Articles by "AFYA"
Showing posts with label AFYA. Show all posts
Na Veronica Mrema, Pretoria

Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika Kusini, Profesa Blade Nzimande, amesema Bara la Afrika linahitaji kwa kiwango kikubwa waandishi wa habari waliobobea katika masuala ya sayansi ili kusaidia kukuza ubunifu, tafiti na maendeleo kwa ujumla.

Akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa 13 wa Waandishi wa Habari za Sayansi Duniani (WCSJ2025) unaofanyika Pretoria kuanzia Desemba 1–5, Prof. Nzimande alisema uandishi wa sayansi ni daraja muhimu kati ya wanasayansi na jamii, na umuhimu wake ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

“Sayansi haimaanishi chochote kama haiwezi kufahamika kwa jamii,” alisema. “Waandishi wa habari ni daraja muhimu la kuileta sayansi kwa watu, lakini ni daraja lenye haki ya kuikosoa pale inapostahili. Afrika bado tunahitaji waandishi wengi mahiri wa uandishi wa sayansi.”

Amesema bara hilo lina mikakati mikubwa kama Mkakati wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika (STISA 2034), lakini utekelezaji wake unategemea pia uwepo wa mawasiliano imara na weledi wa waandishi wa habari.
Kupambana na dhana potofu na taarifa za uongo

Waziri huyo ameeleza kuwa waandishi wa habari wana jukumu la kupambana na dhana potofu, ubaguzi na taarifa za uongo (fake news), hasa katika enzi ambayo mitandao ya kijamii inatawala mawasiliano.

“Mitandao ya kijamii imeleta faida, lakini pia imekuwa chanzo kikubwa cha kusambaa kwa taarifa zisizo sahihi. Wakati wa COVID tumeshuhudia madhara yake. Madai kama chanjo kusababisha autism ni mifano ya hatari tunazopaswa kupambana nazo,” alisema, akiwataka waandishi kuwa jasiri kuuliza maswali makubwa na muhimu.
Umuhimu wa AI katika uandishi wa habari za sayansi

Prof. Nzimande alisema teknolojia ya akili bandia (AI) ni lazima ipewe nafasi katika sekta ya habari ili kuboresha weledi na uwazi wa taarifa, huku akiitaka Afrika kuongeza ushiriki katika masuala ya kisayansi duniani.

“Hatuwezi kuachwa nyuma. Tunahitaji kuingiza AI katika uandishi wa sayansi na kutatua pengo la namna Afrika inavyoripotiwa katika sayansi,” alisema.
 
Diplomasia ya sayansi na nafasi ya waandishi

Ameeleza kuwa sayansi haina mipaka, hivyo ina nafasi kubwa katika kuimarisha diplomasia kati ya mataifa. Ameongeza kuwa waandishi wa habari za sayansi ni sehemu muhimu katika kufanikisha malengo ya kitaifa na kikanda ya kukuza ushirikiano wa kisayansi.

“Bila ninyi, hatuwezi kuwafikia wale tunaopaswa kuwafikia. Nyinyi ni washirika muhimu katika kuifanya sayansi ifikike kwa watu wote,” alisema.

Mkutano wa WCSJ2025 unaendelea kujadili changamoto na mustakabali wa uandishi wa sayansi barani Afrika na duniani, huku ukilenga kuongeza uelewa, uthabiti na mchango wa sayansi katika maendeleo ya kijamii.
Na Veronica Mrema, Pretoria

Wakati dunia ikikimbiza mageuzi ya teknolojia—kutoka akili bandia (AI) hadi tiba bunifu—ukanda wa SADC bado unakabiliwa na changamoto kubwa: taarifa za sayansi na ubunifu hazimfikii mwananchi kwa kasi inayohitajika.

Mkurugenzi Mkuu wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Sayansi ya Afrika Kusini (DSTI), Mwampei Chaba, amesema nchi nyingi za SADC hazina mkakati mahsusi wa mawasiliano ya sayansi, hali inayowafanya waandishi kukosa taarifa, ushirikiano kutoka serikalini na hata fursa za ufadhili.
Akizungumza kwenye mdahalo wa waandishi wa sayansi kutoka nchi 18 za SADC, ulioungana na Mkutano wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025), Chaba alisisitiza kuwa bila mawasiliano mazuri, sayansi haiwezi kuonekana wala kuthaminiwa na jamii.

“Sayansi inapaswa kuelezeka kwa mtoto wa miaka 5 na mtu wa miaka 85,” alisema, akitoa wito kwa waandishi kuwasukuma wanasayansi kutumia lugha nyepesi na inayoeleweka.
Amesema Afrika inahitaji waandishi mahiri wa sayansi kuliko wakati mwingine wowote, na anaamini vipaji hivyo vinaweza kutoka ndani ya SADC endapo kutakuwa na ushirikiano wa kimkakati.

Chaba pia amehimiza matumizi ya mitandao ya kijamii—TikTok, YouTube na Instagram—kufikisha maudhui ya kisayansi kwa vijana wengi waliopo kwenye majukwaa hayo.

Kwa mara ya kwanza Afrika inaandaa WCSJ, na warsha hiyo inalenga kuimarisha uwezo wa waandishi kuibua, kueleza na kuhamasisha masuala ya sayansi ndani ya jamii.

Na Mwandishi Wetu, Pretoria – Afrika Kusini

Tasnia ya habari nchini imepata heshima mpya baada ya Veronica Mrema, Mwanzilishi wa M24 Tanzania Media na mwanachama wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuteuliwa kuwa miongoni mwa wachangiaji wa jopo la mdahalo katika Mkutano wa 13 wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025) unaofanyika jijini Pretoria, Afrika Kusini.

Uteuzi huo unaonekana kuwa ishara ya kutambuliwa kwa kasi inayoongezeka ya uandishi wa habari za kidijitali na kisayansi nchini Tanzania, na umepokelewa kama fahari kwa TBN na tasnia nzima ya habari.

Mrema, ambaye pia ni Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DAR-PC) na Afisa Habari wa Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Selimundu Tanzania (SCDPCT), amewasili nchini Afrika Kusini kwa udhamini maalum wa safari (Travel Grant) uliotolewa na Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ya Afrika Kusini (DSTI). Udhamini huo umetokana na utambuzi wa mchango wake katika uandishi wa habari za sayansi na afya, huku akitajwa kuwa miongoni mwa wachache kutoka barani Afrika waliopata nafasi hiyo ya kipekee.

Kupitia nafasi yake katika jopo hilo, Mrema anatarajiwa kuwasilisha hoja kuhusu umuhimu wa uandishi wa habari za kisayansi barani Afrika, ikiwemo haja ya kuimarisha ubunifu, weledi na uwasilishaji wa taarifa zenye ushahidi ili kusaidia jamii kufanya maamuzi sahihi yenye tija kwa maendeleo.

WCSJ2025 ni mkutano mkubwa unaowakutanisha waandishi wa habari za sayansi, watafiti na wataalamu kutoka nchi mbalimbali duniani, ambapo washiriki wanajadili mustakabali wa tasnia hiyo, changamoto, fursa na mbinu za kuboresha mawasiliano ya kisayansi.

Kwa mujibu wa TBN, hatua ya Mrema kukaa jukwaa moja na wataalam wakubwa wa kimataifa ni uthibitisho kuwa Tanzania inaendelea kupiga hatua katika anga za habari za kisasa, na kwamba mchango wa wanahabari wa kidijitali nchini unatambulika na kuthaminiwa katika majukwaa ya kimataifa.

Mkutano huo unatarajiwa kuendelea hadi Desemba 5, 2025.
Arusha, Tanzania – October 1, 2025 — More than 100 leading scientists and policymakers from over 30 countries will gather in Arusha next week (October 8–10) for the first-ever International Symposium on Artemisia, underscoring Tanzania’s growing role in global health and environmental innovation.

The event, hosted at the Aga Khan University’s Arusha Climate and Environmental Research Centre (AKU-ACER), will spotlight the plant Artemisia, long valued as a natural treatment for malaria and now being studied for wider applications, including tuberculosis, schistosomiasis, animal health, and sustainable farming.

“This symposium is more than a scientific exchange; it is a call to action,” said Dr. François Laurens, President of the International Society for Horticultural Science (ISHS), one of the co-hosts alongside the Aga Khan Foundation and Maison de l’Artemisia.

African and global experts, including Prof. Francine Ntoumi (Congo-Brazzaville), Prof. Joseph Ndunguru (Tanzania), and Prof. Pamela Weathers (USA), will present the latest findings.

Tanzania’s Ministry of Health welcomed the gathering, with Permanent Secretary Dr. Seif Shekalaghe noting: “This event not only elevates Tanzania as a hub for scientific innovation but also reflects our commitment to sustainable solutions that safeguard health, environment, and development.”

Participants are expected to call for large-scale clinical trials to confirm Artemisia’s safety and effectiveness, a key step toward integrating the plant into mainstream medicine and agriculture.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania Plc, Philip Besiimire, akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Heart Team Africa Foundation (HTAF), Dkt. Naizihijwa Majani, mara baada ya kusaini makubaliano ya ushirikiano wa kuchangia asilimia 30 ya gharama za matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo, huku serikali ikigharamia asilimia 70. Hafla hiyo, iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Septemba 2025 sambamba na Maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani chini ya kaulimbiu “Don’t Miss a Beat”, ilishuhudiwa na Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Zuweina Farah, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge.
Mange Mwandishi Wetu. 

Dar es Salaam, 29 Septemba 2025: Vodacom Tanzania Foundation imeingia makubaliano ya ushirikiano na Heart Team Africa Foundation, asasi inayofanya kazi chini ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), katika hatua ya kuongeza nguvu kwenye mapambano dhidi ya magonjwa ya moyo kwa watoto nchini. Hafla ya utiaji saini imefanyika sambamba na maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani 2025, chini ya kaulimbiu “Don’t Miss a Beat.”

Kwa mujibu wa utafiti wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, watoto 2 kati ya 100 huzaliwa na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (Congenital Heart Disease – CHD), huku asilimia 3 ya watoto wenye umri kati ya miaka 5–15 wakiathiriwa na ugonjwa wa moyo wa Rheumatic (RHD) unaoweza kuzuilika kwa matibabu mapema ya maambukizi ya koo.

Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya watoto 4,000 huhitaji upasuaji wa moyo kila mwaka, lakini huduma hizo bado hazipatikani kwa urahisi. Ingawa serikali inagharamia asilimia 70 ya matibabu, asilimia 30 iliyosalia ni mzigo mkubwa kwa familia nyingi, huku watoto zaidi ya 350 wakiwa kwenye foleni ya kusubiri upasuaji katika JKCI.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Dkt. Peter Kisenge, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, alisema:

"Kila takwimu inawakilisha mtoto mwenye ndoto na mzazi mwenye matumaini. Ushirikiano huu utapunguza pengo kati ya uhitaji na upatikanaji wa huduma, ili watoto wengi zaidi wapate nafasi ya kuishi maisha yenye afya njema."

Naye Dkt. Naizihijwa Majani, Mkurugenzi Mtendaji wa Heart Team Africa Foundation, alibainisha kuwa gharama za matibabu zimekuwa kikwazo kikubwa:

"Ushirikiano huu sio tu msaada wa kifedha, bali ni njia ya kuokoa maisha. Tunataka kila mzazi awe na hakika kwamba mtoto wake atapata huduma bila kuchagua kati ya umasikini na mustakabali wa mtoto wake."
Mapema mwaka huu, Vodacom Foundation ilizindua Amini Initiative huko Zanzibar, ikiahidi kugharamia asilimia 30 ya gharama zinazobaki za watoto 150 wanaohitaji upasuaji. Mpaka sasa watoto 38, wenye umri wa kati ya miezi miwili na miaka 14, wamefanyiwa upasuaji kwa mafanikio.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alisema ushirikiano huo ni sehemu ya kutafsiri imani kuwa vitendo:

"Makubaliano haya ni ishara thabiti ya kuchukua hatua. Kwa kushirikiana na JKCI na Heart Team Africa Foundation, tunafungua kesho ambayo hakuna mtoto atakayepoteza maisha kwa kukosa huduma za kitabibu zinazoweza kuokoa maisha."

Vodacom Foundation, JKCI na Heart Team Africa Foundation wamewataka serikali, kampuni binafsi na watu wote kuungana nao katika juhudi hizi.

"Huu ni wito wa kitaifa," alisema Besiimire. "Ni jukumu letu kuhakikisha mtoto wa Kitanzania hapotezi maisha kwa sababu ya kuchelewa kupata upasuaji wa moyo unaookoa maisha."
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Tanzania sasa imejiweka kwenye ramani ya tiba utalii barani Afrika baada ya Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila (MNH-Mloganzila) kuzindua Kliniki Maalumu (Premier Clinic) yenye viwango vya kimataifa, faragha na teknolojia za kisasa zinazolingana na mataifa yaliyoendelea.

Akizindua kliniki hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, alisema hatua hiyo ni uthibitisho wa uwekezaji mkubwa wa Serikali ya Awamu ya Sita katika sekta ya afya, ambao umechochea ubunifu na kuifanya Tanzania kuwa kituo kipya cha matibabu ya kimataifa.

“Huduma hizi tulizozizoea kuzitafuta nje ya nchi sasa zinapatikana hapa nyumbani. Serikali imejenga misingi imara kwa kuimarisha miundombinu, kuongeza bajeti ya dawa, kusomesha wataalam na kununua vifaa tiba vya kisasa,” alisema Chalamila.

Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Dkt. Delilah Kimambo, alisema Premier Clinic inalenga kuvutia wagonjwa kutoka Tanzania, Afrika Mashariki, Kati na hata nje ya bara, huku ikijikita katika misingi mitatu: ubora wa huduma, ufanisi na ubunifu.
Tunataka Watanzania na wageni waone Muhimbili siyo tu hospitali ya taifa, bali ni kitovu cha tiba cha kikanda na kimataifa,” alisema Dkt. Kim
ambo.

Naye Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MNH, Dkt. Khadija Malima, alisisitiza kuwa bodi itaendelea kuhakikisha huduma bora zinadumu na kuimarisha imani ya wananchi na wageni kutoka nje.

Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Mratibu wa Tiba Utalii, Dkt. Asha Mahita, alisema kuzinduliwa kwa kliniki hiyo kutasaidia Tanzania kushindana kimataifa katika sekta ya tiba utalii, kwani wagonjwa kutoka mataifa jirani na ya mbali wamekuwa wakija nchini kwa ajili ya uchunguzi na matibabu.

Uzinduzi huu unaweka Tanzania katika nafasi mpya, ambapo huduma bora za afya na faragha zinapatikana kwa viwango vya kimataifa bila kulazimika kusafiri kwenda nje ya nchi.