Articles by "ELIMU."
Showing posts with label ELIMU.. Show all posts
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye alivunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Rais Mstaafu Wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Bi. Mary Barney Isaac Laseko Mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria ambaye amevunja rekodi iliyodumu miaka 32 kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Profesa wa sheria UDSM Prof. Hamudi Majamba. Pemebni ni wazazi wake Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza hafla ya Mahafali ya 55 (Duru la Tatu) ya Chuo Kikuu hicho, na kumpongeza mhitimu aliyeng’ara kwa kuvunja rekodi iliyodumu kwa zaidi ya miaka 32 katika historia ya The Law School of Tanzania.

Mhitimu huyo, Bi. Mary Barney Laseko, ambaye ni mhitimu wa Shahada ya Awali ya Sheria (LLB), ameweka historia kwa kupata Daraja la Kwanza katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania—rekodi ambayo mara ya mwisho ilipatikana zaidi ya miongo mitatu iliyopita chini ya Profesa Hamudi Majamba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Aidha, Mary anajiunga katika orodha ya wanawake wachache waliowahi kufanya hivyo, akifuata nyayo za Dkt. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa CCM, ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kupata daraja hilo kutoka Law School of Tanzania.

Hafla hiyo imefanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, ambapo Dkt. Kikwete amewatunuku Shahada na Stashahada wahitimu 2,452. Kati yao, 1,386 (sawa na asilimia 56.6) ni wanawake, ikionyesha mwamko na ushiriki mkubwa wa wanawake katika elimu ya juu.

Katika picha zilizopigwa na mpiga picha mkongwe Issa Michuzi, Dkt. Kikwete anaonekana akimpongeza Bi. Mary kwa mafanikio yake, huku picha nyingine zikimuonyesha akiwa na wazazi wake, Bw. Barney Isaac Laseko na Mama Laseko, waliokuwa wakijivunia mafanikio ya binti yao.

Kwa mujibu wa uongozi wa chuo, mafanikio ya Mary yamepokelewa kama ishara ya ongezeko la ubora, nidhamu na juhudi za wanafunzi wanaosomea sheria nchini.
Dodoma, Tanzania — Mr. Sanjeev Mansotra, Chairman, Planet One Group today announced the launch of the Sanjeev Mansotra Foundation (SMF) in Tanzania, marking a significant milestone in its mission to help transform education in Africa. The Foundation’s inaugural initiative will fund the renovation and expansion of four schools in Dodoma, under the aegis of the City Council.

Founded by Sanjeev Mansotra, SMF is guided by a bold vision to ensure that education and health are no longer privileges, but universal rights. The Foundation is committed to strengthening educational institutions, promoting skills development, and improving the well-being of underserved communities.“The establishment of this Foundation is rooted in my firm belief that education is the cornerstone of a thriving national economy,” said Sanjeev Mansotra. “By expanding access to quality education, we empower individuals and lay the foundation for sustainable economic growth and prosperity.”

The launch comes at a critical juncture for education in Africa. A recent report by UNESCO, UNICEF, and the African Union reveals that while school enrollment has increased by 75 million since 2015, the number of out-of-school children has surged by 13.2 million, now exceeding 100 million. As it stands, four out of five African children aged 10 cannot read and understand a simple text. The report cites rapid population growth, humanitarian crises, and a massive annual education funding gap of US$77 billion as key barriers to progress.

Rural and marginalised communities are disproportionately affected, with secondary school completion rates among rural youth up to 20 percentage points lower than their urban peers.
Recognising these challenges, SMF’s work in Dodoma will include the construction of new classrooms, science laboratories, and libraries, alongside the provision of school uniforms, stationery, clean drinking water, and health camps for students and surrounding communities. These efforts are designed to bridge the urban-rural divide and create pathways to opportunity for future generations.

“By investing in infrastructure and essential resources, we aim to inspire students and teachers alike, boost enrollment, and improve learning outcomes,” Mansotra commented. 

The Foundation’s launch in Tanzania follows a formal invitation from the City Council of Dodoma, which oversees school education in the region. Local stakeholders have welcomed the initiative, offering full support and collaboration.

Looking ahead, SMF plans to expand its philanthropic initiatives to other African nations, including Ghana, Guinea, Togo, and Sierra Leone, as well as India.

“Our long-term vision is to serve as a catalyst for transformative change. We are deeply committed to nurturing the next generation by equipping them with education, skills, and aptitude they need to thrive. From imagination to impact, our mission is to ensure no one is left behind,” Mansotra concluded.
Nchi za Nordic zimethibitisha upya dhamira yao ya kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika kuunga mkono sekta ya elimu hususan katika ngazi ya msingi, sekondari na elimu ya watu wazima (folk high schools).

Ahadi hii imekuja sio tu kama kutambua mchango mkubwa wa Kituo cha Elimu Kibaha (KEC), bali pia kutokana na uongozi imara wa Serikali ya Tanzania na juhudi zake za kuendeleza na kupanua mradi huo kwa miaka mingi.

Akizungumza jana wakati wa ziara ya mabalozi katika kituo hicho, Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Jesper Kammersgaard alisema serikali ya Tanzania imeonesha juhudi kubwa katika kulinda malengo ya msingi ya kituo hicho ambayo ni kutoa elimu jumuishi, huduma za afya na maendeleo ya jamii.

“Kituo hiki ni mfano halisi wa namna ushirikiano wa maendeleo unavyopaswa kuwa,” alisema.

“Mradi huu ulianza kama ushirikiano wa pamoja wa nchi za Nordic na baadaye kukabidhiwa rasmi kwa serikali ya Tanzania mwaka 1970. Ni jambo la faraja kuona bado unaendelea na kutoa elimu bora, huduma za afya na mafunzo ya ufundi,” aliongeza.

Balozi wa Finland, Teresa Zitting, pia alisifu uimara wa kituo hicho na uongozi wa Tanzania katika kukiendeleza.

“Ni jambo la kuhamasisha kuona mradi ulioanza zaidi ya miaka 60 iliyopita bado unaendelea kwa mafanikio,” alisema.

Serikali pia iliulizwa kama kuna mpango wa kukifanya kituo hicho kuwa chuo kikuu, ikizingatiwa kuwa kina zaidi ya hekta 1,300 za ardhi.

Hata hivyo, Balozi wa Sweden, Charlotta Ozaki Macias alifafanua kuwa kwa sasa mkazo wa ushirikiano wa Nordic upo katika elimu msingi.

“Kwa sasa hakuna mpango wa kujenga chuo kikuu hapa, Tanzania tayari ina vyuo vingi vizuri,” alisema.

“Lengo letu kubwa ni kuendelea kuunga mkono elimu ya msingi, sekondari na elimu ya watu wazima kupitia ushirikiano na Serikali ya Tanzania na mashirika kama Global Partnership for Education.”

Balozi wa Norway, Tone Tinnes, alisema ziara hiyo ilikuwa kama kurudi kwenye mizizi ya ushirikiano wa kihistoria kati ya Nordic na Tanzania.

“Zaidi ya miaka 60 baadaye, bado tuko hapa tukishirikiana. Hii inatupa nguvu mpya na mwelekeo wa kuendelea kushirikiana kwa muda mrefu,” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo hicho, Robert Shilingi aliwashukuru mabalozi kwa ziara yao na kupongeza serikali ya Tanzania kwa kuendelea kukilea kituo hicho.

“Tumeendelea kutoa huduma bora za elimu, afya na maendeleo ya jamii kutokana na ushirikiano wa serikali yetu na wadau,” alisema.

Alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika elimu na taasisi za maendeleo ya taifa.
“Kituo hiki kitaendelea kuwa mfano wa mafanikio ya ushirikiano wa muda mrefu na wenye malengo ya pamoja,” alihitimisha.











































KATIKA kuhakikisha mafunzo ya darasani yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amekutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, kwa mazungumzo ya namna ya kuwawezesha vijana wahitimu kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi.

Mkutano huo umefanyika katika ofisi za ATE jijini Dar es Salaam, ambapo Prof. Nombo alisema Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na kuboresha mitaala ya ngazi zote ili vijana wapate ujuzi unaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Aidha, Prof. Nombo alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa walimu walioko kazini ili kuboresha mbinu za ufundishaji, akieleza kuwa ufundishaji bora ndio msingi wa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa maisha na ajira.

“Lengo la ziara hii ni kujadiliana na ATE kuhusu njia bora za kuwashirikisha waajiri katika kusaidia vijana waliopo vyuoni au waliomaliza masomo kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi,” alisema Prof. Nombo.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, alisema ATE imekuwa ikisaidia wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo kupitia wanachama wake, wakiwemo viwanda na makampuni. Alitolea mfano wa Mradi wa Kukuza Ujuzi wa Vijana unaotekelezwa na ATE, uliowawezesha zaidi ya vijana 1,000 waliomaliza kidato cha nne kupata mafunzo ya miezi sita katika vyuo vya ufundi kabla ya kupelekwa makampuni kwa mafunzo ya vitendo, ambapo baadhi yao walipata ajira.

Aidha, alitoa wito kwa Watanzania kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kujifunza ujuzi kwa gharama nafuu bila kujali kiwango cha elimu rasmi walichonacho.

Mazungumzo hayo yameonesha dhamira ya pamoja ya Serikali na sekta binafsi katika kuimarisha ujuzi wa vijana na kuandaa nguvu kazi yenye mchango katika maendeleo ya taifa.
Arusha, 6 Septemba 2025: Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) wamezindua rasmi awamu ya pili ya programu ya Learning for Life katika Tawi la NCT Arusha. Wakitanua ushirikiano ulioanzishwa jijini Dar es Salaam tangu Septemba 2024. Katika udahili huu wa Arusha, zaidi ya vijana 150 wataandikishwa na kupata mafunzo ya vitendo yanayolenga moja kwa moja ajira katika hoteli za kifahari na kawaida, migahawa na baa za kanda ya utalii ya kaskazini.

Awamu hii inakuja baada ya mafanikio ya kundi la kwanza lililoandikishwa Dar es Salaam ambapo wanafunzi 100 walihitimu mwezi Mei 2025. Utekelezaji huu wa Arusha umebuniwa ili kuwa wa kudumu na wenye tija, ambapo SBL imewekeza katika mfumo wa kuwafundisha wakufunzi (ToT) kwa wakufunzi wa NCT, hatua itakayokiwezesha chuo hicho kuendesha makundi yajayo kwa uhuru na uimara. Hii inahakikisha upatikanaji wa uhakika wa vijana wenye ujuzi wa kazi kwa sekta ya ukarimu na utalii, sekta muhimu katika kukuza uchumi wa taifa.

Programu hii inachanganya darasa la nadharia na mafunzo ya vitendo kupitia eneo la kazi. Wanafunzi pia watanufaika na maudhui kutoka Diageo Bar Academy kuhusu uendeshaji wa baa, uandaaji wa vinywaji na huduma kwa wateja, sambamba na stadi muhimu za maisha kama vile mawasiliano, kujenga taswira ya kitaaluma na uongozi. Matokeo yake ni kundi la vijana waliokamilika kitaaluma na kijamii, tayari kuinua viwango vya huduma na kuboresha uzoefu kwa wageni kuanzia siku ya kwanza ya ajira zao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Florian Mtey, aliongelea athari chanya za programu hiyo akisema:

"Programu hii imefungua milango mipya kwa wanafunzi wetu. Inawapa zaidi ya nadharia darasani kwa kuwapeleka kwenye mazingira halisi ya kazi, jambo linaloongeza kujiamini na kuwapa uwezo wa kukidhi matarajio ya waajiri katika sekta ya ukarimu na utalii. Tunajivunia kuendeleza ushirikiano huu na SBL hapa Arusha."

Aidha, NCT inatangaza kwamba mafunzo ya muda mfupi chini ya programu ya Learning for Life yanatarajiwa kuanza tarehe 22 Septemba 2025 na kuhitimishwa tarehe 02 Novemba 2025. Gharama zote za mafunzo haya zitagharamiwa na Serengeti Breweries Limited (SBL), huku wanafunzi wakigharamikia malazi, chakula na usafiri.

Waombaji wanatakiwa kutuma fomu za maombi kabla ya tarehe 16 Agosti 2025. Fomu za maombi zinapatikana kupitia tovuti ya Chuo: www.nct.ac.tz au katika ofisi za kampasi za NCT zilizopo Dar es Salaam, Arusha na Mwanza.

Sifa za mwombaji:

Awe Mtanzania.

Awe na barua ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji au kutoka kwa mwajiri.

Awe na umri kati ya miaka 15 – 35.

Awe mwenye afya njema.

Awe na elimu ya Cheti au zaidi katika fani ya Ukarimu na Utalii.

Naye Mkurugenzi wa Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bw. Christopher Gitau, aliongeza:

"Sisi kama SBL tunaamini kwamba kuwekeza kwa vijana ni kuwekeza kwenye mustakabali wa jamii zetu. Kupitia Learning for Life tunawapa stadi za kiufundi lakini pia tunawajengea uwezo wa kuwa viongozi, wajasiriamali na wachangiaji wakuu wa ukuaji wa sekta ya ukarimu na utalii nchini."

Programu ya Learning for Life ni sehemu ya ajenda ya kijamii ya SBL, Spirit of Progress, ikidhihirisha dhamira yake ya muda mrefu ya kuwekeza kwa jamii, kujenga uwezo na kuwawezesha vijana wa Kitanzania. Kupitia upanuzi huu Arusha, programu hii itatoa njia mpya za ajira na kuimarisha zaidi sekta ya utalii na ukarimu nchini Tanzania.

Dondoo 15 za matumizi sahihi ya muda ambazo zinaweza kukusaidia kazini na hata kwenye maisha ya kila siku:

1. Panga ratiba ya kila siku – andika majukumu yako kabla ya kuanza siku.

2. Weka vipaumbele – fanya mambo ya muhimu kwanza.

3. Tumia kalenda au daftari la kumbukumbu – kusaidia kukumbuka tarehe na mikutano.

4. Epuka kazi nyingi kwa wakati mmoja (multitasking) – maliza moja kabla ya kuanza nyingine.

5. Weka muda maalum wa mapumziko – kupunguza uchovu na kuongeza ufanisi.

6. Tumia teknolojia kwa busara – alarms, reminders, na apps za kupanga muda.

7. Punguza usumbufu – kama simu na mitandao ya kijamii unapofanya kazi.

8. Gawa majukumu (delegation) – usijaribu kufanya kila kitu mwenyewe.

9. Weka muda wa dharura (buffer time) – kati ya majukumu ili kuepuka msongo.

10. Anza mapema – kufanya kazi kubwa kabla ya muda haujaenda sana.

11. Jifunze kusema ‘hapana’ – kwa kazi au shughuli zisizo na umuhimu mkubwa.

12. Weka malengo ya muda mfupi na mrefu – ili kujua unakoelekea.

13. Kagua maendeleo yako – angalia kama unatumia muda vizuri.

14. Tambua saa zako za ufanisi zaidi – fanya kazi ngumu wakati akili ikiwa timamu.

15. Hifadhi muda kwa ajili ya familia na afya yako – usitumie muda wote kazini pekee.
Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Maulilio Kipanyula, akisoma hotuba wakati wa Mahafali ya 11 yaliyofanyika Agosti 28, 2025, ambapo jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.

Na Mwandishi Wetu, Arusha.

TAASISI ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imejivunia kutimiza malengo matano ya msingi iliyojiwekea, likiwemo eneo la utafiti na ubunifu, pamoja na usimamizi madhubuti wa programu za uatamizi wa teknolojia.

Akizungumza Agosti 28, 2025 jijini Arusha wakati wa Mahafali ya 11 ya taasisi hiyo, Makamu Mkuu wa Taasisi, Prof. Maulilio Kipanyula, alisema taasisi hiyo imepanua wigo wake wa kitaaluma kwa kutoa Shahada ya Umahiri katika Ubunifu na Usimamizi wa Ujasiriamali kupitia Shule Kuu ya Mafunzo ya Biashara na Sayansi za Jamii (BuSH), ambapo wahitimu wa kwanza kutoka shule hiyo walitunukiwa shahada kwa mara ya kwanza.

Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada katika mahafali hayo, ambapo 71 walitunukiwa Shahada ya Umahiri na 40 walitunukiwa Shahada ya Uzamivu.

Prof. Kipanyula alieleza kuwa dhana ya kubiasharisha bunifu na teknolojia inayoendelezwa na NM-AIST inalenga kusaidia Serikali katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika kukuza viwanda na uchumi wa nchi kwa ujumla.

“Tunawataka wahitimu wetu kuwa na mtazamo wa soko katika kila bunifu wanayoanzisha. Hadi sasa, zaidi ya bunifu 35 zimepata hatimiliki. Hatua inayofuata ni kuhakikisha zinabiasharishwa kwa tija na kuwa chanzo cha mapato kwa taasisi na taifa,” alisema Prof. Kipanyula.

Aliongeza kuwa usimamizi wa uatamizi, uhaulishaji wa teknolojia na ubia kati ya watafiti na sekta binafsi ni nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi kupitia maarifa yanayotolewa na taasisi hiyo. Hata hivyo, alisisitiza kuwa mafanikio hayo hayawezi kufikiwa bila kushirikisha jamii.

Katika mwaka wa kwanza wa masomo, Prof. Kipanyula alisema NM-AIST imefanikiwa kudahili wanafunzi 250 wa shahada za umahiri na uzamivu, ambapo wengi wao walinufaika na ufadhili wa Samia Scholarship. Kupitia ufadhili huo, wanafunzi 50 wamepata mafunzo katika maeneo ya akili bandia (Artificial Intelligence) na Sayansi ya Takwimu (Data Science).

Aidha, alieleza kuwa taasisi hiyo imenunua vifaa vya kisasa vya maabara na imepata ithibati ya kimataifa, hatua inayowezesha utafiti wa kiwango cha juu kinachokubalika kitaifa na kimataifa, hususan kwa kushirikiana na viwanda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi, Balozi Maimuna Tarish, aliwahimiza wahitimu kutumia ujuzi walioupata kutatua changamoto za jamii, kuanzisha ajira na kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya kiuchumi.

“Maarifa, ujuzi na ubobezi mlioupata lazima uwe chachu ya mabadiliko chanya kwa taifa. Muwe na moyo wa kujituma, mzingatie uadilifu, na mwe mfano wa kuigwa katika jamii,” alisema Balozi Tarish.

Wakati huo huo, mmoja wa wahitimu hao, Isaac Mengele, alishukuru kukamilisha masomo yake katika taasisi hiyo huku akieleza kuwa tafiti yake ilihusu kuenea kwa vinasaba vya kinga kwa ng’ombe wa maziwa dhidi ya ugonjwa wa maziwa, kwenye mashamba madogo ya ufugaji.

“Nitahakikisha matokeo ya tafiti yangu yanawasaidia wafugaji wa ng’ombe wa maziwa kufuga kisasa zaidi, kupunguza magonjwa, na kuongeza tija,” alisema Mengele.

Mlau wa Mahafali ya 11 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Gabriel Shirima, akiongoza maandamano ya wanataaluma kuelekea sherehe za Mahafali, Agosti 28, 2025, katika kampasi ya Tengeru, Arusha. Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.
Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Maulilio Kipanyula, akisoma hotuba wakati wa Mahafali ya 11 yaliyofanyika Agosti 28, 2025, ambapo jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.
Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Mhe. Omari Issa (kulia), akimtunuku mmoja wa wahitimu (kushoto) wa Shahada ya Uzamivu wakati wa Mahafali ya 11 ya taasisi hiyo, Agosti 28, 2025. Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada mbalimbali za Umahiri na Uzamivu.
   

Wahitimu wa Mahafali ya 11 ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wakiwa tayari kwa ajili ya kutunukiwa shahada zao na Mkuu wa Taasisi, Mhe. Omari Issa (hayupo katika picha).
Na Mwandishi Wetu, Bukoba

Shule ya Sekondari ya Wasichana Josiah imeadhimisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake kwa Ibada Kuu ya Shukrani iliyoongozwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa.

Katika mahubiri yake, Askofu Malasusa alisema mafanikio ya shule hiyo yametokana na msingi wa maadili mema na imani kwa Mungu. “Mungu hayuko mbali na shule hii na atawasimamia na kuhakikisha wanashinda kwa kuwa Yeye amejaa neema. Hata sasa Bwana amesaidia,” alisema.

Alisisitiza kuwa shule za Tanzania zinapaswa kuzingatia malezi ya kimaadili sambamba na elimu ya darasani, ili kujenga kizazi bora chenye uzalendo na uadilifu.
Shule ya Josiah, iliyoanzishwa mwaka 2010 katika Kata ya Ijuganyundo, Manispaa ya Bukoba, imekuwa kimbilio kwa wazazi na walezi kutokana na elimu bora na malezi yenye maadili. Mjumbe wa Bodi ya Shule na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, Dkt. Abednego Keshomshahara, alisema shule hiyo imeendelea kufanya vizuri katika mitihani ya kitaifa na kuwa mfano wa kuigwa kwa shule binafsi nchini.

Kwa upande wake, Askofu mstaafu wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini, alipongeza uongozi wa shule kwa kujitolea bila kuchoka na kuendeleza malezi yenye misingi ya maadili. “Nafurahi kuona shule hii imesimama kwa imani na uadilifu, imekuwa chombo cha kujenga jamii yenye maadili mema na kuandaa viongozi wa kesho,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Mhe. Erasto Sima, aliahidi ushirikiano wa karibu kati ya serikali na taasisi binafsi za elimu ili kuboresha miundombinu na kuongeza ubora wa elimu. “Serikali iko tayari kushirikiana na wadau wa elimu kama Josiah Girls’ Secondary School katika kuhakikisha watoto wetu wanapata elimu bora na mazingira salama ya kusomea,” alisema.

Mbali na ibada na hotuba za viongozi, maadhimisho hayo yalihusisha utoaji wa tuzo kwa wadau waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya shule, pamoja na shuhuda kutoka kwa wanafunzi na wahitimu waliothibitisha ubora wa malezi na elimu waliyoipata.

Kwa jumuiya ya Josiah Girls’ Secondary School, miaka 15 ni ishara ya baraka, mshikamano na matumaini ya mafanikio makubwa zaidi katika siku zijazo, ikiwa na dira ya “Ndoto Yangu, Upeo Wangu” inayoendelea kuongoza kila hatua ya safari yake ya kielimu.
Wageni waalikwa wakifuatilia.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Josiah Girls wakitoa burudani kwa wageni waalikwa.
Askofu mstaafu wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini (katikati) akifuatilia utoaji wa zawadi kwa wafanyakazi.
Zawadi za vyeti zikitolewa kwa wafanyakazi na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa (kulia).
Picha ya pamoja ya viongozi wa dini na serikali.