Articles by "HABARI ZA BIASHARA"
Showing posts with label HABARI ZA BIASHARA. Show all posts
Mwamko mdogo wa Watanzania kuhusu bima ya afya ni mojawapo ya changamoto katika kutoa huduma bora za afya kwa wote kutokana na idadi ndogo ya Watanzania wenye bima. Takwimu za Wizara ya Afya (2022) zinaonesha kuwa asilimia 15 tu ya Watanzania, sawa na watu milioni 9.1, walikuwa na bima ya afya mwishoni mwa mwaka 2021, ikishuka kutoka asilimia 32% mwaka 2018.

Vodacom Tanzania PLC imeungana na Assemble Insurance na kuja na bima ya afya ya kijiditali kupitia simu ya mkononi iitwayo AfyaPass ambayo ni rahisi, nafuu, na inapatikana kwa Mtanzania popote pale alipo nchini. Bima hii inapatikana kwa bei nafuu ya Shilingi 70,000 kwa mwaka kwa mtu mmoja na vifurushi vya familia kutoka TZS 105,000 kwa watu wawili hadi TZS 385,000 kwa watu sita kwa mwaka na inapokelewa katika hospitali binafsi na za serikali. Kwa malipo kidogo ya nyongeza, mtumiaji anaweza kupata huduma za uzazi, radiolojia, mazoezi tib ana nyingine nyingi.

Unaweza kujiunga na AfyaPass kupitia M-Pesa ikiwa ni moja ya aina za bima zinazotolewa kupitia VodaBima yenye lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa kila mtu bila kujali kipato chake au umbali wa eneo anapotoka nchini Tanzania.
Kamishna wa Bima kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dk. Baghayo Saqware (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa M-Pesa, Epimack Mbeteni (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Assemble Insurance, Tabia Massudi (kushoto) wakiwa na vipeperushi kuashiria uzinduzi wa kampeni ya “VodaBima kidigitali, Ni Chap, ni Nafuu” inayohamasisha matumizi ya Bima Kidigitali uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kampuni ya Vodacom Tanzania kupitia huduma zake za VODABIMA zinazopatikana kwa M-Pesa, itanufaisha wagonjwa wa kulazwa na kutwa, vyombo vya moto na bima ya maisha kwa mtu mmoja mmoja na vikundi kwa gharama nafuu.
Tanzania Breweries Limited (TBL), one of Tanzania’s top manufacturers and employers and a key partner in the socio-economic development of the country, has today signed a Memorandum of Understanding (MoU) with the CRDB Bank Foundation to collaboratively implement the Barley Farming Pre-financing Seed Capital Scheme.

This collaboration, rooted in TBL's Smart Agriculture Initiative, represents a key milestone in the company's efforts to promote sustainable farming practices and empower local communities across Tanzania.

The TBL’s Smart Agriculture Initiative aims to equip 100% of its direct farmers by 2025, ensuring they are skilled, connected, and financially empowered. By focusing on cultivating sorghum, barley, and grapes, which are essential resources for TBL's operations, the initiative directly supports farmers in enhancing productivity and leveraging natural resources efficiently.
With excitement for the collaboration, Michelle Kilpin, Tanzania Breweries Limited Managing Director, said: “By combining the efforts of both TBL and CRDB Bank Foundation, the partnership aims to significantly boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers in Tanzania.

I believe our partnership is a good example of how collaboration can play a positive role in bringing about positive change and creating value for various stakeholders. Having reached this milestone today, we are confident that it will be the catalyst for similar activities across the country, and we believe that this initiative will be an inspiration to others.”
Through this alliance with the CRDB Bank Foundation, TBL seeks to integrate financially empowered criteria into its smart agriculture framework, enabling farmers to adopt sustainable practices that promote environmental stewardship and reduce reliance on chemical inputs.

This partnership underscores TBL's broader commitment to achieving the United Nations Sustainable Development Goals, particularly SDG 2, which emphasizes achieving zero hunger; SDG 12, for responsible consumption and production; SDG 13, for climate action; and SDG 17, to enhance partnership for the goals.

The Foundation’s initiative, named the iMbeju program, aims to boost the barley sector and enhance the economic welfare of small-holder farmers across Manyara, Karatu, and Monduli Districts for the 2024 agriculture season. The TBL and CRDB Bank Foundation aspire to drive long-term sustainability and resilience in the agriculture sector.
The CRDB Bank Foundation Managing Director, Ms. Tully Esther Mwambapa, says the iMbeju program has been on the market for almost a year now and has attracted a huge number of youth and women, its primary target. To date, she says that the program, which involves financial literacy training and the provision of seed capital, has trained around 250,000 women and offered seed capital to the tune of TZS 5 billion.

“We both seek to enhance sustainable agricultural practices through empowering our farmers. Once farmers are financially stable, production will more than double in all key produce, stabilize our food safety, and increase surpluses for local trading and export. This will have a positive impact on our GDP, where agriculture contributes a lion’s share,” she narrated.
Under this affiliation, farmers will have timely access to agricultural inputs, be exposed to smart technology utilization, and receive comprehensive training, all of which are going to boost yields and improve incomes for farming families.

Furthermore, the effort fosters economic growth and rural prosperity in Tanzania by supporting community development.
Through the collaboration, TBL and the CRDB Bank Foundation will be providing capacity-building programs, seed capital, insurance coverage, the supply of essential agricultural inputs such as fertilizers and agrochemicals, and support for cost-effective harvesting logistics. The goal is not only to boost barley production but also to equip farming communities with the necessary tools and knowledge for sustainable agricultural practices and financial management.
The MoU includes a comprehensive framework for collaboration, detailing roles, responsibilities, and operational mechanisms to ensure the scheme’s success.

TBL and the CRDB Bank Foundation will work together to deliver on commitments around the following:
Community Development: By prioritizing livelihood improvement, the program contributes to broader community development, fostering economic growth, food security, and rural prosperity.

Sustainable Agricultural Practices: By promoting smart agriculture and financially empowering farmers, the program encourages sustainable practices that protect the environment and reduce chemical inputs.
Capacity Building: The partnership facilitates the transfer of financial literacy knowledge and skills to local farmers, empowering them to make informed decisions and adapt to evolving agricultural practices and market demands.

Increased Yields and Incomes: Through timely access to agricultural inputs, smart technology utilization, and training, farmers can enhance productivity, leading to higher yields and improved incomes for their families.
Katika kufungua fursa za kuongeza umahiri katika fani zao, Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative (SUGECO) imesaini mkataba wa miaka mitatu kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

Akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa taasisi yake imekuwa ikitekeleza Program ya Imbeju inayotoa mafunzo ya ujasiriamali pamoja na mtaji wezeshi kwa vijana na wanawake.
Tangu walipofungua dirisha la maombi mwaka mmoja uliopita, vijana 709 walijitokeza na kati yao, asilimia 40 kati yao walitoka katika sekta ya kilimo ambayo inaongoza kwa kuliingizia taifa fedha za kigeni huku ikilihakikishia taifa chakula cha kutosha kwa mwaka mzima.

Kwa kushirikiana na wabia, Tully amesema kilimo kinapewa msisitizo zaidi kwa kutambua mchango wake katika kuliingizia taifa fedha za kigeni, kutoa ajira kwa Watanzania pamoja na kuihakikishia Tanzania usalama wa chakula.
“SUGECO ni mbia wetu mpya katika uwezeshaji wa vijana hasa wanaojihusisha na kilimo. Kwa kutambua umuhimu wa mafunzo kwa vitendo katikakuwajengea uwezo vijana, CRDB Bank Foundation imetenga Euro milioni 24 sawa na Shilingi bilioni 67 kwa ajili ya programu hii zitakazotolewa ndani ya miaka mitatu ya ushirikiano wetu na SUGECO ili kuwaandaa vijana mahiri watakaoajiria au kujiajiri kwenye sekta ya kilimo,” amesema Tully.

Tangu kuanzishwa kwake, SUGECO huwapeleka nje ya nchi wahitimu wa SUA hasa katika mataifa ya Ulaya, Amerika na Asia ambako hujifunza namna nzuri ya kufanya kilimo chenye tija lakini mchakato huo huhitaji fedha za awali kumwezesha mhitimu husika kujiandaa ipasavyo.

Kwa mwaka huu wa kwanza, Tully amesema wanatarajia kuwawezesha zaidi ya wahitimu 2,500 kwa kati ya dola 3,500 za Marekani (shilingi milioni 8.7) mpaka dola 4,500 (shilingi milioni 11.29) zinazotosha kwa mahitaji yao yanayojumuisha gharama za pasi ya kusafiria, visa pamoja na fedha ya kujikimu kabla ya kuanza kulipwa huko waendako.

“Mpango wa uwezeshaji baada ya mafunzo pia umeshaandaliwa kwa kushirikiana na SUGECO pamoja na USAID kwa kutenga maeneo maalum ya kuwekeza katika kilimo cha kisasa, na chenye tija zaidi. Taasisi yetu imejipanga kikamilifu pia katika hatua hiyo ya pili ya uwezeshaji kwa kutoa mitaji wezeshi, pamoja kuwapa mafunzo ya ujasirimali,” amesisitiza Tully.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO, Ndugu Revocatus Kimario amesema ushirikiano na Taasisi ya CRDB Bank Foundation utaongeza idadi ya wanufaika kwa kiasi kikubwa kwani mwaka jana waliweza kuwapeleka vijana 500 tu kupata mafunzo hayo kwa vitendo nje ya nchi ili kupata elimu na kujengewa uwezo zaidi katika kilimo, fani ambazo wamezisomea.

“Ushirikiano huu, tunaamini utakuwa na tija kubwa kwani ili ufanye biashara endelevu ni muhimu kuwekeza kwa watu unaowahudumia. Mkataba huu ni kati ya uwekezaji mkubwa kwa Benki ya CRDB kwani si wahitimu peke yao watakaonufaika bali wafanyakazi wao, familia hata ndugu, jamaa na marafiki zao,” amesema Kimario.
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi ya SUGECO naye, Dkt Anna Temu alikumbusha namna walivyouanzisha ushirika huo ambao mpaka sasa umewaneemesha maelfu ya wahitimu wa SUA kwa kuwaongezea maarifa juu elimu waliyoipata darasani.

“Kwa kuwa sisi tunawahudumia zaidi vijana na wanawake, tuliona CRDB Bank Foundation wenye Program ya Imbeju ni wabia muhimu wa kufikisha malengo yetu kwa jamii,” amesema Dkt Anna.
Meneja Mawasiliano (Corporate Communication and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa (wa pili kutoka kushoto) akimkabidhi moja ya vifaa vya kisasa vya kupima ulevi kwa madereva vilivyotolewa na Barrick kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama barabarani kanda maalum ya Dar es Salaam, Mohamed Bahashwan, katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa hivyo kwa Jeshi la Polisi iliyofanyika katika Kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam , wengine pichani ni Kamanda wa Polisi wa Kinondoni SACP Mtatiro Kitinkwi (kushoto) na Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani wa Dar es Salaam SACP William Mkonda.

Na Mwandishi Wetu.

Katika kuendeleza mkakati wa kuhamasisha jamii kuzingatia usalama wakati wote, kampuni ya Barrick kupitia kampeni yake ya ‘Journey to Zero’ imekabidhi Jeshi la Polisi msaada wa vifaa vya kupima ulevi kwa madereva wa vyombo vya moto vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100 katika hafla iliyofanyika katika kituo cha polisi cha Oysterbay kilichopo wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika hafla ya kupokea vifaa hivyo,Kamanda wa Polisi wa kanda ya Kinondoni, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mtatiro Kitinkwi,alisema msaada huyo wa vifaa vya kisasa vya kupima kilevi umetolewa kwa wakati mwafaka ambao Jeshi hilo linaendelea na mikakati ya kukomesha vitendo vya ulevi kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto ambao umekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali nyingi za barabarani zinazotokea nchini.

“Tunawashukuru Barrick kwa kuendelea kuwa wadau wakuu wa kusaidia kampeni za ualama barabarani nchini na sisi tunawahodi kuwa vifaa hivi tutavitumia vizuri ili vifanikishe lengo lililokusudiwa la udhibiti wa madereva kutumia vinywaji vyenye kilevi kupita kiasi”.alisema Kitinkwi.

Alisema Jeshi la Polisi kupitia kikosi chake cha Ualama Barabarani pia litaendelea kutoa elimu ya unywaji kistaarabu kwa madereva wa vyombo vya moto ili kuhakikisha ajali nyingi zinazotokana na ulevi zinatokomezwa nchini na alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizi kwa kuwa suala la usalala linamgusa kila mwananchi.

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa, alisema kuwa msaada huo ni mwendelezo wa kampeni ya Barrick ya Journey to zero ambayo inalenga kuhamasisha afya na usalama kwa wafanyakazi wake na wadau wengine wote kwenye jamii.

“Kampeni yetu ya 'Journey to Zero' inalenga kuhakikisha wafanykazi wote wa kampuni wanakuwa salama wakati wote wanapokuwa kazini hadi wanaporudi nyumbani hivyo tumehakikisha kampeni hii inavuka mipaka hadi nje ya kampuni kuhakikisha jamii nzima inakuwa salama na ndio maana tunaendelea kuunga mkono Serikali kupitia Jeshi la Polisi kupambana na changamoto ya ajali za barabarani.

Mutagahywa alisema Barrick, siku zote itaendelea kuwa mstari wa mbele kushirikiana na wadau mbalimbali kuunga mkono kampeni hizi za usalama barabarani na inaamini vifaa hivi vya kisasa vya kupima kilevi vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Polisi vitasaidia kuwabaini madereva wanaoendesha vyombo vya moto wakiwa wamelewa na kuchukuliwa hatua za kisheria ili kudhibiti na kupunguza matukio ya ajali za barabarani.

Naye Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan, aliishukuru Barrick, kwa kutoa msaada huo na kwa kuwa mdau mkuu wa kusaidia kampeni ya usalama , alitoa rai kwa watumiaji wa vifaa hivyo kuvitunza vizuri ili kuweza kufanikisha malengo mazuri yaliyokusudiwa sambamba na kuwarahisishia kazi, “Katika dunia ya sasa ya matumizi ya teknolojia nina imani vifaa hivi vitarahisisha kazi ya polisi wetu kuwanasa madereva walevi” alisisitiza.
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan akiongea katika hafla hiyo.
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi walipata fursa ya kuongea katika hafla hiyo.
Viongozi wa kamati za usalama barabarani, Jeshi la Polisi na Barrick walipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na wageni waliohudhuria katika hafla hiyo.
MKUU wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga leo mapema akiwa kwenye ziara yake katika Mji mdogo wa Mererani Wilayani Simanjiro, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Naepo iliyopo katika Kata ya Naisinyai kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Aprili 2024 mradi uwe umekamilika na unaanza kufanya kazi.

Zahanati ya Naepo inajengwa kwa fedha kutoka vyanzo mbalimbali ambapo shilingi Mil. 50 ni fedha za mapato ya ndani, Mil. 48 fedha za nguvu za Wananchi na Mil. 20 ni fedha ambazo zimechangiwa na mdau hivyo kufanya jumla ya Shilingi Mil. 118.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya Sokoni Mirerani - Mgodini Tanzanite kilomita 1.2 kwa kiwango cha lami inayotekelezwa na Mkandarasi M/S EMMA & SONS CONTRACTORS LTD. Mradi huu ulitengewa jumla ya shilingi milioni 898 hadi kukamilika. 

Katika hatua nyingine, Mhe. RC Sendiga amemuagiza na kumpa mwezi mmoja Meneja wa TARURA Wilaya ya Simanjiro kusimamia na kuhakisha mradi huo uwe umeshakamilika alipotembelea mradi huo unaotekelezwa kwa fedha za tozo ya mafuta.

Miradi mingine ambayo imetembelewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa ni pamoja na ujenzi wa Soko la madini, mradi unaotekelezwa kwa fedha shilingi Bilioni 5.43 na hadi sasa mradi upo katika asilimia 80 (80%) ya utekelezaji. Mradi mwingine ni ujenzi wa kituo cha Afya cha Tanzanite kilichopo kata ya Mirerani. Mradi huu umetengewa fedha kutoka Serikali kuu shilingi milioni 500 kujenga jengo la wagonywa wa nje (OPD), Maabara na jengo la mama na mtoto. Mradi huu upo katika hatua ya msingi.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (Kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau, aliyefika Ofisini kwa Waziri wa Fedha kwa ajili ya kujitambulisha, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo wamejadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza wakati wa kikao chake na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau, aliyefika Ofisini kwa Waziri wa Fedha kwa ajili ya kujitambulisha, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo wamejadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (watano kushoto) na Balozi Mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chritine Grau (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka Wizara ya Fedha na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini baada ya kikao chao, katika Ofisi Ndogo za Hazina jijini Dar es Salaam, ambapo Balozi huyo alifika kujitambulisha na pia kujadiliana namna ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia misaada ya kibajeti na miradi mingine ya maendeleo.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)

Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameushukuru Umoja wa Ulaya kwa kutenga zaidi ya EURO milioni 703 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika kipindi cha miaka 7 kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka 2027.

Dkt. Nchemba ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi mpya wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Chistine Grau aliyefika kujitambulisha rasmi.

Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa fedha hizo zimegawanywa katika awamu mbili ikiwemo awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka 4 ilitengewa zaidi ya euro milioni 426 ambapo mpaka sasa Umoja huo umetoa zaidi ya euro milioni 373 ambazo zimeelekezwa katika miradi kadhaa ikiwemo uchumi wa buluu, ujenzi wa miji ya kisasa, upatikanaji wa mitaji, utawala wa fedha, upatikanaji wa mitaji kwa sekta binafsi, usawa wa kijinsia na mradi wa kuendeleza masuala ya kidigiti.

Aliiomba EU kuangalia uwezekano wa kutumia sehemu ya fedha, zaidi ya euro milioni 200 zitakazotumika katika awamu ya pili ya program hiyo itakayoanza mwakani kitumike kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya barabara ya kutoka Mikumi hadi Kidatu yenye urefu wa kilometa 35 ili kuchochea uchumi na maendeleo ya wakazi watakaonufaika na barabara hiyo.

Kwa upande wake, Balozi mpya wa Umoja wa Ulaya, Mhe. Christine Grau, alisifu mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea nchini kupitia kwa ungozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya MUungano wa Tanzania, yaliyoifanya Tanzania kuendelea kuwa imara na kuvutia uwekezaji na mitaji kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Aidha, Mhe. Balozi Grau aliarifu kuwa majadiliano ya awali ya ushirikiano mwingine wa miaka 7 unaotarajiwa kuanza mwaka 2028 hadi 2034 yataanza rasmi mwakani 2025.

Mhe. Balozi Grau aliipongeza Tanzania kwa kuridhia na kusaini mkataba mpya wa ushiriakiano kati yake na Umoja huo ujulikanao kama SAMOA ambao pamoja na mambo mengine utaiwezesha Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya kuendelea kufanyakazi zake nchini.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akifafanua kuhusu utaratibu wa kurejesha fedha kwa wamiliki wa maduka ya kubadilisha fedha waliobatilishiwa leseni zao baada ya wenye maduka hayo kukidhi vigezo vya kisheria, bungeni jijini Dodoma.
Peter Haule na Josephine Majura, WF, Dodoma

Serikali imesema kuwa ilibatilisha leseni za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni yaliyokutwa na makosa mbalimbali yakiwemo ya kujihusisha na uhamishaji wa fedha nje ya nchi bila kuwa na leseni wala kibali cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, aliyetaka kufahamu sababu za maduka ya kubadilisha Fedha kuondolewa katika biashara na Wananchi wengi kupoteza ajira zao.

Mhe. Chande alisema kuwa mwaka 2016, Benki Kuu ya Tanzania ilifanya ukaguzi wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni na kugundua miamala mbalimbali kwa baadhi ya maduka inafanyika kinyume na matakwa ya sheria na kanuni za usimamizi wa maduka ya fedha za kigeni na udhibiti wa utakasishaji wa fedha haramu.

“Mwaka 2018 na 2019, Benki Kuu kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za Serikali ilifanya operesheni ya ukaguzi maalum kwenye maduka yote ya kubadilisha fedha za kigeni nchini na kubaini makosa mbalimbali yaliyosababisha Serikali kusitisha leseni kwa waliokiuka Sheria kwa mujibu wa Kanuni ya 36 (1)(b) na 2 (d) ya Kanuni za Biashara ya Kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015 iliyorejewa mwaka 2019 ”, alisema Mhe. Chande.

Mhe. Chande alisema kuwa makosa mengine yaliyobainika ni pamoja na kutofanya utambuzi wa wateja kabla ya kutoa huduma kinyume na kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Udhibiti wa Utakasishaji Fedha Haramu, Sura 423 na kanuni ya 17 ya Kanuni za Udhibiti wa Utakasishaji Fedha Haramu.

Aidha alisema kuwa kosa lingine lilikuwa kugawa miamala ya wateja kwa lengo la kukwepa kutunza kumbukumbu muhimu zinazoonyesha uhalali wa miamala kinyume na Kanuni ya 23 ya Kanuni za Biashara ya kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015 na kutokutoa stakabadhi za miamala kinyume na Kanuni ya 23(1) ya Kanuni za Biashara ya Kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2015

Mhe. Chande alibainisha makosa mengine kuwa ni pamoja na kutokuwasilisha taarifa sahihi za miamala Benki Kuu na hivyo kuathiri upatikanaji wa takwimu muhimu kwa ajili ya sughuli za kiuchumi na baadhi ya maduka yalikuwa yanajihusisha na uhamishaji wa fedha nje ya nchi bila kuwa na leseni wala kibali cha Benki Kuu.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, aliyetaka kufahamu sababu za maduka ya kubadilisha Fedha kuondolewa katika biashara na wananchi wengi kupoteza ajira zao. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Fedha)
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Asasi za Kifedha Tanzania (TAMFI) limesema lina programu maalumu ya kuchangia uhifadhi wa mazingira na kupambana na ukataji miti kwa kuwezesha nishati safi ya kupikia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry katika kongamano la Wanawake katika fedha:Kukumbatia mabadiliko ya tabia nchi lililofanyika mwishoni mwa wiki.
Alisema katika kongamano hilo lenye nia ya kuchanganya jinsia na uendelevu wa mazingira ndani ya sekta ya fedha, kuwa kuna haja kwa wadau kama wao kuchukua hatua na kuunga mkono juhudi za serikali kukabili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwezesha wanawake nishati safi ya

"Ahadi yetu ya 'Kukumbatia Mabadiliko ya Tabianchi' inazidi mjadala tu; ni wito wa kuchukua hatua. Kwa kulingana na maono ya serikali ya ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, tunalenga kushughulikia vipengele muhimu vya maji, nishati mbadala, na mabadiliko ya tabianchi na kujitolea kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu namba kumi na nne (14)" alisema Winnie.

Mkutano huo uliopata ufadhili kutoka Foundation ya Charles Stewart Mott uliweka wazi ushawishi muhimu wa taasisi za kifedha kuwezesha wanawake ndani ya sekta ya fedha kuongoza mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.
Mwenyekiti wa Bodi ya TAMFI, Devotha Ntuke Minzi alisema ni jukumu la wanawake kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.

Akisisitiza athari zisizo sawa za mabadiliko ya tabianchi kwa wanawake, hasa nchini Tanzania na kote duniani, Minzi alitaka ushirikishi katika kufanya maamuzi na kutekeleza mipango kwa vitendo. Alihimiza haja ya kuongeza sauti za wanawake katika fedha kama waendeshaji muhimu wa suluhisho endelevu kwa changamoto hizi za kimataifa.

Naye Ofisa Programu wa TAMFI, Deodati Bernard alielezea mchango mkubwa wa wanawake kwa maendeleo ya Tanzania.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa wanawake na Wakurugenzi Mtendaji kutoka Taasisi za Fedha za Daraja la Kwanza na la Pili, pamoja na wajumbe kutoka Chama cha Benki Tanzania (TBA), Chama cha Nishati Mbadala Tanzania (TAREA), Mtandao wa Maji na Usafi Tanzania (TaWaSanet), New Faces New Voices (NFNV), Amshaamsha Foundation, IMED Foundation, Elico Foundation, Water.org, Kampuni ya Huduma za Nishati Endelevu (SESCOM) na wanawake katika nyanja mbalimbali za mfumo wa mabadiliko ya tabianchi nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Philip Besiimire (Kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Abdulmajid Nsekela, wakipiga makofi mara baada ya kuzindua ushirikiano kati ya taasisi hizo unaoenda kuwezesha upatikanaji wa simujanja kwa mkopo ili kuchochea matumizi ya intaneti na ukuaji wa uchumi wa kidijiti nchini. Kulia kwa Besiimire ni Mkurugenzi wa Biashara wa Vodacom Bi. Linda Riwa na kushoto kwa Nsekela ni Afisa Biashara Mkuu wa benki hiyo Bw. Boma Raballa.
Dar es Salaam - Machi 27, 2024. Katika jitihada za kuongeza upatikanaji na matumizi ya simu janja ili kuziba pengo la kidijitali nchini, makampuni ya Vodacom Tanzania PLC na Benki ya CRDB wamezindua mpango wa kuwezesha Wateja wao kumiliki simujanja zenye ubora kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo wa kukopesha simu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire, alieleza kuwa kampuni hiyo ya simu inatekeleza mipango mbalimbali ya kupunguza gharama za vifaa vya mawasiliano ili kuwawezesha wateja wake kuhama kutoka kwenye matumizi ya mtandao wa 2G na kumiliki simu zenye uwezo wa 4G na kutumia fursa hiyo ili kunufaika na faida kemkem zinazopatikana kupitia mtandao huo.

"Tukiwa ni mdau na mshirika mkubwa wa sekta ya mawasiliano na teknolojia, Vodacom tunajivunia kuzindua mpango huu na Benki ya CRDB ambayo ni taasisi kubwa ya fedha nchini. Ushirikiano wetu unalenga kuwawezesha wateja kutoka pande zote mbili kupata aina mbalimbali za simujanja kwa bei nafuu na mpango wa malipo kwa awamu kwa kipindi fulani. Ili kujua kama amekidhi vigezo, mteja atatakiwa kupiga *150*00*44# nbaada ya hapo atafanya malipo ya awali na kupewa simujanja. Mkopo huu unaweza kulipwa kwa siku, kwa wiki au kwa mwezi kwa kipindi cha hadi miezi 12 kupitia M-Pesa," alifafanua bwana Besiimire.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema, “ushirikiano huu baina yetu na Vodacom ni fursa nzuri kwa Watanzania kupata huduma za kifedha na mawasiliano kwa gharama nafuu. Kwa hiyo kama wadau muhimu tunapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuhakikisha wananchi wake wanafaidika na ukuaji na maendeleo katika sekta hizi.”

Bwana Nsekela aliongeza kuwa, “Kwa mtandao wetu ulioenea nchi nzima, CRDB tumekuwa na mchango muhimu katika maendeleo ya Watanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha. Hivyo basi, kwa kushirikiana na Vodacom, tutaweza kutoa mchango wetu ili kuongeza matumizi ya simujanja nchini.”

Licha ya juhudi za mamlaka nchini kusogeza huduma za mawasiliano, wananchi wengi bado wanatumia huduma za mtandao wa 2G. Hii inapunguza upatikanaji wa fursa zilizopo mtandaoni pamoja na kufurahia na kunufaika na intaneti yenye kasi zaidi kutoka Vodacom pamoja na bidhaa nyingine za kidijitali.

Matumizi ya simujanja na intaneti yana faida kwa jamii kama vile kukuza ukuaji wa kiuchumi kwa kuwezesha ujasiriamali wa kidijitali na kuchochea uvumbuzi, utafutaji masoko mitandaoni pamoja na kuongeza kipato kwa wananchi wanaoamua kujiajili kupitia dijitali.
Vodacom Tanzania imekuwa ikishirikiana na watengenezaji mbalimbali wa simu za mkononi na taasisi za kifedha ili kuwezesha Watanzania kumiliki simu kupitia mikopo nafuu na mipango rafiki ya malipo kwa mteja.

Mwezi August 2020, Vodacom ilizindua programu ambayo inawaruhusu wateja wake kumiliki simujanja kupitia mkopo unaolipwa kwa awamu, huku kianzio kikiwa ni Shilingi 20,000 za Kitanzania kwa muda wa miezi 12.

Bwana Nsekela alimalizia kwamba anaamini kuwa taasisi hizo mbili zina huduma mbalimbali za kibunifu ambazo zitawanufaisha na kuboresha maisha ya wateja wao. Pia alitoa wito kwa Watanzania wanaotumia simu za kawaida na wanataka zenye ubora zaidi kufika katika maduka ya Vodacom na kupata simujanja kwa bei nafuu ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa kidijitali duniani.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba (kushoto) akimkabidhi leseni ya kuongezewa muda wa uchimbaji wa mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido katika hafla hiyo , wanaoshuhudia nyuma (kushoto) ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha. Leseni hii mpya iliyotolewa ni ya kipindi cha miaka 27.
---
Serikali kupitia Wizara ya Madini imeongeza muda wa leseni ya uchimbaji wa dhahabu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, uliopo katika wilaya za Kahama na Nyang’hwale mkoani Shinyanga kwa kipindi cha miaka 27 kuanzia mwaka huu.

Hafla ya kukabidhi leseni hiyo ilifanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Maofisa waandamizi kutoka Wizara ya madini, Wakuu wa mikoa ya Tanga na Shinyanga na wadau mbalimbali kutoka sekta ya madini ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde.

Aliyekabidhi leseni hiyo ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, na Mwakilishi wa Barrick, aliyepokea leseni hiyo kwa niaba ya kampuni ni Meneja wa Barrick Tanzania, Melkiory Ngido.

Mgodi wa Bulyanhulu tangu uanze kuendeshwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals, umefanikisha kuleta mafanikio chanya katika kukuza uchumi wa nchi ,kuongeza fursa za ajira sambamba na kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii kupitia fedha za uwajibikaji wa jamii (CSR) ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi katika maeneo yanayozunguka mgodi huo hususani katika sekta ya afya na elimu.
Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kushoto) katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa makampuni ya uchimbaji wa madini waliokabidhiwa leseni katika hafla hiyo.

Maofisa Waandamizi wa Barrick waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu.

Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita wakati wa hafla hiyo.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Antony Mavunde katika hafla hiyo.