Articles by "MSIBA"
Showing posts with label MSIBA. Show all posts
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi (kushoto kwa Rais) wakizungumza na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt. Amani Abeid Karume, alipika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutowa mkono wa pole, kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja .
Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt.Amani Abeid Karume akiagana na Mkewe wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, baada ya kumaliza kutowa mkono wa pole na kuhani msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, Ikulu Migamoni Jijini Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Emmanuel Tutuba, alipofika Ikulu Migombani Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar, kwa ajili ya kutowa mkono wa pole na kuhani, msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.n 5-3-2024.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akizungumza na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Emmanuel Tutuba, alipofika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutowa mkopo wa pole, kufuatia msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza na kutoa mkono wa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, kwa kufiwa na Baba yake Mzazi, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi,alipofika Ikulu Migombani Wilaya ya Mjini Uguja Jijini Zanzibar kwa ajili ya kuhani na kutowa pole kwa familia, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akisalimiana na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariamn Mwinyi, alipofika Ikulu Migombani Zanzibar kwa ajili ya kutoa mkono wa pole, kufuatia Kifo cha Baba Mzazi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakizungumza na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa alipofika Ikulu Migombani kwa ajili ya kutoa mkono wa pole na kuhani Msiba wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa, baada ya kumaliza kutoa mkono wa pole kufuatila kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Ahajj Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki wiki iliyopita na kuzikwa Kijijini kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)
Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Dotto Biteko pamoja na Viongozi mbalimbali wakiwasili kuhudhuria shughuli ya mazishi ya aliyekuwa waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa leo Februari 17, 2024 katika kijiji cha Ngarash wilayani ya Monduli mkoa wa Arusha asubuhi hii.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi anasikitika kutangaza kifo cha Ndg. Gerald Mwanilwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, kilichotokea tarehe 02 Novemba, 2022 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mipango ya Mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Goba Dar es Salaam, Ilazo Dodoma na Makorongoni Iringa.

Kwa masikitiko makubwa tunatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene akitoa heshima za mwisho wakati wa kuaga Mwili wa Mzee William Kusila katika ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwake Kijiji cha Mtitaa-Bahi Mkoani Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akitoa heshima za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Mzee William Kusila.
Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mzee William Kusila.
Mhe. Adamu Kimbisa akisaini Kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mzee William Kusila.
---
Na mwandishi wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amesema Mzee William Kusila alipenda kuona viongozi wanazingatia miiko, na kuishi kwa kuwa mfano mwema kwa jamii.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene alipokuwa akitoa salamu za serikali katika ibada ya mazishi ya Mzee Williamu Jonathan Kusila aliyezaliwa Mwaka 28/02/1944 na kufariki 21/08/2022, iliyofanyika nyumba kwake kata ya Mtitaa-Bahi Dodoma 26/August/2022.

“Mzee kusila ni kipimo cha mtu muadilifu; mtu mwenye Upendo, na mtu aliyefanya mambo mengi mazuri ambayo tunapaswa kuyaiga na kuyaenzi.”

Tumepoteza kiongozi wa kisiasa aliyeshika nafasi mbalimbali za umma na kutimiza majukumu yake ipasavyo, ni mtu aliyepinga na kukataa rushwa, alisema Waziri.

Aidha ametoa rai kwa Watoto wa Mzee Kusila kuzidi kushirikiana na kushikamana ili kutunza jina na heshima ya baba.

“Amefafanua watu hawazaliwi sawa, mtatofautiana kwa uwezo wa elimu, uwezo wa kipato na mambo mengine lakini wote ni Watoto wa mzee Kusila ni lazima mtengeneze mamlaka itakayosaidia kuwaongoza kama familia”

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema Mzee William Kusila alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Saba wa Dodoma kati ya Mwaka (1993-19995) alikuwa Mbunge wa jimbo la Bahi na katika vipindi tofauti amekuwa waziri wa kilimo, Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi na amewahi kuwa Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma.

“Alifanya kazi kwa upendo Mkubwa; aliokuwa nao kwa wananchi wa Dodoma, Baba yetu aliongoza kwa Vitendo na sio kwa kuagiza, kama alisema limeni nayeye alikuwa analima”

Naye Mbunge Mstaafu wa jimbo la Chilowa Mhe. Hezekiah Chibulunje akitoa salamu za rambirambi amesema anamkumbuka mzee Kusila kwa jitihada zake za kuondoa Njaa Dodoma na kuhakikisha tunapanda mazao yanayostahimili ukame.

“Alikuwa na uchungu sana katika kuondoa njaa na vile vile katika swala la zima la kusimamia elimu, nimefanya naye kazi kwa ushirikiano mkubwa sana bila nongwa”
ILIKUWA NI SEKUNDE, DAKIKA, SAA, WIKI, MWEZI MWAKA NA SASA NI MIAKA KUMI (10) KAMILI UMETIMIZA TANGU BIBI YETU, MAMA YETU, KIPENZI CHETU AKANASHE SHEDRACK MAKERE UTUTOKE GHAFLA TAREHE 08/05/2012 SAA 10 JIONI BILA YA KUTUAGA KUTOKANA NA MARADHI YALIYOKUWA YAKIKUSUMBUA.

UNAKUMBUKWA SANA KWA UCHESHI, UPENDO NA KUWAJALI KILA KIUMBE CHA HAPA DUNIANI. HALIDHALIKA UNAKUMBUKWA SANA NA WANAO, WAJUKUU, VITUKUU, VILEMBWE, NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI ZAKO. UMETUACHIA HUZUNI NA PENGO KUBWA KATIKA UKOO.

MWENYEZI MUNGU, MUUMBA WA MBINGU NA NCHI AENDELEE KUKUPA MWANGA NA RAHA YA MILELE HUKO ULIPO KWANI YEYE NDIYE ALIYETOA NA YEYE NDIYE ALIYETWAA. JINA LA BWANA DAIMA LIHIMIDIWE. AMEN!
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Aprili 27, 2022 amewaongoza waombolezaji kupokea mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Irene Ndyamkama kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma. Mheshimiwa Spika Dkt. Tulia Ackson (wa pili kulia) pia alishiriki katika mapokezi ya miili wa Mbunge huyo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Aprili 27, 2022 amewaongoza waombolezaji kupokea mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Irene Ndyamkama kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma. Mheshimiwa Spika Dkt. Tulia Ackson (kulia kwa Waziri Mkuu) pia alishiriki katika mapokezi ya mwiili wa Mbunge huyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Katibu wa Bunge, Mhe. Nenelwa Mwihambi, ndc akishiriki zoezi la kuuga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Irene Alex Ndyamkama leo Aprili 27, 2022 katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Profesa Honest Ngowi enzi za uhai wake.
Rasi wa ndaki ya Dar es Salaam, Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa Honest Ngowi akiwa na Dereva wake Innocent Gerson Muringo wakati walipotembelea Mahabusu ya watoto iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam Machi 11, 2022. Ambao wote wamefariki duni leo
Gari alilokuwa akisafiria Profesa Honest Ngowi.
Eneo la ajali

MAKAMU Mkuu wa Chuo Prof. Lughano Kusiluka anasikitika kutangaza kifo cha Prof. Honest Ngowi na Dereva wake, waliofariki asubuhi ya leo Machi 28, 2022 kwa ajali ya gari wakiwa njiani kuja Kampasi Kuu Morogoro.

Taarifa hiyo imethibitishwa na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Lughano Kusiluka, ambaye ametangaza kifo cha Prof. Ngowi na Dereva wake, waliofariki kwa ajali ya gari wakiwa njiani kwenda Kampasi Kuu Morogoro.

"Tunaomba muwe watulivu wakati Menejiementi inaendelea kufuatilia taarifa kamili ya tukio hili, na kuweka taratibu zingine.

"Taarifa zaidi zitatolewa rasmi na taratibu zingine za kuwahifadhi wenzetu. Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina la Bwana lihimidiwe. Poleni Wote kwa msiba huu mzito.

Aidha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imetoka eneo la Mlandizi mkoani humo ikihusisha magari matatu.

"Ni kweli ajali imetokea leo saa 12 asubuhi ikihusisha magari matatu aina ya Noah, Land Cruiser alilokuwa anasafiria yeye na lori ambalo ndio chanzo cha ajali lilihama njia na kuiangukia Noah ubavuni kisha kuilalia gari ya Ngowi," amesema Lutumo.

Lutumo amesema hadi wanamtoa eneo la tukio alikuwa bado mzima akiwaishwa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi Mkoa wa Pwani.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina leo tarehe 10.02.2022 amefanya ziara ya siku moja Wilayani Chato yenye lengo la kutoa salamu za pole kwa familia ya hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Dkt. Adesina amepokewa katika uwanja wa ndege wa Geita uliopo Chato na kaimu Mkuu wa Wilaya ya Chato ndugu Wilson Shimo pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya.

Akiwa nyumbani kwa hayati Dkt. John Pombe Magufuli Dkt. Akinwumi Adesina amesema amefika nyumbani kwa hayati Magufuli kutokana na urafiki mkubwa aliokuwa nao na hayati Rais Maguli pamoja na kutambua mchango mkubwa ambao hayati Magufuli aliutoa kwa watanzania na kwa watu wengine. “Rais Magufuli alikuwa mfano mzuri kwa viongozi barani Afrika, aliwapenda watanzania na waafrika wote kwa moyo wake wote” alisema Dkt. Adesina.

Rais wa AfDB amesema pamoja na kuodokewa na Rais Magufuli anafarijika kuona Tanzania bado ipo kwenye mikono salama chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anaendeleza yale yote mazuri yaliyoachwa na hayati Magufuli.

Dkt. Akinwumi Adesina amemshukuru Rais Samia kwa ushirikiano na kumruhusu kufika Wilayani Chato kwa ajili ya kutoa salamu za pole. Dkt. Akinwumi Adesina na ujumbe ulioambatana naye wamerejea jijini Dar es Salaam.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina katika matukio ya uwekaji wa shada kwenye kaburi la hayati Dkt. John Pombe Magufuli
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato ndugu Mandia Kihiyo.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Chato Ndugu Wilson Shimo wakati Rais huyo alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Geita uliopo Chato leo Tarehe 10. 02.2022
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Gita Ndugu Musa Chogero wakati Rais huyo wa AfDB alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Geita uliopo Chato leo Tarehe 10. 02.2022
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akisalimiana na mdogo wa hayati Dkt. John Pombe Magufuli ndugu Gorodian Joseph Magufuli nyumbani kwa hayati Magufuli Mlimani kata ya Muungano Wilayani Chato.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akiwa kwenye picha ya pamoja na maafisa wengine walioambatana na Rais huyo wa AfDB na Mdogo wa hayati Dkt. John Pombe Magufuli ndugu Gorodian Joseph Magufuli nyumbani kwa hayati Magufuli Mlimani kata ya Muungano Wilayani Chato.