Articles by "HABARI ZA KIJAMII"
Showing posts with label HABARI ZA KIJAMII. Show all posts
Hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto mkoani Manyara imeondokana na changamoto ya kukatiza baadhi ya huduma za matibabu kama upasuaji na pindi umeme unapokatika baada ya Bohari kuu ya dawa MSD kukabidhi jenereta lenye thamani ya shilingi milioni 65 itakayotumika kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga ameagiza uongozi wa hospitali ya Halmashauri hiyo kutenga bajeti ya mafuta ya jenereta hilo ili litumike wakati wowote pindi umeme unapokatika. 
"Niwaombe viongozi mjipange ili hili jenereta mlilopewa liwe linafanyakazi kwa ufasaha, tengeni bajeti ya mafuta ili pindi umeme unapokatika linawaka na mambo yanakwenda vyema," amesema RC Sendiga.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano mjini Kibaya wilayani Kiteto, meneja wa MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amesema jenereta hilo lenye uwezo wa KVA 75 ni sehemu ya mahitaji ya vifaa vya afya vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 699 vilivyoagizwa na hospitali hiyo kwa bohari kuu ya dawa MSD katika mwaka wa fedha 2023/2024. 


 Amesema tayari MSD imeshakabidhi vifaa vingine vilivyoagizwa katika hospitali hiyo vyenye thamani ya shilingi milioni 683 sawa na asilimia 98 ya vifaa vilivyoagizwa na halmashauri hiyo kupitia MSD na ameahidi wakati wowote kuanzia sasa kukamilisha sehemu iliyobaki ambayo ni mfumo wa kuhifadhi miili (mortuary cabinet). 
Jenereta lenye thamani ya shilingi milioni 65.

Mganga mkuu wa wilaya ya Kiteto Dkt Vicent Gyunda ameshukuru bohari kuu ya dawa kanda ya Dodoma kukabidhi jenereta hilo kwa wakati ambayo sasa itawezesha uhakika wa huduma za upasuaji wa wagonjwa, kuwapa joto watoto njiti pamoja na huduma ya kuhifadhi maiti. 

Wilaya ya Kiteto ni miongoni mwa maeneo ambayo huduma ya umeme hukatika kila mara kutokana na uchakavu wa miundombinu hali ambayo imekiwa ikitatiza utoaji wa huduma za kitabibu zinazohitaji uwepo wa umeme katika hospitali ya Halmashauri ya wilaya hiyo mjini Kibaya.
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar, Mh. Mudrick Soraga (kulia), akimsikiliza Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania, Shani Kinswaga, wakati wa kongamano la Z-Summit 2025 lililofanyika katika Chuo Kikuu cha SUZA, Zanzibar. Kongamano hilo la kila mwaka, lililofanyika kuanzia Februari 19-20, liliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ili kujadili changamoto na suluhisho za kuendeleza Zanzibar kama moja ya maeneo bora ya utalii duniani.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.

Zanzibar, Tanzania – Benki ya Exim Tanzania imeimarisha dhamira yake ya kukuza na kuendeleza sekta ya utalii Zanzibar kwa kushirikiana na wadau muhimu wa sekta hiyo, wakiwemo Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), ili kuwezesha waendeshaji wa shughuli za utalii kufanya malipo kama ada za kuingia kwenye hifadhi kwa haraka, kwa usalama na kwa urahisi.

Mkutano wa Z-Summit 2025, uliofanyika katika Chuo Kikuu cha SUZA, Tunguu, uliwakutanisha wadau wa serikali, wafanyabiashara, na wadau wa sekta ya utalii na ukarimu ili kujadili suluhisho bunifu za kuboresha nafasi ya Zanzibar kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani.  
Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim, Shani Kinswaga, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, alisisitiza safari ya benki hiyo na Z-Summit tangu kuanzishwa kwake, akieleza kuwa huu ni mwaka wa tatu mfululizo wa udhamini wao katika mkutano huo.  

“Mkutano huu ni jukwaa muhimu la kushirikiana, kubadilishana maarifa na kujadili mikakati ya kuimarisha zaidi nafasi ya Zanzibar kama moja ya vivutio bora vya utalii duniani. Uungwaji mkono wa Benki ya Exim unaonesha imani yetu thabiti katika sekta ya utalii kama kiini cha ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii,” alisema Kinswaga.  

Kinswaga alielezea juhudi za benki hiyo katika kutumia teknolojia kutoa suluhisho rahisi za kifedha zinazokidhi mahitaji ya biashara za utalii. Kwa kuongezeka kwa mahitaji ya miamala ya kidigitali, Benki ya Exim imeanzisha huduma bunifu za kibenki, zikiwemo kutumia simu, kadi, na mifumo ya malipo mtandaoni, ili kuhakikisha ufanisi, usalama, na urahisi kwa wafanyabiashara na watalii.  
Akizungumzia ushirikiano wao na TANAPA, Andrew Lyimo, Mkuu wa Kitengo cha Benki ya Rejareja wa Benki ya Exim, alisema, “Katika Benki ya Exim, tunatambua kuwa ufanisi, usalama, na urahisi ni muhimu katika sekta ya utalii. Ndiyo maana tumeshirikiana na wadau kama TANAPA na NCAA kuwezesha malipo yasiyo ya fedha taslimu kwa huduma mbalimbali, ikiwemo ada za kuingia kwenye hifadhi. Akaunti ya Waendeshaji wa shughuli za Utalii inajumuisha Kadi ya Exim TANAPA, iliyoundwa mahsusi kurahisisha miamala katika maeneo yote ya hifadhi nchini Tanzania.”  

Katika kuthibitisha dhamira yake ya kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha, Benki ya Exim ilitangaza mpango wake wa kuendelea kupanua huduma zake Zanzibar. Ikiwa tayari na matawi mawili yanayofanya kazi, benki hiyo ina mpango wa kufungua matawi katika maeneo mengine ya kimkakati. Hii inaonesha azma ya Benki ya Exim ya kusogeza huduma za kibenki karibu na biashara, ikiwawezesha kupata suluhisho za kifedha zinazosaidia maendeleo ya miundombinu, ukuaji wa biashara, na ufanisi wa uendeshaji.  

Kadri mazingira ya utalii yanavyoendelea kubadilika, Benki ya Exim inasalia kuwa mshirika wa kuaminika wa kifedha kwa biashara zinazotaka kupanuka, kuboresha huduma zao, au kuwekeza katika fursa mpya. Suluhisho zake maalum za kifedha zimeundwa kusaidia kupata rasilimali zinazohitajika ili kustawi katika soko lenye ushindani.  

Kupitia ushirikiano imara, matumizi ya teknolojia za kidigitali, na upanuzi wa huduma zake, Benki ya Exim haitoi tu msaada kwa sekta ya utalii bali pia inachangia katika maendeleo ya uchumi wa Zanzibar kwa ujumla. Ushiriki wa Benki ya Exim katika mkutano wa Z-Summit 2025 ni uthibitisho wa dhamira yake isiyotetereka ya kusaidia ukuaji endelevu wa sekta ya utalii Zanzibar. 

Kwa kushirikiana na wawekezaji, wafanyabiashara, na mamlaka za serikali, benki hiyo inaunda mustakabali ambapo utalii utaendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya uchumi, kuongeza ajira, na kuifanya Zanzibar kuendelea kuwa kivutio kikubwa kwa watalii kutoka kote ulimwenguni.  
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza tarehe 18 hadi 19 Februari, 2025 Mkoani Morogoro . Zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura mkoani humo linataraji kuanza Machi mosi 2025 na kufikia tamati Machi 07,2025 huku vituo vikitaraji kufunguliwa Saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:jioni kwa siku zote saba.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza tarehe 18 hadi 19 Februari, 2025 Mkoani Morogoro . Zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura mkoani humo linataraji kuanza Machi mosi 2025 na kufikia tamati Machi 07,2025 huku vituo vikitaraji kufunguliwa Saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:jioni kwa siku zote saba.

Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia hotuba za kufunga.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Ndg. Kailima R. K wakati wa kufunga mafunzo hayo. Mwenyekiti wa Mafunzo ambaye pia ni Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, Ndg. Emmanuel Vuri akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.

Meza kuu ikimsikiliza Mwenyekiti wa mafunzo.

Mjumbe Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magdalena Rwebangira akiwa wakati wa kufunga mafunzo hayo. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Ndg. Kailima R. K akizungumza jambo na washiriki.


Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia hotuba za kufunga.
******************Na. Mwandishi Wetu
Watendaji wa uboreshaji wa Daftari; la Kudumu la Wapiga Kura wameaswa kutekeleza majukumu waliyopewa kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Balozi Omari Ramadhan Mapuri wakati akifunga mafunzo ya watendaji wa uboreshaji wa daftari mkoani Morogoro leo Machi 19, 2025.

“Mnapaswa kutekeleza majukumu mliyopewa kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume,” amewaasa watendaji hao ambao wamehudhuria mafunzo ya siku mbili.

Balozi Mapuri ametoa wito kwa watendaji hao kuendelea kutumia muda wao wa ziada kusoma na kupitia maelekezo yote waliyopewa ili kuongeza uelewa zaidi kuhusu wajibu na majukumu yao wakati wa kutekeleza zoezi lililopo mbele yao.

Akifunga mafunzo kama hayo mkoani Tanga, Mjumbe wa Tume ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari amewataka watendaji hao kusoma katiba na sheria ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“Someni kwa makini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria ya Uchaguzi, Kanuni za uboreshaji, Maelekezo na Miongozo yote inayotolewa na Tume ili kazi yenu ifanyike kwa unadhifu na haki,” amesema.

Jaji Asina amewakumbusha watendaji hao juu ya wajibu wao wa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao kwenye uchaguzi mkuu utakoafanyika mwaka huu.

Uboreshaji wa Daftari utafanyika mkoani Morogoro na kwenye Mkoa wa Tanga katika Halmashauri za Wilaya ya Bumbuli, Handeni, Pangani na Mkinga kwa siku saba kuanzia tarehe 01 hadi 07 Machi, 2025 ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa saa 02:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) wakati wa Kikao cha Baraza hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Nishati, Judith akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni (kushoto). Kulia ni Katibu wa Baraza Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Ebeneza Mollel,wakati wa Kikao cha Baraza hilo cha kujadili Mpango na Bajeti hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) wakati wa Kikao cha Baraza hilo linalofanyika tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro. Kushoto Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni.
---------
*Ataka Duru ya Tano ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia kuwa na matokeo chanya

*Aipongeza PURA kuwashirikisha Watumishi kujadili mipango ya Bajeti ya Taasisi

MOROGORO

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga ameielekeza Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) kuendelea kuvutia uwekezaji katika vitalu vilivyo wazi vya mafuta na gesi asilia ili kuongeza kiasi cha nishati hiyo nchini.

Mhe. Kapenga amesema hayo leo wilayani Morogoro, Mkoa wa Morogoro wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa PURA kinacholenga kujadili masuala mbalimbali ikiwemoMpango na Bajeti ya Taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26.

” Mkifanikiwa kuvutia uwekezaji katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi, nchi itaongeza ugunduzi wa rasilimali hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na kuogeza futi za ujazo wa gesi inayopatikana nchini, Pia mkiendelea kuvutia uwekezaji kupitia Duru ya Tano ya kunadi vitalu itakayozinduliwa mwezi machi mwaka huu, pamoja na faida zilizopo, mtakuwa mmeendeleza jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuendelea kuifungua Tanzania kiuchumi na kuvutia uwekezaji zaidi.”Amesema Kapinga.

Amesema Wizara ya Nishati inatambua umuhimu wa tukio la Duru ya Tano ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini pamoja na kutambua kazi kubwa ambayo imeshafanyika kuelekea uzinduzi wa tukio hilo ambalo amesema kuwa ni muhimu katika

kuvutia uwekezaji zaidi katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini.

“ Kwa muda mrefu sasa tumekuwa tukizungumzia ugunduzi wa futi za ujazo trilioni 57.54 pekee ni wakati sasa wa kufanya zaidi na zaidi ili tuweze kuongeza ugunduzi wa rasilimali hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa.” Amesisitiza Mhe.Kapinga

Katika kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi, ameupongeza uongozi wa PURA kwa kuendelea kuwashirikisha watumishi wake katika kujadili, kupanga na kupitisha mipango na Bajeti ya Taasisi kwenye Baraza la Wafanyakazi ikiwa ni utekelezaji pia wa Sheria ya Majadiliano ya Pamoja katika Utumishi wa Umma.

Amesema kufanyika kwa vikao hivyo ni ishara tosha ya utawala bora mahala pa kazi kwa kuwa watumishi wanapata fursa ya kuchangia mawazo yao kuhusu hali ya uendeshaji wa Taasisi hivyo kuendelea kuwa ni sehemu muhimu ya Taasisi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) Mhandisi. Charles Sangweni, amesema duru ya tano (5) ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na

gesi asilia nchini inatarajiwa kuzinduliwa mwezi Machi, 2025 Jijini Dares salaam wakati wa Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki (EAPCE’25).

Amesema PURA inaendelea kusimamia na kudhibiti shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa gesi asilia katika vitalu mbalimbali nchini na Kuhakikisha watanzania wazawa wanashirikishwa katika miradi mbalimbali ya mkondo wa juu wa petroli nchini.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoa wa Morogoro unaotaraji kuanza kufanyika Machi 01 hadi 07, 2025. Vituo vikifunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi 12:00 jioni kwa siku saba.Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoa wa Morogoro unaotaraji kuanza kufanyika Machi 01 hadi 07, 2025. Vituo vikifunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi 12:00 jioni kwa siku saba.





Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Kailima Ramadhani akiwasilisha mada wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoa wa Morogoro unaotaraji kuanza kufanyika Machi 01 hadi 07, 2025. Vituo vikifunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi 12:00 jioni kwa siku saba.

Mkurugenzi wa Daftari na TEHAMA wa Tume, Ndg. Stanslaus Mwita akiwasilisha mada wakati wa mkutano huo hayo.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani wakati wa mkutano wa wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoa wa Morogoro unaotaraji kuanza kufanyika Machi 01 hadi 07, 2025. Vituo vikifunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi 12:00 jioni kwa siku saba.
Onesho la vitendo la uandikishaji likifanywa na wataalam kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.


Washiriki mbalimbali wakiwa katika mkutano huo mkoani Morogoro.
 
********************** 
Na. Mwandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kuanza kwa mzunguko wa 12 wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambao utafanyika mkoani Morogoro na sehemu ya mkoa wa Tanga kwa siku saba kuanzia tarehe 01 had 07 Machi, 2025.

Akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoani Morogoro leo tarehe 17 Februari, 2025, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa, Jacobs Mwambegele amesema uboreshaji huo utafanyika kwenye mkoa huo na mkoani Tanga kwenye halmashauri za Wilaya ya Bumbuli, Handeni, Pangani na Mkinga.

“Kwa mujibu wa ratiba, kwa sasa Tume imeanza maandalizi ya mzunguko wa 12 kati ya mizunguko 13 ya uboreshaji wa Daftari. Mzunguko huu wa 12 unahusisha Mkoa huu wa Morogoro na Mkoa wa Tanga katika Halmashauri za Wilaya ya Bumbuli, Handeni, Pangani na Mkinga,” amesema Jaji Mwambegele.

Amesema mikoa 27 tayari imekamilisha zoezi hilo ambayo ni pamoja na Kigoma, Tabora, Katavi, Geita, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Manyara, Dodoma na Singida.

Ameitaja mikoa mingine kuwa ni Mjini Magharibi, Kusini Unguja, Kaskazini Unguja, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Rukwa, Songwe, Njombe, Ruvuma, Lindi na Mtwara.

“Mikoa miwili ya Pwani na sehemu ya mkoa wa Tanga kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza inatarajia kukamilisha zoezi hilo tarehe 19 Februari, 2025,” amesema.

Wakati huohuo, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ndugu. Kailima Ramadhani amesema Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 302,752 mkoani Morogoro sawa na ongezeko la asilimia 18.7 ya wapiga kura 1,612,952 waliokuwepo kwenye daftari la wapiga kura mwaka 2020.

“Tume inatarajia baada ya uandikishaji Mkoa wa Morogoro utakuwa na wapiga kura 1,915,704. Idadi hii inaweza kuongezeka kwa kuwa inawezekana wapo watanzania ambao walikuwa na sifa za kuandikishwa kuwa wapiga kura wakati wa uboreshaji wa Daftari mwaka 2019/20, lakini kwa sababu moja au nyingine hawakuweza kujiandikisha,” amesema.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Morogoro una vituo 2,816 vitakavyotumika kwenye uboreshaji wa daftari ikiwa ni ongezeko la vituo 112 katika vituo 2,704 vilivyotumika kwenye uboreshaji mwaka 2019/20.
Obinna Anyalebechi (Mkurugenzi Mtendaji wa SBL) akizungumza katika warsha ya siku moja iliyokutanisha wadau wa sekta binafsi na wadau wa maendeleo kutoka mashirika mbalimbali kuzungumzia mikakati ya kupambana na biashara haramu ya pombe nchini Tanzania. Kuanzia kulia ni Khadija Ngasongwa (Mkurugenzi wa bidhaa bandia kutoka FCC), Mwenyekiti wa zamani wa Shirikisho la wenye Viwanda (CTI) ambae pia ni Mwenyekiti wa bodi ya SBL, Paul Makanza na Lazaro Masasalaga (Mkurugenzi Udhibiti Ubora kutoka TBS). Warsha hii ilifanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa zamani wa Shirikisho la wenye Viwanda (CTI) na mwenyekiti wa bodi ya SBL, Paul Makanza akizungumza katika warsha ya siku moja iliyokutanisha wadau wa sekta binafsi na wadau wa maendeleo kutoka mashirika mbalimbali kuzungumzia mikakati ya kupambana na biashara haramu ya pombe nchini Tanzania. Kuanzia kulia ni Khadija Ngasongwa (Mkurugenzi wa bidhaa bandia kutoka FCC), Obinna Anyalebechi (Mkurugenzi Mtendaji wa SBL), na Lazaro Masasalaga (Mkurugenzi Udhibiti Ubora kutoka TBS). Warsha hii ilifanyika leo jijini Dar es Salaam.
Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) liliendesha warsha na wadau mbalimbali kujadili changamoto kubwa la unywaji wa pombe haramu na hatarishi. 

Warsha hiyo iliwaunganisha wadau muhimu wa sekta ya viwanda, watunga sera, na mamlaka za udhibiti kama Wizara ya Afya, Wizara ya Mambo ya Ndani, Tume ya Ushindani (FCC), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), na wadau wengine muhimu katika sekta ya pombe.

CTI ilisisitiza hatari kubwa za kiafya zinazotokana na pombe zisizodhibitiwa, ikiwa ni pamoja na viwango vya juu vya sumu, madhara ya muda mrefu kama ugonjwa wa ini, upofu, na hata vifo. Aidha, pombe haramu inachangia matatizo ya kijamii kama uhalifu, unyanyasaji wa majumbani, na kushuka kwa ufanisi kazini, hali inayoongeza mzigo kwa mifumo ya afya na ustawi wa jamii.
Mwenyekiti wa zamani wa CTI, Paul Makanza, alisema, “Mapambano dhidi ya pombe haramu si tu suala la udhibiti—ni juhudi za kulinda maisha ya Watanzania, kulinda mapato ya serikali, na kuendeleza mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki. Pombe haramu inahatarisha afya ya umma, inachochea matatizo ya kijamii, na inadhoofisha sekta rasmi ambayo inatoa maelfu ya ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi. Tunahitaji kuimarisha utekelezaji wa sheria na sera huku tukiendelea kuongeza uelewa ili kuhakikisha sekta ya pombe inayowajibika na endelevu ambayo inachangia maendeleo ya Tanzania kwa njia chanya.”

Akiunga mkono maoni ya Mwenyekiti wa zamani, Mkurugenzi Mtendaji wa SBL, Obinna Anyalebechi, aliongeza: “Sisi, kama wazalishaji wa pombe, tuko tayari kushirikiana katika jitihada hizi. Tunaamini kuwa mafanikio ya kweli katika sekta hii hayapimwi tu kwa utendaji wa kifedha, bali pia kwa uwezo wetu wa kuchangia maendeleo endelevu ya jamii yetu. Matumizi mabaya ya pombe ni hatari kwa kila mtu—sekta, afya ya umma, na jamii—na kushughulikia changamoto hii kunahitaji ushirikiano.”
Mbali na athari za kiafya, CTI ilielezea wasiwasi wake juu ya athari za kiuchumi zinazotokana na pombe haramu. Utafiti uliofanywa na Ernest & Young mnamo Novemba 2018 ulibaini kuwa serikali ya Tanzania inapoteza takriban shilingi trilioni 1.2 kila mwaka kutokana na biashara ya pombe haramu. Mauzo yasiyodhibitiwa yanadhoofisha biashara halali na kusababisha hasara kubwa ya mapato ya kodi, hali inayopunguza uwezo wa serikali kufadhili huduma muhimu kama afya na elimu. Zaidi ya hayo, sekta rasmi ya pombe—ambayo inatoa maelfu ya ajira—inakabiliwa na ushindani usio wa haki kutoka kwa waendeshaji wasiosajiliwa ambao wanakwepa kanuni za usalama na viwango vya ubora.

Ili kulinda afya ya umma na uthabiti wa uchumi, CTI ilitoa wito wa udhibiti mkali wa sekta ya pombe, ikisisitiza umuhimu wa kuimarisha imani ya wawekezaji, kuhamasisha unywaji wa pombe kwa uwajibikaji, na kuwalinda wananchi dhidi ya bidhaa hatari.

CTI na washirika wake wanatoa wito kwa serikali na wadau kuongeza juhudi za kupambana na pombe haramu kupitia utekelezaji madhubuti wa sheria, kuongeza uelewa wa umma, na kuboresha utekelezaji wa sera. Ushirikiano kati ya viongozi wa sekta, mamlaka za udhibiti, na vyombo vya usalama ni muhimu ili kuhakikisha sekta salama na yenye uwajibikaji katika unywaji pombe inayosaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Tanzania.

Na Oscar Assenga, TANGA

MABALOZI 23 wa Mkoa wa Tanga unaoundwa na Wasanii wa Filamu,Waandishi pamoja na watangazaji wametua Jijini Tanga kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Kupiga kura .

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari leo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga Ramadhani Omary alisema wameamua kujikusanya kwa pampoja kuja mkoani kwao kuleta hamasa kwenye dafrati la kudumu la wapiga kura.

Alisema kwamba watu wanapozungumzia mkoa wa Tanga hawawezi kuacha kuitaja Bandari,Zao la Mkonge ,Reli na Viwada na ukiangalia Bandari,Reli ndio ina hudumia viwanda na Rais Dkt Samia Suluhu ameweka fedha nyingi kwa ajili ya upanuzi kwenye Bandari ya Tanga .

Aidha alisema pia mkakati wa kuiboresha reli kuelekea mkoa wa Arusha na ambao itaifungua mkoa wa Tanga na serikali ina mkakati baada ya ubinafsishaji wale watu ambao hawakuviendelea viwanda vitarudi chini ya Serikali.

“Waliposikia Rais Dkt Samia Suluhu anatarajiwa kuja Tanga nao wakaamua kuja nyumbani kumpokea tutashiriki kwenye maandalizi na tutakuwepo Tanga muda wote mpaka Rais atakapowasili na leo tumeona tuhabarisha umma kupitia nyie wanahabari”Alisema

Awali akizungum za Chuchu Hans alisema kwamba wameungana na mabalozi wa Tanga na wao ni watu wa kujituma wana vipaji vingi ikiwemo ukarimu na wao wanawakilisha wenzao.

“Tumeona ni muda sahihi na umefika wakati wa kujiandikisha na tukaona tutumia nafasi hii kuhamasisha wananachi na sisi kuja kujiandikisha kwenye Daftari lakini pia Rais anakuja”Alisema.
Hata hivyo aliwaomba wananchi amba bado hawajajiandikisha kwenye daftari la kudumu la kupigia kura wakajiandikishe vituo vyote vipo wazi hivyo watumie haki yao ya msingi kwa ajili ya baadae kuwachagua viongozi wao.
Awali akizungumza katika mkutano huo na wanahabari Salim Awadhi “Gabo”- alisema wao wamekuja kuwakilisha wenzao kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kutumia haki yao ya msingi ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.



Alisema kwasababu mkoa wa Tanga ni watu wa ukarimu wao wameliona wabebe jukumu hilo kumsaidia Mkuu wa Mkoa huo Balozi Batilda Burian ambaye amekuwa kinara wa maendeleo kwenye mkoa huo.


Hata hivyo kwa upande wake Maliki Bandawe ambaye ni Msanii wa Bongo Fleva kutoka kundi la TNG alisema wameamua kurudia Tanga ili kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura lakini pia kutoa hamasa na kuwakumbusha vijana kujiandikisha kwenye daftari hilo.
“Wana Tanga tujitokezeni kwenye mapokezi ya Rais Dkt Samia Suluhu anakuja kwa mara ya kwanza baada ya kupitishwa na CCM kuwa Mgombea Urais kwenye uchaguzi Mwaka huu 2025”Alisema

Akielezea malengo ya ziara hiyo, Kiongozi wa Msafara Khalidi Swalehe alisema msafara huo mabalozi 23 kutoka mikoa tofauti wote ni wazawa wa mkoa wa Tanga ambao wanaitumia kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na mapokea ya kumlaki Rais Dkt Samia Suluhu.

“Naombeni wakazi wa Tanga waunge mkono na tulichokuja kukifanya ni kuhamasisha watu kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la kupiga kura na kuhakikisha tunaunga mkono jitihada za maendeleo kwa mkoa wa Tanga zinaofanywa na Mkuu wa Mkoa huo Balozi Dkt Batilda akimuwakilisha Rais Dkt Samia”Alisema
Hata hivyo alisema kwamba mkoa huo umeendelea kuamka kwa maana Tangu Tanzania ipate uhuru ilikuwa inasifika na kuna miradi mingi ya maendeleo imefanywa na Rais Dkt Samia Suluhu na wao wanahamasisha yale yanayopaswa kwenda masikioni mwa watu.