Articles by "KITAIFA"
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa habari za mitandaoni kutoka vyama vya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari (kulia) akizungumza na waandishi wa habari za mitandaoni kutoka vyama vya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari akifafanua jambo katika kikao kazi na waandishi wa habari za mitandaoni kutoka vyama vya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari akipokea maoni ya Tanzania Bloggers Network (TBN) kuhusu changamoto za wanachama wake toka kwa, Mwenyekiti wa TBN Taifa, Bw. Beda Msimbe.
Kikao kikiendelea.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam Desemba 18, 2025: Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeahidi kushughulikia changamoto na vikwazo vinavyowakabili waandishi wa habari za mitandaoni na bloga ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maslahi ya taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, wakati wa kikao kazi kilichofanyika jijini Dar es Salaam, kikishirikisha TCRA na waandishi wa habari za mitandaoni kutoka Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA).

Bw. Msigwa alisema Serikali iko tayari kufanya marekebisho ya sera na kanuni endapo zitabainika kuwa zimepitwa na wakati au kuwa kikwazo kwa waandishi wa habari za mitandaoni, mradi tu marekebisho hayo yafanywe kwa ushirikiano na kwa kuzingatia maslahi ya taifa.

“Kama kuna sera au taratibu zinaonekana kuwa kikwazo kwa waandishi wa habari za mitandaoni, tunaweza kukaa pamoja tukazipitia na kuzifanyia marekebisho. Lakini ni muhimu nanyi katika kazi zenu mtangulize maslahi ya taifa,” alisema Msigwa.

Alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kujenga mazingira wezeshi kwa waandishi wa habari za mitandaoni, huku akisisitiza kuwa kundi hilo lina wajibu wa kutumia fursa hiyo kwa uzalendo na kulinda maslahi ya nchi.

“Tusitegeane. Haiwezekani Serikali ijenge mazingira mazuri ya kazi halafu ninyi mnatumika kulidhuru taifa. Rais ndiye kiongozi Mkuu wa Serikali anayewaunga mkono, na ndio maana mnaalikwa katika matukio ya Serikali kama wanahabari wengine,” alisema.

Aidha, aliipongeza TCRA kwa kupokea maoni ya waandishi wa habari hao na kuonesha utayari wa kuyafanyia kazi, akibainisha kuwa ada na leseni siyo kikwazo kikubwa kuliko umuhimu wa kazi wanayoifanya kwa taifa.

“Leseni na ada tusiziogope. Ni ulinzi na utambulisho wa kazi zenu. Kinachotakiwa ni kuhakikisha taarifa mnazozitoa zina manufaa kwa taifa letu,” alisisitiza.

Bw. Msigwa alieleza kuwa uwepo wa utaratibu wa kuwatambua waandishi wa habari za mitandaoni ni muhimu ili kulinda taaluma hiyo dhidi ya watu wasiokuwa na sifa, hali inayoweza kudhoofisha tasnia ya habari.

Kutokana na hilo, aliwahimiza waandishi wa habari za mitandaoni na bloga kujisajili katika Bodi ya Ithibati ya Wanahabari Tanzania ili waweze kutambulika rasmi na kunufaika na mafunzo maalum yatakayoratibiwa na Serikali.

“Nawaomba mjisajili kwenye Bodi ya Ithibati ya Wanahabari. Mafunzo yakianza, mtakuwa miongoni mwa wanufaika na mtakuwa bora zaidi katika kazi zenu,” alisema.

Kuhusu malalamiko ya kodi, Bw. Msigwa alisema suala hilo limeshachukuliwa na Serikali, huku akiahidi kuzungumza na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kuandaa mazungumzo ya pamoja yatakayolenga kupata muafaka.

“TRA ni taasisi makini na ina maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwezesha sekta mbalimbali kufanya kazi. Ninaamini mtapata suluhu ya changamoto hizi,” alisema.

Aliongeza kuwa kazi za waandishi wa habari zina mchango mkubwa katika kukuza mapato ya taifa kwa kuhamasisha ulipaji kodi, uwekezaji na utalii, akisisitiza umuhimu wa kutoa taarifa chanya kuhusu usalama na fursa zilizopo nchini.

“Habari zako zinaweza kuhamasisha uwekezaji, utalii na hata kuongeza mapato ya kodi. Waambieni watalii kuwa Tanzania ni nchi salama na iko tayari kuwakaribisha,” alisema.

Pia aliwataka waandishi wa habari za mitandaoni kupuuza taarifa za uzushi na uchochezi zinazolenga kulichafua taifa, akisisitiza kuwa uzalendo ni nguzo muhimu ya maendeleo ya sekta ya habari.

Kwa upande mwingine, Bw. Msigwa alisema Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeanza mchakato wa kuanzisha mfuko wa waandishi wa habari utakaosaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili wanahabari katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Tumeanza mchakato wa kuanzisha mfuko wa waandishi wa habari. Tuombeeni dua ili ufanikiwe na ufanye kazi kama ulivyokusudiwa. Lazima tuwe wazalendo ili jitihada hizi zifanikiwe,” alisema.
Balozi wa Tanzania nchini Uswidi, Mhe. Mobhare Matinyi (wa nne kutoka kushoto mstari wa mbele), akiwa pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Raddy Energy ya Tanzania, Ramadhani Mlanzi (kulia kwake), katrŕ⁴ika picha ya pamoja na wawakilishi wa taasisi za fedha za Serikali ya Uswidi, kampuni ya Siemens Energy, Benki ya CRDB, Ubalozi na Raddy Energy, jijini Stockholm, mara baada ya kikao kilichofanyika siku chache zilizopita kukamilisha mchakato wa ununuzi wa mitambo minne ya kuzalisha umeme wa gesi itakayoletwa nchini ili kuimarisha uzalishaji wa umeme nchini.
Kikao cha pamoja baina ya Ubalozi wa Tanzania nchini Uswidi, kampuni ya Raddy Energy, Benki ya CRDB na wawakilishi wa taasisi za fedha za Serikali ya Uswidi wakiendelea na kikao jijini Stockholm, hivi karibuni.
---
Stockholm, Sweden Desemba 19, 2025:  Kampuni ya Raddy Energy Solution Limited ya Tanzania imeingia makubaliano ya kununua mitambo minne ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia yenye jumla ya megawati 177 (MW) kutoka kampuni ya Siemens Energy ya Sweden kwa thamani ya dola za Marekani milioni 320, hatua inayotarajiwa kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, mitambo hiyo inatarajiwa kuwasili na kufungwa nchini Tanzania ifikapo mwishoni mwa mwaka 2027. Ununuzi huo umewezeshwa na Benki ya CRDB kama mshirika wa ndani katika uratibu na ufadhili wa mradi. Raddy Energy ni kampuni dada na Kiwanda cha Raddy Fibers kilichopo Mkuranga, mkoani Pwani.

Katika utekelezaji wa mradi, CRDB itashirikiana na taasisi za fedha za Serikali ya Sweden zikiwemo Wakala wa Mikopo ya Mauzo ya Nje wa Sweden (EKN), Shirika la Mikopo ya Mauzo ya Nje (SEK), Taasisi ya Fedha za Maendeleo ya Sweden (Swedfund), Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Sweden (SIDA) pamoja na Business Sweden. Taasisi hizi zote ni za serikali ya Sweden.

Aidha, Baraza la Kimataifa la Viwanda la Sweden (NIR) litakuwa sehemu ya timu ya ushauri wa kimataifa itakayouendesha mradi huo. Raddy Energy imesema mpango huu ni mwanzo wa safari kubwa, ambapo kampuni inalenga kufikisha uzalishaji wa umeme hadi MW 1,000 ifikapo mwaka 2030, ili kukidhi mahitaji ya ndani na kuwezesha uuzaji wa umeme nje ya nchi.

Katika kuimarisha makubaliano hayo, watendaji wa Raddy Energy walifanya ziara ya kimkakati nchini Sweden kuanzia Desemba 10–13, 2025, chini ya uratibu wa Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden. Ujumbe huo ulikutana na watendaji wa Siemens Energy na taasisi za fedha za serikali ya Sweden katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje, Stockholm, kabla ya kuzuru makao makuu ya Siemens mjini Finspäng.

Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, huku Raddy Energy ikiwakilishwa na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Ramadhan Hassan Mlanzi, pamoja na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara na Miradi, Bw. Ediphine Masase. Timu ya CRDB iliongozwa na Bw. Musa Lwila, ikijumuisha Bw. Saidi Salehe na Bw. Andrew Mbunda.

Kwa upande wa Siemens Energy, kikao hicho kilihusisha Mkurugenzi wa Ufadhili wa Miradi, Bw. Joakim Tornberg, na Meneja Mwandamizi wa Mauzo, Bi. Christiane Carlsson, huku timu ya Serikali ya Sweden ikiongozwa na Mshauri Mwandamizi wa Biashara na Uendelezaji kwa Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Pia Roed. Wawakilishi wengine walitoka Business Sweden, SIDA, Swedfund, EKN, SEK na NIR.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Balozi Matinyi alieleza mwelekeo wa kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Sweden, akisisitiza kuwa Tanzania ina fursa kubwa katika sekta za nishati, madini, viwanda, kilimo cha biashara, usafirishaji, utalii, teknolojia na ubunifu.

Mradi huo unatajwa kuwa miongoni mwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya nishati, unaotarajiwa kuongeza uzalishaji wa umeme, kuchochea viwanda, kuimarisha ajira na kuisogeza Tanzania katika lengo la kuwa kitovu cha nishati ya uhakika katika ukanda.

Imetolewa na:
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Sweden
Stockholm, 19 Desemba 2025.
Dar es Salaam Desemba 18, 2025: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewapongeza waandishi wa habari za mtandaoni na bloga wanaounda Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) na Jukwaa la Mitandao Tanzania (JUMIKITA), na kuagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuwalea vizuri na kuwapa fursa ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Pongezi na maelekezo hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, alipokuwa akifunga kikao cha pamoja cha wanachama wa TBN na JUMIKITA kilichoandaliwa na TCRA jijini Dar es Salaam, Desemba 18, 2025.

Bw. Msigwa alisema Rais Samia anatambua mchango mkubwa wa waandishi wa habari za mtandaoni katika kusambaza taarifa na kuimarisha mawasiliano kati ya serikali na wananchi, hivyo akaagiza wapewe malezi, miongozo na fursa zitakazowawezesha kufanya kazi zao kwa weledi.

“Mheshimiwa Rais amewapongeza sana na anatambua kazi zenu nzuri. Ni maelekezo yake kwamba kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Idara ya Habari MAELEZO na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kupitia TCRA, waandishi wa habari za mitandaoni na bloga walelewe vizuri na wapewe fursa ili wafanye kazi zao vizuri,” alisema Msigwa.

Alisisitiza kuwa maelekezo hayo ni maagizo ya moja kwa moja kutoka kwa Rais na kwa utaratibu wa kiserikali, yanapaswa kutekelezwa bila mjadala.

“Haya kwetu ni maelekezo. Kwa utaratibu wa serikali, ukishapewa maelekezo kinachofuata ni utekelezaji. Ndiyo maana tupo hapa kuhakikisha maagizo ya Mheshimiwa Rais yanatekelezwa,” alisema Msigwa huku akishangiliwa na washiriki wa kikao hicho.

Aidha, alisema mwelekeo huo unaendana na falsafa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inayosisitiza ushirikiano kati ya serikali na wadau mbalimbali kwa manufaa ya taifa.

Aliitaja Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jukwaa la Mitandao Tanzania (JUMIKITA) kuwa ni wadau wakubwa wa serikali katika tasnia ya habari, akibainisha kuwa mchango wao ni muhimu katika kusambaza taarifa sahihi na kujenga mawasiliano yenye tija kati ya serikali na wananchi.

“Serikali imewaamini waandishi wa mitandaoni. Sasa ni wajibu wenu kuendeleza imani hiyo kwa kuzingatia maadili, ukweli na uzalendo katika kazi zenu. Ushirikiano wetu umeendelea kuimarika na changamoto zinazojitokeza tunazitatua kwa pamoja,” alisema Msigwa.

Kikao hicho kililenga kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na wadau wa habari za mtandaoni pamoja na kujadili masuala ya maendeleo ya tasnia ya habari katika mazingira ya kidijitali.

Geita, Tanzania – Kampuni ya Buckreef Gold imezidi kuimarisha ushirikiano wake na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia makubaliano mapya ya Uwajibikaji kwa Jamii yenye thamani ya Shilingi milioni 600, yanayolenga kuboresha huduma za afya, elimu, maji na usafi wa mazingira kwa jamii zinazozunguka mgodi.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martine Shigella, aliipongeza kampuni hiyo kwa kujali maendeleo ya jamii kwa nidhamu na kwa kuzingatia sheria. “Buckreef imeonyesha umakini katika kutekeleza wajibu wake kwa kupanga, kutenga bajeti na kutekeleza miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii kwa kuzingatia matakwa ya serikali. Muhimu zaidi ni kuona matokeo ya wazi na ya kudumu kupitia maendeleo ya shule, vituo vya afya na huduma za maji zinazoboreshwa maisha ya kila siku,” alisema Mhe. Shigella.
Maeneo ya uchimbaji madini mkoani Geita yameendelea kushuhudia ongezeko la idadi ya watu kutokana na shughuli za kiuchumi kuvutia wafanyakazi na familia. Hali hii imezidi kusababisha shinikizo kwa huduma za umma, hasa katika kata za Rwamgasa, ambapo idadi ya wakazi imezidi 60,000. Zahanati zinahudumia wagonjwa wengi zaidi ya uwezo wake, shule zina ukosefu wa vyumba vya madarasa na miundombinu ya vyoo, na upatikanaji wa maji safi bado ni changamoto.

Ni katika muktadha huu ndipo mpango wa sasa wa Uwajibikaji kwa Jamii umebuniwa. Katika sekta ya elimu, ujenzi wa madarasa na vyoo unalenga kutoa mazingira salama ya kujifunzia, kupunguza msongamano na kurejesha heshima kwa wanafunzi. Madarasa mapya katika Shule ya Msingi Isunganghoro na uboreshaji wa miundombinu katika Shule ya Msingi Lubanda vitawawezesha watoto kusoma katika mazingira yenye afya na usalama, jambo linaloathiri mahudhurio na matokeo ya muda mrefu.
Katika sekta ya afya, uwekezaji katika zahanati za Rwamgasa, Lubanda na Ibisabageni unalenga kukidhi mahitaji yanayoongezeka. Ujenzi wa majengo ya wodi, nyumba za watumishi, mifumo ya maji na miundombinu ya vyoo unalenga kuboresha huduma kwa wagonjwa huku ukiimarisha wahudumu wa afya. Makazi ya watumishi karibu na zahanati pia husaidia uendelevu wa huduma na mwitikio wa dharura.

Miradi ya maji na usafi wa mazingira, ikiwa ni pamoja na kisima cha maji safi katika zahanati ya Lubanda, ni suluhisho la moja ya mahitaji muhimu zaidi ya jamii. Upatikanaji wa maji safi husaidia kudhibiti maambukizi, kuboresha huduma kwa wakina mama na watoto, na kudumisha usafi wa mazingira, hasa wakati wa kiangazi.
Meneja Mkuu wa Buckreef Gold, Bw. Isaac Bisansaba, alisema kampuni inachukulia kuboresha huduma za jamii kama jukumu la msingi. “Shughuli zetu zinafanyika ndani ya jamii halisi. Kadri uzalishaji unavyoongezeka, ndivyo wajibu wetu kwa jamii unavyoongezeka. Miradi hii inalenga afya, elimu na maji kwa sababu hapo ndipo athari chanya huhisiwa moja kwa moja na familia,” alisema Bw. Bisansaba.

Zaidi ya miradi ya jamii, Buckreef Gold pia inachangia uchumi wa kila siku wa Geita kupitia ajira na ununuzi wa bidhaa na huduma ndani ya nchi. Ajira huwezesha familia kukidhi mahitaji, kuendeleza elimu na kuimarisha ustawi wa kaya, huku ununuzi kutoka kwa biashara za ndani ukiwapa wasambazaji fursa ya kukua na kuunda ajira zaidi.

Mwaka uliopita, Buckreef Gold iliwekeza Shilingi milioni 420 katika miradi ya jamii, ikiwemo ujenzi wa madarasa salama, ukamilishaji wa vituo vya afya na kazi za barabara zilizoboreshwa. Tangu kuanza kwa shughuli za mgodi, jumla ya Shilingi bilioni 1.86 zimewekezwa katika miradi ya maendeleo ya jamii kote Geita.
Makubaliano mapya ya Uwajibikaji kwa Jamii yanathibitisha kwamba uchimbaji madini unaowajibika unajengwa juu ya watu, ushirikiano na vitendo vinavyoleta matokeo chanya na kudumu kwa jamii za Geita. Mgodi wa Buckreef Gold unaendeshwa kwa ubia kati ya TRX Gold Corporation na STAMICO, unaunganisha utaalamu wa kimataifa wa uchimbaji madini na ushiriki wa moja kwa moja wa Serikali, kuhakikisha uwekezaji wa jamii unalingana na vipaumbele vya kitaifa na mipango ya maendeleo ya wilaya.
Dodoma, Desemba 17, 2025: Serikali ya Marekani imetangaza kuiweka Tanzania katika kundi la nchi zilizoanza kudhibitiwa kwa taratibu za visa za kuingia nchini humo, hatua iliyotokana na viwango vya juu vya raia wanaokiuka masharti ya visa, hususan kwa kuzidisha muda wa ukaaji.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, uamuzi huo ulitangazwa na Rais wa Marekani, Donald Trump, tarehe 16 Desemba 2025, na unahusisha jumla ya nchi 15, zikiwemo pia baadhi ya nchi za Afrika.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Tanzania ina viwango vya ukaaji wa zaidi ya muda unaoruhusiwa vya asilimia 8.30 kwa visa za B1/B2 (biashara na utalii) na asilimia 13.97 kwa visa za F, M na J zinazohusisha wanafunzi, mafunzo ya ufundi na programu za kubadilishana.

Kutokana na viwango hivyo, Serikali ya Marekani imeeleza kuwa hatua hiyo inalenga kulinda mifumo yake ya uhamiaji na kuhakikisha kuwa waombaji wa visa wanazingatia kikamilifu masharti wanayopewa.

Hata hivyo, Serikali ya Tanzania imesisitiza kuwa vikwazo hivyo si marufuku kamili, bali ni udhibiti wa taratibu za utoaji visa, na kwamba Watanzania wanaokidhi vigezo na masharti wataendelea kupewa visa kulingana na tathmini itakayofanywa.

Serikali imesema itaendelea kufanya mazungumzo ya kidiplomasia na Serikali ya Marekani ili kufikia muafaka kwa maslahi ya wananchi, huku ikiwasisitiza Watanzania wanaosafiri kwenda Marekani kuzingatia kikamilifu masharti ya visa ili kuepuka athari binafsi na kwa taifa kwa ujumla.

Wizara ya Mambo ya Nje imesisitiza kuwa itaendelea kutoa taarifa kadri mazungumzo na hatua zaidi zitakavyoendelea.

Nairobi, Desemba 17, 2025: Kampuni ya East African Breweries PLC (EABL) imetangaza kuwa kampuni ya Diageo imekubali kuuza hisa zake zote za EABL na umiliki wake katika kampuni ya vinywaji vikali ya UDV (Kenya) Limited kwa kampuni ya Asahi Group kutoka Japan.

Hatua hii inaifanya Asahi kuwa kampuni ya kwanza kubwa kutoka Japan kuingia rasmi na kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika biashara ya vinywaji barani Afrika.

Baada ya ununuzi huu kukamilika, Asahi itakuwa mmiliki mkuu wa EABL na itasimamia shughuli zake zote nchini Kenya, Uganda na Tanzania. Kampuni hiyo imeeleza kuwa itaendelea kuziendeleza chapa za ndani ambazo wananchi wamezizoea, huku pia ikileta baadhi ya chapa zake maarufu duniani kwa walaji wa Afrika Mashariki.

Kwa makubaliano haya, Diageo inatarajia kupata mapato ya takribani dola bilioni 2.3 za Marekani baada ya kodi na gharama nyingine, sawa na shilingi Trilioni 5.69 za Tanzania. Thamani ya jumla ya EABL kwa makubaliano haya imekadiriwa kufikia dola bilioni 4.8, sawa na takribani  Shilingi trilioni 11.87 za Tanzania.

Ununuzi huu unaonesha imani kubwa ya wawekezaji katika ukuaji wa EABL na mustakabali wa soko la Afrika Mashariki, eneo ambalo linaendelea kukua kwa kasi kiuchumi na kwa idadi ya watu. Chini ya umiliki mpya, EABL inatarajiwa kuendelea kufanya vizuri na kupanua biashara yake zaidi.

EABL imeeleza kuwa inaingia katika ukurasa mpya wa ukuaji pamoja na Asahi, kampuni ambayo itanufaika na viwanda vya kisasa vya EABL, uzoefu wa uongozi wake, chapa imara, mtandao mzuri wa usambazaji pamoja na mahusiano mazuri na wafanyakazi, washirika na wateja.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa EABL, Bi. Jane Karuku, alisema kuwa ununuzi huo ni fursa kubwa kwa kampuni. Alisema mmiliki mpya analeta uzoefu mkubwa wa kimataifa katika ubunifu na ukuzaji wa chapa, jambo litakalosaidia EABL kufikia lengo lake la kuwa kampuni ya vinywaji inayoheshimika zaidi barani Afrika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa mpito wa Diageo, Bw. Nik Jhangiani, alisema Diageo inajivunia safari na mafanikio ya EABL katika nchi za Kenya, Uganda na Tanzania. 

Aliongeza kuwa Diageo itaendelea kushirikiana na Asahi kupitia matumizi ya baadhi ya chapa zake katika eneo la Afrika Mashariki, huku muamala huu ukiisaidia Diageo kuimarisha hali yake ya kifedha.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Asahi Group, Bw. Atsushi Katsuki, alisema EABL ni kampuni imara yenye nafasi kubwa sokoni, ikiwa na chapa zenye nguvu, viwanda vya kisasa na timu yenye uzoefu. Alisema Asahi inalenga kukuza biashara kwa njia endelevu na kuchangia maendeleo ya uchumi wa nchi zinazohusika.

Muamala huu bado unahitaji kibali kutoka kwa mamlaka za serikali na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka 2026. EABL imesisitiza kuwa hakutakuwa na mabadiliko katika shughuli zake za kila siku na hakuna wafanyakazi watakaopoteza ajira kutokana na mabadiliko haya.

Katika kipindi cha mpito, Diageo itaendelea kushirikiana na Asahi ili kuhakikisha mabadiliko yanafanyika kwa utulivu na shughuli zinaendelea bila usumbufu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Kenya nchini Tanzania anayemaliza muda wake Mhe. Isaac Njenga Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 17 Desemba 2025. Balozi wa Kenya Mhe. Isaac Njenga alifika Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumuaga Mhe. Rais Dkt. Samia ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia kuimarika kwa uhusiano wa kibiashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Kenya nchini Tanzania anayemaliza muda wake Mhe. Isaac Njenga Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 17 Desemba 2025.
Nairobi. Rais wa Jamhuri ya Kenya, Dkt. William Ruto, amemtunuku mwanaharakati wa mazingira Truphena Muthoni Medali ya Head of State Commendation (HSC) kwa mchango wake wa kipekee katika kuhamasisha uhifadhi wa mazingira na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Tuzo hiyo imetolewa kufuatia hatua ya kihistoria ya Muthoni ya kutumia saa 72 mfululizo akikumbatia mti wa asili, tukio lililovunja rekodi na kuvutia hisia za kitaifa na kimataifa kuhusu umuhimu wa kulinda mazingira.
Rais Ruto alisema alifurahishwa na ujasiri, uthubutu na dhamira ya dhati aliyoionesha Muthoni, akieleza kuwa vitendo vyake vinaakisi roho ya uzalendo na uongozi unaohitajika katika kukabiliana na changamoto za mazingira.

“Hatua yake ni ujumbe mzito kwa dunia nzima kuhusu wajibu wetu wa kulinda mazingira kwa vizazi vijavyo,” alisema Rais Ruto.
Katika kutambua mchango huo, Rais amemteua Truphena Muthoni kuwa Balozi wa Kampeni ya Kitaifa ya Kupanda Miti Bilioni 15, mpango mahsusi wa serikali unaolenga kurejesha misitu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Kenya.

Aidha, Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Kenya (KTB) limempa Muthoni pamoja na timu yake likizo iliyodhaminiwa kikamilifu kama sehemu ya kuthamini juhudi zake za kuhamasisha jamii.
Wakati huo huo, Wizara ya Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Misitu imetangaza kuunga mkono ndoto ya Muthoni ya kutembelea Brazil ili kupata uzoefu wa kimataifa kuhusu uhifadhi wa mazingira na uongozi wa kimazingira.

Hatua ya serikali kumuenzi Truphena Muthoni inaonesha dhamira ya Kenya ya kuwa mstari wa mbele katika mapambano ya kulinda mazingira, huku ikiendelea kuhimiza ushiriki wa vijana katika kulinda rasilimali za taifa.
Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa letu lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.

Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:

"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."

Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania

Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.

Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:

"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."

Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.

Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi

Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:

"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."

Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.

Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.

TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!

Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!

Beda Msimbe
Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)
Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership.

Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania.

“The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said.

The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active technical review.

President Samia welcomed Washington’s renewed commitment and assured the delegation that Tanzania remains focused on completing the remaining procedural steps.

“As a non-aligned nation, Tanzania is open, ready, and committed to working with all partners who respect our sovereignty and share our vision for prosperity,” the President said.

“These strategic projects are of national importance, and we are determined to finalise them so they can unlock jobs, investment, and sustainable prosperity for our people.”

The President highlighted that more than 400 American companies currently operate in Tanzania—reflecting the country’s stability, openness to investment, and strong historical ties with the United States.

Beyond investments, the meeting touched on broader areas of cooperation, including political stability, regional security, economic reforms, private-sector growth, health-sector partnerships, and people-to-people exchanges.

Ambassador Lentz congratulated President Samia for her vision and long-term national planning through Vision 2050, noting the U.S. Government’s readiness to support its implementation and reinforce the President’s 4R philosophy of reconciliation, resilience, reforms, and rebuilding trust.

Both sides agreed that strengthened communication, consistent engagement, and timely action on pending agreements are key to unlocking the full potential of U.S.–Tanzania relations.

This meeting marks a pivotal moment in redefining and revitalising the U.S.–Tanzania relationship. The reaffirmed commitment from both governments signals the emergence of a modern, transparent, private-sector-driven partnership rooted in shared prosperity, mutual respect, and long-term strategic cooperation.

Flagship Projects

1. LNG Project — Estimated Value: USD 42 Billion

A transformative natural gas development involving leading international energy companies. The project aims to unlock Tanzania’s vast offshore gas reserves, boost national revenue, create thousands of jobs, and position the country as a major global LNG supplier.

2. Tembo Nickel Project — Value: USD 942 Million

A major critical-minerals investment in Ngara focused on nickel—an essential component in electric-vehicle batteries. The project will support global clean-energy supply chains, stimulate industrialisation, and expand Tanzania’s export base.

3. Mahenge Graphite Project — Value: USD 300 Million

One of the world’s largest high-grade graphite deposits, positioned to serve the fast-growing battery and renewable-energy sectors. The project will reinforce Tanzania’s role as a leading supplier of battery-grade minerals.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili.
Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili.

“Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz.

Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaendelea kufanyiwa uchambuzi wa kiufundi.
Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.

“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”

Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania—kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.

Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.

Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais—maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.

Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.

Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi—ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.

Miradi Mikuu ya Kimkakati

1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42

Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.

2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942

Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.

3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300

Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.

Na Veronica Mrema, Pretoria

Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika Kusini, Profesa Blade Nzimande, amesema Bara la Afrika linahitaji kwa kiwango kikubwa waandishi wa habari waliobobea katika masuala ya sayansi ili kusaidia kukuza ubunifu, tafiti na maendeleo kwa ujumla.

Akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa 13 wa Waandishi wa Habari za Sayansi Duniani (WCSJ2025) unaofanyika Pretoria kuanzia Desemba 1–5, Prof. Nzimande alisema uandishi wa sayansi ni daraja muhimu kati ya wanasayansi na jamii, na umuhimu wake ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

“Sayansi haimaanishi chochote kama haiwezi kufahamika kwa jamii,” alisema. “Waandishi wa habari ni daraja muhimu la kuileta sayansi kwa watu, lakini ni daraja lenye haki ya kuikosoa pale inapostahili. Afrika bado tunahitaji waandishi wengi mahiri wa uandishi wa sayansi.”

Amesema bara hilo lina mikakati mikubwa kama Mkakati wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika (STISA 2034), lakini utekelezaji wake unategemea pia uwepo wa mawasiliano imara na weledi wa waandishi wa habari.
Kupambana na dhana potofu na taarifa za uongo

Waziri huyo ameeleza kuwa waandishi wa habari wana jukumu la kupambana na dhana potofu, ubaguzi na taarifa za uongo (fake news), hasa katika enzi ambayo mitandao ya kijamii inatawala mawasiliano.

“Mitandao ya kijamii imeleta faida, lakini pia imekuwa chanzo kikubwa cha kusambaa kwa taarifa zisizo sahihi. Wakati wa COVID tumeshuhudia madhara yake. Madai kama chanjo kusababisha autism ni mifano ya hatari tunazopaswa kupambana nazo,” alisema, akiwataka waandishi kuwa jasiri kuuliza maswali makubwa na muhimu.
Umuhimu wa AI katika uandishi wa habari za sayansi

Prof. Nzimande alisema teknolojia ya akili bandia (AI) ni lazima ipewe nafasi katika sekta ya habari ili kuboresha weledi na uwazi wa taarifa, huku akiitaka Afrika kuongeza ushiriki katika masuala ya kisayansi duniani.

“Hatuwezi kuachwa nyuma. Tunahitaji kuingiza AI katika uandishi wa sayansi na kutatua pengo la namna Afrika inavyoripotiwa katika sayansi,” alisema.
 
Diplomasia ya sayansi na nafasi ya waandishi

Ameeleza kuwa sayansi haina mipaka, hivyo ina nafasi kubwa katika kuimarisha diplomasia kati ya mataifa. Ameongeza kuwa waandishi wa habari za sayansi ni sehemu muhimu katika kufanikisha malengo ya kitaifa na kikanda ya kukuza ushirikiano wa kisayansi.

“Bila ninyi, hatuwezi kuwafikia wale tunaopaswa kuwafikia. Nyinyi ni washirika muhimu katika kuifanya sayansi ifikike kwa watu wote,” alisema.

Mkutano wa WCSJ2025 unaendelea kujadili changamoto na mustakabali wa uandishi wa sayansi barani Afrika na duniani, huku ukilenga kuongeza uelewa, uthabiti na mchango wa sayansi katika maendeleo ya kijamii.

Dar es Salaam, 30 Novemba 2025: Dhamira ya PUMA Energy Tanzania ya kutoa ubora, ubunifu na huduma yenye kujikita kwa mteja, imethibitishwa kwa matokeo chanya. Usiku wa jana kwenye hafla ya mwaka ya Consumer Choice Awards, baada ya kutunukiwa tuzo mbili kubwa zaidi za usiku huo ambazo ni “Kampuni Inayopendwa Zaidi ya Mafuta na Nishati Barani Afrika” na “Kituo cha Mafuta kinachotoa Huduma kwa Wepesi na Kupatikana kwa urahisi.”

Ushindi huu wa tuzo mbili unaonesha kwamba PUMA Energy si tu kinara katika huduma za rejareja za nishati hapa Tanzania, bali pia katika bara zima la Afrika. Tuzo hizi, zilizopigiwa kura na watumiaji pamoja na wataalamu wa sekta, ni uthibitisho wa mkakati wa kampuni katika kutoa bidhaa bora za mafuta na nishati, mtandao mpana wa vituo vya kisasa, na kiwango cha juu cha utoaji wa huduma.
Tuzo ya “Kampuni Inayopendwa Zaidi ya Mafuta na Nishati Barani Afrika” ni uthibitisho wa taswira chanya ya PUMA Energy barani kote Afrika na picha ya uaminifu, weledi wa kiutendaji, na suluhu bunifu za nishati. Tuzo hii inaonyesha imani ambayo mamilioni ya watumiaji, wafanya biashara, na washirika wanaendelea kuwa nayo kwa PUMA Energy katika shughuli zao za kila siku.

Wakati huo huo, tuzo ya “Kituo cha Mafuta kinachotoa Huduma kwa Wepesi na Kupatikana kwa urahisi.” inaonesha ubora wa utekelezaji wa kampuni hapa nchini. PUMA Energy imewekeza kwa uthabiti kwenye maeneo ya kimkakati, miundombinu ya kisasa, na huduma zinazokidhi mahitaji ya madereva wa kisasa wa Kitanzania kuanzia vituo vyenye mwanga wa kutosha, usalama, usafi wa mazingira, malipo ya kidigitali, hadi mtandao mpana unaohakikisha kituo cha PUMA hakiko mbali na mteja.
Mkurugenzi Mtendaji wa PUMA Energy Tanzania, Fatma Abdallah, alisema:Tunapenda kurudisha shukrani zetu kwa wateja na watumiaji wetu, kwa kutupa sisi nafasi ya kupokea tuzo hizi kubwa. Tuzo hii ya Kampuni inayopendwa zaidi ni mafanikio makubwa yaliyochangiwa na kila mshiriki wa timu ya Puma Enenrgy Tanzania, wauzaji wetu, na wateja wetu wapedwa. Na Tuzo ya Kituo Kinachopatikana kwa Urahisi ni uthibitisho wa kujitoa kwetu na kuhakikisha kila mteja anayeingia kwenye vituo vyetu anapa huduma bila usumbufu, bidhaa za uhakika na kuondoka akifurahi. Tuzo hizi si mwisho wetu, bali zimekuwa chachu ya kutusukuma kuendelea kutoa huduma za viwango vya juu zaidi”

Mwisho, Mkuu wa Sheria na Masuala ya Ushirika wa PUMA Energy Tanzania, Emmanuel G. Bakilana, alisema, “Tunajitahidi kila mara kuhakikisha mteja yupo katikati ya kila tunachofanya.”
Na Veronica Mrema, Pretoria

Wakati dunia ikikimbiza mageuzi ya teknolojia—kutoka akili bandia (AI) hadi tiba bunifu—ukanda wa SADC bado unakabiliwa na changamoto kubwa: taarifa za sayansi na ubunifu hazimfikii mwananchi kwa kasi inayohitajika.

Mkurugenzi Mkuu wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Sayansi ya Afrika Kusini (DSTI), Mwampei Chaba, amesema nchi nyingi za SADC hazina mkakati mahsusi wa mawasiliano ya sayansi, hali inayowafanya waandishi kukosa taarifa, ushirikiano kutoka serikalini na hata fursa za ufadhili.
Akizungumza kwenye mdahalo wa waandishi wa sayansi kutoka nchi 18 za SADC, ulioungana na Mkutano wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025), Chaba alisisitiza kuwa bila mawasiliano mazuri, sayansi haiwezi kuonekana wala kuthaminiwa na jamii.

“Sayansi inapaswa kuelezeka kwa mtoto wa miaka 5 na mtu wa miaka 85,” alisema, akitoa wito kwa waandishi kuwasukuma wanasayansi kutumia lugha nyepesi na inayoeleweka.
Amesema Afrika inahitaji waandishi mahiri wa sayansi kuliko wakati mwingine wowote, na anaamini vipaji hivyo vinaweza kutoka ndani ya SADC endapo kutakuwa na ushirikiano wa kimkakati.

Chaba pia amehimiza matumizi ya mitandao ya kijamii—TikTok, YouTube na Instagram—kufikisha maudhui ya kisayansi kwa vijana wengi waliopo kwenye majukwaa hayo.

Kwa mara ya kwanza Afrika inaandaa WCSJ, na warsha hiyo inalenga kuimarisha uwezo wa waandishi kuibua, kueleza na kuhamasisha masuala ya sayansi ndani ya jamii.

Na Mwandishi Wetu, Pretoria – Afrika Kusini

Tasnia ya habari nchini imepata heshima mpya baada ya Veronica Mrema, Mwanzilishi wa M24 Tanzania Media na mwanachama wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuteuliwa kuwa miongoni mwa wachangiaji wa jopo la mdahalo katika Mkutano wa 13 wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025) unaofanyika jijini Pretoria, Afrika Kusini.

Uteuzi huo unaonekana kuwa ishara ya kutambuliwa kwa kasi inayoongezeka ya uandishi wa habari za kidijitali na kisayansi nchini Tanzania, na umepokelewa kama fahari kwa TBN na tasnia nzima ya habari.

Mrema, ambaye pia ni Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DAR-PC) na Afisa Habari wa Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Selimundu Tanzania (SCDPCT), amewasili nchini Afrika Kusini kwa udhamini maalum wa safari (Travel Grant) uliotolewa na Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ya Afrika Kusini (DSTI). Udhamini huo umetokana na utambuzi wa mchango wake katika uandishi wa habari za sayansi na afya, huku akitajwa kuwa miongoni mwa wachache kutoka barani Afrika waliopata nafasi hiyo ya kipekee.

Kupitia nafasi yake katika jopo hilo, Mrema anatarajiwa kuwasilisha hoja kuhusu umuhimu wa uandishi wa habari za kisayansi barani Afrika, ikiwemo haja ya kuimarisha ubunifu, weledi na uwasilishaji wa taarifa zenye ushahidi ili kusaidia jamii kufanya maamuzi sahihi yenye tija kwa maendeleo.

WCSJ2025 ni mkutano mkubwa unaowakutanisha waandishi wa habari za sayansi, watafiti na wataalamu kutoka nchi mbalimbali duniani, ambapo washiriki wanajadili mustakabali wa tasnia hiyo, changamoto, fursa na mbinu za kuboresha mawasiliano ya kisayansi.

Kwa mujibu wa TBN, hatua ya Mrema kukaa jukwaa moja na wataalam wakubwa wa kimataifa ni uthibitisho kuwa Tanzania inaendelea kupiga hatua katika anga za habari za kisasa, na kwamba mchango wa wanahabari wa kidijitali nchini unatambulika na kuthaminiwa katika majukwaa ya kimataifa.

Mkutano huo unatarajiwa kuendelea hadi Desemba 5, 2025.
Kampuni ya Bima ya SanlamAllianz imewashukuru mawakala wao kwa kufanya kazi nao

Akizungumza wakati wa halfa ambayo imefanyika Novemba, 28,2925 jijini Dar-es-Salaam, Meneja mkuu wa biashara na mawakala, Geofray Masige amesema kuwa kampuni hiyo ya SanlamAllianz wanawashukuru mawakala wake kwa mchango mkubwa walioufanya katika kukuza biashara ya bima.

Pia naenda kuchukua nafasi hii kuwatambulisha mawakala watu juu ya muunganiko wetu mpya wa Sanlam na Allianz.
"Mnamo Septemba 2023, kampuni ya Sanlam bingwa wa huduma za bima barani Afrika na Allianz ambao ni miongoni mwa makampuni makubwa zaidi ya bima duniani ziliungana kutengeneza kampuni kubwa ya kifedha isiyo ya kibenki barani Afrika, inayojulikana kama SanlamAllianz.

Hadi sasa, SanlamAllianz ipo katika nchi 26 barani Afrika.

"Muungano huu umeunganisha uzoefu wa pamoja wa zaidi ya miaka 200 barani Afrika na duniani.
Malengo yetu ni kutoa huduma bora zaidi, kuunda bidhaa zinazokidhi matarajio ya wateja, na kujenga jamii inayopata ulinzi wa maisha, fedha, mali, na mafanikio endelevu.

Na hapa ndipo inapotoka kauli mbiu yetu: “Ishi kwa Kujiamini” – Live with Confidence.

Kwa wale old school, sio ile ya kina Msondo na Sikinde hapa tunazungumzia zama za James Bond na Titanic.

"Kufuatia uzinduzi rasmi wa chapa yetu mpya mwishoni mwa mwezi wa kumi, Sanlam General Insurance imeungana na Jubilee General Insurance kuunda SanlamAllianz General Insurance Tanzania.

Vilevile, Sanlam Life Insurance imebadili jina na kuwa SanlamAllianz Life Tanzania.
"Kazi kubwa iliyofanywa na wafanyakazi wenzangu hapa nchini pamoja na wenzetu wa SanlamAllianz Group imetuwezesha kushiriki kikamilifu mabadiliko haya muhimu.

Kwa mujibu wa takwimu za soko la bima nchini.

SanlamAllianz Life inaendelea kuwa kinara katika bima za maisha.

SanlamAllianz General inaelekea kuwa kampuni inayoongoza katika bima za mali kufikia mwisho wa mwaka 2025.

Kwa upande wa General Insurance, tumenufaika sana kupitia muunganiko wa Jubilee Allianz na Sanlam General.

Wafanyakazi wote wanaendelea na majukumu yao kama kawaida, uwezo wetu wa kuandikisha bima (underwriting capacity) umeongezeka, na sasa tunapata utaalamu wa kimataifa kutoka SanlamAllianz Group.

"Hii ni fursa muhimu kwa ukuaji wa soko la bima nchini na pia kwenu ninyi mawakala wetu kwa kuwa ninyi ni sehemu muhimu ya mafanikio haya.

Kwa sasa, SanlamAllianz General Insurance ina takribani mawakala 300 nchi nzima, na lengo letu ni kufikia mawakala 350 ifikapo mwaka 2026.

Mimi na ninyi ni sehemu ya familia hii kubwa ya mawakala wa SanlamAllianz. Mfululizo wa matukio kama haya utafanyika katika matawi yetu yote makubwa ili kila wakala apate nafasi ya kushiriki, amesema,"Masige.

Pia amesema Wana mtandao wa matawi 11, ikiwemo jijini la Mwanza, Arusha, Dodoma, Morogoro, Mbeya, Zanzibar, Moshi, Tanga, Mbagala, Quality Center na Tegeta.