Articles by "MSIBA"
Showing posts with label MSIBA. Show all posts
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

ALIYEKUWA mfanyakazi wa Kampuni ya Mabasi ya NBS, Mzee Nassor Hamdan Seif (NBS), amefariki dunia leo asubuhi, na kuacha huzuni kwa familia, ndugu, jamaa na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia na uongozi wa NBS, mwili wa marehemu kwa sasa upo Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, na unatarajiwa kusafirishwa leo jioni kwa ndege kwenda mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mazishi ya Mzee Nassor Hamdan yatafanyika kesho saa 7 mchana mkoani Tabora, nyumbani kwao, ambapo ndugu, jamaa na marafiki wanatarajiwa kuhudhuria kumpa heshima ya mwisho.

Aidha, Kampuni ya Mabasi ya NBS imetangaza kuweka mabasi maalum kwa ajili ya kusafirisha waombolezaji wanaotaka kwenda Tabora kushiriki mazishi hayo. Mabasi hayo yatakuwa Temeke, jijini Dar es Salaam, na yataondoka leo jioni kuelekea Tabora.

Imesisitizwa kuwa usafiri huo ni bure kwa waombolezaji wote na utahusisha safari ya kwenda na kurudi, ikiwa ni sehemu ya mchango wa NBS katika kuungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi.

Familia ya marehemu imewashukuru waombolezaji wote kwa michango, dua na faraja wanayoendelea kutoa, na imetoa wito kwa Watanzania kuendelea kushirikiana katika kumpa marehemu heshima ya mwisho.

Marehemu Nassor Hamdan atakumbukwa kwa mchango wake katika sekta ya usafiri na kwa ushirikiano wake mzuri na jamii aliyokuwa akiishi nayo. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu, ametuma ujumbe mzito wa rambirambi kufuatia kifo cha Mwenyekiti Mwanzilishi wa chama hicho, Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, akimtaja kama mjenzi wa taifa, kiongozi wa mfano na hazina ya historia ya Tanzania.

Katika ujumbe wake alioutoa akiwa Gereza Kuu la Ukonga, Lissu amesema kifo cha Mzee Mtei ni pigo kubwa si tu kwa familia yake na wanachama wa CHADEMA, bali kwa taifa lote la Tanzania kutokana na mchango wake mkubwa katika ujenzi wa taifa, uchumi na demokrasia.

Lissu ameeleza kuwa marehemu Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa misingi ya uchumi wa Tanzania baada ya uhuru, akihudumu kama Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na baadaye Waziri wa Fedha, ambapo jina na saini yake zilionekana kwenye noti za kwanza kabisa za taifa.

Akizungumzia uadilifu wake, Lissu amesema Mzee Mtei alionesha ujasiri wa kipekee wa kisiasa pale alipothubutu kumshauri Mwalimu Julius Nyerere kubadili sera za kiuchumi za Azimio la Arusha baada ya kubaini kuwa zilikuwa zimeshindwa, na baadaye akaamua kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Fedha kwa misingi ya dhamira na uaminifu kwa nchi.

“Huu ndio uzalendo wa kweli. Mzee Mtei hakutafuta madaraka, bali alisimamia ukweli na maslahi ya taifa,” amesema Lissu katika ujumbe wake.

Kuhusu mchango wake ndani ya CHADEMA, Lissu amesema marehemu alikuwa mfano wa uongozi wa kujitolea, kwani hakuwahi kupokea mshahara, posho wala kunufaika binafsi kupitia nafasi yake ya uongozi ndani ya chama.

Ameongeza kuwa Mtei aliimarisha utamaduni wa uongozi wa kupisha damu changa, alipostaafu uenyekiti wa chama mwaka 1998 akiwa na umri wa miaka 66, jambo linaloendelea kuifanya CHADEMA kuwa chama chenye misingi ya kidemokrasia.

Lissu pia amemsifu marehemu kwa kuchapisha kitabu chake cha maisha “From Goatherd to Governor” mwaka 2009, akisema kitabu hicho kimekuwa hazina muhimu ya historia ya kisiasa na kiuchumi ya Tanzania.

Akihitimisha ujumbe wake, Lissu amesema badala ya kuomboleza kifo cha Mtei, Watanzania wanapaswa kusherehekea maisha yake yenye maana, busara na mchango mkubwa kwa taifa, huku akimuombea apumzike kwa amani.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na Makamu wa Kwanza wa Rais wa zamani, Mzee Edwin Isaac Mbiliewe Mtei, aliyefariki dunia usiku wa tarehe 19 Januari, 2026 jijini Arusha.

Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais Samia alisema kifo cha Mzee Mtei ni pigo kubwa kwa taifa kutokana na mchango wake mkubwa katika ujenzi wa uchumi na uongozi wa nchi. Rais alitoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote walioguswa na msiba huo.

Rais Samia alimtaja Mzee Mtei kuwa miongoni mwa watumishi na viongozi waliotoa mchango mkubwa katika kuimarisha misingi ya uchumi wa taifa, hususan kupitia nafasi yake kama Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (1966–1974), ambapo alishiriki katika kuweka mifumo imara ya fedha na taasisi za kifedha nchini.

Aidha, Rais alieleza kuwa marehemu ataendelea kukumbukwa katika historia ya siasa za Tanzania kama mmoja wa waasisi wa demokrasia ya ushindani wa vyama vingi na kiongozi aliyetoa mchango mkubwa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akitambuliwa kwa misimamo yake na uadilifu katika uongozi.

Rais Samia pia aliwahimiza Watanzania kuendelea kujifunza kutoka katika maisha na falsafa ya Mzee Mtei, ikiwemo kupitia maandiko yake binafsi (autobiografia), ambayo yanaeleza safari yake ya maisha na mchango wake katika kujenga taifa.

Akihitimisha, Rais aliomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na kuwapa familia, ndugu na taifa kwa ujumla faraja, nguvu na amani katika kipindi hiki cha majonzi.

Taarifa hiyo imesainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu, na kutolewa rasmi Zanzibar tarehe 20 Januari, 2026.

ZANZIBAR: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu, kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Halima Idd Nassor.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, marehemu Halima Idd Nassor amefariki dunia leo Januari 18, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili – Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mazishi ya marehemu yamefanyika leo Januari 18, 2026 katika eneo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Katika salamu zake, Rais Samia ameeleza masikitiko makubwa kwa msiba huo na kusema marehemu alikuwa kiongozi mahiri aliyetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Chama Cha Mapinduzi na Taifa kwa ujumla, hususan kupitia majukumu yake ya kibunge na ndani ya chama.

Rais pia ametoa pole kwa familia ya marehemu, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wanachama wa CCM, Waheshimiwa Wabunge pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo.

Aidha, Rais Samia amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na subira, mshikamano na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Taarifa hiyo imesainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu.
Mwanahabari Joachim Ernest Mushi amefiwa na mama yake mzazi, Mecktilda Joseph Lugazu, aliyefariki dunia Januari 6, 2026, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya General Jijini Dodoma, tukio lililoacha simanzi kwa familia, ndugu, jamaa na wadau wa tasnia ya habari.

Kwa mujibu wa taarifa za familia, taratibu za msiba zinaendelea kufanyika nyumbani kwa marehemu Kifuru–Kinyerezi jijini Dar es Salaam, ambako waombolezaji wanaendelea kujitokeza kutoa pole na faraja kwa familia iliyopatwa na msiba huo.

Imeelezwa kuwa mwili wa marehemu utasafirishwa kutoka Dodoma kuelekea Uru Mawela, mkoani Kilimanjaro, siku ya Januari 9, 2026, kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika siku inayofuata.

Mazishi ya marehemu Mecktilda Joseph Lugazu yanatarajiwa kufanyika Januari 10, 2026, nyumbani kwao Uru Mawela, huku familia ikitoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutoa pole na kuomba dua ili Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Dodoma, Tanzania – 12 Desemba 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea jijini Dodoma.

Kupitia taarifa yake, Rais Samia amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo mzito na kutoa pole kwa Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu, wananchi wa Jimbo la Peramiho, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki.

Rais Samia amemuelezea Marehemu Mhagama kama kiongozi shupavu na mtumishi wa umma aliyejitoa kwa moyo wake wote kwa kipindi cha zaidi ya miaka 38 ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Katika safari yake ya kisiasa, Mhagama aliwahi kuwa kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali za serikali, pamoja na kuwa mshauri wa wanasiasa na wananchi wengi.

“Kwa miaka 38, Mheshimiwa Mhagama amekuwa mwanachama mahiri wa CCM, kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali na mnasihi wa wengi katika siasa na maisha,” amesema Rais Samia katika salamu zake.

Rais Samia amewaombea wafiwa faraja katika kipindi hiki cha majonzi na kumkabidhi marehemu kwa Mungu, akisema: “Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina.”

Mipango ya mazishi inaratibiwa kwa ushirikiano kati ya Serikali, Bunge na familia ya marehemu, na taarifa zaidi zinatarajiwa kutolewa.

Dodoma, 11 Desemba 2025

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo jijini Dodoma. Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), kupitia taarifa rasmi ya Ofisi ya Bunge.

Katika taarifa hiyo, Spika Zungu alieleza kusikitishwa na msiba huo mzito, akisema:

“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba 2025 jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Peramiho. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”

Ofisi ya Bunge imesema kuwa mipango ya mazishi itaendelea kutolewa kwa ushirikiano na familia ya marehemu.

Mhe. Jenista Mhagama alizaliwa tarehe 23 Juni 1967 na amehudumu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi nchini, ikiwemo kuwa Mbunge na Waziri katika wizara tofauti.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.
Na Mwandishi Wetu - Kilimanjaro.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa upendo kwa kugharamia mazishi ya miili 42 ya watu waliofariki dunia kufuatia ajali iliyotokea Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.
Mhe. Nderiananga ametoa shukrani hizo tarehe 03 Julai, 2025 wakati aliposhiriki tukio la kuaga miili 35 katika viwanja vya Hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) akisema miili Saba ilichukuliwa na ndugu zao na miili miwili bado vipimo vya DNA vinafanyiwa kazi ili kutambulika.
Tukio hilo lilioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Nurdin Babu ambapo Mhe. Nderiananga alimpongeza kwa kujitoa kwa kiasi kikubwa tangu ilipotokea ajali hiyo akishirikiana na watendaji wake wote.
Amesema Serikali kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa iliyopo Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro kwa juhudi kubwa zilizofanyika kuokoa manusura wa ajali hiyo pamoja na miili ya walioungua kwa moto mara baada ya ajali kutokea.
Vilevile ameipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kuchukua sampuli za miili hiyo (DNA) kuhakikisha ndugu wanatambua miili ya wapendwa wao.
Hata hivyo Mhe. Nderiananga ameendelea kutoa pole kwa Serikali, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huo mzito kwa Taifa huku akiwaomba kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu hadi watakapokamilisha kuwahifadhi wapendwa wao.
Aidha, ajali hiyo iliyotokea Juni 28 2025 katika Kitongoji Mahuu, Kata ya Same, takribani kilomita nne kutoka Same mjini, ililihusisha basi kubwa la abiria, Mali ya Kampuni ya Chanel One, lenye namba za usajili T 179 CWL na basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster, lenye namba T 199 EFX linalomilikiwa na Kampuni ya Mwami Trans.

Coaster hiyo, ilikuwa ikitokea Same kuelekea Manispaa ya Moshi, wakati basi la Chanel One lilikuwa likitokea Arusha kuelekea Tanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisisitiza jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akifafanua jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) wakati Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. George Simbachawene (wa kwanza kulia) alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bi. Joyce Msuya Mpanju (aliyenyanyua mikono) akitoa shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa pili kutoka kulia) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Watatu kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi na Wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi. Mary Mwakapenda.
Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bw. Job Msuya (katikati) akizungumza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya wakati alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Na. Mwandishi Wetu-Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ametoa wito kwa Watanzania kumuenzi aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya kwa kuendelea kudumisha umoja, amani na mshikamano na kuyaenzi mazuri yote aliyoyafanya enzi za uhai wake.

Mhe. Simbachawene ameyasema hayo leo tarehe 22 Mei, 2025 alipoitembelea familia ya Hayati Msuya nyumbani Upanga jijini Dar es Salaam.

Mhe. Simbachawene amesema Hayati Mzee Msuya atakumbukwa kwa kuwagusa watu wengi kwa namna alivyokuwa na upendo, kuwasaidia watu wengi pamoja na kuhamasisha maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Mhe. Simbachawene amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwathamini Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu kwa mujibu wa Sheria.

Akiongea kwa niaba ya familia, mtoto wa Hayati Msuya, Bi. Joyce Msuya-Mpanju ameishukuru Serikali kwa mchango wake mkubwa na ushirikiano uliotolewa kwa familia hiyo tangu enzi za uhai wa Baba yao alipoanza kuugua hadi umauti ulipomkuta na kusimama bega kwa bega wakati wa msiba mpaka kukamlisha salama taratibu za mazishi yake.

Tunaishukuru sana Serikali kwa kuwa pamoja na familia yetu tangu Mama alipofariki mmekuwa na Baba bega kwa bega, hii ilisaidia sana hata kumfanya Baba aishi maisha marefu maana tunaelewa mtu anapofiwa na Mwenza hali inavyokuwa. Mhe. Waziri tunaomba utufikishie salamu zetu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samila Suluhu Hassan, Viongozi wote wa Serikali na Ofisi unayoiongoza kwa upendo mliotuonesha kwetu, Bi. Joyce ameongeza.

Hayati Cleopa Msuya alifariki dunia tarehe 7 Mei, 2025 na kuzikwa nyumbani kwake Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.
Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan awaongoza Watanzania kwenye maziko ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.




















Matukio mbalimbali kwenye mazishi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.












Viongozi mbalimbali pamoja na waombolezaji wakiwa kwenye Ibada maalum ya mazishi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mwanga, Usharika wa Usangi kivindu, wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.
The news arrived, both sharp and low,
A whisper first, then heavy blow.
A great pillar has fallen, now laid to rest,
His journey complete, in peaceful quest.

Cleopa David Msuya, a name that rings so clear,
Through the mountains, his vision drew near,
In Tanzania's land, his legacy stayed,
A servant’s soul, with no debt unpaid.

A scholar first, with books in hand,
From Makerere to his native land,
He brought the wisdom of those halls,
To lift up farmers, towns and all.

From the halls of Parliament he came,
In the fierce blaze, a leader’s flame,
With hands that built, and words that healed,
A Prime Minister's strength, never concealed.

He stood with Nyerere in testing days,
Through shifting tides and heavy haze.
Together they dreamed, together they tried,
For a land that no one could divide.

In Sokoine's shadow, brief he stood,
Then stepped aside as one who could,
No bitterness, no vain regret,
Just service given with no debt.

In Mwanga’s fields, his work remains,
Tarmac roads and schools in the plains,
His efforts etched in every stone,
A legacy of seeds he had sown.
When Mwanga's hills cried out for light,
He brought them power through the night,
Not for fame or fleeting praise,
But for the children's future days.

A father, a leader, ever so kind,
Our prayers for him, like morning wind.
In every corner, his memory stays,
In every soul, his spirit sways.

At ninety years, he paused to smile,
At roads he'd built mile after mile,
"Not mine," he said, "but all our deed,"
Such humble words from one so great indeed.

Now rest you well, you faithful son,
Your mighty race at last is run,
But in each school, each lamp, each road,
Your love for Tanzania still abode.

And so, dear Msuya, journey on,
Though gone from sight, you are not gone.
The sun you lit in quiet grace
Still warms the soul of every place.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396

— The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.
Ni Dakika, Saa, Siku, Wiki, Mwezi, Mwaka na hatimaye mika 17 sasa imetimia tangu Mzee Shauri Timoth Nathan (18/08/1925 – 18/09/2007) ututangulie Mbele za haki kama ulivyotutangulia kuja duniani.

Ni majonzi sana kwetu na pengo lako halijazibika hadi hivi leo.

Unakumbukwa na wengi sana maana ulikuwa ni mhimili mkuu katika familia, kipekee unakunbukwa na Mke wako Mary O Nathan pamoja na watoto wako wote, wakwe zako, wajukuu wako na vitukuu.

Wananchi na majirani zako wa pale Kijiji cha Kinyenze, Kata na Tarafa ya Mlali, Wilayani Mvomero mkoani Morogoro, Same na Ugweno mkoani Kilimanjaro pia wanakukumbuka sana na kukuombea kila lililo jema katika mapumziko yako.

Tunakumbuka maneno yako ya Mwisho uliotuachia watoto wako kuwa TUPENDANE, TUSAIDIANE na TUSHIRIKIANE, baba hakika hili linatendeka na tupo na umoja uliotujengea na tunajivunia hilo daima.

Tunazidi kukuombea Baraka na pumziko jema maana sote uliotuacha tutakufuata kama tulivyo kufuata hapa duniani.

Jina la Bwana Lihimidiwe Amina.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi (kushoto kwa Rais) wakizungumza na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt. Amani Abeid Karume, alipika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutowa mkono wa pole, kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja .
Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt.Amani Abeid Karume akiagana na Mkewe wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, baada ya kumaliza kutowa mkono wa pole na kuhani msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, Ikulu Migamoni Jijini Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Emmanuel Tutuba, alipofika Ikulu Migombani Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar, kwa ajili ya kutowa mkono wa pole na kuhani, msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.n 5-3-2024.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akizungumza na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Emmanuel Tutuba, alipofika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutowa mkopo wa pole, kufuatia msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza na kutoa mkono wa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, kwa kufiwa na Baba yake Mzazi, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi,alipofika Ikulu Migombani Wilaya ya Mjini Uguja Jijini Zanzibar kwa ajili ya kuhani na kutowa pole kwa familia, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akisalimiana na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariamn Mwinyi, alipofika Ikulu Migombani Zanzibar kwa ajili ya kutoa mkono wa pole, kufuatia Kifo cha Baba Mzazi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakizungumza na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa alipofika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutoa mkono wa pole na kuhani Msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa, baada ya kumaliza kutoa mkono wa pole kufuatila kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Ahajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)