Articles by "ELIMU."
Showing posts with label ELIMU.. Show all posts
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt. Tumaini Msowoya, amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Iringa kuwa makini na maisha ya chuoni kwa kujiepusha na ndoa za rejareja, makundi yasiyo na tija pamoja na tabia zinazoweza kuwavuruga kimasomo, huku akisisitiza umuhimu wa uzalendo na nidhamu binafsi.

Akizungumza wakati wa sherehe za kuwapokea wanafunzi wa mwaka wa kwanza, Dkt. Msowoya alisema licha ya wanafunzi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18 kisheria, bado wanapaswa kujiuliza iwapo ndoa au mahusiano ya kuishi pamoja ndiyo yamewaleta chuoni, au ni dhamira ya kutimiza ndoto zao za kielimu.
“Najua mna umri wa zaidi ya miaka 18 hivyo si watoto kwa mujibu wa sheria, lakini jiulizeni: je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wenu wanajua mmeoa au mmeolewa mkiwa hapa?” alihoji Dkt. Msowoya.

Aliongeza kuwa tafiti alizowahi kufanya kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu zimebaini kuwa wanafunzi wengi huishi na wenza wao kwa siri bila familia zao kufahamu, jambo alilolitaja kuwa ni hatari na linaloweza kuathiri mwenendo wa masomo na maisha ya baadaye.

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka kujiingiza katika makundi yasiyo na mwelekeo chanya, akisisitiza kuwa wasomi ndio tegemeo la maendeleo ya taifa.

Katika hafla hiyo, Dkt. Msowoya alimwakilisha Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa ambaye alikuwa mgeni rasmi. Mwipopo aliwapongeza wanafunzi hao na kuchangia shilingi milioni 2,000,000 kwa ajili ya kuwasaidia katika safari yao ya masomo.

Amesisitiza kuwa nidhamu, maamuzi sahihi na uzalendo ni misingi muhimu kwa mwanafunzi yeyote anayelenga kufanikiwa chuoni na katika maisha kwa ujumla.
Buyu, Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imedhamiria kufanya mageuzi makubwa katika sekta za elimu, sayansi, utafiti na ubunifu ili kujenga uchumi imara, shindani na endelevu, unaowanufaisha Watanzania kwa upana zaidi.

Rais Samia ameyasema hayo Januari 8, 2026, katika eneo la Buyu, visiwani Zanzibar, mara baada ya kuzindua Jengo la Taaluma na Utawala la Taasisi ya Sayansi za Bahari Zanzibar (UDSM–IMS). Amesisitiza kuwa taasisi hiyo ni mdau muhimu wa Serikali katika kukuza uchumi shirikishi, hususan uchumi wa buluu, unaotegemea rasilimali za bahari.

Amesema uwepo wa IMS utaimarisha uvuvi endelevu, utalii wa baharini, pamoja na ulinzi na matumizi bora ya rasilimali za bahari, hivyo kuchangia moja kwa moja katika kukuza pato la Taifa na ustawi wa wananchi.
Katika hotuba yake, Rais Samia ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa usimamizi mzuri wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), akisema mradi huo umeleta matokeo chanya katika miundombinu na ubora wa elimu ya juu nchini. Aidha, amewahimiza vijana kutumia fursa zilizopo kupata elimu na ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Rais pia amewapongeza viongozi na watumishi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa kukamilisha mradi huo kwa wakati na kwa viwango vya juu, huku akiishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa Mradi wa HEET.

Aidha, amewataka wahadhiri na watafiti kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi ili tafiti na bunifu zitakazofanywa ziweze kuleta matokeo ya moja kwa moja katika maendeleo ya Taifa. Vilevile, amewahimiza wanafunzi kuwa walinzi na mabalozi wa rasilimali za bahari kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amesema ameiomba Serikali kushirikiana na Benki ya Dunia ili kuanzisha Awamu ya Pili ya Mradi wa HEET, itakayowezesha kukamilisha maeneo ya utekelezaji ambayo bado hayajakamilika.

Dkt. Kikwete amesema majengo mapya yaliyozinduliwa ni msingi muhimu wa kuendeleza tafiti za kisasa, kutoa mafunzo bora na kukuza uchumi wa buluu, sambamba na kuchochea maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa William Anangisye, amesema uwekezaji huo utaongeza kwa kiasi kikubwa idadi ya wanafunzi katika Taasisi ya Sayansi za Bahari (IMS). Amesema kwa sasa IMS ina uwezo wa kudahili takribani wanafunzi 172 kwa mwaka, lakini baada ya kukamilika kwa miundombinu hiyo, uwezo utaongezeka hadi wanafunzi 472 kwa mwaka, sawa na ongezeko la wanafunzi 300.

Prof. Anangisye ameongeza kuwa IMS inaingia awamu mpya ya maendeleo kufuatia uzinduzi wa miundombinu ya kisasa katika eneo la Buyu, pamoja na kuimarishwa kwa vituo vya Mizingani na Pangani, hatua itakayoongeza uwezo wa taasisi katika kufundisha, kufanya tafiti na kuendeleza bunifu zitakazochangia maendeleo ya Taifa.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye alivunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bi. Mary Barney Isaac Laseko Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye amevunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba. Pemebni ni wazazi wake Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza hafla ya Mahafali ya 55 (Duru la Tatu) ya Chuo Kikuu hicho, na kumpongeza mhitimu aliyeng’ara kwa kuvunja rekodi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 32 katika historia ya The Law School of Tanzania.

Mhitimu huyo, Bi. Mary Barney Laseko, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria (LLB), ameweka historia kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania—rekodi ambayo mara ya mwisho ilipatikana zaidi ya miongo mitatu iliyopita chini ya Profesa Hamudi Majamba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Aidha, Mary anajiunga katika orodha ya wanawake wachache waliowahi kufanya hivyo, akifuata nyayo za Dkt. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa CCM, ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kupata daraja hilo kutoka Law School of Tanzania.

Hafla hiyo imefanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, ambapo Dkt. Kikwete amewatunuku Shahada na Stashahada wahitimu 2,452. Kati yao, 1,386 (sawa na asilimia 56.6) ni wanawake, ikionyesha mwamko na ushiriki mkubwa wa wanawake katika elimu ya juu.

Katika picha zilizopigwa na mpiga picha mkongwe Issa Michuzi, Dkt. Kikwete anaonekana akimpongeza Bi. Mary kwa mafanikio yake, huku picha nyingine zikimuonyesha akiwa na wazazi wake, Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko, waliokuwa wakijivunia mafanikio ya binti yao.

Kwa mujibu wa uongozi wa chuo, mafanikio ya Mary yamepokelewa kama ishara ya ongezeko la ubora, nidhamu na juhudi za wanafunzi wanaosomea sheria nchini.
Dodoma, Tanzania — Mr. Sanjeev Mansotra, Chairman, Planet One Group today announced the launch of the Sanjeev Mansotra Foundation (SMF) in Tanzania, marking a significant milestone in its mission to help transform education in Africa. The Foundation’s inaugural initiative will fund the renovation and expansion of four schools in Dodoma, under the aegis of the City Council.

Founded by Sanjeev Mansotra, SMF is guided by a bold vision to ensure that education and health are no longer privileges, but universal rights. The Foundation is committed to strengthening educational institutions, promoting skills development, and improving the well-being of underserved communities.“The establishment of this Foundation is rooted in my firm belief that education is the cornerstone of a thriving national economy,” said Sanjeev Mansotra. “By expanding access to quality education, we empower individuals and lay the foundation for sustainable economic growth and prosperity.”

The launch comes at a critical juncture for education in Africa. A recent report by UNESCO, UNICEF, and the African Union reveals that while school enrollment has increased by 75 million since 2015, the number of out-of-school children has surged by 13.2 million, now exceeding 100 million. As it stands, four out of five African children aged 10 cannot read and understand a simple text. The report cites rapid population growth, humanitarian crises, and a massive annual education funding gap of US$77 billion as key barriers to progress.

Rural and marginalised communities are disproportionately affected, with secondary school completion rates among rural youth up to 20 percentage points lower than their urban peers.
Recognising these challenges, SMF’s work in Dodoma will include the construction of new classrooms, science laboratories, and libraries, alongside the provision of school uniforms, stationery, clean drinking water, and health camps for students and surrounding communities. These efforts are designed to bridge the urban-rural divide and create pathways to opportunity for future generations.

“By investing in infrastructure and essential resources, we aim to inspire students and teachers alike, boost enrollment, and improve learning outcomes,” Mansotra commented. 

The Foundation’s launch in Tanzania follows a formal invitation from the City Council of Dodoma, which oversees school education in the region. Local stakeholders have welcomed the initiative, offering full support and collaboration.

Looking ahead, SMF plans to expand its philanthropic initiatives to other African nations, including Ghana, Guinea, Togo, and Sierra Leone, as well as India.

“Our long-term vision is to serve as a catalyst for transformative change. We are deeply committed to nurturing the next generation by equipping them with education, skills, and aptitude they need to thrive. From imagination to impact, our mission is to ensure no one is left behind,” Mansotra concluded.
Nchi za Nordic zimethibitisha upya dhamira yao ya kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika kuunga mkono sekta ya elimu hususan katika ngazi ya msingi, sekondari na elimu ya watu wazima (folk high schools).

Ahadi hii imekuja sio tu kama kutambua mchango mkubwa wa Kituo cha Elimu Kibaha (KEC), bali pia kutokana na uongozi imara wa Serikali ya Tanzania na juhudi zake za kuendeleza na kupanua mradi huo kwa miaka mingi.

Akizungumza jana wakati wa ziara ya mabalozi katika kituo hicho, Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Jesper Kammersgaard alisema serikali ya Tanzania imeonesha juhudi kubwa katika kulinda malengo ya msingi ya kituo hicho ambayo ni kutoa elimu jumuishi, huduma za afya na maendeleo ya jamii.

“Kituo hiki ni mfano halisi wa namna ushirikiano wa maendeleo unavyopaswa kuwa,” alisema.

“Mradi huu ulianza kama ushirikiano wa pamoja wa nchi za Nordic na baadaye kukabidhiwa rasmi kwa serikali ya Tanzania mwaka 1970. Ni jambo la faraja kuona bado unaendelea na kutoa elimu bora, huduma za afya na mafunzo ya ufundi,” aliongeza.

Balozi wa Finland, Teresa Zitting, pia alisifu uimara wa kituo hicho na uongozi wa Tanzania katika kukiendeleza.

“Ni jambo la kuhamasisha kuona mradi ulioanza zaidi ya miaka 60 iliyopita bado unaendelea kwa mafanikio,” alisema.

Serikali pia iliulizwa kama kuna mpango wa kukifanya kituo hicho kuwa chuo kikuu, ikizingatiwa kuwa kina zaidi ya hekta 1,300 za ardhi.

Hata hivyo, Balozi wa Sweden, Charlotta Ozaki Macias alifafanua kuwa kwa sasa mkazo wa ushirikiano wa Nordic upo katika elimu msingi.

“Kwa sasa hakuna mpango wa kujenga chuo kikuu hapa, Tanzania tayari ina vyuo vingi vizuri,” alisema.

“Lengo letu kubwa ni kuendelea kuunga mkono elimu ya msingi, sekondari na elimu ya watu wazima kupitia ushirikiano na Serikali ya Tanzania na mashirika kama Global Partnership for Education.”

Balozi wa Norway, Tone Tinnes, alisema ziara hiyo ilikuwa kama kurudi kwenye mizizi ya ushirikiano wa kihistoria kati ya Nordic na Tanzania.

“Zaidi ya miaka 60 baadaye, bado tuko hapa tukishirikiana. Hii inatupa nguvu mpya na mwelekeo wa kuendelea kushirikiana kwa muda mrefu,” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo hicho, Robert Shilingi aliwashukuru mabalozi kwa ziara yao na kupongeza serikali ya Tanzania kwa kuendelea kukilea kituo hicho.

“Tumeendelea kutoa huduma bora za elimu, afya na maendeleo ya jamii kutokana na ushirikiano wa serikali yetu na wadau,” alisema.

Alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika elimu na taasisi za maendeleo ya taifa.
“Kituo hiki kitaendelea kuwa mfano wa mafanikio ya ushirikiano wa muda mrefu na wenye malengo ya pamoja,” alihitimisha.











































KATIKA kuhakikisha mafunzo ya darasani yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amekutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, kwa mazungumzo ya namna ya kuwawezesha vijana wahitimu kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi.

Mkutano huo umefanyika katika ofisi za ATE jijini Dar es Salaam, ambapo Prof. Nombo alisema Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na kuboresha mitaala ya ngazi zote ili vijana wapate ujuzi unaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Aidha, Prof. Nombo alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa walimu walioko kazini ili kuboresha mbinu za ufundishaji, akieleza kuwa ufundishaji bora ndio msingi wa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa maisha na ajira.

“Lengo la ziara hii ni kujadiliana na ATE kuhusu njia bora za kuwashirikisha waajiri katika kusaidia vijana waliopo vyuoni au waliomaliza masomo kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi,” alisema Prof. Nombo.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, alisema ATE imekuwa ikisaidia wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo kupitia wanachama wake, wakiwemo viwanda na makampuni. Alitolea mfano wa Mradi wa Kukuza Ujuzi wa Vijana unaotekelezwa na ATE, uliowawezesha zaidi ya vijana 1,000 waliomaliza kidato cha nne kupata mafunzo ya miezi sita katika vyuo vya ufundi kabla ya kupelekwa makampuni kwa mafunzo ya vitendo, ambapo baadhi yao walipata ajira.

Aidha, alitoa wito kwa Watanzania kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kujifunza ujuzi kwa gharama nafuu bila kujali kiwango cha elimu rasmi walichonacho.

Mazungumzo hayo yameonesha dhamira ya pamoja ya Serikali na sekta binafsi katika kuimarisha ujuzi wa vijana na kuandaa nguvu kazi yenye mchango katika maendeleo ya taifa.
Arusha, 6 Septemba 2025: Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) wamezindua rasmi awamu ya pili ya programu ya Learning for Life katika Tawi la NCT Arusha. Wakitanua ushirikiano ulioanzishwa jijini Dar es Salaam tangu Septemba 2024. Katika udahili huu wa Arusha, zaidi ya vijana 150 wataandikishwa na kupata mafunzo ya vitendo yanayolenga moja kwa moja ajira katika hoteli za kifahari na kawaida, migahawa na baa za kanda ya utalii ya kaskazini.

Awamu hii inakuja baada ya mafanikio ya kundi la kwanza lililoandikishwa Dar es Salaam ambapo wanafunzi 100 walihitimu mwezi Mei 2025. Utekelezaji huu wa Arusha umebuniwa ili kuwa wa kudumu na wenye tija, ambapo SBL imewekeza katika mfumo wa kuwafundisha wakufunzi (ToT) kwa wakufunzi wa NCT, hatua itakayokiwezesha chuo hicho kuendesha makundi yajayo kwa uhuru na uimara. Hii inahakikisha upatikanaji wa uhakika wa vijana wenye ujuzi wa kazi kwa sekta ya ukarimu na utalii, sekta muhimu katika kukuza uchumi wa taifa.

Programu hii inachanganya darasa la nadharia na mafunzo ya vitendo kupitia eneo la kazi. Wanafunzi pia watanufaika na maudhui kutoka Diageo Bar Academy kuhusu uendeshaji wa baa, uandaaji wa vinywaji na huduma kwa wateja, sambamba na stadi muhimu za maisha kama vile mawasiliano, kujenga taswira ya kitaaluma na uongozi. Matokeo yake ni kundi la vijana waliokamilika kitaaluma na kijamii, tayari kuinua viwango vya huduma na kuboresha uzoefu kwa wageni kuanzia siku ya kwanza ya ajira zao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Florian Mtey, aliongelea athari chanya za programu hiyo akisema:

"Programu hii imefungua milango mipya kwa wanafunzi wetu. Inawapa zaidi ya nadharia darasani kwa kuwapeleka kwenye mazingira halisi ya kazi, jambo linaloongeza kujiamini na kuwapa uwezo wa kukidhi matarajio ya waajiri katika sekta ya ukarimu na utalii. Tunajivunia kuendeleza ushirikiano huu na SBL hapa Arusha."

Aidha, NCT inatangaza kwamba mafunzo ya muda mfupi chini ya programu ya Learning for Life yanatarajiwa kuanza tarehe 22 Septemba 2025 na kuhitimishwa tarehe 02 Novemba 2025. Gharama zote za mafunzo haya zitagharamiwa na Serengeti Breweries Limited (SBL), huku wanafunzi wakigharamikia malazi, chakula na usafiri.

Waombaji wanatakiwa kutuma fomu za maombi kabla ya tarehe 16 Agosti 2025. Fomu za maombi zinapatikana kupitia tovuti ya Chuo: www.nct.ac.tz au katika ofisi za kampasi za NCT zilizopo Dar es Salaam, Arusha na Mwanza.

Sifa za mwombaji:

Awe Mtanzania.

Awe na barua ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji au kutoka kwa mwajiri.

Awe na umri kati ya miaka 15 – 35.

Awe mwenye afya njema.

Awe na elimu ya Cheti au zaidi katika fani ya Ukarimu na Utalii.

Naye Mkurugenzi wa Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bw. Christopher Gitau, aliongeza:

"Sisi kama SBL tunaamini kwamba kuwekeza kwa vijana ni kuwekeza kwenye mustakabali wa jamii zetu. Kupitia Learning for Life tunawapa stadi za kiufundi lakini pia tunawajengea uwezo wa kuwa viongozi, wajasiriamali na wachangiaji wakuu wa ukuaji wa sekta ya ukarimu na utalii nchini."

Programu ya Learning for Life ni sehemu ya ajenda ya kijamii ya SBL, Spirit of Progress, ikidhihirisha dhamira yake ya muda mrefu ya kuwekeza kwa jamii, kujenga uwezo na kuwawezesha vijana wa Kitanzania. Kupitia upanuzi huu Arusha, programu hii itatoa njia mpya za ajira na kuimarisha zaidi sekta ya utalii na ukarimu nchini Tanzania.