

Dar es Salaam Desemba 24 2025: Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam limetangaza kuwa Kardinali Mstaafu wa Jimbo hilo, Kardinali Polycarp Pengo, anakabiliwa na changamoto za kiafya na anatarajiwa kusafiri kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu zaidi.Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Askofu Thaddaeus S. Ruwa’ichi OFMCap, Kardinali Pengo amekuwa akipatiwa matibabu nchini kwa muda, hata hivyo hali yake imehitaji huduma za kitaalamu zaidi zitakazopatikana nje ya nchi.
“Baada ya juhudi za kimatibabu hapa nyumbani, imeonekana kuwa kuna haja ya kumpa matibabu ya hali ya juu zaidi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa Desemba 24, 2025.
Kanisa limeeleza kuwa mipango yote ya safari na matibabu imekamilika, na kwamba Kardinali Pengo atasafiri kwenda India kwa lengo la kupata huduma bora zitakazomsaidia kurejea katika hali njema ya afya.
Aidha, waumini na watu wote wenye mapenzi mema wametakiwa kuendelea kumuombea Kardinali Pengo ili Mungu amjalie nafuu ya haraka na kumrejesha salama nchini.
Katika taarifa hiyo, Askofu Mkuu pia ametumia nafasi hiyo kuwatakia waumini wote Heri ya Krismasi na Baraka za Mwaka Mpya 2026, akisisitiza umuhimu wa mshikamano na sala katika kipindi hiki.
Taarifa hiyo imesainiwa na Askofu Thaddaeus S. Ruwa’ichi OFMCap pamoja na Katibu Mkuu wa Jimbo, Padre Vincent Mjwaji.

Iringa, Septemba 30, 2025: Kanisa Katoliki Jimbo la Mafinga limeweka wazi sintofahamu kuhusu Padre Jordan Kibiki, aliyeripotiwa kujiteka wiki iliyopita, na kufafanua kuwa tukio hilo lilitokana na changamoto ya afya ya akili, hususan msongo wa mawazo.Kwa mujibu wa taarifa ya Kanisa hilo, Jeshi la Polisi limefuta tuhuma dhidi ya Padre Kibiki na kumwachia huru baada ya uchunguzi kuthibitisha ukweli huo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Askofu wa Jimbo la Mafinga, Mhashamu Vicent Mwagala, alisema Padre Kibiki ambaye ni Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Nyololo na Paroko Msaidizi wa Parokia hiyo, alitarajiwa Septemba 18, 2025 kuhudhuria kikao cha afya katika ofisi za Halmashauri ya Mufindi, lakini hakuwasili licha ya kuondoka nyumbani asubuhi.
Askofu Mwagala alieleza kuwa gari lake lilipatikana limeegeshwa barabarani bila dereva na juhudi za kumpata ziligonga mwamba, hali iliyosababisha hofu kubwa miongoni mwa waumini na viongozi wenzake.
Kwa mujibu wa maelezo ya Polisi, Padre Kibiki alikiri kujitenga kutokana na msongo wa mawazo uliosababishwa na shinikizo la kifedha baada ya kupoteza fedha alizokuwa amekopa kwenye biashara ya mtandao (online scam).
“Baada ya uchunguzi wa kitabibu, madaktari walithibitisha kuwa Padre Kibiki alikuwa anakabiliwa na depression. Kwa ushauri wa wataalamu, amepelekwa Hospitali ya Rufaa ya Tosamaganga kwa uangalizi wa karibu na matibabu ya afya ya akili,” alisema Askofu Mwagala.
Aliongeza kuwa Jimbo la Mafinga linaendelea kufuatilia afya ya Padre Kibiki ili aweze kurejea katika hali ya kawaida na kuendelea na majukumu yake ya kiroho.
“Tunawaomba waumini na jamii kwa ujumla waendelee kumwombea Padre Jordan ili apone haraka,” alisema, huku akilishukuru Jeshi la Polisi na vyombo vya habari kwa ushirikiano katika kipindi hicho kigumu.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO, 2023), msongo wa mawazo ni moja ya changamoto kubwa za kiafya duniani, na unaweza kumpata mtu yeyote bila kujali nafasi, kazi au wito wake wa kidini.
Baada ya miaka ya utumishi wa kichungaji, alijiunga na Shule ya Kidiplomasia ya Vatican (Pontifical Ecclesiastical Academy), ambapo alifundishwa masuala ya kidiplomasia na sheria za kanisa.
Mnamo 1991, alianza rasmi kutumikia Huduma ya Kidiplomasia ya Vatican, akihudumu katika balozi mbalimbali za kitume duniani, ikiwemo Sudan, Turkey, Pakistan, na Indonesia.
Mwaka 2010, Papa Benedict XVI alimteua kuwa Askofu Mkuu na Balozi wa Vatican (Apostolic Nuncio) nchini Angola na Sao Tome and Principe. Baadaye alihamishiwa Honduras (2015), kisha New Zealand, Fiji, Tonga na Samoa (2019).
Mbali na jukumu la kidiplomasia, Askofu Mkuu Rugambwa alikuwa pia mjumbe wa kudumu wa Vatican katika mashirika mbalimbali ya kimataifa.
Kote alikopita, alijulikana kwa unyenyekevu wake, hekima ya kidiplomasia na moyo wa upendo, uliomfanya kuwa daraja kati ya Vatican, makanisa ya eneo husika na serikali.
Urithi wake
Kifo cha Askofu Mkuu Rugambwa kimeacha pengo kubwa, lakini mchango wake katika Kanisa na katika kuliletea taifa heshima kwenye meza ya kidiplomasia ya kimataifa utabaki kuwa sehemu ya urithi wake.

























.jpg)






