Articles by "WAZIRI MKUU"
Showing posts with label WAZIRI MKUU. Show all posts
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza katika Ibada ya Jumpili aliyoshiriki katika Usharika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Kisasa jijini Dodoma, Novemba 16, 2025.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuwasisitiza Watanzania kuyaombea taifa ili amani, upendo na mshikamano viendelee kudumu nchini, akisema maombi ni nguzo muhimu ya utulivu wa taifa.

Wito huo umetolewa leo Jumapili, Novemba 16, 2025 na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, alipowasilisha salamu za Rais Samia kwa waumini na viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kisasa mkoani Dodoma.

“Mheshimiwa Rais anawasalimu sana. Rai yake kwa Watanzania wote ni kuendelea kuiombea nchi yetu, tuwe watulivu na tuendelee kudumisha amani,” alisema Waziri Mkuu wakati akisoma salamu hizo.

Dkt. Mwigulu alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kulinda amani ya nchi kwa sababu bila amani hakuna shughuli yoyote muhimu inayoweza kufanyika, ikiwemo ibada, maendeleo ya kijamii na utekelezaji wa mipango ya serikali.

“Pasipo amani hatuwezi kutekeleza majukumu yetu mengine. Pasipo amani hatuwezi hata kufanya ibada. Ndiyo maana tunapaswa kuiombea nchi yetu kila mara. Tukidumisha amani, tunaweza kukabiliana hata na mambo magumu,” alisema.

Ibada hiyo iliongozwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Dkt. Christian Ndossa, ambaye aliwahimiza waumini na Watanzania kwa ujumla kumtanguliza Mungu katika maisha yao, kuwa na matumaini na kujiepusha na matendo maovu.

Katika ibada hiyo, Waziri Mkuu aliambatana na mke wake, Mama Neema Mwigulu Nchemba, sambamba na viongozi mbalimbali wa serikali na Bunge akiwemo Naibu Spika wa Bunge, Daniel Sillo; Mbunge wa Kilolo, Ritha Kabati; Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya; Mbunge wa Viti Maalumu, Balozi Dkt. Pindi Chana; Mbunge wa Itigi, Yohana Msita na Mbunge wa Kalenga, Jackson Kiswaga.

Ibada hiyo imeendelea kuwa sehemu ya mwamko wa viongozi kuitaka jamii kuenzi amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.

Na Mwandishi Wetu.

Alizaliwa mwaka 1960 katika kijiji kidogo cha Namoto, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi. Leo hii, jina la Kassim Majaliwa Majaliwa linaandikwa kwa heshima kubwa katika historia ya Tanzania. Safari yake ni ya kuvutia kutoka maisha ya kawaida kabisa hadi kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa taifa.
‎Kiu yake kubwa ilikuwa ni kufundisha, hivyo hakuchelewa alisomea ualimu katika Chuo cha Ualimu Mtwara na baadaye Chuo cha Ualimu Kitangali kilichopo Mtwara.
‎Alianza kuwa mwalimu, akilea vijana kwa bidii na maadili, Akawa mkufunzi katika Chuo cha Ualimu mtwara huku akijijengea misingi imara kwa huduma ya jamii,
‎Hakika alijitengeneza kama kiongozi mwenye maarifa, nidhamu, na mwelekeo wa maendeleo kwa taifa.
Kiu yake ya kujifunza iliendelea hadi alipopata shahada kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania).
‎Majaliwa aliyeanzia ualimu, ukufunzi wa chuo cha ualimu, ukatibu wa chama cha walimu, Ukuu wa wilaya ya Rufiji, Unaibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu tawala za mikoa na Serikali za motaa TAMISEMI yana hatimaye Waziri Mkuu wa –
‎ leo ameandika historia isiyo futika katika taifa letu.
‎CHAMA CHA WALIMU MKOA WA SINGIDA CWT wanamkumbuka zaidi hasa kipindi ambacho alianzisha, kusimamia na kukamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa la ofisi za chama cha walimu mkoani Singida alipokuwa akihudumu kama Katibu wa CWT mkoani Singida.
‎Majaliwa amechagua historia imjadili katika maisha yake yote.
Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliiona nyota ya Majaliwa kutokea Singida, akamteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo alipowekwa kiti moto na wabunge wawili wababe wa wilaya hiyo – marehemu Samuel Sitta na Juma Kapuya waliokuwa wabunge wa Jimbo la Urambo na Kaliua.
‎Hamad, Majaliwa akahamishiwa wilaya ya Rufiji alipohudumu hadi mwaka 2010 ndipo alipoamua kujitosa jimboni Ruangwa kugombea ubunge wa jimbo hilo.
‎Hakika nyota njema iliyoanzia ualimu haikazimika baada ya uchaguzi huo ambapo siku anawaaga watumishi wa wilaya ya Rufiji alikohudumu kama mkuu wa wilaya baada ya kushinda ubunge.
‎Katikati ya maandalizi ya kuelekea jimboni, analisikia jina lake akiwa miongoni mwa manaibu mawaziri wa serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.
‎Mwaka 2010, alichaguliwa kuwa Mbunge wa Ruangwa, kutokana ile kasi yake ya utendaji, jicho la hayati John Pombe Joseph Magufuli lilimuona Novemba 2015 na kumteua kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
‎Mtu mwema aliyewahi kutokea katika ardhi ya nchi yetu.
Leo hii tunamzungumzia Kasim Majaliwa
‎Kiongozi imara ambaye ameziishi Enzi na kuziheshimu nyakati zake
‎Kwa ridhaa yake mwenyewe Ameamua kuuwaga Waziri Mkuu baada ya kutangaza kutogombea ubunge wa Ruangwa.
‎Vyovyote iwavyo, vyovyote itakavyotafsiriwa, na vyovyote itakavyoonekana – lakini ukweli usemwe, Majaliwa ameandika historia yake. Sio rahisi kwa kiongozi wa ngazi yake kuamua kung’atuka na kuachia madaraka makubwa kama Uwaziri Mkuu.
‎Watangulizi wake kadhaa iliwabidi wastaafu siasa baada ya kushindwa kupata uteuzi wa nafasi ya juu baada ya kuhudumu kama Waziri Mkuu. Naam, tulimuona hayati Msuya akishindwa urais na hayati Mkapa ndipo akastaafu rasmi siasa mwaka 1995. Ilimchukua hadi kushindwa urais na Jakaya Kikwete mwaka 2005 ndipo akaamua kuistaafu rasmi siasa na kuitwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye. Sio hao tu, hata Mizengo Pinda ilimbidi ashindwe kwanza kura za maoni za urais mwaka 2015 na kuteuliwa Magufuli ndipo akatangaza kustaafu siasa.
‎Tofauti kabisa na Majaliwa Kassim Majaliwa aliyetangaza kutogombea tena ubunge wa Ruangwa. Ifahamike kuwa kutokugombea ubunge ni sawa na kusema ameamua kustaafu Uwaziri Mkuu, kwa sababu hauwezi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kama hautokani na ubunge wa kuchaguliwa jimboni. Hii ndiyo kusema kuwa Majaliwa amestaafu rasmi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.

Amestaafu akiwa bado ana nguvu, ana nishati na uwezo wa kuendelea kuwa mtumishi mwandamizi wa serikali. Waziri Mkuu mwenye historia ya utumishi uliojaa uadilifu na kujitolea. Ni kiongozi wa kipekee anayestaafu mapema kuliko waliomtangulia, lakini akiacha alama ya kudumu. Kassim Majaliwa ni kielelezo cha uongozi wa kweli – unaotanguliza maadili, unyenyekevu, na maslahi ya taifa kuliko jina binafsi.
‎Tanzania itamkumbuka daima kama mtumishi mwadilifu, ambaye alitumikia taifa kwa moyo wote – kwa utulivu, busara, na heshima ya juu. Hongera sana Majaliwa, tumeuona na kuuonja utamu wa utumishi wako kama Waziri Mkuu wa nchi hii.
Hakika wewe ni shujaa unayestahili kukumbukwa, ni mwamba unayehitaji kuegemewa.
‎Unaanza maisha mapya ya ustaafu ukiwa na nguvu na maarifa mapana kiasi cha kuwa mshauri bora kwa wa watakaoendelea madarakani.
‎Itoshe kusema umafanya kila ulichotakiwa kufanya katika nchi, Taifa limafaidika katika kila idara ulipokwepo
‎Sasa ni muda wa wajukuu kufurahia wema wa Babu Kasim Majaliwa
‎Kila la heri, Fahari ya Kusini.
‎Kila la heri, Mpiganaji.

Na. Mwandishi wetu - Kilimanjaro


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa siku 100 kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Wafanyakazi wa Umma (PSSSF) Ndg. Abdul-Razaq Badru kuhakikisha Awamu ya Pili ujenzi wa kiwanda cha kuchakata Bidhaa za Ngozi Kilimanjaro unakamilika na kuanza kufanya kazi ifikapo Julai 2024.
Agizo hilo amelitoa leo Februari 22, 2024 alipo fanya ziara ya kukagua ujenzi katika kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) ikiwa ni sehemu ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.
Mhandisi Luhemeja amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani ya zao la ngozi ghafi, kufungua fursa za soko la uhakika la Ngozi kutoka kwa wafugaji, kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya fedha za ndani na za kigeni.


Aidha, amefurahishwa na ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo na kutoa wito kwa watanzania kuwa na tamaduni za kuthamini bidhaa zinazo zalishwa nchini.


Awali akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Ndg. Abdul-Razaq Badru amesema amepokea maagizo hayo ya Katibu Mkuu Mhandisi Luhemeja na kuahidi kuwa PSSSF kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza watahakikisha wanafanya kazi kwa weledi kama ilivyo elekezwa ili watanzania waanze kunufaika na mradi huo.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho Mhandisi Saiba Edward amesema mradi huo pamoja na mambo mengine, utaongeza kipato kwa wakazi wa Kilimanjaro na Mikoa jirani kupitia fursa za uzabuni, uwakala na usambazaji wa bidhaa.


Kwa upande wake Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza Frank Mwakijungu amebainisha kuwa Magereza ni mbia wa utekelezaji wa Mradi huo hivyo watasimamia ujenzi wa kiwanda hicho ili kikamilike kwa wakati kwa manufaa ya watanzania.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhandisi Cyprian Luhemaja (kushoto) akikagua bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha bidhaa za Ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) leo Februari 22, 2024 ikiwa ni mwendelezo wa kukagua miradi inayotekelezwa na serikali kupitia Ofisi hiyo.




















Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa wakati alipokagua ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) ya Dodoma katika eneo la Mkonze jijini Dodoma
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa (kulia) wakati alipokagua ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) ya Dodoma katika eneo la Mkonze jijini Dodoma,
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kukagua ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) iliyopo eneo la Mkonze jijini Dodoma,
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa (katikati) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRC, Profesa John Kondoro (kulia) wakati alipokagua ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) katika eneo la Mkonze jijini Dodoma
Baadhi ya mafundi waoshiriki katika ujenzi wa Stesheni Kuu ya Reli ya Kisasa (SGR) katika eneo la Mkonzi jijini Dodoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao baada ya kukagua ujenzi huo,
Muonekano wa Jengo la Makao Mkuu ya Shirika la Reli Tanzania TRC jijini Dodoma ambalo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikagua ujenzi wake, Novemba 24, 2022. Mheshimiwa Majaliwa pia alikagua ujenzi wa Setesheni Kuu ya Reli ya Kisasa SGR katika eneo hilo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 06 Septemba, 2022.

PICHA NA IKULU
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akifuatilia Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8) unaoendelea katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Palais des Congres mjini Tunis,Tunisia, Agosti 27, 2022. Waziri Mkuu anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Tunisia Kais Saied alipowasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Palais des Congres kuhudhuria Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8), mjini Tunis,Tunisia, Agosti 27, 2022. Waziri Mkuu anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akisalimiana na Rais wa Tunisia Kais Saied alipowasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Palais des Congres kuhudhuria Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kimataifa kuhusu Maendeleo ya Japan na Afrika (TICAD 8), mjini Tunis,Tunisia, Agosti 27, 2022. Waziri Mkuu anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
---
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemshukuru Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida kwa misaada ambayo nchi yake inaipatia Tanzania ili kuleta unafuu kwenye maisha ya wananchi wake.

“Tanzania tunaishukuru sana Serikali ya Japan kwa kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwakwamua wananchi wake kiuchumi na kuwezesha ujenzi wa miundombinu hadi vijijini,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Agosti 27, 2022) wakati akizungumza naye kwa njia ya mitandao kwenye ukumbi wa Palais des Congres, jijini Tunis, Tunisia. Mheshimiwa Kishida ameshindwa kuhudhuria mkutano kwa sababu ya maambukizi ya UVIKO 19.

Mheshimiwa Majaliwa ambaye anamwakilisha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Nane wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa TICAD ulioanza leo, alimweleza Waziri Mkuu huyo kwamba Tanzania bado inaomboleza na wananchi wa Japan kufuatia kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu, Shinzo Abe na akatumia fursa hiyo kuwapa pole.

Akigusia miradi ambayo Serikali imeisaidia Tanzania, Waziri Mkuu amesema: “Iko miradi mingi ambayo imetekelezwa na Japan kupitia taasisi ya JICA, wako wawekezaji wanafanya biashara nasi na pia yako makampuni ambayo yamejitoa kusaidia sekta muhimu.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuiomba Japan ikamilishe ahadi yake ya kutekelza miradi waliyoiahidi kwenye mkutano wa TICAD 7 ambayo inahusu ujenzi wa barabara ya Arusha mpaka Holili mkoani Kilimanjaro, mradi wa maji wa Zanzibar, ujenzi wa bandari ya Kigoma na bandari ya uvuvi Zanzibar.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Japan, amemtumia salamu Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania wote na akataka uhusiano wa nchi hizo mbili kupitia taasisi yao ya JICA.

Mapema, akitoa tamko kwa niaba ya Rais Samia kwenye mkutano huo wa wakuu wa nchi na Serikali, Waziri Mkuu alisema bara la Afrika linakabiliwa na matatizo ya kiuchumi ambayo kwa kiasi kikubwa chimbuk lake ni UVIKO 19.

“Nimewaeleza madhara ya UVIKO 19 ambayo yanaikumba Afrika Tanzania ikiwemo, matatizo ya vita ya Ukraine na Urusi ambavyo vimesaabisha bei za bidhaa nyingi kupanda. Nimewaambia ujko umuhimu wa mataifa makubwa ya G20 kuungana na Japan ambayo ni ya tatu kwa ukubwa kiuchumi ili kuzisaidia nchi za Afrika.”

Amesema iko haja ya kuziwezesha nchi za Afrika kujitegemea ili ziweze kuwasaidia wananchi wake kupata fursa za elimu, kujenga uweza wa shughuli za kilimo, utalii ili waweze kukuza uchumi wao.

Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Rais Tunisia, Mhe. Kais Saied ambapo Rais wa Senegal, Mhe. Macky Sall alitoa hotuba ya ufunguzi na Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Kishida Fumio akahutubia kwa njia ya mitandao kutokea Japan.

Pamoja na masuala mengine, mkutano huo wa siku unatarajiwa kukubaliana kuhusu namna ya kuiwezesha Afrika kukabiliana na changamoto zinazoikabili Dunia ili kuiwezesha kufikia Agenda ya Maendeleo ya Umoja wa Afrika (Agenda 2063).

Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na janga la UVIKO 19, amani na usalama, mabadiliko ya tabia nchi, upatikanaji mgumu wa malighafi na mfumuko wa bei kwa bidhaa zinazotegemewa na nchi za Afrika kama vile gesi, mafuta na pembejeo za kilimo ambazo ni muhimu katika ukuaji wa uchumi wa Bara la Afrika.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inatambua mchango wa michezo shuleni, hivyo itaendelea kuhamasisha ufundishaji wa michezo katika shule za msingi na sekondari ili kuibua vipaji vipya vya michezo nchini.

Amesema katika kuwaandaa vijana kuwa na afya bora ya akili na mwili, Mheshimiwa Rais Samia ameahidi kuwa Serikali anayoiongoza itaendelea kuimarisha na kuongeza miundombinu ya shule pamoja na mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi na sekondari.

Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Alhamisi, Agosti 4, 2022) wakati akizindua mashindano ya Michezo na Taaluma kwa shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) na Umoja wa Michezo kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) wanafunzi, yanayofanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mkoani Tabora.

“Serikali imedhamiria kuboresha miundombinu ya michezo katika shule teule 56 nchini ikiwa ni wastani wa shule mbili kwa kila mkoa. Nimefurahi kuona utekelezaji wa mradi huu kwa mkoa wa Tabora tayari umeanza katika Shule za Sekondari Tabora Wavulana na Tabora Wasichana na viwanja vilivyojengwa vitatumika katika mashindano ya mwaka huu 2022.”

Amesema ujenzi wa miundombinu ya michezo utafanyika kwa awamu katika shule nyingine ili kuhakikisha kunakuwa na shule zenye miundombinu bora ya kuwezesha wanafunzi kusoma somo hilo kwa nadharia na vitendo. “Lengo ni kuzalisha wataalamu watakaobobea katika eneo hili la michezo.”

Amesema pamoja na ujenzi wa viwanja, Serikali itajenga kumbi kubwa katika shule hizo zitakazotumika kwa kazi za sanaa na michezo ya ndani. “Sambamba na hayo, Serikali imeendelea kuajiri walimu wa michezo ambapo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 walimu wa michezo 83 wameajiriwa.”

Amesema Serikali inatambua umuhimu wa michezo na utamaduni katika ukuaji na maendeleo ya wanafunzi kiakili na kijamii, kwa sababu michezo na sanaa ni miongoni mwa stadi muhimu zinazochangia ukuaji wa kiuchumi na kijamii ikiwemo kutengeneza fursa za ajira.

“Ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunajenga msingi imara wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji wa somo la elimu kwa michezo ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa vipaji vya michezo kwa wanafunzi wa elimu ya awali, msingi, sekondari hadi vyuo vya elimu ya juu.”

Ili kufanikisha azma ya kuboresha michezo na taaluma nchini, Waziri Mkuu amewaelekeza viongozi wa elimu katika ngazi ya shule, kata, shehia, Halmashauri na Mkoa wafuatilie ufundishaji na ujifunzaji shuleni na kushauriana na walimu ili kuhakikisha wanafunzi wanapata umahiri uliokusudiwa kwa masomo yote badala ya kukaa muda mwingi ofisini.

“Kila mwalimu ahakikishe anajiwekea malengo yake binafsi katika masomo anayofundisha na kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayeshindwa kupata umahiri uliokusudiwa katika somo lake ifikapo mwishoni mwa kila mwaka.

Pia, Waziri Mkuu ameagiza uteuzi wa viongozi wanaopewa dhamana ya kusimamia Elimumsingi na Sekondari katika ngazi za Shule, Kata, Shehia, Halmashauri na Mkoa uzingatie umahiri, weledi, ubunifu na uzoefu kama ilivyobainishwa kwenye mwongozo waliouandaa.

Mbali na kufungua mashindano ya michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA kwa mwaka 2022, Waziri Mkuu pia amezindua vitabu vya miongozo na mikakati kwa ajili ya kuboresha elimu nchini inayolenga kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazoathiri sekta ya elimu na kuongeza uelewa wa pamoja.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, David Silinde amesema Serikali imetoa shilingi bilioni 2.1 kwa ajili ya kugharamia michezo hiyo na kwamba ofisi yake itahakikisha inafanyika kwa ufanisi mkubwa.

Naye, Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Pauline Gekul amesema katika kuhakikisha elimu kwa michezo inaendelea kutolewa vizuri shuleni Serikali imetenga shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya michezo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akipokea Maandamano ya Wanamichezo wanaoshiriki Mashindano ya UMITASHUMTA mwaka huu 2022 leo Agosti 04, Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, alipowasili kuzindua mashindano hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 27, 2022 amezungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Nchini Marekani (CDC) Dkt. Rochelle Walensky (kulia kwake) alipokutana nae Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam
Katika mzungumzo hayo Mheshimiwa Majaliwa amemuhakikishia Dkt. Walensky kuwa Tanzania itaendelea kukipa ushirikiano Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Nchini Marekani (CDC)