Articles by "DINI"
Showing posts with label DINI. Show all posts
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akiwa kwenye futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhamani akizungumza katika halfa hiyo
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akitunzwa baada ya kusoma Quarn Tukufu katika halfa hiyo.
Na Oscar Assenga, PANGANI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu mkoa huo umepokea fedha kiasi cha Sh.Trilioni 2.6 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Balozi Batilda aliyasema hayo wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyokwenda sambamba na Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji Jumaa Aweso iliyofanyika wilayani Pangani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali,Chama na Taasisi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa maji Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji,Mkurugenzi wa Ruwasa na wataalamu mwengine.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo likiwemo Daraja la Mto Pangani na Barabara ya Pangani pamoja na mengine ikiwemo ya elimu ambapo wanamshukuru Rais kwa ujenzi wa mabweni ya watoto wenye mahitaji maalumu yamejengwa, zahanati, nyumba za walimu na miradi ipo mingi kazi kubwa imefanywa.

“Katika hili tunamshukuru sana Mh Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutuletea fedha hizi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini namshukuru kwa imani kubwa kwangu ninahaidi sitamuangusha nitajitahidi kwa ushirikiano wenu na dua zengu niweze kutimiza yale ambayo anakusudia nitimize nikiwa hapa Tanga” Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwamba wataendelea kuhakkikisha fedha zinazokuja zinatekeleza kazi iliyokusudiwa na sio vyenginevyo pamoja na usimamizi mzuri katika miradi inayotekeleza ili iweze kuleta tija inayotakiwa.

“Nimshukuru Waziri Aweso amefanya jambo kubwa na ameendelea kufanya mambo mengi kwenye Sekta ya Maji nimetoka Tabora kwenye miradi 28 nasi tulikuwa tunanufaika nimekuja hapa Tanga nimeambiwa napo ipo ni kijana mdogo lakini mwenye hekima, hofu ya mungu, mchapakazi “Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwa hakika dhamana aliyopewa na Rais Dkt Samia Suluhu kuhakikisha anawatua wakina mama ndoo kichwani ameitekeleza vizuri kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara maji wanaendelea na kazi nzuri.

Akizungumzia suala la mabadiliko ya tabia ya nchi hasa kwenye wilaya ya Pangani RC Balozi Batilda alisema wilaya hiyo ni moja ya maeneo yaliyoathirika na kuna maeneo yakichimbwa visima kuna maji ya chumvi ndio maana kwenye mradi wa maji ya miji 28 na wao wamepelekewa na maeneo watachimba visima ili wananchi waweze kunufaika kwa kupata maji safi na salama.

Akizungumzia suala la uvuvi RC huyo alisema suala hilo katika mkoa huo ni moja ya maeneo ya uvuvi hivyo suala la maboti na vifaa vya uvuvi vitaendelea kupatikana kwenye mji wa Pangani na maeneo mengine.

“Tunapozungumzia masuala ya mazingira niwape kongole Pangani mazingira mmeendelea kuyatuza na msitu wenu wa asili unapendeleza”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema katika moja ya kuendeleza ukwekezaji Serikali kupitia Wizara Madini ilisaini mkataba na wawekezaji wa madini ya Ndovu au tembo ambayo yatachimbwa kwenye Mwambao wa Pangani karibu kilomita 15 ya ufukwe.

Alisema walichowaambia wahakikisha hawawanyi ruhusu ya wavuvi kutumia mwambao huo na matumbawe hayatavurugwa ikiwemo mikoko iliyopo wakati wanaendelea kunufaika na mradi huo na kuendelea na uvuvi,matango pori yote kuhakikisha wanakuwa na shughuli mbalimbali zinaendelea.

Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa wa Tanga ndio ambao kila kitu kinaweza kuota hivyo lazima wahakikishe utajiri huo unawanufaisha wananchi wao wote kwa kuhakikisha wanachangamkia fursa zilizopo.

“Katika ujenzi wa bomba la mafuta litapita kwenye wilaya kadhaa tunataka wana tanga wanufaike na miradi hiyo na kazi yake katiba tawala na wakuu wa wilaya na makatibu tawala ni kuwawezesha wananchu kuona fursa za uwepo wa mradi huo ili waweze kuchangamkia fursa hizo”Alisema RC Balozi Batilda ,

Awali akizungumza katika futari hiyo Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew alisema kwamba maadili mema ambayo tumeyaonyesha katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani tuendelee kuifanya na kufanya ibada ndio tunaweza kuwaponya wengi na kujiponya na sisi.

Mhandisi Mathew alisema pia waendelee kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu ili aendelea kuifanya kazi nzuri anaoendelea kuifanya na kuhakikisha wanashirikiana na Mbunge wao na kamwe wasimwangushe .

“Nataka kuwaambie wana Pangani “Dhahabu ya Pangani tunaijua wana Pangani na Dhahabu ya Tanzania tunaijua na tusije kudanganyika na kuachia dharabu hii na kwenda kuokota mawe”Alisema

Hata hivyo alimshukuru Waziri Aweso kwa jambo kubwa alilolifanya kwa wananchi wake kutokana na uwepo wa umoja na mshikamano kwa wananchi wake ambao wameitika kwa wingi kwenye tukio hilo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema safari ya kuifungua pangani kimaendeleo itafanywa na wana Pangani wenyewe na mimi ni miongoni mwa watu walishawishika na Waziri Aweso kipindi kile kwa maneno yake kwa dhamira iliyojificha ndani ya moyo wake akanitamkia ya kutaka kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo.

Alisema kwa sasa tunayaona maendeleo makubwa sana kwenye Jimbo la Pangani ikiwemo ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani –Saadani ambayo itaifungua wilaya hiyo pamoja na uwepo wa miradi ya maji ambayo awali wananchi walikuwa wakiifuata umbali mrefu.
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Asasi za Kifedha Tanzania (TAMFI) limesema lina programu maalumu ya kuchangia uhifadhi wa mazingira na kupambana na ukataji miti kwa kuwezesha nishati safi ya kupikia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMFI, Winnie Terry katika kongamano la Wanawake katika fedha:Kukumbatia mabadiliko ya tabia nchi lililofanyika mwishoni mwa wiki.
Alisema katika kongamano hilo lenye nia ya kuchanganya jinsia na uendelevu wa mazingira ndani ya sekta ya fedha, kuwa kuna haja kwa wadau kama wao kuchukua hatua na kuunga mkono juhudi za serikali kukabili mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwezesha wanawake nishati safi ya

"Ahadi yetu ya 'Kukumbatia Mabadiliko ya Tabianchi' inazidi mjadala tu; ni wito wa kuchukua hatua. Kwa kulingana na maono ya serikali ya ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, tunalenga kushughulikia vipengele muhimu vya maji, nishati mbadala, na mabadiliko ya tabianchi na kujitolea kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu namba kumi na nne (14)" alisema Winnie.

Mkutano huo uliopata ufadhili kutoka Foundation ya Charles Stewart Mott uliweka wazi ushawishi muhimu wa taasisi za kifedha kuwezesha wanawake ndani ya sekta ya fedha kuongoza mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.
Mwenyekiti wa Bodi ya TAMFI, Devotha Ntuke Minzi alisema ni jukumu la wanawake kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.

Akisisitiza athari zisizo sawa za mabadiliko ya tabianchi kwa wanawake, hasa nchini Tanzania na kote duniani, Minzi alitaka ushirikishi katika kufanya maamuzi na kutekeleza mipango kwa vitendo. Alihimiza haja ya kuongeza sauti za wanawake katika fedha kama waendeshaji muhimu wa suluhisho endelevu kwa changamoto hizi za kimataifa.

Naye Ofisa Programu wa TAMFI, Deodati Bernard alielezea mchango mkubwa wa wanawake kwa maendeleo ya Tanzania.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa wanawake na Wakurugenzi Mtendaji kutoka Taasisi za Fedha za Daraja la Kwanza na la Pili, pamoja na wajumbe kutoka Chama cha Benki Tanzania (TBA), Chama cha Nishati Mbadala Tanzania (TAREA), Mtandao wa Maji na Usafi Tanzania (TaWaSanet), New Faces New Voices (NFNV), Amshaamsha Foundation, IMED Foundation, Elico Foundation, Water.org, Kampuni ya Huduma za Nishati Endelevu (SESCOM) na wanawake katika nyanja mbalimbali za mfumo wa mabadiliko ya tabianchi nchini.
WAUMINI wa Kanisa la Baptist Kinondoni mkoani Dar es Salaam wakiongozwa na Mchungaji wa kanisa hilo Samweli Kabonaki wamefanya ibada maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi cha majanga yakiwemo mafuriko yanayosababishwa na vua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalmbli za nchi yetu na nchi jirani.Akizungumza wakati wa ibada hiyo ,Mchungaji Kabonaki amesema Watanzania na Dunia wanajua kipindi wanachopitia kutokana na uwepo wa majnga yanayoleta madhara katika maeo mbalimbali ya nchini na nje ya nchi."Tumeona ni vema Kanisa hilo likafanya maombi maalum kuombea nchi yetu na mataifa mengine na duna kiujumla,"amesema na kusisitiza katika kukabiliana na majanga hayo ni vema kila mmoja wetu akamtanguliza Mungu zaidi na yvema ikajulikana Mungu ambaye ndiye mwenye majibu yote na ni mponyaji Mkuu."









Ibaada ikiendelea


Waimbaji wa kwaya ya Shalom wakiimba wakati wa ibaada ya maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi hiki cha majanga mbalimbali leo Mkoa wa Dar es Salaam.



















Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Jaffari Matundu, akizungumza na wadau (hawapo pichani) katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya benki na wadau wake wakiwemo wateja na jamii katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akitoa pongezi kwa Benki ya Exim kwa kuandaa Iftar akielezea namna ambavyo imewaleta pamoja waumini wa dini ya kiislam kama ishara ya upendo, umoja na heshima kwa wadau wote katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim, Jaffari Matundu (wa tatu kutoka kushoto) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar (watatu kutoka kulia) wakiwa na baadhi ya viongozi wa Exim Bank wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Wadau mbalimbali na wawakilishi wa Benki ya Exim wakifurahia Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwaleta pamoja katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani kuashiria furaha, umoja, na upendo katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omar (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Exim Bank, Jaffari Matundu (watatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa benki hiyo wakati wa hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwakutanisha wateja wake pamoja katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani iliyofanyika tarehe 15 meezi Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
---
(Dar es Salaam, Machi 15 2024). Benki ya Exim imeandaa futari ya pamoja kwa wateja wake katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 15 mwezi Machi 2024.

Mgeni Rasmi katika tukio hili alikuwa Sheikh Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akiwakilisha waumini wa dini ya Kiislam ambao wapo kwenye mfungo katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza katika hafla hiyo, Sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, aliipongeza Benki ya Exim kwa juhudi zake katika kukuza maendeleo ya kijamii na kueleza shukrani zake kwa mchango wa benki hiyo kwa jamii. Alisema, “Benki ya Exim inaonyesha dhamira ya kweli katika kutumikia wateja wake na jamii kwa ujumla, lengo kuu la Ramadhani ni kuleta watu pamoja, na usiku huu, benki ya Exim imehakikisha kuendeleza lengo hilo kwa vitendo”.

Bwana Jaffari Matundu, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim, aliwakaribisha wadau wote katika Iftar hiyo huku akitambua mahusiano mazuri ya tija yaliopo baina ya Benki ya Exim na wateja wake na umuhimu wa kuyaendeleza kwa ajli ya ustawi na maendeleo ya jamii.

“Wateja wetu ni zaidi ya wateja tu, ni sehemu muhimu ya familia yetu. Tunaona kila mmoja wenu kama mshirika na mwenzetu katika safari yetu ya mafanikio”, alisisitiza Jaffari Matundu.

Pia, Mkurugenzi huyo alizungumzia hatua na maboresho mbalimbali ambayo yamefanywa na benki ya Exim ili kuendana na mabadiliko katika sekta mbalimbali ikiwemo maendeleo ya teknolojia ya kidijitali na kusogeza huduma kwa wateja.

Jaffari alifafanua kuwa, “tumefanya maboresho makubwa katika mfumo wetu wa Benki ili kuendelea kuhudumia wateja wetu vizuri zaidi kwa kutoa huduma zinazoendana na mabadiliko ya kidigitali”.

“Vile vile tumeendelea kuongeza idadi ya Mawakala wetu (maarufu kama Exim Wakala) ili kuleta huduma zetu karibu na wateja wetu popote walipo”, alimalizia Afisa Mtendaji Mkuu huyo.

Exim Bank pia imeboresha huduma za kidijitali kwa wateja wake ambapo wanaweza kupata huduma za kibenki popote pale walipo ndani na nje ya Tanzania. Hii ni kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki kwa wateja wao na maendeleo ya teknolojia yanayoendelea kutokea duniani.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC inashiriki katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Utaratibu huu wa kushiriki katika maonesho mbalimbali nchini ni sehemu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kutoa elimu ya Mpiga Kura endelevu ambapo wadau mbalimbali wa Tume hufika katika Banda hilo na kupata elimu hiyo.

Maonesho haya ambayo huandaliwa na Mahakama ya Tanzania ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya sheria na kuanza kwa mwaka mpya wa Mahakama.

Mwaka huu maonesho haya yamebeba kauli mbiu isemayo "Umuhimu wa Dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa:Nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha mfumo Jumuishi wa Haki Jinai" yameanza tarehe 24 Januari,2024 na yanatarajia kumalizika tarehe 30 Januari, 2024.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Cuthbert Mapunda (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Cuthbert Mapunda (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.
Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bi.Neseria Leng’ida (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma
Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakiwa katika banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayoendelea jijini Dodoma katika viwanja vya Nyerere Square.

Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakizungumza na mdau aliyetembelea banda la Tume katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma

Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakizungumza na mdau aliyetembelea banda la Tume katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Loshilu Saning’o (Kulia) akizungumza na mdau wa Uchaguzi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea jijini Dodoma.
Unguja. Tarehe 10 Septemba 2023: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt Hussein Ali Mwinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuanzisha huduma za kibenki zinazofuata misingi ya sharia hivyo kuwahamasisha Waislamu wengi kutumia huduma zake jambo linalochochea ujumuishi wa kifedha.

Rais Mwinyi ambaye alikuwa mteja wa kwanza kufungua akaunti ya Al Barakah mwishoni mwa mwaka 2021 huduma hiyo ilipozinduliwa, ametoa pongezi hizo alipokabidhiwa kadi ya akaunti hiyo mwishoni mwa wiki alipotembelewa na ujumbe wa Benki ya CRDB ikulu mjini Zanzibar.
“Tulijua Al Barakah itakuwa na mafanikio lakini hatukutarajia kuwa yangepatikana ndani ya muda mfupi namna hii. Nawapongeza kwa mafanikio mliyoyapata na niwaahidi kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendeleza ushirikiano na benki yenu kuhakikisha huduma hizi zinawafikia Waislamu wengi walipo visiwani humu ili kwa Pamoja tushiriki kulijenga Taifa letu huku tukimwabudu Mwenyezi Mungu bila kukiuka maagizo yake,” amesema Dkt Mwinyi.

Rais Mwinyi pia ameishukuru Benki ya CRDB kwa heshima iliyompa ya kuwa mteja wa kwanza kukabidhiwa kadi ya Akaunti ya Al Barakah na akasema jambo hilo limemhamasisha zaidi hivyo ataangalia namna ya kuongeza amana kwenye akaunti yake ili kufurahia huduma hizo zinazokidhi mahitaji yake ya kifedha na imani ya kiroho.
Akimkabidhi kadi ya Al Barakah, Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya CRDB inayojumuisha Zanzibar na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, Badru Idd amesema Rais Mwinyi sio tu alihamasisha kuanzishwa kwa huduma hizo bali alionyesha mfano kwa kuwa wa kwanza kufungua akaunti hiyo mwaka 2021 ambayo mpaka sasa ina wateja zaidi ya 70,000 nchini kote.

“Mpaka sasa hivi, tumekopesha zaidi ya shilingi bilioni 90 kwa misingi ya sharia na tumepokea amana za wateja zaidi ya shilingi 85 bilioni ndani ya miaka miwili ya kutoa huduma hizi. Huduma za CRDB Al Barakah Banking zinaendelea kutoa mchango mkubwa sana katika serikali yako ya Zanzibar na wananchi wake kwani tumekopesha zaidi ya shilingi 18 bilioni kwenye uchumi wa buluu na wafanyabiashara wamepata Zaidi ya shilingi bilioni 33,” amesema Idd.

Ili kusogeza huduma kwa wananchi visiwani humu, Benki ya CRDB ilifungua tawi mjini Wete lililozinduliwa na Rais Mwinyi mwaka 2021 alikoiomba benki kuanzisha huduma zenye misingi ya sharia na mpaka sasa, kwenye matawi manne ya Benki ya CRDB yaliyomo Zanzibar, wananchi wameweka amana za zaidi ya shilingi bilioni 28.
Kuhusu kadi za Akaunti ya Al Barakah, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Benki Zinazofuata Sharia (Islamic Bankink) wa Benki ya CRDB, Rashid Rashid amesema zipo za aina nne na zote zinaweza kutumika katika majukwaa yote ikiwamo kwa mawakala zaidi ya 200 waliopo Zanzibar kama ilivyo kwa kadi zinazotumiwa na wateja wengine wote wa Benki ya CRDB.

“Pamoja na mafanikio haya makubwa, CRDB Al Barakah Banking tunaendelea kuboresha huduma zetu ili kuwafikia wateja wetu na kuwapa amani wanayoitegemea kwa kuweka pesa zao katika akaunti za Al Barakah zinazofuatisha misingi ya sharia. Kila mteja mwenye akaunti hii, ana amani kwa kujua kwamba pesa zake ziko mahala salama na zina uangalizi maalum unaoendana na imani na maadili yake,” amesema Rashid.
Akizungumzia umuhimu wa huduma za fedha kwa maendeleo ya Taifa, Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Fedha Zinazofuata Misingi ya Sharia ya Benki ya CRDB, Abdul van Mohammed amesema kuna fursa nyingi ambazo Zanzibar inaweza kunufaika nazo iwapo itafungua milango.

“Zanzibar ndio yenye matumizi makubwa ya Islamic Banking Afrika Mashariki. Naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuifanya kuwa ya kwanza kuuza hatifungani ya Kiislam ili kupata fedha zitakazochangia maendeleo ya watu wetu,” amesema Mohammed.