Vodacom Tanzania imeadhimisha miaka 25 ya kuwahudumia Watanzania tangu kuanzishwa kwake katika hafla iliyofanyika Agosti 15, 2025, ikianzia makao makuu yake jijini Dar es Salaam. Sherehe hizo zilipambwa na ukataji wa keki iliyoashiria robo karne ya ukuaji, ubunifu na uongozi wa sekta ya mawasiliano nchini.
Baada ya hafla hiyo, familia ya Vodacom ilijumuika na wateja wake katika Soko la Stereo lililoko Temeke, ikiwa ni ishara ya kuthibitisha msemo wao wa “Tupo Nawe, Tena na Tena.” Kupitia tukio hilo, Vodacom iliendelea kuonesha dhamira yake ya kusogea karibu zaidi na wananchi, kusherehekea nao mafanikio yaliyopatikana kwa pamoja.
Vodacom pia ilitumia fursa hiyo kuwashukuru wateja kwa mapokezi makubwa ya huduma ya M-Pesa, tangu ilipoanzishwa mwaka 2008. Huduma hiyo imekuwa chachu ya mageuzi makubwa katika ujumuishi wa kifedha nchini kwa kutoa suluhisho kama mikopo midogo, uwekezaji kupitia M-Wekeza, pamoja na huduma za vikoba vya kidigitali kupitia M-Koba.
.jpg)




.jpg)
.jpg)
.jpg)
Toa Maoni Yako:
0 comments: