Articles by "ELIMU."
Showing posts with label ELIMU.. Show all posts

Africa Global Logistics (AGL), kupitia kampuni dada ya EALS, imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na Shule ya Sekondari Mabibo kwa kukabidhi madumu 12 ya kuhifadhia taka, vizima moto 3 vya CO2 (kg 9), vizima moto 24 vya ABC (kg 9), pamoja na king'ora kimoja cha tahadhari ya moto kinachotumia mfumo wa mkono. Mchango huu ni sehemu ya dhamira endelevu ya kampuni katika kuimarisha usalama, kuhifadhi mazingira na kuchangia maendeleo ya jamii, kufuatia ujenzi wa miundombinu ya vyoo shuleni hapo mwaka 2025.
Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya AGL Tanzania imezindua mpango wa “Plastic-Less” unaolenga kupunguza matumizi ya plastiki zinazotumika mara moja, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kulinda mazingira na kuhamasisha jamii kuzingatia matumizi endelevu ya rasilimali.

Kupitia mpango huo, kampuni imegawa chupa za maji zinazoweza kutumika tena kwa wafanyakazi wake wote na kuweka visambaza maji katika vyumba vya mikutano pamoja na maeneo mbalimbali ya kazi, hatua inayolenga kupunguza utegemezi wa chupa za plastiki zinazotupwa baada ya matumizi.

Kwa wageni wanaotembelea ofisi za kampuni hiyo, AGL imeanza kutumia glasi zinazoweza kuoshwa na kutumika tena badala ya vyombo vya plastiki vya matumizi ya mara moja, ikiwa ni mkakati wa kupunguza uzalishaji wa taka zinazochafua mazingira.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo uliofanyika Juni 5 sambamba na maadhimisho ya juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Meneja wa Masuala ya Sheria wa AGL, Angeline Mtulia, alisema uendelevu ni sehemu ya utamaduni wa kampuni na wajibu wa pamoja kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

“Kupitia mpango wa ‘Plastic-Less’, tunaonesha kuwa mabadiliko madogo ya tabia yanapoungwa mkono na miundombinu sahihi na ushirikiano wa kijamii yanaweza kuleta matokeo makubwa katika uhifadhi wa mazingira na ustawi wa jamii,” alisema Mtulia.

Katika kuimarisha uelewa wa wafanyakazi, timu ya QHSE kwa kushirikiana na kundi la urejelezaji taka la The Recyclers ilitoa mafunzo kuhusu usimamizi wa taka na athari za matumizi ya plastiki kwa mazingira, huku ikisisitiza umuhimu wa kubadili mtindo wa maisha ili kupunguza uchafuzi wa mazingira.
Mbali na shughuli za ndani ya kampuni, AGL kupitia kampuni dada ya EALS ilitekeleza programu za uwajibikaji kwa jamii kwa kutembelea Shule ya Sekondari Mabibo na kukabidhi mapipa 12 ya kuhifadhia taka, vizima moto 27 pamoja na king'ora cha tahadhari ya moto kwa lengo la kuimarisha usafi wa mazingira na usalama shuleni.

Wanafunzi wa shule hiyo pia walipatiwa elimu kuhusu madhara ya taka za plastiki, mbinu za kutenganisha taka kwa usahihi na umuhimu wa kuhifadhi mazingira, sambamba na mafunzo ya kujikinga na majanga ya moto.

AGL imesema itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mpango huo kwa kupima kiwango cha matumizi ya plastiki kabla na baada ya utekelezaji wake ili kutathmini mafanikio yake katika kupunguza taka na kuchangia uhifadhi wa mazingira.

Kupitia mpango wa “Plastic-Less”, kampuni hiyo imeonesha dhamira ya kuunga mkono Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kuunganisha uhifadhi wa mazingira, matumizi bora ya rasilimali na maendeleo ya jamii, huku ikijenga utamaduni wa uwajibikaji kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajia kuadhimisha Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026, katika Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere, huku Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Maadhimisho hayo yatakayowakutanisha watafiti, wabunifu, wanafunzi, sekta binafsi, taasisi za umma na wadau wa maendeleo, yanalenga kuonesha mchango wa utafiti na ubunifu katika kuharakisha maendeleo ya taifa na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Utafiti, Profesa Nelson Boniface, alisema maadhimisho ya mwaka huu yataongozwa na kaulimbiu isemayo: "Kutumia Utajiri wa Madini wa Tanzania katika Kukuza Nishati Jadidifu, Mageuzi ya Kidijitali na Usalama wa Jamii."

Alisema kaulimbiu hiyo imechaguliwa kutokana na umuhimu wa madini katika maendeleo ya teknolojia za kisasa ikiwemo Akili Mnemba (AI), vituo vya kuhifadhi taarifa (Data Centres), magari ya umeme na nishati jadidifu.

“Tunataka kuonesha namna Tanzania inaweza kutumia rasilimali zake za madini kuchochea mageuzi ya kidijitali, kuimarisha usalama wa nishati na kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” alisema Profesa Boniface.

Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatahusisha maonesho ya tafiti na ubunifu, mawasilisho ya kitaaluma, makongamano pamoja na majadiliano ya ushirikiano wa kimkakati yatakayowawezesha washiriki kubadilishana maarifa na kujenga mitandao ya kitaaluma na kibiashara.

Kwa mujibu wa UDSM, maadhimisho hayo yatatoa nafasi kwa watafiti na wabunifu kuonesha suluhisho mbalimbali za kisayansi na kiteknolojia zinazolenga kukabiliana na changamoto za maendeleo nchini katika sekta za madini, nishati, kilimo, afya na uchumi wa kidijitali.

Profesa Boniface alisema chuo kinaendelea kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuunganisha taaluma, ubunifu na maendeleo ya taifa kwa kuwafikia wananchi, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo.

"Utafiti na ubunifu ni msingi wa maendeleo endelevu. Tunawaalika Watanzania wote kushiriki katika Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu UDSM 2026 ili kujionea kazi na mafanikio ya watafiti na wabunifu wetu," alisema.

NA MWANDISHI WETU – SONGEA

Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki  maghala ya kuifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hii kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa  katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,

Ambao  umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga

Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika  katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.


Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.

‘Mkoa  hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.

Aidha Aliwaasa wanufaika wa Mradi huo kuwapatia wengine ujuzi walioupata na kuwa waaminifu wanapopata mikopo kupitia Bank ya Kilimo nchini TADB kwa kuirejesha kwa wakati kwa amendeleo ya Taifa.Afisa Uvuvi kutoka Cameroon Bi Audrely Tchoundi aliwapongeza wafugaji wa Tanzani kwa kuwa wabunifu katika eneo la ufungaji viumbemaji na ukulima wa mwani kwa kutumia mbinu mbadala akitolea mfano wakulima wa Mwani wa Kijiji cha Shuka Mkoani Lindi, pamoja na usimamizi mzuri wa mabwawa ya samaki.

Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana  Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.

Na Jawadu kinyobwa - Dsm

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka Wanafunzi wa sheria kujenga taaluma zao katika misingi ya nidhamu, ubunifu na uzalendo ili waweze kufanikiwa katika soko la ajira la kimataifa linalozidi kuwa na ushindani.

Akizungumza leo Juni 5, 2026 katika hafla ya Siku ya Kazi na Taaluma ya Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amesema mafanikio ya kitaaluma hayawezi kupatikana bila kuzingatia maadili hayo matatu muhimu.
Akifafanua kuhusu nidhamu, amesema ubora si jambo la muda mfupi bali ni tabia inayojengwa kwa kujifunza kwa bidii, kutunza muda, kuwa na hamu ya kujifunza mambo mapya na kuzingatia maadili ya taaluma. 

Amefafanua kuwa, nidhamu inayojengwa kupitia mahakama za mfano, kazi za kitaaluma na shughuli za msaada wa kisheria ndiyo msingi wa kukabiliana na changamoto za taaluma katika ngazi za kitaifa na kimataifa.
Aidha, kuhusu ubunifu, Waziri huyo amesema maendeleo ya teknolojia yamebadili kwa kiasi kikubwa namna taaluma ya sheria inavyotekelezwa duniani. Ametaja matumizi ya Akili Mnemba, mifumo ya kidijitali ya usajili na teknolojia za kisheria kuwa miongoni mwa mabadiliko yanayounda upya mazingira ya kazi za sheria. 

Katika hatua nyingine, amesisitiza umuhimu wa uzalendo, akieleza kuwa wao ni walinzi wa utawala wa sheria na utawala bora hivyo wanapopata fursa ya kufanya kazi katika taasisi za kimataifa au kampuni kubwa nje ya nchi, wanapaswa kutumia maarifa na uwezo wao kuisaidia Tanzania kutambulika vyema nje ya nchi.
Sambamba na hayo, Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha sekta ya sheria na haki kupitia mageuzi ya mfumo wa haki, matumizi ya teknolojia, uwekezaji katika miundombinu ya utoaji haki na kuhamasisha mifumo mbadala ya utatuzi wa migogoro.

Awali, akizungumzia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mhe. Ridhiwani amesema sekta ya sheria ni nguzo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii kupitia mchango wa wataalamu wa sheria katika kulinda maslahi ya taifa, kuimarisha utawala wa sheria na kusaidia mageuzi ya kidijitali.

 

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Shahada ya Uzamivu ya Heshima (Honoris Causa) aliyotunukiwa na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) nchini Urusi, maarufu kama Patrice Lumumba University ni heshima kubwa kwake binafsi na kwa taifa la Tanzania kwa ujumla.

Akihutubia baada ya kutunukiwa shahada hiyo Rais Samia amesema katika dunia ya sasa inayobadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, ni muhimu kwa nchi kuwekeza katika wataalamu waliobobea ambao wanaelewa kuwa ujuzi wao ni chachu ya maendeleo endelevu ya taifa.

Ameongeza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya elimu, utafiti na teknolojia ili kuhakikisha vijana wanapata maarifa yatakayowezesha kushindana katika soko la ajira la kimataifa na kuchangia maendeleo ya kiuchumi.

Rais Samia ametunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima na Chuo Kikuu cha RUDN, kwa kutambua mchango wake katika uongozi bora, diplomasia na maendeleo ya jamii.

Shahada hiyo imetolewa wakati wa ziara ya kitaifa ya Rais Samia nchini Urusi, ambapo amekuwa akifanya mazungumzo ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Urusi.
Na Chalila Kibuda, Dar es Salaam

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yusuf Masauni, amewahimiza vijana nchini kutumia ubunifu, teknolojia na maarifa yao kunufaika na fursa zinazotokana na uchumi wa kijani ili kujikwamua kiuchumi na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira.

Masauni alitoa wito huo Juni 2, 2026 wakati akifungua Kongamano la Vijana kuhusu Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Alisema mazingira si suala la uhifadhi pekee, bali ni sekta yenye uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira, biashara na fursa mbalimbali za maendeleo kwa vijana.
Kwa mujibu wa Masauni, changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi zinaweza kubadilishwa kuwa fursa za kiuchumi kupitia shughuli mbalimbali zikiwemo biashara ya kaboni, urejelezaji wa taka, matumizi ya nishati safi, uhifadhi wa mikoko, kilimo kinachostahimili mabadiliko ya tabianchi pamoja na matumizi ya teknolojia za kijani.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi yanayowawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi wa mazingira huku ikikuza uchumi wa kijani unaolenga kuongeza ajira na ustawi wa wananchi.

Masauni alibainisha kuwa vijana ndio watakaobeba athari kubwa za uharibifu wa mazingira katika siku zijazo, hivyo wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kulinda rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
“Tunataka kila kijana aelewe kuwa mazingira ni utajiri. Ukiona taka, usione uchafu pekee, ona fursa ya biashara. Ukiona mikoko, usione miti tu, ona rasilimali inayoweza kuchangia mapato kupitia biashara ya kaboni,” alisema.

Aidha, aliwataka vijana kutumia mitandao ya kijamii na teknolojia za kisasa kutafuta masoko, kuandaa miradi ya mazingira na kuvutia uwekezaji badala ya kutumia muda mwingi katika shughuli zisizo na tija.

Akizungumza katika kongamano hilo, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi, alisema vijana ni nguvu kubwa ya mabadiliko katika Bara la Afrika kutokana na idadi yao kubwa, hivyo ushiriki wao katika masuala ya mazingira ni muhimu kwa maendeleo endelevu.

Alisema Serikali imefanikiwa kuifanya Tanzania kuwa mwenyeji wa Kituo cha Vijana wa Afrika cha Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabianchi, hatua itakayowajengea vijana uwezo katika utafiti, ubunifu, diplomasia ya mazingira na matumizi ya teknolojia za kisasa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mazingira, Kemirembe Mutasa, alisema Serikali imeweka sera, sheria na miongozo mbalimbali inayolenga kuongeza ushiriki wa vijana katika kukabiliana na changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi.

Kongamano hilo liliwakutanisha wanafunzi wa shule za sekondari na vyuo vikuu, taasisi mbalimbali za Serikali, sekta binafsi pamoja na wadau wa maendeleo. Tukio hilo limefanyika ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.

Maadhimisho ya mwaka huu nchini yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Dira 2050: Tuwajibike Kupigania Tanzania,” inayolenga kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda mazingira na kuhakikisha maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Mafunzo Elekezi kwa Watumishi Wapya wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) yameanza leo, Mei 28, 2026, ikiwa ni hatua muhimu ya kuandaa wataalamu wa mamlaka hiyo kwa kuzingatia misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali. Watumishi wapya 29 wanashiriki mafunzo haya .yanayotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. 


"Tunatarajia kuwa baada ya mafunzo haya, mtakuwa watumishi wa umma wanaofuata maadili ya utumishi wa umma, wakiwasiliana kwa ufanisi na kuheshimu usiri wa taarifa na nyaraka za serikali, huku pia wakielewa haki na wajibu wao," amesema.

Kwa upande wake, Bi. Zena Hussein ambaye ni Meneja wa kituo cha mafunzo kwa njia ya Mtandao  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, amesema kuwa mafunzo haya ni muhimu na lazima kwa watumishi wapya katika utumishi wa umma. 
"Mafunzo haya yanalenga kuimarisha uelewa wa misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi," amesisitiza.

Aidha amesema kuwa Mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza uelewa wa watumishi wapya kuhusu misingi ya utumishi wa umma na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ndani ya TISEZA. Vilevile, mchakato huo unazingatia taratibu na miongozo ya serikali, kwa lengo la kuhakikisha majukumu yanatekelezwa kwa uwajibikaji, uadilifu, na ufanisi.
Mafunzo haya ni utekelezaji waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2011, uno wataka waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wapya wanapatiwa mafunzo elekezi ndani ya miezi sita tangu kuajiriwa,
By Zamda George, CMU

DAR ES SALAAM — An atmosphere of pride, academic excellence and national prestige filled Mlimani City Hall on May 25, 2026, as the University of Dar es Salaam (UDSM) conferred degrees to 876 graduates, including 94 new PhD holders, during Cluster I of its 56th Graduation Ceremony.

The ceremony, presided over by the University Chancellor and former President of Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, reaffirmed UDSM’s position as one of Africa’s leading centres of research, innovation and intellectual leadership.

The 94 doctoral graduates came from 15 academic disciplines, reflecting the University’s growing role in producing highly skilled researchers, innovators and professionals capable of contributing to national transformation and global development.

Unlike the lively celebrations commonly associated with undergraduate graduations, the PhD ceremony carried an atmosphere of academic maturity and scholarly prestige. Dressed in elegant academic regalia, the graduates proudly crossed the stage, symbolizing years of sacrifice, resilience, rigorous research and dedication.

Speaking during the ceremony, Chancellor Kikwete urged graduates to use their education and research to solve societal challenges and contribute to national development.

“Your education must become a tool for bringing positive change to society. The knowledge and expertise you have acquired should help drive innovation, leadership and transformation for the benefit of Tanzania and the wider global community,” said Dr. Kikwete.

He further emphasized the importance of research and knowledge creation in shaping Africa’s future, noting that universities must continue producing scholars capable of providing evidence-based solutions to emerging challenges.

UDSM Vice Chancellor, Prof. William A. L. Anangisye, described the graduation ceremony as a reflection of the University’s continued growth in teaching, research, innovation and international competitiveness.

Presenting the University’s annual progress report, Prof. Anangisye revealed that UDSM currently has 235 researchers ranked among Tanzania’s top 1,000 researchers according to the AD Scientific Index 2026. This represents 23.5 percent of all top researchers across 50 institutions nationwide.

He added that the University has continued strengthening academic quality and labour market relevance through curriculum reforms, with 285 undergraduate and postgraduate programmes reviewed based on stakeholder feedback and changing market demands.

Prof. Anangisye also highlighted major achievements in innovation and research commercialization. During the 2025/2026 academic year, UDSM researchers and innovators registered six patents through BRELA, some involving student innovators.

The registered innovations include technologies for bioethanol production, mushroom cultivation using sisal waste, organic fertilizer production, protein feed development using Black Soldier Fly larvae, and wine production from bamboo juice.

“These achievements demonstrate UDSM’s ability to add value to local resources, promote the green economy and use science to provide practical development solutions,” said Prof. Anangisye.

The Vice Chancellor further revealed that through the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project, the University is currently constructing 21 new buildings and renovating three others, a move expected to increase student capacity by 4,812 spaces.

He added that UDSM has also expanded digital learning infrastructure by increasing internet capacity, digitizing more than 1,000 courses and providing short-term professional training to nearly 3,000 staff members.

Addressing graduates directly, Prof. Anangisye reminded them that education is both a privilege and a responsibility to society.

“Education is not merely a personal achievement or decoration. It is a responsibility and a debt to the nation. Use the knowledge you have acquired to serve society, create opportunities and contribute to national development,” he said.

He encouraged graduates to embrace innovation, entrepreneurship and opportunities within the digital economy, especially in situations where formal employment opportunities may not immediately be available.

One of the most inspiring moments of the ceremony was the graduation of Dr. Paul Msoka, a visually impaired scholar who earned a PhD in Education after previously completing both his Bachelor’s and Master’s degrees within the UDSM system.

Dr. Msoka’s achievement stood out as a powerful testimony to resilience, determination and the University’s commitment to inclusive education and equal access to academic opportunities.

A researcher specializing in inclusive education and visual impairment studies, Dr. Msoka has contributed scholarly work focused on improving learning opportunities for students with visual impairment in Tanzania’s inclusive schools.

His achievement inspired many graduates, lecturers, family members and guests attending the ceremony, particularly young Tanzanians living with disabilities who aspire to pursue higher education and professional excellence.

Throughout the ceremony, emotional moments unfolded as graduates celebrated with supervisors, colleagues, friends and family members. Smiles, embraces and photographs reflected years of perseverance, sacrifice and academic dedication behind every success story.

Established in 1961, the University of Dar es Salaam remains Tanzania’s premier institution of higher learning and a symbol of academic excellence. Over the decades, the University has produced influential leaders, policymakers, scholars, diplomats, entrepreneurs and professionals who continue shaping Tanzania, Africa and the wider world.

For the Class of 2026, the graduation ceremony marked not only the completion of an academic journey, but also the beginning of a new chapter of leadership, innovation and national service.

As celebrations continued outside Mlimani City Hall, one message remained clear — the future of Tanzania’s intellectual, scientific and developmental transformation continues to be shaped at the University of Dar es Salaam.




Na Mwandishi Wetu

Serikali ya Kenya imetoa hati rasmi za vyuo vikuu kwa Kenya Advanced Institute of Science and Technology na Kenya Medical Research Institute katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Nairobi, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya juu, utafiti wa kisayansi na ubunifu nchini humo.

Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya mkakati wa makusudi wa kupanua fursa za elimu ya juu pamoja na kuimarisha mazingira ya utafiti na uvumbuzi yatakayosaidia maendeleo ya taifa.

Kupitia hatua hiyo, Kenya inalenga kujenga mustakabali unaotegemea elimu bora, ubunifu wa ndani na maendeleo endelevu ya tafiti mbalimbali za kisayansi.

Viongozi waliozungumza wakati wa hafla hiyo walisisitiza kuwa vyuo vikuu vina nafasi muhimu katika kuandaa wataalamu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasayansi, wahandisi, madaktari na wabunifu ambao watasaidia kuleta mabadiliko ya maendeleo nchini.

Aidha, ilielezwa kuwa pamoja na kuchangia maendeleo ya kitaifa, wataalamu hao pia wanatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika nyanja mbalimbali duniani kupitia maarifa, teknolojia na suluhisho za changamoto zinazokabili jamii.

Hatua hiyo pia inatazamwa kama juhudi za Kenya za kuimarisha sekta ya elimu na kuifanya nchi hiyo kuwa kitovu cha utafiti, teknolojia na ubunifu katika ukanda wa Afrika.









Dar es Salaam- Mei 5, 2026: Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Serikali Kenya (KSG), Prof. Nura Mohamed na ujumbe wake   wametembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania leo, Mei 5, 2026, jijini Dar es Salaam.
Ziara hiyo ni sehemu ya kuanza kwa utekelezaji wa mkataba wa ushirikiano uliosainiwa Ikulu, Mei 4, 2026, mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto.

Katika kikao cha pamoja na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, chini ya Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho, wamejadiliana kwa kina kuhusu mikakati ya kuanza utekelezaji wa makubaliano hayo, huku lengo likiwa ni kuboresha utendaji wa utumishi wa umma kwa kuwajengea uwezo watumishi na Tafiti Tumizi.
Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amesema  kuwa, ushirikiano kati KSG na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania  (TPSC) unalenga kuleta maendeleo makubwa na ufanisi zaidi katika sekta ya utumishi wa umma, kwa kujenga uwezo wa watumishi kupitia mafunzo na tafiti.

 Aidha, alisisitiza kuwa, kutokana na uzoefu wa zaidi ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa KSG, ni fursa adhimu kwa TPSC kujifunza na kupata uzoefu wa kuboresha utumishi wa umma nchini Tanzania, ili kujenga utumishi wa umma imara.

Dkt. Mabonesho ameongeza kuwa, mashirikiano pia yanalenga kujenga utumishi wa umma wenye tija, wenye kuzingatia matokeo, na kuleta maendeleo chanya kwa wananchi wa Tanzania, Kenya, na jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla.
Kwa upande wake, Prof. Nura Mohamed alieleza kuwa, utekelezaji wa mkataba huo utaleta maendeleo makubwa kwa pande zote mbili, kwa kuimarisha mafunzo yanayozingatia ubora na haki za wananchi.

 Prof. Mohamed amesisitiza  kuwa, ushirikiano huo utahusisha pia kufanya tafiti za pamoja kuhusu kuboresha sera na huduma zinazohudumia jamii, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, ambazo ni haki yao ya msingi.

Ziara hiyo pia iliwapa nafasi ujumbe kutoka KSG kutembelea Makao Makuu ya Chuo yaliyopo Barabara ya Bibi Titi, Kampasi ya Dar es Salaam iliyopo Magogoni, na Kituo cha Mafunzo kwa njia ya Mtandao, ambapo walijionea mazingira ya mafunzo na shughuli zinazofanywa na chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania.