
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania, Askofu Mkuu Angelo Accattino, amewasili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo na kutoa salamu za pole kufuatia kifo cha Polycarp Kardinali Pengo kilichotokea Februari 19, 2026.
Katika ziara hiyo ya maombolezo, balozi huyo alitoa pole kwa Thaddaeus Ruwa'ichi, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, pamoja na Kanisa Katoliki nchini na waumini wote walioguswa na msiba huo mkubwa.
Ibada za kumuombea marehemu zinaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini huku waumini wakiendelea kuungana katika sala, wakimuombea apumzike kwa amani ya milele.





Toa Maoni Yako:
0 comments: