Dar es Salaam Desemba 24 2025: Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam limetangaza kuwa Kardinali Mstaafu wa Jimbo hilo, Kardinali Polycarp Pengo, anakabiliwa na changamoto za kiafya na anatarajiwa kusafiri kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu zaidi.Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Askofu Thaddaeus S. Ruwa’ichi OFMCap, Kardinali Pengo amekuwa akipatiwa matibabu nchini kwa muda, hata hivyo hali yake imehitaji huduma za kitaalamu zaidi zitakazopatikana nje ya nchi.
“Baada ya juhudi za kimatibabu hapa nyumbani, imeonekana kuwa kuna haja ya kumpa matibabu ya hali ya juu zaidi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa Desemba 24, 2025.
Kanisa limeeleza kuwa mipango yote ya safari na matibabu imekamilika, na kwamba Kardinali Pengo atasafiri kwenda India kwa lengo la kupata huduma bora zitakazomsaidia kurejea katika hali njema ya afya.
Aidha, waumini na watu wote wenye mapenzi mema wametakiwa kuendelea kumuombea Kardinali Pengo ili Mungu amjalie nafuu ya haraka na kumrejesha salama nchini.
Katika taarifa hiyo, Askofu Mkuu pia ametumia nafasi hiyo kuwatakia waumini wote Heri ya Krismasi na Baraka za Mwaka Mpya 2026, akisisitiza umuhimu wa mshikamano na sala katika kipindi hiki.
Taarifa hiyo imesainiwa na Askofu Thaddaeus S. Ruwa’ichi OFMCap pamoja na Katibu Mkuu wa Jimbo, Padre Vincent Mjwaji.


WATAALAM wa huduma za mionzi Katika vituo vya Afya wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya mionzi ili kuepuka kiwango kikubwa kinachoweza kuleta madadhara kwa wagonjwa na wataalam husika.

Rai hiyo imetolewa na 19 desemba 2025 Peter Pantaleo Kaimu Mkuu Ofisi ya Kanda ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania kwa wataalama wa Radiolojia zaidi ya 90 waliopatiwa mafunzo yaliyoandaliwa na TAEC,na kuwataka kuwa makini na kufuata viwango vilivyowekwa kitaalam ili kulinda Afya ya wagonjwa na watoa huduma.
Pantaleo alisema kuwa matumizi makubwa ya mionzi yanamadhara makubwa zaidi ukilinganishwa na kidogo, hivyo amewashauri wataalam hap kuwa makini zaidi, na kutambua wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum zaidi ikiwemo Kuwakinga wagonjwa pamoja na wale wanaoambatana na ndugu zao hospitalini wakati wanapopatiawa huduma za mionzi.
"Ni Imani yetu kwamba mlichojifunza mta kwenda kukifanyia kazi nanyi mtakuwa mfano bora na kioo kwa wenzenu, na mafunzo haya ni muhimu sana kuhakikisha u salama wenu pamoja n wagonjwa mnaowahudumia pamoja na watu wengine waliopo mazingiellra ya hospitalini. Alisema Pantaleo.
Mungubariki Nyaki ni mkufunzi wa mafunzo TAEC , amewataka waajiri kuendelea kuwaruhusu walaalam wa Rdijioloji kupata mafunzo kwani ni muhimu Katika Kada hiyo ili waweze kutoa huduma Bora kwa wagonjwa kwa kuzingatia matumizi sahihi ya mionzi sawa sawa na mwongozo wa kitaalam na kisheria.
Nyaki amesema kuwa mafunzo hayo yalilenga kuwaelimisha wafanyakazi wanaofanya Katika kitengo cha Rajiolojia kwenye mahospitali yote nchini ikiwa ni pamoja na kufahamu zaidi juu ya mionzi na kazi wanazozifanya kwaajili ya kuwasaidia wagonjwa, kuwa makini zaidi na wao wenyewe na wale ambao hawapo. Kwenye kitengo hicho
"Mafunzo haya yanafanyika Kila mwisho Wa Mwaka na yanatolewa Katika awamu mbili, (a) yana kuwa ni yale ya kawaida (basic) (b)Yale ya kuwa Katika level ya juu (advanced training program) Alisema. "
Amesema TAEC inawataka kutambua kuwa ni sheria wafanyakazi hao kupatiwa mafunzo kama sheria inavyoelekeza , hivyo amewashauri wale ambao hawajafika kwaajili ya mafunzo wafanye hivyo kwaajili ya kupata uwezo zaidi na kujenga ushirikiano
Amesema TAEC inahamasisha Matumizi salama ya mionzi hivyo jamii isiogope kupata huduma hiyo kwani yapo salama ni kwaajili ya matumizi ya kuchunguza magonjwa na kufanya matibabu
Amesema changamoto Kubwa ni baadhi ya Taasisi wanamtazamo kwamba wanapoteza fedha kwa kuwaleta wapate Elimu jambo ambalo siyo sawa,
Peter Pantaleo Kaimu Mkuu Ofisi ya Kanda ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania akizungumza na wataalam wa Radiolojia zaidi ya 90 waliopatiwa mafunzo yaliyoandaliwa na TAEC
Wataalam wa Radiolojia zaidi ya 90 waliopatiwa mafunzo yaliyoandaliwa na TAEC kutoka Katika hospitali mbalimbali nchini

.jpeg)


Meneja Mauzo wa Vodacom eneo la Makambako mkoani Njombe, Elly Mwambene (kulia), akikabidhi kapu la sikukuu kwa mmoja wa wateja wao Sigfrid Lomanus Chaula (kushoto), katika muendelezo wa kampeni ya “Tupo Nawe Tena na Tena” inayolenga kugawa makapu kwa wateja katika msimu huu wa sikukuu. Kampeni hiyo imeendelea kugawa makapu hayo katika mikoa mbalimbali nchini, Tukio hili limefanyika kwa lengo la kusherehekea pamoja na wateja katika msimu huu wa sikukuu, sambamba na kuhitimisha maadhimisho ya miaka 25 ya Vodacom tangu kuanzishwa kwake hapa nchini, na limefanyika mjini Makambako mwishoni mwa wiki.
Mpogolo aliyasema hayo wilayani Ilala wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu kwa madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, yaliyolenga kuwajengea uwezo katika utekelezaji wa majukumu yao.
Mpogolo alisisitiza kuwa mafunzo hayo yanapaswa kuwa na tija kwa wananchi kwa kuwahudumia kwa ufanisi katika maeneo yao. Alisema kiongozi anayefahamu changamoto za wananchi hawezi kuona ni mzigo kuwahudumia.

.jpeg)

.jpeg)














.jpeg=w378-h243-p-k-no-nu)





