Wednesday, March 21, 2012

UJUMBE WA LEO... SOMA KWA MAKINI


JENGO LA CM PLAZA LAFANYIWA USAFI NA TEKNOLOJIA MPYA YA ROPE ACCESS

 Mkurugenzi wa kampuni ya Equilibrium Rope Access Bw. Abdulkarim Tumba akipanda juu kwa ajili ya kusafisha vioo kwa kutumia teknolojia ya Rope Access ambayo ni mpya kwa hapa nchini. Aliongeza kuwa ni vyema Watanzania wenye majengo ni vyema wakajitoa kwa kuitumia teknolojia hii ambayo ni salama. Na leo kwa mara ya kwanza tokea teknolojia hiyo imeingia nchini Tanzania wameifanya katika Jengo la CM Plaza lililopo jijini Dar es Salaam.
 ...Akielekea juu kwa ajili ya kuanza kusafisha jengo hilo; ambapo usafi unafanyika kwa ustadi kabisa.
 Muonekano wa jengo huku akionekana Bw. Abdulkarim Tumba akiendelea na usafi.
Hapa akiendelea na usafi ambapo haitaji vifaa vingi wala umeme na ni haraka na salama.
Jengo la CM Plaza kama linavyoonekana wakati likifanyiwa usafi.

MAGAZETI YA LEO; DK SLAA ALIPUA NA MAFISADI, MKUU WA WILAYA AFANYA UNYAMA NA KANISA KATORIKI WAMSHUKIA WASSIRA KUHUSU SLAA

MAHOJIANO YA BW. SAMWELI TENGA AMBAYE ALIKUWA MWANACHANA WA FREEMASONS KATIKA KIPINDI CHA NJIA PANDA YA CLOUDS FM, JIJINI DAR

Habari zenu wapenzi wasomaji wa Kajunason Blog, napenda kuchukua nafasi hii kuwaletea mahojiano ya Bw. Samweli Tenga katika kipindi cha Njia Panda kinachorushwa na Clouds Fm 88.4 ya jijini Dar es Salaam, mahojiano hayo yalifanyika kwa muda wa wiki tatu mfululizo.
Japokua anadai alikua mwanachama wa FREEMASONS, Samwel alikua anajihusisha na biashara ya dawa za kulevya pia na amekiri kufanya biashara hiyo na baadhi ya viongozi wakubwa wa dini wa Tanzania na hata kukaa nao meza moja, hiyo alama kwenye sikio lake la kulia anasema waliwekewa kwa makusudi ili iwe rahisi kutambulika popote atakapotokea, yani ukimuona tu unajua huyu anauza madawa ya kulevya.
 Alama hii ni kubwa ambayo amepigwa katika mguu wake wa kushoto kumtambulisha kuwa ni mwanachama wa FREEMASON, ni alama kama muhuri ambayo imechora ndani ya mfupa ambapo kwa sasa mguu umekuwa ukimuuma sana mpaka kutaka kufanyiwa uparesheni, nembo hiyo baada ya kupigwa iliambatana na KIAPO ambacho popote atakapokwenda atatambulika, alisema kwa sasa ndio inamsumbua sana kwa sababu chuma kilichotumika kumuwekea kimevunja mfupa, na hii aliifanywa huko Afrika Kusini.
---
Bw. Samweli  Tenga ambaye yeye alikwenda nchini Afrika Kusini lakini alikutana na mauza uza mwengi. Alisema kuwa aliamua kukimbilia na kujiondoa kwenye dini hiyo inayodaiwa kuwa ya kishetani baada ya kutoka gerezani huko Afrika Kusini, walikua wanatumwa kwenda kuua watu kwenye ajali na sehemu nyingine, walipewa hirizi maalum za kuwafanya wasioneane lakini baada ya kuona hayawezi hayo maisha alikimbia lakini mpaka sasa anatafutwa kwa sababu alikuwa ndio anamalizia hatua ya mwisho kuingia kwenye  kutajirishwa kwa mali kama inavyotokea kwa waumini wengine, ila akatoroka na baadae ndio akasikia jamaa aliempeleka kwenye hiyo dini nae ameuwawa baada ya kugundulika kwamba alikuwa anataka kujiondoa.

Fuatilia mahojiano hayo:

Siku ya kwanza... ilikuwa ni tarehe 26/02/2012
Siku ya pili.... ilikuwa ni tarehe 11/03/2012
Siku ya Tatu... ilikuwa ni tarehe 18/03/2012

Tuesday, March 20, 2012

WANANCHI WA ELGEIYO NCHINI KENYA WAHAMISHWA MAKAZI YAO


Wenyeji wa eneo la Elgeyo Marakwet wanaishi katika hali ya wasiwasi baada ya bonde la Elgeyo marakwet huko Keiyo nchini Kenya kufanya nyufa ardhini na kuibua hofu yakuporomoka. Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya Keiyo Bw. Mohammed Abbas amekariri kuwa kuna haja ya wenyeji hao kuyahama makazi yao ili kuzuia maafa makubwa zaidi kuzuka. Mwanaisha Chidzuga wa KTN ana taarifa zaidi.

GLOBAL PUBLISHERS ILIVYOADHIMISHA MIAKA 14 YA KUANZISHWA

Steji ilipambwa hivi. Twanga Pepeta wakiporomosha burudani katika sherehe hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa  Global, Eric Shigongo (mbele) akimwongoza mgeni rasmi katika sherehe hiyo, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja (wa tatu kushoto) kuingia ukumbini. Wengine pichani ni wafanyakazi wa Global, Issa Mnally (wa pili kushoto), Sud Kivea (wa pili kulia) na Makongoro Oging' (wa kwanza kulia).
Wafanyakazi wa Global na wageni waalikwa wakijisevia msosi.
Wahariri wa Championi, John Joseph (kushoto) na Phillip Nkini wakigonga menyu.
Wanamuziki wa Twanga Pepeta nao wakishiriki msosi katika sherehe hiyo.
Mgeni rasmi, William Ngeleja (kulia) na Erick Shigongo nao wakipata msosi.
Musa Mateja (kushoto) akiwa na Shakoor Jongo wakati wa msosi.
Mambo yalikuwa hivi pande hizo.
BAADA YA MENYU ILIKUWA NI VINYWAJI NA BURUDANI
Kulwa Mwaibale (kushoto) akiwa na Issa Mnally.
Makongoro Oging' (kushoto) akipozi na Flowers; Khadija Mngwai na Sophia.
Shakoor Jongo (kushoto) akikamua sambamba na Twanga Pepeta.
Twanga wakizidi kupagawisha.
Walusanga Ndaki akiserebuka sambamba na Luiza Mbutu wa Twanga Pepeta.
Wafanyakazi wa GPL wakifuatilia makamuzi ya Twanga Pepeta.
Ally Mbetu (kushoto) katika pozi na Richard Bukos. 
Akina Rihanna nao walikuwepo.
Wafanyakazi wakisakata rhumba.
Kampuni ya Global Publishers and General Enterprises Ltd, wachapishaji wa Magazeti ya Uwazi, Championi, Ijumaa, Risasi, Amani na Ijumaa Wikienda, Jumamosi Machi 17, 2012 ilitimiza miaka 14 ya kuzaliwa ambapo sherehe ya maadhimisho hayo ilifanyika katika Hoteli ya Atrium, iliyopo Afrika Sana, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi katika sherehe hiyo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja. Wageni waalikwa pamoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo walisherehekea vilivyo siku hiyo huku bendi ya Twanga Pepeta International ikitoa burudani kwa wanafamilia hao wa Global.

AICC YAPATA WAWAKILISHI MICHUANO YA MEI MOSI, MWAKA HUU

 Wafanyakazi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Eva Kunkuta (kulia) na Latifah Amiri wakichuana katika mchezo wa Draft uliofanyika mwishoni mwa wiki katika mashinda ya kutafuta wachezaji watakao iwakilisha AICC katika mashindano ya Mei Mosi jijini Tanga.
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa AICC, Savo Mung’ong’o (kushoto) akisukuma kete dhidi ya Leonard Ngasa katika mchezo wa Draft uliofanyika mwishoni mwa wiki Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kutafuta wawakilishi watakaoenda Tanga katika mashindano ya Mei Mosi.
 Boniface Rutunda akimaliza mbio za baiskeli na kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano yaliyo andaliwa na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mwishoni mwa wiki jijini Arusha kutafuta wawakilishi watakaoenda Tanga katika mashindano ya Mei Mosi.
 Wafanyakazi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) kutoka  kushoto-Saumu Kilari, Elizabeth Amandus, Evalyna Kunkuta na Zainab Ramadhan, wakijiandaa kuanza mbio za baiskeli katika mashindano yaliyoandaliwa na kituo hicho  katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mwishoni mwa wiki jijini Arusha, kutafuta wawakilishi watakaoenda Tanga katika mashindano ya Mei Mosi. Katika mbio hizo Elizabeth Amandus aliibuka mshindi.
 Wilfred Julius akiwa akipata huduma ya kwanza kutuliza maumivu ya msuli baada ya nyama za misulu kubana wakati akishiriki mbio za baiskeli katika mashindano yaliyo andaliwa na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mwishoni mwa wiki jijini Arusha kutafuta wawakilishi watakaoenda Tanga katika mashindano ya Mei Mosi.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Savo Mung’ong’o (wa nne kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho na waamuzi baada ya kumalizika kwa mashindano ya kutafuta wachezaji watakao wakilisha kituo hicho katika mashindano ya Mei Mosi jijini Tanga. Mashindano hayo ya mchujo yalifanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mwishoni mwa wiki jijini Arusha.
---
Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) kimechagua wachezi timu ya wachezaji kumi itakayo wakilisha kituo hicho katika mashindano ya kuadhimisha sherehe za Mei Mosi mwaka huu zitakazo fanyika kitaifa jijini Tanga.

Wachezaji hao walichaguliwa baada ya kituo hicho kufanya mashindano ya mchujo mwishoni mwa wiki kupata wawakili watakaoenda Tanga katika mashindano hayo yatakayoanza katikati ya mwezi wa nne.

Mashindano hayo ya mchujo yalishikisha mchezo wa mbio za baiskeli kwa wanaume mita 4000 na mita 2000 kwa wanawake, riadha mita 1200 kwa wanaume na wanawake mita 800, drafti kwa wanaume na wanawake, bao wanaume na wanawake na karata wanaume na wanmawake.

Katika mbio za baiskeli wanaume, Boniface Rutunda aliibuka mshindi akifuatiwa na Rodney Thadeus na nafasi ya tatu ilishikwa na Proches Kamugisha. Wakati wanawake Elizabeth Amandus alinyakua ushindi wa kwanza akiwaacha Saumu Kilari na Zainabu Ramadhan walioshika nafasi ya pili na tatu.

Kwa upande wa riadha, Fidel Kweka aliongoza na kuwaacha John Martin aliyeshika nafasi ya pili na Hiza alishika nafasi ya tatu wakati Zamda Mfaume aliibuka kidedea akifuatiwa na Redempta Shirima aliyeshika nafasi ya pili.

Kwa upande wa mchezo wa draft kwa wanaume, Rashid Rashid aliibuka mashinda baada ya kumshinda Leonard Ngasa katika hatua ya fainali, huku Eva Kunkuta akiibuka bingwa kwa upande wa wanawake baada ya kufunga Teddy Mapunda.

Katika mchezo wa karata, John Martin akiibuka mshindi katika mchezo wa Karata baada ya kumshinda Proches Kamugisha na kwa upande wa wanawake June Masubo aliibuka mshindi.

Meneja wa timu za AICC, Rodney Thadeus amesema kuwa washindi waliopatikana wanaandaliwa programu ya mazoezi ili kuhakikisha wanapata ushindi katika mashindano hayo yatakayofanyika jijini Tanga.

Nae Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa AICC, Savo Mung’ong’o amesema AICC itaendelea kuhamasisha wafanyakazi wake kushirii michezo mbalimbali na kwamba shiriki linaandaa utaratibu wa kufanya mazoezi kila wiki.

VURUGU ZILIZOTOKEA KWENYE MCHEZO WA VODACOM PREMIER LEAGUE TAREHE 10/03/2012 KATI YA TIMU YA YANGA NA AZAM


TAKUMBUKWA YA KWAMBA KWENYE MCHEZO KATI YA TIMU YA YANGA NA AZAM MCHEZO WA VODACOM PREMIER LEAGUE TAREHE 10/03/2012 MWAMUZI WA MCHEZO HUO ISRAEL NKONGO ALIPIGWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA TIMU YA YANGA KATIKA VURUGU ZILIZOTOKEA DAKIKA YA KUMI NA MOJA YAMCHEZO, BAADA YA MWAMUZI HUYO KUFANYA MAAMUZI SAHIHI YA KUMUONYESHA KADI YA PILI YA MANJANO NA KUFUATIWA NA KADI NYEKUNDU MCHEZAJI WA YANGA HARUNA NIYONZIMA.

BAADA YA KUONYESHWA KADI NYEKUNDU MCHEZAJI HUYO BAADHI YA WACHEZAJI WA YANGA HAWAKUKUBALIANA NA ADHABU HIYO NA KUANZISHA VURUGU KWA MWAMUZI ISRAEL NKONGO NA HATA KUDIRIKI KUMPIGA. KATIKA TUKIO HILO LA KUMPIGA MWAMUZI WACHEZAJI WENGINE WALIPEWA KADI NYEKUNDU  NA KUISABABISHIA TIMU YAO KUENDELEA NA MCHEZO WAKIWA NA WACHEZAJI PUNGUFU.

KUTOKANA NA TUKIO HILO CHAMA CHAMA CHA WAAMUZI NCHINI FRAT KINALAANI KWA NGUVU ZOTE VITENDO VYA VURUGU VILIVYOFANYWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA YANGA KWA VILE VITENDO HIVYO SI VYA KIUANAMICHEZO HASA KATIKA MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU, MCHEZO UNAOCHEZWA KWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI ZA MASHINDANO HUSIKA, NA KUWATAKA WACHEZAJI WOTE NCHINI KUTOFANYA KAMA WALIVYOFANYA BAADHI YA WACHEZAJI WA YANGA, KWANI WACHEZAJI HAO WAMEIPAKA MATOPE TIMU YA YANGA KWANI VITENDO HIVYO SI SEHEMU YA HISTORIA BORA YA WACHEZAJI WA TIMU YA YANGA.

AIDHA, FRAT INATOA PONGEZI ZA DHATI KWA KAPTENI WA TIMU YA YANGA NA TIMU YA TAIFA SHADRAK MSAJIGWA KWA KUONYESHA UKOMAVU KAMA KAPTENI KWA KUWAZUIA WACHEZAJI WAKE KUTENDA YALE WALIYOKUWA WANAKUSUDIA KUYATENDA PIA KAPTENI HUYO AMENUKULIWA NA VYOMBO VYA HABARI AKIKEMEA VITENDO VILIVYOFANYWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WENZAKE.

 PIA FRAT INAMPONGEZA KOCHA MKUU WA TIMU YA YANGA KOSTADIN PAPIC KWA KUKEMEA VITENDO VYA WACHEZAJI WAKE NA KUIKEMEA NIDHAMU MBOVU ILIYOONYESHWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA TIMU YAKE.

 PIA TUNAWAPONGEZA WACHEZAJI WOTE NA DAKTARI WA TIMU YA YANGA,AMBAO KWA NAMNA MOJA WALIJARIBU KWA NGUVU ZOTE KUWAZUIA WACHEZAJI WALIOKUWA NA HALI YA KUMPIGA MWAMUZI WA MCHEZO HUO.

 VURUGU HIZO ZIMEKEMEWA NA VIONGOZI WA SERIKALI, RAIS WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU NCHINI NA WALE WOTE WANAOPENDA MAENDELEO YA MCHEZO HUO HAPA NCHINI.

CHAMA CHETU KINAUNGA MKONO KWA DHATI KAULI ILIYOTOLEWA NA RAIS WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU NCHINI KWA KUKEMEA VITENDO AMBAVYO HAVIKUZI MAENDELEO YA SOKA HAPA NCHINI BALI VINADUMAZA NA KUTUWEKA KATIKA SURA MBAYA KWA WADAU MBALIMBALI WA MCHEZO WA SOKA IKIWA NI PAMOJA NA KUFANYIKA KWA UHARIBIFU WA MALI ZA SERIKALI NA WATU BINAFSI BILA SABABU ZA MSINGI ZA KUHALALISHA MATENDO HAYO.

 VITENDO VYA WACHEZAJI HAO VILIWAHI KUTOKEA MIAKA YA AROBAINI NA SABA KATIKA LIGI NDOGO NA SI KWENYE LIGI KUU NCHINI. KWA HIYO WALE WOTE WALIOFANYA VITENDO HIVYO WANAWAJIBIKA KUWAOMBA RADHI WATANZANIA KWA VITENDO VYAO AMBAVYO VIMETENGENEZA  HISTORIA MBAYA KATIKA LIGI KUU HAPA NCHINI.

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU HAPA NCHINI  LIMEWEKA KANUNI NA TARATIBU AMBAZO KAMA TIMU HAIKURIDHIKA NA YALE YANAYOJITOKEZA KWENYE MCHEZO, ZITATAKIWA  KUZIFUATA ILI KUDAI HAKI ZAO NA SI VINGINEVYO.

NI IMANI YETU KWAMBA MAFUNZO TULIYOYAPATA KUTOKANA NA TUKIO HILO YATABAKI KUWA SEHEMU YA HISTORIA NA KUTORUDIWA TENA NA TIMU YOYOTE. TIMU YA YANGA NI MIONGONI MWA TIMU KUBWA HAPA NCHINI AMBAPO WACHEZAJI, VIONGOZI NA WAPENZI WAKE WANAPASHWA KUWA MFANO BORA WA KUIGWA NA HILO LINAWEZEKANA ENDAPO KUTAKUWA NA UTASHI WA DHATI WA KUJENGA TIMU BORA NA YENYE KUHESHIMIWA TANZANIA NA NJE YA TANZANIA.

 MCHEZAJI MWASIKA MMOJA KATI YA WACHEZAJI WALIOSHIRIKI KUMPIGA MWAMUZI AMENIPIGIA SIMU AKINIOMBA RADHI MIMI  NA WAAMUZI WOTE KWA UJUMLA NA KUNIOMBA NIMSAIDIE KUMUOMBEA MSAMAHA KWA MWAMUZI WA MCHEZO HUO LAKINI HIYO HAITOSHI;NAMSHAURI MCHEZAJI HUYO AJITOKEZE HADHARANI ASIOMBE RADHI KWA SIRI KWANI WALIOATHIRIKA SIKU ILE SI NKONGO PEKE YAKE NI PAMOJA NA WATU WENGINE AMBAO WALIKUJA KUONA MCHEZO WA SOKA NA SI MASUMBWI, NAAMINI MWASIKA ANAJUTIA MAKOSA YAKE NA NI MUUNGWANA, ATAJITOKEZA KUOMBA RADHI HADHARANI  ILI AWE SEHEMU YA JAMII INAYOPENDA MAMBO MEMA.

MWISHO NAOMBA VIONGOZI WA YANGA, WAPENZI NA WACHEZAJI,KWAMBA HUU SI WAKATI WA KULUMBANA KWA YALIYOTOKEA BALI NI WAKATI WA KUJISAHIHISHA ILI AIBU ILE ISITOKEE TENA; TUSIPOKEMEA YALE YALIYOJITOKEZA JANA KWENYE UWANJA WA TAIFA KESHO TUTAFANYA VILE VILE KWENYE NCHI ZA WATU, ITAKUWA NI AIBU KWA TAIFA NA SI YANGA PEKEE NA HIYO SI HULUKA YA WATANZANIA.

 MICHEZO NI FURAHA, UPENDO, UNDUGU, MSHIKAMANO NA KUSHINDANA. 

WAKALI NIGHT, ZOTE MPYA...ZOTE ZA UKWELI.... UNGANA NA TWANGA PEPETA

WAHI TIKETI YAKO MAPEMA

BIASHARA YA MITALIMBO BANDIA YA KIUME YAINGIA JIJINI DAR, WANAUME KAENI CHONJO

Florence Majani -Gazeti la Mwananchi.

KATIKA kile kinachoonekana kuwa baadhi ya wanawake wamedhamiria kumaliza hisia zao za kimapenzi wao kwa wao, biashara ya uuzwaji viungo bandia vya siri vya kiume, imeshamiri jijini Dar es Salaam. Mwananchi Jumapili lilifika hadi katika duka maarufu la vipodozi wilayani Kinondoni na kubahatika kuzungumza na muuzaji aliyejitambulisha kwa jina moja la Kelvin ambaye alisema, viungo hivyo bandia vimekuwa vikigombewa kwa kasi pindi vinafikishwa dukani hapo.

Kelvin alisema, inamuwia vigumu mmiliki wa duka hilo kuwatosheleza wateja wake wengi, wanaoweka oda ya bidhaa hiyo, kutokana na idadi yao kuongezeka.

“Akileta viungo 50, havikai kwa zaidi ya siku tatu, akileta 70 au 90, havimalizi wiki,” alisema Kelvin.

Hata hivyo, muuzaji huyo alidai kuwa, kwa sasa hakuna viungo hivyo kwa sababu mzigo bado haujaingia jambo ambalo limesababisha wateja wengi kuulizia kila siku.

“Kama jana amekuja msanii maarufu wa kike wa nyimbo za taaribu, alikuwa anahitaji viungo, na mbunge mmoja wa kike naye aliviulizia majuzi, lakini ndo hivyo mzigo bado haujaingia,” alisema Kelvin.

Bei ya viungo hivyo Akizungumzia gharama za viungo hivyo, muuzaji huyo alisema, bei inategemea umbile akimaanisha, urefu au upana wa kiungo chenyewe.

“Kuna uume wenye inchi sita, nane hadi 12, pamoja na ukubwa wa kiuno cha mvaaji, kila moja kina bei yake, lakini kiwango cha kawaida ni kuanzia Sh45,000 hadi Sh 80,000,” alisema muuzaji huyo.

Kelvin aliwataja wateja wakubwa kuwa ni wanawake maarufu, raia wa kigeni na wanawake waliozoea maisha ya starehe. Alisema: “Wanaokuja kununua hapa ni wale watu wa ‘viwanja,’ wengine wale walioshindikana kabisa tunawajua wanavuta bangi na unga, lakini pia wanawake wa kizungu nao huviulizia.”

Aidha alisema, duka hilo haliuzi viungo vinavyotumia umeme,(vibrator) kwa sababu vinasemekana kuwa na madhara.

Mwananchi Jumapili lilipotaka kujua ni mahali gani pengine viungo hivyo vitapatikana, jijini Dar es Salaam, kijana huyo alisema, anaweza kwenda kuvipata kwa mama mmoja mkazi wa Msasani ingawa bei itaongezeka.

Kelvin aliyataja maeneo mengine ambapo viungo hivyo vinaweza kupatikana kuwa ni katika maduka makubwa ya vipodozi ya Kariakoo na Sinza.

Ili kupata uhakika wa ni lini viungo hivyo vitawasili, muuzaji huyo alitoa namba ya mmiliki wa duka hilo ambaye baada ya kupigiwa , alidai yeye huwa hauzi, lakini humtafutia wateja mwanamke mmoja mwenye asili ya kiarabu, mkazi wa Upanga ambaye ndiye muuzaji mkongwe.

“Havijawasili hapa nchini siku nyingi, lakini mimi huwa siuzi, namtafutia wateja mama mmoja hivi mwarabu wa Upanga, hata hivyo bado nina bidhaa nyingine kama unahitahi dawa za kuongeza matiti, kuwa mweupe,” alisema mmiliki wa duka hilo.

Wanawake wanasemaje? Baadhi ya wanawake waliohojiwa kuhusu kuongezeka kwa manunuzi ya viungo hivyo, walidai kuwa, hali hiyo inasababishwa na kukata tamaa katika mahusiano.

Pendo Mallya mkazi wa Tabata jijini, Dar es Salaam, alitaja usaliti wa kimapenzi kuwa ndiyo chachu ya wanawake kuchukua uamuzi wa kununua viungo bandia.

“Tumechoka kutendwa (heartbroken), wanaume hawaaminiki, kwa hiyo ili kuepusha kubadili wanaume kila siku, ni bora ujitimizie haja zako mwenyewe,” alisema Pendo.

Aliongeza kuwa licha ya kuepuka kutendwa na wanaume, lakini matumizi ya viungo hivyo yanakutoa katika hatari ya maambukizi ya magonjwa ya zinaa ukiwemo Ukimwi.

“Kitu kingine, ni kuwa unakitumia kila unapokuwa na haja, tofauti na mwanaume atakuambia sipo, nimesafiri leo nimechoka na sababu nyingi,” alisema.

Lakini Edwin Mnzeru alikuwa tofauti na Pendo ambapo yeye aliona wanawake wanaotumia viungo hivyo, wanashabikia ujinga. “Hizi ni athari za utandawazi, tujaribu kuiga mazuri, tuyaache mabaya, siyo kila kitu lazima tufanye,” alisema

Aliongeza kuwa, serikali inatakiwa idhibiti uingizwaji wa bidhaa zote zinazoonekana kuvunja maadili.

Mtaalam wa Saikolojia Mtaalamu wa masuala ya Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Msambaiga, aliitaja sababu kuu inayowasababisha wanawake kununua viungo hivyo kuwa ni usaliti katika mapenzi.

“Mwanamke anapoona anasalitiwa kimapenzi, anaona njia bora ni kujimalizia haja zake mwenyewe, kisaikolojia, anahisi ametibu majeraha kwa kujimiliki,” alisema.

Aliongeza kuwa, wapo wenye hisia kuwa, kufanya mapenzi mwanamke na mwanaume, ni mfumo dume, hivyo anapopata nyenzo kama hizo, hudhani kuwa ametatua matatizo ya mfumo dume.

Alizungumzia suala la utandawazi na kusema, umeruhusu kila taka kuingia, hivyo watu wamepata uhuru wa kujichagulia kile wakitakacho kiwe kibaya au kizuri.

Alisema, wanawake kutumia viungo bandia vya kiume kufanya tendo la ndoa, ni suala la kina lenye sababu chekwa za kisaikolojia, kikubwa kikiwa ni wanawake kukata tamaa katika mahusiano na utandawazi.

Nchi za Magharibi Katika nchi za magharibi, uuzwaji wa viungo bandia, umekuwa jambo la kawaida ambapo yapo maduka na kampuni mahususi kwa ajili ya bidhaa hizo tu.

Hivi karibuni, kampuni za Magharibi ziliibuka na kuanza kuajiri watu watakaoweza kujaribu nyeti hizo bandia kabla ya kuziuza.

Mmoja wa watu walioajiriwa ni Nat Garvey ambaye hulipwa kiasi cha Sh milioni 50 kwa mwezi kwa ajili ya kujaribu uwezo na ubora wa nyeti hizo bandia za kiume.

Anachokifanya ni kujaribu, kisha kuitaarifu kampuni husika kasoro au ubora uliopo katika bidhaa hiyo. Takwimu zinaonyesha kuwa, kiasi cha viungo bandia vya siri milioni nne huuzwa barani Ulaya kila mwaka na huenda idadi hiyo ikaongezeka hadi kufikia milioni 400 katika siku za usoni.

Hivi karibuni kumekuwapo taarifa za ongezeko la wanawake nchini, kufanya mapenzi wenyewe kwa wenyewe wakidaiwa kutumia nyeti badia za kiume.

NIPO MAKINI KAZINI NASIMAMIA LINDO LANGU

Nipo kazini makini kabisa wala msijali na mali zenu nazisimamia vilivyo.

WAKAWAKA BEACH PARTY COMING ON MARCH 25, 2012

MZEE MUHIDIN GURUMO AENDELEA VIZURI, KWA SASA AMELAZWA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI JIJINI DAR

Msanii Mkongwe wa bendi Kwongwe ya Msondo Ngoma Music,Muhidini Gurumo akiwa katika hospital ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam jana, akipimwa mapigo ya Moyo na Ofisa Muuguzi Msaidizi wa Hospital hiyo,Suraiya Mohamed alipolazwa kufanyiwa uchunguzi wa kina toka mwishoni mwa wiki iliyopita.(Picha na www.burudan.blogspot.com)
----
Na Mwandishi Wetu

MWANAMUZIKI maarufu wa bendi kongwe ya  Msondo ngoma, Muhidin Gurumo aliyelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ugojwa wa shinikizo la damu anaendelea vizuri.

Akizungumza na Dar es Salaam jana, Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super 'D' alisema Afya ya  Gurumo inaendelea vizuri na wakati wowote anaweza kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.

Alisema kuwa madaktari wanataka kuchukua vipimo vya mwisho kwa kina kujua kila kitu kinachop msumbua  katika mwili wake.

"Kwa sasa tunashukuru Mungu afya ya Gurumo inaendelea vizuri tofauti na mara ya kwanza na akiendelea hivi anaweza hakurusiwa hivi karibuni"alisema Super D.

Hata hivyo aliwataka wapenzi wa bendi hiyo kumuombea duwa mwanamziki huyo ili apone upesi pia aliongeza kwa kusema maonesho yao ya wiki hii ni kama ifuatavyo Alhamisi watakuwa Mwandege Mkoa wa Pwani, Ijumaa watapiga katika viwanja vya Lidaz Clab jumamosi watakuwa katika viwanja vya TCC Sigara na Jumapili watamaliza wiki endi katika ukumbi wa Max Bar uliopo Ilala Bungoni alisema Super D.

EVANS BUKUKU'S COMEDY CLUB KUANZA KUNG'AA NDANI YA CLOUDS TV JIJINI DAR ES SALAAM

Mchekeshaji wa maarufu nchini kutoka kundi la Vuvuzela Entertainment, Evans Bukuku akitoa maelezo machache juu ya kipindi chao cha Evans Bukuku's Comedy Cloub kilichozinduliwa jana usiku, katika mgahawa wa Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam. Kipindi kilichozinduliwa kwa kuonyeshwa Clouds TV kitakuwa kikionyeshwa kila Jumatatu kuanzia saa 3 usiku na marudio yake yatakuwa kila Jumamosi saa 8mchana.

Mchekeshaji wa maarufu nchini kutoka kundi la Vuvuzela Entertainment, Evans Bukuku akiwa pamoja na wageni wake.
Wageni walialikwa kutoka Clouds Fm&Tv Wasiwasi Mwabulambo, Arnold Kayanda, Abuu.

Mmoja ya watangazaji katika kipindi cha Evans Bukuku's Comedy Club, Taji Liundi akiwa na warembo.

Ilikuwa ni full uhondo kwa hao wachekeshaji wenyewe
Mchekeshaji wa maarufu nchini kutoka kundi la Vuvuzela Entertainment, Evans Bukuku akiwatambulisha wachekeshaji wenzake wanaounda kundi hilo katika uzinduzi wa kipindi uliofanyika Nyumbani Lounge, jijini Dar es Salaa.
...Huyu ndiyo kijana machachali katika upande wa vunja kero.
Evans akionyesha vitu vyake.
Kiongozi wa kundi la Vuvuzela Entertainment, Jacob Mwakamele akielezea machache mbele ya wageni waliokuwa wamealikwa katika uzinduzi huo.

Truck Driving Schools
Idadi ya Watu