Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka vijana nchini kulinda amani na kutokubali kutumika katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama na taswira ya nchi.
Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo jirani na Uwanja wa Ndege wa Dodoma, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam, aliposimamishwa na maelfu ya wakazi wa Dodoma waliokusanyika barabarani kwa ajili ya kumsalimia Kiongozi huyo.
Wananchi hao, wakiwemo vijana, maafisa usafirishaji, wafanyabiashara wadogo, machinga, Mamalishe na Babalishe, walijitokeza wakiwa wamevaa fulana na mabango yenye ujumbe wa “Never Again” (Yasijirudie) sambamba na bendera za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akiupokea ujumbe huo, Rais Dkt. Samia amesema matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea nchini hayapaswi kujirudia kwa kuwa yaliathiri taswira ya Taifa na maisha ya wananchi kwa ujumla, hususan vijana.
“Niwaombe sana vijana, katika miji yenu, katika kazi zenu, katika shughuli zenu zote, ambizaneni yaliyotokea yasijirudie tena, kwani yamelitia doa Taifa letu,” amesema Rais Dkt. Samia, akisisitiza wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha matukio hayo, ambayo si sehemu ya hulka ya Watanzania, hayapewi tena nafasi katika jamii.
Aidha, amewataka vijana kulindana, kuelimishana na kuwa walinzi wa amani katika maeneo yao ya kazi, biashara na shughuli za kila siku, na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kusikiliza hoja za wananchi na kufanyia kazi changamoto zinazogusa maisha yao.
Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo jirani na Uwanja wa Ndege wa Dodoma, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam, aliposimamishwa na maelfu ya wakazi wa Dodoma waliokusanyika barabarani kwa ajili ya kumsalimia Kiongozi huyo.
Wananchi hao, wakiwemo vijana, maafisa usafirishaji, wafanyabiashara wadogo, machinga, Mamalishe na Babalishe, walijitokeza wakiwa wamevaa fulana na mabango yenye ujumbe wa “Never Again” (Yasijirudie) sambamba na bendera za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akiupokea ujumbe huo, Rais Dkt. Samia amesema matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea nchini hayapaswi kujirudia kwa kuwa yaliathiri taswira ya Taifa na maisha ya wananchi kwa ujumla, hususan vijana.
“Niwaombe sana vijana, katika miji yenu, katika kazi zenu, katika shughuli zenu zote, ambizaneni yaliyotokea yasijirudie tena, kwani yamelitia doa Taifa letu,” amesema Rais Dkt. Samia, akisisitiza wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha matukio hayo, ambayo si sehemu ya hulka ya Watanzania, hayapewi tena nafasi katika jamii.
Aidha, amewataka vijana kulindana, kuelimishana na kuwa walinzi wa amani katika maeneo yao ya kazi, biashara na shughuli za kila siku, na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kusikiliza hoja za wananchi na kufanyia kazi changamoto zinazogusa maisha yao.
Kuhusu mikopo kwa wafanyabiashara wadogo, Rais Dkt. Samia amesema Serikali imeanza hatua za kusimamia zoezi la utoaji wa mikopo kupitia taasisi zaidi za kifedha tofauti na ilivyokuwa awali, ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa mitaji kwa vijana na makundi mbalimbali ya wajasiriamali.
Amesema mahitaji ya mikopo kwa vijana ni makubwa, na Serikali itaendelea kuongeza rasilimali kadiri uchumi utakavyoruhusu.
Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amesema Serikali itatathmini uwezekano wa kuanzisha soko lingine la wafanyabiashara wadogo mkoani Dodoma, pembezoni mwa Soko la Machinga Complex lililopo sasa, ili kukuza fursa zaidi kwa wajasiriamali, kupunguza msongamano na kuboresha mazingira ya biashara.
Awali, wawakilishi wa wafanyabiashara wadogo walieleza namna Soko la Machinga Complex lilivyo mfano bora wa utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kuhusu upangaji wa biashara ndogondogo katika maeneo rasmi, salama na rafiki kwa shughuli za kiuchumi, pamoja na kuomba kuimarishwa kwa huduma za usafiri wa daladala kuingia eneo la soko, uratibu na usimamizi endelevu wa biashara katika maeneo rasmi, na ongezeko la huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo.
Kwa upande wao, Mamalishe na Babalishe waliwasilisha ombi la kuendelea kuboreshewa masharti ya mikopo ya makundi maalum inayotolewa na Serikali ili makundi zaidi, hasa ya kipato cha chini, yaweze kunufaika.
Amesema mahitaji ya mikopo kwa vijana ni makubwa, na Serikali itaendelea kuongeza rasilimali kadiri uchumi utakavyoruhusu.
Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amesema Serikali itatathmini uwezekano wa kuanzisha soko lingine la wafanyabiashara wadogo mkoani Dodoma, pembezoni mwa Soko la Machinga Complex lililopo sasa, ili kukuza fursa zaidi kwa wajasiriamali, kupunguza msongamano na kuboresha mazingira ya biashara.
Awali, wawakilishi wa wafanyabiashara wadogo walieleza namna Soko la Machinga Complex lilivyo mfano bora wa utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kuhusu upangaji wa biashara ndogondogo katika maeneo rasmi, salama na rafiki kwa shughuli za kiuchumi, pamoja na kuomba kuimarishwa kwa huduma za usafiri wa daladala kuingia eneo la soko, uratibu na usimamizi endelevu wa biashara katika maeneo rasmi, na ongezeko la huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo.
Kwa upande wao, Mamalishe na Babalishe waliwasilisha ombi la kuendelea kuboreshewa masharti ya mikopo ya makundi maalum inayotolewa na Serikali ili makundi zaidi, hasa ya kipato cha chini, yaweze kunufaika.
Nao, Maafisa Usafirishaji wameahidi kuendelea kushirikiana na mamlaka za Serikali katika kulinda amani na kuzuia matumizi mabaya ya vyombo vya usafiri ikiwemo vitendo vya fujo.
Akihitimisha, Rais Dkt. Samia ameagiza viongozi wa Mkoa wa Dodoma kufanyia kazi hoja zilizotolewa na wananchi, na kutaka ripoti ya utekelezaji pindi atakaporejea Dodoma.
Akihitimisha, Rais Dkt. Samia ameagiza viongozi wa Mkoa wa Dodoma kufanyia kazi hoja zilizotolewa na wananchi, na kutaka ripoti ya utekelezaji pindi atakaporejea Dodoma.







































.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)