Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye alivunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bi. Mary Barney Isaac Laseko Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye amevunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba. Pemebni ni wazazi wake Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza hafla ya Mahafali ya 55 (Duru la Tatu) ya Chuo Kikuu hicho, na kumpongeza mhitimu aliyeng’ara kwa kuvunja rekodi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 32 katika historia ya The Law School of Tanzania.
Mhitimu huyo, Bi. Mary Barney Laseko, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria (LLB), ameweka historia kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania—rekodi ambayo mara ya mwisho ilipatikana zaidi ya miongo mitatu iliyopita chini ya Profesa Hamudi Majamba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha, Mary anajiunga katika orodha ya wanawake wachache waliowahi kufanya hivyo, akifuata nyayo za Dkt. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa CCM, ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kupata daraja hilo kutoka Law School of Tanzania.
Hafla hiyo imefanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, ambapo Dkt. Kikwete amewatunuku Shahada na Stashahada wahitimu 2,452. Kati yao, 1,386 (sawa na asilimia 56.6) ni wanawake, ikionyesha mwamko na ushiriki mkubwa wa wanawake katika elimu ya juu.
Katika picha zilizopigwa na mpiga picha mkongwe Issa Michuzi, Dkt. Kikwete anaonekana akimpongeza Bi. Mary kwa mafanikio yake, huku picha nyingine zikimuonyesha akiwa na wazazi wake, Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko, waliokuwa wakijivunia mafanikio ya binti yao.
Kwa mujibu wa uongozi wa chuo, mafanikio ya Mary yamepokelewa kama ishara ya ongezeko la ubora, nidhamu na juhudi za wanafunzi wanaosomea sheria nchini.





Toa Maoni Yako:
0 comments: