




Mfumo huo umeundwa mahususi kusaidia ufundishaji na ujifunzaji wa masomo yote kwa kuzingatia mtaala wa taifa, huku ukimwezesha mwalimu kufundisha wanafunzi waliopo maeneo mbalimbali nchini kwa wakati mmoja. Lengo ni kuunganisha shule, walimu na wanafunzi kwa kutumia zana za kidijitali ili kuongeza ubora wa elimu na kuifanya ipatikane kwa usawa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa RAOMA Foundation, Rahma Abdallah, alisema ushirikiano wao na Vodacom unalenga kuhakikisha teknolojia inasaidia kutimiza ndoto za wanafunzi na kuboresha mazingira ya ujifunzaji.
Aliongeza kuwa taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na serikali, wadau wa maendeleo na sekta binafsi ili mfumo huo ufike katika shule nyingi zaidi na kuchochea elimu jumuishi.
Katika ziara hiyo, Mhe. Ulega alipata fursa ya kumsalimia na kufanya mazungumzo ya kina na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Anangisye, ambapo walijadili kwa kina masuala ya maendeleo ya taifa hususan katika sekta ya ujenzi, uhandisi, pamoja na fursa zilizopo kwa wahandisi wazawa vijana.
Akizungumza baada ya mazungumzo hayo, Waziri Ulega alisema Profesa Anangisye alimkaribisha kushirikiana kwa karibu na chuo hicho kwa kutumia wataalamu waliopo, wakiwemo wakufunzi na wanafunzi, katika kutoa mapendekezo ya kitaalamu yatakayosaidia kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo zinazolikabili taifa.Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
KAMISHNA wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa (Pichani) amesema uwekezaji katika elimu ya awali ni msingi muhimu wa kujenga rasilimali watu bora kwa maendeleo ya Taifa, akibainisha kuwa changamoto kubwa iliyopo nchini ni uelewa mdogo wa jamii kuhusu mahitaji halisi ya mtoto katika umri wa awali.
Akizungumza kuhusu maendeleo ya elimu ya awali nchini, Dkt. Mtahabwa alisema uzoefu wake wa muda mrefu katika taaluma hiyo umeonesha wazi kuwa hatua za mwanzo za maisha ya mtoto, hususan kuanzia miaka sifuri hadi nane, zina mchango mkubwa katika kumjenga mtoto ambaye baadaye anakuwa rasilimali yenye tija kwa Taifa.
“Nimezeekea katika taaluma ya elimu ya awali na nina Shahada ya Tatu katika fani hiyo. Changamoto kubwa ninayoiona hapa Tanzania, hasa kwa watoto wa elimu ya awali, Darasa la Kwanza na la Pili, ni jamii kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu kile ambacho mtoto anatakiwa kupewa ili baadae awe na faida kubwa kwa Taifa,” alisema Dkt. Mtahabwa.
Alifafanua kuwa utu uzima wa mtu ni matokeo ya malezi, mazingira na elimu aliyopitia akiwa mtoto mdogo, akisisitiza kuwa umri wa miaka 0 hadi 8 ni kipindi nyeti kinachohitaji uangalizi, malezi sahihi na uwekezaji wa makusudi.
Dkt. Mtahabwa alieleza kuwa jitihada za Serikali za kujenga rasilimali watu bora haziwezi kufanikiwa endapo jamii haitatambua umuhimu wa kuwekeza ipasavyo katika maendeleo ya watoto wachanga. Alisisitiza kuwa elimu ya awali si suala la hiari, bali ni nguzo muhimu ya maendeleo ya Taifa kwa muda mrefu.
Aidha, aliitaka jamii kushirikiana na Serikali na wadau wa elimu kuhakikisha watoto wanapata mazingira bora ya kujifunza, malezi yenye upendo, lishe bora, afya njema na misingi imara ya maadili tangu wakiwa wadogo.
Alimalizia kwa kusisitiza kuwa dhana ya kujenga rasilimali watu bora inaanza na kujenga rasilimali watoto bora, akihimiza uwekezaji wa dhati katika elimu ya awali kama mkakati wa uhakika wa maendeleo endelevu ya Taifa.
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) leo Januari 31, 2026 jijini Dar es Salaam limetangaza matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne uliofanyika Novemba 17, 2025, yakionyesha kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kwa asilimia 2.61 na kufikia asilimia 94.98, hatua inayodhihirisha maboresho katika sekta ya elimu ya sekondari nchini.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said Mohamed, amesema jumla ya watahiniwa 595,810 walisajiliwa kufanya mtihani huo, wakiwemo wasichana 318,910 sawa na asilimia 53.53 na wavulana 276,900 sawa na asilimia 46.47. Kati yao, watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata daraja la I, II, III na IV.
Profesa Mohamed amesema ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu umeongezeka na kufikia jumla ya wanafunzi 255,404 sawa na asilimia 46.1 ya watahiniwa wote waliopata matokeo, hali inayoonesha kuimarika kwa ubora wa ufaulu ukilinganisha na mwaka uliopita.
Ameeleza kuwa jumla ya wanafunzi 569,883 walifanya mtihani huo wakiwa wamesajiliwa katika shule 5,864 nchini kote, huku watahiniwa wa kujitegemea wakiwa 25,927 waliosajiliwa katika vituo 813 vya mitihani.
Hata hivyo, NECTA imesema imefuta matokeo ya wanafunzi 77 kutokana na makosa ya kinidhamu ikiwemo kuandika lugha ya matusi katika skripti za mitihani na udanganyifu. Kati ya wanafunzi hao, 47 walitoka katika vituo vya mitihani na 30 walitoka shuleni.
Kwa mujibu wa NECTA, kati ya watahiniwa 526,620 waliofaulu, wasichana ni 278,108 sawa na asilimia 94.26 ya wasichana wote wenye matokeo, huku wavulana waliofaulu wakiwa 248,512 sawa na asilimia 95.79 ya wavulana wote wenye matokeo, jambo linaloonesha ufaulu wa juu kwa jinsia zote.
NECTA imeendelea kuwasisitiza wadau wa elimu kuimarisha maadili na nidhamu katika mitihani ya taifa, huku ikiwapongeza walimu, wazazi na wanafunzi kwa juhudi zinazoendelea kuchangia kuboresha matokeo ya elimu nchini.


Profesa Mkenda ameongeza kuwa mkakati huo unaweka mkazo katika uwajibikaji, uwazi na kuzingatia matokeo halisi ya ujifunzaji wa watoto badala ya taarifa pekee, ili kuhakikisha watoto wote wanapata stadi stahiki za kusoma, kuandika na kuhesabu mapema.
Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) unalenga kubadilisha kwa kiasi kikubwa matokeo ya ujifunzaji wa awali nchini, sambamba na mchango wa Tanzania katika utekelezaji wa Ajenda ya Afrika 2063.