Articles by "HABARI ZA BIASHARA"
Showing posts with label HABARI ZA BIASHARA. Show all posts

SHIRIKA lisilo la kiserikali la BRAC Tanzania limeweka mikakati zaidi kusaidia kuwawezesha wanawake kiuchumi kwa kuwapa mafunzo kwenye fani mbalimbali na kuwapatia mitaji.

Wakiadhimisha siku ya wanawake duniani BRAC yenye wanachama zaidi ya 450,000 katika Mikoa 27 Tanzania wamelenga wakufikia wanawake wote kupitia vikundi vya kuweka na kukopa.

Kupitia kauli mbiu ya Siku ya wanawake duniani mwaka 2026 ni “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050”, ikilenga kujenga uelewa wa kuwekeza katika maendeleo jumuishi kwa kutambua na kutekeleza haki za wanawake na wasichana kwa vitendo.

‎Amesisitiza kuwa kaulimbiu hiyo imejikita katika nguzo za Dira ya Taifa ya 2050 na inahusisha makundi yote ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Mtaalamu wa Elimu na Mafunzo kutoka BRAC , Sophia Nyanda amesema shirika lao lina mchango mkubwa katika jamii kwani imewawezesha wasichana waliokatisha masomo kwa sababu mbalimbali ili kuweza kufikia malengo yao.

Nyanda amesema, wana mradi wa Elimu unaojulikana kama AIM ambao umeweza kuwafikia wasichana hao na kuwapa mafunzo ya fani mbalimbali na kupatiwa vifaa na kisha kuwapatia mtaji ili waweze kuendesha miradi yao.

" sisi kama BRAC tunataka kuwafikia wanawake kwa kiwango kikubwa, tunataka kufika kila mkoa ili kuwasaidia mabinti hawa ambapo baadae wakiahapata ujuzi watajiendeleza na kuendesha maisha yao bila kuwa tegemezi," amesema Nyanda.
Mtaalamu wa Masuala ya Mikopo kutoka BRAC Tanzania Bi. Graciana Rimoy akitoa elimu kwa wanawake juu ya namna ya kuweka na kukopa ili waweze kujiendeleza kiuchumi. Hayo yamefanyika katika kuadhimisha Siku ya wanawake duniani yakiwa na kauli mbiu ya “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050”, ikilenga kujenga uelewa wa kuwekeza katika maendeleo jumuishi kwa kutambua na kutekeleza haki za wanawake na wasichana kwa vitendo.

Kwa upande wa Mtaalamu wa Mikopo Kutoka BRAC Graciana Rimoy amesema shirika lao limekuwa linawafikia wanawake wengi kupitia mikopo ya vikundi vya kuweka na kukopa ambao kwa sasa wanahudumia zaidi ya wanawake 450,000 nchi nzima.

Amesema, wanafanya hivyo ili kuwawezesha wanawake wajiendeleze kibiashara na kabla ya kumpa mkopo huo huwa wanampa elimu ya biashara na namna ya kuweka akiba.

" tumekuwa na utaratibu wa kutoa elimu ya mikopo kwa wanawake wote ambao tunawahudumia, na hili limesaidia sana kwani wamekuwa wanaweza kuendesha biashara zao huku wakiweka akiba," amesema Rimoy.

Ameongeza kuwa, kumekuwa na wimbi la wanawake kuingia kwenye madeni ya mara kwa mara kutokana na kukosa elimu ya mikopo na namna ya uendeshaji wa biashara, ambapo ameshauri wanawake hao kuacha kutanguliza shida binafsi pindi wanapohitaji mikopo bali wazingatie vigezo na masharti ambavyo Kampuni wanaziweka.

Aidha, ameshauri Benki kuu kuweza kuweka mfumo wa pamoja wa makampuni wanayokopesha ili pindi mteja atakapokuwa anaenda kukopa iweze kuonesha taarifa za mteja huyo.

Naye Siwema Chuma mmoja wa wanufaika amewashukuru Brac kwa mazuri wanayoyatenda kwao kwani wameweza kusoma fani ya Upishi na kupewa mtaji ambao hadi sasa amesema kufungua ofisi nyingine kupitia biashara hiyo pamoja na kuajiri watu ili waweze kumsaidia.

Brac wamekuwa na utaratibu wa kutoa elimu ya mafunzo ya fani mbalimbali kwa wasichana ambapo wakishamaliza huwapatia mtaji au vifaa na kisha kuwapa mikopo ili waendeleze biashara zao.
Mwanasaikolojia na mtoa elimu Aunty Sadaka akizungumza na wanawake waliojitokeza wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake mwaka 2026 yenye kauli mbiu “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050”, ikilenga kujenga uelewa wa kuwekeza katika maendeleo jumuishi kwa kutambua na kutekeleza haki za wanawake na wasichana kwa vitendo.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mjasiriamali Daniel Deogratus Sambo, mkazi wa Kigoma Mjini, na mwanadada Doreen Masawe wameibuka washindi wa pikipiki aina ya TVS kupitia promosheni ya “Shinda Boda” inayoendeshwa na kampuni ya michezo ya kubahatisha ya PigaBet.

Akizungumza baada ya kupokea zawadi yake, Sambo alisema ushindi huo ni fursa muhimu itakayomsaidia kurahisisha shughuli zake za kila siku pamoja na kukuza biashara zake.

Alisema kuwa licha ya kucheza kwa muda mrefu bila mafanikio makubwa, hakukata tamaa na hatimaye juhudi zake zimemletea matokeo chanya.

“Nilianza kucheza muda mrefu, lakini leo nimebahatika kushinda pikipiki. Hii itanisaidia sana katika shughuli zangu za kila siku na kuongeza kipato,” alisema Sambo huku akiwahimiza vijana wengine nchini kushiriki promosheni hiyo kwa uwajibikaji kwani inaweza kuwapatia fursa kama aliyopata yeye.
Katika tukio hilo, mshindi mwingine Doreen Massawe naye alieleza kufurahishwa na ushindi wake akisema pikipiki hiyo itamsaidia katika shughuli zake za kilimo na kurahisisha usafiri wakati wa kusimamia kazi zake mashambani.

“Ninajihusisha na kilimo, hivyo pikipiki hii itanisaidia sana katika kurahisisha shughuli zangu za kila siku,” alisema.
Kwa upande wake, Afisa Masoko wa PigaBet Tanzania, Hemed Msonge, alisema kampuni hiyo imeanzisha promosheni ya “Shinda Boda” ikiwa na lengo la kuwainua Watanzania kiuchumi kupitia zawadi za pikipiki zitakazotolewa kila wiki.

Alisema kuwa katika promosheni hiyo pikipiki mbili zitatolewa kila wiki kwa kipindi cha wiki sita mfululizo, hatua inayolenga kuwapa washiriki fursa ya kujiongezea kipato kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo usafiri wa bodaboda.

Msonge aliwahimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki katika promosheni hiyo huku akisisitiza umuhimu wa kucheza michezo ya kubahatisha kwa uwajibikaji.

Aliongeza kuwa droo za promosheni hiyo zitaendelea kufanyika kila wiki hadi mwisho wa kampeni, akibainisha kuwa kaulimbiu ya kampeni hiyo ni “Cheza, shinda boda na ubadilishe maisha yako.”
Na Mwandishi Wetu.

Kampuni ya kubeti ya SportPesa Tanzania imeendelea kuwapa Watanzania fursa ya kubadilisha maisha yao kupitia ushindi wa jackpot pamoja na michezo mbalimbali ya kasino na Aviator, huku zaidi ya shilingi bilioni moja zikitolewa kwa washindi wa jackpot pekee katika kipindi cha mwaka uliopita.

Miongoni mwa washindi waliopata bahati hiyo ni Hamza Athman ambaye alijishindia kiasi cha shilingi 237,897,560 kupitia mchezo wa Midweek Jackpot. Ushindi huo umeelezwa kuwa umeleta mabadiliko makubwa katika maisha yake.

Akizungumza baada ya kupokea zawadi yake rasmi, Hamza alisema ushindi huo umemfungulia ukurasa mpya wa maisha na kumpa matumaini makubwa ya baadaye. Alisema siku zote alikuwa na imani kuwa ili kushinda lazima uwe sehemu ya jukwaa la SportPesa.

Mbali na jackpot, kampuni hiyo pia imeendelea kushuhudia ushindi mkubwa kupitia michezo ya kasino na Aviator, ambapo washindi hupatikana kila siku kwa kuweka dau dogo. Katika tukio moja la hivi karibuni, mchezaji mmoja aliweka dau la shilingi 420 na kufanikiwa kujishindia kiasi cha shilingi 27,964,800.

Ushindi huo unaonyesha kuwa michezo hiyo imeendelea kutoa fursa kwa wachezaji wa viwango mbalimbali, iwe ni kupitia jackpot zenye odd ndefu, ubashiri wa michezo au michezo ya kasino yenye multiplier kubwa. Wachezaji wamekuwa wakipokea ushindi wao moja kwa moja kwenye akaunti zao bila ucheleweshaji.

Akizungumzia mafanikio hayo, Mkuu wa Masoko wa SportPesa Tanzania, Tracy Humplick, alisema kampuni hiyo inaendelea kuboresha mifumo yake ili kuhakikisha wateja wanapata uzoefu bora wa kucheza na kupata ushindi wao kwa urahisi.

Alisema kampuni inawekeza katika teknolojia, huduma kwa wateja na kuboresha masharti ya michezo ili kuhakikisha uwazi, haki na uendelevu wa huduma kwa wachezaji wote.

Aidha, SportPesa Tanzania inaendelea kufanya shughuli zake kwa kuzingatia sheria na kanuni za serikali, huku pia ikichangia katika mapato ya taifa, kukuza sekta ya michezo na kutoa ajira kwa maelfu ya Watanzania.

Kwa mujibu wa kampuni hiyo, hadithi za washindi kama Hamza zinaendelea kuwahamasisha Watanzania wengi kujiunga na jukwaa hilo, huku zikionesha kuwa fursa ya ushindi ipo kwa kila mchezaji anayejitosa kwa nidhamu na ujasiri. Kadri idadi ya washiriki inavyoongezeka, ndivyo mzunguko wa ushindi na fursa unavyozidi kupanuka kwa Watanzania wengi zaidi.

Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania, Bw. Shani Kinswaga, akipokea moja ya tuzo mbili kutoka kwa Makamu wa Rais Mwandamizi – Meneja wa Nchi, Afrika Mashariki na Visiwa vya Bahari ya Hindi wa Mastercard, Shehryar Ali (wa pili kushoto), wakati wa ziara ya Mastercard katika ofisi za Benki hiyo jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki hii. Benki ya Exim ilitunukiwa tuzo ya “Best Elite Banking Proposition - 2025” pamoja na tuzo ya “Highest Spend Per Card in Tanzania - 2025”. Tukio hilo lilishuhudiwa na Makamu wa Rais na Meneja wa Akaunti wa Mastercard, Elsie Kaguru (kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na wa Kati wa Benki ya Exim Tanzania, Andrew Lyimo (wa pili kulia), pamoja na Mkuu wa Uendeshaji na Utoaji wa Huduma wa Exim Benki, Tumaini Mwakafwaga (kulia). Hafla hiyo imefanyika mwanzoni mwa wiki hii, jijini Dar es salaam.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Februari 26, 2026 — Benki ya Exim Bank Tanzania imeendelea kuthibitisha ubora wake katika sekta ya huduma za kifedha baada ya kutunukiwa tuzo mbili muhimu na kampuni ya kimataifa ya malipo ya kidijitali, Mastercard, kufuatia mafanikio yake ya mwaka 2025. Tuzo hizo zilikabidhiwa wakati wa ziara maalum ya Mastercard katika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizo mbili.

Katika hafla hiyo, Exim Bank ilitunukiwa tuzo ya “Best Elite Banking Proposition – 2025” pamoja na “Highest Spend Per Card in Tanzania – 2025”, tuzo zinazoonesha mafanikio ya benki hiyo katika kubuni na kuendesha huduma za kibenki za hadhi ya juu na kuongoza kwa kiwango cha matumizi ya kadi kwa kila mteja nchini. Mafanikio hayo yanatokana na uzinduzi wa huduma ya Elite Banking uliofanyika Julai 2025, uliolenga kuwahudumia wateja wa hadhi ya juu kwa kuwapatia suluhisho za kifedha zilizobuniwa mahsusi kulingana na mahitaji yao na mtindo wao wa maisha.

Kupitia huduma hiyo, wateja hupatiwa Meneja Mahusiano binafsi anayetoa ushauri wa uwekezaji, mikopo maalum na huduma nyingine za kifedha, sambamba na manufaa ya kimataifa ikiwemo upatikanaji wa lounge za viwanja vya ndege kupitia huduma ya Mastercard DragonPass.
Aidha, tuzo ya “Highest Spend Per Card” imeakisi mafanikio ya benki katika kuhamasisha matumizi ya kadi, hatua iliyochangiwa na kampeni mbalimbali za kimkakati ikiwemo UEFA Priceless Campaign, ambayo ilihamasisha malipo kwa kutumia kadi huku ikitoa fursa za kipekee kwa washindi kufurahia ofa za kimataifa.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi tuzo hizo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Exim Bank, Andrew Lyimo, alisema tuzo hizo ni uthibitisho wa mkakati wa benki wa kubadilisha na kuinua viwango vya huduma za premium banking nchini. Alisema uzinduzi wa Elite Banking ulikuwa hatua muhimu katika safari ya benki hiyo kuwahudumia wateja wake kwa ubora wa hali ya juu kwa kuunganisha suluhisho za kifedha zilizo bora na ofa za kipekee zinazolingana na mfumo wa maisha ya wateja.

Kwa upande wake, Makamu Rais na Meneja wa Akaunti wa Mastercard, Elsie Kaguru, alisema Exim Bank imeonesha uongozi wa kipekee katika kukuza huduma za premium banking na kuimarisha matumizi ya kadi nchini Tanzania, akibainisha kuwa ukuaji wa haraka wa huduma ya Elite Banking pamoja na kiwango cha juu cha matumizi kwa kila kadi vinaakisi uelewa sahihi wa mahitaji ya wateja wa kisasa.

Ushirikiano kati ya Exim Bank na Mastercard umejikita katika kuimarisha mifumo salama ya malipo ya kidijitali, kuboresha huduma za kadi za hadhi ya juu na kupanua upatikanaji wa manufaa ya kimataifa kwa wateja wa Tanzania. Mafanikio haya yanaonesha ushindani unaoongezeka katika soko la huduma za kibenki za hadhi ya juu nchini, huku taasisi za kifedha zikizidi kuwekeza katika ubunifu na teknolojia ili kukidhi mahitaji ya wateja wa kizazi kipya na kuchochea ukuaji endelevu wa sekta ya fedha.
DAR ES SALAAM, Feb. 27, 2026 — Samsung Electronics has launched its Galaxy S26 smartphone series in Tanzania, positioning the new lineup as a strategic move to strengthen its premium device footprint in the country’s fast-growing digital economy.

The launch, led by the flagship Galaxy S26 Ultra, signals Samsung’s focus on capturing high-value smartphone consumers by emphasizing data privacy, artificial intelligence integration and professional-grade imaging — features increasingly in demand among business users, entrepreneurs and content creators.
At the centre of the device’s value proposition is its new built-in Privacy Display, a screen-level protection technology designed to shield confidential information from side viewing. The feature responds to growing concerns among corporate users and financial service clients who rely on smartphones for transactions, communications and document access in public environments.

Speaking during the launch, Samsung Tanzania Head of Mobile Business Mgopelinyi Kiwanga said the device reflects shifting market priorities where privacy, productivity and reliability are now key purchasing drivers. He noted that smartphones have evolved into essential work tools, making secure data handling a competitive differentiator in the premium segment.
Industry analysts view the S26 series as part of Samsung’s broader strategy to consolidate its leadership in Africa’s upper-tier smartphone market while supporting the region’s accelerating digital transformation. Tanzania’s expanding fintech sector, remote work adoption and content creation economy are expected to increase demand for high-performance devices with strong security credentials.
In addition to privacy features, the S26 Ultra integrates advanced Galaxy AI tools capable of assisting with scheduling, communication workflows and information retrieval, functions that could appeal to corporate executives and small-business operators seeking efficiency gains. Enhanced night photography and professional video capabilities also position the device as a viable tool for digital marketing, media production and social commerce.
The Galaxy S26 series is now available for pre-order through authorized retail partners nationwide, with Samsung projecting strong uptake in the premium segment driven by enterprise users, professionals and high-income consumers.

The launch underscores Samsung’s continued investment in Tanzania’s technology ecosystem and its intention to remain a dominant player as smartphone usage increasingly shapes the country’s business environment.
Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam, Februari 27, 2026: Kampuni ya Puma Energy Tanzania imeandaa futari maalum kwa wateja na washirika wake ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha mahusiano na kuonesha shukrani katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Mkusanyiko huo uliwakutanisha wateja, wadau pamoja na viongozi wa kampuni katika mazingira ya umoja na mazungumzo ya karibu, yakilenga kuimarisha ushirikiano unaochangia mafanikio ya shughuli za kampuni nchini. Futari hiyo ilielezwa kuwa ishara ya kuthamini wateja ambao mchango wao wa muda mrefu unaendelea kuwa nguzo muhimu ya ukuaji wa kampuni.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Fatma M. Abdallah, alisema mkusanyiko huo ni njia ya kutambua nafasi ya wadau katika safari ya kampuni.

“Ramadhani ni kipindi cha kuonesha shukrani na kuthibitisha upya dhamira yetu ya kutoa huduma kwa uadilifu, ushirikiano na uwajibikaji kwa jamii,” alisema.
Kwa upande wake, Sheikh Mkowe Abdallah alisisitiza umuhimu wa mshikamano katika kipindi cha Ramadhani, akibainisha kuwa futari za pamoja huimarisha uhusiano wa kijamii na kuhimiza maadili ya huruma, heshima na uadilifu.

Mbali na tukio hilo, kampuni hiyo imeendelea kupanua uwekezaji wake katika nishati mbadala nchini, ikiwemo mradi wa gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) jijini Dar es Salaam unaolenga kuongeza upatikanaji wa mafuta safi na nafuu kwa magari ya abiria na mizigo. Mradi huo pia umechangia ajira kwa mamia ya Watanzania pamoja na kushirikisha wakandarasi wa ndani na biashara ndogo na za kati.

Akihitimisha, Mkuu wa Idara ya Sheria na Mahusiano wa kampuni hiyo, Emmanuel G. Bakilana, alisema mikusanyiko kama hiyo ni sehemu ya kujenga biashara yenye maadili na ushirikiano wa kudumu.

Alisema futari hiyo imeonesha wazi dhamira ya kampuni ya kuendelea kuimarisha mahusiano na wadau wake huku ikiunga mkono maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini kupitia uwekezaji katika miundombinu ya nishati.

Dar es Salaam. Taasisi isiyo ya kiserikali ya RAOMA Foundation kwa kushirikiana na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania Plc wamezindua mfumo mpya wa kidijitali wa elimu unaoitwa SOMO, chini ya kampeni ya Twende Zetu Darasani, hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa elimu bora kupitia teknolojia.

Mfumo huo umeundwa mahususi kusaidia ufundishaji na ujifunzaji wa masomo yote kwa kuzingatia mtaala wa taifa, huku ukimwezesha mwalimu kufundisha wanafunzi waliopo maeneo mbalimbali nchini kwa wakati mmoja. Lengo ni kuunganisha shule, walimu na wanafunzi kwa kutumia zana za kidijitali ili kuongeza ubora wa elimu na kuifanya ipatikane kwa usawa.


Akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri wa Elimu, Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Ladslaus Mnyone, alisema matumizi ya teknolojia katika elimu ni msingi muhimu wa kufikia malengo ya maendeleo ya taifa.

Alisema kuwa kupitia mifumo ya kidijitali, taifa linaongeza fursa za elimu, linaimarisha ubora wake na kuwaandaa wanafunzi kuwa na stadi zitakazochochea uchumi wa baadaye. Pia aliwapongeza wadau waliohusika katika ubunifu huo akisema ni hatua kubwa ya mapinduzi ya elimu nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa RAOMA Foundation, Rahma Abdallah, alisema ushirikiano wao na Vodacom unalenga kuhakikisha teknolojia inasaidia kutimiza ndoto za wanafunzi na kuboresha mazingira ya ujifunzaji.

Aliongeza kuwa taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na serikali, wadau wa maendeleo na sekta binafsi ili mfumo huo ufike katika shule nyingi zaidi na kuchochea elimu jumuishi.

Naye Mkuu wa Bidhaa za Biashara na Suluhisho kutoka Vodacom Tanzania, Ali Z. Ali, alisema ubunifu wa SOMO ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuiwezesha Tanzania kuingia kikamilifu katika ulimwengu wa kidijitali.

Alieleza kuwa mfumo huo utamwezesha mwalimu mmoja kufundisha wanafunzi wengi katika shule tofauti bila kulazimika kuwepo darasani, jambo litakalosaidia kupunguza changamoto za upungufu wa walimu na kuongeza ubora wa ufundishaji.
Uzinduzi wa mfumo wa SOMO unatazamwa kuwa hatua muhimu katika safari ya Tanzania kuelekea elimu ya kisasa, jumuishi na inayotumia teknolojia, huku ukilenga kuandaa kizazi chenye ujuzi wa kidijitali na uwezo wa kushindana kimataifa.

Dar es Salaam — Benki ya Exim Bank Tanzania imeandaa hafla ya futari kwa wateja wake jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mahusiano ya karibu yanayojengwa juu ya uaminifu, uwajibikaji na maadili ya pamoja.

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Jaffari Matundu, alisema mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya kutafakari na kuimarisha misingi ya maadili mema katika maisha na biashara.
Alisisitiza kuwa benki hiyo inathamini mahusiano na wateja wake zaidi ya miamala ya kifedha, akieleza kuwa dhamira yao ni kujenga imani, kupanua fursa na kugusa maisha ya watu kwa namna chanya.
Katika hatua ya kuendeleza ujumuishi wa kifedha, benki hiyo imeendelea kupanua mtandao wake wa matawi kwa kufungua ofisi katika maeneo ya Kahama, Ubungo na Paje, huku mipango ikiendelea kufungua tawi jingine Geita, lengo likiwa kusogeza huduma karibu zaidi kwa wafanyabiashara na wananchi.

Matundu alisema uaminifu wa wateja ndio mtaji mkubwa wa benki hiyo, akiahidi kuendelea kutoa huduma bora zinazolenga kusaidia ukuaji wa biashara na maendeleo ya wateja wake kwa muda mrefu.
Hafla hiyo iliwakutanisha viongozi wa dini, wateja na wageni waalikwa mbalimbali katika mazingira ya mshikamano, tafakari na kuimarisha ushirikiano kwa maendeleo ya pamoja.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Khadija Ngasongwa, akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari iliyoandaliwa na Tume hiyo, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana, Februari 24, 2026.
Makamu wa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi Habari Mkoa wa Dar ea Salaam (DARPC) Mary Geofrey akitoa maelezo kuhusiana na semina ya FCC itavyochochea ushindani wa soko ,jijini Dar es Salaam.
Semanina ikiendelea 
Picha pamoja ya wafanyakazi wa FCC na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Khadija Ngasongwa katika Semina ya Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam.
Picha pamoja ya waandishi wa Habari na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Khadija Ngasongwa katika Semina ya Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam.



Dar es Salaam — Tume ya Ushindani nchini, Fair Competition Commission (FCC), imesema itaendelea na mchakato wa marekebisho ya sheria zake ili kuimarisha ulinzi wa walaji, kudhibiti bidhaa bandia na kuhakikisha kunakuwepo ushindani wa haki unaochochea ukuaji wa uchumi na ajira.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Ngasongwa alisema marekebisho hayo yanalenga kumlinda mlaji dhidi ya bidhaa zisizo na ubora, matangazo ya upotoshaji pamoja na vitendo vinavyokiuka misingi ya ushindani wa haki sokoni.

Alibainisha kuwa moja ya vipaumbele vya tume hiyo ni kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia zinazoingia nchini, akieleza kuwa bidhaa hizo huathiri afya za wananchi, hupunguza mapato ya Serikali na kuwanyima wafanyabiashara halali fursa ya kukuza biashara zao.

“Jukumu letu ni kuhakikisha uchumi unakua kwa misingi ya ushindani wa haki, jambo linalochochea uwekezaji na kuongeza ajira kwa wananchi,” alisema.

Aidha, FCC imesema itaendelea kukutana mara kwa mara na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali ili kutoa taarifa sahihi kuhusu majukumu yake na kusikiliza changamoto za wananchi kwa lengo la kuzitatua kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Ngasongwa alisema kuna maboresho yanayoendelea kupitia mfumo wa TANOGA, unaojumuisha taasisi za udhibiti na mawakala wa forodha, kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa bidhaa zinazoingia nchini.

Aliongeza kuwa taasisi hizo zinaelekea kuingia katika mfumo wa kidijitali utakaopunguza mwingiliano wa moja kwa moja kati ya watumishi na wateja, hatua itakayosaidia kuongeza uwazi, kupunguza urasimu na kudhibiti mianya ya vitendo visivyo vya kiadilifu.

FCC imeahidi kuendelea kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali pamoja na sekta binafsi ili kuhakikisha mazingira ya biashara nchini yanabaki kuwa salama, yenye ushindani wa haki na yenye manufaa kwa wananchi.

Na Mwandishi Wetu, Doha

Serikali ya Tanzania imeanza mkakati mpya wa kimataifa wa kutangaza madini ya Tanzanite katika soko la Mashariki ya Kati, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kurejesha hadhi na thamani ya madini hayo adimu duniani.

Akizungumza Februari 25, 2026 jijini Doha, Waziri wa Madini Anthony Mavunde alisema serikali imeamua kuongeza juhudi za kuitangaza Tanzanite kimataifa baada ya kubaini kuwa baadhi ya masoko bado hayafahamu asili ya madini hayo kuwa yanapatikana Tanzania pekee.

Alisema kushuka kwa uelewa wa soko la kimataifa kumeathiri bei na mauzo ya madini hayo, hivyo wizara imeanza hatua za kuyafikia masoko mapya na kuwavutia wawekezaji pamoja na wafanyabiashara wa vito.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde alitembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar ambapo alikutana na watumishi wa ubalozi na kukubaliana kuandaa mkutano wa wawekezaji na wafanyabiashara wa madini kati ya nchi hizo mbili.

Aidha, serikali imepanga kuratibu ushiriki wa wafanyabiashara wa madini ya vito kutoka Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya madini yatakayofanyika Doha mwezi Aprili 2026, yakilenga kupanua masoko, kuongeza uwekezaji na kuimarisha utalii unaotokana na rasilimali madini.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mheshimiwa Habibu Awesi Mohamed, alisema fursa za ushirikiano katika sekta ya madini ni kubwa na zikiendelezwa zinaweza kuongeza mapato ya taifa na kukuza uchumi

Hatua hiyo inaonekana kuwa sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa kuitangaza Tanzanite kama alama ya kipekee ya Tanzania duniani na kuongeza mcvhango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.