Articles by "AJALI"
Showing posts with label AJALI. Show all posts

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Uboreshaji wa Daftari utafanyika Mkoa wa Tanga kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza sambamba na Mkoa wa Pwani kuanzia Februari 13 hadi 19,2025 ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.


Akizungumza na Maafisa hao Mhe. Jaji Mwambegele aliwasisitiza kutambua umuhimu wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kitaifa na kuwahimiza pia kushirikiana na wadau wa Uchaguzi wakiwepo Vyama vya Siasa alivyovitaka vihakikishe vinateua mawakala katika kila kituo ili waweze kusaidia kuwatambua wananchi kutoka maeneo husika.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo tarehe 07 Februari, 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira, amewataka watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ngazi Kata, kuwa waadilifu wakati wote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Mhe.Rwebangira ametoa maelekezo hayo leo Februari 07, 2025, alipotembelea mafunzo kwa watendaji hao katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, unaotarajiwa kuanza Februari 13, 2025 hadi Februari 19, 2025, katika mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.


Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Pwani na Tanga katika Halmashauri za Wilaya Lushoto, Kilindi, Muheza, Korogwe, Mji wa Korogwe, Mji wa Handeni na Jiji la Tanga unatarajia kuanzia tarehe 13 Februari hadi 19 Februari, 2025 na vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 Asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni kwa muda wa siku Saba.




Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Jiji la Tanga , Mwanaidi Nondo, akiwa katika mafunzo hayo.




Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.










Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.





Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele ametembelea na kukagua mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo wa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga katika siku ya pili na ya mwisho ya mafunzo yao leo Februari 7,2025.


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Asina Omari, leo Februari 07 , 2025 ametembelea mafunzo ya Maafisa Uandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mwinyi, uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ikiwa ni siku ya pili ya Mafunzo hayo.




Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira akitembelea mafunzo kwa mafunzo ya vitendo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo katika Hamashauri ya Wilauya ya Handeni mkoani Tanga,leo Februari 07, 2025, ambapo pia amewasisitiza kuzingatia mafunzo hayo, ili wakaweze kutekeleza majukumu hayo kwa ufanisi.



Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe.Dkt. Zakia Mohamed Abubakar akitembelea mafunzo ya kwa vitendo ya Maafisa Uandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia mkoani Pwani ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua eneo la maafa ya ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua eneo la maafa ya ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwajulia hali na kuwapa pole majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo ambao wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Novemba, 2024.

Na Mwandishi Wetu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya ziara katika eneo la Kariakoo, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 20, 2024, mara baada ya kurejea kutoka Brazil. Ziara hiyo ililenga kukagua shughuli za uokoaji kufuatia ajali ya kuporomoka kwa jengo lililosababisha maafa makubwa.

Akizungumza na wananchi baada ya ukaguzi, Rais Samia alithibitisha kuwa watu 20 wamepoteza maisha kutokana na ajali hiyo.

“Jitihada kubwa katika tukio hili zililenga kuwaokoa wenzetu waliokuwa wamekwama ndani ya jengo hilo wakiwa hai, lakini jitihada hizi haziondoshi kudra ya Mungu. Pamoja na juhudi zilizofanywa, tumepoteza wenzetu, na hadi sasa idadi yao ni 20,” alisema Rais Samia.

Aidha, alieleza kuwa miili ya marehemu hao tayari imeshazikwa kwa ushirikiano wa familia na serikali.

Rais Samia alibainisha kuwa ajali hiyo ni pigo kubwa kwa taifa, kwa kupoteza nguvu kazi muhimu, na kwa familia zilizopoteza wapendwa wao.

Kwa lengo la kuzuia matukio kama haya siku zijazo, Rais Samia alisema akiwa nchini Brazil alimwagiza Waziri Mkuu kuunda tume ya watu 20 ili kufanya ukaguzi wa majengo yote katika eneo la Kariakoo.

“Naambiwa tume hiyo tayari imeundwa. Baada ya kukamilisha kazi yao, tutazingatia mapendekezo yao. Kama wataelekeza kwamba majengo yaliyo chini ya kiwango yabomolewe, hatutasita kuchukua hatua hiyo,” alisisitiza Rais Samia.

Mbali na vifo vilivyoripotiwa, idadi ya majeruhi wa tukio hilo bado inaendelea kufanyiwa tathmini. Timu za uokoaji, zikiwemo vikosi vya zimamoto, polisi, na wanajamii wa kujitolea, zimekuwa zikifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha usalama wa manusura na kurejesha hali ya kawaida katika eneo hilo.

Wakazi wa Kariakoo na maeneo jirani wamehimizwa kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa zozote zitakazosaidia uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (katikati mbele) akiwasili mkoani Njombe kwa ajili ya kutoa elimu na uhamasishaji juu ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Septemba 21,2024. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Kasongwa na kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Mhe. Olivanus Thomas.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme akivalishwa skafu na skauti mkoani Njombe mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya kutoa elimu na uhamasishaji juu ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Septemba 21,2024.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme akitoa elimu na uhamasishaji juu ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia mkoani Njombe Septemba 21,2024 ambapo mikoa mingine iliyonufaika na elimu hiyo ni pamoja na Katavi, Rukwa, Songwe na Mbeya.
Kamishina kutoka Wizara ya Nishati Bw. Styden Rwebangira akitoa elimu na uhamasishaji juu ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia mkoani Njombe, Septemba 21,2024.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme amekamilisha ziara yake ya mkoa mitano ambayo alikuwa akitoa elimu pamoja na kuhamisha wananchi juu ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Akiwa mkoani Njombe Septemba 21, 2024 Bi. Mndeme amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kutokana na mijadala, maswali na ushauri ambao wananchi walikuwa wakichangia kila siku baada ya uwasilishwaji wa maada mbalimbali.

Amesema baada ya kumaliza Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya na Njombe bado elimu itaendelea kutolewa sababu inahitajika zaidi ili kuhakikisha lengo la Serikali lililowekwa la kuhakikisha hadi mwaka 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia.

“Katika ziara hii tumegundua vitu vingi ikiwemo watu bado wanaamini Nishati Safi ni gharama kuitumia hasa taaasisi zile zinazolisha watu zaidi ya 100 wakihofia ufungaji wa mitambo.

“Hata hivyo hawaangalii athari zake ambazo zinatokana na matumizi ya nishati isiyokuwa salama, wengi wanaangalia unafuu wa upatikanaji wa nishati lakini hayo yote tumeyaona na yanafanyiwa kazi,” amesema Bi. Mndeme.

Kwa upande wake, Kamishina kutoka Wizara ya Nishati Bw. Styden Rwebangira ameeleza kuwa kila mmoja anapaswa kuliangalia jambo hili kwa kuijali afya yake na jamii inayomzunguka kwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia.

Naye, Naibu katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Bi. Felista Mdemu amesema jamii imeanza kuelewa taratibu umuhimu wa kutumia Nishati Safi ya kupikia japo elimu inapaswa kutolewa zaidi.
Tume ya Ushindani (FCC), imeendelea kutumia fursa ya Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) kwa kutoa elimu kwa Umma ambao ndio walaji au watumiaji wa bidhaa na huduma.

Wananchi mbalimbali wameendelea kujitokeza na kutembelea banda la FCC ambapo wamenufaika kwa kupata elimu zaidi inayohusu masuala ya Ushindani, Udhibiti wa Bidhaa Bandia na Kumlinda Mlaji kutoka kwa wafanyakazi wa FCC.

Maonesho haya yaliyoanza tarehe 28 Juni na kufunguliwa rasmi tarehe 3 Julai, 2024 yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai, 2024.









Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele (wapili kulia) na Mjumbe wa Tume, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wakishuhudia ufunguzi wa kituo cha kupigia kura No 1 katika Skuli ya Sebleni Jimbo la Kwahani Mkoa wa Mjini Mgaharibi leo tarehe 08 Juni,2024 ambapo wananchi wa jimbo hilo wanapiga kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo kumchagua Mbunge wao.
Wananchi wa jimbo la Kwahani wakihakiki majina yao kabla ya kwenda kupiga kura. 
Msimsmizi wa Kituo No. 1 Shehiya ya Sebleni kilichopo katika Skuli ya Sebleni akifunga sanduku la kura kabla ya kuzanza zoezi la Uchaguzi.  
Mpiga Kura akiandaliwa karatasi ya Kura tayari kwa Kupiga Kura 

Mkazi wa Shehiya ya Sebleni akipiga Kura leo Juni 8, 2024 kumchagua Mbunge wa Jimbo hilo. 

Wapiga Kura wakiwa katika mstari katika moja ya vituo vya Kupiga Kura Jimbo la Kwahani.
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele ameshuhudia wananchi wa Jimbo la Kwahani Mkoa wa Mjini Magharibi wakipiga kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo kumchagua Mbunge wao.
 
Jaji Mwambegele aliambatana na Mjumbe wa Tume hiyo, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar ambapo walitembelea vituo hivyo vya kupigia kura na kushuhudia ufunguaji wa vituo  saa moja kamili asubuhi.
 
Akizungumza baada ya kutembelea vituo vya kupigia kura katika Skuli ya Sebleni, Uwanja wa Negro na Kariakoo, Jaji Mwambegele alisema zoezi linakwenda vizuri na wao walishuhudia vituo vikifunguliwa kwa wakati na wananchi kupiga kura.
 
Aidha, amesema vyama vya siasa vimeweka mawakala wakutosha katika katika vituo vyote vya kupigia kura walivyotembelea.
 
“Tumeshuhudia ufunguzi wa vituo na upigaji kura, vituo vimefunguliwa kwa wakati na wananchi wamejitokeza kwa wingi kuja kutumia haki yao ya kupiga kura pia vyama vya siasa vimeweka mawakala wakutosha katika vituo hivyo,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Jaji Mwambegele amesema wananchi wa Jimbo la Kwahani wameonesha mwitikio mkubwa kwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kuchagua kiongozi wanayemtaka.
 
Vyama 14 vimesimamisha wagombea katika Uchaguzi huo mdogo wa kiti cha Ubunge jimbo la Kwahani ambapo majina yao na vyama katika Mabano ni Bw.  Bashir Yatabu Said (Demokrasia Makaini), Bi. Nuru Abdulla Shamte (DP), Bi. Mwanakombo Hamad Hassan (NLD), Bi. Zainab Maulid Abdallah (CCK), Bi. Tatu Omary Mungi (UPDP), Bw. Khamis Yussuuf Mussa (CCM) na Bi. Jarade Ased Khamis (AAFP).
 
Wengine ni  Bw. Kombo Ali Juma (NRA), Bi. Shara Amran Khamis (ADC), Bi. Naima Salum Hamad (UDP), Bi. Madina Mwalim Hamad (ADA TADEA), Bw. Amour Haji Ali (SAU), Bi. Mashavu Alawi Haji (UMD) na Bw. Abdi Khamis Ramadhan (CUF).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akisalimia mawakala wa vyama waliokua katika Kituo cha Kupigia Kura.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele na Mjumbe wa Tume, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wakiangalia vituo vya wazi vya kupigia kura 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele akiangalia vituo vya wazi vya kupigia kura 
Karani Muongozaji akihakiki jina la Mpiga Kura kabla ya kumruhusu kwenda Kupiga Kura.
Waangalizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kwahani wakishuhudia wananchi wa Jimbo la Kwahani wakipiga Kura leo.