Baada ya miaka ya utumishi wa kichungaji, alijiunga na Shule ya Kidiplomasia ya Vatican (Pontifical Ecclesiastical Academy), ambapo alifundishwa masuala ya kidiplomasia na sheria za kanisa.
Mnamo 1991, alianza rasmi kutumikia Huduma ya Kidiplomasia ya Vatican, akihudumu katika balozi mbalimbali za kitume duniani, ikiwemo Sudan, Turkey, Pakistan, na Indonesia.
Mwaka 2010, Papa Benedict XVI alimteua kuwa Askofu Mkuu na Balozi wa Vatican (Apostolic Nuncio) nchini Angola na Sao Tome and Principe. Baadaye alihamishiwa Honduras (2015), kisha New Zealand, Fiji, Tonga na Samoa (2019).
Mbali na jukumu la kidiplomasia, Askofu Mkuu Rugambwa alikuwa pia mjumbe wa kudumu wa Vatican katika mashirika mbalimbali ya kimataifa.
Kote alikopita, alijulikana kwa unyenyekevu wake, hekima ya kidiplomasia na moyo wa upendo, uliomfanya kuwa daraja kati ya Vatican, makanisa ya eneo husika na serikali.
Urithi wake
Kifo cha Askofu Mkuu Rugambwa kimeacha pengo kubwa, lakini mchango wake katika Kanisa na katika kuliletea taifa heshima kwenye meza ya kidiplomasia ya kimataifa utabaki kuwa sehemu ya urithi wake.


.jpg)
Toa Maoni Yako:
0 comments: