Articles by "DKT MWINYI"
Showing posts with label DKT MWINYI. Show all posts
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo tarehe 20 Novemba 2025 amepokea Kitabu Maalum chenye mkusanyiko wa habari picha za kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar 2025.

Kitabu hicho kimekabidhiwa na Mkurugenzi wa Tahsil Solutions, Bw. Benny Kisaka, aliyewasili Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kukikabidhi rasmi kwa Rais Dkt. Mwinyi.

Akizungumza mara baada ya kukipokea kitabu hicho, Rais Dkt. Mwinyi amempongeza Bw. Kisaka kwa ubora, umakini na weledi mkubwa uliotumika katika kuandaa na kukusanya taarifa zilizomo ndani ya kitabu hicho, akibainisha kuwa kazi hiyo ni ya thamani katika kuhifadhi historia ya kampeni za uchaguzi.

Kwa upande wake, Bw. Kisaka amesema Kitabu hicho kitaanza kusambazwa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuifikisha taarifa hiyo kwa umma na kuhakikisha historia hiyo muhimu inabaki kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa Hayati Mzee Mkapa atabaki kuwa mfano wa kuigwa kwa kizazi cha sasa na kijacho kutokana na mchango wake mkubwa katika kujenga misingi ya maendeleo, utawala bora na ustawi wa Taifa.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilijenga nguzo muhimu za umoja wa kitaifa, Muungano, amani na mshikamano wa Watanzania, pamoja na nafasi ya Tanzania katika bara la Afrika na ulimwenguni.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Ibada Maalum ya Kumbukumbu ya Miaka Mitano ya Hayati Benjamin William Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika leo tarehe 23 Julai 2025 Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkoa wa Mtwara.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha kuwa Hayati Mzee Mkapa alikuwa muumini wa ujamaa na uchumi wa soko unaoongozwa na sekta binafsi, lakini pia alihakikisha kuwa maendeleo yanawanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

Ameeleza kuwa Hayati Mzee Mkapa ndiye aliyeanzisha Dira ya Maendeleo 2025, ambayo imekuwa chombo muhimu katika mageuzi ya maendeleo, na mafanikio yake yamekuwa msingi wa kuzinduliwa kwa Dira mpya ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito kwa viongozi wa dini, wanasiasa na wanahabari kuwa sehemu ya kulinda na kuendeleza tunu ya amani kama njia ya kumuenzi Hayati Mkapa.

Amesema kuwa Watanzania wanayo sababu ya kujivunia viongozi waliopo ambao wanaendeleza maono ya viongozi waasisi na kuipeleka Tanzania mbele katika nyanja zote za maendeleo.

Rais Dkt. Mwinyi alizuru kaburi la Hayati Benjamin William Mkapa na kuweka shada la maua, akiongozana na Rais Mstaafu wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi, na Mkewe pamoja na Mjane wa Hayati Mkapa, Mama Anna Mkapa.

Hayati Mzee Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 24 Julai 2020 akiwa na umri wa miaka 81, jijini Dar es Salaam.







































Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akichangia mada wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akiwa katika kazi ya vikundi wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dr. Maulid Maulid akielezea malengo ya Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo (kulia) akizungumza jambo na Kiongozi wa Timu (Shule Bora) Bi. Virginie Briand (kushoto) na Bi. Zainab Dhanani (katikati) kwenye Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dr. Maulid Maulid akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera,Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo.

Na Veronica Mwafisi-Dar es Salaam.

Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Bi. Mwanaamani Mtoo amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya jitihada kubwa katika kuwawezesha wanawake kupiga hatua kimaendeleo.

Bi. Mtoo ameyasema hayo leo kwenye Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.

Amesema uwezeshwaji wa wanawake umefanyika kwa ushirikiano wa Viongozi wa Serikali pamoja na wanawake na wanaume kwani hakuna maendeleo ya wanawake pasipokuwa na wanaume kama ambavyo Sera ya Menejimenti na Ajira ya Mwaka 2008 ilivyotanabaisha katika Sura ya 5 ambayo inazungumzia Anuai za Jamii katika Utumishi wa Umma ambao umeleta msukumo mpya wa ufanisi na tija kwenye utendaji kazi kwa kutumia ujuzi na vipaji walivyonavyo.

Aidha, Bi. Mtoo amesema kwenye Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 298 pamoja na Kanuni za Mwaka 2022 zimeelekeza uzingatiaji wa masuala ya kijinsia ambapo Ofisi hiyo imetoa Mwongozo wa Ujumuishwaji wa Jinsia unaopaswa kutumika wakati wa usimamizi wa rasilimaliwatu ikiwemo kwenye masuala ya usaili na michakato ya ajira ili kuhakikisha watumishi wanawake au kundi la jinsi yenye uwakilishi mdogo linapewa fursa katika nafasi za ajira kwa kuzingatia sifa na vigezo.

“Mwongozo huu ni kielelezo tosha cha dhamira ya Serikali ya kuimarisha ujumuishwaji wa jinsia katika Utumishi wa Umma jambo ambalo ni muhimu katika kuboresha utendaji kazi serikalini unaoiwezesha Serikali kuimarisha uchumi wa nchi na utoaji wa huduma kwa wananchi wote. Amesisitiza Bi. Mtoo.

Ameipongeza Wizara ya Elimu kwa kuleta mapinduzi kwenye Sekta ya Elimu ambayo kwa kiasi kikubwa imewezesha kuibua viongozi mbalimbali wakiwemo wanawake kujumuishwa na kuleta uwiano sawa wa jinsia.

Ameongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kutambua thamani ya mwanamke, inampongeza Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo katika taifa hili.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid Maulid amesema kongamano hilo limelenga kujadili mustakabali wa Mwanamke na Uongozi katika Elimu ambapo itawawezesha kupata maoni, ushauri na mapendekezo yatakayoleta matokeo na mikakati itakayowezesha kupiga hatua kubwa kwa maendeleo ya ustawi wa taifa.
Dar es Salaam, Tanzania – Vodacom Tanzania inayo furaha kutangaza kuunganishwa kwa My Vodacom App na M-Pesa Supa App, hatua inayolenga kurahisisha na kuboresha zaidi huduma kwa wateja. 

Kupitia muunganiko huu, wateja wataweza kufurahia huduma zote wanazozipenda za Vodacom kwenye aplikesheni moja, hivyo kuongeza ufanisi na urahisi wa matumizi.

Kama sehemu ya mabadiliko haya, My Vodacom App itasitishwa rasmi tarehe 1 Desemba 

Tunawahimiza wateja wote kupakua na ku-update M-Pesa Supa App ili kuendelea kufurahia huduma zetu bila usumbufu.Hatua hii inadhihirisha dhamira yetu ya kuboresha huduma kwa wateja kupitia suluhisho za kibunifu. Asante kwa kuichagua Vodacom Tanzania.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza wakati alipofunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi la Ulinzi Tanzania Brigedia Jenerali Abubakari Charo akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Kikosi cha Jeshi 838 JKT Maramba Kanali Ashraf Hassan akizungumza wakati wa mafunzo hayo.

Na Oscar Assenga, MKINGA.

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amesema mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba huku akieleza umuhimu wa vijana hao ni mkubwa kutokana na kwamba wanaingia kwenye Jeshi la akiba ambalo inapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa wanaitwa kwa mujibu wa sheria.

Jenerali Mkunda aliyasema hayo Jumanne Aprili 30 mwaka huu wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ambapo aliwakilishwa na Brigedia Jenerali Abubakari Charo ambapo alisema kutokana na miongozo mbalimbali iliyopo kwa mafunzo hayo ya vijana hasa kwa kuzingatia kwamba vijana hao wanapohitimu mafunzo yao wanaingia kwenye jeshi la akiba.

Alisema kwamba linapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa na Rais na Amri Jeshi Mkuu akatangaza hali ya hatari vijana hao wanaitwa kwa mujibu wa sheria kwenda kuungana na Jeshi la Wananchi (JWTZ) kulinda ulinzi wa Taifa.

Aidha alisema kutokana na umuhimu wa vijana kwenye Jeshi hilo wanapenda kuona wanafikia viwango na malengo ya mafunzo hayo na amewaona wamefikia viwango vinavyotakiwa huku akieleza yanawajenga kwenye nidhamu, ukakamavu, uzalengo, uhodari wa kujiamini na kulipenda taifa lao.

“Nichukue fursa hii kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kutoa shukrani kwa dhati kwa Serikali kwa juhudi zinazofanyika kuhakikisha mazingira ya mafunzo kwa vijana ndani ya JKT yanaboreshwa”Alisema

“Kwani katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetoa kiasi cha sh Milioni 950 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa vijana wanaojiunga na JKT fedha hizo zimeweza kujenga mabweni 12 kila moja lenye uwezo wa kuchukua vijana 120 hivyo kusaidia kikosi kuongeza uwezo kuchukua vijana 1440 na hii ni ishara za wazi kwamba serikali inatambua na kuthamini mafunzo ya vijana wa JKT”Alisema

“Lakini pia ujenzi wa vyoo vitano ambapo kila choo kina matundu 22 vitatumika kwa vijana hilo sio suala dogo ni jambo kubwa ambalo serikali imefanya kwa mazingira hayo wanawaomba vijana ambao hawapati fursa kujiunga na JKT wasije kufikiria wametengwa na kunyimwa fursa bali lengo vijana wote wapite Jkt na wale vijana wanaomaliza kidato cha sita”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Kujenga Taifa litakuwa likiendelea kuongozewa uwezo huku akieleza wanathamini juhudi za serikali katika kuboresha mazingira ya jeshi hilo ambapo mafunzo ambayo wameyapata yatawawezesha kuajiriwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,sekta mbalimbali za serikali au makampuni mbalimbali .

Awali akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema mafunzo hayo kwa vijana wa JKT ni muhimu sana kwa vijana kwa maana wao ndio tegemeo la Taifa.

Balozi Batilda alisema Rais Dkt Samia Suluhu kupitia falsafa yake ya 4R ameendelea kusimamia na ndio maana juzi chadema walikuwa na maandamano yao wakasimamiwa vizuri na jeshi la Polisi wakafanya mkutano wao wakatembea.

Alisema kwa hakika wakawa na matumaini watapata mambo ya msingi yatakayowasaidia kujenga nchi lakini wakasikia mambo tofauti kwanini wakuu wa mikoa hawapigiri kura, kama madiwani sasa akasema hata RC akipigiwa kura atachaguliwa Tanga na RC ni msaidizi wa Rais anaweza kuhamishwa kila eneo.

“Tulitegemea kwamba hivi sasa nchi ipo kwenye kipindi kigumu na mvua zinanyesha madhara maeneo mengi barabara nyingi zimepata changamoto na maeneo mengi lami zimepasuka changamoto ni nyingi vita vya israel vinaendelea duniani gharama zinapanda bei ya dola ipo kubwa kulingana na bei yetu sisi tukaona haja hoja zao za za kwamba hazikuwasaidia wakapata mawazo mbadala hazipo"Alisema.

Hata hivyo Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda alisema kwamba alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa sababu yanaleta tija kwa vijana katika shughuli za kujitegemea huku akiwataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya.

Aliwataka pia vijana hao kutumia elimu waliyoipata wakaweze kutatua changamoto mbalimbali pasipo kuvunja sheria na taratibu zilizowekwa hapa nchini huku akisiistiza watumie nidhamu pekee kama silaha kwenye jambo lolote mbeleni.