Mchezo huo ulisitishwa kwa takribani dakika 17 baada ya wachezaji wa Senegal kuondoka uwanjani, kabla ya mshambuliaji nyota Sadio Mané kuwashawishi kurejea na mchezo kuendelea hadi dakika za nyongeza. Senegal hatimaye walitwaa ubingwa baada ya Pape Gueye kufunga bao la ushindi katika dakika ya nne ya muda wa nyongeza, na kuipa taifa hilo taji lake la pili la AFCON ndani ya kipindi cha miaka mitano.Kwa upande wa wachezaji, CAF imewafungia washambuliaji wa Senegal Iliman Ndiaye na Ismaila Sarr mechi mbili kila mmoja kwa tabia isiyofaa dhidi ya mwamuzi. Aidha, Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limetozwa jumla ya faini ya Dola 615,000 ikijumuisha adhabu kwa utovu wa nidhamu wa mashabiki, wachezaji na benchi la ufundi.
Morocco nayo haikuachwa salama, ambapo beki nyota Achraf Hakimi amefungiwa mechi mbili za mashindano ya CAF, huku mshambuliaji Ismael Saibari akifungiwa mechi tatu na kutozwa faini ya Dola 100,000. Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF) pia limetozwa faini ya Dola 200,000 kwa mwenendo usiofaa wa wachezaji wake uwanjani, pamoja na Dola 100,000 nyingine kwa wafanyakazi wa kiufundi na wachezaji waliovamia eneo la VAR na kuzuia kazi ya mwamuzi.
CAF pia ilitupilia mbali ombi la FRMF la kutaka matokeo ya fainali hiyo yafutwe au kubadilishwa, ikieleza kuwa hatua za kinidhamu zilitosha na matokeo ya mchezo yanasalia kuwa halali.
Licha ya adhabu hizo, CAF imethibitisha kuwa vifungo vyote vinahusu mashindano yake pekee, hivyo havitaathiri maandalizi ya Senegal wala Morocco kuelekea Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika Marekani, Canada na Mexico.
Katika ujumbe alioutoa kupitia mtandao wa Instagram, Kocha Thiaw aliwashukuru mashabiki kwa sapoti yao, lakini akawaomba kutoandaa michango ya kumsaidia kulipa faini hiyo, akisisitiza fedha hizo zielekezwe kwenye misaada ya dharura kwa wahitaji zaidi.



Toa Maoni Yako:
0 comments: