Articles by "TEKNOLOJIA"
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Na Mwandishi Wetu.

KAMPUNI ya Mati Super Brands Ltd kupitia tawi lake la Mati Technology imezindua teknolojia mpya ya ndege nyuki (drone) zinazotengenezwa nchini, zenye uwezo wa kuboresha sekta ya kilimo na huduma nyingine za kijamii.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Group of Companies, David Mulokozi, amesema kampuni hiyo imeamua kuwekeza katika uzalishaji wa drone zinazotumika kunyunyizia dawa mashambani, kupima maeneo, kupanda mbegu, kusafirisha mizigo na kusaidia kaguzi mbalimbali.

Mulokozi ameeleza kuwa drone hizo zitauzwa kuanzia Shilingi milioni 17, bei ambayo ni nafuu ukilinganisha na gharama kubwa za kuagiza kutoka nje ya nchi. Pia, kampuni ipo katika mazungumzo na benki ili kuwezesha wakulima kupata mikopo kwa ajili ya kumudu teknolojia hiyo.


“Tumeona changamoto kubwa inayowakabili wakulima hasa kwenye upuliziaji wa dawa. Kwa kutumia drone hizi, hekari moja inaweza kunyunyiziwa dawa ndani ya dakika saba pekee, jambo linaloongeza ufanisi na kulinda afya za wakulima,” alisema Mulokozi.

Aidha, amebainisha kuwa uzalishaji wa drone hizo utatoa ajira kwa wahandisi wa Kitanzania na kufanikisha uhamishaji wa teknolojia kutoka kwa wataalamu wa kigeni
Kwa upande wake, Afisa Ushirika kutoka ofisi ya Msajili mkoa wa Manyara, Godamen Merinyo, amesema teknolojia hiyo ni mkombozi mkubwa kwa wakulima wa mazao kama mbaazi ambayo hukua kwa urefu na kufanya unyunyiziaji wa dawa kuwa mgumu na wa gharama kubwa.

“Hii itasaidia kuongeza uzalishaji kwa gharama nafuu na kuimarisha vyama vya ushirika. Tutaanza kutoa elimu kwa wakulima kuhusu matumizi ya teknolojia hii,” alisema Merinyo.
Naye Afisa Kilimo wa mkoa wa Manyara, Paulo Eugine, amesema drone hizo zitasaidia kuwalinda wakulima dhidi ya madhara ya kiafya yaliyokuwa yanawapata kutokana na kutumia pampu za mgongoni.

“Sasa mkulima ataweza kutumia remote control bila kuingiliwa na sumu, jambo linaloimarisha usalama na afya zao,” alisisitiza Eugine.

Hatua hii ya Mati Technology inatarajiwa kuchochea mapinduzi ya kilimo nchini na kuunga mkono jitihada za serikali katika kukuza tija kwa kutumia teknolojia za kisasa.

 
Vodacom Tanzania imeadhimisha miaka 25 ya kuwahudumia Watanzania tangu kuanzishwa kwake katika hafla iliyofanyika Agosti 15, 2025, ikianzia makao makuu yake jijini Dar es Salaam. Sherehe hizo zilipambwa na ukataji wa keki iliyoashiria robo karne ya ukuaji, ubunifu na uongozi wa sekta ya mawasiliano nchini.

Baada ya hafla hiyo, familia ya Vodacom ilijumuika na wateja wake katika Soko la Stereo lililoko Temeke, ikiwa ni ishara ya kuthibitisha msemo wao wa “Tupo Nawe, Tena na Tena.” Kupitia tukio hilo, Vodacom iliendelea kuonesha dhamira yake ya kusogea karibu zaidi na wananchi, kusherehekea nao mafanikio yaliyopatikana kwa pamoja.

Vodacom pia ilitumia fursa hiyo kuwashukuru wateja kwa mapokezi makubwa ya huduma ya M-Pesa, tangu ilipoanzishwa mwaka 2008. Huduma hiyo imekuwa chachu ya mageuzi makubwa katika ujumuishi wa kifedha nchini kwa kutoa suluhisho kama mikopo midogo, uwekezaji kupitia M-Wekeza, pamoja na huduma za vikoba vya kidigitali kupitia M-Koba.
Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango akizungumza kwenye kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (kushoto kwake) wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Mifumo na Huduma za TEHAMA, Bw. Mohamed Mashaka.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Mary Mwakapenda (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu TEHAMA wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Bw. Paul Seadin (aliyesimama) akichangia hoja wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu TEHAMA wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Ibrahim Toure (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Na Veronica Mwafisi-Dar es Salaam.

Mradi wa Tanzania ya Kidijitali umeleta mapinduzi makubwa ya miundombinu ya TEHAMA nchini ikiwemo kuunganisha jumla ya taasisi za umma 600 ambazo ni Wizara, Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi na watumishi wa umma.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.

“Mradi huu umeleta mafanikio makubwa katika kuunganisha Serikali kwenye mitandao ya TEHAMA ambapo taasisi 600 ikiwemo Wizara, Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma zimeunganishwa na mifumo ya TEHAMA ili kutoa huduma kwa wananchi na watumishi wa umma nchini, amesema Bw. Kiwango
Ameongeza kuwa katika kutoa huduma bora, watumishi wa umma wameendelea kutekeleza majukumu yao kupitia mifumo mbalimbali na kupimwa kupitia mifumo iliyojengwa ya Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma na Taasisi (e-Utendaji).

Aidha, Mfumo wa Daftari la Huduma za Serikali utawasaidia wananchi kupata huduma sehemu moja kwa urahisi, kwa wakati na kwa uwazi.

Mkurugenzi Kiwango ametoa wito kwa wananchi kutumia simu zao za viganjani kupiga namba *152*00# kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali za Serikali bila kufika katika ofisi husika endapo hawatakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.

 

Na Mwandishi Wetu.

Mawaziri wa Mawasiliano kutoka Tanzania na Kenya wamezindua rasmi maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) wa Tanzania unaosimamiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), na mikongo ya baharini ya Mombasa kupitia Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (ICTA).

Uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidigitali wa Kenya, Injinia William Kabogo Gitau, pamoja na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mhe. Jerry Silaa.

Mawaziri hao wamesisitiza kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria, ikilenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya uhakika, pamoja na kupunguza changamoto za kukatika kwa mtandao.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Gitau amesema: “Jambo la msingi ni ushirikiano wa dhati kati ya nchi zetu mbili. Ni muhimu kuhakikisha tunatunza miundombinu hii ya kimkakati ili kuepuka uharibifu unaoweza kusababisha kukatika kwa umeme na mtandao. Pia tuendelee kuimarisha mahusiano yetu kwa manufaa ya pande zote.”

Kwa upande wake, Mhe. Jerry Silaa alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya pamoja ya mawasiliano kati ya nchi washirika ni wajibu wa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya kikanda.

“Kuna faida kubwa ya kuwa na maunganisho mengi ya mikongo ya mawasiliano. Hii husaidia kuwepo kwa mtandao wa uhakika, unaotegemewa hata wakati wa changamoto za kiufundi katika njia moja ya mawasiliano,” alisema Silaa.

Mkongo huo tayari umeanza kufanya kazi nchini Kenya, hatua inayowezesha huduma za intaneti na mawasiliano kusambaa kwa kasi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Uzinduzi huu unaashiria mafanikio makubwa katika juhudi za kuunganisha ukanda huu kidigitali na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Na Mwandish wetu, Dar es Salaam.

CHAMA cha Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) kimeshukuru uamuzi wa serikali ya kuwapatia mafunzo maalumu ya kunoa weledi na uzalendo wa wanachama wake kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Mabloga zaidi ya 200 wakiwemo wa diaspora walioanzisha Mtandao huo mwaka 2015 watapata mafunzo hayo.
 
“Tumekuwa na mazungumzo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambao kimsingi ndio wasimamizi wakuu wa maudhui na wametuthibitishia kwamba wapo hatua za mwisho za kutekeleza maagizo ya serikali ya kutoa mafunzo kwa mabloga wote nchini,” alisema Mwenyekiti wa TBN , Beda Msimbe.

Akifafanua kuhusu mafunzo hayo, Msimbe alisema kwamba lengo kuu la mafunzo ni kuwajengea mabloga weledi, uzalendo, na umakini katika kutambua na kupambana na habari feki, huku wakiwezesha usambazaji wa taarifa sahihi zitakazowawezesha wananchi kufanya maamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu ujao.

“ Tunahitaji kukumbushana kuhusu nchi hii, katiba yetu, amani na umuhimu wa uchaguzi katika demokrasia ya aina yetu.Uamuzi huu wa serikali wa kutupiga msasa ni muhimu sana” alifafanua.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Mwenyekiti huyo wa TBN, Beda Msimbe, alieleza kuridhishwa na juhudi zinazofanywa na serikali kufanikisha mafunzo. Alisema wameomba mafunzo hayo kipindi cha sasa kwa kuwa wapo wanablogu ambao ni mara ya kwanza kuelekea katika uchaguzi mkuu, na kurejea ombi lao tena wakati wa mkutano wa wadau ulioandaliwa na Wizara ya Habari,Utamaduni,sanaa na michezo.

Alisema kwamba uongozi wa TBN kwa sasa unafanya kazi kwa karibu na serikali kuhakikisha kuwa zaidi ya wanachama 150 wa chama hicho waliotawanyika nchini kote wanafaidika kikamilifu na mafunzo haya muhimu.

Msimbe aliwataka mabloga wote nchini kuhakikisha wanawasiliana na Mratibu wa TBN, Bw. Gadiola Emanuel ili kuthibitisha anwani zao na kuhakikisha taarifa zao ziko sahihi kwa ajili ya ushiriki. Pia alitumia fursa hiyo kuwaalika wale wote ambao bado hawajajiunga na TBN kufanya hivyo sasa ili waweze kunufaika na fursa hii muhimu ya mafunzo.

Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) kinajumuisha mabloga wanaotengeneza aina mbalimbali za maudhui, ikiwemo michezo, habari za siasa, afya, uchumi, na habari mchanganyiko. Mafunzo haya yanatarajiwa kuimarisha uwezo wao wa kutoa taarifa zenye ukweli na uhakika, hivyo kuchangia katika mazingira ya uchaguzi yenye uwazi na uwajibikaji.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri Wa Maliasili Na Utalii Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb), amepokea na kukabidhi vifaa vya kisasa vya kusaidia kupambana na kudhibiti ujangili na kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu kutoka kwa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kupitia mradi wa kupambana na ujangili na biashara haramu wa (IWT).

Akizungumza jijini Dodoma leo 14 Julai, 2025 wakati wa hafla fupi wa makabidhiano hayo, Waziri Chana amesema vifaa hivyo vya doria vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 91,000 sawa na shilingi za Kitanzania millioni 240 na vimekuwa chachu katika juhudi za serikali za kupambana na ujangili hapa nchini.

“Leo hii tunapokea vifaa (Pikipiki 20 na ndege nyuki (Drones) 07) kwa ajili ya kupambana na ujangili na biashara haramu ya nyara, vifaa hivi ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huu na niwatake mkavitumie katika kuimarisha shughuli za uhifadhi na kudhibiti ujangili katika maeneo yenu” amesema Waziri Chana.

Aidha Mhe. Chana ametaja manufaa ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuwezesha juhudi za serikali katika kudhibiti ujangili wa tembo ambapo idadi yao imeongezeka kutoka 43,000 mwaka 2014 hadi kufikia zaidi ya 60,000 mwaka 2022.
Awali, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Fortunata Msoffe ameseama Mradi huo wa IWT pia umechangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha Vikundi vya Kuratibu Doria (TCGs) kwenye Kanda za kiikolojia, kutoa Mafunzo kwa Askari na Maafisa wa Uhifadhi, kuwezesha matumizi ya Taarifa za Kiintelijensia, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa taasisi mbalimbali za ulinzi na uhifadhi.

“Mradi huu unaendelea kutekeleza miradi ya kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori na kuchangia kuboresha maisha ya jamii kupitia njia ya uwezeshaji wa shughuli za kuongeza kipato kama vile ufugaji nyuki, kilimo cha mazao yasiyopendwa na wanyamapori kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na ushirikishwaji wa jamii husika.” amesema Dkt. Msoffe.
Naye Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Godfrey Mulisa, amesema ufadhili wa vifaa hivyo kwa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara hiyo ni kutokana na kufurahishwa na juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutangaza utalii na kukabiliana na ujangili na biashara haramu


Morogoro, Tanzania: Kampuni ya Puma Energy Tanzania imetangaza uzinduzi rasmi wa kituo cha umeme wa jua chenye uwezo wa kilowati 570 katika kiwanda cha tumbaku cha Alliance One Tanzania Tobacco Limited (AOTTL). 

Mradi huu mkubwa, ulioko takriban kilomita 200 kutoka jijini Dar es Salaam katika eneo la Kingolwira, Morogoro, ni hatua muhimu katika dhamira ya Puma Energy ya kuziwezesha sekta za viwanda Tanzania kwa suluhisho la nishati safi, nafuu, na ya kuaminika.

Kituo hiki cha kisasa kinajumuisha paneli za sola 1,296 na inverter 6 zenye ufanisi wa hali ya juu. Mfumo huu uliounganishwa na gridi ya taifa umetengenezwa kutoa umeme wa kutosha wakati wa mchana kipindi chote cha uzalishaji wa kiwanda kuanzia Mei hadi Oktoba. Mradi huu ni matokeo ya Mkataba wa Ununuzi wa Umeme (PPA) wa miaka 10 ulioingiwa kati ya Puma Energy na AOTTL mwezi Aprili 2024, ambao unahakikisha upatikanaji wa umeme safi na wa kuaminika huku ukipunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa vyanzo vya kawaida vya umeme. Ujenzi ulianza mwezi Machi 2025 na kukamilika haraka mwezi Aprili, huku mfumo ukianza rasmi kazi tarehe 4 Mei 2025.

Bi. Fatma Abdallah, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, alisema "Mradi huu wa sola katika kiwanda cha Alliance One ni mafanikio makubwa, si tu kwa Puma Energy bali pia kwa sekta ya viwanda Tanzania. Unadhihirisha dhamira yetu ya dhati ya kutoa suluhisho la nishati safi, nafuu, na ya kuaminika linalowezesha biashara kustawi huku tukichangia katika ulinzi wa mazingira na mustakabali wa taifa letu. Tunajivunia kuwa mstari wa mbele katika mabadiliko haya ya nishati, tukionesha namna ubunifu unavyoweza kuchochea maendeleo ya kiuchumi sambamba na uwajibikaji wa kimazingira.

"Ikiwa na dhamana ya utendaji wa miaka 30, mfumo huu wa sola unahakikisha ufanisi wa nishati wa muda mrefu na uendelevu wa mazingira. Ni ushahidi thabiti wa maono ya Puma Energy ya kuwezesha sekta ya viwanda Tanzania kupitia suluhisho la nishati safi, bunifu, na imara, kwa ajili ya kukuza uchumi unaokwenda sambamba na utunzaji wa mazingira.

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Mafunzo ya Mitaala katika Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Dkt. Angela Katabaro (kushoto), na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom na Vodacom Tanzania Foundation, Zuweina Farah (kulia), wakishiriki katika hafla ya utiaji saini wa ishara kwa niaba ya taasisi zao kwa ajili ya ushirikiano wa kuviwezesha Vituo 184 vya Rasilimali za Walimu kwa vifaa vya TEHAMA na intaneti ili kusaidia mafunzo ya walimu kupitia mpango wa MEWAKA. Hafla hii imefanyika leo katika Hoteli ya Mount Meru, Arusha wakati wa uzinduzi rasmi wa Wiki ya CSO 2025.

Na Mwandishi Wetu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza East Africa, Bi. Anna Bwana (kushoto), na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom na Vodacom Tanzania Foundation, Zuweina Farah (kulia), wakionyesha makubaliano ya ishara ya ushirikiano wao unaotarajiwa kupanua mpango wa KiuFunza Pay-by-Skill unaolenga kuboresha elimu ya msingi. Tukio hili limefanyika leo katika Hoteli ya Mount Meru, Arusha wakati wa Wiki ya CSO 2025.

●Ushirikiano wazinduliwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya AZAKI 2025 jijini Arusha, Tanzania.

Dar es Salaam, 02 Juni 2025 — Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation leo umetangaza uwekezaji wa TZS bilioni 3.25 kwa kipindi cha miaka mitatu ili kuendeleza sekta ya elimu nchini Tanzania kupitia ushirikiano mpya na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE) na Twaweza Afrika Mashariki. Tangazo hili lilitolewa wakati wa ufunguzi rasmi wa Wiki ya AZAKI 2025, kwa heshima ya uwepo wa Mhe. Adolf Mkenda, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Akizungumza katika hafla hiyo, Zuweina Farah, Mkurugenzi wa Mahusiano wa Vodacom Plc na Vodacom Tanzania Foundation, alisema: "Kupitia ushirikiano huu, tunalenga kuimarisha ubora wa elimu nchini Tanzania kwa kuwapa walimu zana sahihi na kuwasaidia wanafunzi kujenga ujuzi madhubuti wa msingi. Uwekezaji katika elimu leo utatoa fursa zaidi kwa vizazi vijavyo."

Kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Vodacom itaviwezesha Vituo 184 vya Rasilimali za Walimu (TRCs) kwa vifaa vya TEHAMA na huduma ya intaneti ya uhakika ili kusaidia utekelezaji wa mpango wa serikali wa Maendeleo Endelevu ya Utaalamu wa Walimu (TCPD) ujulikanao kama MEWAKA. Miundombinu hii ya kidijitali itawawezesha walimu zaidi ya 300,000 nchini kote kufikia vifaa vya kujifunza kupitia Mfumo wa Usimamizi wa Kujifunza (LMS), na hivyo kuboresha ubora wa ufundishaji kwa mujibu wa mtaala mpya wa msingi wa umahiri wa mwaka 2023 wa Tanzania.

Dkt. Angela Katabaro, Mkurugenzi Mkuu wa TIE, alisema: "Uwezeshaji wa walimu kwa TEHAMA ni jambo la msingi katika utoaji wa elimu bora. Kupitia ushirikiano na Vodacom, tunaweza kupanua mpango wetu wa MEWAKA na kuziba pengo la kidijitali."

Aidha, ushirikiano wa Taasisi ya Vodacom Foundation na Twaweza utaunga mkono upanuzi wa mpango wa KiuFunza Pay-by-Skill, ambao unawapa motisha walimu wa darasa la 1-3 kuwasaidia wanafunzi kumudu stadi za msingi za kusoma, kuandika na kuhesabu. Mpango huu utafanyika katika shule 865, ukifikia zaidi ya wanafunzi 360,000 wa madarasa ya awali ya msingi. Takwimu za kitaifa zinaonesha kuwa asilimia 60 ya watoto wa miaka 10 nchini Tanzania bado wanapata changamoto ya kusoma na kuelewa hadithi rahisi.

Anna Bwana, Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza Afrika Mashariki, alisema: "Ushirikiano huu unahakikisha kuwa kujifunza kunatokea katika kila darasa. Tuna ushahidi dhabiti kuwa Pay-by-Skill unafanya kazi. Unawatia motisha walimu na kuboresha matokeo kwa watoto."

Uwekezaji wa elimu wa Vodacom Tanzania unalingana na vipaumbele vya kitaifa vya elimu nchini Tanzania, Lengo la Maendeleo Endelevu namba 4 (elimu bora), pamoja na dhamira ya Vodacom ya kuwawezesha watu kupitia elimu jumuishi, mabadiliko ya kidijitali, na ubunifu kwa ajili ya matokeo chanya. Katika kipindi cha miaka mitatu, Vodacom Foundation itatoa fedha pamoja na msaada wa kitaalamu katika kuimarisha utekelezaji wa programu, utafiti, ufuatiliaji, na utetezi.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Kupitia Mradi wa FemAILeaders, Shirika la Women Political Leaders (WPL), GIZ Makao Makuu, GIZ Tanzania na Omuka imeandaa Mafunzo ya Akili Mnemba “Artificial Intelligence - AI” yaliyoanza Mei 19 hadi 20 mwaka 2025, Dar es Salaam yaliyolenga mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi wa mtandao,ubunifu na matumizi ya AI.
Mafunzo haya yaliwaleta pamoja Wabunge, Wabunifu na Makundi mengine kwa lengo la kuangazia ubunifu na matumizi ya AI, ulinzi wa kimtandao, utatuzi wa changamoto za AI na uhitaji wa kisera.
Delegation ya Bunge iliongozwa na Mhe Salome Makamba na kujumisha Mhe Prof Joyce Ndalichako, Mhe Esther Matiko, Mhe Ng’wasi Kamani na Makatibu wa Kamati za Bunge, Adv Ganjatuni Kilemile na Pius Katabazi.
Tanzania imeendelea kuongoza barani Afrika kwa Kuimarisha Uelewa na Ushawishi wa Wabunge Wanawake ili wawe Vinara wa AI hivyo kuchangia kwa Tanzania kunufaika na fursa zinazotokana na Akili Mnemba - AI. Tanzania imechaguliwa kuwa Mfano wa Kuigwa barani Afrika katika eneo hili.
Aidha, Mradi wa FemAILeaders umeweza kufanyika Tanzania kufuatia jitihada za Mhe Neema Lugangira (Mb) ambae pja ni Mwakilishi wa Afrika/Mjumbe Maalum wa Afrika wa Shirika la Women Political Leaders (WPL) hivyo ametumia nafasi hiyo kuileta fursa hii Tanzania.