Beki kinda wa Senegal na bingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON25, El Hadji Malick Diouf, ameendelea kuishi katika kilele cha furaha baada ya kupewa heshima maalum ya Guard of Honour na wachezaji wa klabu yake mpya ya West Ham United, kufuatia mafanikio makubwa ya Senegal kutwaa ubingwa wa Afrika.
Tukio hilo lilifanyika katika mazoezi ya kikosi cha West Ham, ambapo wachezaji waliunda mistari miwili na kumpigia makofi Diouf alipokuwa akipita katikati yao, ishara ya kutambua na kuthamini mafanikio yake makubwa akiwa na timu ya taifa.
Mashabiki wa West Ham wameanza kumuona Diouf kama nguzo muhimu ya safu ya ulinzi kwa siku zijazo, wakiamini kuwa atakuwa sehemu ya mabadiliko makubwa ndani ya kikosi hicho kinachoshiriki Ligi Kuu England (EPL).






Toa Maoni Yako:
0 comments: