NaDodoma, Machi 31, 2026 — Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka kampuni ya Liaoning Fangda wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania.
NaDodoma, Machi 31, 2026 — Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka kampuni ya Liaoning Fangda wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania.Na Mwandishi Wetu.
Dodoma, Machi 30, 2026 — Kamishna wa Kamisheni ya Polisi Jamii, Alex Sospeter Mkama, amekabidhiwa rasmi ofisi ya kuongoza kamisheni hiyo katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dodoma.
Hafla hiyo ya makabidhiano imeongozwa na aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ulrich Matei, ambaye alimkabidhi majukumu hayo kwa utaratibu rasmi, akimtakia mafanikio mema katika uongozi wake mpya.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa ofisi, CP Mkama alieleza dhamira yake ya kuendeleza juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi, akisisitiza umuhimu wa jamii kushiriki kikamilifu katika kudumisha amani na usalama nchini.
Kwa upande wake, DCP Matei alisema kuwa ana imani uongozi mpya utaongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamisheni ya Polisi Jamii, hasa katika kujenga uhusiano chanya na wananchi na kushughulikia changamoto za kiusalama kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Kiongozi wa Chama hicho, Dorothy Semu, marehemu Bungara alifariki dunia wakati akiwa hospitali alipokwenda kupata huduma ya kusafisha figo (dialysis).
Chama hicho kimetoa pole za dhati kwa familia ya marehemu, hususan kwa mjane wake Bi. Mwanawetu Said Zarafi, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo mzito.
ACT Wazalendo imemkumbuka marehemu Bungara kama mwanasiasa wa upinzani aliyekuwa jasiri na aliyejitolea kupigania haki, demokrasia na ustawi wa wananchi katika maisha yake yote.
Aidha, chama hicho kimeeleza kushiriki kikamilifu katika msiba huo kwa kuchangia hali na mali, ikiwemo kugharamia mazishi ya marehemu. Pia kimewaomba wanachama wake, hususan kutoka Kanda ya Kilwa Kusini, kujitokeza kwa wingi kushirikiana na familia katika kipindi hiki kigumu.
“Tunaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi, na tunaomba Mwenyezi Mungu aipokee roho ya marehemu mahali pema peponi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Kifo cha Bungara kimeacha pengo kubwa ndani ya chama hicho na kwa wanasiasa wa upinzani nchini, huku akitarajiwa kukumbukwa kwa mchango wake katika harakati za kisiasa na kijamii.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Véron Mosengo-Omba, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake baada ya zaidi ya miaka 30 ya utumishi katika soka la kimataifa.
Katika taarifa rasmi iliyotolewa jijini Cairo Machi 29, 2026, Mosengo-Omba amesema amefikia uamuzi huo ili kujikita katika miradi binafsi baada ya kujitolea kwa muda mrefu kukuza soka kama chombo cha kuunganisha watu, kutoa elimu na kuleta matumaini.
Amesema kuwa sasa anaondoka akiwa na amani ya moyo baada ya kuondoa tuhuma zilizokuwa zikimkabili, akibainisha kuwa anaiacha CAF ikiwa imara zaidi na yenye mafanikio makubwa kuliko ilivyokuwa awali.
Mosengo-Omba pia alimshukuru Rais wa CAF, Patrice Motsepe, pamoja na timu yake na wadau wote wa soka barani Afrika kwa ushirikiano wao uliochangia mafanikio ya maendeleo ya mchezo huo.
Amehitimisha kwa kueleza matumaini yake kuwa mafanikio yaliyopatikana ndani ya CAF yataendelea kudumu na kuimarika zaidi katika siku zijazo.

Rais wa Kenya, William Ruto, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ol Kalou, David Njuguna Kiaraho, akieleza kusikitishwa kwake na msiba huo alioutaja kuwa pigo kubwa kwa taifa.
Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto amesema mawazo na maombi yake yako pamoja na familia ya marehemu, marafiki pamoja na wananchi wa Ol Kalou katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Akimzungumzia marehemu Kiaraho, Rais Ruto alimtaja kuwa kiongozi mnyenyekevu, thabiti na mwenye maono, aliyekuwa nguzo muhimu kwa jamii yake kutokana na kujitolea kwake kuwatumikia wananchi wake kwa dhati.
Aliongeza kuwa marehemu atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya elimu pamoja na utumishi wake uliotukuka ndani ya Bunge la Taifa, ambako alisimamia maslahi ya wananchi wake kwa uadilifu.
Rais Ruto pia alibainisha kuwa maisha ya marehemu ni funzo kwa viongozi wa kizazi cha sasa, akiwahimiza kuweka mbele huduma kwa wananchi badala ya siasa zisizo na tija, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza kaulimbiu yake ya “Kazi Kwanza, Siasa Baadaye.”
Amehitimisha kwa kutoa pole na kumuombea marehemu apumzike kwa amani, huku taifa la Kenya likiendelea kuomboleza kiongozi huyo aliyegusa maisha ya wengi.


Batuli Hemedi Mtendaji wa Kijiji cha Ngukumo wilayani Nzega akipanda moja ya miti iliyotolewa na kampuni ya Tumbaku Alliance One kwa ajili kuchangia zoezi upandaji miti milioni 1.5 wilayani humo sambamba na agizo la serikali.
Na Mwandishi Wetu -Narok, Kenya.
Rais wa Kenya, William Ruto, amempongeza mwanasiasa David Keter maarufu kama Dollarline kwa kushinda katika kura za mchujo za chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika Jimbo la Emurua Dikirr Constituency.
Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto alimpa pongezi Keter kufuatia ushindi huo muhimu uliompa tiketi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo ujao wa jimbo hilo.
Aidha, Rais Ruto alimpongeza pia mpinzani wake Bernard Ng'eno maarufu kama Buluu kwa kuendesha kampeni imara, akieleza kuwa ushindani huo umeimarisha misingi ya demokrasia ndani ya chama hicho kuanzia ngazi za chini.
“Tunapongeza ushindani wa haki na wa kidemokrasia uliofanyika, ambao unaimarisha chama chetu na kuonesha mshikamano wa wanachama,” ilieleza sehemu ya ujumbe wa Rais Ruto.
Rais huyo alisisitiza kuwa baada ya mchakato wa mchujo kukamilika, ni muhimu kwa wanachama wote wa UDA kuungana na kumuunga mkono mgombea aliyepitishwa ili kuhakikisha ushindi katika uchaguzi mdogo.
“Tunakwenda mbele kama timu moja imara, tukiwa tumeungana nyuma ya mgombea wetu na ajenda ya chama,” aliongeza.
Ushindi wa Keter unatarajiwa kuongeza ushindani mkali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, huku chama cha UDA kikilenga kuimarisha nafasi yake kisiasa katika Kaunti ya Narok na maeneo ya jirani.
Moshi ilichangamka kwa mara nyingine tena huku maelfu ya wakimbiaji, mashabiki, na watazamaji wakikusanyika kwa toleo la mwaka 2026 la Kilimanjaro Marathon. Kilichoanza zaidi ya miongo miwili iliyopita kama mbio, kimekua na kuwa moja ya majukwaa yenye nguvu zaidi kitaifa nchini Tanzania, yakileta pamoja michezo, utalii, utamaduni, na jamii kwa namna ya kipekee.
Mbio za mwaka huu zilivutia ushiriki mkubwa kutoka kote Tanzania na duniani kwa ujumla, na kuimarisha nafasi yake kama tukio muhimu la utalii wa michezo. Kuanzia wanariadha wa kiwango cha juu hadi wakimbiaji wa mara ya kwanza, tukio hili liliunda uzoefu wa pamoja uliovuka mstari wa mwisho wa mashindano. Haikuwa tu kuhusu ushindani, bali pia ushiriki, muunganiko, na fahari ya taifa.
Afya na ustawi pia vinaendelea kuwa sehemu muhimu ya faida ya marathon hii. Kwa miaka mingi, tukio hili limechangia kujenga utamaduni wa kukimbia na kuishi maisha yenye afya nchini. Watu wengi zaidi wanashiriki katika shughuli za mazoezi, na taasisi mbalimbali zinaanzisha majukwaa yanayohamasisha harakati na ustawi wa mwili. Marathon imekuwa mfano wa kile ambacho juhudi endelevu za afya ya jamii zinaweza kufanikisha nchini Tanzania.
Burudani haikuishia kwenye mbio pekee. Kili Dome kwa mara nyingine ilileta pamoja michezo, muziki, sherehe, na kuunda mazingira yenye hamasa ambapo washiriki na watazamaji waliweza kuungana na kujiburudisha. Mchanganyiko huu wa michezo na maisha ya kijamii unaakisi nafasi pana ya marathon katika kuunda uzoefu wa pamoja.
Akizungumza baada ya tukio, Mkurugenzi Mtendaji Michelle Kilpin alieleza ukuaji na umuhimu unaoendelea wa marathon hii kama jukwaa la kitaifa.
“Marathon ya Kilimanjaro inaendelea kuwaleta watu pamoja kutoka asili mbalimbali kwa namna inayoakisi maana halisi ya Tanzania. Inaunga mkono utalii, inakuza afya, na inajenga mahusiano yenye maana katika jamii. Tunajivunia kuona jinsi tukio hili linavyoendelea kukua na kutoa thamani zaidi ya mbio zenyewe.”
Kadri toleo la mwaka 2026 linavyohitimishwa, Kilimanjaro Marathon inabaki kuwa zaidi ya tukio la kila mwaka la michezo. Ni jukwaa linalochochea shughuli za kiuchumi, linaimarisha mshikamano wa jamii, linahamasisha maisha yenye afya, na linaonesha Tanzania kwa dunia.
Kupitia uungwaji mkono wake unaoendelea, Tanzania Breweries Plc kupitia Kilimanjaro Lager inaendeleza dhamira yake ya kusaidia mipango inayowaunganisha watu na kuchangia maendeleo ya muda mrefu ya taifa. Mbio zinaweza kuishia kwenye mstari wa mwisho, lakini faida yake inaendelea kwa muda mrefu zaidi.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa George Masaju akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.










.jpeg)



















