Articles by "MICHEZO"
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Kumekuwa na taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusiana na Timu ya Tabora United zikimuhusisha Kocha Mkuu Denis Laurence pamoja na msaidizi wake Masoud Juma kuwa wanataka kuondoka kwa kile kinachoelezwa hawajaridhishwa na mazingira lakini pia hawajasainishwa mikataba yao ya kazi.

Kwanza kabisa Klabu inapinga vikali upotoshwaji wa taarifa hizi kwa baadhi ya watu ambao hawanania njema na Timu ya Tabora United. Ikumbukwe kuwa Tabora United inaongozwa na viongozi ambao wanatambua na kufahamu umuhimu wa mfanyakazi kwa kila idara.

Tukianza na suala la Kocha Mkuu Denis Laurence ni kwamba kabla ya kuwasili kwa Kocha Laurence akiwa Ufaransa amekuwa akiifuatilia Timu ya Tabora United kupitia video za mechi mbalimbali lakini pia anaifahamu Timu kutokana na mazungumzo ambayo yalikuwa fakifanyika baina yake na viongozi wa klabu.

Lakini pia Kocha Laurence amewahi kufanya kazi na Msaidizi wake ambaye wanafanya kazi pamoja ndani ya Tabora United Masoud Juma na ndiye aliyempendeza hivyo hata suala la mazingira tafsiri yake ni kwamba analifahamu kwa kuwa anaifahamu vyema Timu ya Tabora United.

Kuhusu mikataba kwa hali ya kawaida hakuna mtumishi yoyote ambaye anaweza kuanza kufanya kazi pasipo kusainishwa mkataba wake hicho kitu hakiwezekani na hakijawahi kutokea tangu Dunia imeumbwa.

Kocha Laurence pamoja na Msaidizi wake Masoud walipewa mkataba na kusaini kulingana na taratibu za kazi zinavyotaka na ndio mana waliweza kuanza kazi mara moja na hadi sasa wanaendelea na majukumu yao kama kawaida ikiwa ni siku ya sita tangu walipotambulishwa.

Na hili jambo linafahamika kabisa kuwa mtu anapoanza kufanya kazi maana yake ni kwamba tayari walishakubalina na mwajiri hivyo kusema Kocha Mkuu na msaidizi wake wanaweza kuacha kazi hizo ni taarifa za uzushi na uongo na tunaomba mzipuuze.

Kuhusu mishahara ya wachezaji, viongozi pamoja na Benchi la ufundi, hakuna ambaye anadai hadi sasa na kwamba mara nyingi uongozi umekuwa ukijali masilahi ya watumishi wa idara zote kwa kuhaikisha kuwa stahiki zao wanalipwa kwa wakati.

Uongozi wa Tabora United umekuwa ukifanya mrejesho wa matumizi ya fedha zinazotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania TPLB kupitia kwa mzamini Mkuu wa haki za matangazo Azam Media kila mwezi na kwamba tumekuwa tukipokea fedha hizo. Hivyo kusema kwamba Tabora United haipatiwi fedha za haki ya matangazo huo ni upotoshwaji na kutaka kutugombanisha na mamlaka husika.

Kuhusu wachezaji wa Timu ya vijana Under 20, wote waliwasili tangu juzi Tabora wakitokea Geita ambapo walikuwa na mchezo wa Ligi ya vijana hatua ya makundi hivyo wachezaji hawajakwama sehemu yoyote.

Hivyo kauli ya Klabu ni kwamba mashabiki na wadau wote wampira ambao wanaiunga mkono Timu ya Tabora United wapuuze taarifa hizo kwani zinalenga kuchafua Brandi ya Klabu kwa makusudi hivyo kama uongozi unatambua thamani na umuhimu wa kila mmoja ndani na nje ya Klabu.

Timu inaendelea kujifua kwa ajili ya michezo ya Michuano ya kombe la Azam Sports Federation ASFC dhidi ya Singida Fountaingat pamoja na Ligi ya NBC soka Tanzania Bara itakayoendelea baada ya kumalizika kwa kalenda ya FIFA.

Imetolewa leo Machi 27
Na Christina Mwagala
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Tabora United.
Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro kushoto akimkabidhi Kombe la Mashindano ya Odo Ummy Cup Nahodha wa timu ya Kiomoni FC mara baada ya kuibuka Mabingwa kwa kuifunga Nguvumali FC penati 3-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga juzi ambapo mshindi huyo alipatiwa pia kitita cha Sh Milioni 3,pikipiki ya magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mpira kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya ambaye ndie muandaaji wa Mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman
Na Oscar Assenga, TANGA

TIMU ya Kiomoni FC wametawazwa kuwa Mabingwa wapya wa Michuano ya Kombe la Odo Ummy Cup baada ya kuibamiza timu ya Nguvumali FC penati 3-1 katika mchezo wa Fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Lamore Jijini Tanga.

Kutokana na ushindi huo waliweza kujinyakulia kitita cha Sh.Milioni 3,Pikipiki yenye Magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mipira huku Mshindi pili timu ya Nguvumali FC waliweza kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 2.5 na Mpira na Jezi Seti 1.

Michuano hiyo ya Odo Ummy Cup huchezwa kila mwaka kwa kushirikisha kata zote za Jimbo la Tanga yakiwa na lengo la kuibua vipaji na kukuza kiwango cha soka kwa vijana ambao kupitia mpira wanaweza kujikwamua kiuchumi.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikitaka kuibuka na ushindi ili kuweza kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko zilitoka sare tasa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia ikiwa na hari kubwa kutokana na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ili kuweza kujiimarisha kwa lengo la kufanya vizuri katika michuano hiyo.

Wakionekana kucheza kwa umahiri mkubwa Kimoni FC walianza kwa kulishambulia lango la wapinzani wao bila kuwepo kwa mafanikio yoyote ambapo kila wachezaji walipokuwa wakipiga mashuti langoni mwao liligonga mwamba na kutoka nje.

Kutokana na ushindani wa mchezo huo ulizilazimu timu zote kutoka uwanjani dakika 90 bila kuona milango ya kila mmoja na hivyo mwamuzi wa mchezo huo kulazimika kupelekea mchezo huo kwenye mikwaju ya penati ambao ndipo kiomoni waliposhinda mabao hayo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mcheo huo wa Fainali Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni aliwapongeza waandaaji wa mashindano hayo huku akieleza kwamba mashindano ikiwemo Mbunge Ummy Mwalimu.

“Ukiona vyaelea ujue vimeundwa hili ya leo tuna kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza Mbunge wetu Ummy Mwalimu niseme kama Waziri mwenye thamana ya michezo nimeshahudhuia mashindano yanayoandaliwa na wabunge mwengi sana sijaona mashindano mazuri kama haya”Alisema

Alisema mashindano haya ni mazuri na makubwa ambayo sijapata kuyaona katika maeneo mengine na Mbunge Ummy ana sifa ya kipekee kwa kuwajali wananchi wa Jimbo lake kutokana na kuhakikisha anawapigania ili kuweza kuondoa kero zenu.

Aidha alisema wanaposema michezo ni ajira wanaamini pia ni uchumi na wao kama Wizara wamemua hivi sasa michezo ni ajira na uchumi hivyo mashindano kama hayo watashirikiana na waandaaji kuhakikisha wanaibua vipaji na kuviendeleza.

Hata hivyo alisema kwamba mkoa wa Tanga ndio chimbuka la vipaji na wao serikali wataendelea kuiangalia Tanga huku akieleza kwamba Mbunge Ummy amepeleka ombi kwao kwamba uwanja huo wa Lamore ambao umechezewa fainali hiyo upandwe nyasi uwe mzuri ili fainali za mwakani ziwe nzuri .

“Na mimi nimemuhaidi Mbunge Ummy kwamba nitawaleta wataalamu kufanya tathimini ili uwanja uweze kuwa katikaa hali nzuri kutokana na kwamba umuhimu wa mashindano hayo ya Odo Ummy Cup”Alisema

Awali akizungumza katika fainali hiyo ,Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya alisema kwamba suala la Odo Ummy Cup ni mchango wake katika kutekeleza ilani ya CCM ibara ya 243 ambayo inawataka kuwekeza kwenye mpira wa migu hasa kwa vijana.

Alisema wanamshukuru pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman kutokana na kwamba amekuwa akiwasaidia na kuwaleta na kuwaongoza kwenye kutekeleza ilani.

Aidha alisema mashindano hayo lengo ni kuwaleta pamoja vijana wa Tanga mjini na yameleta moja,mshikamano na hamasa ya kumweka karibu na vijana huku akishukuru timu zote kutoka Kata 27 ambazo zilishiriki kwenye michuano hiyo.

“Lakini pia nishukuru kamati za Siasa za CCM kwa kujitoa kusimamia mashindano hayo pamoja na timu ya Hamasa ya UVCCM pia niwashukuru wadhamini wetu kwa kuuunga mkono wakiwemo wadau wetu Assemble Insurance kwa kutuunga mkono”Alisema

Hata hivyo kwa upande wake,Mwenyeiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman atumia fursa hiyo kuwataka wabunge na madiwani wa mkoa huo wahakikisha wanaendelea michezo katika maeneo yao.

“Kwani kufanya hivyo ni kutekeleza kwa vitendo ilani ya CCM ambayo tumehaidi kuendeleza michezo hivyo lililofanyika linatafsiri ilani kwa vitendo hivyo wabunge na madiwani hakikisheni hili linatekelezwa”Alisema.




Na Oscar Assenga,TANGA.

WAZIRI wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro amepongeza Mashindano ya Oddo Ummy Cup huku akieleza kwamba watayatumia kuangalia vipaji vya wachezaji na baadae aone namna ya kumpigia simu Kocha wa timu ya Taifa ili kuona namna ya kuwapeleka kwenye Taifa ya Taifa.

Dkt Ndumbaro aliyasema hayo Machi 10 mwaka huu Jijini Tanga ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Fainali ya Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Oddo Ummy Cup ambayo yameandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kwa lengo la kuibua vipaji vya wachezaji wachanga.

Mashindano hayo hufanyika kila mwaka katika viwanja vya Lamore Jijini Tanga na yanashirikisha timu mbalimbali kutoka kwenye Jimbo la Tanga Mjini linaongozwa na Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya

“Leo nimekuja Tanga kwa lengo la kuja kuangalia viwango vya wachezaji ili baadae nimpiga simu kocha wa timu ya Taifa kuona namna nzuri ya kuweza kuwajumuisha kwenye timu zetu za Taifa”Alisema Waziri Ndumbaro.

Katika Fainali hiyo timu za Nguvumali na Kiomoni zilitinga hatua hiyo kwa kufanya vizuri kwa kila mmoja kumtoa mpinzani mwenzake na hivyo kulazimika kukutana kwenye hatua hiyo ya kumsaka Bingwa ambapo Bingwa alikuwa ni timu ya Kiomoni

“Kwa heshima ya Waziri Ummy Mwalimu nimeacha shughuli zote nimekuja Tanga mimi Waziri wa michezo ili niweze kuona vipaji vilivyopo hapa Tanga kwa maana historia ya mpira ni kubwa na nimeambiwa Juma Mgunda yupo hapa hivyo tunaweza kutumia mashindano haya kupata wachezaji wa timu ya Taifa”Alisema Waziri Ndumbaro.

Akubali Ombi la Mbunge Ummy

Katika hatua nyengine Waziri Ndumbaro amekubali ombi la Mbunge Ummy Mwalimu ambaye alimuomba atafute shule mmoja mkoani humo waifanye kuwa ya vipaji vya michezo.

Akijibu Ombi hilo Waziri Dkt Ndumbaro alisema kwamba yeye akisema wataona namna ya kwenda kulitekeleza ili uwepo wa shule hiyo uweze kupatikana mkoani Tanga.

“Mh Ummy nimepokea ombi lao wewe ukisema mimi ni utekelezaji tu hivyo nitakwenda kulifanyia kazi”Alisema.
Dar es Salaam. Tarehe 2 Novemba 2023: Benki ya CRDB kwa kushirikiana na kampuni ya Visa inayoongoza katika mfumo wa malipo ya kidigitali, imezindua kampeni yake ya ‘Tisha na Tembocard Tukakiwashe AFCON’ inayohamasisha matumizi ya kazi zake za TemboCard Visa, ambapo wateja nane watakaofanya miamala mingi zaidi watapelekwa nchini Ivory Coast kushuhudia mashindano ya TotalEnergies CAF Africa Cup of Nations (AFCON) 2024.

Kampeni hiyo ambayo ni sehemu ya juhudi zinazofanywa na Benki ya CRDB kupunguza matumizi ya fedha taslimu na kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidigitali ilizinduliwa Ijumaa jioni jijini Dar es Salaam na itadumu kwa miezi mitatu mpaka Januari mwakani.
Akiongea katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa ameipongeza Benki ya CRDB na kampuni ya Visa kwa kuanzisha kampeni hiyo aliyosema imekuja wakati muafaka ambapo sio tu itasaidia kupunguza matumizi ya fedha taslimu bali itahamasisha michezo miongoni mwa Watanzania.

“Mwaka huu timu yetu ya Taifa imefuzu kushiriki Fainali za AFCON 2024 zitakazofanyika nchini Ivory Coast, hivyo kampeni hii inatoa fursa kwa mashabiki kwenda kuishangilia. Nawapongeza sana Benki ya CRDB na kampuni ya Visa kwa kuja na kampeni hii madhubuti ambayo itatoa fursa adhimu ya watu kushuhudia fainali za AFCON,” amesema Msigwa.

Katibu Mkuu huyo amesema washindi wa kampeni hii watapata nafasi ya kwenda kushuhudia fainali ya michuano hiyo itakayohudhuriwa na mashabiki na viongozi wa michezo kutoka sehemu mbalimbali duniani watakaoenda kujionea vipaji vya vijana wa Kiafrika.


Msigwa aliongeza kwamba pamoja na kampeni ya “Tisha na TemboCard Visa Tukakiwashe AFCON” kuhamasisha michezo, pia inaunga mkono juhudi za serikali katika kukuza uchumi wa kidigitali.


"Uchumi wa kidigitali unahitaji njia mpya za malipo ambazo hazimlazimu mtu kutembea na fedha taslimu. TemboCard Visa inarahisisha malipo hayo kupitia majukwaa tofauti ya ndani hata kimataifa,” amesema.
Afisa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema "tunatambua upendo wa Watanzania walionao kwenye mpira wa miguu. Tunaamini kuwapa fursa hii ya kushuhudia fainali za AFCON 2024 kutawaongezea ladha isiyosahaulika.”

Raballa amesema washindi 8 watakaopata nafasi hiyo watachukuliwa miongoni mwa watumiaji wa TemboCard Visa watakaofanya miamala isiyopungua 30 kwa mwezi sawa na wastani wa muamala mmoja kila siku. Amesisitiza kuwa nafasi za kushinda zipo wazi kwa wateja wote zaidi ya milioni nne pamoja na wapya watakaojiunga na huduma za benki yao na kutumia TemboCard Visa kufanya malipo.

Salma Ingabire, Meneja mkazi wa Visa Tanzania amesema “kama mtoa huduma pekee wa huduma za malipo pekee wa TotalEnergies CAF AFCON, Visa tunafurahi kuingia ubia na Benki ya CRDB ili kuwatuza wateja watakaobahatika kwa kuwapa nafasi ya kushuhudia timu bora za Afrika zikicheza.
Washindi wa kampeni hii watalipiwa nauli ya safari yao ya kwenda Abidjan, malazi katika hoteli ya kifahari, tiketi za daraja la juu (VIP) za kushuhudia mchezo wa fainali, kuhudhuria matukio maalum na vingine vingi ambavyo bila shaka vitawaachia kumbukumbu isiyofutika.

Mbali na kushinda safari hiyo, wateja watakuwa na fursa ya kushinda zawadi nyingine ikiwemo seti ya sofa na vifaa vya kielektroniki mfano runinga na friji. Ili kushinda, amesema wateja wanaweza kutumia kadi zao kulipia bidhaa wanapozinunua dukani au sokoni, kwenye vituo vya mafuta, hotelini, wanaponunua tikiti au kulipia huduma.





Dar es Salaam. Tarehe 20 Agosti 2023: Katika kuhamasisha mazoezi ya kujenga mwili na kuimarisha afya, Benki ya CRDB imezindua mashidano ya Super League kwa timu zinazoundwa na wafanyakazi wake.

Michuano hiyo inayofanyika kwa mwaka wa tatu sasa, itashirikisha timu za mpira wa miguu na mpira wa pete na kufanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), inazishirikisha timu zinazoundwa na wafanyakazi kutoka idara, kanda na matawi ya benki hiyo nchi nzima.
Akifunbua michuano hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba amesema ni jambo jema kuona menejimenti inatoa fursa kwa wafanyakazi wake kufanya mazoezi ya mwili.

“Mnachokifanya Benki ya CRDB ni kitu kikubwa sana. mnatoa mfano wa kuigwa na taasisi zote. Afya ndio mtaji muhimu kwa kila mfanyakazi hivyo ni vyema kuilinda na mazoezi ndio namna ya uhakika ya kufanya hivyo. Hongereni sana Benki ya CRDB kwa kuwa na program hii,” amesema Komba.
Akimakaribisha mgeni rasmi, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo amesema mafanikio endelevu si ya kifedha pekee bali yanahusisha ustawi wa kila mmoja katika familia ya Benki ya CRDB.

“Kwa kukuza mazingira ambayo wafanyakazi wanaweka kipaumbele katika afya na furaha yao, tunaongeza ari ya uvumbuzi na ushirikiano hivyo kuimarisha utendaji wa benki kwa ujumla. Katika ulimwengu wetu wa leo, ni rahisi kusahau umuhimu wa kujijali na kudumisha usawa kati ya Maisha ya kazi na maisha ya binafsi hivyo tunappata fursa kama hii tuitumie vyema,” amesema Nsekela.

Ligi hiyo, Nsekela amesema ni mwendelezo wa mpango wa Benki ya CRDB kuimarisha afya za wafanyakazi wake na anaamini kila mfanyakazi atashiriki michuano hiyo kwa namna moja au nyingine.
Sambamba na uzinduzi wa ligi hiyo, Benki hiyo imefunga program yake ya "Ustawi, Afya na Furaha" (Wellness, Health and Fun) ambayo imefanyika kwenye kanda zake zote saba nchini kwa wafanyakazi kufanya mazoezi pamoja na kupima afya zao hasa magonjwa yasiyoambukiza.

Program hiyo iliyoenda na kaulimbiu ya "live well, work well" yaani kuishi vyema, kufanya kazi vizuri, inalenga kuhamasisha ustawi wa mwili, akili na hisia za wafanyakazi wote wa Benki ya CRDB.

“Program hii ya wellness, health and fun inadhihirisha kuwa nguvukazi yenye afya ina uzalishaji na ukuaji, na tunajivunia mafanikio ambayo tumeyapata katika kanda nyengine tulikoitekeleza program hii. Kama nilivyoeleza hapo awali, siku hii tunayoiita 'Wellness Health & Fun Day' inalenga kuhamasisha ustawi, utimilifu wa afya, na mtindo bora wa maisha kwa wafanyakazi wetu,” amesema mkurugenzi huyo.
Katika viwanja hivyo, kulikuwa na wataalamu waliofanya vipimo tofauti vya afya kikiwamo cha tezi dume, BMI na shinikizo la damu, huku wakifundisha namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo, ufanyaji wa mazoezi na ulaji salama.

“Msisitizo mkubwa tumeuweka katika afya ya akili, lengo kuu ni kuongeza uelewa wa kila mfanyakazi. Tungependa kuona kila mfanyakazi wa Benki ya CRDB anao ujuzi wa kuzitambua dalili za awali za msongo wa mawazo na hatua za kuchukua ili kuokoa jahazi lisizame iwe ni kwake mwenyewe, mwanafamilia yake hata jamii nzima,” amesisitiza Nsekela.

Licha ya vipimo na ushauri wa kitaalumu uliotolewa, wafanyakazi walishiriki mazoezi tofauti kwa lengo la kuimarisha afya huku wakiendelea kufahamiana na kukuza mahusiano baina yao.
Nshekanabo amesema kwa kuwekeza katika ustawi na afya binafsi sio tu mtu anakuwa anaboresha maisha yake bali anawahamasisha wanaomzunguka kufanya vivyo hivyo, jambo linalotoa chachu ya mafanikio kwa benki.

Licha ya kutenga siku ya mazoezi na vipimo vya afya kwa wafanyakazi wake, na kuwahamasisha kushiriki michezo, Benki ya CRDB inayo miundombinu ya kisasa ya kufanyia mazoezi (gym) kwenye ofisi zake za makao makuu ambayo mkurugenzi huyo amewataka wafanyakazi wote kuitumia kwani kila mmoja anayo ruksa ya kuingia kufanya mazoezi ili kujenga na kuimarisha afya yake.

Wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiwa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhitimisha program ya "Ustawi, Afya na Furaha" (Wellness, Health and Fun) Kanda ya Mashariki iliyofanyika kabla ya uzinduzi wa Super League.
Wakati maelfu ya Watanzania kutoka kila pembe ya nchi wakiacha shughuli zao na kuelekea Lupaso kushuhudia ‘Wenye Nchi,’ Klabu ya Simba ikiukaribisha msimu mpya kwa tamasha lililofana, kikosi cha timu ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB jana kiling’ara kwenye tamasha la Simba Day baada ya kuwanyamazisha wapinzani wao, Benki ya NMB kwa ushindi wa bao 1-0.

Kwenye tamasha hilo ambalo Simba iliendeleza utamaduni wake wa kuujaza uwanja kwa mashabiki wenye ari kubwa ya kuishangilia, walipata burudani murua kutoka kwa maofisa wa benki hizo mbili kubwa zaidi nchini walioziacha suti zao na kutupia bukta na fulana na kukiwasha mbele ya wapenda soka 60,000 walioujaza Uwanja wa Taifa almaarufu kama Uwanja wa Benjamini Mkapa au Lupaso jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kupata ushindi huo, Kapteni wa Timu ya Benki ya CRDB, Nicodemus Milinga amesema ilikuwa ni lazima washinde kwani walijiandaa vilivyo.

“Kujituma na kufuata maelekezo ya kocha. Wote tulikuwa na ari ya juu ya kuipigania brand (nembo) kama vile tunavyotoa huduma bora kwa wateja wetu kila siku, ndani na nje ya nchi,” amesema Milinga.

Twaha Beimbaya, kocha aliyejifunzia Uingereza na akaja akachukua kombe la U17 na JKT Tanzania mwaka 2021 halafu akaisaidia Pan Africa isishuke daraja la kwanza mwaka jana anayeinoa timu ya Benki ya CRDB, anasema uzoefu walioupata kwa kushiriki michuano ya Sikukuu ya Mei Mosi walikomenyana na vikosi vigumu vya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, umewaongezea kujiamini wachezaji wake.

“Tulipotoka huko, niliwaomba wachezaji kuhakikisha wanapata muda wa kufanya mazoezi ndio maana walikuwa vizuri kwenye pambano hili lililoshuhudiwa na mashabiki wengi zaidi nchini,” amesema Beimbaya.

Bao hilo pekee katika msimu huu wa 15 wa Simba Day, liliwekwa kimiani na mshambuliaji makini Abdallah Magohe baada ya makosa ya kipa wa Benki ya NMB kuanzisha mpira kimakosa hivyo kuwapa Benki ya CRDB ushindi ulioshangiliwa na Mkurugenzi Mtendaji wake, Abdulmajid Nsekela.

Kipindi cha kwanza cha mchezo huo uliokuwa burudani tamu kwenye tamasha hilo kutokana na soka la kitabuni lililoonyeshwa na timu zote huku washindi wakifunika, kilimalizika bila milango ya timu hizo kufunguliwa.

Kocha wa timu ya Benki ya NMB, nyota wa zamani wa Yanga, Mohammed Hussein almaarufu kama Mmachinga alikiri kuzidiwa na wapinzani wao waliotumia nafasi waliyoipata kushinda mchezo huo.