Friday, July 17, 2009
GROOVEBACK
MISS ILALA WAINGIA KAMBINI KWA KISHINDO!
Baadhi ya walibwende wa miss Ilala wakiwa katika mwendo wa maringo! kutoka kulia ni Zena Rashidy (22), Slyvia Shally (19) pamoja na Irene Karugaba (19).
Baada ya kuwatembelea warembo ambao ni washiriki wa Miss Ilala 2009 kambini kwao katika hoteli ya Lamada, Ilala jijini Dar es Salaam, shukrani zimwendee mwenyekiti wa kamati ya miss Ilala, Bw. Jackson Kalikumtima.
Walimbwende hao tayari wameingia kambini juzi kwa ajili ya kujinoa vyema tayari kwa kushindana.
Monday, June 29, 2009
KARIBU SABA SABA BANDA LA ARTI-TZ
Karibu sana ujionee teknolojia mbali mbali.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa simu
+255 (0) 713 234 604
+255 (0)786 427 949
+255 (0) 713 797 465
Au ofisi kwetu;
Appropriate Rural Technology
Institute (ARTI-TZ)
Tupo karibu na Massana
(MHS) Hospital
Barabara ya Goba, Mbezi Beach
Dar es Salaam, Tanzania
E-mail: arti.tanzania@gmail.com
Friday, June 26, 2009
CHANNEL O PAYS TRIBUTE TO KING OF POP
Channel O is paying tribute to Michael Jackson in the most fitting way possible – by a video mix and so much more - featuring hit after massive hit from the global icon.
The 30-minute specialised O-Xpress will provide a platform for the universally acknowledged King of Pop’s astonishing array of hits, starting on Saturday 27 June at 09:30 CAT on DStv.
The Michael Jackson O-Xpress tribute will also air at 12:00 CAT and 17:00 CAT and will continue on Sunday June 28 (12:00 CAT and 17:30 CAT), Monday June 29 (13:00 CAT) and Tuesday June 30 (11:00 CAT).
Hit songs like Thriller, Beat It, Billie Jean, Black and White, Scream, Wanna Be Startin' Somethin', I Just Can't Stop Loving You, Bad, The Way You Make Me Feel and You Are Not Alone will be showcased in this unique video mix.
O-Boma (16:00 CAT) and O-Boma Xpress (from 22:00 CAT) will be dedicating today’s live shows to the man.The poll question is – “What is your all time Michael Jackson track?”
Alongside the music, it was Jackson’s dancing – most ironically the Moonwalk – that ensured even his early videos would be something special, and over his career he took care to push the benchmark when it came to creating the visuals to go with his endless supply of hit songs.
Over the course of his career, Jackson sold more than 750m albums worldwide and won 13 Grammy awards. Channel O joins in the other thousands of voices around the world mourning the loss of this one-of-a-kind entertainer and truly gifted musician.
Channel O is available across the continent on DStv channel 320.
Tuesday, June 16, 2009
Mustafa Hassanali Collection At ARISE AFRICA FASHION WEEK 2009


"MDUARA" Mustafa Hassanali launched his PrĂȘt a Porter Spring/Summer 2009/10 Collection “Mduara” on 14 June at the Arise Africa Fashion Week.
Thursday, June 11, 2009
UZINDUZI WA MASHINE MPYA ZA CT-SCAN NA X-RAY
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,DkAmani Abeid Karume,(katikati) Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Shamsi Vuai Nahodha,wakipata maelezo kutoka kwa Mtaalam Mzalendo Dk Khamis Abrahman kuhusu Mashin ya CT-Scan,inayochunguza matatizo mabli mbali ya Binadamu huko Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja jana.
Picha na Ramadhan Othman Ikulu.
Jeff Msangi: Jinsi Ya Kuamsha Na Kulinda Ari
Jinsi ya kuamsha na kulinda ari ya kutimiza malengo yako
Na Jeff Msangi,
Kila mtu ana malengo. Tunachotofautiana ni jinsi tunavyofafanua malengo yetu na mbinu tunazozitumia ili kutimiza malengo yetu. Iwe ni kumaliza madeni uliyonayo, kuwekeza pesa kwa ajili ya kuchukua likizo ndefu,utajiri,familia bora,ndoa nzuri iliyojaa furaha,watoto wenye heshima na adabu, kufanya mazoezi ili kuwa na afya njema zaidi nk yote ni malengo ambayo binadamu hujiwekea mara kwa mara katika safari ya maisha.
Wengine hufanikiwa na wengine hushindwa. Furaha,mafanikio na maendeleo maishani ni vita ya kudumu.Kuna kupanda na kushuka. Cha msingi ni jinsi mtu anavyokabiliana na hali halisi katika wakati halisi.
Kama ambavyo nimeshaandika katika makala zangu za siku za nyuma,kujiwekea na kufafanua vizuri malengo yako ni sehemu muhimu sana ya maisha,maendeleo na mafanikio.
Ni lazima ujue unataka kufanya nini,kwanini na kwa namna au mtindo gani. Malengo ya uhakika ni kama vile kuwa na uhakika na unapotaka kwenda. Usipojua unapotaka kwenda kamwe hutokuwa na uhuru wa kusema “umepotea” kwani hata ulikuwa hujui unapotaka kwenda!Umepoteaje?
Ulikuwa unataka kwenda wapi? Maswali magumu.
Lakini pamoja na malengo ni lazima pia pawe na tamaa au ari ya kutimiza malengo hayo.
Hapo ndipo swali la kwanini linapokuja. Kwanini unatamani utajiri? Kwanini unataka kuwa mwanafunzi bora kushinda wengine wote?Kwanini? Tunapojiuliza maswali kama hilo la kwanini,inatusaidia kuamsha tamaa au ari.Tunakumbuka zaidi malengo yetu na yanakuwa ya uhakika zaidi.Tunajua tunapotaka kwenda na sababu za safari yetu tunazo.
Hata hivyo, mara kwa mara mambo mbalimbali hutokea maishani ambayo yanaweza kutukatisha tamaa. Hapo ndipo tunapohitaji motisha kama ambavyo niliongelea wiki kadhaa zilizopita.
Sasa ili kuhakikisha kwamba siku zote unabakia kuwa katika mstari mnyoofu kuelekea kwenye malengo yako, yapo mambo mbalimbali (unaweza kuyaita maandalizi ukipenda) ambayo unaweza kufanya ili kuhakikisha kwamba safari yako kuelekea kwenye kutimiza malengo yako inakuwa ngumu(siku zote ni ngumu) lakini yenye mbinu mbalimbali za kukabiliana na ugumu wowote utakaojitokeza.Hicho ndicho ninachotaka kuongelea hivi leo; ufanye nini ili usikate tamaa katika kuelekea kwenye malengo yako?
Chagua malengo yanayofaa: Kama nilivyotangulia kusema,tuna malengo tofauti hapa duniani. Jambo la msingi ni kuchagua malengo yanayokufaa.Ni lazima kujifanyia uhakiki binafsi na kujikosoa kwa dhati.Unataka kufanya nini au kuwa kama nani? Unavyo vitendea kazi(vikiwemo vya kimaadili) ili kutimiza malengo yako?Umechagua malengo yanayofaa na hata kukubalika katika jamii yako?Yapo maswali kadhaa(mfano tu) ambayo yanaweza kukusaidia katika kuchagua malengo yanayokufaa
-Je ulimwengu usingekuwa na kitu “pesa” bado ungetaka kutimiza lengo ulilonalo?
-Je tayari umeshaanza kuyafanyia kazi malengo uliyonayo?
-Je ningekupatia Tshs Bilioni moja hivi leo bado ungeendelea kushikilia malengo uliyonayo?
Kama umejibu Hapana katika swali moja au yote hapo juu,una haja ya kuyakagua upya malengo yako. Swali la mwisho hapo juu ni muhimu sana kwani pengine hutopenda kusikia nikikuambia kwamba pesa haitokupa furaha maishani.Kinachoweza kukupa furaha ni ile process ya kuzipata pesa.Hili nitakuja kuliongelea kwa undani katika siku za mbeleni.
Tambua kwamba unaweza kufanya unachotaka kufanya: Ukimuuliza mtu yeyote ambaye tayari ana malengo kwamba ni kwa kiasi gani na kwanini angependa kutimiza malengo aliyonayo, utasikia hadithi nzuri na ndefu ya jinsi ambavyo maisha yake yangebadilika endapo itatokea akatimiza malengo yake. Sasa jiulize, ni kwanini hatimizi malengo yake?
Nini kinamzuia? Au nikuulize wewe msomaji,nini kinakuzuia? Jibu rahisi ni kwamba kama ilivyo kwa wengi wetu,hatuamini kwamba tunaweza kufanya tunachotaka kufanya.
Kwa hiyo tunabakia kuwa na “ndoto za malengo”.Hatuthubutu hata kujaribu!Tunaingiwa na woga. Tunawaza jinsi tutakavyoshindwa kama tutajaribu. Tunaona jinsi tutakavyochekwa,tutakavyodhihakiwa nk.
Kwa hiyo ni lazima ujenge kwa ndani imani kwamba unaweza,inawezekana na hakuna cha kukuzuia.
Kama alivyowahi kusema bwana mmoja aitwaye David Deida; “Kitu pekee kinachofanya ndoto zisitimie ni uoga wa kushindwa”. Usikubali.
Weka Nukuu za Mafanikio ya Wengine:
Uwezekano ni mkubwa sana kwamba kile unachotaka kufanya au ambacho ndio malengo yako,mafanikio yako, tayari kuna mtu au watu ambao wameshakifanya hapa duniani. Ni kina nani? Wao walifanyaje? Ni kitu gani kiliwasaidia kufanikiwa au kufikia walipofikia?
Hayo ni baadhi tu ya maswali ambayo ni muhimu ukayapatia majibu kwani majibu hayo bila shaka yatakusaidia katika safari yako.Pia kwa kuona na kujifunza kutoka kwa wengine, itakupa ari na moyo zaidi kwamba inawezekana. Kama wao walifanya na wakafanikiwa,kwanini wewe ushindwe?
Tafuta Wenzako Wenye Malengo Sawa na Wewe: Mojawapo ya mambo yanayoleta faraja au ahueni katika maisha yetu ni pale unapokutana na mtu ambaye ana “matatizo” au mtu mwenye “misheni” sawasawa na yale uliyonayo.
Ahueni inakuja pale unapogundua kwamba kumbe haupo peke yako.Kunakuwa na nafasi ya kujifunza kutoka kwa uzoefu wa wengine.
Hali ni hiyo hiyo kama unatamani mafanikio na hutaki kukatishwa tamaa njiani.
Jaribu kutafuta marafiki au watu ambao mnafanana katika mawazo na malengo.Ukishawapata nenda nao sambamba. Shirikiana na pia saidiana nao.Mara nyingi motisha hutoka kwa watu kama hao.Jipime mwenendo wako kuelekea katika mafanikio kwa kujilinganisha nao.Shindana nao ikibidi.
Kwa ufupi kila mmoja wetu,ukiwemo wewe unayesoma makala hii, ana uwezo wa kujiwekea malengo na kuyatimiza. Amini kwamba unaweza kufanya unachotaka kukifanya.Amini kwamba malengo uliyonayo yanaweza kufikiwa(kumbuka kujiwekea malengo halisia au yanayotimizika).
Tafuta wenzako ambao aidha wameshafanikiwa au walio njiani kufanikiwa.Angalia mienendo yao.Waulize na upate majibu kutoka kwao ikiwezekana.
Soma habari zao iwe ni magazetini au mitandaoni.Kumbuka kama wao wameweza basi hakuna cha kukuzuia.Kuwa jasiri katika malengo yako.Wapo watakaojaribu kukuyumbisha na kukukatisha tamaa. Usiwajali.Mwisho kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza siku zote;Fanya kazi kwa bidii,uadilifu na maarifa.Tuonane wiki ijayo.
Jeff Msangi ni Mhariri wa mtandao wa www.bongocelebrity.com Unaweza kuwasiliana naye kupitia makala@bongocelebrity.com
HENRY MDIMU AKUTANA NA ANKO MO, FACE TO FACE
Zee la nyeti Henry Mdimu wa Mwananchi Communication akiwa na Anko Mo- wa Tanga walipokutana mjini humo.
Ukitaka mtembelee http://www.ankomo.blogspot.com/
WALIOPATA ULEMAVU MBAGALA KULIPWA MAFAO YAO MILELE
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Wiliam Lukuvi, alisema watu hao watalipwa fidia kulingana na madhara yaliyowapata.
Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa Serikali ipo pamoja nao kwamba na itawasaidia kuendesha maisha yao ya kila siku.
Alifafanua kuwa mafao watakayokuwa wakilipwa watu hao , yatajulikana baada ya wataalamu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutoa mchanganuo wa kile wanachostahili kuwa wanalipwa kulingana na aina ya ulemavu waliopata.
"Wizara ya Afya ndio inahusika na kufanya hesabu, nimewaagiza watuletee idadi kamili ya watu waliopata ulemavu wa kudumu pamoja na mapendekezo yao," alisema Bw. Lukuvi.
Alisisitiza kuwa taarifa hiyo itaambatana na ile tathmini ya maafa itakayotolewa Juni 13, mwaka huu.
Bw. Lukuvi alisisitiza kuwa yupo makini kwa kuwa anaguswa na maafa yaliyowapata wakazi wa Mbagala.
Kuhusu vurugu zilizotokea wakati wa ugawaji misaada kwa waathirika wa mabomu, Bw. Lukuvi alisema kazi ya kusimamia ugawaji wa misaada hiyo ameachiwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bw. Said Mkumbo.
BUSANDA OYEEEEEEEE!!!!
Tuesday, June 9, 2009
Mustafa Hassanali to Showcase at “ARISE AFRICA FASHION WEEK”
Mustafa Hassanali, Tanzania’s renowned Fashion Designer has been invited to the inaugural Arise Africa Fashion Week by Africa Fashion International to be held from June 12- 19, 2009 at the Sandton Convention Centre in Johannesburg, South Africa.
Arise Africa Fashion week shall feature 52 designers from 21 African Countries over a period of 8 Days. Mustafa Hassanali is among the invited designers from Tanzania. This shall be his Seventh Showing in The Republic of South Africa.
(M’Net Face of Africa Finals November 2008 Sun City, Tanzanite One Jewellery Showing in Cape Town during Mining Indaba 2007, Durban Fashion week 2006, Cape Town Fashion week 2005 & 2006 and Vukani Fashion Fair and awards in Pretoria 2004).
Mustafa Hassanali Says “This is a perfect Platform not only for networking but to look at diverse Market opportunities hence the diversification into the Ready to wear market segment” Mustafa Hassanali shall launch his PrĂȘt a Porter Spring/Summer 2009/10 Collection “Mduara”.
The collection has been inspired by the sacred, savoury, significance, Sensual, soulful, synergetic Rhythms of our Swahili nation Mustafa adds “The Vibrancy of our Music, Culture, myths and Beliefs form an integral part of our being hence “Mduara”.
The Local Dance Rhythms has inspired this ready to wear Women Collection which is an eclectic mix of Tradition meeting Modernity and vice versa”
Mustafa Hassanali’s commitment is to not only to promote the creative sector Industry especially Fashion in Tanzania, but also emphasise the Made in Tanzania Concept. He will be accompanied by A Media Contingment that Shall Not only Cover his Showcase on 14 June but also report on the behind the Scenes of the Arise Africa Fashion Week.
The tour of the Media Contingment has been sponsored by Vodacom (www.Vodacom.co.tz), Tanzania Broadcasting Corporation (www.tbcorp.org) and 1time Airlines (www.1time.co.za).
JIUNGE g5click.com

Wadau wako kutoka G5 CLICK ENTERTAINMENT COMPANY
Mustapha B. Selemani







