Mwanariadha nyota wa Tanzania, Gabriel Geay, ameshinda mbio za Daegu Marathon za mwaka 2026 kwa muda wa saa 2:08:09, akifanikiwa kutetea ubingwa wake wa mwaka uliopita.
Katika ushindani huo mkali, jukwaa la washindi (podium) lilishuhudia historia ya kipekee baada ya Watanzania wawili kuingia katika tatu bora:
Matokeo ya Juu – Wanaume
Gabriel Geay (🇹🇿) – 2:08:09
Chimdesa Gudeta (🇪🇹) – 2:08:09
Josphat Gisemo (🇹🇿) – 2:08:17
Tukio hilo limeacha gumzo kubwa kwenye mbio za kimataifa baada ya Tanzania kupata wawakilishi wawili kwenye tatu bora huku hakuna mwanariadha kutoka Kenya aliyeingia kwenye tano bora.
Mkenya wa kwanza kumaliza mbio hizo alikuwa Stanley Bett, aliyeshika nafasi ya sita kwa muda wa 2:10:31.
Ushindi huo unaendelea kuimarisha hadhi ya Tanzania katika mbio za masafa marefu duniani na kuthibitisha kuwa taifa hilo linaendelea kuzalisha wakimbiaji wa kiwango cha juu.



Toa Maoni Yako:
0 comments: