Friday, July 17, 2009

GROOVEBACK


THIS SATURDAY, 18TH OF JULY, KUANZIA SAA 3 USIKU

AT ZHONG HUA GARDEN, GROOVEBACK NITE With DJ PETER MOE/KELVIN/RANKIM Wanakuletea ‘’BACK TO THE 80S SPECIAL’’

COME N KICK WITH US……

Kwa KIINGILIO CHA SH 5000/=TU..

BAJAJ

Bajaj usafiri wetu wa kujidai mjini, hakuna asiyeufahamu. Hata madereva wa taix wanazijua bajaj.

MISS ILALA WAINGIA KAMBINI KWA KISHINDO!

Baadhi ya walibwende wa miss Ilala wakiwa katika mwendo wa maringo! kutoka kulia ni Zena Rashidy (22), Slyvia Shally (19) pamoja na Irene Karugaba (19).

Baada ya kuwatembelea warembo ambao ni washiriki wa Miss Ilala 2009 kambini kwao katika hoteli ya Lamada, Ilala jijini Dar es Salaam, shukrani zimwendee mwenyekiti wa kamati ya miss Ilala, Bw. Jackson Kalikumtima.
Walimbwende hao tayari wameingia kambini juzi kwa ajili ya kujinoa vyema tayari kwa kushindana.

ARTI-TZ NEWS LETTER


Monday, June 29, 2009

KARIBU SABA SABA BANDA LA ARTI-TZ


Tunapatikana Saba saba, ndani ya Banda la Maliasili na Utalii,
Karibu sana ujionee teknolojia mbali mbali.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa simu

+255 (0) 713 234 604
+255 (0)786 427 949
+255 (0) 713 797 465

Au ofisi kwetu;

Appropriate Rural Technology
Institute (ARTI-TZ)
Tupo karibu na Massana
(MHS) Hospital
Barabara ya Goba, Mbezi Beach
Dar es Salaam, Tanzania
E-mail: arti.tanzania@gmail.com

Friday, June 26, 2009

CHANNEL O PAYS TRIBUTE TO KING OF POP

Channel O is paying tribute to Michael Jackson in the most fitting way possible – by a video mix and so much more - featuring hit after massive hit from the global icon.

The 30-minute specialised O-Xpress will provide a platform for the universally acknowledged King of Pop’s astonishing array of hits, starting on Saturday 27 June at 09:30 CAT on DStv.

The Michael Jackson O-Xpress tribute will also air at 12:00 CAT and 17:00 CAT and will continue on Sunday June 28 (12:00 CAT and 17:30 CAT), Monday June 29 (13:00 CAT) and Tuesday June 30 (11:00 CAT).

Hit songs like Thriller, Beat It, Billie Jean, Black and White, Scream, Wanna Be Startin' Somethin', I Just Can't Stop Loving You, Bad, The Way You Make Me Feel and You Are Not Alone will be showcased in this unique video mix.

O-Boma (16:00 CAT) and O-Boma Xpress (from 22:00 CAT) will be dedicating today’s live shows to the man.The poll question is – “What is your all time Michael Jackson track?”

Alongside the music, it was Jackson’s dancing – most ironically the Moonwalk – that ensured even his early videos would be something special, and over his career he took care to push the benchmark when it came to creating the visuals to go with his endless supply of hit songs.

Over the course of his career, Jackson sold more than 750m albums worldwide and won 13 Grammy awards. Channel O joins in the other thousands of voices around the world mourning the loss of this one-of-a-kind entertainer and truly gifted musician.

Channel O is available across the continent on DStv channel 320.

Tuesday, June 16, 2009

Mustafa Hassanali Collection At ARISE AFRICA FASHION WEEK 2009

Greating from JohannesburgThank You for all the Support you have shown In not only Supporting my work but that of Tanzania Fashion Industry at Large.

"MDUARA" Mustafa Hassanali launched his PrĂȘt a Porter Spring/Summer 2009/10 Collection “Mduara” on 14 June at the Arise Africa Fashion Week.
The collection has been inspired by the sacred, savoury, significance, Sensual, soulful, synergetic Rhythms of our Swahili nation Mustafa Believes “The Vibrancy of our Music, Culture, myths and Believes form an integral part of our being hence “Mduara” The Local Dance Rhythms which has Inspired this ready to wear Women Collection which is An eclectic mix of Tradition meeting Modernity and Vice versa” The Collection Comprised of Ready to wear structured Kitenge (Printed Cotton) and flowing Chiffons accessorised by Mustafa Hassanali Signature Bling.
With this I would Like to thank Almighty for leading my path, You the Media without whom My creativity would go Unnoticed, Africa Fashion International and Arise Africa Fashion week, Vodacom, 1Time Airline, TBC, My friends and the Staff at Mustafa Hassanali who worked tirelessly to realise the collection. God Bless you all Ameen. Warmest wishes Yours sincerely Mustafa Hassanali

Thursday, June 11, 2009

UZINDUZI WA MASHINE MPYA ZA CT-SCAN NA X-RAY

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,DkAmani Abeid Karume,(katikati) Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Shamsi Vuai Nahodha,wakipata maelezo kutoka kwa Mtaalam Mzalendo Dk Khamis Abrahman kuhusu Mashin ya CT-Scan,inayochunguza matatizo mabli mbali ya Binadamu huko Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja jana.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,wapili kushoto),pamoja na Viongozi wengine wakiangalia matokea ya vipimo na picha,baada ya kuchnguza mgojwa kwa kutumia mashine ya CT-Scan,ambayo huchunguza magonjwa mbali mbali katika mwili wa Binadamu hoko,katika hopitali Kuu ya Mnazi Mmoja,mara baada ya kuzindua mashine za CT-SCAN na X-RAY.

Picha na Ramadhan Othman Ikulu.

Jeff Msangi: Jinsi Ya Kuamsha Na Kulinda Ari

Jinsi ya kuamsha na kulinda ari ya kutimiza malengo yako

Na Jeff Msangi,

Kila mtu ana malengo. Tunachotofautiana ni jinsi tunavyofafanua malengo yetu na mbinu tunazozitumia ili kutimiza malengo yetu. Iwe ni kumaliza madeni uliyonayo, kuwekeza pesa kwa ajili ya kuchukua likizo ndefu,utajiri,familia bora,ndoa nzuri iliyojaa furaha,watoto wenye heshima na adabu, kufanya mazoezi ili kuwa na afya njema zaidi nk yote ni malengo ambayo binadamu hujiwekea mara kwa mara katika safari ya maisha.

Wengine hufanikiwa na wengine hushindwa. Furaha,mafanikio na maendeleo maishani ni vita ya kudumu.Kuna kupanda na kushuka. Cha msingi ni jinsi mtu anavyokabiliana na hali halisi katika wakati halisi.
Kama ambavyo nimeshaandika katika makala zangu za siku za nyuma,kujiwekea na kufafanua vizuri malengo yako ni sehemu muhimu sana ya maisha,maendeleo na mafanikio.

Ni lazima ujue unataka kufanya nini,kwanini na kwa namna au mtindo gani. Malengo ya uhakika ni kama vile kuwa na uhakika na unapotaka kwenda. Usipojua unapotaka kwenda kamwe hutokuwa na uhuru wa kusema “umepotea” kwani hata ulikuwa hujui unapotaka kwenda!Umepoteaje?

Ulikuwa unataka kwenda wapi? Maswali magumu.
Lakini pamoja na malengo ni lazima pia pawe na tamaa au ari ya kutimiza malengo hayo.

Hapo ndipo swali la kwanini linapokuja. Kwanini unatamani utajiri? Kwanini unataka kuwa mwanafunzi bora kushinda wengine wote?Kwanini? Tunapojiuliza maswali kama hilo la kwanini,inatusaidia kuamsha tamaa au ari.Tunakumbuka zaidi malengo yetu na yanakuwa ya uhakika zaidi.Tunajua tunapotaka kwenda na sababu za safari yetu tunazo.

Hata hivyo, mara kwa mara mambo mbalimbali hutokea maishani ambayo yanaweza kutukatisha tamaa. Hapo ndipo tunapohitaji motisha kama ambavyo niliongelea wiki kadhaa zilizopita.

Sasa ili kuhakikisha kwamba siku zote unabakia kuwa katika mstari mnyoofu kuelekea kwenye malengo yako, yapo mambo mbalimbali (unaweza kuyaita maandalizi ukipenda) ambayo unaweza kufanya ili kuhakikisha kwamba safari yako kuelekea kwenye kutimiza malengo yako inakuwa ngumu(siku zote ni ngumu) lakini yenye mbinu mbalimbali za kukabiliana na ugumu wowote utakaojitokeza.Hicho ndicho ninachotaka kuongelea hivi leo; ufanye nini ili usikate tamaa katika kuelekea kwenye malengo yako?

Chagua malengo yanayofaa: Kama nilivyotangulia kusema,tuna malengo tofauti hapa duniani. Jambo la msingi ni kuchagua malengo yanayokufaa.Ni lazima kujifanyia uhakiki binafsi na kujikosoa kwa dhati.Unataka kufanya nini au kuwa kama nani? Unavyo vitendea kazi(vikiwemo vya kimaadili) ili kutimiza malengo yako?Umechagua malengo yanayofaa na hata kukubalika katika jamii yako?Yapo maswali kadhaa(mfano tu) ambayo yanaweza kukusaidia katika kuchagua malengo yanayokufaa

-Je ulimwengu usingekuwa na kitu “pesa” bado ungetaka kutimiza lengo ulilonalo?

-Je tayari umeshaanza kuyafanyia kazi malengo uliyonayo?

-Je ningekupatia Tshs Bilioni moja hivi leo bado ungeendelea kushikilia malengo uliyonayo?

Kama umejibu Hapana katika swali moja au yote hapo juu,una haja ya kuyakagua upya malengo yako. Swali la mwisho hapo juu ni muhimu sana kwani pengine hutopenda kusikia nikikuambia kwamba pesa haitokupa furaha maishani.Kinachoweza kukupa furaha ni ile process ya kuzipata pesa.Hili nitakuja kuliongelea kwa undani katika siku za mbeleni.

Tambua kwamba unaweza kufanya unachotaka kufanya: Ukimuuliza mtu yeyote ambaye tayari ana malengo kwamba ni kwa kiasi gani na kwanini angependa kutimiza malengo aliyonayo, utasikia hadithi nzuri na ndefu ya jinsi ambavyo maisha yake yangebadilika endapo itatokea akatimiza malengo yake. Sasa jiulize, ni kwanini hatimizi malengo yake?

Nini kinamzuia? Au nikuulize wewe msomaji,nini kinakuzuia? Jibu rahisi ni kwamba kama ilivyo kwa wengi wetu,hatuamini kwamba tunaweza kufanya tunachotaka kufanya.

Kwa hiyo tunabakia kuwa na “ndoto za malengo”.Hatuthubutu hata kujaribu!Tunaingiwa na woga. Tunawaza jinsi tutakavyoshindwa kama tutajaribu. Tunaona jinsi tutakavyochekwa,tutakavyodhihakiwa nk.
Kwa hiyo ni lazima ujenge kwa ndani imani kwamba unaweza,inawezekana na hakuna cha kukuzuia.

Kama alivyowahi kusema bwana mmoja aitwaye David Deida; “Kitu pekee kinachofanya ndoto zisitimie ni uoga wa kushindwa”. Usikubali.
Weka Nukuu za Mafanikio ya Wengine:

Uwezekano ni mkubwa sana kwamba kile unachotaka kufanya au ambacho ndio malengo yako,mafanikio yako, tayari kuna mtu au watu ambao wameshakifanya hapa duniani. Ni kina nani? Wao walifanyaje? Ni kitu gani kiliwasaidia kufanikiwa au kufikia walipofikia?

Hayo ni baadhi tu ya maswali ambayo ni muhimu ukayapatia majibu kwani majibu hayo bila shaka yatakusaidia katika safari yako.Pia kwa kuona na kujifunza kutoka kwa wengine, itakupa ari na moyo zaidi kwamba inawezekana. Kama wao walifanya na wakafanikiwa,kwanini wewe ushindwe?

Tafuta Wenzako Wenye Malengo Sawa na Wewe: Mojawapo ya mambo yanayoleta faraja au ahueni katika maisha yetu ni pale unapokutana na mtu ambaye ana “matatizo” au mtu mwenye “misheni” sawasawa na yale uliyonayo.

Ahueni inakuja pale unapogundua kwamba kumbe haupo peke yako.Kunakuwa na nafasi ya kujifunza kutoka kwa uzoefu wa wengine.
Hali ni hiyo hiyo kama unatamani mafanikio na hutaki kukatishwa tamaa njiani.

Jaribu kutafuta marafiki au watu ambao mnafanana katika mawazo na malengo.Ukishawapata nenda nao sambamba. Shirikiana na pia saidiana nao.Mara nyingi motisha hutoka kwa watu kama hao.Jipime mwenendo wako kuelekea katika mafanikio kwa kujilinganisha nao.Shindana nao ikibidi.

Kwa ufupi kila mmoja wetu,ukiwemo wewe unayesoma makala hii, ana uwezo wa kujiwekea malengo na kuyatimiza. Amini kwamba unaweza kufanya unachotaka kukifanya.Amini kwamba malengo uliyonayo yanaweza kufikiwa(kumbuka kujiwekea malengo halisia au yanayotimizika).

Tafuta wenzako ambao aidha wameshafanikiwa au walio njiani kufanikiwa.Angalia mienendo yao.Waulize na upate majibu kutoka kwao ikiwezekana.

Soma habari zao iwe ni magazetini au mitandaoni.Kumbuka kama wao wameweza basi hakuna cha kukuzuia.Kuwa jasiri katika malengo yako.Wapo watakaojaribu kukuyumbisha na kukukatisha tamaa. Usiwajali.Mwisho kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza siku zote;Fanya kazi kwa bidii,uadilifu na maarifa.Tuonane wiki ijayo.

Jeff Msangi ni Mhariri wa mtandao wa www.bongocelebrity.com Unaweza kuwasiliana naye kupitia makala@bongocelebrity.com

HENRY MDIMU AKUTANA NA ANKO MO, FACE TO FACE

Zee la nyeti Henry Mdimu wa Mwananchi Communication akiwa na Anko Mo- wa Tanga walipokutana mjini humo.
Ukitaka mtembelee http://www.ankomo.blogspot.com/

WALIOPATA ULEMAVU MBAGALA KULIPWA MAFAO YAO MILELE

SERIKALI imeahidi kuwalipa mafao kwa muda wa maisha yao yote, watu wote waliopata ulemavu wa aina mbalimbali kutokana na milipuko ya mabomu iliyotokea katika ghala la silaha la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Aprili 29, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Wiliam Lukuvi, alisema watu hao watalipwa fidia kulingana na madhara yaliyowapata.

Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa Serikali ipo pamoja nao kwamba na itawasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku.

Alifafanua kuwa mafao watakayokuwa wakilipwa watu hao , yatajulikana baada ya wataalamu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutoa mchanganuo wa kile wanachostahili kuwa wanalipwa kulingana na aina ya ulemavu waliopata.

"Wizara ya Afya ndio inahusika na kufanya hesabu, nimewaagiza watuletee idadi kamili ya watu waliopata ulemavu wa kudumu pamoja na mapendekezo yao," alisema Bw. Lukuvi.

Alisisitiza kuwa taarifa hiyo itaambatana na ile tathmini ya maafa itakayotolewa Juni 13, mwaka huu.

Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa yupo makini kwa kuwa anaguswa na maafa yaliyowapata wakazi wa Mbagala.

Kuhusu vurugu zilizotokea wakati wa ugawaji misaada kwa waathirika wa mabomu, Bw. Lukuvi alisema kazi ya kusimamia ugawaji wa misaada hiyo ameachiwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bw. Said Mkumbo.

BUSANDA OYEEEEEEEE!!!!


Mbunge mteule wa Jimbo la Busanda (CCM), Lolesia Bukwimba, amepishwa ndani ya ukumbi wa bunge muda mfupi uliopita huku kambi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ikipuuza vikali uapishaji huo na kudai hawautambui.

Wakati hayo yakitokea wabunge wa CCM walimsindikiza ndani ya ukumbi wa bunge, wakiimba: “ CCM,…CCM..CCM.”

Katika msafara huo ambao mbunge mwanaume alikuwa ni William Ngeleja pekee, wabunge hao waliendeleza shamrashamra hizo hadi karibu na eneo la kiapo ndipo wakarejea katika viti vyao.
Wakiwa katika viti vyao, baada ya Bukwimba kula kiapo, vilisikika vigelegele, nderemo na vifijo.
Nderemo hizo na vifijo, vilisikika huku kukiwa na maneno ya chini kwa chini ambapo sauti ya Waziri wa Nchi (Ofisi ya Rais Utawala Bora) Sophia Simba, ilisikika akichomekea maneno kama: “Habari ndiyo hiyo…”“Chadema wako wapi, wameingia mitini… Chadema mpo?…”

Tuesday, June 9, 2009

ISANGA FAMILY

ISANGA FAMILY Show kazi a.k.a Mabegi bila nauli, wanawakilisha.

Mustafa Hassanali to Showcase at “ARISE AFRICA FASHION WEEK”


Mustafa Hassanali Talking to the Press to his right by Vodacom marketing Manager Emilianm Rwejuna.
*Launch of Mustafa Hassanali Ready to Wear Collection Named “MDUARA”
*Tanzania Media to Cover Mustafa Hassanali Showcase

Mustafa Hassanali, Tanzania’s renowned Fashion Designer has been invited to the inaugural Arise Africa Fashion Week by Africa Fashion International to be held from June 12- 19, 2009 at the Sandton Convention Centre in Johannesburg, South Africa.

Arise Africa Fashion week shall feature 52 designers from 21 African Countries over a period of 8 Days. Mustafa Hassanali is among the invited designers from Tanzania. This shall be his Seventh Showing in The Republic of South Africa.

(M’Net Face of Africa Finals November 2008 Sun City, Tanzanite One Jewellery Showing in Cape Town during Mining Indaba 2007, Durban Fashion week 2006, Cape Town Fashion week 2005 & 2006 and Vukani Fashion Fair and awards in Pretoria 2004).

Mustafa Hassanali Says “This is a perfect Platform not only for networking but to look at diverse Market opportunities hence the diversification into the Ready to wear market segment” Mustafa Hassanali shall launch his PrĂȘt a Porter Spring/Summer 2009/10 Collection “Mduara”.

The collection has been inspired by the sacred, savoury, significance, Sensual, soulful, synergetic Rhythms of our Swahili nation Mustafa adds “The Vibrancy of our Music, Culture, myths and Beliefs form an integral part of our being hence “Mduara”.

The Local Dance Rhythms has inspired this ready to wear Women Collection which is an eclectic mix of Tradition meeting Modernity and vice versa”

Mustafa Hassanali’s commitment is to not only to promote the creative sector Industry especially Fashion in Tanzania, but also emphasise the Made in Tanzania Concept. He will be accompanied by A Media Contingment that Shall Not only Cover his Showcase on 14 June but also report on the behind the Scenes of the Arise Africa Fashion Week.

The tour of the Media Contingment has been sponsored by Vodacom (www.Vodacom.co.tz), Tanzania Broadcasting Corporation (www.tbcorp.org) and 1time Airlines (www.1time.co.za).

JIUNGE g5click.com


G5 inatumaini upo pouwa. G5 entertainment company inaomba msaada wako kutangaza mtandao wa marafiki wa G5 world katika blogspot yako.. http://www.g5click.com/
Mtandao wa G5 unawezesha watu kutoka sehemu mbalimbali kukutana, kuchat, kushare videos, miziki na mambo mengine mbalimbali
G5 contacts: Email: info@g5click.com or clickg5@gmail.com Web:
http://www.g5click.com/ or m.g5click.com
Phone: +255-714-204-490, +255-713-794-343
Wadau wako kutoka G5 CLICK ENTERTAINMENT COMPANY
******* Tumeattach image ya G5 Advert *********

Mustapha B. Selemani
Production Manager
G5 Entertainment Company
Dar Es Salaam, Tanzania

Saturday, June 6, 2009

HESHIMA NA UVUMILIVU UMENIFANYA NIFIKE MBALI -MSANII ELIAS BARNABAS




Kijana machachari katika fani ya muziki wa kisasa kwa hapa bongo tunauita muziki wa kizazi kipya, Elias Barnaba aka Barnabas aliyetamba sana na nyimbo yake 'Njia Panda' amesema kwamba heshima na uvulimu alionao ndio chanzo cha mafanikio yake kiasi cha kualikwa na mwanamuziki maarufu wa Kongo Fally Ipupa kurekodi nyimbo pamoja. Pichani Barnabas akiwa na Dorine aka Pipi.

Kijana machachari katika fani ya muziki wa kisasa kwa hapa bongo tunauita muziki wa kizazi kipya, Elias Barnaba aka Barnabas aliyetamba sana na nyimbo yake 'Njia Panda' amesema kwamba heshima na uvulimu alionao ndio chanzo cha mafanikio yake kiasi cha kualikwa na mwanamuziki maarufu wa Kongo Fally Ipupa kurekodi nyimbo pamoja.


Barnabas alizaliwa miaka 19 iliyopita katika jiji la Dar es Salaam ,wazazi wake wakiwa wenyeji wa mkoa wa Morogoro kabila la wapogoro.


Elias akiwa mtoto wa kwanza katika familia yao alipata bahati ya kumaliza elimu ya msingi na baada ya hapo alijiunga na sekondari ya Mikoji ambapo aliacha shule alipokuwa kidato cha pili na kuamua kujikita katika fani ya muziki.

Uamuzi wake huo ulipingwa vikali na wazazi wake ambao walitegemea angejikita zaidi kwenye elimu kwa kuwa waliamini elimu ndio msingi wa maisha.

Katika kipindi chote hicho Barnabas alijikita zaidi kwenye muziki kwa kuwa ndio ulikuwa hobi yake ingawa alikuwa hajui apitie wapi ili afike kileleni.Mambo yakienda tofauti na alivyotegemea Barnabas aliamua kufanya maonyesho mbalimbali katika kumbi tofauti za hapa bongo Dar es Salaam.

Mungu si Athumani mwaka 2007 alifanikiwa kusaini makataba katika Shule ya kukuza vipaji vya muziki hapa nchini Tanzania House of Talent (THT) shule hiyo ipo chini ya Mkurugenzi Ruge Mutahabwa.


Barnabas alisema kwamba jukumu la kwanza la THT lilikuwa ni kumsaidia kimawazo na kumpa elimu ya muziki ambayo hivi sasa anamini kabisa ndio chanzo cha mafanikio yake.


Elias Barnabas tayari ameshatunga nyimbo zaidi ya kumi kiasi cha kumfanya awe na albamu ambayo mpaka sasa hajaipa jina wala kufanya uzinduzi, lakini tayari nyimbo zilizomo katika albamu hiyo zimeshaanza kukonga nyoyo za watanzania.Barnabas anatamba hivi sasa na nyimbo yake ya NJIAPANDA akiwa amemshirikisha mwanadada Dorine Kasia Pipi.


Nyimbo nyingine za Barnabas ni Kodi mangasubi, mbalimwezi, nivumilie, nimelimiss, beby i love, mdomo, mwongo, dukuduku na huruma. Wimbo wa Njiapanda umekubalika sana kiasi cha kumfanya ashindwe hata kupata siku ya mapumziko kutokana na mialiko mingi katika matamasha.


Barnabas anasema kuwa hali hii imemfanya ajitume ili aweze kuwa kama wengine ambao kwa sasa wana mafanikio makubwa ya kimuziki. Kutokana na kipaji alicho nacho Barnabas na gwiji la muziki wa dansi toka nchini Kongo Fally Ipupa alimwagia sifa kibao Barnabas na kumwahidi atarekodi naye nyimbo na kumtumia mialiko ya kwenda nchini Kongo.


Ipupa alikutana na Barbas wakati alipokuja Tanzania kufanya shoo pamoja na Mbilia Bel mwaka jana.

Monday, May 4, 2009

HUTU NDIYE MWANZILISHI WA BLOG TZ


Mwanzilishi wa Blog nchini Tanzania...Bw. Muhidini Issa Michuzi. Kwa maelezo zaidi unaweza kutembelea www.issamichuzi.blogspot.com

Monday, April 6, 2009

WANGARI MAATHAI REVEALED ON CNN

Tune in this April, as global news channel, CNN features Wangari Maathai, Nobel peace laureate, Kenyan conservationist and human rights activist on DStv.
Airing on Wednesday April 15 at 10:30 CAT the program, Revealed, follows Wangari now almost 70 who continues to travel the world tirelessly spreading her message that global citizens must protect and cherish the planet's limited resources. Wangari grew up walking among trees, and today she walks among the world's leaders.
Revealed follows Wangari to London, where she meets British Prime Minister Gordon Brown to launch the Congo River Basin Fund, an initiative aimed at helping combat the rapid deforestation of the rainforest in central Africa.
The British PM introduces Wangari as "a great leader, an incredibly courageous woman, who is an encouragement to anyone who cares about our planet".
Revealed also joins Wangari on a number of projects around the world from Japan to London to Kenya to Washington, where she gives speeches, meets with officials, plants trees with children and delights old friends and fans with her presence, inspiring people to do what they can to "help the planet heal".
Tune in for Revealed on Wednesday April 15, (10:30 CAT), Saturday April 18 (09:30 CAT and 20:00 CAT) and on Sunday April 19 (06:30 CAT and 19:30 CAT) on CNN, channel 401, on DStv.