Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Januari 31, 2026 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ziara rasmi inayolenga kuendeleza juhudi za Serikali katika kukuza uhifadhi na utalii nchini.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mwigulu anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Kitaifa za Uhifadhi na Utalii maarufu kama The Serengeti Awards, tuzo zinazotolewa kwa wadau waliotoa mchango mkubwa katika kulinda maliasili na kukuza utalii.
Tuzo za Serengeti ni miongoni mwa tuzo muhimu zinazotambua mchango wa taasisi, mashirika, sekta binafsi na watu binafsi katika kuhifadhi mazingira, wanyamapori na vivutio vya utalii, huku Serikali ikiendelea kusisitiza ushirikiano wa wadau wote katika kulinda rasilimali za taifa.
Ziara ya Waziri Mkuu inadhihirisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha sekta ya utalii kama nguzo muhimu ya uchumi, ajira na maendeleo endelevu kwa Watanzania.






Toa Maoni Yako:
0 comments: