Salamu kwa mashabikiAkizungumzia siku yake ya kuzaliwa, baadhi ya wanamuziki wenzake wamempongeza kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa dansi kimataifa. “Kamanda Ras Makunja ni alama ya ubunifu na uthubutu. Bila yeye, muziki wa dansi ungekuwa tofauti kabisa kwenye ramani ya kimataifa,” alisema mmoja wa wanabendi.
Mwisho wa habari
Kwa sasa, shangwe na burudani zinaendelea kambini kwao FFU-Ughaibuni, huku mashabiki wakiungana kumtakia maisha marefu, afya njema na mafanikio zaidi katika safari yake ya muziki.
Happy Birthday Kamanda Ras Makunja! 🎉🎶
Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Mbwana Yusuph maarufu kama Mbosso, amewashukuru uongozi na mashabiki wa Simba Sports Club kwa kumpa nafasi ya kipekee kuwa headliner wa Tamasha la kihistoria la SIMBA DAY lililofanyika hivi karibuni.
Kupitia barua yake ya wazi aliyoiandika kwenye mtandao wa Instagram, Mbosso alisema uongozi wa Simba SC uliweza kumpa nafasi hiyo adhimu ambayo ingeweza kupewa msanii mwingine yeyote, lakini badala yake walimchagua yeye kuongoza burudani ya tamasha hilo kubwa.
“Kwangu mimi hili ni tamasha langu kubwa la kwanza kufanyia kwenye uwanja linalohusiana na mpira wa miguu katika maisha yangu ya muziki. Ndiyo maana nilijitahidi kwa uwezo wangu wote kuhakikisha nawapa furaha mashabiki na wadau wa Simba SC,” aliandika Mbosso.
Ameeleza kuwa SIMBA DAY kwake haikuwa tu tamasha, bali pia jukwaa la kuonyesha vipaji vyake vingine ambavyo huenda havijawahi kuonekana, ikiwemo kuigiza kwa uhalisia, kuimba na kuwasilisha ubunifu kwa kiwango cha juu.
Aidha, Mbosso alibainisha kuwa licha ya kutumia gharama kubwa kuhakikisha onyesho lake linafanikiwa, hakufanya hivyo kwa faida binafsi bali kwa mapenzi yake makubwa kwa Simba Sports Club na mashabiki wake.
“Nina imani mlifurahi, na kama kulikuwa na sehemu nilikosea au kulikuwa na mapungufu, naomba mnisamehe kwa kuwa mimi ni mwanadamu na siwezi kufanya vyote kwa ukamilifu,” alisema Mbosso huku akimalizia barua yake kwa kutia sahihi ya jina lake la kisanii Mad Max Mbosso Khan.
Tamasha la SIMBA DAY ni tukio la kila mwaka la Simba SC linalokutanisha mashabiki kutoka maeneo mbalimbali nchini, likiwa na lengo la kutambulisha kikosi kipya cha wachezaji na kutoa burudani ya muziki.






“Sherehe hizi ni sehemu ya kusherehekea safari yetu ya miaka 25 ya kuunganisha Watanzania. Tunataka tuendelee kushirikiana na wateja wetu si tu kupitia huduma za kidijitali, bali pia kwa kutengeneza kumbukumbu za pamoja za furaha na mshikamano,” alisema Venanty.
Vodacom imesisitiza kuwa itaendelea na mfululizo wa matukio ya kusherekea miaka 25 yake katika mikoa mbalimbali nchini, ikilenga kuimarisha uhusiano wa karibu na wateja wake.

Na Mwandishi Wetu, Arusha.
.jpeg)


















.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)




















