Thursday, May 23, 2013

HALI YA MJI WA MTWARA BADO NI TETE MABOMU YAENDELEA KULINDIMA, MPAKA SASA WATU 91 WAMEKAMATWA

Habari zilizofikia toka Mtwara na kudondokea dawati letu la habari Kajunason Blog, hali ya mji wa Mtwara bado si shwari ambapo mpaka sasa nyumba kadhaa za wananchi, vibanda vya biashara katika eneo la Mgomeni zimeteketezwa kwa moto tokea asubuhi na nyingine zinaendelea kuteketea.

Kwa mujibu wa mwandishi wetu aliyepo eneo la tukio anasema hali bado tete huduma za kijamii katika mji huo zimesimama zikiwemo usafiri, huduma za kibenki na shule huku wasafiri kutoka jijini Dar es Salaam wakidaiwa kukwama katika eneo la usijute wakihofia kuingia mjini humo.

Taarifa za polisi zinasema kuwa mpaka sasa jumla ya watu 91 wamekamatwa huku wengine wakiendelea kukamatwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo. Kwa habari zaidi kuhusiana na vurugu hizo endelea kuunga nasi.

RIPOTI TOKA KWA BARAKA UFUNGUO, MTWARA.
-Mwanafunzi wa CHUNO afikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni.

-Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza na uhalifu ukifanyika vidole vinawaelekea Polisi.

-Afisa Usalama wa Taifa ambaye anamiliki nyumba ya wageni naye amevamiwa na kuporwa mali ikiwamo fedha katika gesti yake. Haijajulikana ni kiasi gani cha mali kilichopotea.

-Mabomu yanaendelea kupigwa tofauti kwa sasa hayapigwa mfululizo.
Mabomu yametulia. Hali ya ukimya imetawala.

-Mabasi 5 ya Champion yamebeba Wanajeshi yako njiani yanakuja.
Serikali yatoa tamko yasema watu 91 wanashikiliwa.

-Bunge laahirishwa tena. Kupisha uchunguzi na kuepusha uchochezi kutoka kwa baadhi ya wabunge. (Kwa mujibu wa Spika).

-Maeneo ya Magomeni, Chikongola, Nkanaledi, Mikindani maaskari wanaingia majumbani mwa watu na kumsomba mtu yeyote ambaye ni mwanaume awe amehusika awe hajahusika na kumkamata. Pia inaripotiwa na uhalifu unafanywa na maaskari hao hao. Jambo linaloamsha hisia kwa wananchi.

-RPC anaongea na vyombo vya habari na kuwasihi wananchi waende makazini. Lakini kiuhalisia hali sio shwari.

-Mahakama ya mwanzo ya Mitengo imechomwa moto, mpaka sasa ni vita baina ya wananchi na maaskari. Mabomu yamesikika pamoja na milio ya risasi masaa 24. Na milio ya Risasi na mabomu inaendelea kusikika.

-Raia wapatao 7 wameripotiwa kufariki (wengine walipelekwa hospitali ya Ndanda Ndogo na mmoja ameripotiwa kupokelewa Ligula.

-Nyumba za viongozi zinaendelea kuchomwa moto, Majibizano baina ya Polisi na Raia yanaendelea maeneo ya Magomeni, Nkanaledi na Mikindani.

-Maduka yamefungwa na hakuna huduma zozote

-Barabara zimewekwa vizuizi magogo na matairi yamechomwa moto. Hakuna njia ya kupita.

TANZANIA ALL FEMALE STARS -KIDOLE KIMOJA (FISTULA SONG).

SHULE ZA KATA ZAENDESHWA KWA FEDHA ZA WALIMU WAKUU

Na Thehabari.com, Rombo

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT), Wilaya ya Rombo kimesema shule nyingi za Sekondari za Kata wilaya hiyo na maeneo mengine nchini zinajiendesha kwa kutegemea fedha za mifukoni kwa walimu wakuu wanaoziongoza shule hizo.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa CWT Wilaya ya Rombo, Erasmo Mwingira alipokuwa akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi. Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na gazeti hili hivi karibuni kwa kutembelea shule kadhaa za sekondari wilayani hapa umebaini kuwepo na mazingira magumu ya uendeshaji wa shule hizo kutokana na ugao wa fedha za uendeshaji shule hizo kutokuwa wa uhakika huku hata kiasi kinachozifikia hakitoshelezi gharama za uendeshaji.

Akifafanua Mwingira alisema fedha zinazotolewa kuziendesha shule hizo 'capitation' licha ya kuwa hazitoshi huwa hazifiki kabisa shuleni hali ambayo huwafanya walimu wakuu kubuni mbinu mbalimbali za uendeshaji wa shule zao ikiwemo kuweka utitiri wa michango kwa wazazi ili kuhakikisha mambo yanakwenda shuleni.
"Sasa hivi shule za msingi na sekondari (za serikali) zinaendeshwa na mifuko ya walimu wakuu...capitation haifiki kabisa shuleni, fedha inayowafikia ni kidogo sana na haiwezi kuendesha zile shule, walimu wanatumia mbinu zao kuziendesha shule ndio maana unaona michango inakuwa mingi shuleni," alisema Mwingira.

Alisema licha ya serikali kusema ada ya sekondari ni shilingi 20,000 kwa sasa michango katika shule hizo ni mingi kiasi cha kufikia 120,000 jambo ambalo limewafanya baadhi ya wazazi kuelemewa na mzigo wa michango na wengine kushindwa kabisa kuimudu.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi katika shule za Sekondari za Tanya, Nduweni, Urauri, Holili na Ngaleku na nyinginezo zote za wilayani Rombo umebaini uwepo wa utitiri wa michango jambo ambalo limelalamikiwa na baadhi ya wazazi na wadau wa elimu wilayani hapa. Mfano shule ya Sekondari Tanya jumla ya michango yake imefikia sh. 115,000; mgawanyiko wake ukiwa kama ifuatavyo:- Ada sh 20,000, Madawati sh 15,000, Chakula sh 60,000, Tahadhari sh 5,000, Ulinzi 5,000, Taaluma sh 5,000 na Kitambulisho sh 5,000.

Aidha uchunguzi zaidi umebaini shule nyingi za sekondari za kata hazina walimu wa masomo ya sayansi jambo ambalo huwalazimisha walimu wakuu kutafuta walimu wa kukodi hasa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita kuja kuwafundisha wanafunzi masomo ya sanyansi kama Hisabati, Fizikia, Kemia, Baiolojia na mengineyo huku wakitumia mbinu anuai kukusanya michango kuwalipa walimu hao wa kukodi.
"Nashauri Serikali iongeze fungu la uendeshaji wa fedha shuleni maana fedha za michango zinazotolewa na wazazi hazitoshi kuendesha shule...huwa tunakodi walimu (wanafunzi waliomaliza kidato cha sita) kuja kutufundishia masomo ya sayansi kwa muda unakuta gharama zinakuwa kubwa za uendeshaji shule," alisema Mkuu wa Sekondari ya Tanya, Victus Kiwango.

"Sisi tumelazimika kuajiri kwa muda wanafunzi sita waliomaliza kidato cha sita kufundisha masomo ya sayansi kwa fedha za shule...tunajibanabana kwa michango pamoja na wazazi na kuhakikisha tunapata chochote kuwalipa walimu hawa wa muda bila hivyo mambo hayaendi," alisema Mkuu Msaidizi wa Sekondari ya Nduweni, Venance Mramba akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Kwa upande wake Mwingira alisema vijana wa kidato cha sita ambao hutumiwa na shule nyingi kuokoa jahazi ya masomo ya sayansi wamekuwa wakiwakaririsha wanafunzi kujibu mitihani na sio kuwafundisha jambo ambalo alisema ni hatari kwa elimu ya Tanzania. "Kujua kusoma na kuandika si kigezo cha kumfundisha mtu...vijana hawa wa kidato cha sita hawana mbinu za ufundishaji wanachokifanya ni kuwakaririsha wanafunzi. Pamoja na hayo aliishauri serikali kutojitoa katika jukumu la kuendesha shule za kata na kuwaachia wazazi kwani shule hizo ziko katika hali mbaya na zinahitaji kuongezewa fedha za uendeshaji.

Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, Judethadeus Mboya alikiri kuwepo na tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi katika shule nyingi za wilaya yake, hivyo walimu kulazimika kuajiri kwa muda vijana wa kidato cha sita kusaidia wanafunzi huku jitihada zikiendelea kufanya kukabiliana na tatizo hilo.
"Walimu wa sayansi ni tatizo Rombo hawatoshi...mwaka huu tumejitahidi na kuajiri takribani walimu 134 wakiwemo wachache wa masomo ya sayansi lakini tatizo bado lipo," alisema Mboya kikilitolea ufafanuzi suala hilo ofisini kwake wilayani Rombo hivi karibuni.

UJUMBE TOKA MTWARA

UJIO WA BARACK OBAMA NCHINI TANZANIA WAZIDI KUZUA MIJADALA KWA WAKENYA

JE? UNAFAHAMU KUWA KORODANI ZA KUKU NI DAWA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

CHANZO, ATHARI NA SULUHISHO LAKE
 
Wanaume  wengi  wanasumbuliwa  na  tatizo  la  ukosefu/ upungufu  wa  nguvu  za  kiume, hii  ni  kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu. Hapa  kwetu  hususani  katika  maeneo  ya  mijini, katika  kila wanaume  kumi  wanao  tembelea  barabarani angalau  watatu  kati  yao wanakabiliwa  na  tatizo  la  upungufu/ ukosefu  wa  nguvu za  kiume, wamewahi  kukabiliwa  na  tatizo  hilo  ama hawana  uhakika  kama wanazo  nguvu  za  kiume  za  kutosha. Tunazo  shuhuda  nyingi  sana  za  watu wanao  sumbuliwa  na  tatizo la  nguvu  za  kiume  ambao  wanakuja  kupata  tiba  na  ushauri  kituoni  kwetu  lakini  kwa  sababu  za  ki-ethics   hatutoweza  kuzipublish hapa  mtandaoni, ila  kiukweli  tatizo  la  upungufu  ama  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  lisipo tafutiwa  ufumbuzi  wa  kina, linaweza  kuwa  na  athari  kubwa  sana  kwa  muhusika  katika  maisha  yake  yote.

Ukosefu   wa  nguvu  za  kiume  ni  nini?


Ni hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa  kufanya/ kukamilisha  tendo  la ndoa  kwa  ufasaha..


Mwanaume  mwenye  nguvu  za  kiume  ni  yupi?

Mwanaume  mwenye  nguvu  za  kiume  ni  yule  mwenye  uwezo  wa  kufanya/ kukamilisha  tendo  la  ndoa kwa  ufasaha.

CHANZO  CHA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME


Kwa  ufupi  sana, hizi  ni  baadhi  ya  sababu  zinazo  sababisha  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  wanaume.


1. Msongo  wa  mawazo

 2. Ulevi  kupita  kiasi.
3.Kupooza  kwa  mwili
4. Presha  na  ugonjwa  wa  kisukari.
5.Wasiwasi  wa  kutekeleza   tendo  la  ndoa
6. Uoga  wa  kufanya  tendo  la  ndoa.
7.Uzoefu  wa  kukatisha  tamaa  wa  siku  za  nyumaa
8.Chango  la  kiume.
9. Kuugua  ugonjwa  wa  ngiri
10. Mazingira  yasiyoridhisha  wakati  wa  tendo  la  ndoa.
11.  Ulaji  mbovu  wa  vyakula  haswa  haswa  ulaji  wa  vyakula  vya  mafuta  kwa  wingi  kupita  kiasi.
12. Kufanya  masturbation  kwa  muda  mrefu   n.k
ATHARI  ZA  UPUNGUFU / UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME

Ukosefu  ama  upungu  wa  nguvu  za  kiume  una  athari  nyingi  sana, zifuatazo  ni  baadhi  ya  athari  za  ukosefu/ upungufu  wa  nguvu  za  kiume.

1. Kuvunjika  kwa  mahusiano  ya  kimapenzi.

2. Kuvunjika  kwa  ndoa.
3. Kujiua :  Baadhi  ya  wanaume  hufikia  uamuzi  wa  kujiua  baada  ya  tatizo  kuwa  kubwa  na kutumia  dawa  za  aina  mbalimbali   bila  mafanikio.
4. Upungufu   wa  nguvu  za  kiume  huongeza  chachu  ya  maambukizi  ya  v.v.u  kwa  wanandoa.Tatizo  la  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  linapokuwa  sugu, hupelekea  rafiki  wa  kike/ mke  wa  mwanaume anaye  sumbuliwa  na  tatizo  la  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, kutoka  nje  ya  ndoa kwa  ajili  ya  kutimiziwa  haja  zake  za  kimwili, mwisho  wa  siku  mwanamke huyo  huweza  kumletea  magonjwa  mume  wake  mwenye  tatizo  la  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  pindi  wanapokutana  kimwili  katika  hali hiyo  hiyo  ya  kutoridhishana
5. Ulevi  kupita  kiasi ; Wakati  mwingine  wanaume  wanao  sumbuliwa  na  tatizo  hili, huamua  kuwa  walevi  kupita  kiasi  ili  angalau  kupunguza  mawazo.
Kwa  ufupi  ukosefu/ upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  tatizo  kubwa  sana  ambalo  endapo  halitatafutiwa  usumbufu  na  muhusika linaweza  kuyaathiri  maisha  ya  muhusika  kwa  kiasi  kikubwa  sana.
SULUHISHO  LA  UPUNGUFU/ UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Zipo  dawa  za  asili  za  aina  mbalimbali  ambazo  zimethibitika  kumaliza  kabisa  tatizo  la  ukosefu/ upungufu  wa  nguvu  za  kiume, kwa  leo   tutaelezea  kuhusu vitu  vitatu  ambavyo endapo  vitatumiwa  kwa  pamoja   basi  vinaweza  kumaliza  kabisa  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  na  kukufanya  uwe  fit  kama  dume  la  simba, na  ngangari  kama  livyokuwa  wakati  una  balehe.


.1. KORODANI  ZA  JOGOO WA  KIENYEJI   ALIYEKOMAA
Picha  ya  korodani  za  jogoo wa  kienyeji  aliyekomaa.
Korodani  za  kuku  ni  dawa  nzuri  sana  ya nguvu  za kiume, na  imekuwa  ikitumiwa  na  mababu  zetu  tangu  enzi na enzi, vijana  wa  siku  hizi  hawajui  ukweli  huu  kwa  sababu  wana  kasumba  ya  kudharau  vitu  vya  asili.

MATAYARISHO :

1. Tafuta  JOGOO  WA  KIENYEJI  ALIYEKOMAA  ..Nimeweka  msisitizo  hapo  kwenye  neno  " Jogoo  Wa  Kienyeji  Aliyekomaa  "  kwa  sababu  najua  kuna  watu  wanaweza  kuchukua kuku wa  kizungu, ama  jogoo  ambaye  hajakomaa. Kamwe  usifanye  kosa  hilo  na  usithubutu  kabisa  kutumia  korodani za  kuku  wa  kizungu. Kama  haujui  jogoo  aliyekomaa  ni  yupi, uendapo  kwa  muuzaji  wa  mwambie  akusaidie  kupata  jogoo  aliyekomaa.

2.  Unga  wa  HABBAT  SAWDA  au  Unga  wa  MJAFARI  robo  kilo.
3. Andaa  kisaani  ambacho  utakitumia  kuweka   korodani  zako  baada  ya  kumchinja  kuku.
 
NAMNA  YA  KUFANYA :

1. Mchinje  jogoo  wako  kisha  mpasue  kwa  ajili  ya  kutoa  korodani  zake. Unapozitoa  korodani za  jogoo  wako  hakikisha  unafanya  bila  korodani  zako  kupaa  damu  ila  kama  ikitokea  bahati  mbaya  korodani  zako  zikigusana  na  damu, unaweza  kuzisafisha  lakini  inashauriwa  zaidi  uzitoe  korodani  zako bila  korodani hizo  kugusana  na  damu. Kuna  namna  ambayo  ukifanya, korodani  haziwezi  kugusana  na  damu  wakati  unazi  toa. ( N.B:  Korodani  za  jogoo  unapozitoa, huwa  kama  mayai  na  haziwi  na  damu  damu  kama  unavyo  weza  kudhania)

2.   Chukua  unga  wa  HABBAT  SAWDA (Tamka  HABAT SODA) au   unga  wa  MJARIFU  kiasi  cha  robo  kiganja  na  kuutia kwenye  kisahani  chako.

3.    Baada  ya  kuzinyofoa  korodani  hizo  za  kuku, ziweke  juu  ya  kisahani  chako ambacho  juu  yake  umeweka  unga  wa  HABBAT  SAWDA  ama  unga  wa MJARIFU  na  kufanya  kama  unazi  biringisha  biringisha  hivi ili  kuzichanganya.

4.  Chukua  korodani  zako  zote  mbili , moja  baada  ya  nyingine  weka  kinywani, meza  na  maji  kama  vile  unavyo  meza  dawa. Hapo  zoezi  lako  litakuwa  limekamilika.
Hautakiwi kumeza  zaidi  ya   korodani mbli, korodani  mbili  tu  zinatosha  sana, ila  kama  utataka  kuwa  na  nguvu  mara  dufu  unaweza  kuwa  unafanya  zoezi  hili  kila  mwezi, mra  moja  kwa  wiki, mara mbili kwa  wiki  ama kila  siku, kwa  kadri  unavyo  jiweza  .Endapo  utafanya zoezi hili  mara  kwa  mara  basi  nguvu  zako  zitakuwa  sio  za kawaida.

KAZI  YA  KORODANI ZA  KUKU Zitakufanya  uwe  na  nguvu  za  ajabu na  wala  usichoke  kufanya  tendo  la  ndoa, unaweza  kufanya  tendo  la  ndoa  hata  mara  nne, bila  ya  kuchoka  na  utakuwa  unajisikia  upo  ngangari  muda  wote, sana  sana  labda  ukose  pumzi  ama  uchoke  kiuno, but  nguvu  za  kiume, utakuwa  safi  sana..

2.  SUPU  YA  KORODANI  ZA  MBUZI : Korodani  za  mbuzi  zinapatikana  maeneo kama  vile  machinjioni  n.k  na  zinapztikana  kwa  bei  nafuu  sana. Chukua  korodani  zako  za  mbuzi, zitumie  kutengeneza  supu  kishs  kunywa  supu  yako  pamoja  na  korodani  hizo  za  mbuzi ambazo  zinakuwa  zimekwisha  wiva. Ukifanya  hivi  angalau  mara  moja  kwa  wiki  kwa  muda  wa  mwezi  mmoja, amini  ninacho  kwambia, utakuwa  vizuri  sana.  Kama  hauna  nafasi  au  muda  wa  kutengeneza  supu  unawezan kwenda  katika  maeneo  ambayo  wanatengeneza  supu ama  wanauza  mbuzi  choma  na  kuweka  oda  wakutengenezee  supu  ya  korodani  za  mbuzi. ..Mgahawa  wa wazi  uliopo  katika  eneo  la  Sinza  Afrika, sana  ni  maarufu  kwa  kutengeneza    supu  ya korodani za  mbuzi, unaweza  kutafuta  muda  ukaenda  hapo  kwa  ajili  ya  kujipatia  supu  ya  korodani  za  mbuzi  ambayo  hujulikana  zaidi  kama " ASHUSHI "

3.  DAWA YA  ASILI  IITWAYO  " JIKO " : Dawa  hii  imebatizwa  jina  la  "Jiko "  kutokana  na  uwezo  wake  mkubwa  wa  kuwasaidia  wanaume  kuyalinda  majiko  yao. Ni  dawa   safi  sana na   yenye  nguvu  za  ajabu. Ni  dozi  ya  siku  kumi  na  mbili tu  ambayo  inaanza  kuonyesha  matokeo  baada  ya  wiki  mbili. Dawa  hii  inafanya  mambo  mengi  sana  ikiwa  ni  pamoja  na  kuimarisha  mishipa  ya  uume  uliolegea  ama  uume  ulioingia  ndani, inaongeza  hamu  ya  tendo  la  ndoa  maradufu, inakufanya  uweze  krudia  tendo  mara nne  bila  ya  kuchoka ( labda  uchoke  kiuno au pumzi  ), na  inakupa uwezo  wa  kukaa  juu  ya  kiuno  kwa  muda  mrefu .

Endapo  utatumia  vitu  vyote  vitatu, kama  vilivyo  orodheshwa  hapo  juu, yaani  korodani  za  kuku, supu  ya  korodani  za  mbuzi  pamoja  na  "Jiko" au  "Nguvu Kazi" kwa  jina  lingine. Kuwa  na  uhakika kwamba  tatizo  lako  la  upungufu ama ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, litakuwa  limekwisha  kabisa  ndani  ya  mwezi  mmoja  wa  kutumia  dozi  yako.

N.B : Dawa  hii ni  kwa  ajili  ya  watu  waliopungukiwa  ama  kuishiwa  nguvu  za  kiume ambao wamewahi  kuwa  na  nguvu  za  kiume, dawa  hii  haiwezi  kumsaidia  mtu  ambaye  amezaliwa  akiwa  hana  nguvu  za  kiume.( Hanithi ). Zipo  tiba  za  asili  kwa  ajili  ya  watu  hao, tutandika  makala  kuhusu  tiba  hiyo  siku  za  usoni.


Kama  unahitaji  kupata  dawa  ya " Jiko "  wasiliana  nasi  kwa  simu : 0767010756  AU  0766538384 NEEMA HERBALIST AND NUTRITIONAL FOODS CLINIC. AU  fika  katika  ofisi  zetu  zilizopo  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI  karibu  na  Chuo  Cha Takwimu.

TANZANIA KUSHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA KOMBE LA DUNIA LA WATOTO WA MITAANI NCHINI BRAZIL

 Mkurugenzi wa Mipango wa British Council Tanzania, Andrew Piner (Kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya uzinduzi wa mashindano ya watoto wa Mazingira magumu yanayotarajiwa kufanyika jijini Brazil mwakani. Pembeni yake ni Mwakilishi wa Rotary Club ya Bahari Beach, Mkurugenzi wa Kituo cha Tanzania Street Children Sports Academy pamoja na Erica Campayne kutoka shirika la LIFT nchini Marekani ambao wanasimamia upande wa kuwafundisha walimu na wakuu wa vituo vya watoto wenye mazingira magumu jinsi ya kutambua uwezo wa watoto ili waweze kujieleza, kutumia vipaji vyao tofauti na mpira.
 Mkurugenzi wa Kituo cha Tanzania Street Children Sports Academy ambao ni waandaaji wa mashindano hayo ya watoto wa wanaoishi katika mazingira magumu akielezea juu ya mchakato wa kutafuta watoto watakaoshiriki kuunda timu ya Taifa itakayoshiriki katika mashindano yatakayofanyika nchini Brazil. Kwa mara ya kwanza tumepanua wingo wa kuja jijini Dar es Salaam ili kuunganisha na jiji la Mwanza. (Pembeni yake ni Mwakilishi wa Rotary Club ya Bahari Beach, na Erica Campayne kutoka shirika la LIFT nchini Marekani).

Aliongeza kuwa katika mashindano yaliyofanyika nchini Afrika Kusini mwaka jana Timu ya Tanzania iliweza kuchukua nafasi ya tano baada ya kuzichakaza timu za Brazil, Ufilipino, Karagwa na Uingereza ambayo tulitoka sare.

Mwaka huu timu zinazoshiriki mashindano hayo zipo 16 na kwa Bara la Afrika zipo timu 7 ambazo ni Kenya, Burundi, Libya, Sea-lion, Egypt, Afrika Kusini na Tanzania pia alisema kuwa jumla ya Mabara manne yanatarajia kushiriki.

British Council Tanzania pamoja na Rotary Club ya Bahari Beach ndiyo wadhamini wa michakato yote ya kusimamia Semina, pamoja kuiwezesha timu kuundwa. 
 Waandishi wa Habari wakifuatilia.
 Mkurugenzi wa Kituo cha Tanzania Street Children Sports Academy akijibu maswali ya waandishi wa habari.
 Walimu na wakuu wa vituo vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu vya jijini Dar wakiwa katika semina kuwafundisha jinsi ya kutambua uwezo wa watoto ili waweze kujieleza, kutumia vipaji vyao tofauti na mpira.
 Wakimsikiliza mkufunzi.
 Wakiwa makini kufuatilia mafunzo wanayoyapata.
 Mkufunzi akitoa maelekezo jinsi ya kufanya.
Mkufunzi akitoa mafunzo kwa vitendo juu kuwajengea uwezo watoto wao na kutambua vipaji walivyonavyo.

Wednesday, May 22, 2013

VURUGU ZA WANANCHI WA MJINI MTWARA

MTOTO WA SIKU 3 AOKOTWA AKIWA AMETUPWA MJINI SONGEA

 Ama kweli dunia kuna mambo, wakati wengine wanahangaika kutafuta watoto mpaka kwa waganga wengine nao watoto hao wanawatupa, tukio hilo limetokea mjini Songea baada ya Mtoto Bahati Upendo mwenye siku 3 toka azaliwe alipo wekwa na mama yake kwenye mfuko wa mbolea na kutumbukizwa kwenye shimo, Ndani ya shimo hilo amekaa siku 6 bila kula wala kunywa hadi alipo okotwa na wasamalia wema.

Hivi sasa mtoto huyo yupo hospitali ya mkoa wa Ruvuma akiwa Salama Salimini, uongozi wa hospitali huo unaomba msaada kwa yeyote anayeweza kusaidia mtoto huyo; anaweza kwenda moja kwa moja hospitalini au wasiliana na namba zifuatayo mchango utafwatwa 0755061588 au 0755 731 234.
Waganga na maofisa wa Jeshi la Polisi wakiwa wamefika hospitalini hapo kumjulia hali. (Picha kwa hisani ya Jeshi la Polisi, Ruvuma.)

WATU WATATU WACHOMWA MOTO KWA WIZI NCHINI KENYA

PATA COPY YAKO YA NON STOP MIX TOKA KWA DJ D OMMY WA TIMES FM

Mmoja wa ma-Dj wakali toka Times Fm DJ. D Ommy aka The Transform Master ametoa non stop yake mpya kwa ajili ya wasikilizaji na wapenzi wake.
Non stop hiyo inaitwa THE RETURN OF THE TRANSFORM MASTER MIX VOL 1. Ina cover hii hapa chini.
Na ukitaka kui-download ni rahisi sana, just click on this link
PATA COPY YAKO HAPA.

POLISI WAWATAWANYA WAANDAMANAJI MJINI MTWARA, YAHOFIWA WATU 4 WAMEPOTEZA MSIAHA MPAKA SASA

Wananchi hao Mkoani Mtwara wameamua kuingia barabarani na kuanza kufanya fujo zilizopelekea polisi kuanza kufyatua mabomu ya machozi kwa ajili ya kuwatawanya waandamanaji hao wanaoshindana na serikali kwa miezi kadhaa sasa.

Awali, wananchi wote mkoani Mtwara siku ya leo ilikuwa kufuatilia mambo ya Bunge yanavyokwenda, huku wakiwa na hamu ya kuona nini kitaamuliwa katika Bajeti ya Muhongo, wakitaka kuona mkoa wao unapendelewa zaidi kwa uwapo wa gesi.

Baada ya kuona bajeti hiyo ipo tofauti na dhamira yao, waliamua kurudi tena kwenye harakati zao kwa ajili ya kushinikiza malengo yao kwa serikali juu ya gesi.

Hadi sasa, mabomu yanaendelea kulipuliwa mjini hapa na wengi wasiokuwa na uwezo wa kushiriki, hasa wazee wakiwa wamejichimbia majumbani mwao.

Sera ya mkoani Mtwara ni gesi kwanza, uhai baadaye, moja ya kauli mbiu zinazotumika kuwapa kiburi wananchi. Tangu kuzuiwa kufanyika kwa mikutano ya hadhara, wananchi wanatumia mbinu mpya ya kuhamasishana kwa njia ya meseji na vipeperushi na wakati mwingine kwa njia ya usafiri wa umma na kwenye maduka.

Taarifa zaidi zitaendelea kukujia ikiwa ni pamoja na maddhara ya vurugu hizo mkoani Mtwara.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA NANE YA KAMISHENI YA VYUO VIKUU MBALIMBALI JIJINI DAR

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, yatakayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yamefunguliwa leo. Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR
Baadhi ya washiriki  wa maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya kufungua rasmi maonyesho hayo ya siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Maofisa wa mfuko wa PPF, kutoka (kushoto) ni Meneja wa Kanda ya Ilala, Evans Musiba, Meneja Uhusiano, Lulu Mengele na Ofisa Masoko, Sereki Michael, wakati alipotembelea katika banda la maonyesho la PPF, leo kwenye maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere, Africa Junior, kuhusu Kituo cha utafiti wa Usafirishaji, wakati alipotembelea kwenye banda la Chuo Kikuu cha Makerere kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa, Ofisa Udahiri Mwandamizi wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, Hilder Kawiche, wakati alipotembelea Banda hilo kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa, Makamu Mwenyekiti wa Chuo Kikuu cha United African-Tanzania, Jo, Do Hyun, kuhusu matumizi ya gari ndogo inayotumia Chaji ya Umeme wakati alipotembelea katikia Banda hilo,kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Sakina Taki (kushoto) na Tannaz Naseri, kutoka 'University of the Future' , Kuala Lumpur, wakati alipotembelea Banda hilo kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa, Msimamizi Mkuu wa Teknolojia wa Chuo Kikuu cha SUA, Gaudencia Donati, wakati alipotembelea Banda hilo kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Akitembelea katika Mabanda ya maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee, leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo.

WATU WAWILI WAJINYONGA AKIWEMO DOKTA WA MENO MJINI MOROGORO

DAKTARI wa meno Anord Rimo umri wa miaka kati ya 30 hadi 40 wa hospitali ya Sabasaba manispaa ya Morogoro amekutwa amejinyonga katika nyumba ya kulala wageni ya Camel iliopo Kihonda mjini hapa.

Kamanda wa polisi mkoani hapa Faustine Shilogile alisema kuwa tukio hilo limetokea Mei 22 saa 10 alfajiri katika nyumba hiyo ya kulala wageni.

Kamanda huyo alisema kuwa Daktari huyo alikuwa amepanga katika nyumba hiyo ya kulala wageni kwenye chumba namba 2 na kwamba alikutwa amejinyonga dirishani kwa kutumia foronya za mto pamoja na taulo.

Alisema kuwa usiku wa kuamikia siku hiyo marehemu huyo alikwenda katika sehemu ya mapokezi ya nyumba hiyo ya kualala wageni na kufanya fujo zilizokuwa huku akionyesha sehemu zake za siri kuwa hazifanyi kazi.

Kamanda huyo alisema kuwa marahemu huyo alikuwa peke yake katika chumba hicho na haikufahamika mara moja anaishi wapi hku chanzo cha kujinyonga kwake bado hakujajulikana na polisi wanaendela na uchunguzi zaidi.

Wakati huo huo msichana Dorosia Michael (15) alifariki dunia Mei 17 mwaka huu huko eneo la Sultani manispaa ya Morogoro baada ya kujinyonga kwa kutumia kitenge.

Kamanda Shilogile alisema kuwa tukio hilo limetokea Mei 17 mwaka huu huko Sultani nyumbani kwa Masud Ramadhani ambako msichana huyo alikuwa akifanya kazi.

Alisema kuwa chanzo cha kujinyonga msichana huyo bado hakijajulikana na polisi wanaendela na uchunguzi zaidi huku wakisubiri taarifa za madaktani juu ya uvumi uliopo kuwa msichana huyo kabla ya kujinyonga alibakwa.

AIRTEL YAZINDUA OFA KABAMBE KUPIGA SIMU KWENDA NJE YA NCHI

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo (wa pili kutoka kulia) wakizindua huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso. Na Mpigapicha Wetu.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya kupiga simu kwenda India kwa gharama nafuu. Wengine wanaofuatia ni Balozi wa India hapa nchini, Debnath Shaw, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Sunil Colaso na Meneja Biashara za Kimataifa wa Kampuni hiyo, Prisca Tembo. Na Mpiga picha Wetu.
---
• Wateja kupata kifurushi cha dakika 25 kupiga simu kwenda India
• Ofa hii inapatikana masaa 24 siku 7 za wiki,

Kampuni ya Bharti (“Airtel”) inayoongeza kwa kutoa huduma za
mawasiliano inayoendesha shughuli zake katika nchi 20 barani Afrika na Asia leo imetangaza uzinduzi wa ofa itakayowawezesha wateja wa Airtel Tanzania kupiga simu kwenda nje kwa gharam nafuu zaidi.

Ofa hii inaendelea kuonyesha dhamira ya Airtel Tanzania ya kuendelea
kuwanganisha watanzania katika mtandao wa mawasiliano na kuwapa huduma bora zenye gharama nafuu. Uzinduzi huu unafatia utambulsho wa huduma kabambe ya Airtel yatosha iliyofanyika week chache zilizopita.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hii mpya, Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bwn. Sunil Colaso alisema ”baada ya uzinduzi wa mafanikio ya huduma yetu ya Airtel yatosha. leo tunazindua ofa ya mawasiliano ya gharama nafuu na kuwawezesha wateja wetu kuwasiliana na familia
,marafiki na washirika wa kibiashara walioko nje ya mipaka ya nchi.
Kwa kiasi cha chini cha hadi shilingi3, 000 sasa wateja wa Airtel
wanaweza kupiga simu India masaa 24 kwa siku 7 za wiki. Ofa hii
itampatia mteja dakika 25 za muda wamaongezi kwa muda wa wiki nzima.

Aliongeza “Hii ni ya kwanza kutoka Airtel, na tunaendelea kuwahakikishia wateja wetu nchi nzima huduma bora, za uhakika na
gharama nafuu za mawasiliano wakati wote. Tumesikiliza kile wateja
wetu wanachokitaka na kutengeneza ofa inayokidhi mahitaji yao hivyo
tutaendelea kutekeleza dhamira kwa watanzania ya kuleta huduma zenye ubunifu, bora na gharama nafuu ambazo kwa uhakika zitaleta uhuru wa kuongea nje ya mipaka. Ofa hii itawawezesha wateja wanaosafiri au kuwasiliana na India iwe kimasomo, kibiashara , wanaotembelea India kimatibabu kuwa na mawasiliano na familia zao kwa gharama za kiushindani zilizo nafuu zaidi. Uzinduzi huu ni mwanzo wa kuleta mapinduzi ya mawasiliano katika soko la Tanzania.

HAYAWIHAYAWI, SASA YAMEKUWA! USIKU WA HIP HOP KURINDIMA J’MOSI HII DAR LIVE

Wakali tisa wa Hip Hop wanaowania gari aina ya Toyota FunCargo (new model), katika pozi mbele ya gari lao.
Na Mwandishi Wetu

ILIPANGWA, ikapangika. Baada ya kusubiririwa kwa muda mrefu, hatimaye msimu mpya wa shoo ya Usiku wa Hip Hop (2013) unachukuwa nafasi Jumamosi hii ndani ya Ukumbi wa Dar live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar.


Wasanii wanaotamba kwenye gemu la Hip Hop, Kala Jeremiah, Fid Q, Nay wa Mitego, Joh Makini, Stamina na wengine kibao pamoja na washiriki wa Shindano la The Vodacom Mic King watakamua shoo baab’kubwa kuweka historia mpya ya burudani.


Meneja Matukio wa Ukumbi wa Dar Live, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ amewahakikishia mashabiki wote wa muziki wa Hip Hop kuwa Jumamosi kutasheheni matukio kibao, ulinzi mzito utakuwepo pamoja na parking kubwa ya magari hivyo watu wafike kwa wingi watainjoi kwa nafasi na kuondoka salama ukumbini.


“Vijana tisa waliosalia katika Shindano la The Vodacom Mic King watapanda jukwaani na kushusha mistari ambapo mshiriki mmoja anatarajiwa kuondoka na gari jipya aina ya Toyota FunCargo (new model),” alisema Abby Cool na kuongeza:


“Mashabiki wanaweza kulifuatilia shindano hilo kupitia Runinga ya DTV kuweza kujua jinsi ya kuwapigia kura.”


Washiriki hao na namba zao za ushiriki kwenye mabano ni Ally (MK 02), Anold (MK 03), Bahati (MK 05), Boniface (MK 07), Emmanuel (MK 10), Ibrahim (MK 12), Karrys (MK 13), Lusajo (MK 14) na Martin (MK15). Jinsi ya kuwapigia kura, wasomaji wanatakiwa kuandika neno MK wakiambatanisha na namba ya mshiriki kisha kutuma ujumbe huo kwenda namba 15564.
OFA ZAIDI KWA MSHINDI

Mbali na mshindi kuondoka na gari, Mrisho aliongeza kuwa washindi watatu wa nafasi za juu watajipatia dili la kurekodi singo mojamoja kutoka kwa prodyuza kiwango aliyezalisha ngoma kali Bongo ikiwemo ya Kundi la Kigoma All Stars iitwayo Leka Dutigite, Tudd Thomas.
TUZO KUTOLEWA

Mrisho alitiririka na mistari kuwa, mbali na shoo kali kutoka kwa wakali hao wa Hip Hop, kutakuwa na kipengele cha kutoa tuzo za muziki wa Hip Hop katika vipengele tofauti hivyo mashabiki pia waendelee kuwapigia kura wasanii wanaowapenda.


Vipengele vitakavyotolewa tuzo ni Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Legendary) ambapo yamepita majina matatu; Fid Q, Joh Makini na Profesa Jay. Pia kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi) ambacho kina majina kama Young Killer, P The Mc na Tabla huku akianisha kipengele cha mwisho ambacho ni Wimbo Bora wa Hip Hop (2012/13) chenye nyimbo kali za Dear God (Kala Jeremiah), Sihitaji Marafiki (Fid Q) na Najuta Kubalehe (Stamina).


“Ili kuwapigia kura, mashabiki wanatakiwa kuandika neno BHL wakiambatanisha na jina la msanii husika kwenda namba 15564 katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop (Legendary).


“Kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi), mashabiki waandike neno BUA na kufuatiwa na jina la msanii wanayempenda kwenda namba 15564,” alisema Abby Cool na kuongeza:


“Kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka, mashabiki waandike neno BHS likifuatiwa na jina la msanii wanayempenda kisha watume ujumbe huo kwenda namba 15564.”
KUWAENZI WASANII/SOKA KWENYE SKRINI KUBWA

Abby Cool aliweka bayana kuwa katika shoo hiyo kutakuwepo na documentary maalumu ya kuwakumbuka wasanii wa Hip Hop waliotangulia mbele za haki kupitia skrini kubwa bila kusahau mashabiki wa soka watapata fursa ya kushuhudia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) kati ya Bayern Munich na Borrusia Dortmund. Twendeni Dar Live J’mosi!

KIKUYU SONG: NDEREBA RUGAMA TU - JOHN DAMATHEW

NDAGUSHIMA - CHORALE EVANGELIQUE ADEPR CYARWA, BUTARE- RWANDA

KARIBU IGO LOUNGE ILIYOPO SINZA MAPAMBANO JIJINI DAR

Muonekano wa IGO Lounge iliyopo Sinza Mapambano jijini Dar es Salaam. Kiota hiko kina raha mbali mbali zinapatikana ikiwemo Wahudumu wakarimu... Vyakula vya Kila Aina, Nyama Choma, Supu Ya Kuku wa Kienyeji wa Maziwa... Vinywaji vya Kila aina. Pia wale wapenzi wa Mpira... kuna TV za kutosha.
Muonekano wa Kaunta na sehemu ya kupumzikia upande wa kushoto unapoingia.
Upande wa Kulia unapoingia.
Sehemu ya Mbele.
Muonekano wa Kaunta.
Upande wa Jikoni, Mpishi akiandaa Mishkaki.
Nyama Choma.
Supu ya Kuku wa Kienyeji wa Maziwa.
Upande wa Mbele wa kupumzika.
Mambo ya Digitali... Hakuna Chenga.
Vinywaji vya kila aina vinapatikana katika Kiota hicho. Atakayepata ujumbe huu amjulishe na Mwenzake... Karibuni sana marafiki...

FANI YA UANDISHI WA HABARI IMEVAMIWA, TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA.

Pichani ni waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa katika maandamano ya amani (Picha na Maktaba).
 ---
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).

Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.

Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake. Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na kuisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, 'ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI' nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?

Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.

Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.

Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya 'kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.

Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.
Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.

Asanteni sana kwa kusoma.
Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna

Truck Driving Schools
Idadi ya Watu