Articles by "BURUDANI"
Showing posts with label BURUDANI. Show all posts

Mkurugenzi wa Lamata Village entertainment, Bi. Leah Mwendamseke ‘Lamata’ akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA (Ukweli Upe Muda) itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.
Akizungumza leo Aprili 23, 2024 katika Uzinduzi wa app mpya ya VTV ambapo ndani yake unaweza kustream tamthilia mpya kabisa ya EZRA inayoandaliwa na kampuni ya Lamata Village entertainment, Lamata amesema kuwa tamthilia EZRA ndani yake kuna visa na mikasa, story ya aina yake ambayo itawaacha watazamaji na wasikilizaji mdomo wazi huku ukitaka kujua yaliyojiri.

Pia alitoa shukrani zake za kipekee kwa Uongozi wa Bodi ya Filamu kwa kushirikiana nao katika uzinduzi huo, huku akiwamwagia maua ya pekee kwa Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kuweza kuwashika mkono na kufanikisha kazi hiyo.Mshehereshaji Bw. Evance Bukuku akizungumza katika halfa ya uzinduzi wa Tamthilia ya EZRA na app ya VTV.Kwa upande wao Vodacom Tanzania wamewaalika watazamaji kuweza kupakua app ya VTV ili kuweza kuiona tamthilia hiyo kidijitali zaidi.

Usibaki nyuma! pakua app ya VTV leo google play au Appstore ufaidi mchapo mzima wa Ezra na burudani nyingine mbalimbali.

Wageni waalikwa.
Meneja wa Lamata Village entertainment, Bw. Danny Nyalusi akitoa machache.
Waigizaji waliopo katika tamthilia ya EZRA.
Viongozi mbali mbali wakiwa na waigizaji.
Wasanii mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa tamthilia mpya iitwayo EZRA itakayokuwa ikirushwa katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Online app ya VTV inayomilikiwa na Vodacom Tanzania.

Kumekuwa na taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusiana na Timu ya Tabora United zikimuhusisha Kocha Mkuu Denis Laurence pamoja na msaidizi wake Masoud Juma kuwa wanataka kuondoka kwa kile kinachoelezwa hawajaridhishwa na mazingira lakini pia hawajasainishwa mikataba yao ya kazi.

Kwanza kabisa Klabu inapinga vikali upotoshwaji wa taarifa hizi kwa baadhi ya watu ambao hawanania njema na Timu ya Tabora United. Ikumbukwe kuwa Tabora United inaongozwa na viongozi ambao wanatambua na kufahamu umuhimu wa mfanyakazi kwa kila idara.

Tukianza na suala la Kocha Mkuu Denis Laurence ni kwamba kabla ya kuwasili kwa Kocha Laurence akiwa Ufaransa amekuwa akiifuatilia Timu ya Tabora United kupitia video za mechi mbalimbali lakini pia anaifahamu Timu kutokana na mazungumzo ambayo yalikuwa fakifanyika baina yake na viongozi wa klabu.

Lakini pia Kocha Laurence amewahi kufanya kazi na Msaidizi wake ambaye wanafanya kazi pamoja ndani ya Tabora United Masoud Juma na ndiye aliyempendeza hivyo hata suala la mazingira tafsiri yake ni kwamba analifahamu kwa kuwa anaifahamu vyema Timu ya Tabora United.

Kuhusu mikataba kwa hali ya kawaida hakuna mtumishi yoyote ambaye anaweza kuanza kufanya kazi pasipo kusainishwa mkataba wake hicho kitu hakiwezekani na hakijawahi kutokea tangu Dunia imeumbwa.

Kocha Laurence pamoja na Msaidizi wake Masoud walipewa mkataba na kusaini kulingana na taratibu za kazi zinavyotaka na ndio mana waliweza kuanza kazi mara moja na hadi sasa wanaendelea na majukumu yao kama kawaida ikiwa ni siku ya sita tangu walipotambulishwa.

Na hili jambo linafahamika kabisa kuwa mtu anapoanza kufanya kazi maana yake ni kwamba tayari walishakubalina na mwajiri hivyo kusema Kocha Mkuu na msaidizi wake wanaweza kuacha kazi hizo ni taarifa za uzushi na uongo na tunaomba mzipuuze.

Kuhusu mishahara ya wachezaji, viongozi pamoja na Benchi la ufundi, hakuna ambaye anadai hadi sasa na kwamba mara nyingi uongozi umekuwa ukijali masilahi ya watumishi wa idara zote kwa kuhaikisha kuwa stahiki zao wanalipwa kwa wakati.

Uongozi wa Tabora United umekuwa ukifanya mrejesho wa matumizi ya fedha zinazotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania TPLB kupitia kwa mzamini Mkuu wa haki za matangazo Azam Media kila mwezi na kwamba tumekuwa tukipokea fedha hizo. Hivyo kusema kwamba Tabora United haipatiwi fedha za haki ya matangazo huo ni upotoshwaji na kutaka kutugombanisha na mamlaka husika.

Kuhusu wachezaji wa Timu ya vijana Under 20, wote waliwasili tangu juzi Tabora wakitokea Geita ambapo walikuwa na mchezo wa Ligi ya vijana hatua ya makundi hivyo wachezaji hawajakwama sehemu yoyote.

Hivyo kauli ya Klabu ni kwamba mashabiki na wadau wote wampira ambao wanaiunga mkono Timu ya Tabora United wapuuze taarifa hizo kwani zinalenga kuchafua Brandi ya Klabu kwa makusudi hivyo kama uongozi unatambua thamani na umuhimu wa kila mmoja ndani na nje ya Klabu.

Timu inaendelea kujifua kwa ajili ya michezo ya Michuano ya kombe la Azam Sports Federation ASFC dhidi ya Singida Fountaingat pamoja na Ligi ya NBC soka Tanzania Bara itakayoendelea baada ya kumalizika kwa kalenda ya FIFA.

Imetolewa leo Machi 27
Na Christina Mwagala
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Tabora United.
Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro kushoto akimkabidhi Kombe la Mashindano ya Odo Ummy Cup Nahodha wa timu ya Kiomoni FC mara baada ya kuibuka Mabingwa kwa kuifunga Nguvumali FC penati 3-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga juzi ambapo mshindi huyo alipatiwa pia kitita cha Sh Milioni 3,pikipiki ya magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mpira kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya ambaye ndie muandaaji wa Mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman
Na Oscar Assenga, TANGA

TIMU ya Kiomoni FC wametawazwa kuwa Mabingwa wapya wa Michuano ya Kombe la Odo Ummy Cup baada ya kuibamiza timu ya Nguvumali FC penati 3-1 katika mchezo wa Fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Lamore Jijini Tanga.

Kutokana na ushindi huo waliweza kujinyakulia kitita cha Sh.Milioni 3,Pikipiki yenye Magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mipira huku Mshindi pili timu ya Nguvumali FC waliweza kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 2.5 na Mpira na Jezi Seti 1.

Michuano hiyo ya Odo Ummy Cup huchezwa kila mwaka kwa kushirikisha kata zote za Jimbo la Tanga yakiwa na lengo la kuibua vipaji na kukuza kiwango cha soka kwa vijana ambao kupitia mpira wanaweza kujikwamua kiuchumi.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikitaka kuibuka na ushindi ili kuweza kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko zilitoka sare tasa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia ikiwa na hari kubwa kutokana na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ili kuweza kujiimarisha kwa lengo la kufanya vizuri katika michuano hiyo.

Wakionekana kucheza kwa umahiri mkubwa Kimoni FC walianza kwa kulishambulia lango la wapinzani wao bila kuwepo kwa mafanikio yoyote ambapo kila wachezaji walipokuwa wakipiga mashuti langoni mwao liligonga mwamba na kutoka nje.

Kutokana na ushindani wa mchezo huo ulizilazimu timu zote kutoka uwanjani dakika 90 bila kuona milango ya kila mmoja na hivyo mwamuzi wa mchezo huo kulazimika kupelekea mchezo huo kwenye mikwaju ya penati ambao ndipo kiomoni waliposhinda mabao hayo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mcheo huo wa Fainali Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni aliwapongeza waandaaji wa mashindano hayo huku akieleza kwamba mashindano ikiwemo Mbunge Ummy Mwalimu.

“Ukiona vyaelea ujue vimeundwa hili ya leo tuna kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza Mbunge wetu Ummy Mwalimu niseme kama Waziri mwenye thamana ya michezo nimeshahudhuia mashindano yanayoandaliwa na wabunge mwengi sana sijaona mashindano mazuri kama haya”Alisema

Alisema mashindano haya ni mazuri na makubwa ambayo sijapata kuyaona katika maeneo mengine na Mbunge Ummy ana sifa ya kipekee kwa kuwajali wananchi wa Jimbo lake kutokana na kuhakikisha anawapigania ili kuweza kuondoa kero zenu.

Aidha alisema wanaposema michezo ni ajira wanaamini pia ni uchumi na wao kama Wizara wamemua hivi sasa michezo ni ajira na uchumi hivyo mashindano kama hayo watashirikiana na waandaaji kuhakikisha wanaibua vipaji na kuviendeleza.

Hata hivyo alisema kwamba mkoa wa Tanga ndio chimbuka la vipaji na wao serikali wataendelea kuiangalia Tanga huku akieleza kwamba Mbunge Ummy amepeleka ombi kwao kwamba uwanja huo wa Lamore ambao umechezewa fainali hiyo upandwe nyasi uwe mzuri ili fainali za mwakani ziwe nzuri .

“Na mimi nimemuhaidi Mbunge Ummy kwamba nitawaleta wataalamu kufanya tathimini ili uwanja uweze kuwa katikaa hali nzuri kutokana na kwamba umuhimu wa mashindano hayo ya Odo Ummy Cup”Alisema

Awali akizungumza katika fainali hiyo ,Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya alisema kwamba suala la Odo Ummy Cup ni mchango wake katika kutekeleza ilani ya CCM ibara ya 243 ambayo inawataka kuwekeza kwenye mpira wa migu hasa kwa vijana.

Alisema wanamshukuru pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman kutokana na kwamba amekuwa akiwasaidia na kuwaleta na kuwaongoza kwenye kutekeleza ilani.

Aidha alisema mashindano hayo lengo ni kuwaleta pamoja vijana wa Tanga mjini na yameleta moja,mshikamano na hamasa ya kumweka karibu na vijana huku akishukuru timu zote kutoka Kata 27 ambazo zilishiriki kwenye michuano hiyo.

“Lakini pia nishukuru kamati za Siasa za CCM kwa kujitoa kusimamia mashindano hayo pamoja na timu ya Hamasa ya UVCCM pia niwashukuru wadhamini wetu kwa kuuunga mkono wakiwemo wadau wetu Assemble Insurance kwa kutuunga mkono”Alisema

Hata hivyo kwa upande wake,Mwenyeiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman atumia fursa hiyo kuwataka wabunge na madiwani wa mkoa huo wahakikisha wanaendelea michezo katika maeneo yao.

“Kwani kufanya hivyo ni kutekeleza kwa vitendo ilani ya CCM ambayo tumehaidi kuendeleza michezo hivyo lililofanyika linatafsiri ilani kwa vitendo hivyo wabunge na madiwani hakikisheni hili linatekelezwa”Alisema.




Na Oscar Assenga,TANGA.

WAZIRI wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro amepongeza Mashindano ya Oddo Ummy Cup huku akieleza kwamba watayatumia kuangalia vipaji vya wachezaji na baadae aone namna ya kumpigia simu Kocha wa timu ya Taifa ili kuona namna ya kuwapeleka kwenye Taifa ya Taifa.

Dkt Ndumbaro aliyasema hayo Machi 10 mwaka huu Jijini Tanga ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Fainali ya Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Oddo Ummy Cup ambayo yameandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kwa lengo la kuibua vipaji vya wachezaji wachanga.

Mashindano hayo hufanyika kila mwaka katika viwanja vya Lamore Jijini Tanga na yanashirikisha timu mbalimbali kutoka kwenye Jimbo la Tanga Mjini linaongozwa na Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya

“Leo nimekuja Tanga kwa lengo la kuja kuangalia viwango vya wachezaji ili baadae nimpiga simu kocha wa timu ya Taifa kuona namna nzuri ya kuweza kuwajumuisha kwenye timu zetu za Taifa”Alisema Waziri Ndumbaro.

Katika Fainali hiyo timu za Nguvumali na Kiomoni zilitinga hatua hiyo kwa kufanya vizuri kwa kila mmoja kumtoa mpinzani mwenzake na hivyo kulazimika kukutana kwenye hatua hiyo ya kumsaka Bingwa ambapo Bingwa alikuwa ni timu ya Kiomoni

“Kwa heshima ya Waziri Ummy Mwalimu nimeacha shughuli zote nimekuja Tanga mimi Waziri wa michezo ili niweze kuona vipaji vilivyopo hapa Tanga kwa maana historia ya mpira ni kubwa na nimeambiwa Juma Mgunda yupo hapa hivyo tunaweza kutumia mashindano haya kupata wachezaji wa timu ya Taifa”Alisema Waziri Ndumbaro.

Akubali Ombi la Mbunge Ummy

Katika hatua nyengine Waziri Ndumbaro amekubali ombi la Mbunge Ummy Mwalimu ambaye alimuomba atafute shule mmoja mkoani humo waifanye kuwa ya vipaji vya michezo.

Akijibu Ombi hilo Waziri Dkt Ndumbaro alisema kwamba yeye akisema wataona namna ya kwenda kulitekeleza ili uwepo wa shule hiyo uweze kupatikana mkoani Tanga.

“Mh Ummy nimepokea ombi lao wewe ukisema mimi ni utekelezaji tu hivyo nitakwenda kulifanyia kazi”Alisema.

Chuo cha Usafiri wa Anga(CATC) kimefanya hafla ya kufunga Kozi mbili za ‘Area Control Procedure’ namba 35 na Kozi ya Ndege nyuki (Drone) namba 16 kwa wakufunzi hao kuhimizwa juu ya kufanya kazi kwa weledi.

Nasaha hizo zimetolewa Machi 08, 2024 na Mkuu wa Chuo cha CATC, Aristid Kanje wakati wa kufunga kozi hizo mbili ambazo zimeambatana na mafunzo ya weledi yaliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Chama cha Wamiliki wa Mashirika ya Ndege nchini (TAOA) Bi Lathifa Sykes.

CATC moja ya vyuo vinavyotoa kozi ya Usalama wa Usafiri wa Anga (ASTC) na ni moja kati ya vyuo tisa vyenye sifa hizo Afrika na 35 duniani.