mashirika ya umma, yakilenga kutambua mchango wa wafanyakazi katika maendeleo ya taifa na kujadili masuala ya ustawi wao mahali pa kazi.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye alitoa wito kwa wafanyakazi wote nchini kuzingatia uadilifu, uwajibikaji na nidhamu kazini ili kulinda taswira ya serikali.

Akizungumza mbele ya mamia ya wafanyakazi waliojitokeza kusherehekea siku hiyo, Chalamila alisema kuwa wafanyakazi ndio sura halisi ya serikali kwa wananchi, hivyo wanapaswa kutambua uzito wa nafasi walizonazo katika kuhudumia jamii.

“Tunaposherehekea siku hii muhimu, ni vyema tukatambua kuwa mfanyakazi mmoja anaweza kufanya serikali ipendwe au ichukiwe. Hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kufanya kazi kwa uaminifu, bidii na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma,” alisema Chalamila.

Aliongeza kuwa serikali inaendelea kuthamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuboresha mazingira ya kazi pamoja na maslahi yao ili kuongeza tija na ufanisi katika utoaji huduma kwa wananchi.

Kwa upande wao, watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania walieleza kuwa ushiriki wao katika maadhimisho hayo ni sehemu ya kuonesha mshikamano na wafanyakazi wengine nchini pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha utumishi wa umma.

Maadhimisho ya Mei Mosi hufanyika kila mwaka duniani kote, yakilenga kuenzi mchango wa wafanyakazi na kuhamasisha haki, usawa na ustawi wao katika maeneo ya kazi.