Articles by "SIASA"
Showing posts with label SIASA. Show all posts
Na Oscar Assenga Tanga

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman ametangaza kuunda kamati maalumu itakayochunguza sababu zilizosababisha uwanja wa CCM Mkwakwani kufungiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokuchezewa mechi.

Akizungumza na waandishi wa habari siku baada ya uwepo wa Taarifa za kufungiwa uwanja huo na TFF,Rajabu alisema kwamba tume hiyo itajumuisha kamati ndogo kutoka CCM,Maafisa wa TFF na baadhi ya wadau soka mkoa wa Tanga.

Alisema kwamba wameamua kufanya hivyo kutokana na kwamba waanaamini kuna uzembe ulijitokeza kwa wale ambao walipewa jukumu la kusimamia uwanja huo na kupelekea kukumbana na rungu hilo la TFF.

Aidha alisema kwamba ameshangazwa na hatua ya TFF kufungia uwanja huo kutokana na hivi karibuni waliufanyia marekebisho makubwa na kujiridhisha kwamba unaweza kutumika kwa ajili ya mashindano mablimbali ya ndani na nje ya hicho hivyo walishangazwa kuona taarifa hiyo.

“Nilikuwa nimesafiri nje ya mkoa wa Tanga kikazi lakini nimelazimika kuhairisha safari yangu ili niweze kushughulika tatizo hilo na ndio maana leo hiii nimefika hapa uwanja kujionea na kuzungumza nanyi wanahabari na kukubaliana na uamuzi wa TFF kwamba zipo dosari ambazo zinapaswa kurekebishwa na hili tutalifanyia kazi”Alisema

Katika hatoba yake fupi iliyojaa hekima alionyesha kutokuwa na imani na viongozi ambao wamepewa dhamana ya kusimamia uwanja hatua iliyopelekea kuwaita mbele ya wanahabari na wadau wengine watoe maelezo.

Awali akizungumza kabla ya mkaribisha Mwenyekiti huyo,Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Mfaume Kizito alisema kwamba uwanja huo ulikuwa kwenye hali nzuri lakini alishtushwa na uamuzi ambao ulichukuliwa na TFF kuufungia uwanja huo.
Pamoja na kauli hiyo Mwenyekiti wa CCM Mkoa alimtaka Meneja wa Uwanja wa CCM Mkwakwani Akida Machai aeleze nini ambacho kimepelekea uwanja huo kufungiwa licha ya kufanyiwa maboresho makubwa katika siku zilizopita.

Ambapo Meneja huyo alidai kuwa moja ya changamoto iliysababisha hali hiyo ni kutokuwepo na maji ya kutosha kutokana na chanzo cha maji kwenye uwanja huo kukauka na kupelekea nyasi za uwanja kukauka.

Alisema kwamba changamoto nyengine ni uwepo wa mchwa katika eneo lenye majani na hivyo kuwalazimu kutumia dawa ya kumwagilia na kufanikiwa kuwaondosha
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 20 Novemba 2025 amepokea Kitabu Maalum chenye mkusanyiko wa habari picha za kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar 2025.

Kitabu hicho kimekabidhiwa na Mkurugenzi wa Tahsil Solutions, Bw. Benny Kisaka, aliyewasili Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kukikabidhi rasmi kwa Rais Dkt. Mwinyi.

Akizungumza mara baada ya kukipokea kitabu hicho, Rais Dkt. Mwinyi amempongeza Bw. Kisaka kwa ubora, umakini na weledi mkubwa uliotumika katika kuandaa na kukusanya taarifa zilizomo ndani ya kitabu hicho, akibainisha kuwa kazi hiyo ni ya thamani katika kuhifadhi historia ya kampeni za uchaguzi.

Kwa upande wake, Bw. Kisaka amesema Kitabu hicho kitaanza kusambazwa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuifikisha taarifa hiyo kwa umma na kuhakikisha historia hiyo muhimu inabaki kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini (CCM), Mhe. Daniel Baran Sillo, amechaguliwa kwa kishindo kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika uchaguzi uliofanyika leo Alhamisi, Novemba 13, 2025, mjini Dodoma.

Uchaguzi huo umefanyika muda mfupi baada ya Bunge kumthibitisha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia uteuzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Katika uchaguzi huo, Mhe. Sillo amepata kura 371 za ndiyo kati ya kura 371 zilizopigwa, ikiwa ni ushindi wa asilimia 100, jambo lililoonyesha imani kubwa ya wabunge kwa uongozi wake.

Baada ya kutangazwa mshindi, Mhe. Sillo alikula kiapo cha uaminifu na kuahidi kushirikiana kwa karibu na Spika wa Bunge pamoja na wabunge wote katika kuhakikisha Bunge linafanya kazi kwa ufanisi, weledi na kwa maslahi ya Taifa.

“Ninaahidi kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu na uwazi mkubwa. Nitahakikisha Bunge linaendelea kuwa jukwaa la mijadala yenye tija kwa wananchi,” alisema Mhe. Sillo baada ya kula kiapo.

Naibu Spika huyo mpya anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge, katika lango kuu la kuingilia bungeni.

Kabla ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, Mhe. Sillo amekuwa mbunge anayejipambanua kwa utendaji na ushiriki wake katika mijadala mbalimbali bungeni, huku akitambulika kama kiongozi kijana mwenye msimamo na uwajibikaji mkubwa.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa hiyo imetangazwa leo, Novemba 13, 2025, ambapo jina la Dkt. Mwigulu, ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), limewasilishwa rasmi bungeni jijini Dodoma kwa ajili ya kupigiwa kura ya kumthibitisha na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wabunge wanatarajiwa kupiga kura muda mfupi ujao kuthibitisha uteuzi huo kabla ya kula kiapo cha wadhifa huo mkubwa wa kitaifa.

Dkt. Mwigulu, ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwemo Waziri wa Fedha na Mipango pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, anatajwa kuwa miongoni mwa viongozi vijana waliopitia ngazi nyingi za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wadadisi wa siasa wanasema uteuzi huo unaonesha dhamira ya Rais Samia kuendelea kuimarisha uongozi wa serikali yake kwa kuwapa nafasi viongozi wenye uzoefu, nidhamu na ufanisi katika utumishi wa umma.

Baada ya kuthibitishwa na Bunge, Dkt. Mwigulu atachukua rasmi nafasi ya Waziri Mkuu na kuanza majukumu yake mara moja.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza Kikao Maalumu cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (CC) kilichofanyika leo Jumatano, Novemba 5, 2025, jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Ofisi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ya kisera na kiutendaji, pamoja na kufanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za Spika na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sambamba na uteuzi wa wagombea wa nafasi hizo katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.


Kikao hicho kinafuatia maandalizi ya kikao cha kwanza cha Bunge la Kumi na Tatu, kinachotarajiwa kufanyika jijini Dodoma wiki ijayo, ambapo wabunge wateule wataapishwa na baadaye kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa juu wa Bunge.

Aidha, ndani ya kikao hicho, Dkt. Samia aliwahimiza wajumbe wa Kamati Kuu kuendelea kudumisha misingi ya chama, umoja, na nidhamu ya kisiasa, akisisitiza umuhimu wa kuweka mbele maslahi ya wananchi na taifa.

“CCM itaendelea kusimama kidete katika kuhakikisha uongozi unaozingatia haki, umoja na maendeleo ya Watanzania wote,” alinukuliwa akisema Dkt. Samia wakati wa kikao hicho.
Kamati Kuu ni chombo cha juu cha maamuzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, chenye wajibu wa kupanga mikakati ya kisiasa na kiutawala kabla ya maamuzi rasmi ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).

Kikao hicho cha leo kimekuwa miongoni mwa vikao muhimu vinavyoashiria mwanzo wa mwelekeo mpya wa uongozi wa Bunge jipya, huku Watanzania wakisubiri kwa hamu majina ya wagombea walioteuliwa kuwania nafasi hizo za juu za uongozi.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Angellah Kairuki, ameendelea na kampeni zake kwa kishindo katika Kata ya Msigani ambapo amewaahidi wananchi kushughulikia changamoto za kijamii na kiuchumi zinazoikabili kata hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Zone, Kairuki alisema kipaumbele chake ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu karibu na makazi yao, ikiwemo ujenzi wa zahanati na shule ya sekondari katika maeneo yanayokosa huduma hizo.

Aidha, ameahidi kufuatilia kwa karibu mchakato wa urasimishaji wa ardhi ili kuhakikisha wananchi wanamilikishwa ardhi kwa haki, uwazi na utaratibu unaoeleweka.
Katika sekta ya miundombinu, Kairuki aliahidi kutatua changamoto ya vivuko katika maeneo ya Kwa Mkama, Kwa Daba, Kwa Mariam, Ukombozi Tanesco, Zone na maeneo mengine, kwa kuweka vivuko bora vitakavyokidhi mahitaji ya wakazi.

Kuhusu usalama wa wananchi, mgombea huyo alisema atasimamia uanzishwaji wa kituo cha polisi katika mitaa ya Msingwa na Malamba Mawili ili kuimarisha hali ya ulinzi na kupunguza matukio ya uhalifu.

Amewaomba wananchi wa Msigani na jimbo lote la Kibamba kumpa kura katika uchaguzi ujao ili aweze kulivalia njuga bungeni tatizo la huduma za kijamii na miundombinu, na kulipatia ufumbuzi wa kudumu.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ratiba ya uchaguzi wa marudio wa udiwani katika Kata ya Nyakasungwa, Jimbo la Buchosa, Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza, kufuatia kifo cha aliyekuwa mgombea wa CCM, Ndugu Feruzi Rajabu Kamizula, kilichotokea Oktoba 9, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Oktoba 18, 2025 na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bw. Kailima R. K., tume ilisitisha shughuli zote za uchaguzi kuanzia Oktoba 10, ikiwemo kampeni, na sasa imetoa ratiba mpya ya kufanyika kwa uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa NEC, fomu za uteuzi kwa mgombea wa udiwani kupitia CCM zitatolewa kuanzia Oktoba 18 hadi 24, 2025, na uteuzi rasmi wa mgombea utafanyika Oktoba 24, 2025.

Kampeni za uchaguzi zitaanza Oktoba 25 hadi Oktoba 28, 2025, na kusimama kuanzia Oktoba 29 hadi Novemba 1, ili kupisha siku ya kupiga kura na kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Kampeni zitaendelea tena kuanzia Novemba 2 hadi Desemba 29, 2025.

Siku ya kupiga kura kwa uchaguzi wa marudio katika Kata ya Nyakasungwa imepangwa kufanyika Jumanne, Desemba 30, 2025.

Tume imeeleza kuwa uteuzi mpya hautahusisha mgombea mwingine yeyote aliyechaguliwa kihalali kabla ya kusitishwa kwa uchaguzi, isipokuwa kama atajitoa rasmi. Aidha, imezikumbusha chama husika na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia Katiba, Sheria na taratibu za uchaguzi ili kuhakikisha mchakato unafanyika kwa amani na haki.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha siku moja baina ya Tume na Waangalizi wa Ndani ya Nchi na Wakimataifa wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 jijini Dodoma leo Oktoba 17, 2025. Kikao hicho kililenga kuwapa waangalizi hao taarifa za maandalizi ya Uchaguzi pamoja na mambo ya kuzingatia ya kiusalama na afya wakati wa uchaguzi. (Picha na INEC).
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha siku moja baina ya Tume na Waangalizi wa Ndani ya Nchi na Wakimataifa wa uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 jijini Dodoma leo Oktoba 17, 2025. Kikao hicho kililenga kuwapa waangalizi hao taarifa za maandalizi ya Uchaguzi pamoja na mambo ya kuzingatia ya kiusalama na afya wakati wa uchaguzi. (Picha na INEC).
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kishereia wa INEC , Ndg. Cyprian Mbugano akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa.
Afisa wa Jeshi la Polisi akiwasilisha mada kuhusu usalama wakati wa uchaguzi
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Dharula na Maafa kutoka Wizara ya Afya, Bi. Yustina Muhaji akiwasilisha mada kuhusu masuala muhumu ya kuzingatia ya kiafta.

Na Mwandishi wetu, Dodoma

Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria za nchi na kuepuka kuingilia au kushiriki katika vitendo vyovyote vinavyoweza kuathiri au kuingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025 wakati wanapotekeleza majukumu yao ya uangalizi.

Wito huo umetolewa leo tarehe 17 Oktoba 2025 na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari, wakati akifungua kikao cha siku moja na Waangalizi hao kwa lengo la kuwapa maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

Katika hotuba yake, Mhe. Jaji Asina amewakumbusha waangalizi hao kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uhuru, na kutokuwa na upendeleo, huku wakizingatia sheria za nchi na Mwongozo wa Waangalizi wa Uchaguzi wa mwaka 2025.

“Waangalizi wanapaswa kuepuka kuingilia shughuli za uchaguzi, kutoonyesha dhihaka kwa watendaji wa uchaguzi, au kutoa maelekezo kwa maafisa wa Tume kuhusu namna ya kufanya kazi zao,” amesisitiza Jaji Asina.

Mhe Jaji Asina ameongeza kuwa endapo kuna malalamiko au dosari yoyote inayojitokeza, waangalizi hao hawana budi kuwasilisha malalamiko hayo kwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa njia ya Tume.

Katika kikao hicho, mada tatu kuu ziliwasilishwa kwa waangalizi wa uchaguzi ambapo mada ya Maandalizi ya Uchaguzi iliwasilishwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi mada ya ma Masuala ya Usalama iliwasilishwa na mwakilishi wa Jeshi la Polisi Tanzania, na mada kuhusu Masuala ya Afya iliwasilishwa na mwakilishi kutoka Wizara ya Afya.

Pia Waangalizi hao walikabidhiwa nyaraka mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha kutekeleza majukumu yao. Nyaraka hizo ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya 2024, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya 2024, Kanuni za Uchaguzi za mwaka 2025, Kanuni za Maadili ya Uchaguzi wa 2025 na Mwongozo wa Waangalizi wa Uchaguzi wa 2025

Aidha, walikabidhiwa vitambulisho rasmi na kuaswa kuvitumia wakati wote wa kutekeleza majukumu yao. Pia walihimizwa kujitambulisha kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika maeneo watakayofika ili kurahisisha ushirikiano na kupata msaada inapohitajika.



Sehemu ya Washiriki wa kikao cha siku ambao ni Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wakisikiliza maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.


Sehemu ya Washiriki wa kikao cha siku ambao ni Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wakisikiliza maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.


Sehemu ya Washiriki wa kikao cha siku ambao ni Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wakisikiliza maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

Sehemu ya Washiriki wa kikao cha siku ambao ni Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifawakisikiliza maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

Sehemu ya Washiriki wa kikao cha siku ambao ni Waangalizi wa uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wakisikiliza maelekezo, taarifa muhimu na miongozo kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao ya uangalizi wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.