Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM – Juhudi za kuukuza mchezo wa baseball nchini Tanzania zimepata msukumo mpya baada ya programu ya mafunzo iliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya wadau wa ndani na taasisi ya kimataifa ya Play Global, ikiwahusisha makocha wa kimataifa Antony Bennett na Brian Scott.

Akizungumza kwa niaba ya wanufaika wa programu hiyo, Hellen Ulaya, mmoja wa wanafunzi na makocha wanaonufaika na mafunzo hayo, amesema kuwa mafunzo yaliyotolewa yamewaongezea ujuzi, nidhamu na kujiamini, hali itakayochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa mchezo huo nchini.
“Kwa ukuaji na maendeleo ya baseball Tanzania, kujengeana uwezo, nidhamu, mafunzo ya msingi na ushirikiano wa kimataifa ni muhimu. Tunawashukuru kwa dhati Makocha Antony Bennett na Brian Scott kwa kujitoa kwao, maarifa na mapenzi makubwa kwa mchezo huu,” alisema Hellen.

Aliongeza kuwa ujio wa makocha hao umechochea ari mpya kwa makocha na wachezaji wa ndani kuota ndoto kubwa zaidi na kufanya kazi kwa bidii ili kuifikisha baseball ya Tanzania katika viwango vya juu.
Programu hiyo pia imepongezwa kwa kuwalenga watoto na vijana katika ngazi ya msingi, hatua inayotajwa kuwa nguzo muhimu ya kujenga kizazi kipya cha wachezaji wenye nidhamu, ushirikiano na uwezo wa kushindana kimataifa.

Kwa upande wake, taasisi ya Play Global imepongezwa kwa kuleta programu hiyo nchini, ambayo imefungua fursa kwa makocha wa Kitanzania kujifunza mbinu za kisasa za ufundishaji wa baseball.
“Tunajitoa kikamilifu kuhakikisha kila mtoto anapata nafasi ya kucheza na kukua kupitia mchezo huu. Nidhamu, ushirikiano na baseball vitakuwa msingi wa kazi yetu,” aliongeza Hellen.

Wadau wa michezo wameeleza kuwa juhudi kama hizi zinaendana na ajenda ya kuimarisha michezo na utalii nchini, huku baseball ikitajwa kuwa miongoni mwa michezo yenye fursa kubwa ya kukuza vipaji na kufungua milango ya kimataifa kwa vijana wa Kitanzania.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: