
Dodoma, 11 Desemba 2025
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo jijini Dodoma. Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), kupitia taarifa rasmi ya Ofisi ya Bunge.
Katika taarifa hiyo, Spika Zungu alieleza kusikitishwa na msiba huo mzito, akisema:
“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba 2025 jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Peramiho. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”
Ofisi ya Bunge imesema kuwa mipango ya mazishi itaendelea kutolewa kwa ushirikiano na familia ya marehemu.
Mhe. Jenista Mhagama alizaliwa tarehe 23 Juni 1967 na amehudumu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi nchini, ikiwemo kuwa Mbunge na Waziri katika wizara tofauti.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.


Toa Maoni Yako:
0 comments: