Uongozi wa Singida Black Stars SC kupitia Kamati ya Nidhamu umewachukulia hatua za kinidhamu wachezaji wake wawili, Khalid Aucho na Amas Obasogie, kufuatia tuhuma zinazowakabili.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu iliyotolewa Februari 27, 2026, Aucho amepewa adhabu ya kusimamishwa kazi kwa miezi mitatu kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu na ukiukwaji wa majukumu ya kazi. Naye kipa Amas Obasogie amesimamishwa kwa muda huo huo wakati uchunguzi ukiendelea kuhusu tuhuma za upangaji wa matokeo.

Klabu hiyo imesisitiza kuwa hatua hizo zimechukuliwa kulinda misingi ya nidhamu, uwajibikaji na heshima ndani ya timu, huku ikiwataka wachezaji na watumishi wote kuzingatia maadili ya kazi.

Wakati huo huo, Aucho ameonekana kujibu hali hiyo kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, akieleza kuwa katika maisha yake yote ya soka amekuwa akijituma kwa weledi, heshima na nidhamu kwa kila klabu aliyowahi kuitumikia. Amesisitiza kuwa hajawahi kuhusishwa na tukio lolote la utovu wa nidhamu, akibainisha kuwa anaelewa wajibu mkubwa unaokuja na taaluma ya soka la kulipwa.

Aidha, aliwashukuru mashabiki wake kwa kuendelea kumuunga mkono katika kipindi hiki, akisema anaamini hali ya sasa itapita na ataendelea kusimama imara katika taaluma yake.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: